Professional Documents
Culture Documents
18 Februari, 2013
mbali Global fund, malaria pia imekuwa ikifadhiliwa na Mfuko wa Ufadhili wa Rais wa Marekani (PMI USAID), Benki ya Dunia (World Bank) pamoja na wahisani wengine. Yapo makampuni makubwa manne ambayo yameteuliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya kuleta dawa hizo hapa nchi. Makampuni haya yanatambulika kimataifa kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuzalisha na kusambaza dawa hizo kwa vipindi maalum. Tatizo tunaloliona hapa ni Wizara yetu kushindwa kufanya makadirio na kuagiza dawa hizo kwa wakati. Ni wakati sasa kwa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria (NMCP), Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD), Kitengo cha Dawa cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (PSS) na Waganga Wakuu wa Wilaya (DMOs) kuchukua hatua madhubuti za kutatua tatizo la uhaba wa Alu. Suluhu ya tatizo hili ni kwa wote wanaohusika kuwajibika kwa dhati ili kuokoa maisha ya watanzania. Vilevile, tunaishauri serikali kupanua wigo wa matumizi ya mfumo wa SMS for Life ili kuongeza dawa zingine muhimu na vifaa tiba. Mfumo huu unasaidia sana kutoa taarifa zenye ukweli na uhalisia na kuhusu uhaba wa dawa ili wizara ijipange kukabiliana na tatizo hilo kwa kusambaza dawa zinazohitajika kwa wakati. Mfumo huu pia utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha uwazi na uwajibikaji katika usambazaji wa dawa, hatimaye kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini. Kwa namna ya pekee, Sikika inavipongeza vyombo vya habari kwa juhudi zao za dhati katika kuuhabarisha umma juu ya tatizo la uhaba wa Alu. Vyombo hivyo vilitanguliza zaidi maslahi ya umma bila kujali matamko ya wazi ya baadhi ya viongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya kuupindisha ukweli. Kwa mara nyingine tena, vyombo vya habari vimeweza kuonesha uzalendo kwa kuweka maslahi ya taifa mbele.
Mr. Irenei Kiria, Mkurugenzi wa Sikika, S.L.P 12183 Dar es Salaam, Simu: +255 222 666355/57, Nukushi: 2668015, Barua pepe: info@sikika.or.tz, Twitter: @sikika1, Facebook: Sikika Tanzania, Tovuti: www.sikika.or.tz