Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1106 RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA , JANUARI 3-9, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Habari Uk. 3
MWAKILISHI wa Jimbo la Mji Mkongwe Zanzibar (CUF), Ismail Jussa Landu amesema ikiwa kweli serikali ya umoja ya kitaifa inataka kuonekana kuwa inaheshimu utawala bora na haki za binaadamu, itende haki kwa kuwapa dhamana na kuwaachia Masheikh wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) waliowekwa ndani zaidi mwaka sasa. Habari kamili Uk. 12
PICHA juu: Wanajeshi wa Al Shabaab wakiwa katika mstari tayari kwa mapambano dhidi ya kikundi cha Ahlu Sunna wal Jamaa (wanaonekana katika picha chini). Wote hawa bendera zao zina Laailha ilallah, lakini wanapigana, wanauwana. Soma uk. 6, 7.
Habari Uk. 3
2
www.annuurpapers.co.tz
Tahariri/Habari
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
AN-NUUR
na T-Shirt, matiti nje. Sasa huwezi kusema mpiganaji wa namna hiyo anapigania kusimamisha Uislamu. Anaweza kuwa Muislamu, lakini hapiganii Uislamu. Ndio pale ikasemwa kuwa kinachoendelea Afrika ya Kati ni Civil War, ila imetumbukizwa chuki za kidini, sasa yamekuwa ni mauwaji ya Waislamu na Wakristo. Kwa upande wa Syria na Somalia, hili gumu kidogo kuwa na jibu la wazi kwa tulio wengi. Linahitaji uchambuzi wa kina na akili ya kutizama mambo kwa undani na kwa mapana. Sio kwa uoni finyu. Muhimu tunachosema hapa ni kuwa kamwe hoja haijawa Jihadkwa maana ya kukubali au kukataa. Hoja ni tahadhari. Ukisema nakwenda Jihad, iwe kweli unachofanya ni Jihad. Kama mtu anaamini kuwa Syria/Somalia kuna Jihad na yeye kama Muislamu anawajibika kwenda, na mazingira yana mruhusu kwenda, basi afanye safari aende. Asiache kwenda kwa kutoa kisingizio kuwa kuna watu wanapinga Jihad ndio wamemkwaza. Au kama anaona hawezi kwenda, lakini anaweza kutoa msaada wowote kwa namna yoyote, basi afanye hivyo. Quran inasema: Watasema: Mola wetu! Hakika tumewafuata mabwana wetu na wakubwa wetu, basi wao wametupoteza njia. Mola we tu ! W a pe hawa adhabu maradufu (kubwa zaidi) na uwalaani laana kubwa. (33:67-68) Na katika aya nyingine tunasoma: (Wakumbushe wakati) waliofuatwa watakapowakataa wale waliowafuata, na hali ya kuwa wamekwisha kuiona adhabu, na yatakatika mafungamano yao. Na watasema wale waliofuata, Laiti tungeweza kurudi (duniani) tukawakataa kama
wanavyotukataa. Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu atakavyowaonyesha vitendo vyao kuwa majuto yao, wala hawatakuwa wenye kutoka Motoni. (2:166167) Hoja ya msingi hapa ni kuwa hapatakuwa na utetezi kwamba mimi sikufanya jambo la kheri kwa sababu ya kupotoshwa na fulani. We ukiridhika kuwa jambo hili linafaa, fanya wala usitafute visingizio na kuleta malumbano kama yale ya kusema Ansaara wanapinga kuswaliwa Mtume, wakati wanachosema ni namna ya kumswalia. Ila sisi tutaendelea kutahadharisha kuwa hizi harakati za kuwatoa vijana katika shughuli zao za kimaisha, mashuleni na katika vyuo, eti wakaishi maisha ya kambi kwa ajili ya kujiandaa kusimamisha Uislamu, si sahihi na ni hadaa ya kuja kuwaangamiza Waislamu na kuivuruga nchi. Na harakati kama hizi haziwezi kuwa zimetokana na Waislamu, bali maadui wa Uislamu. Tumewahi kujiuliza vijana kama hao wakiibuka watakuja na agenda gani? Je, wakija na yale yanayotajwa kufanywa na Boko Haram, itakuwa ndio salama kwa Waislamu na Uislamu? Kutakuwa kunakalika? Je, yale yanayodaiwa kufanywa na Boko Haram, tunadhani kuwa kwa namna yoyote yanasaidia Uislamu? Basi tujue kuwa kila atakayekuja na agenda ya kuwakusanya vijana wa Kiislamu kuwapa mafunzo ya mwelekeo wa kimapambano, anacholenga ni kuzalisha watu ki-Boko Haram. Na huyu hawezi kuwa mtu mwema si kwa nchi wala Uislamu. Ni mamluki na wakala wa kuangamiza Waislamu na nchi. Ubaya wa jambo hili ni kuwa mawakala hawa ni watu wanaocheza na saikolojia ya Watu. Wanajua kuwa Waislamu wana malalamiko kinchi na kilimwengu na wanajua kuwa Waislamu ukiwaaminisha kuwa wanapigania Jihad, utawapeleka unavyotaka, hawarudi nyuma wala kuogopa chochote. Hapo ndipo wanapotupata Waislamu kwa wepesi mno na kututumia kwa masilahi yao. Tunaweza kusema kwa uhakika kuwa hawa ni mawakala wanaotumiwa katika kufanikisha ile agenda
Habari/Tangazo
AN-NUUR
Chaani na kufungua barza ya vijana, iliyoyopewa jina la barza ya Maalim Seif Sharif Hamad, katika kijiji cha Bandamaji Chaani.
limeendeleza tafsiri ya kuendelezwa utamaduni wa kupuuzwa Waislamu katika mambo ya msingi na ya kisera nchini. Tumesikitika sana kuona kwamba maoni yetu hayapo. Maana ya Waislamu kushiriki kutoa maoni yao, ilikuwa ni pamoja na kusukumwa na fikra kwamba sasa mwarobaini wa matitizo yao ya kiimani
Inaendelea Uk. 4
Na Bakari Mwakangwale
SERIKALI imebainisha kuachana na utaratibu wa awali wa kupanga alama za ufaulu kwa wanafunzi katika mitihani ya Taifa zilizo kuwa zikitumiwa na Baraza la Mitihani Taifa (NECTA). Hayo yamebainishwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Dkt. Shukuru Kawambwa, wakati akizungumza na wanafunzi wa Kiislamu katika Mkutano wao Mkuu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Kiislamu (TAMSYA), mjini Bagamoyo. Dkt. Kawambwa, alisema Serikali imeshughulikia na kurekebisha taratibu za Baraza la Mitihani zilizokuwa zinasababisha mashaka mengi kwa wadau. Kuhusu Baraza la Mtihani (NECTA) Waislamu wamekuwa na malalamiko kwa muda mrefu kuhusu Baraza hilo, naomba nitumie fursa hii kwa niaba ya serikali, kwamba taratibu za utunzi na usahihishaji wa mitihani na kupanga matokea sasa umebadilishwa, ile dhana ya ubaguzi wa kidini au ukabila nadhani haitakuwepo. Alibainisha Waziri Kawambwa. Alifafanua kuwa moja ya masuala yaliyolalamikiwa sana na wadau wa elimu, ni utaratibu wa kupanga madaraja ya ufaulu unaobadilika mara kwa mara, yaani flexible grade range. Alisema katika kushughulikia hilo, kuanzia mwaka 2012 serikali iliamua kutumia
ya wanafunzi wa Kiislamu mashuleni yanasikilizwa na kupatiwa ufumbuzi unaotakiwa. Alibainisha kwamba, Wizara yake imetoa nyaraka mbalimbali zikielekeza mambo muhimu yakiwemo, vipindi vya Dini mashuleni, uendeshaji wake, utaratibu wa mavazi kwa mabinti wa Kiislamu shuleni na nyakati za swala sambamba na mambo mengine yanayohusu Dini. Nikiri tu kama risala ilivyosomwa kwamba, nyaraka nyingine ni za muda mrefu, ni jambo la kibinadamu inawezekana sehemu nyingine zimeanza kusaulika na hazijulikani zipo wapi. Nikiri kwamba wakati wa kuhuisha nyaraka hizo umefika, ili ijuliakane kwamba serikali msimamo wake ni ule ule katika yale mambo ambayo ilikuwa imeelekeza. Alisisitiza. Waziri Kawambwa alisema nyaraka hizo ni juhudi za Serikali katika kuhakikisha wanafunzi wa Kiislamu wakiwa ni sehemu ya jamii ya Kitanzania, wanapata fursa na stahili sawa katika kupata elimu, huku wakiendelea kuabudu kwa imani zao wakiwa masomoni. Hata hivyo, alisema Wizara yake inatambua kuwepo changamoto kadhaa kwa wanafunzi wa Kiislamu nchini katika vituo vya elimu, ambapo alidai uzoefu unaonyesha migogoro mingi inatokana na kukosekana mawasiliano ya kutosha kati ya walimu au viongozi na Taasisi za dini na wanafunzi mashuleni.
4
AHLU Sunna Waljama'a ni kundi la wapiganaji w a K i i s l a m u linaloundwa na watu wa Twarika (Sufis) ambao wanalipinga kundi la Al-Shabaab. Hawa wameshika silaha wakipigana na Al Shabab kwa madai kuwa hawa Al Shabab wakifanikiwa kushika nchi, wataifanya Somalia kuwa nchi ya Wahhabi. Wakati ule Somalia ikiwa imeshikiliwa na makundi ya wababe wa kivita, hawa ASWJ walikuwa wakishirikiana na mbabe wa kivita Mohamed Farrah Aidid. Hata hivyo wakati huo Ahlu Sunna Waljama'a hawakuwa ni wenye kusikika sana mpaka mwaka 2008 waliposhika silaha kupambana na alShabaab. Inaelezwa kuwa kilicholipua uhasama na vita kati ya Ahlu Sunna Waljamaa, ni kitendo cha Al Shabab kubomoa makaburi ya Masheikh na Makhalifah wakubwa wa-Kisufi katika maeneo wanayoshikilia. Katika mapambano y a o , A S W J , w a m e f a n i k i w a kuwatimua Al Shabab katika maeneo mengi ya katikati ya Somalia na kusini hasa kule Mudug, Gedo, Galgaduud, baadhi ya sehemu za Hiiraan, Shebelle ya kati na Bakool. Machi 15, 2010, Ahlu Sunna Waljama'a walifanya makubaliano na serikali ya Somalia ambapo walipewa wizara tano wachague watu kutoka kundi lao wawe Mawaziri. Walipewa pia nafasi za kidiplomasia na ndani ya vyombo vya usalama. Kwa upande wake wapiganaji wa ASWJ walikubali kuendelea kushirikiana na jeshi la serikali dhidi ya alShabab. Katika jumla ya mapambano ya makundi haya mawili ya Kiislamu yaliyoacha mamia kwa makumi ya askari wa pande zote mbili wakiuwana halikadhalika raia wasio na hatia, ni pamoja na l i l e l i l i lopelekea Ahlu Sunna Waljama'a kutwaa Dhuusamareeb kule Galguduud kutoka mikononi mwa Al Shabab. Hiyo ilikuwa
Makala
AN-NUUR
WAPIGANAJI wa Ahlu Sunna Waljamaa ambao wanapigana na Al Shabab. huo unaoendelea mpaka Shabab, waliuwawa. Aprili 24, 2011. leo? Mapambano mengine Sheikh (Mwenyekiti) L a b d a t u a n g a l i e wa ASWJ wa mkoa wa ni ya Aprili 28, 2011, m a t u k i o m e n g i n e . Gedo, Sheikh Hassan ambapo Ahlu Sunna Mei 3, 2011, yalitokea Sheikh Ahmed (aka Waljama'a wakiwa mapigano makali kwa Qoryoley) alijeruhiwa pamoja na askari wa masaa kadhaa katika na kukimbizwa Nairobi TFG, walipambana na mji wa Garbaharey, Al Shabab katika mji Gedo. Katika mapigano kwa matibabu ambapo wa Luuqin mkoa wa h a y a A h l u S u n n a alifariki siku mbili Gedo. Askari wengi wa Waljama'a walifanikiwa baadae. pande zote waliuwawa. Mapambano ya kuteka eneo hilo Mtu utajiuliza, lililokuwa chini ya Al namna hii yamekuwa katika askari hawa Shabab. Inaelezwa kuwa ya kawaida ambapo waliouwawa au k a t i k a m a p a m b a n o Waislamu wa makundi waliouwana (Waislamu hayo askari 3 wa ASWJ haya mawili, wamekuwa kwa Waisla m u), n i na askari 23 wa Al wakiendesha darsa za wa kutoka kundi lipi watakuwa wamekufa mashahidi? Wote hawa wanadai kupigania Dini isiharibiwe! tukajaribu katika Inatoka Uk. 3 H a w a A S W J rasimu hii ya pili, nako u m e p a t i k a n a . S a s a pia hayakujumuishwa, wanawaona Al Shabab hatuna fursa tena hakuna fursa tena wanaowavunjia alisema kwa masikitiko iliyobaki , alifafanua heshma Masheikh Sheikh Musa Kundecha, Sheikh Kundecha. wao wa Twariqa, ni Amir wa Baraza Kuu la Kufuatia hali hiyo, watu waliopotea njia. Jumuia na Taasisi za Amir Kundecha Wanapotosha Uislamu. Kiislamu nchini. alisema viongozi wa Alisema dhana nzima Kiislamu wamejitahidi Al Shabab nao hivyo ya Waislamu kushiriki kutoa maoni yao kama hivyo. Je, mgogoro wa kikamilifu katika kutoa namna hii, mgogoro wa m a o n i y a o k a t i k a taasisi na kuhamasisha kiitikadi na mtizamo mchakato huo, pamoja u m m a w a K i i s l a m u wa kidini, utatuzi wake na mambo mengine k u s h i r i k i i p a s a v y o utapatikana kwa njia ilikuwa ni kujaribu katika kutoa maoni yao, ya risasi? kutafuta suluhu ya lakini rasimu ya pili Mwaka 1846 Sheikh kudumu kikatiba juu ya imethibitisha kwamba Ali alisema watu wa matatizo yao ya kiimani, maoni ya Waislamu Qadiria katika utawala lakini sasa fursa hiyo hayapo. Geledi waliokufa vitani imepotea kufuatia Nachukua fursa hii wakipigana dhidi yake, maoni yao kuwekwa kuufahamisha umma wanakwenda motoni. kando licha ya ushiriki wa Kiislamu kwamba, Ila maiti wake katika wao. wasifikiri viongozi kundi la Sunna, Tulitoa maoni yetu wao wamewaangusha wanakwenda Peponi. katika rasimu ya kwanza na hawakuwajibika Hatuoni kuwa h a i y a k u j u m u i s h w a , ipasavyo, wamejitahidi mkanganyiko ule ndio
Habari za Kimataifa/Tangazo
AN-NUUR
WANAWAKE Waislamu wa kabila la Rohingya nchini Myanmar, wanakabiliwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyofanywa na maafisa usalama katika vituo vya polisi nchini humo. Kwa mujibu wa ripoti, maafisa wa usalama nchini Myanmar wamekuwa wakiwateka nyara wanawake na wasichana Waislamu wa kabila hilo na kuwapiga na kuwatukana.
jamii hiyo haki yoyote kwa madai kuwa sio raia wa nchi hiyo. Aidha mara kadhaa Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kutetea haki za binaadamu, yamekuwa yakiituhumu serikali ya nchi hiyo kwa kufumbia macho vitendo vya ukatili wa kijinsia vimavyofanywa na maafisa wa usalama na jeshi, dhidi ya wanawake Waislamu wa kabila la Rohingya nchini humo.
6
Na Omar Msangi KUWA Msomali, ni kuwa Muislamu. Huo ni msemo mashuhuri wa Wasomali. Wanachomaanisha ni kuwa Wasomali wote ni Waislamu. Wanasema kuwa kama yupo Msomali anayedai kuwa yeye sio Muislamu, basi atakuwa mamluki tu anayepewa pesa ili akanushe Usomali na Uislamu wake. Msomali anaweza akawa asi, mlevi, haswali, hatoi zakka, lakini hamtaelewana ukimgusa katika Uislamu wake au kumtaka aritadi. Ndio walivyo kwa asili. Kama ni kubadilika, labda wabadilike hawa wanaohamia nchi nyingine wakakulia katika mazingira ambayo si ya Kisomali. Iwapo Uislamu umekuwa kama ndio mila na utambulisho wa Msomali, swali ni je: mbona Uislamu huu tunaoambiwa ni dini ya amani, neno lenyewe Islam ni amani; haujaweza kuwasaidia Wasomali na kuwaepusha na mapigano na mauwaji ya wao kwa wao? Je, hii hali ya kupigana na kuuwana wenyewe kwa wenyewe miaka nenda miaka rudi, haiwi sababu ya kuupaka Uislamu matope na kuonesha kuwa hauna msaada wowote kwa jamii? Why has Islam not kept us from killing each other? (Kwa nini Uislamu haujatusaidia ukatuepusha na kuuwana wenyewe kwa wenyewe?). Wanajiuliza Wasomali na wanauliza baadhi ya watafiti na waandishi wa vitabu. Hivi sasa Somalia ipo katika vita. Jeshi la serikali- Transitional Federal Government (TFG), linapambana na makundi ya Kiislamu ambayo yanapinga serikali yakidai kuwa ni kibaraka wa nchi za kikafiri. TFG inaongozwa na Sharif Sheikh Ahmed. Huyu alikuwa ndiye kiongozi wa Umoja wa Mahakama za Kiislamu ambao uliweza kusimamisha vurugu, mauwaji na uhalifu ikaanza kujenga serikali ya Kiislamu. Serikali hiyo ya Kiislamu ambayo ndio kwanza ilikuwa ikijengwa, ilivurugwa
Makala
AN-NUUR
WAFUASI wa Ahlu Sunna wakidhikiri, wakimaliza kudhikiri wanashika bunduki kwenda kupambana na Al Shabab.
na kungolewa baada ya uvamizi uliofanywa na Ethiopia ikisaidiwa na Marekani. Marekani ilidai kuwa Umoja wa Mahakama za Kiislamu ni magaidi wenye
uhusiano na Al Qaidah. Baada ya kungolewa utawala wa Mahkama za Kiislamu, hawa waliokuwa ndio waanzilishi na wapiganaji walioweza
kusimamisha mamlaka iliyoleta amani ya muda Somalia, wakagawika. Baadhi wakaingia katika serikali mpya (TFG), wengine wakapinga na wale vijana waliokuwa
7
Inatoka Uk. 6 kwa wao. Badala ya kupambana na askari wa AMISOM na wale wa serikali, hutokea nao wakashikiana silaha wakauwana na kuuwa raia katika mapigano yao. Inasemekana kumekuwa na harakati katika nchi mbalimbali kuhamasisha vijana wajitolee kwenda Somalia kupigana upande wa Al Shabab. Jaaliya hilo ni kweli na wanapatikana Waislamu wa kwenda huko. Kwa upande mwingine, Sharif Sheikh naye anazidi kupewa msaada wa askari na silaha kupitia AMISOM na sasa jeshi la Kenya lipo ndani ya Somalia likipigana. Picha ya kwanza t u n a y o t a k i w a tuitizame ni hii: Hawa ni Waislamu ambao wote walikuwa katika Umoja wa Mahakama za Kiislamu. Hivi sasa wamegawanyika ni makundi mawili yanayohasimiana. Moja linapata misaada kutoka nchi unaweza kuziita za kikafiri (AMISOM na UN) pamoja na za Waislamu. Kundi jingine linatangaziwa ugaidi. Hakuna nchi inayoweza kujitokeza waziwazi kuwasaidia Al Shabab. Ndio unakuta hii inayoitwa kampeni ya chini kwa chini ya watu binafsi, sio katika ngazi ya kiserikali au nchi, kutafuta vijana kwenda kupigana Somalia. V y o v y o t e utakavyoitafsiri picha hii, kwamba ni Jihad au sio, lakini wanaouwana na kuangamizana ni Wasomali. Ni Waislamu wenyewe kwa wenyewe! Pengine labda turejee nyuma tutizame historia ya Somalia tukitaraji kuwa huenda tukapata jibu la lile swali la msingi: Kwa nini Uislamu haujasaidia kuondoa mauwaji ya Wasomali wenyewe kwa wenyewe? Ukifanya rejea mbalimbali za vitabu, zitakuonesha kuwa makundi ya mwanzo yaliyoingia na kuingiza
Makala
AN-NUUR
WAPIGANAJI wa kikundi cha Hizbu Islamiyah. Uislamu Somalia katika karne ya 17, 18 na 19, yalikuwa ya Masufi-Twarika (watu wa dhikri). Na hawa walikuwa Qadiriyah, Ahmadiyah na Salihiyah. Masheikh mashuhuri na viongozi wa Twarika hizi wakitajwa kuwa ni Sheikh Madar, Sheikh Abdirahman AlZayli, Sheikh Aweys al-Baraawi, Sheikh Mohamed Guleed, Sayid MohamedAbdulle Hassan, Sheikh Ali Maye, Sheikh Sufi na wengineo walioheshimiwa sana na watu wa Somalia. Inaelezwa kuwa awali Masheikh hawa, Murid hawa, walihubiri kwa amani, hawakuwa wagumu kwa watu na wakati mwingine waliwaacha kufanya mambo waliyozoeya hata kama hayapo katika Uislamu. Kwa namna moja au nyingine, hawakushiriki kabisa katika migogoro au hali iliyoleata umwagikaji damu, bali walikuwa wasuluhishi wakubwa. Hata hivyo inaelezwa kuwa yapo matukio makubwa matatu ambayo, pengine yanaonyesha kuwa toka mwanzo Uislamu haukuwa umepokewa katika ufahamu ulio sahihi na ndio ikawa sababu ya kuanza uhasama miongoni mwa makundi ya Kiislamu na
8
Inatoka Uk. 4 wa Ki-Ansaar Sunna kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine ni kukosa uvumilivu na kuwastahamilia wengine ambapo katika hali hiyo wanadaiwa kupinga na kuwashambulia watu wa Sufi kwamba ni makafiri pamoja na kubomoa makaburi ya Masheikh wao pamoja na sehemu wanazoamini kuwa ni takatifu katika Kismayo kutokana na historia ya Usufi katika Somalia. Usufi, ndio mtizamo mkubwa na ulioenea sehemu kubwa ya Somalia ambapo mara nyingi na mahali pengi, wakuu wa Twarika katika miji ndio hao hao wakuu wa koo. Hofu iliyoingia kwa ma-Sufi hawa ni kuwa iwapo Al Shabab wataachwa washike nchi, basi wataangamiza aqida ya ki-Sufi na badala yake kuweka walichodai kuwa ni Uwahabi (kwa mtizamo wao, sio mtizamo wa mwandishi). Katika historia ya Kiislamu tunasoma juu ya Khawarij (Kharijite) waliouwa Waislamu waliokuwa na mitazamo tofauti na ya kwao. Hawa ASWJ, wanaamini kuwa Al Shabab nao wamekuja kuuwa Wasomali wasio wafuata. Ni Khawarij wa leo. Ni katika kikao cha Nairobi, As Ahlu Sunna wal Jamaa waliunda Baraza la Vita (war council) , na kuanza kuweka mikakati ya kupata silaha na wapiganaji. Kwa upande mwingine, Ahlu Sunna wal Jamaa (ASWJ), wamepiga marufuku baadhi ya vitabu vya dini vinavyochapishwa na kusambazwa na Al Shabab wakidai kuwa vinafundisha vijana kujilipua kwa nia ya kujitoa muhanga (suicide bombers). Madai mengine ni kuwa Al Shaba wanawachukulia Waislamu wasiofuata msimamo wao kuwa ni makafiri. Humkufurisha kila asiyekuwa Salafi
Makala
AN-NUUR
MPIGANAJI wa kikundi cha Hizbu Islamiyah. Katika zoezi hilo, ASWJ, wamefanikiwa kuondoa Vitabu hivyo katika miji ya Dhusamareb, Adado, Guriel, Harardhere, Hobyo na maeneo mbalimbali wanayomiliki katika Somalia ya kati. Katika zoezi hili, ASWJ, wamepata uungwaji mkono mkubwa na wananchi ambao wamekuwa wakidai kuwa wanahofia kuona watoto wao wakipotoshwa na kupambana na Waislamu wenzao. I am happy that Ahlu Sunna wal Jamaa clerics, who have a deep understanding of the religion, are prohibiting our children from being taught al-Shabaabs wrong ideology about suicide bombing. All praise is due to God for guiding our clerics to prevent such dangers. Alinukuliwa Mama Sadia Mohamed, akisema akimaanisha kuwa anawashukuru Masheikh wa ASWJ, kwa kuondoa hatari hiyo. A child is not born believing in suicide bombing and viewing other Muslims as infidels. This is an idea that is indoctrinated and it will cause many societal problems if it is not combated. Aliongeza Mama huyo, hali inayoonyesha kuwa hata kama Al Shabab watafanikiwa kushinda vita ya silaha na kushika madaraka ya kuongoza nchi, bado kutakuwa na vita ya kiitikadi ambayo itaendelea kusumbua na kuibua vita ya silaha mara kwa mara. Sio ASWJ pekee wapo pia na Hizbul Islam Hizbul Islam iliundwa Januari 2009, Sheikh Omar Iman, akiwa mwenyekiti wake wa kwanza. Msimamo wa Hizbul Islami kama walivyoutangaza hapo tarehe 7 Februari, 2009, ni kupambana na serikali ya Sharif Sheikh Ahmed na majeshi ya African Union (AMISON) yaliyo Mogadishu. Kundi hili limekuwa dhaifu ikilinganishwa na Al Shabab kutokana na migogoro na ugomvi wa kugombea madaraka. Hali hiyo imepelekea kwamba kila wanapopigana na Al Shabab, hupigwa. Baadhi ya wakati migogoro hiyo hupelekea kugawika makundi mawili moja likajiunga na Al Shabab kupigana na jingine. Katika kuzidi kusambaratika, pengine na kutafuta namna ya kujihami, ilifikia kundi zima likatangaza kujiunga na Al Shabab. Hata hivyo mwaka jana (2012) lilijitenga tena kutoka alShabaab na kuanza mapambano. Walifanya hivyo Septemba 2012, baada ya al-Shabab kupigwa sana na majeshi ya serikali/ AMISON na kutimuliwa katika maeneo mbalimbali waliyokuwa wakishikilia. Ndugu waliokuwa wakipigana katika safu moja kupambana na adui, sasa wakashika bunduki kuuwana wenyewe kwa wenyewe wakiacha pembeni adui waliyekuwa wakimpiga kwa pamoja. Ukichukua ugomvi huu wa Al Shabab na Hizbul Islami, unakuta kuwa mgogoro wa Somalia unakuwa katika hali ya utata zaidi maana unazaa Vita ya wenyewe kwa wenyewe ndani ya vita ya wenyewe kwa wenyewe (Civil-warwithin-a-civil-war.) Civil war ya kwanza ni kati ya Majeshi ya Serikali yakiwa pamoja na Ahlu Sunna Wal Jamaa yakipambana na Al Shabab/Hizbul Islam (Islamists vs. TFG) na Civil war ya pili ni al Shabab wakipambana na Hizbul Islam (Al Shabab vs. Hizbul Islam). Swali la msingi hapa ni je, Waislamu hawa, Wasomali hawa, wanasaidiwaje? Ukirejea mkanganyiko wa itikadi za Kisufi
9
Inatoka Uk. 7 tukio hili kama mapambano kati ya nguvu inayoibuka ya kuhuisha Uislamu na Waislamu wahafidhina katika Geledi. Baadhi ya waandishi wanataja kuwa sultani wa Geledi (Geledi Sultanate), alikuwa na mahusiano mazuri na Sultan wa Zanzibar wakati huo, Sultan Sayid Barghash, na hivyo alipata msaada kutoka kwake. Hilo ni tukio la kwanza linaloonesha historia ya mapambano ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe katika Somalia. Tukio la pili linahusishwa na kuingia Sheikh Ali Abdurahman (1787-1952) katika mji wa Merca mwaka 1946 ambapo alizua mapambano na uongozi katika usultani wa Geledi. Huyu Sheikh Ali anatajwa kuzaliwa katika mkoa wa Nugal ulio kati ya Growe na Laas-Aanood katika Puntland ya leo. Kabla ya kufika hapo alikuwa Makka, Saudi Arabia kisha Baghdad, Iraq kwa ajili ya masomo. Akiwa huko anadaiwa kukutana na wafuasi wa Sheikh Mohamed Abdulwahab na aliporejea Somalia akaja na misimamo ya wafuasi hao katika dini na akataka kuilazimisha kwa watu wa Somalia, wengi wakiwa Sufi/ Twarika. Alianza kujenga chuo cha Kiislamu. Hata hivyo akalazimika kuhama baada ya kukataliwa na watu wa mji/koo yake. Alihamia mji mwingine, lakini napo akakataliwa kabla ya kwenda kwa Sultan Nur Osman. Hata hivyo napo aliona hapamfai kwa kuona kuwa Shariah za Kiislamu zinapingwa waziwazi na Sultan Ali. Hapo akaungana na Haji Farah Hirsi, ambaye aliasi familia akitaka kusimamisha usulutani wake. Wakakubaliana kuwa wakishinda, Haji Farah atakuwa kiongozi wa kisiasa wakati Sheikh Ali akisimamia mambo ya dini. Ilikufanikisha lengo hili, Sheikh Ali alitafuta msaada kutoka kwa
Makala
AN-NUUR
BENDERA ya chini ni ya Al Shabab na ya juu ni ya Ahlu Sunna Waljamaa. Wote wanapepea bendera ya Laailha ila llahu Muhammadar rasuulullah, lakini wanapigana, wanauwana.
mtawala wa Sharja, Sheikh Saqar al-Qasimi, lakini hakufanikiwa. Baada ya kukosa msaada huo, Sheikh Ali alikwenda Zanzibar a k ita k a m s a a d a wa Sultan Said al-Bu-Saidi. Akiwa na wazo la kusimamisha Falme ya Kiislamu, Sheikh Ali alifika Merca mwaka 1946, miaka mitatu baada ya kushindwa utawala mwingine wa Kiislamu Baardheere na badala yake Usultani wa
Geledi Sultanate kuwa ndio nguvu iliyotawala sehemu kubwa ya kusini mwa Somalia. Hata hivyo, koo ya Biimal, ambayo ndiyo koo kubwa kabisa katika Merca, iliasi kipindi hicho na Sheikh Ali akaona kuwa hao ndio watu wa kuwatumia katika mipango yake. Mwanzo alijifanya mpatanishi baina ya Sultan Yusuf na watu wa koo ya Biimal. Hata hivyo Sultan Yusuf
akakataa upatanishi wake. Hapo Sheikh Ali akatumia fursa hiyo kutangaza vita dhidi ya Sultan Yusuf akitaraji kuwa watu wa Biimal watamsaidi. Lakini hawakufanya hivyo. Akaingia vitani na watu wachache aliohama nao na ikawa rahisi sana kwake kushindwa. Hiyo ilikuwa mwaka 1846. Kwa upande mwingine, matarajio yake ya kupata msaada kutoka kwa Sultan wa
10
Inatoka Uk. 9 fatwah mbalimbali kupinga mambo yaliyokuwa yakifanyika. H a t a h i v y o , Masheikh wa Qadiriyah walishinda changamoto hii kupitia midahalo na mihadhara iliyoelimisha na kuwaimarisha wafuasi wao. Na kazi hii haikufanywa na Masheikh wa eneo hilo pekee, bali walialikwa Masheikh kutoka sehemu mbalimbali wakiwemo Sheikh Madar kutoka Hargeysa, aliyekuwa mkuu wa Qadiriyah katika mkoa/Jimbo hilo. Hiyo ilikuwa mwaka 1897 na haukupita muda, Waislamu Qadiriyah wa Berbera wakamtimua Sayid Mohamed. Lakini la kufahamika hapa ni kuwa kabla ya Sayid Mohamed kulazimika kukimbia kutoka Berbera, ilibidi serikali ya kikoloni kuingilia kati kutuliza ghasia baina ya makundi mawili ya Kiislamu, Qadiriyah na wafuasi wa Sayid Mohamed. Ugomvi huu wa Qa d iriy a h n a S ayid Muhamad, ukawa chanzo cha chuki na uhasama wa muda mrefu kati ya Waislamu Qadiriyah na Salihiyah. Na unatajwa kuwa wa kisiasa upande mmoja na kwa upande mwingine dini. Kisiasa kwa sababu Sayid Mohamed alikuwa na lengo la kusimamisha utawala wa Kiislamu kwa mtizamo wa Twariqa yake, lakini hakuchukua muda kuwaelimisha na kupata kuungwa mkono na Masheikh wengine waliokuwa na sauti. Hiyo ikamjengea chuki na kutengwa na Masheikh wenzake pamoja na viongozi wa koo. Kwa upande wa dini, Salihiyah waliwakufurisha Qadiriyah, wakidai kuwa Uislamu sahihi ni ule tu wa Salihiyah. Ugomvi ulikuwa mkubwa kiasi cha Masheikh wa pande mbili kutungiana mashairi ya kutukanana na kukufurishana na kuingizana motoni (Angalia B. G. Martin,
Makala
AN-NUUR
HAWA ni wapiganaji wa kikundi cha Hezb al-Islamiya aluyetafsiri baadhi ya mashairi hayo). Hali hii ilipelekea mapambano ya silaha baina ya Waislamu wa makundi haya mawili ambapo Aprili 14, 1909, wafuasi wa Salihiyah walimuuwa Sheikh Aweys al-Baraawi wa Biyooley. Kwa bahati mbaya au katika kilele cha kuonesha chuki na uhasama uliokuwepo, Sayid Mohamed alipopata habari za kuuliwa Sheikh Aweys, alisikika akiimba kibwagizo cha kujipongeza kwa ushindi. Akasema tizameni, hatimaye, tulipomuuwa mjusi kikongwe, mvua imeanza kunyesha. (Candhagodoble goortaan dilaa roobki noo daaye). Hakuishia hapo na wafuasi wake, lakini wanatajwa pia kuchoma moto madrasa nyingi za makundi yasiyokuwa yakifuata mtizamo wao. Hii ilileta chuki, uhasama, mapambano na mauwaji baina ya Waislamu. Ukiangalia na kuchambua historia na matukio haya matatu, utaona kuwa yalikuwepo mambo matatu ambayo ni tatizo. Moja, ni kushindwa kutambua, kukubali na kuvumilia uwepo wa watu wenye mtizamo tofauti. Pili, kundi moja kujipa Hati Miliki ya Dini (monopoly of religious legitimacy). Kwa maana kuwa wao ndio pekee halali kuwepo. Tatu, utumiaji wa nguvu, vurugu, mapambano (violence) dhidi ya makundi ya Kiislamu yanayotofautiana. Na nne, ni utumiaji wa Shariah, hovyo hovyo (kwa kuchagua). Hali hii ya kimapambano ya sasa, inaanzia kwa kuibuka Al-itihad al-Islami katika miaka ya 1980s ambapo harakati zake za vita vya silaha dhidi ya Waislamu wasio katika mtizamo wa kundi hilo, kuliwaletea maafa makubwa katika mapambano ya Kismayo (1991), Puntland (1992) na Gedo (1996). Pamoja na kuwepo makundi mengi ya Kiislamu kama Al-Ahl, Takfiir Wal-Hijra, Jama Islamiyah, Wahdatul Islamiyat na Al-Ittihad al-Islami (AIAI), lakini makundi makubwa ambayo hivi sasa yameshika silaha ni Al-Shabab na Hizb alIslami. Pamoja na kuwa wote hawa wanapigana dhidi ya serikali ya Sharif Sheikh Ahmed, lakini nao pia ni maadui. Hutokea wakapigana wao kwa wao na kusababisha maafa baina yao na kwa Waislamu wasio na hatia. Wapo pia Ahlu Sunnah Wal-jamaa, ambao nao pia hutwangana na Al Shabab. Swali ni hili: kama kundi moja wapo katika haya yaliyoshika silaha kupigana na serikali litashinda, kuna uwezekano wa makundi mengine kutambua ushindi huo na kuweka silaha chini kuacha kundi hilo litawale? Au baada ya kushinda na kuondoka askari wa AMISOM, wataanza kupigana wenyewe kwa wenyewe? Kama wameshindwa kuwa wamoja katika lengo la kupigana na adui, watakuwa wamoja baada ya adui kuondoka? Hapana shaka kinachokwamisha
11
Habari/Matangazo
AN-NUUR
Inatoka Uk. 12
Masheikh waachiwe
rumande kunawanyima haki zao kikatiba na hakuwatendei haki wao na familia zao. Katika mkutano huo wajumbe wa Kamati ya Maridhiano wakiongozwa na Mzee Moyo waliungana na Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kwa kuwataka Wazanzibari kuungana na kuacha kusikiliza maneno ya chokochoko ambazo mwisho wake ni kuumizana na kujenga hasama miongoni mwao. Maalim Seif alisema ni wakati mwafaka sasa Wazanzibari kukataa kufitinishwa kwani ni muda mrefu wamekuwa katika mifarakano isiyokuwa na maana na sasa wameungana kwa maslahi ya nchi na wananchi wote bila ubaguzi hivyo alitoa wito kuendelea kushikamana ili kufikia lengo la kuitetea Zanzibar na Mamlaka yake.
peke yao, lakini tutizame wale akina mama waliopo majumbani mwao ambayo wana watoto wadogo watakuwa wameathirika kiasi gani kwa waume zao kuwekwa ndani siku zote tokea mwezi wa 10 mwaka jana (juzi) mpaka leo kesi inakwenda na kurudishwa nakuna linalokuwa sasa mimi natoa wito kwa Waziri wa Sheria, Makamo wa kwanza wa Rais ambao mpo hapa katika mkutano nyinyi ni miongoni mwa serikali tunasema suala hili tunaomba mlizingatie suala la kuendelea kuwaweka ndani Masheikh wananchi wamechoka, alisema Eddy. Kauli za kutetewa Masheikh hao zimeonekana kuvuta hisia za wananchi wengi ambapo baadhi yao walikuwa wakisema ni wakati mwafaka sasa Serikali kushughulikia kama ni kuwatia hatiani au kuwapa dhamana lakini kuendelea kuwaweka
TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO RIDHWAA SEMINARI-KINONDONI MKWAJUNI KIDATO CHA KWANZA NA CHEKECHEA-2014
UONGOZI WA RIDHWAA SEMINARI UNAPENDA KUWATANGAZIA WAISLAMU WOTE NAFASI ZA MASOMO KWA KIDATO CHA KWANZA NA CHEKECHEA-2014 MASOMO YANAYOFUNDISHWA NI HAYA YAFUATAYO: KOMPYUTA, ARABIC ,ENGLISH ,KISWAHILI , MATHEMATICS, GEOGRAPHY, HISTORY, CHEMISTRY, PHYSICS, BIOLOGY, CIVICS, COMMERCE, BOOKKEEPING NA ELIMU YA DINI YA KIISLAMU. SIFA ZA SHULE: -SHULE IMESAJILIWA KWA NAMBA S.537 NA S.738 -SHULE INA WAALIMU MAHIRI, WENYE UZOEFU NA NIDHAMU YA HALI YA JUU KAMA VILE SHEIKH RUSAGANYA, ABU BILALI, SOVU N.K -SHULE INA MAKTABA,UKUMBI NA MAABARA ZA KISASA KWA MASOMO YA SAYANSI. -SHULE NI YA KUMI BORA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM MATOKEO YA KIDATO CHA SITA-2013 -SOMO LA QURAAN HUSOMESHWA KILA SIKU ASUBUHI KABLA YA KUANZA VIPINDI. WAHI SASA NAFASI NI CHACHE NA IKUMBUKWE KATIKA KUJALI HALI YA KIPATO CHA WAZAZI WETU ADA NI NAFUU MNO NA INALIPWA KWA AWAMU MBILI TU. KAULI MBIU YETU NI: MLETE MWANAO APATE ELIMU BORA ILIYOSHEHENI MAADILI NA MALEZI MEMA YA KIISLAMU KWA MAENDELEO YA KIROHO NA YA KIDUNIA. USAILI HUFANYIKA KILA SIKU YA JUMAMOSI KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU YA MEZANI- 022-2762144 AU SIMU YA MKONONI 0713-215918 AU 0713-400079. WAHI SANA NAFASI NI CHACHE MNO!
Mahitaji ya Vifaa yanayohitajika kufikia hatua ya Zege la Jamvi PLOT No. 152 Block A, Masjid Jumuiyatil Islamia Ubungo Darajani.
Na Mahitaji 1 2 3 4 5 6 7 8 9 Nondo 12 MM Nondo 8 MM Binding Wire 20 MAWE 200 CM KOKOTO 70 CM Mchanga 40 CM Cement Mbao Cypruss Misumari JUMLA NDOGO Deni la Mkandarasi (mjenzi) JUMLA KUU
Tshs 2,160,000.00 480,000.00 52,000.00 5,000,000.00 5,250,000.00 4,725,000.00 1,080,000.00 30,000.00 19,657,000.00
220,000 880,000.00
35,657,000.00
Nb: haya ni Mahitaji kwa ajili ya Zege la Jamvi Kwa mawasiliano zaidi Tupigie Mwenyekiti 0754 462 050 Katibu 0719 760 777 Mwenyekiti Kamati ndogo ya ujenzi ( Goha) 0787 318 116. International Commercial Bank No A/c 00001/01/601059/01 au A/c 0000/01/ 0009/94/02. Au tutembelee katika Msikiti wetu uliopo Ubungo Darajani. Wabillah Taufiq
12
AN-NUUR
MAKALA
12
AN-NUUR
kuwa masuala hayo yanahitaji gharama kubwa za uendeshaji. Aidha Bw. Nahodha amesema wakati Zanzibar ikiendelea kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi, muungano utaendelea kubaki kuwa uti wa mgongo wa maendeleo ya ulinzi na usalama wa Zanzibar. Alisema kwamba licha ya mfumo wa muungano wa serikali mbili kujaa matatizo, lakini njia ya kuyapatia ufumbuzi matatizo hayo ziko huru badala ya kungangania muungano wa mkataba au serikali tatu ambao alidai haitakuwa salama na Zanzibar.
ambaye ametoa wito kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa kuwapa dhamana Masheikh kwani imekuwa kero kubwa kwa wananchi kila unapopita mitaani. Eddy alisema kuendelea kuwekwa ndani na kunyimwa dhamana Masheikh hao kunaleta kero kwa wananchi walio wengi ambao wamekuwa wakifuatilia habari za Masheikh hao ambao wana mchango mkubwa kwa jamii hasa ukizingatia Masheikh hao ni walimu wa vyuoni na wengine ni Maimamu wa Misikiti. Mkereketwa huyo ambaye alifuatana na Kamati ya watu sita ya Maridhiano iliyoongozwa na Mzee Hassan Nassor Moyo, alisema kwamba mbali ya kukosekana darsa na kusalisha kwa Masheikh hao lakini pia familia zao zimeathirika kiuchumi na kisaikolojia kutokana na kuwa waume ndio waliokuwa wakitizama familia na sasa kuwekwa ndani kumeathiri familia hizo. Tusiwatizame wao
Inaendelea Uk. 11
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.