Professional Documents
Culture Documents
com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1205 SAFAR 1437, IJUMAA , NOV. 27 - DES. 3, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Zanzibar
inaelekea
kubaya
Baada ya Karume kuwavusha salama
Wanaelekea kutangatanga Jangwani
Saamiriyyu wanawavuruga
ANNUUR NEW.indd 1
WA Z A N Z I B A R I
tutafakari
na
k u j i h a d h a r i .
T u m t a m b u e
S a a m i r i y y u
tumuepuke.
Hatutoi Nchi kwa
K a r a t a s i . Wa k i t a k a
wapindue, ni kauli za
akina Saamiriyyu.
Hao ni pamoja na wale
ambao wanatuambia
kuwa katika watoto
pacha, yule wa
Jamhuri halali, ila
mwenzie Zanzibar,
mwanaharamu.
Bila uamuzi wa busara
na kurejea kwenye haki
na ukweli, tutaonja joto
ya jiwe la Bani Israil.
Kutangatanga
Jangwani miaka arobaini
tukitafuta nchi,
Amani na Maendeleo,
hatutaipata.
Tu t a z a m a k a t i k a
Idhilali na hatutapata wa
kutunusuru wala kuona
mlango wa kutokea.Uk.9
11/26/2015 6:13:19 PM
Makala
Fethullah-Gulen
ANNUUR NEW.indd 2
AN-NUUR
25
35
45
40
20
30
MASUALA
1.Walioshi na Mtume (SAW) wakiwa wa Islamu wanaitwaje? Jawabu:
Sahaba.
2.Mwaka aliozaliwa Mtume (SAW) waitwaje? Jawabu: Mwaka wa Tembo.
3.Ami yake Mtume (SAW) jina lake. Jawabu: Abu Talib
4.Mtume Muhammad (SAW) alipomuoa Bibi. Khadija alikuwa na umri
gani na Bibi Khadija akiwa na umri gani? Jawabu: 25 Mtume (SAW) 40 Bi.
Khadija.
5.Jina la ami yake Mtume Muhammad (SAW) aliouwawa katika vita vya
Uhud. Jawabu: Hamza
6.Majina ya watoto wa kiume wa Mtume Muhammad (SAW. Jawabu:
Kassim, Abdalla, Ibrahim.
7.Chakula alacho mnyama Panda. Jawabu: Bamboo.
8.Mnyama Kangaroo maarufu anaonekana nchi gani? Jawabu: Australia.
9.Millennium 1,000 au 10,000 au 1,000,000. Jawabu: 1,000
10.Mwanadamu ana mbavu ngapi? Jawabu: 2
M A
W A
M A
M I
M O
125 45
12 56 24 35 33 23 33 43 11
22
570 CE 4
W A
MASUALA
1.Uislamu ni dini: (i)Inayopungua idadi kila siku (ii) Inakua kwa
kasi, (iii) Ina idadi kubwa Asia.
2.Uislamu unaruhusu kuoa mpaka wake wangapi? 1, 4, 0.
3.Mtume Muhammad kazaliwa mwaka 570 CE, 670 CE, 622 CE.
4.Vugu vugu la Waislamu Weusi Marekani linajulikana kama,
Nation of Islam, Black Muslim, Elijah Muhammed.
5.Waislamu walio wengi wanaonekana barani Africa, Asia, Ulaya?
6.Mtume (SAW) alikuwa hana mke mwengine alipoishi na Bibi
Khadija binty Khuwayld. Ndio au Sio?
7.Mtume alikuwa na umri wa miaka mingapi alipofariki mama
yake? 3, 6, 12.
8.Uislamu una pinga haki za mwanamke na inasisitiza
ukandamizwaji wa Wanawake. Ndio au Sio?
9.Quran imeteremshwa kwa kipindi cha miaka 23, 33, 43.
10. Aya ipi ilioelezea kuwa Leo nimekukamiliishieni Dini
yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni
UISLAMU uwe ndiyo Dini. Na mwenye kushurutishwa na njaa, bila
ya kupendelea dhambi, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehevu
Jee Unajua?
1. Misikiti 10 yenye haiba duniani wa mwanzo ni AlHaram uliopo Makka ukifwatiwa na Al-Masjid an-Nabawi
uliop Madina, Al-Aqsa-Palestina, Hassan II-Morocco, Sultan
Omar Ali Saifuddin-Brunei, Masjd Zahir-Malaysia, Masjid
Faisla-Islamabad/Pakistan, Taj ul uliopo Bhopal nchini India,
Masjid Badshaihi uliopo Lahore Pakistan na MAsjid SultaSingapore: http://www.wonderslist.com/10-most-beautifulmosques-in-the-world/
2. Nchi 10 zenye Waislamu wakazi wengi duniani
inayoongoza kuwa na idadi kubwa ni nchi ya Indonesia
ikifwatiwa na Pakistan, India, Bangladesh, Misri, Nigeria,
Iran, Uturuki, Algeria na Morocco: http://malaysiandigest.
com/features/555150-10-countries-with-the-largest-muslimpopulation-in-the-world.html au link hii: http://www.
mapsofworld.com/world-top-ten/world-top-ten-countrieswith-largest-muslim-populations-map.html
3.
Nchi inayoongoza kuwa na Waislamu wengi barani
Afrika kwa asilimia (%) inayoongoza ni Mauritania ikiwa na
asilimia 100, ikifwatiwa na Libya 99.8, Algeria 99.7, Comoro
98, Sudan 97, 96 Djibouti, 95 Niger, Misri 95: http://www.
muslimpopulation.com/africa/
4. Katika nchi za Ulaya Albania inaongoza kuwa na
asilimia kubwa ya Waislamu ikiwa na idadi ya asilimia 79.9
(%) ikifwatiwa na Bosnia Heregzovinian 60.06, Macedonia
34.9: http://www.muslimpopulation.com/Europe/
11/26/2015 6:13:22 PM
3
Na Mwandishi wetu
Washington-Mzalendo.
net
M S H I N D I
wa uchaguzi
atangazwe.
M a a m u z i
ya
Wazanzibari
yaheshimiwe. Bila haki
hakuna Amani.
Wakati vikao vya siri
v ya k u t a f u t a s u l u h u
ya m z o z o wa k i s i a s a
visiwani Zanzibar vikiwa
vikiripotiwa kuendelea,
juhudi za kuupatia
ufumbuzi mzozo huo
zimefika Ikulu ya Marekani
(White House).
Wanachama wa Jumuia
ya Wazanzibar wanaoishi
nchini Marekani (ZADIA)
kutoka majimbo tofauti
nchini humo, wakionyesha
m a b a n g o ya o m n a m o
Novemba 21 waliandamana
hadi kwenye Ikulu ya nchi
hiyo ikiwa ni katika juhudi
za kutafuta uingiliaji kati
wa kimataifa ili kuupatia
suluhisho mzozo huo.
Akizungumza na
waandishi wa habari mbele
ya Ikulu hiyo, Mwenyekiti
wa Jumuiya hiyo iliyoandaa
maandamano hayo Bw.
Omar Haji Ali, alisema
kuwa maandamano
h a y o ya m e k u j a i k i wa
ni juhudi za Jumuiya
hiyo kutafuta uingiliaji
kati wa kimataifa katika
kuukwamua mgando wa
kisiasa visiwani Zanzibar.
Bw. Omar Haji, alisema
kuwa maandamno hayo
pia yalikuwa na lengo la
kumkumbusha Rais Barack
O b a m a wa M a r e k a n i ,
kutekeleza ahadi yake
ya kuilinda demokrasia
Barani Afrika.
Katika hotuba yake
aliyoitoa kwenye Makao
Makuu ya Umoja wa Afrika
mapema mwaka huu, Rais
Obama alisema ... pale
ambapo raia hawawezi
kutekeleza haki zao, basi
ulimwengu una jukumu
la kukemea. Na Marekani
itafanya hivyo, hata
kama wakati mwengine
itakuwa inauma..., Bw.
Ali alikumbusha k wa
kunukuu matamshi ya
Obama.
Aliongeza kuwa
Wananchi wa Zanzibar
wameshindwa kutekeleza
haki yao kwa zaidi ya nusu
karne sasa na kwamba,
wakati umefika sasa kwa
u l i mweng u k uch ukua
jukumu lake.
Wa k a t i u m e f i k a
sasa kwa Marekani
siyo tu kukemea, lakini
pia kuchukua hatua za
kivitendo ili kuhakikisha
kuwa sauti za Wazanzibari
ANNUUR NEW.indd 3
Habari
AN-NUUR
zinasikilizwa na
kuheshimiwa, alisema.
Mwenyekiti huyo wa
ZADIA alipoulizwa ni hatua
gani watakazochukuwa
iwapo Serikali ya Marekani
haikuchukua hatua yoyote
kusaidia kumaliza mgando
wa k i s i a s a Z a n z i b a r ,
alisema wana imani na
Rais Obama na tayari
wa m e m f i k i s h i a b a r u a
ya malalamiko yao na
wanachosubiri ni jibu lake.
Alisema, imani yao ni
kuwa atachukua hatua
madhubuti, hususan
ikizingatiwa kuwa
Ubalozi wa Marekani
nchini Tanzania ulikuwa
wa kwanza kutoa taarifa
kuelezea kuwa uchaguzi
wa Zanzibar ulikuwa wa
haki na huru.
Aliongeza kuwa iwapo
hali itaendelea kubaki
kama ilivyo, basi ZADIA
itaelekea kwenye Umoja
wa Mataifa.
Katika maandamano
hayo yaliyowashirikisha
pia wapenda amani na
demokrasia kutoka sehemu
mbalimbali ulimwenguni,
waandamanaji walibeba
mabango yaliyokuwa na
maneno kama vile Mshindi
wa uchaguzi atangazwe,
maamuzi ya Wazanzibari
yaheshimiwe, bila
haki hakuna amani na
mengineyo.
Aidha waandamanaji hao
walipaza makelele wakidai,
tunataka matokeo yetu ya
uchaguzi..
Akizungumza na
Swahilivilla, raia mmoja
wa Marekani aliyeshiriki
kwenye maandamano hayo
alisema, Nilimpeleka
mwanangu kwenda
kusoma kule, bado ana
mapenzi na Zanzibar
Mshindi
wa u c h a g u z i
atangazwe.
Maamuzi ya
Wazanzibari
yaheshimiwe.
Bila haki hakuna
Amani.
na amenisimulia habari
nzuri za amani, utulivu na
ukarimu wa watu wake.
Amekuwa akifuatilia hali
ilivyo, na kwa hamasa
kubwa alipopata habari
za maandamano haya,
akaniomba tuje kuwaunga
mkono Wazanzibari katika
kudai haki yao
T u t a f a n y a
maandamano kuitaka
S e r i k a l i ya M a r e k a n i
kuingilia kati na kuweka
shindikizo kwa Serikali
ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ili mshindi
aliyeshinda atangazwe na
serikali ya umoja wa kitaifa
i u n d we Wa z a n z i b a r i ,
washirikiane wajenge nchi
yao, alisema mmoja wa
Wazanzibari anayeishi
Marekani.
Wananchi wa Zanzibar
wa l i p i g a k u r a k a t i k a
uchaguzi mkuu wa Oktoba
25 mwaka huu, lakini
Mwenyekiti wa Tume
ya Uchaguzi Zanzibar
(ZEC) Bw. Jecha Salum
Jecha, baadae Oktoba
28 alitangaza kufutwa
uchaguzi huo Mkuu
visiwani humo katika hatua
za mwisho za majumuisho
ya kura, kitendo ambacho
wa t a a l a m u wa S he r i a
wamesema kuwa
kinakwenda kinyume na
Katiba ya Zanzibar.
Wachambuzi wanaona
kuwa hatua hiyo ya
Bw. Jecha ilikuja wakati
asilimia kubwa ya
matokeo yaliyokuwa
yameshatangazwa
yalikuwa yamempa
ushindi mgombea wa urais
wa Zanzibar kutoka chama
cha upinzani CUF, Maalim
Seif Shariff Hamad.
Kitendo cha kufutwa
kwa uchaguzi huo ambao
wachunguzi wa nje na
ndani waliulezea kuwa
ulikuwa wa haki na huru,
kimezua mtafaruku wa
kisiasa visiwani Zanzibar,
na juhudi za ndani na nje
zimekuwa zikifanyika ili
kumaliza mgogoro wa
kisiasa visiwani humo.
N o v e m b a
1 9
Wazanzibari wanaoishi
nchini Uingereza walikuwa
wa m wa n z o k u f a n ya
maandamano katika nchi
11/26/2015 6:13:22 PM
Tahariri
AN-NUUR
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.
E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top
Usangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam
www.annuurpapers.co.tz
R a i s k u m t e u a Wa z i r i
anayepimika kwa matokeo
ya utendaji wake na wenye
maono thabiti juu ya taifa
lake ni bora na vizuri zaidi.
Mtendaji wa serikali bora,
a n a ye p i m a m a t o k e o ya
utendaji wake na mwenye
maono thabiti juu ya nchi
yake, ni dhahiri ataweza
kutatua na kupunguza kero
nyinyi zaidi, kuliko yule
atakayeteuliwa kwa mazoea
na ambaye amedhihirisha
kufanya kazi kwa mazoea
huko alikopita.
Katika ulimwengu
wa s a s a wa u s h i n d a n i ,
ulimwengu unaomlazimu
kila mtu kusaka kwa udi
na uvumba mafanikio kwa
ajili ya mustakabali mzuri
wa maisha yake, familia na
jamii kwa ujumla. Viongozi
wanatakiwa kuacha
kuongoza kwa mazoea, lakini
pia Watanzania wanatakiwa
kuacha kuchagua viongozi
wao kwa mazoea.
Habari za kujuana katika
kusaka watu wa kuongoza
taifa au katika utendaji
serikalini na katika jamii
k wa u j u m l a , h a b a r i z a
kupeana nafasi kwa kigezo
cha huyu ni mwenzetu ,
ametumikia chama muda
mrefu nk. ni chanzo cha
uzembe na sababu kubwa
ya kuua taifa kiuchumi
na maendeleo ya jamii na
hatimaye kudhoofisha ustawi
wa wananchi wengi.
Ukiacha sintofahamu
iliyopo Zanzbar, tayari
Tanzania kumeshafanyika
Uchaguzi
Mkuu,
waliochaguliwa, hususan
Rais, wabunge na madiwani.
Hawa tunaweza kusema ni
viongozi waliochaguliwa na
wananchi wenyewe na kwa
namna moja au nyingine,
watakuwa wakiwajibika
moja kwa wananchi
waliowachagua.
Lakini wapo viongozi
n a wa t e n d a j i wa k u b wa
wa serikali, ambao pamoja
na kwamba wengine
wanatokana na hao hao
wabunge, lakini wanapewa
m a m l a k a ya k i u t e n d a j i
serikalini na Rais.
Kwamba Rais anateua
Mawaziri na Manaibu Waziri
watakaokuwa wanamsaidia
kazi. Wao ndio watakaokuwa
wapangaji, waidhinishaji,
watendaji, wafuatiliaji na
wasimamizi wa rasilimali
za serikali zinazoelekezwa
kwa ajili ya maendeleo ya
wananchi.
ANNUUR NEW.indd 4
AN-NUUR
SERIKALI imetoa
mwongozo wa ufundishaji
na ujifunzaji wa somo la dini
ambao unaondoa masuala ya
ibada.
Mwongozo huo na sera
hiyo mpya ya ufundishaji
wa Somo la Dini kwa watoto
wa shule za msingi, utakuwa
mtihani wa mwanzo kwa
Rais Dr. John Pombe
Magufuli kwani ni jambo
ambalo lilikwisha kupingwa
na Wakristo na Waislamu
l i l i p o l e t wa n a s e r i k a l i
zilizotangulia.
Mwongozo huo ambao
utatumika katika kuandaa
mitaala ya usomeshaji wa
Somo la Dini katika elimu
ya msingi (darasa la I-VI),
unaelekeza kuwa Somo
la Dini lifundishwe kama
taaluma na si ibada.
Hoja ya serikali ni
kuwa ibada haiwezi
kuwaunganisha Watanzania
wa dini tofauti, bali kuwaletea
chuki, mifarakano na hata
kuleta uvunjifu wa Amani.
N a k wa m a a n a h i y o ,
kinachotakiwa sasa ni Somo
la Dini kufundishwa kwa
lengo la kuwaunganisha
Wa t a n z a n i a we n ye
Imani tofauti za kidini ili
kuwafanya wapendane na sio
kuwafanya wanafunzi kuwa
wachamungu kwa mujibu
wa dini zao.
Kwa mujibu wa taarifa
zilizopatikana kutoka
Islamic Education Panel,
chombo kinachohusika na
kuandaa mitaala na vitabu
vya usomesjaji wa Somo
la Dini ya Kiislamu, hivi
sasa serikali kupitia Taaasisi
ya Elimu Tanzania (TET)
ishasambaza mwongozo huo
kwa wadau wa Elimu na hivi
karibuni kitaitishwa kikao
cha kuupitisha na kuubariki
mwongozo huo.
Wadau
muhimu
wanaotarajiwa kuitwa katika
kikao hicho ni taasisi kuu za
Kiislamu na zile za Kikristo.
Awali kulifanyika kikao
ambapo taasisi hizo zilipewa
kabrasha la Mwongozo huo
na kuambiwa kwamba mara
baada ya uchaguzi mkuu
wataitwa tena ili kuupitisha.
Hata hivyo, taarifa kutoka
msingi wa maadili.
Watoto wadogo wa shule
ya msingi kufundishwa elimu
ya dini ili wawe waumini
wazuri wa dini kwa mujibu
wa imani zao ni jambo jema,
ambalo litawaimarisha pia
kuwapenda na kuwahurumia
watu wengine, hata kama sio
raia kwani wote ni waja wa
Mwenyezi Mungu.
Imesema sehemu ya barua
ya IEP kwa Mkurugenzi
Taasisi ya Elimu ambayo
imenakiliwa kwa Baraza
la Maaskofu, Jumuiya ya
Kikristo Tanzania na Katibu
Mkuu, Wizara ya Elimu.
Barua hiyo ya hivi karibuni
ikaongeza kuwa ni jambo
lisilokubalika, mwalimu
Muislamu kuwafundisha
watoto wadogo wa shule ya
msingi wa Kikatoliki Elimu
ya dini ya Kikristo au
kinyume chake, kwa hoja tu
kwamba anaifundisha kama
taaluma.
IEP iliongeza hoja hiyo kwa
msingi kwamba kama Somo
la Dini litafundishwa kama
taaluma, ina maana anaweza
k u c h u k u l i wa m wa l i m u
Muislamu akafundisha
somo la Dini ya Kikristo na
kinyume chake.
Ikasisitizwa katika barua
hiyo kwamba Mwalimu
mahiri wa wa Elimu ya Dini
ya Kikatoliki, lazima awe
Mkatoliki mzuri anayeakisi
mafundisho ya dini hiyo, na
sio tu mwalimu japo akijua
Biblia vizuri lakini si mfuasi
wa dini hiyo.
Na kwamba mwalimu
wa namna hiyo atakuwa
anafundisha mambo
a s i y o ya a m i n i n a h i v y o
hawezi kumuathiri mtoto
kimalezi.
Katika hoja ya serikali ya
kuhusisha dini na uvunjifu
wa Amani, IEP wanatoa hoja
kuwa machafuko mengi
yanayosababisha uvunjifu
wa Amani na hata ukitizama
hapa nchini, ni kwa sababu
za kisiasa.
Wanasema, matukio mengi
ya uvunjifu wa amani na
hata watu kupoteza maisha,
yaliyojiri nchini baina ya
2010 na 2015, yametokana
na uchochezi na mihemko
ya kisiasa.
Inaendelea Uk. 9
11/26/2015 6:13:23 PM
Habari za Kimataifa
5
Na Shaaban Rajab
AKATI wazee wa
Tanzania wakiishi
maisha ya taabu
katika uzee wao, wakiishi
bila kuwepo huduma
za matuinzo za serikali,
wakikosa hata huduma za
matibabu licha ya kuwepo
mpango wa matibabu
bure kwa wazee, waja
wazito na watoto, serikali
ya China imekuwa mfano
wa kuigwa kwa kuenzi
maisha ya wazee.
Serikali ya Tanzania
kwa muda mrefu
imeshindwa kuwa na
sera zinazotekelezeka za
kuwahudumia wazee.
Serikali wala haionekani
kushughulishwa na suala
zima za kuwahudumia
wazee wetu, licha ya
kutumia nguvu zao
nyingi kuzaa na kulea
kizazi cha sasa cha
watanzania. Kutumia
nguvu zao kutumikia
Taifa letu katika nyanja
mbalimbali za kihuduma
na kimaendeleo. Leo
wanaachwa na wastani
wa umri wao wa kuishi
umeshuka kutokana na
kukosa huduma nzuri za
malezi.
Hata zile kambi chache
za kuwatunza kama ile
ya Nunge Kigamboni na
ile Funga Funga iliyopo
mkoani Morogoro, badala
ya kuwa mfano mzuri wa
kuwaenzi wazee wetu kwa
kuwapa huduma nzuri na
bora za malezi, zenyewe
zimegeuka kuwa mfano
kambi za kuwadhalilisha
babu na bibi zetu. Wanaishi
kwa kutegemea majaaliwa
ya wale wanaojisikia kutoa
misaada na sadaka. Kwa
kutizamama mifano ya
kambi hizi mbili za serikali,
hakuna mtanzania ambaye
anatamani mzee wake
akaishi huko kwa udhalili.
Serikali imeshindwa
kutambua ukweli kwamba
kila mtoto au kijana wa
leo ni mzee wa kesho.
Kwa msingi huo ni wajibu
serikali kuandaa sera ya
kulea wazee pamoja na
kuweka mazingira safi na
salama ya kuwawezesha
wazee kuishi maisha ya
stara na salama hata baada
ya nguvu zao za uzalishaji
kwisha.
Licha ya kwamba
desturi na utamaduni
wa kitanzania haujazoea
kuwatunza wazee
katika vituo vya
serikali, lakini ni ukweli
usipopingika kwamba
kama kungekuwepo na
huduma za kuridhisha
za wazee katika vituo
vichache vilivyopo, wezee
wengi wangehifadhiwa
huko. Hii ni kutokana na
ukweli kwamba si kila
familia inaweza kuishi na
kuwatunza wazee wao.
Kuna haja ya serikali
yetu, kwa makusudi kabisa
kujifunza kwa swahiba
ANNUUR NEW.indd 5
AN-NUUR
11/26/2015 6:13:28 PM
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 6
11/26/2015 6:13:28 PM
7
Mhe. Ban Ki Moon
Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa
Mhe. Magniz Lyketoft
M/kiti wa Mkutano Mkuu
wa Umoja wa Mataifa
Mhe. Mathayo Rekroft
M/kiti wa Baraza la
Usalama
Mhe. Ford Sik M/
kiti wa Kamati husika ya
haki za Wapalestina zisizo
hamishika.
Napenda kuchukua
nafasi hii kufikisha
salamu za Palestina
na za wananchi wake,
waliohudhuria na kwa
marafiki kote duniani,
walioshiriki nao katika
maadhimisho ya siku hii
ya kimataifa ya kuungana
na Wapalestina.
Hii ni baada ya
miezi miwili tu tokea
kupeperushwa kwa
shangwe na nderemo,
bendera ya Palestina mjini
New York Marekani,
jambo linalotufurahisha
wote.
Rais pia amechukua
nafasi kuzishukuru nchi
zote zilizokubali uwepo
wa dola ya Palestina, pia
zile zote zilizochangia
ufanisi wa suala hilo
kupitia kura zao katika
Umoja wa Mataifa na
sekta zake zote.
Mchango huo ni
katika ufanisi wa sekta
na maazimio mbalimbali
ya h u s u y o Pa l e s t i n a ,
kikiwemo kituo chake
ndani ya umoja wa
Mataifa kitachosaidia
kuleta amani ya kweli
Mashariki ya Kati na
duniani kwa ujumla.
Aidha amerejea
shukrani zake kwa taasisii
zisizokuwa za kiserikali,
asasi za kiraia, marafiki
na wadau wote wa
uhuru na amani duniani,
wanaosimama kidete na
ndugu zao Wapalestina
katika kufikia uhuru
wao, ili kuleta amani ya
kudumu.
A m e o n g e z a k u wa ,
Umoja wa Mataifa
umeshughulikia suala la
Palestina tokea mwanzo na
kuliweka katika agenda za
vikao vingi vya kimataifa,
huku ikilijengea mikakati
na maazimio mbalimbali
ya s i y o e p u k i k a k wa
lengo la kufikia suluhisho
lifaalo.
Hivyo tunathibitisha
uwepo wa suala hilo kwake
hadi hapo patapofikia
ufumbuzi unaoridhiwa na
pande husika kwa mujibu
wa kanuni za kimataifa.
Hivyo, tunapongeza
juhudi zinazofanywa na
Katibu Mkuu wa Umoja
wa mataifa Mhe. Ban Ki
Moon, pia kamati husika
ya haki za Wapalestina
zisizo hamishika, iliyo
chini ya M/kiti wake
balozi wa Senegal Mhe.
ANNUUR NEW.indd 7
MAKALA
AN-NUUR
inapuuza mpango wa
amani na kuendeleza
uvamizi wake wa
kimabavu.
M i a k a
m i n g i
imetahadharisha matokeo
ya yanayoendelea mjini
Jerusalem iliyovamiwa
kimabavu na maeneo
yake ya jirani, yakiwemo
mambo kadhaa mabaya
dhidi ya Wapalestina,
huku walowezi wakiwa
chini ya kivuli cha majeshi
ya kizayuni ya Israeli ili
kubadili historia ya Msikiti
Mtukufu wa Agswa
iliyopo tokea mwaka 1967.
Hii inalenga kugeuza
migogro ya kisiasa na
kisheria iwe ya kidini
zaidi, jambo ambalo
litaleta matokeo mabaya
mno kwa wote na ambalo
halikubaliki kamwe.
Hivyo ni lazima kusitisha
juhudi za kuendeleza
m a k a z i ya wa l o w e z i
na zile zote za Israeli
zinazolenga kuharibu
bali kufuta kabisa historia
ya Wapalestina na mji
mtukufu ili Israeli ichukue
Msikiti Mtukufu na eneo
zima.
K wa k u f e l i j u h u d i
za jamii ya kimataifa
k u i e p u s h a Pa l e s t i n a
na dhuluma za Israeli,
imepelekea wananchi
wa Pa l e s t i n a k u k o s a
mustakabali mwema, hasa
vijana. Tunatilia mkazo wa
kufanyika juhudi zaidi za
kimataifa ili kuleta amani
Mashariki ya kati, kwa
msingi wa kuwepo dola
mbili iliyopo tokea mwaka
1967.
Kwa mujibu wa
maazimio ya Umoja wa
M a t a i f a ya l i y o f i k i wa
mjini Madrid-Hispania
kuhusu amani na usalama
wa Kiarabu yanataja pia
kumaliza uvamizi huo wa
Israeli, kwani hakuna haja
tena ya kupoteza muda
bali ni lazima ifanyike kazi
ya ziada ili kufanikisha
mpango wa amani.
Rais ameendelea zaidi
kusema kuwa, ninyi nyote
mnajua kwamba lengo
letu ni kuleta amani, ndio
maana bado tunaendelea
kutoa fursa ya hilo. Mara
kadhaa Israeli imeharibu
juhudi hizo, ili iendelee
kujenga makazi ya
kilowezi na ukuta wa
kibaguzi katika ardhi ya
Palestina.
Tunajiuliza nini lengo
la Israeli katika kuweka
kiasi cha makazi laki sita
(600,000) ndani ya ardhi
ya Palestina, huku ikielewa
kuwa kufanya hivyo ni
miongoni mwa uhalifu
wa kivita kwa mujibu
wa maazimio ya Geneva
ya m wa k a 1 9 4 9 , p i a
inapingana na ufumbuzi
wa kuwepo dola mbili.
Hatua ya Israeli
kubomoa misingi
iliyowekwa kisiasa,
kiuchumi na kiusalama,
inatufanya tushindwe
kuendelea na utekelezaji
wa maazimio hayo upande
mmoja bila ya Israeli.
Isipokuwa tunaendelea
kutekeleza sheria na ahadi
za kimataifa kwa nia njema
ili kufikia mpango wa
amani.
Hivyo, tutaendelea
kujiunga na jamii za
kimataifa na mikataba
yake ili kulinda haki
zetu, huku tukihakikisha
usalama wa taifa letu
kwa njia mbalimbali za
kisheria na kiusalama
tulizo nazo. Hakika
kuliondolea dhuluma
taifa letu ni jukumu la
kitabia na kibinaadamu,
tunazidi kuiomba jamii
ya kimataifa kuilazimisha
Israeli kuachana na
kuikandamiza Palestina,
bali ifanyie kazi maazimio
ya kimataifa ili kumaliza
hali hiyo.
Kwa upande mwingine,
Rais Abbas amehoji kuwa,
hadi lini itaachwa Israeli
ikikiuka maazimio ya
kimataifa kana kwamba
ni dola iliyo juu ya sheria?
Huku wananchi wa
Palestina wakiendelea
kukaliwa kimabavu na
kudhulumiwa haki zao
kwa maslahi ya walowezi
wa c h a c h e wa k i g a i d i
wa n a o f u m b i a m a c h o
maovu yao na adhabu
yao?
Hakika jamii ya
kimataifa inatakiwa zaidi
leo kuilinda Palestina
muda wote wa uvamizi,
huku ikiisaidia kupata
haki yake na kupanga
mustakabali wake,
ikiwemo haki ya kupata
uhuru wake na kuwa dola
yenye mji mkuu wake
Jerusalem ya Mashariki
kama ilivyo katika mipaka
ya mwaka 1967.
Hii itatuwezesha
kuishi kwa amani na
jirani yetu Israeli huku
tukiheshimiana kwa
mujibu wa makubaliano
ya Umoja wa Mataifa na
kimataifa, pia kuwepo
suluhisho la wakimbizi wa
Palestina kwa mujibu wa
agizo la Mkutano Mkuu
waUmoja huo namba 194,
inayotaja pia kuwatoa
wafungwa na waliotekwa
nyara wote wa Kipalestina
waliopo katika jela za
Israeli.
Rais ametilia mkazo
kwamba, lengo ni
kumaliza kabisa uvamizi
wa Israeli katika ardhi
ya Palestina, pia kupata
uhuru wake na uongozi
wake na sio kumdhulumu
yeyote kama wanavyodai
baadhi ya watu. Ni dola
itayosifika na yote mazuri
bila ya ubaguzi wa aina
yoyote, hivyo tutaendelea
na harakati kwa msaada
wa m a r a f i k i n a w o t e
wengine ili kufikia lengo
hilo.
Vile vile mikono yetu
bado imenyooshwa kutaka
amani ya kweli kwa misingi
ya sheria za kimataifa na
maazimio ya Umoja wa
Mataifa, kinyume na hivyo
ni kurefusha muda wa
mgogoro, kukata matarajio
mema na kuzidisha
kinyongo na chuki kwa
walengwa.
Wananchi wa Palestina
ni haki yao kupata neema
ya uhuru na yote mazuri
chini ya dola yao huru
yenye mji mkuu wake
Jerusalem ya Mashariki,
hili ni jambo la lazima ili
kuleta amani, usalama na
utulivu katika Mashariki
ya kati. Amani ndio lengo
letu kuu na ndio maslahi
hasa ya Palestina, nchi
za Kiarabu na dunia kwa
ujumla.
Rais Mahmuud Abbas
amemalizia hotuba yake
kwa kusema kwamba;
Hilo linawezekana endapo
tu kukiwepo uongozi
thabiti na uthubutu wa
k isiasa unaoong ozwa
na nia njema, kwa lengo
la kujenga mustakabali
mwema kwa wote.
Contact us: P.O Box
20307, 612 UN Road
Upanga West, Dar es
Salaam Tel: 2152813,
2150643 Fax: 2153257
Email: pict@pal-tz.
orgWebsite: www.pal-tz.
Org.
11/26/2015 6:13:29 PM
Makala
Tathmini ya uchaguzi na
Viburi Mauti Zanzibar
WA N Z A n i a n z e
kwa kuwataka
radhi waungwana
wote hapa barzani
kwa kuadimika kwangu
au kukaa kimya kirefu
japokuwa niliutolea
u f a f a n u z i u k i m ya h u u
kabla, lakini kwa kuwa
nimezidisha muda, basi
wajibu kuanza kwa
kutakana radhi. Lakini pia
kabla ya yote au awalani
ya hayo, ni lazima sana
kuanza kwa kumshukuru
Mola wetu kwani bila yeye
hapa leo tusingekutana
kuongea, kunongonezana
au kuambizana neno.
Uchaguzi umekwisha
kama tunavyojua na
mshindi anajulikana, ingawa
hakutangazwa bado na
wahusika na tunavyoambiwa
kuwa ametenda dhambi
mbaya sana iliyo juu
ya uhaini kwa kuwa
amejitangaza mwenyewe na
hilo ni kosa kwa sheria za
Zanzibar kama nchi, ZEC,
polisi au CCM kwa ujumla.
Binafsi silioni kosa hapa kwa
sababu halipo. Mgombea
wa urais Maalim Seif Sharrif
Hammad wa chama cha CUF
hakuvunja sheria yoyote
na wala hajatamka kuwa
yeye ndie RAIS wa Zanzibar.
Alichokisema na kudai ni
kutaka chombo husika yaani
Z E C wa m t a n g a z e ye ye
mshindi baada ya kuweka
wazi au kuonyesha kura zake
HALALI zilizothibitishwa na
kuwekwa sahihi na mihuri
na wahusika wote na vituo
vyao wa Tume ya Uchaguzi
Zanzibar na zile za mpinzani
wake.
Kuhusu Zanzibar kama
nchi, nafikiri tumeshawahi
kupata jawabu ya kitendawili
hicho wakati wa ile kesi
iliyowakabili watuhumiwa
waliotaka kupindua visiwa
hivi na kesi kufika mahakama
ya kuu/rufaa ya Tanzania na
ndipo tulipo pata jawabu
ya kuwa hapa hakuna nchi,
kuna nini... hilo mtanisaidia.
Kilichotendeka Oktoba
25 siku ya uchaguzi ndio
kile kile nilisema sana hapa
kuwa chama changu, yaani
CCM kitashindwa vibaya.
Nimeandika sana kuhusu
hatma hii hapa na wengi
mtakuwa mashahidi wangu
kwa kuwa haya sio mageni
k w e t u s o t e h a s a wa l e
tunaotumia muda mrefu
na kuumiza vichwa vyetu
kwa kuitakia kheri nchi hii
isiyotakiwa na Tanganyika.
Nilifika kuweka wazi kuwa
nitakuwa tayari kuja mbele
yenu tena hapa kuwataka
radhi ikiwa CCM itashinda
uchaguzi huu, tutashinda
pia niliyajua zamani kuwa
hapa hapana uchaguzi, bali
tujitayarishe na uchafuzi na
ndio huu unaoendelea sasa
baada ya mwenyekiti wa
ZEC bwana Jecha kuamua
kuufuta uchaguzi na kuanza
machafuzi ya makusudi ili
kukinusuru chama chetu
baada ya kuona matokeo
halali na halisi ya uchaguzi
ANNUUR NEW.indd 8
AN-NUUR
wenyewe.
Ni vema tukayadhukuru
yote ya nyuma ili tuweze
kujua wapi tulikosea au wapi
hakuhitaji marekebisho na
nini la kufanya tuepukane na
maafa tunayotengenezewa
na viongozi wetu wa CCM
Zanzibar na Tanganyika
waliopo madarakani na
wale waliostaafu, lakini bado
wanafanya kazi za chama
Cha Mapinduzi kwa malipo
wanayoyajua wao wenyewe.
Kwa sababu hakuna karatasi
au vocha hata moja utakayo
iona inayoidhinisha malipo
ya viongozi hao akiwemo
Bwana Ali Hassan Mwinyi.
Sasa la kujiuliza safari zote
hizi za Zanzibar/Dar za kila
kukicha, zinafanywa kwa
mapenzi ya nchi peke yake?
Au chama peke yake? Au
kuna tija gani ndani yake?
Sababu kubwa ya
mwenyekiti wa ZEC kufuta
uchaguzi inayopewa
kipaumbele hapa visiwani na
watetezi wengi kama si wote
wa chama changu cha CCM
isipokuwa mimi, au baadhi
yetu tusiopenda au kufarijika
kwa kujidanganya makusudi
kwa sababu kuna uwezekano
mtu ukajidanganya kwa
b a h a t i m b a ya , n i k u l e
kusema kuwa Pemba ndio
kumetokea uchafuzi wa hali
ya juu na huko ni sawa na
kusema kuwa hakukuwa na
wasimamizi wala ukaguzi
wa kura hata uhesabuji wa
kura pia ulifanyika chini
ya miti kwa kuwa ofisi
zilikuwa zinavuja maji na viti
vinawasha kama upupu. Pia
nambari za uhakiki wa kura
na vitambulisho zilifutwa
na kuandikwa kwa wino
baada ya kukarabatiwa. Huu
ni uongo uliojaa uzandiki.
Pemba hawana bahati siku
zote kwa sababu wameamua
kwa kujua tena kwa ridhaa
ya o n a k wa m a k u s u d i
matupu kuikataa CCM
miaka yote na kuinyima kura
hata ya balozi wa nyumba
na Tanzania, ni shamba la
shemeji yetu na hati miliki ya
eka hizi anazo dada yetu chini
ya mto kwa amani kabisa
hatukuwa na budi kulala
usingizi mnono kwa sababu
shemeji hawezi kuipata hati
miliki ya shamba hili bila
kumuamsha dada yetu. Kitu
ambacho hatukujua, hati
miliki haikuwepo uchagoni
kama tulivyodhani. Wenye
nchi walikuwa nayo
mikononi siku nyingi wala
hawakulala usingizi. Siku
imefika wanataka nchi yao
siku za kucheza na kuimba
mguu mbele mguu nyuma
zimekwisha, sisi ndio
tunataka uchaguzi urudiwe
ili tuendelee kuburudika
n a m u z e k a wa p i h a ya
tumeyakaanga wenyewe kwa
miaka yote hii tuliyoifanya
dhulma kwa viumbe hawa
wa kila rangi wanaopumua
h a p a v i s i wa n i n a wa l e
waliotangulia. Tumehutubia
ubaguzi wakati wote wa
kampeni tukiongozwa na
borafya huku viongozi
wa juu wakiwa nyuma ya
majukwaa wakitoa baraka
zao! Leo tunavuna matunda
ya ubaguzi tuliyo yapigia
debe kama wendawazimu
k wa
k u wa h o f i a
Waislamu wenzetu sijui
w a n g e l i k u wa m a k a f i r i
tungeliwasherekekea vipi?
Zanzibar kwa sasa
tunaenda kama MV
Jamhuri. Kwa wale wanao
ikumbuka yaani bega moja,
viburi vilivyojaa mauti
ndio vinavyoongoza visiwa
hivi. Kwa sasa tumechoka
na amani ya miaka mingi.
Hatuna budi kuitafuta shari
kwa bei yoyote. Hayo ndio
yaliyomo ndani ya mioyo
ya watawala wetu ambao
kwa sasa neno watawala
ndio neno sahihi kabisa kwa
kuwa hawana ridhaa yetu
kutuongoza na hatutaki
kuongozwa kwa nguvu au
11/26/2015 6:14:10 PM
9
Inatoka Uk. 4
N a k wa m a a n a h i y o ,
kinachotakiwa ni kuimarisha
Somo la Uraia (Civics), ili
liweze kuwaweka pamoja
watoto wa dini zote na
kuwapatia mafunzo yote
yanayohusu kuwa raia wema.
Pengine la kutaja hapa
kwa muktadha wa nukta hii
ya IEP ni kuwa mauwaji ya
mwaka 2001 mara baada ya
uchaguzi mkuu, haikuwa
k wa s a b a b u z a wa t o t o
wa Pemba wanafundiswa
sana kuswali na kusimama
Qiyamul layl.
Lakini hata ukitizama
zogo lililotokea Arusha hadi
kuuliwa watu baada tena ya
uchaguzi mkuu 2010 huku
wengine wakitamba kuwa
wataifanya nchi isitawalike,
haikuwa kwa sababu watoto
wa Kikatoliki na Kiislamu
walisomeshwa na kuhimizwa
kunyenyekea katika Sala zao.
Hivi sasa kuna mgogoro
unaofukuta Geita unaotishia
hali ya amani kutokana
n a k u u l i wa a l i y e k u wa
Mwenyekiti wa CHADEMA
mkoani humo, Bwana
Alphonce Mawazo.
Wanaotuhumiwa
kumuuwa Mawazo,
hawajafanya jinai hiyo kwa
sababu Tanzania imechelewa
kufuata nyayo za Liberia
kufundisha Somo la Dini
kama taaluma.
Hivi sasa Charles
McArthur Ghankay Taylor
anatumikia kifungo cha
Na A. S. M Chachika
NIMESOMA kwa
m s h i t u k o t a a r i f a ya
Polisi Zanzibar juu
ya kushitakiwa watu
wanaodaiwa kuchafua
uchaguzi mkuu Zanzibar.
Na ikatajwa katika jumla
ya madai kwamba kuna
watu walikutwa na visu
na mapanga katika vituo
vya kupigia kura.
Akifafanua miongoni
mwa makosa hayo
ni pamoja na kukutwa
watuhumiwa na silaha
katika vituo vya uchaguzi
kama vile visu na mapanga,
kuvamiwa au kupigwa
mawakala na kutolewa
mawakala katika vituo vya
kupigia kura.
Limeandika gazeti la
Zanzibar Leo katika toleo
lake la jana Novemba 26,
2015, likinukuu taaifa ya
Naibu Mkurugenzi wa
Upelelezi Mashitaka ya
Jinai, Salum Msangi.
Ta a r i f a y a A f a n d e
Salum Msangi kama
alivyonukuliwa na gazeti
hilo ikasema kuwa mengi
ya matukio hayo ya kihalifu
na kuchafua uchaguzi
yalifanyika Pemba, japo
na Unguja yalikuwepo.
N i m e s e m a
nimeshtushwa kwa sababu
kubwa mbili. Moja ni
kuwa siku mbili kabla
ANNUUR NEW.indd 9
Makala
AN-NUUR
WA Z I R I M k u u , M h e .
Majaliwa Kassim Majaliwa.
miaka 50 katika moja ya
magereza ya Uingereza baada
ya kupatikana na hatia ya
uhaini wa kivita na mauwaji
yaliyofanyika wakati wa vita
ya wenyewe kwa wenyewe
S i e r r a L e o n e . A l i p e wa
hukumu hiyo na Mahakama
Maalum ya Umoja wa Mataifa
juu ya Sierra Leone (UNbacked Special Court for Sierra
Leone-SCSL).
S i e r r a
L e o n e
haikutumbukia katika
m a c h a f u k o n a m a u wa j i
yaliyokuja kumtupa Charles
Taylor katika gereza la The
Hague kwa sababu ilikuwa
haina Mwongozo wa
Ufundishaji na Ujifunzaji wa
Somo la Dini uliotayarishwa
na serikali isiyo na dini.
Lakini ilikuwa ni
mambo ya siasa na ugomvi
wa wakubwa kugombea
dhahabu.
Juzi hapa kuamkia
uchaguzi mkuu, Rais Mstaafu
Jakaya Mrisho kikwete,
alitangaza kuimarishwa kwa
jeshi na polisi wakimiminiwa
vifaa.
S e r i k a l i h a i k u wa n a
wa s i wa s i k wa m b a k wa
vile watoto wa Kikristo na
Kiislamu katika shule za
msingi, hawasomi dini kama
taaluma, basi watatengana na
kugombana katika masiku ya
uchaguzi mkuu.
Na hivi sasa moshi unafuka
Zanzibar, wala likitokea
la kutokea haitakuwa kwa
sababu Zanzibar wao hawapo
katika mpango huu wa TET
kusomesha Somo la Dini
kama taaluma Tanganyika.
Juu ya hoja ya serikali
kuwa somo la dini
limeshindwa kutoa raia
wema wenye maadili na
ndio maana matukio ya uovu
yamekithiri, IEP imesema
kuwa wa kulaumiwa ni
serikali yenyewe.
Katika kulifafanua hilo
wakasema kuwa wakati
viongozi wa serikali
wakihimiza watu wa dini
k u f u n d i s h a wa t u t a b i a
njema na kukemea vitendo
vya uasherati na mavazi
na ukizingatia pia
kwamba Polisi hao hao
ndio walikuwa wakilinda
usalama katika vituo vya
kupigia na kuhesabia kura,
lakini hakuna tukio lolote
ambapo walikamata watu
wakiwa na silaha ambao
walidhuru watu na silaha
hizo kiasi cha kuvuruga
uchaguzi. Kushtuka
kwangu kunatokana
na jinsi taarifa katika
mtandao zilivyofuatana
na hili analosema Afande
Msangi.
N a s h t u k a m a r a ya
pili kwa kuona taarifa
nyingine katika mitandao
ya kijamii ikitoa tahadhari
kwamba kuna mpango
umeandaliwa ambapo
watatumika wahuni wa
ndani au watu wa nje ya
nchi kulipua mabomu.
Mpango wa kuutatua
mzozo wa Uchaguzi kwa
kutega mabomu, ndivyo
taarifa hizo zinavyosema
na kufafanua kuwa lengo
ni kuleta mkanganyiko na
kuzuiya juhudi zozote za
kuleta utatuzi wa amani
ili yale yanayotakiwa na
waliohusika na kufuta
uchaguzi yatimie.
Sasa hapa lazima
nishtuke kwa sababu kama
11/26/2015 6:14:11 PM
10
Na Omar Msangi
TA A S I S I y a E l i m u
Ta n z a n i a ( T E T )
imetoa Mwongozo
wa Ufundishaji na
Ujifunzaji wa Somo la
Dini katika Elimu ya
Msingi Tanzania Bara.
Mwongozo huu unapiga
marufuku kusomesha
Somo la Dini kama Ibada,
bali sasa lisomeshwe
kama taaluma. Hoja
ya TET ni kuwa Somo
la Dini likisomeshwa
kwa mwelekeo wa
kumfanya mtoto kufanya
ibada na kuwa mchaMungu, itavunja umoja
n a m s i h i k a m a n o wa
Wa t a n z a n i a n a h a t a
kuvuruga amani iliyopo.
Kwamba somo likitoa
wahitimu Waswaliji na
wafungaji wazuri wa
Kiislamu, watajiona bora
kuliko watu wengine,
kujenga chuki, mfarakano
na mwishowe kuhatarisha
amani.
Ni maoni ya TET
(Serikali) kuwa Somo
la Dini likisomeshwa
kama taaluma, litakuwa
chombo madhubuti
cha kuwaunganisha
Inatoka Uk. 9
ya kusahau tofauti zao,
kuweka kando ukubwa
wao katika taasisi zao
na kuangalia umuhimu
wa kuwaondolea
Wa z a n z i b a r i m a d h i l a
yaliyokuwa yakiwasibu.
Tu l i f i k i a u a m u z i wa
kuwanasibisha na Mfalme
Jalali na Mtaabadi Karama
kama walivyosimuliwa
na Marehemu Shaaban
Robert katika riwaya
ya k e ya K u s a d i k i k a ,
walivyoafikiana kuwaacha
hu ru vi jan a wao s ita
waliotiwa Jela bila kuwa na
kosa la kisheria. Vijana hao
walileta uongozi ulioweza
kuwakomboa Wasadikika
kutokana na madhila ya
ujahili.
Pamoja na kuwapongeza
waungwana Karume na
Seif, tulitumia pia makala
ile kuwatahadharisha
k u wa : Wa j i e p u s h e
na kulaumiana,
wajitahadharishe na wale
miongoni mwao ambao
ni mfano wa Saluli katika
kisa cha Muhajirina na
Answar.
Katika gazeti hilo hilo
Na. 874, Mhariri aliweka
Tahariri iliyochambua
kwa undani na waledi
na ushahidi mzito mengi
yanayoisibu Zanzibar.
Nitakumbushia machache
tu lakini msomaji zingatia
kuwa haya yote hayakuwa
mawazo wala maoni ya
Mhariri, bali marejeo
yaliyohifadhiwa katika
ANNUUR NEW.indd 10
Makala
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 11
Rais wa Muungano na
Wabunge wa Muungano
ambao uchaguzi huo ni
halali. Inakuwaje kura
walizopiga kuchagua Rais
wa Zanzibar na Wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi
ziwe haramu? Hiki ni
kiroja cha watoto pacha,
mmoja wa halali mwingine
wa haram (bastard).
Tujiulize, hivi mama
mjamzito akajifungua
mapacha, kuna uwezekano
watoto hao mmoja ni
mtoto halali ndani ya ndoa
na pacha wake yeye ni wa
nje ya ndoa?
Mzanzibar gani
mwenye akili timamu
asiyehuzunishwa na
uamuzi wa Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi
(ZEC) kuhalalisha pacha
mmoja na kuharamisha
pacha wa pili.
Tutafakari na tumuombe
Allah atuepushe na
fitina inayotunyemelea.
Bila uamuzi wa busara
na kurejea kwenye haki,
uadilifu na ukweli,
tutaonja joto ya jiwe la
Bani Israil kuhangaika
miaka arubaini tukitafuta
nchi, Amani na
Maendeleo, hatutaipata.
Tutazama katika Idhilali na
hatutapata wa kutunusuru
wala kuona mlango wa
kutokea.
11/26/2015 6:14:12 PM
11
Inatoka Uk. 10
iliyosababisha wanajeshi
kutoka Kaskazini kufanya
jaribio la mapinduzi
Septemba 2002 wakiongozwa
na Guillaume Soro. Baadae
wanajeshi hao waliunda
kikosi chao cha uasi
wakikiita New Forces (FN)
na wakafanikiwa kukamata
na kuiweka chini ya udhibiti
wao sehemu kuibwa ya
Kaskazini ya Ivory Coast
na hapo ndio machafuko na
vita kamili ya wenyewe kwa
wenyewe ikaanza rasmi.
Ilikuwa ni vita kati ya serikali
ya Kikristo Kusini (Christian
southern government) dhidi
ya waasi wa Kiislamu wa
Kaskazini (Muslim northern
rebels.)
Vi t a h i y o i l i m a l i z wa
mwaka 2007 kwa kusainiwa
makubaliano ya Ougadougou
(Ouagadougou Agreement)
ambapo pamoja na mambo
mengine ilikubaliwa kuwa
Gbagbo abaki kuwa Rais na
Soro awe Waziri Mkuu.
Katika uchaguzi mkuu
wa Desemba 2010, matokeo
ya awali yalionyesha kuwa
Ouattara alikuwa mshindi
kwa asilimia 54%. Ghafla
ikatangazwa kuwa matokeo
hayo yamefutwa na badala
ya k e L a u r e n t G b a g b o
akatangazwa kuendelea
kuwa Rais. Kilichofuatia
kinajulikana. Ni nchi
kutumbukia tena katika
machafuko na mauwaji
ambapo inakisiwa kuwa
zaidi ya watu 3000 waliuliwa.
A decade ago, Ivory Coast
was seen as a haven of peace and
prosperity in West Africa. But
under the surface, the country
has long been deeply divided
along ethnic, religious and
economic lines.
Ndivyo mchambuzi mmoja
anavyohitimisha utafiti wake
juu ya nini kiliisibu Ivory
Coast. Kwamba haitoshi
watu kusema kuwa nchi ni
kisiwa cha amani, lakini je,
katika hali halisi hakuna
malalamiko, japo ya chini
kwa chini, ya baadhi ya watu
kubaguliwa na kuonewa?
Panapofuka moshi, dalili
ya mvua mawingu na cheche
huzaa moto.
Ukija kwa Anti-Balaka
n a S e l e k a , J a m h u r i ya
Afrika ya Kati, mchezo ni
huo huo. Inaelezwa kuwa
Waislamu ambao ni kama
asilimia 10 mpaka 15 ya
wananchi wa Afrika ya
Kati, wakiwa kama wapo
katika Bahari ya Ukatoliki,
wamekuwa wakibaguliwa
k i a s i u n a a m b i wa k u wa
maeneo yao yameachwa bila
ya miundo mbinu ya msingi
kiasi kwamba unaambiwa
nchi haipitiki kwa zaidi ya
nusu mwaka (wakati wa
mvua). Hakuna barabara,
shule wala hospitali za
kueleweka. Na kwa vile ni
vigumu kwao kufika miji
kama Bangui yenye huduma
nzuri za afya, Waislamu wa
Aftika ya Kati wamejikuta
wakikimbilia hospitali za miji
ANNUUR NEW.indd 11
Makala
AN-NUUR
LAURENT Gbagbo.
Catherine Samba-Panza,
Afrika ya Kati
ALASSANE Ouattara
ya mpakani ya Chad na hasa
mji wa Nyala, Sudan kupata
matibabu. Na ili kupata elimu
wanalazimika kuwapeleka
watoto wao Khartoum.
Ubaguzi, unyanyasaji,
upendeleo na hujuma za
namna hii zinazofanywa na
serikali dhidi ya makundi
tofauti ya raia, ndiyo iliyozaa
Anti-Balaka na Seleka.
Sasa turudi kwa Taasisi
yetu ya Elimu ambayo katika
kusisitiza nukta yake kwamba
suala la ibada lisihusishwe
katika Somo la Dini, inasema
kuwa, ibada na uchamungu
ukisomeshwa utaondoa
upendo na uvumilivu baina
ya waumini wa dini na
madhehebu tofauti. Kwamba
baadhi ya waumini wataona
kuwa dini yao na dhehebu
lao ni bora Zaidi kuliko
jingine hali itakayosababisha
dharau, chuki na kejeli
baina ya watu wa dini na
madhehebu tofauti.
Chuki iliyozaa machafuko
akiungana na Masheikh
na Wazee wa Kiislamu
katika funga za Sunna
na Dua. Leo Taasisi ya
Elimu inatuambia kuwa
kama dini haitafundishwa
kama taaluma, italeta
ubaguzi na chuki baina ya
Wakatoliki na Waislamu.
Sheikh Ramia na Mzee
Tambaza na akina Mshume
Kiate na Dossa Azizi
waliompokea na kumlea
Julius Nyerere Mkatoliki,
hawakuwa wanajua
Ukatoliki wa Mwalimu
unasema nini. Uislamu
wao waliusomea katika
Madrasa wakihimizwa
kuwa wacha-Mungu. Tena
wakati ule wakiwa na
Mahakama ya Kadhi. Sasa
leo kama serikali inaona
kuwa kunaanza kuibuka
chuki na mpasuko baina
ya Waislamu na Wakristo,
ijiulize kimetokea nini.
Lakini isisingizie dini.
Cote d'Ivoire na Afrika
ya K a t i wa m e u wa n a
Waislamu na Wakristo,
lakini sababu haikuwa
Dini. Sababu ilikuwa
serikali inayowabagua
na kuwakandamiza
Waislamu.
Sasa kama leo tunafikia
m a h a l i p a k u wa t o z a
Watanzania kodi, lakini
huku pembeni na kwa siri
serikali ikawa na MoU
na baadhi ya makundi
ya kidini, huku mitaani
napo kanzu, kilemba
na ndevu ikawa sababu
ya mtu kukamatwa na
k u i n g i z wa S h i m o n i
na Guanatanamo, hii
ni hali ile ile aliyosema
mwandishi mmoja juu
ya Ivory Coast kwamba
Ivory Coast was seen as a
haven of peace and prosperity
in West Africa. But under
the surface, the country has
long been deeply divided
along ethnic, religious and
economic lines.
Na hilo sio tatizo la
somo la dini. Sio tatizo
la jinsi Somo la Dini
linavyosomeshwa. Na ndio
maana machafuko ya Ivory
Coast hayakumalizwa kwa
kufundisha Somo la Dini
kama taaluma.
Bila shaka maofisa
wa TET watakuwa na
kumbukizi za kadhia ya
mabucha ya nguruwe.
Katika tukio lile Waislamu
waliwasilisha malalamiko
yao serikalini wakiomba
sheria za miji zizingatiwe
juu ya ufugaji wa
nguruwe na uwekaji wa
mabucha ya nyama ya
mnyama huyo. Maimamu
11/26/2015 6:14:18 PM
12
Na Omar Msangi
YULE nyoka akatupwa,
yule mkubwa, nyoka wa
zamani, aitwaye Ibilisi na
Shetani, audanganyaye
ulimwengu wote,
akatupwa hata nchi
Ole wa nchi na bahari!
Kwa maana yule Ibilisi
ameshuka kwenu
mwenye ghadhabu
nyingi, akijua kuwa
ana wakati mc hac he
tu! (Biblia, Ufunuo wa
Yohana 12: 9, 12)
Naomba wasomaji wa
makala hii kabla au baada
ya kumaliza kuisoma,
wafungue rejea zifuatayo
na naamini bado zitakuwa
zinapatikana katika
mtandao:
1. T w o T i m e r s Multiple Role Crisis Actors
Revealed.
2. 2. James Foley ISIS
Beheading Hoax Siblings
Kate and Michael Duping
Delight - Fake Tears Obama
Style!
Itizame mpaka mwisho
mpaka uungane kucheka
na mshereheshaji wa
Makala. Tazama pia:
Same Actor playing in
two different crisis acting
roles-(One as Michael
Foley-Brother of James Foley
in the 2014 ISIS beheading
HOAX and another as
Victim Jamie Rohrs in
the 2012 Batman theater
shooting hoax.)
Usichoke, tazama tena
video hii: The Hacked
Jihad John Footage Smoking
Gun Evidence that Emwazi
is CIA. Au CIA Caught
Filming Fake ISIS Beheading.
W a l i m w e n g u
wamehamanika na hasa
katika ulimwengu wa
U l a ya n a M a r e k a n i .
Kila uchao, utasikia
limefanyika hili au lile
k a t i k a k u wa s a k a n a
k u wa t i a a d a b u wa t u
wanaodaiwa kufanya
shambulizi la kigaidi Paris
pamoja na washirika wao.
Waislamu katika Ufaransa
na Ubeligiji hawana raha.
U k i l a l a h u j u i i wa p o
itakuwa zamu yako ya
kuvamiwa na Polisi na
kubambikwa ugaidi
au itakuwa jirani yako.
Ilimuradi harakati za
kuwasaka wanaodaiwa
kuwa magaidi wakitajwa
kuwa ni IS au Waislamu
wa siasa kali, linakwenda
kwa kasi. Na mpaka
sasa zoezi limefanikiwa
kwa kiwango kikubwa
kuhuisha kitisho cha
ugaidi lakini kubwa Zaidi
ambalo ndio lengo:
K u w a t i s h a
Wa l i m w e n g u k u w a
ANNUUR NEW.indd 12
MAKALA
AN-NUUR
Uislamu na Waislamu
ni mbegu hatari, kama
si kwa watu wote, lakini
angalau kwa wastaarabu
wa Ulaya na Marekani.
Lakini hayo yakiendelea
n a k u s h i k i wa b a n g o
na vyombo vya habari,
maarufu, main stream
media, baada ya ule
mhemko wa mwanzo,
watu wenye akili zao
t i m a m u n a wa s i o n a
uvivu wa kufikiri,
wanaanza kuchambua
wakitenganisha pumba
na mchele. Na wengi
katika uchambuzi wao,
wanatumia taarifa na
picha zile zile rasmi za
serikali na main stream
media, kuhoji, nini hasa
kilitokea na nani kafanya
nini na kwa lengo gani?
Pengine na sisi tutumie
fursa hii kuangalia
machache katika
yaliyoibuka ili kupata
uelewa sahihi wa nini
kilitokea Paris katika
kilichoitwa shambulio la
kigaidi lililofanywa na IS.
Tuanze na taarifa kutoka
Israel.
Likiripoti juu ya
s h a m b u l i o l a Pa r i s ,
gazeti la Times of Israel
la Novemba 14, 2015
liliripoti kuwa, ukumbi
wa Disco ulioshambuliwa
ulikuwa unamilikiwa na
Mayahudi wawili ndugu,
na ukauzwa kwa mtu
mwingine siku chache
kabla ya tukio hilo.
Jewish owners recently
sold Pariss Bataclan theater,
where IS killed dozens.
wakilipua mabomu ya
kujitoa muhanga kama
tulivyoambiwa kuwa
ndivyo ilivyokuwa katika
ukumbi wa Bataclan. Je,
katika hali hiyo, unakimbia
kusalimisha roho yako au
unahangaika kumpigia
simu mtu aliyeko mbali
mpaka unamsikizishia
milio ya risasi?
Akiendelea kusimulia
Joel anasema: a member
of the Eagles of Death
Metal was hit by a bullet
and killed.There is blood
everywhere. It will take three
days just to clean that up.
Joel yupo Israel wakati
shambulio likitokea, lakini
muda huo huo, kabla hata
polisi hawajatoa taarifa
anasema kuwa mmoja wa
wapiga muziki wa bendi
ya Eagles of Death Metal
iliyokuwa ikitumbuiza
alikuwa amepigwa risasi
na kufa.
Tujaaliye ni mtu alikuwa
amempigia simu, katika
hali ile ya mtafaruku,
magaidi wanapiga
na kuuwa watu ovyo,
huyo aliyempigia simu
ameweza kuwachambua
vipi waliokwisha kufa
na k u m t a m b u a h u y o
marehemu wa Eagles of
Death Metal Band?
Lakini zaidi anasema
There is blood everywhere.
It will take three days just to
clean that up, akimanisha
kuwa damu imetapakaa
kila mahali na kwamba
11/26/2015 6:14:19 PM
13
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 18
K AT I K A k u e n d e l e a
kuwazungumzia wana
wazuoni wetu waliopita,
leo nitazungumzia gwiji
ambaye aliendeshana nyuga
na puta na watawala, huyo
sio mwengine ni Sheikh Ali
bin Khamis bin Salim AlBarwany.
Sheikh Ali bin Khamis bin
Salim Al-Barwany ni katika
Masheikhe ambao waliishi
katika umri mdogo sana
na kupitia misukosuko ya
kufungwa pale alipokuja
kukhitalifiana na mtawala
wa nyakati hizo kutokana
na madhebeu aliozaliwa
nayo nakuingia madhehebu
nyengine.
Sheikh Ali bin Khamis bin
Salim Al-Barwany alizaliwa
mwaka wa 1267 AH( 1852)
katika mtaa wa Baghani mtaa
ambao ukikaliwa na tajiri
mmoja mkubwa wa Zanzibar
aliokuwa akijulikana kwa
jina la Bwana Udi. Sheikh
Ali bin Khamis alikulia
katika mtaa huo wa Baghani.
Akiwa katika umri mdogo
alianza kujiunga na baraza
ya mfalme na kujadiliana
na wana baraza masuala ya
kila aina, kuanzia ya dini na
mambo ya kijamii. Akiwa
mwana baraza alikubalika
ANNUUR NEW.indd 13
SHEIKH Ali bin Khamis bin Salim Al-Barwany, huyu ni mwalimu wa Sayyid
Mansab na hawakupishana kwa namna ya mitizamo yao ilivyokuwa. Sheikh
Ali bin Khamis bin Salim Al-Barwany ni katika Masheikhe ambao waliishi
katika umri mdogo sana na kupitia misukosuko ya kufungwa pale alipokuja
kukhitalifiana na mtawala.
vilivyo kwani alitokana na
aila ambayo ilishikamana
vilivyo na majlisi ya mfalme,
kwa hiyo haikuwa tabu naye
kukubalika.
Sheikh Ali bin Khamis
bin Salim Al-Barwany
alibahatika kukutana na
wanavyuoni mbalimbali
ambao walikuwa wakimvutia
na kuanza kusoma kwao.
Kwa muda mfupi kabisa
aliweza kubadilika katika
macho ya watu kutokana na
uwezo aliokuja kuwa nao
wenye upeo mkubwa wa
elimu na hoja zilizokuwa na
uthabiti ndani yake.
Kati ya walimu wake
walioanza kumiminia elimu
walikuwa Makadhi wakubwa
wa madhehebu ya Ibadhi
a k i we m o S h e i k h Ya h ya
bin Khalfan Al-Kharusy
na Sheikh Muhammad bin
Suleiman Al-Mendhary.
Aidha, alisoma sana
kwa Sheikh Abdul Aziz
Abdulghany Al-Amawy,
ambaye akitajikana kati
ya maulamaa wakubwa
wa Kisuni wa wakati
huo. Akiwa anasoma kwa
mashekhe mbalimbali na
kupanua uwezo wake wa
kielimu na kushikamana nao
sawasawa, mara akaingia
nchini gwiji aliobobea katika
fani mbalimbali za dini ya
Kiislamu Sheikh Khamis bin
Slim Al-Khasby, Sheikh Ali
bin Khamis kusikia ujio wa
shekhe huyo akamvaa akawa
hatoki kwenye darasa zake
na aliweza kujifunza lugha ya
Kiarabu kwa upeo mkubwa
na fani mbalimbali za dini
ya Kiislamu na akawa ni
mmoja wa watu wanaoweza
kucheza na lugha ya Kiarabu
vilivyo na kuwa mwandishi
wa mashairi anayesifikana.
Syd Barghash alikuwa kati
ya wafalme ambao akipenda
maendeleo na kuona nchi
inasonga mbele katika nyanja
mbalimbali za kimaendeleo.
Kati ya mambo aliyoweza
kuyafanikisha kwa haraka
katika utawala wake, ni
kuweza kusambazwa kawa
maji katika maeneo ya mjini,
kuingiza karafuu ambazo
zikaja kuwa ndio uti wa
mgongo wa uchumi wa
Zanzibar pamoja na kuagizia
mtambo wa kuchapishia
vitabu ukiwa ndio mtambo
wa mwanzo kuonekana
katika nchi za Afrika ya
Mashariki.
Mtambo huo wa
kuchapishia vitabu katika
s i k u z a a wa l i u l i k u wa
kupiga chapa vitabu vya
Kiibadhi, ikawa kila kitabu
kinachochapishwa Sheikh
Ali bin Khamis bin Salim
Al-Barwany akikitungia
shairi ya kukisifu na kukipa
sura ambayo msomaji
atakikubali kitabu hicho
kilichochapishwa. Kutokana
na kazi nzuri aliokuwa
11/26/2015 6:14:20 PM
14
MAKALA/MASHAIRI
ANNUUR NEW.indd 14
Msamaha
AN-NUUR
NA SHEIKH MUHSIN
ASAYID MOHAMED
H U K U R A N I
zote anatsahiki
Mwenyezi Mungu,
M o l a m l e z i wa
u l i m we n g u . M w i s h o
mwema ni kwa wacha
mungu na hakuna
uadui isipokuwa kwa
madhalimu.
Rehema na amani
zimfikie mbora wa mitume
na mwisho wa manabii,
aliye nrehema kwa
viumbe wote, mtume wetu
Muhammad na jamaa zake
za sahaba zake wote.
Kwa hakika Uislamu
ni dini inayozungumza
akili na kiwili wili na
humlazimisha Muislamu
k wa l i l e a n a l o l i we z a
kulitekeleza, na wala
hauja mlazimisha hata
mtu mmoja kufanya jambo
asiloliweza isipokuwa lile
analoliweza tu. Mwenyezi
Mungu ndiye ambaye
amemuuomba binadamu
na nafsi na anaijua uwezo
wake.
Amesema Mwenyezi
Mungu mtukufu:Hailazimishi nafsi
isipokuwa inaloliweza
(Baqara: 286).
Uma wetu wa Kiislamu
ameusifu Mwenyezi
Mungu katika kitabu chake
kitukufu kuwa ni uma
wa kati na kati. Amesema
Mwenyezi Mungu
mtukufu:Na hivyo hivyo
tumekufanyeni uma
wakati na kati ili muwe
mashahidi kwa watu na
awe mtume kwenu ni
shahidi (Baqara:143)
Mtume (saw) anasema,
Nimetumilizwa katika
dini nyepesi.
Laiti tutasimama
katika neno nyepesi
kwa kuangalia chochote
m i o n g o n i m wa s o m o
linalopatikana kwa upande
wa lugha na kisheria,
t u t a k u t a u we p e s i wa
kisheria ya Kiislamu tena
kwa uwazi kabisa kwa
yule anayeathirika na
11/26/2015 6:14:20 PM
15
MAKALA
AN-NUUR
Na Said Rajab
JUMAA ya Novemba
13 mwaka huu,
ilidaiwa kuwa jiji la
Paris, nchini Ufaransa,
lilishambuliwa kwa mabomu
ya kujitoa muhanga, hali
iliyosababisha vifo vya
watu 230 na wengine
kadhaa kujeruhiwa. Kwa
takriban wiki yote ya jana,
tulishuhudia vyombo vya
habari vya nchi za Magharibi
vikiripoti tukio lile kama
habari ya kwanza yenye
uzito mkubwa. Licha ya
hatari ya kuhukumu kabla
ya uchunguzi kufanyika,
hisia za watu wote duniani
zikaelekezwa na vyombo
hivyo kwamba waliolipua
mabomu yale ni Waislamu.
Ulimwengu umeshuhudia
maneno ya chuki dhidi
ya Uislamu yakihusishwa
na tukio hilo. Wanajaribu
kuhusisha uhalifu ule na
Uislamu.
Ningependa kuchambua
kidogo baadhi ya mambo
kuhusu shambulizi hili, ili
iwe changamoto ya fikra
kwa wasomaji wanaofuatilia
masuala ya ulimwengu.
Matukio kama hayo
yanapotokea, basi fursa pia
hupatikana ya kuwekana
s a wa k i m t a z a m o . K wa
masikitiko makubwa, kelele
hizi za vyombo vya habari,
zikiungwa mkono na maoni
ya wanasiasa wenye chuki
dhidi ya Uislamu, zinajenga
mtazamo kwamba, ingawa
Wa i s l a m u w o t e s i y o
"magaidi", lakini "magaidi"
wengi hakika ni Waislamu.
Hata hivyo, mtazamo kama
huo unakosa mashiko, pale
unapoulinganisha na idadi
halisi ya mashambulizi ya
kigaidi. Gazeti la Europol
lilichapisha takwimu
zinazoonyesha kwamba kati
ya mwaka 2006 mpaka 2008,
asilimia 99.6 ya shughuli
zote za kigaidi barani
Ulaya, zilifanywa na wasio
Waislamu.
Kinachokera zaidi ni
kwamba taarifa potofu za
vyombo vya habari ndizo
zinazoaminika na kujenga
mitazamo hasi dhidi ya
Waislamu, lakini zile halisi
hazipewi nafasi, kwa hiyo
h a z i j u l i k a n i k wa wa t u
wengi. Tatizo lingine kubwa
la vyombo vya habari ni
kutoa tuhuma za jumla
jumla. Yaani Muislamu
mmoja akituhumiwa kufanya
uhalifu, basi jamii nzima
ya Waislamu inalaumiwa
kwa hilo. Kimsingi, Uislamu
u n a k a t a z a v i t e n d o v ya
ukatili na kumwaga damu
za watu wasio na hatia, kama
tulivyoona katika mabomu
ya Paris. Kwanini Waislamu
wote wanaoishi Ufaransa
walaumiwe, wasumbuliwe
na watishiwe kwa sababu ya
ANNUUR NEW.indd 15
mabomu ya Paris?
Siyo Wakatoliki wote
wanaohusishwa na kashfa
ya kulawiti watoto, kwa
sababu tu baadhi ya mapadri
wamekuwa wakifanya
uchafu huo! Siyo Waingereza
wote ni waongo, kwa sababu
tu Serikali ya nchi hiyo,
iliudanganya ulimwengu
kuhusu Iraq kumiliki silaha
z a m a a n g a m i z i m wa k a
2003! Vilevile kuhusika
kwa Muislamu mmoja
katika uhalifu au tuhuma,
haiwafanyi Waislamu wote
katika jamii husika kuwa
wahalifu wa tuhuma hizo!
Vyombo vya habari vya
Magharibi vimewazoesha
watu wake kuwaangalia
Waislamu kama "Wao" na
wenyewe kujiona "Sisi"
ingawa wote ni raia wa nchi
moja. Mara nyingi utakuta
vyombo hivyo vinaripoti
matukio kama ya Paris katika
misingi ya "Wao", "Sisi", "Yao"
na "Yetu". Huwa wanasema
"Wao" hawapendi maadili
" Ye t u " . Wa m e s h a w e k a
kizingiti katika akili za
watu wao na Waislamu.
Wa m e j e n g a m a z i n g i r a
Waislamu waangaliwe kwa
mashaka kila uhalifu kama
wa Paris unapotokea.
Lakini mtu anahitaji
kuelewa msingi hasa wa
mashambulizi kama haya
ni nini? Kwa bahati mbaya
sana, mjadala kama huu
unapuuzwa kwa makusudi
kwa sababu utatoa taswira
Inatoka Uk. 5
ya vijijini.
Serikali pia imefanya kazi
kubwa kupunguza mzigo
wa gharama za matibabu
kwa wazee na kutoa msaada
maalumu wa tiba kwa wazee
na wagonjwa. Hadi kufikia
m w i s h o n i m wa m wa k a
2005 zahanati zaidi ya elfu
15 zilijengwa katika miji
mbalimbali nchini China,
ambazo zinatoa huduma za
afya na tiba kwa wazee hata
majumbani mwao.
China inazingatia sana
kulinda haki na maslahi ya
wazee, imebuni sheria na
kanuni za kisheria ikiwemo
sheria ya dhamana kwa
haki na maslahi ya wazee na
kujenga mfumo wa sheria
na sera kuhusu huduma
za jamii, utamaduni, elimu
dhamana kwa maslahi na
haki za wazee.
Idara husika ya huduma ya
kisheria imeanzisha mfuko
wa fedha wa kutoa msaada
wa kisheria kulinda haki na
maslahi ya wazee. Katika
miaka 5 iliyopita, idara ya
utoaji huduma ya kisheria
kwa wazee ilitoa wastani wa
misaada zaidi ya elfu 40 kwa
mabomu yanayoangushwa
na jeshi la nchi yao, dhidi
ya watu wasio na hatia
katika baadhi ya nchi hizo!
Wajiulize, wanathamini uhai
wa binadamu wenzao kwa
sababu ni binadamu, au kwa
sababu ni Wazungu wenzao
wanaotoka kwenye nchi
zao? Kama jibu ni binadamu
wenzao, kama mtu yeyote
mwenye akili atakavyojibu,
sasa kwanini tunafanya
upendeleo katika kutoa
huruma, mapenzi na simanzi
zetu? Lazima tuumizwe na
kukasirishwa na vitendo
vyote vya ukiukaji haki na
mauaji ya binadamu wasio
na hatia duniani kote.
Tu n a o n a u p e n d e l e o
waziwazi. Vifo vinavyotokea
ulimwengu wa Magharibi
vinaripotiwa kwa kina na
kugeuzwa ajenda ya dunia,
lakini vifo na madhila
yanayotokea katika
ulimwengu wa Waislamu
vinaripotiwa kidogo sana!
Mbaya zaidi madhila
hayo huletwa na Serikali
za Magharibi, hususan
Ufaransa.
Kwa kumalizia, hatua
zozote zitakazochukuliwa
na Ufaransa kupanga
m a s h a m b u l i z i d h i d i ya
Waislamu kwa kisingizio
cha kupambana na
ugaidi, ikitumia huruma
iliyopatikana kufuatia
uhalifu uliofanyika Paris,
lazima zipingwe kwa nguvu
zote.
mwaka kwa wazee.
Hadi kufikia mwishoni
mwa mwaka 2005, China
ilianzisha shule na vyuo
vya wazee zaidi ya elfu 26
pamoja na nyumba za
11/26/2015 6:14:20 PM
16
MAKALA
U WA m w e n z a
bora, ni muhimu
katika ndoa
yoyote. Ndoa
inatakiwa iwe uhusiano
kamilifu ambako watu
wawili wanaounganika
pamoja muda wote
watakuwa tayari kutoa,
n a s i y o k u t wa a - n a
kujitahidi muda wote
kujiboresha kwa ajili ya
upande wake mwingine.
Ndivyo inavyotakiwa
ili kuwa mume bora wa
Kiislamu, jambo ambalo
Uislamu unasisitiza, na
aliyeita watu kuingia
katika Uislamu,
Muhammad (swallahu
alei wasalaam) alielekeza
hivyo. Fuatilia haya ili
kuondoa kutokuelewa
kuhusu jinsi ya kuwa
mume nyota!
1. Anza na salaam nzuri:
unaporudi kutoka kazini,
au safarini, msalimie mkeo
kwa 'Asalaam aleykum,'
salamu ya kutakiana heri.
Kumbuka alichosema
Mtume Muhammad,
(SAW): "Nikuelelezeni
katika jambo, ambalo
mkilifanya, mtapendana?
Enezeni salaam miongoni
mwenu."
2 . M wa n g a l i e k wa
upendo. Mtume
M u h a m m a d ( S AW )
alisema: "Mume na
mke wakiangaliana
kwa upendo, Allah
huwaangalia wote
wawili kwa huruma."
Umwangalie machoni
unapozungumza na mkeo,
kama mwanamke ataona
thamani ya jambo hilo -na
kumwangalia kwa jicho la
upendo na siyo mradi tu
umemwangalia!
3. Muone na kutabasamu
kwake. Mtume (SAW)
aliona tabasamu kama
zawadi ya furaha - zawadi
ya hisia, si ya kubeba zawadi ambayo undani
wake unapokelewa na
moyo. Swahiba wa
Mtume, Jarir Abdallah,
alisema: "Tangu wakati
nimeukubali Uislamu,
Mtume hakuwahi hata
siku moja kutokuniona.
Wakati wowote aliponiona
alitabasamu kwangu," Na
usemi mwingine maarufu,
kuwa "Unapotabasamu
usoni kwa ndugu yako
(ikiwa na maana mtu
yeyote, si kanuni kwa
ndugu pekee) ni zaka."
Sasa, endapo umefanya
haya mawili katika
ndoa yako, uhusiano wa
msisitizo zaidi, fikiria jinsi
itakavyokuwa na heri
zaidi! Mwache mkeo aone
upendo wako kwake kwa
tabasamu yako ya wazi
unapomwona.
4 .
M w a m b i e
unampenda. Na
umwambie mara nyingi!
Na uwe na ubunifu mara
nyingine ongeza neno la
mahaba! Chukua mfano
kutoka kwa Mtume! Mke
wa Mtume, Hazrat Aisha,
ANNUUR NEW.indd 16
alikuwa anamwuliza:
"Nini upendo wako
kwangu?" Naye anajibn;
"Kama fundo la kamba,"
ikiwa na maana ina nguvu
na onyesho, alimwuliza
"umetosheka?" na alipokiri
hivyo, wakaondoka wote
pamoja.
8. Msaidie: Taarifa moja
inasema mke wa Mtume
alikuwa safarini pamoja
naye. Alichelewa hivyo
Mtume akampokea akiwa
analia. Mtume (SAW)
akafuta machozi yake kwa
mkono wake na kujaribu
awezavyo kumtuliza.
9. Mdsaidie shughuli
za nyumbani, au angalau
usafishe unapotumia.
Hazrat Aisha aliulizwa
kuhusu tabia za Mtume
nyumbani kwake. akajibu:
"Alikuwa akisaidia katika
AN-NUUR
Vidokezo: M s a i d i e
kumtumikia Allah.
Mwamshe katika sehemu
ya tatu ya usiku kusali
'Qiyam al-Layl,. Mfundishe
unachojua kuhusu Kurani,
Usipokipenda, usiseme
lolote. Usimvunjie
heshima. Kama umekwaza
hisia zake mahali fulani
sema "samahani," na
kujaribu kumpendeza.
11/26/2015 6:14:21 PM
17
Makala
HAMA cha
Mapinduzi
n d i c h o
kinachoendelea
kutawala nchini na sasa
kimefikia katika uongozi
wa awamu ya tano chini
rais Dr. John Pombe
Joseph Magufuli au
JPM. Uongozi wa awamu
zote huwa na kauli mbiu
zao na wa awamu hii
unajulikana kwa jina
la hapa kazi tu. Ni
matumaini ya Watanzania
wote kuona kauli mbiu
hiyo ya hapa kazi
inafikiwa na kutekelezwa,
isiwe ni wimbo kama ule
waliousikia na kuuimba
wa maisha bora kwa kila
Mtanzani.
Ndani ya siku hizi
chache zilizopita,
tumeshuhudia mfano wa
hapa kazi tu, lakini sijui
itakuwe kweli hapa kazi
tu au ni hapa mwanzo tu.
Kama ni msimu wa mvua,
tuseme hiyo imekuwa
rasha rasha kwa maeneo
hayo yalopitiwa na wengi
wetu. Tunasubiri mvua
kamili kwa maeneo
mengine.
B a a d a ya u t a n g u l i
huo,sasa niingie pale
nilipokusudia kwa leo ili
nami nichangie juu ya hili
la Mzee wa hapa kazi tu la
kuonyesha kuwa maneno
yake ya matumizi yasio ya
lazima yanaekwa kando
na ya muhimu yanapewa
kipaumbele. Kwa kuanzia
ameagiza na kutaka
sherehe za uhuru wa
Tanganyika kwa mwaka
huu zisiwepo na badala
yake pesa za sherehe
h i z o z i e l e k e z we k wa
jamii katika usafishaji na
uimarishaji wa mazingira,
kwa nia ya kupunguza au
kuondoa kabisa mripuko
wa ugonjwa wa kipindu
pindu ulioikumba nchi
kwa sasa. Kama hiyo
ndio dhamira, hata na
mimi naunga mkono
na wananchi nina
imani wataitikia wito
huo wakiamini kuwa
mazingira yetu ndio uhai
wetu.
Katika sherehe
kama hizi za uhuru wa
Tanganyika, ingependeza
zaidi kama zisingekuwepo
toka zamani na fedha
zake kuelekezwa katika
miradi ya maendeleo.
Ninasema hivi kwa sababu
mara kadhaa imekuwa
ikinadiwa na viongozi
h a o h a o wa s e r i k a l i
ANNUUR NEW.indd 17
AN-NUUR
kwamba Mwenge ni
kichocheo cha maendeleo,
sasa inatupasa tujiulize
kama Mwenge huleta
maendeleo, nchi ambazo
hazina Mwenge hakuna
maendeleo, au tuangalie
hayo maendeleo ya
Mwenge yanayofanyika
ni miradi ya thamani
ngapi inayozungukiwa
na Mwenge wenyewe
unadharimu ngapi.
Tukirudi kwa lile la
usitishwaji wa sherehe
za uhuru wa Tanganyika
mwaka huu yaani
9/12/2015,isijekuwa ni
mwanzo na njia ya kufikia
m a l e n g o ya C C M ya
serikali mbili kuelekea
moja kama ilivodaiwa.
Kama hazitofanyika
tena sherehe hizo za
uhuru wa Tanganyika kwa
miaka inayofuata kwa
upande wa pili wa shilingi
ambao sio wa matumizi
ya s i y o ya l a z i m a , k wa
upande wa siasa itakuwa
ni kutoweka kabisa kwa
jina Tanganyika ambalo
bado wapo wazalendo wa
Tanganyika wanaoisubiri
Tanganyika irudi tena
kama ilivyokuwa kabla
ya 64.
Kwa muono huu
kutokuwepo kwa huo
uhuru wa Tanganyika
kunaweza pia kupelekea
wazalendo ambao
hufarijika japo mara moja
kwa mwaka kusikia neno
uhuru wa Tanganyika
neno hilo lisisikike tena
masikioni mwao.
Ikiwa hivo pia
itapelekea kutokuwepo
na kufutika kabisa sherehe
za muungano ya 26/4 na
badala yake siku hiyo
kujilikana kama siku ya
jamuhuri ya Tanzania.
Ikifikia
hapo
h a k u t a k u wa n a t e n a
sherehe za mapinduzi
wala serikali yake na hapo
ndoto za kila wazalendo
kupoteza ndoto zao yaani
Watanganyika kutorejea
t e n a Ta n g a n y i k a n a
Wa z a n z i b a r k u p o t e a
kabisa fikra na azma ya
kuwa na Zanzibar huru
yenye mamlaka kamili
kama wanavoililia ng'oa
kila uchao.
Na hapo ile safari
ya zamani ya CCM ya
serikali mbili kuelekea
moja itakuwa imetimia
kwa kupatikana Jamhuri
ya Tanzania na sio tena
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Asanteni na Allah
atupe mwisho mwema.
11/26/2015 6:14:24 PM
18
MAKALA
AN-NUUR
Inatoka Uk. 13
ukisaliwa katika miaka ya
50 mwishowe na mwanzo
wa miaka 60 na mmoja wana
wa ukoo wa Kifalme Sayyid
Haroub ambaye alikuwa
peke yake katika ukoo wa
kifalme akifwata madhehebu
ya Sunni/Shafi. Msikiti
huu aidha ukisomeshwa
darsa zake na Syd Hamid
Mansab na akaja kupokewa
na mwanawe Syd Ahmed
Mansab ambao niliwaelezea
katika makala iliopita. Darsa
za Msikiti huu zilikuwa
zikisomeshwa baina ya
magharibi na isha.
Msikiti wa Ijumaa wa
Malindi huu ni Msikiti
mkubwa wa ghorofa moja
ukiwa upo karibu sana na
Bandari Kuu ya Unguja.
Unapoteremka bandarini
kwa boti itakuchukua chini
ya dakika tatu kuufikia
Msikiti huu.
Msikiti wa Ijumaa wa
Malindi umejengwa katika
mwaka wa 1831 na watu wa
ukoo wa Mafazi na mmoja
kati ya wanafamilia alitoa
kipande cha ardhi cha Miafuni
kiwe pesa zinazotokana na
hapo ziusimamie Msikiti
akijulikana kwa jina la
Mwinyi Sheikh bin Haji
Omar al-Mutafi. Msikiti
huu ulikuwa ukisaliwa na
wingi wa waumini katika Mji
Mkongwe. Sheikh Muhydin
al Shaikh bin Abdalla Qahtani
a m b a ye n i s h a m u e l e z e a
katika makala zangu kabla,
ni mmoja wa masheikhe
Inatoka Uk. 13
kwani vumbi lake huko
ANNUUR NEW.indd 18
Zanzibar. Aliporudishwa
Zanzibar alipelekwa jela
moja kwa moja kutokana
na msimamo wake
usiotetereka katika suala
la kujiunga na madehebu
ya Sunni.
Sayyid Barghash akijua
uwezo wa Sheikh Ali Bin
Khamis Al-Barwany na
athari atazoziwacha, kwa
hio hakusita kumtuma
Sheikh Sleiman kuendelea
kwenda kumnasihi Sheikh
Ali bin Khamis bin Salim
Al-Barwa n y k u wa ch a
misimamo yake na
kufahamisha kuwa kama
hatobadili msimamo wake
ajue atafia jela. Sheikh Ali
bin Khamis bin Salim AlBarwany akajibu jela ni
bora kwake na anastahabu
kubakia huko kwani yeye
sio wa mwanzo katika
tarekhe aliopambana
n a wa t a wa l a . S h e i k h
Suleiman akamnasihi
kuwa akubali mdomoni na
ndani ya nafsi yake abakie
alipo, akakubali hilo akiwa
lake khasa lipo moyoni,
mwishowe alikubali na
kula yamini kurudi katika
madhehebu ya asili ya
wazee wake kwa kufanya
hivyo akafunguliwa
jela, wengi waliokuwa
wanamfahamu walimuona
fika ni kuwa bado ni Sunni
kwa vishindo vyake.
Sayyid Barghash
a n a e l e z wa n a S h e i k h
Abdalla Saleh Farsy
kama ifwatavyo, Sayyid
Barghash ni Harun Rashid
wa Ki-Busaidi wa Zanzibar
na ndio Maamun wao
pia. Ukubwa na fahari
na heshima na mengineo
aliotajikana nayo Harun
Rashid akiwa miongoni
wa wafalme wa Ki-Bani
Abass, ndio sifa aliosifika
nayo Sayyid Barghash.
Al-Maamun naye kati
ya wafalme wa BaniAbass alikuwa kipenda
elimu kwa kukusanya
chungu ya wanavyuoni
na ndivyo ilivyokuwa
kwa Sayyid Barghash
pia. Al-Maamuun
aliwataabisha vya
kutosha wale waliokuwa
hawafwati madhehebu
yake ndivyo hivyo
hivyo Sayyid Barghash
alivyowataabisha
waliokuwa hawafwati
madhehebu yake katika
wale aliokuwa karibu naye
kiukoo na karibu zake.
Imam Ahamd bin Hambal
alipata misukosuko
mikubwa yeye na wenziwe
kufungwa na Al-Maamun,
n a ye S a y y i d B a r g h a s
alimfunga Sheikh Ali bin
Khamis bin Salim AlBarwany na Sheikh Sheikh
Ali bin Abdalla Mazrui
pamoja na Sheikh Abdul
Aziz. Hapana aliokamilika
asiokuwa na dowa,
aliokamilika ni Allah.
Mola awarehemu wote,
alimalizia Sheikh Abdalla
Saleh Farsy kumfasili
Sayyid Barghash.
Sheikh Ali bin Khamis
bin Salim Al-Barwany
baada ya kutolewa jela
hakuchukua muda
mrefu na kufariki akiwa
na umri wa miaka 36.
Aliyoyafanya yote na
kishindo alichokiweka
kupambana na mtawala
aliyafanya hayo akiwa na
11/26/2015 6:14:25 PM
19
Inatoka Uk. 12
Mchambuzi anakuletea
picha ya mahali ambapo
limepigwa bomu la kweli
au mashambulizi ya
risasi za kweli, ukumbi
umefumuliwa paa
sikwambii madirisha
ya viyoo kwamba kuna
kilichosalimika.
Parisians no longer feel
safe after what happened
here. The terrorists have
no rules. We have to take
the bull by the horns in the
battle against terror, and
France and the government
never do.
Anasema Pascal
akihitimisha taarifa
yake katika Times of
Israel, akiwaaambia
Wafaransa wajue kuwa
hawapo salama tena
kutokana na ukatili
huu uliooneashwa na
magadi. Kwa hiyo ni
l a z i m a s e r i k a l i ya o
ichukue hatua kali
dhidi ya magaidi hao IS
(Waislamu)!
Na katika kukoleza
madai kuwa wahusika
ni Waislamu taarifa hiyo
ya Mayahudi ikasema
kuwa kuna kundi linajiita
Army of Islam ambalo
limekuwa likiwatishia
na kwamba lilipanga
kuipiga Bataclan toka
mwaka 2011 kwa
vile linamilikiwa na
Mayahudi.
Na unaweza kuona
harakati zinazofanywa
Ufarsana hivi sasa na
Ulaya yote kuwahujumu
Waislamu, huku harakati
za kuipiga Syria nazo
zikipamba moto.
Viroja vya Paris
Katika jumla ya vituko
vilivyoibuliwa katika
shambulio hili la Paris ni
kuwa vichwa vya habari
vya baadhi ya habari
za sasa hivi (Breaking
News, viliandikwa siku
mbili kabla ya tukio.
Tazama hii:
Breaking: Death toll
From Paris Terror Attack
Rises to at least 120 with
270 others Injured.
Wataalamu wa IT,
digitali wamechimbua
na kugundua kuwa
taarifa hii iliandikwa
Jumatano Novemba 11,
2015 saa 1 na dakika
44 jioni (19:44) wakati
shambulio lilifanyika
Ijumaa Novemba 13.
(Tazama: Tweeted two
days before it actually
happened.)
Chini ya taarifa hiyo,
utakuta pia habari ya
Giraldo Rivera wa Fox
News ambaye anamuhoji
Binti yake aliyekuwa
Paris na marafiki zake
ANNUUR NEW.indd 19
TANGAZO
AN-NUUR
KATIKA Picha hii imeelezwa kuwa watu wanasubiri kuokolewa baada ya kupigwa mabomu katika
uwanja wa mpira wa Paris, Ufaransa.
wawili katika mechi
ya kirafiki ya timu ya
Ufaransa na Ujerumani.
Baadae anahojiwa
Simona Rivera, dada
yake na huyo aliyeko
Paris kuangalia mechi.
Katika mahojiano hayo
anasema awali mdogo
wake alionyesha
wasiwasi wa kwenda
akihofia kuwa jambo
baya linaweza kutokea.
Mchambuzi anahoji
na kuwaambia watu
wa Ufaransa na Ulaya
wa j i u l i z e , i n a i n g i a
akilini kweli kwamba
wasichana kutoka
Marekani wanaweza
kuja Paris kwa lengo
la kuangalia mechi ya
kirafiki kati ya nchi hiyo
na Ujerumani? Au ni
wale wale Crisis Actor
ambao wapo kila mahali
iwe Westgate, Nairobi,
Boston Bombing,
Kikambala, Batman
theater shooting?
Katika maelezo hayo
ya Binti wa Giraldo
wa Fox News anaeleza
ilivyokuwa mtafaruku
lilipolipuka bomu katika
uwanja wa mpira, habari
ambayo pia ilibebwa na
ABC News (ya Marekani
pia) kwa kichwa cha
habari: Paris Attacks:
wanakimbia kulikimbia
gari lao, kisha wanarudi.
Anakuonyesha watu
baada ya tukio, hakuna
mwenye damu, hakuna
damu katika sakafu na
hakuna hata mtu mmoja
anayeonyeshwa akiwa
na jeraha la kweli (open
wound).
Katika hali hiyo
mchambuzi anasema
v i r o j a v ya n a m n a
hii, Paris sio mwanzo.
Anaturejesha katika lile
shmabulio la Olympic
Pa r k , k u l e At l a n t a
mwaka 1996. Katika
shambulio lile CNN
katika hali ya kuvuta
hisia za watazamaji
wake katika moja ya
Breaking News zake
likanadi juu ya mabomu
mawili yaliyolipuka kwa
wakati mmoja kama
tulivyoambiwa katika
lile la Dar es Salaam na
Nairobi (simultaneous).
Katika kusherehesha
ikalezwa kuwa mabomu
yalikuwa mazito,
yameuwa, yamejeruhi,
watu wanakimbia ovyo
kusalimisha roho zao.
Ha ta hi v yo, wa tu
walipopitia picha kwa
makini, kilichosikika ni
11/26/2015 6:14:26 PM
AN-NUUR
20
MAKALA
20
WAT U w a l i j i k u t a
wakibubujikwa
na machozi. Ni
wale waliokuwa
wamemzunguka kijana.
Kijana aliyetoa ujumbe
mzito kwa watu wa Paris.
Mimi ni Muislamu.
Ila nashangaa kuna watu
wananiita gaidi.
Mimi nakuamini
wewe. Je, wewe
unaniamini?
Kama unaniamini,
njoo unikumbatie.
Alikuwa akisema na
kupaza sauti kijana huyo
wa Kiislamu akitembea
katika jiji la Paris jirani
na kunakodaiwa kutokea
shambulio la kigaidi
huku akiwa kaziba
macho na kilemba, haoni
anakokwenda.
Kama ilivyo kawaida
ya watu, na hasa mijini,
kufumba na kufumbua,
kundi kubwa la watu
lilikuwa limemzunguka.
Sasa badala ya
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
Mimi ni Muislamu!
Kuwa na amani. Tusalimiane
Tupeane mikono kwa upendo
na machozi na mmoja
mmoja wakijitokeza
kwenda kumkumbatia.
Nakushukuruni
sana nyote. Tambueni
kuwa gaidi ni gaidi.
Hana nembo ya Uislamu
WAISLAMU wametakiwa
kutoa nguvu zao za hali
na mali, katika kujenga na
kuendeleza taasisi za elimu.
Wito huo umetolewa na
Ustadhi Zaharan Baraka,
akizungumza katika hafla
ya uchangiaji wa maendeleo
ya Shule ya Sekondari ya
Kiislamu ya Jioni (MESS)
iliyofanyika Jumamosi
ya wiki iliyopita, katika
viwanja vya Islamic Club,
Mwananyamala Jijini Dar
es Salaam.
Ust. Baraka alisema
uwepo wa vituo vya elimu
ni ukombozi kwa jamii ya
Kiislamu ambayo kwa muda
mrefu imekuwa ikipaza
sauti ya kubaguliwa katika
elimu.
Alisema, kutokana na
historia fupi ya kituo hicho
cha masomo ya Sekondari
yanayotolewa katika mfumo
wa elimu usio rasmi (Jioni
tu), inaonyesha kimekuwa
na msaada mkubwa kwa
Waislamu waliokosa fursa ya
kusoma elimu ya Sekondari
kupitia mfumo rasmi.
Unapotambuwa
kwamba umekwama na njia
ya kujikwamua ipo, usipo
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.
ANNUUR NEW.indd 20
11/26/2015 6:14:27 PM