You are on page 1of 16

Sauti ya Waislamu

Maandamano makubwa kufanyika nchi nzima


Kupinga kudhalilishwa Sheikh Kishki, Mufti Kamanda Ernest awaombe radhi Waislamu
SHEIKH Nurdin Kishki.

ISSN 0856 - 3861 Na. 1024 SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 12, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Reginald Mengi na Mtume Muhammad wapi na wapi?


MASHEIKH wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu nchini wakitoa taarifa ya Waislamu kutoshiriki katika zoezi la sensa katika Hotel ya Tansoma jijini Dar es Salaam Jumatano wiki hii .

Innalillahi wainna ilayhir rajiuun: Mzee wetu Alhaj Ali Hassan Mwinyi

Mbona wapo kina Paulo, Petro na Luka? Ungemfananisha na Mtume Mwingira Wapo pia Mzee wa Upako, Mch. Rwakatare

Karume ampasha Boraa juu ya Masheikh Uamsho Mufti Bakwata amekosea

Uk. 2

Wasema Wanazuoni Dar

Afafanua msaada wao kwa wananchi Wanawaamsha Wazanzibar waliolala

Na Mwandishi Wetu
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar Dk. Amani Abeid Karume amewatoa wasiwasi Wazanzibari akisema kuwa hakuna haja ya kuwahoa Uamsho.

Maamuzi ya kususia sensa yalikuwa ya Shura Kukiuka Shura ni kuvunja maelekezo ya Quran Angelirejesha Suala hilo katika Shura ya awali

Karume amesema, hata wale wanaodhani hawawahitaji Uamsho, watambue pia nao Uamsho ina faida kwao lau watatafakari kidogo. Mheshimiwa Amani Abeid Karume akipiga

Inaendelea Uk. 2

2
Cel: 0784 370 208, 0652 849227, 0755 260 087, DSM. www.ipctz.org E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

TahaririMakala
AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786
MAONI YETU
Wahadhiri wanaoyasema haya kama yalivyokuja katika Qur an 5:75), Mwalimu wao ni Mtume Muhammad (s.a.w). Sasa kama Maaskofu na Wakristo kwa ujumla wanasema kuwa Wahadhiri hawa wanakashifu Ukristo, ina maana kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) ndiye Mwalimu Mkuu wa wanaokashifu Ukirsto. Hii maana yake ni kuwa kama Mtume Muhammad (s.a.w) angekuwa hai leo, ilikuwa awe wa kwanza kukamatwa katika ile kadhia ya mauwaji ya Mwembechai ambapo vyombo vya habari vya Bwana Reginald Mengi vilifanya kazi kubwa sana katika kuwabamiza Waislamu. Ni kwa mantiki hii, sisi hatudhani kuwa Mzee Alhaji Ally Hassan Mwinyi atakuwa

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012


mtu wa Kanisa na ni mtu anayelipenda sana Kanisa lake. Mengi atakuelewa ukimtajia Petro, Marko na Matayo. Lakini sio Abu Huraira, Imam Shafii au hata Barnabas aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu. Tunavyojua sisi Wakristo hawana upungufu katika watakatifu wala manabii. Wapo mpaka akina Kambarage ambao Kanisa hivi sasa lipo katika mchakato wa kumpa utakatifu. Hapana shaka Dr. Reginald Abraham Mengi angefurahi sana kama angesifiwa na kufananishwa na watu ambao anawakubali kwamba ni watakatifu kama Mtume Paulo au hata hawa Manabii wa kileo kama kina Mwingira, Mzee wa Upako na Mchungaji Getrude Rwakatare.

AN-NUUR

Reginald Mengi na Mtume Muhammad wapi na wapi?


YUPO Sheikh mmoja aliwahi kusema mbele ya Nyerere kuwa ni faradhi na amri ya Quran kwa Waislamu kutii viongozi wa serikali. Mwalimu Nyerere akamuuliza, hata akiwa Kaburu ? Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Mstaafu Alhaji Ally Hassan Mwinyi amemfananisha Dr. Reginald Mengi na Mtume Muhammad (s.a.w). Rais mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, amesema Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP Limited, Dkt. Reginald Mengi, ana sifa za kuitumikia jamii kama alivyokuwa Mtume Muhammad (s.a.w), limeripoti gazeti la Nipashe la Jumapili iliyopita. Alhaj Mwinyi: Mengi ana sifa kama za Mtume (Muhammad s.a.w), liliandika gazeti hilo katika kichwa cha habari hiyo na kisha kufafanua kuwa Alhaj Mwinyi amesema kuwa Waislamu wanavutiwa sana na tabia za Mengi kwani zinafanana na alizokuwa nazo Mtume Muhammad (s.a.w). Sifa hizo (za Mengi) ndizo alikuwa nazo Mtume Muhammad S.A.W. ambaye u m m a w a Wa i s l a m u unamheshimu, alifafanua Mwinyi kama alivyonukuliwa na Nipashe. Mzee Mwinyi aliyasema hayo katika hafla ya kumtunuku Mengi Tuzo Iliyotukuka ya Huduma kwa jamii iliyotolewa na iliyotajwa kuwa Kamati ya Amani ya Viongozi Mkoa wa Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Kamati hiyo ni Sheikh Alhad Mussa Salum ambaye alisema kuwa wanamsomea Dua maalum Dr. Mengi kwa kutambua mchango wake katika jamii. Katika haa hiyo Dr. Reginald Mengi alivaa koa sa ya Waislamu wa Pwani na Zanzibar ile ya kushonwa kwa mkono. Ukitaja jina Mtume Muhammad (s.a.w) mbele ya Mkristo yeyote, kwake huyo ni nabii wa uwongo. Kwa Mkristo yeyote, jina Muhammad linaleta picha ya mtu aliyefanya kazi kubwa ya kuvunja misingi ya Ukristo kwa kutangaza na kuwaonya wale wanaosema kuwa Yesu ni Mungu. Ni Mtume (s.a.w) kupitia Wahay aliopewa na Allah (S.W.T), aliyesema kuwa Yesu si Mungu wala si mmoja katika wale waungu watatu wanaoitakidiwa na Wakristo. Ni Mtume Muhammad (s.a.w) aliyefundisha kuwa Yesu hakufa Msalabani wala hatabeba dhambi za Wakristo kama wenyewe wanavyoamini kwamba Yesu aliteswa kwa ajili ya dhambi zao. Katika kusisitiza somo hilo, Mtume (s.a.w) akasema kuwa kwa hakika ni makari wale waliosema kuwa Yesu mwana wa Mariam ni Mungu. Na kafiri mahali pake ni Jahannam, siku ya Kiama. Atafurahi muda mfupi duniani kwa mali zake, watoto na cheo kwa sababu Allah ni Ar-Rahmaan. Lakini kwa mujibu wa yale aliyofundisha Mtume Muhammad (s.a.w), kafiri hana chake siku ya kiama. Kwake itakuwa Fii nari Jahannam; khaalidina iha abada. Kwa msemo uliozoeleka wa Maaskofu, ambao ni viongozi wa kiroho wa Reginald Mengi, Mtume Muhammad (s.a.w) anakashifu Ukristo. Masheikh na Wahadhiri wa Kiislamu wanaodarasisha na kusimama kwenye majukwaa na kuvunja Utatu (Trinity), ambayo ni imani ya msingi katika Dini ya Mengi, basi mwalimu wao ni Mtume Muhammad (s.a.w). Wahadhiri hao wa Kiislamu wanawatanabahisha pia Wakristo kwamba Yesu Si Mungu na kwamba Hakuwa yeye Yesu ila ni Mtume tu, ni binadamu ambaye yeye na mama yake wakila chakula na kwenda haja kubwa.

Inatoka Uk. 1 mfano mwepesi kabisa kumfanya Boraa kufahamu, aliwafananisha Uamsho sawa na waamsha daku. Akasema, kuna Waislamu katika mwezi wa Ramadhani hawahitaji kuamshwa kula daku, wanaamka wenyewe. Lakini wapo wengine, bila kupita kigoma cha kula daku wanaweza wasile daku siku hiyo. Katika hali hiyo akasema kuwa, yule ambaye hana usingizi wa kuhitajia kuamshwa, anaweza kuwaona kula daku kama kero. Lakini akitokea kukurupushwa na kigoma cha kula daku, japo anaweza kukasirika, lakini akitizama saa akiona muda umefika, atafurahi na kula daku yake. Akizungumza katika mkutano uliofanyika Jimbo la Rahaleo Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Dk. Karume alisema kwamba CCM haijalala hivyo wanachama wa CCM hawana sababu ya kuwa na hofu na Uamsho kwani wao hawakulala na wenye kuamshwa ni wale waliolala. Kwani nyie mmelala mpaka muamshwe, nyie mko macho etihao ni kama wale wanaoamsha daku utakasirika, lakini ukiamka unasema ahaa kumbe muda wa kula daku; tena hofu ya nini? Alisema Dk. Karume na kuwachekesha waliohudhuria mkutano huo. Makamu huyo Mwenyekiti alilazimika kutoa maelezo

Karume ampasha Boraa juu ya Masheikh Uamsho


hayo baada ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mjini Unguja, Borafia Silima Juma kueleza wasiwasi wa wanachama wa CCM kuhusu vurugu zilizotokea mwezi Mei mwaka huu na kuhusishwa na kundi la Uamsho. Dk. Karume akijibu hilo, alisema juhudi za kuiweka Zanzibar katika hali ya maelewano ilifanywa na Jumuiya za Kimataifa na Mataifa kutoka nje, lakini hawakuweza kusuluhisha migororo ya kisiasa iliyodumu kwa takriban miongo mitatu, lakini baada ya Wazanzibari wenyewe kuamua kuacha tofauti zao maridhiano yalikiwa mwaka 2009. Akitoa historia feru na miafaka na maridhiano, Dk. Karume alisema wakati wa utawala wake walihakikisha kabla ya kumaliza kipindi cha utawala wake anaiwacha Zanzibar ikiwa salama, yenye umoja na mshikamano na isiyokuwa ya vipande vipande ambapo hali hiyo ilifanikishwa baada ya kufikiwa kwa maridhiano ya kisiasa baina ya Chama ch Wananchi (CUF) na Chama cha Mapinduzi (CCM). Mimi na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad tulikutana Ikulu na kukazungumza kwa nini tusimalize tofauti zetu maana sisi sote ni wamoja na leo mafanikio yake ndio haya ya Zanzibar imetulia kwa hivyo natoa wito wa kuendeleza umoja huu. Alisema Dk.

amemtendea haki Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dr. Reginald Mengi kumfananisha na Mtume wa uwongo kwa mujibu wa imani yake. Hatuamini pia kuwa Dr. Mengi alifurahi kufananishwa na mtu ambaye kwa imani yake na kwa msimamo wa Maaskofu wake ni Mwalimu Mkuu wa Wahadhiri wanaokashifu Ukristo. Japo lengo la Mzee Mwinyi lilikuwa kumsifu Mengi, lakini hatudhani Dr. Reginald Mengi amekia mahali pa kupenda sana sifa kiasi cha kutokujali ni sifa gani anapewa au anafananishwa na nani. Ni kwa sababu hiyo, hatudhani kuwa Mengi atakuwa amefurahi kufananishwa na mtu anayekanusha uungu wa mwokozi wake Yesu Kristu. Sisi tunamjua Dr. Mengi kwamba ni mtu wa dini. Ni

Karume. Akizungumzia suala la maoni kuhusu Muungano, Makamu huyo Mwenyekiti wa CCM alisema watu wote wanaotoa maoni kimsingi wanatumia haki ya kikatiba na kidemokrasia hivyo wana CCM wanachotakiwa ni kuendelea kusimamia azma ya ujenzi wa chama chao huku wakiendelea kuheshimu misimamo yao bila ya kuyumbishwa. Msipatwe na homa, ondoeni hofu na wasiwasi , waacheni Masheikh wajibishane na Masheikh wenzao na sisi wanasiasa tutafute majibu mujarab yatakayofaa ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha vijana wetu kutambua mahali tulikotoka, tulipo sasa na kule tuendako, alisema. Mkutano huo uliofanyika katika Tawi la Gulioni ambako alizungumza na wanachama wa matawi mawili la Gulioni na Mwembeladu ni wanachama wachache waliohudhuria tofauti na matarajio ya watu wengi ambapo kuliwekwa mabomba nje ya tawi hilo lakini wasikilizaji walikuwa kidogo mno. Viongozi walioambatana na Dk. Karume ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini, Yussuf Mohammed, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mjini Borafya Silima, Mbunge wa Rahaleo, Abdallah Juma Abdallah (Maabodi), na Mwakilishi wake Salim Nassor (Aljazira),

3
Na Shaaban Rajab
ZIPO taarifa kuwa Waislamu nchini wanapanga kufanya maandamano nchini kupinga kitendo cha kudhalilishwa Sheikh wao Nurdeen Kishki pamoja na Masheikh wengine aliokuwa nao. Habari zinasema kuwa lengo jingine ni pamoja na kumtaka Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani kuomba radhi kwa udhalilishaji huo na serikali kutoa tamko la kukemea kitendo hicho. Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana tukienda mitaani, kuna vikao vya ushauri vinaendelea katika Misikiti, Taasisi na Jumuiya mbalimbali za Kiislamu ambapo baadae itafanyika Shura ya pamoja kuamua nini la kufanya juu ya kadhia hii. Shura na vikao hivo vinakuja kufuatia taarifa ya kukamatwa na kudhalilishwa Sheikh Nurdin Kishki. Tukio hilo limeelezwa kuwa ni katika kuendeleza mwitikio wa kile kinachoitwa mapambano dhidi ya ugaidi. Katika tukio hilo, Sheikh Nurdin Kishki na Masheikh wenzake wakiwa wameambatana na ujumbe wa Masheikh kutoka Yemen akiwemo Mufti wa Yemen, juzi Jumatano walifanyiwa udhalili mkubwa na polisi baada ya kukamatwa na kudaiwa kuwa ni majambazi. Wakiwa njiani kutokea Tanga kuja jijini Dar es Salaam, Sheikh Kishki na wenzake walivamiwa na polisi Bagamoyo mkoani Pwani na kuamriwa kulala chini huku wakisukwa sukwa wakishukiwa kuwa ni majambazi. Umati wa watu wakiwemo watoto wadogo walijazana katika eneo la tukio kushuhudia Masheikh hao baada ya taarifa kuzagaa kwamba watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamekamatwa na polisi. Hata hivyo wengi walishangaa na kupigwa na butwaa baada ya kukuta kuwa watu waliokuwa wakishukiwa kuwa ni majambazi, walikuwa ni Masheikh akiwemo Mufti wa Yemen, ambao walikuwa wamelazwa chini huku polisi wakiwazingira chini ya ulinzi mkali. Hata baada ya Masheikh hao kujieleza na kujitambulisha kwamba wao sio majambazi kama taarifa za polisi zinavyosema bali ni Masheikh waliokuwa safarini kuja Dar es Salaam, utetezi huo haukutosha kuwafanya polisi kuacha kuwadhalilisha kwani waliendelea kupigwa

Habari

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012


hivi ndivyo wao na viongozi wao wanavyohudumiwa kwa sababu ya itikadi yao. Alibainisha Kishki N a y e S h e i k h Wa z i r Maduga alisema kuwa tukio la kudhalilisha Masheikh akiwemo Mufti wa Yemen, ni agenda ya kuwatoa Waislamu katika mada zao ya msingi hivi sasa ya kutoshiriki zoezi la sensa na kutaka Baraza la Mitihani nchini livunjwe. Alisema msimamo na m a a m u z i y a Wa i s l a m u yataendela kubakia pale pale hata zikiletwa agenda za kutengenezwa ili kuwahamisha Waislamu katika msimamo wao. Alisema, Masheikh wanaojipendekeza serikali huku serikali hiyo hiyo ikija kuwadhuru Waislamu, wao waendelee na njia yao hiyo kwani Waislamu tayari wamejiweka katika njia yao nyingine ya haki katika kudai haki zao na watabaki katika kutetea haki zao hizo. Hata hivyo Waislamu wengi wanaamini kuwa sababu kubwa ya kukamatwa Sheikh Kishki na wenzake ni zilezile zilizozoeleka za kuhusishwa na ugaidi, japo safari hii polisi wamejaribu kupamba sababu hizo kwa ujambazi.

AN-NUUR

Muoneeni huruma Kamanda Ernesti


Na Omar Msangi HAPANA shaka hivi sasa Wa i s l a m u w a t a k u w a wanatokota kwa hasira. Wanajiuliza, vipi ingekuwa msafara wa Mchungaji Zakaria Kakobe, Polisi wangemkamata na kumburura chini? Vipi ingekuwa ni msafara wa mapadiri na Kanzu zao za Kipadiri na misalaba yao shingoni, Kamanda Ernesti angewatuhumu kuwa ni majambazi na kuwalaza chini kifudifudi na kuwagaragaraza katika vumbi? Waislamu wanajiuliza maswali haya baada ya kupata habari kuwa Sheikh Nurdeen Kishki na msafara wa Masheikh wengine aliokuwa nao, walikamatwa na polisi juzi na kudhalilishwa. Ni kutokana na taarifa hizo, Waislamu wanajiuliza, hivi ungekuwa msafara w a mchung a j i S y l v e s t a Gamanywa na watumishi wa Mungu wenzake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Afande Ernesti angewafanyia uhuni na udhalilishaji huu aliowafanyia Masheikh wetu? Japo zimetajwa tuhuma za ujambazi, lakini kinachojidhihirisha ni kuwa walidhaniwa kuwa magaidi. Sheikh Kishki anafahamika. Polisi hasa katika ngazi ya makamanda wa mikoa wanamjua sana kutokana na mihadhara yake na kanda zake zilizosambaa nchi nzima. Kishki alikuwa akitokea Arusha na Tanga na kote huko Polisi walikuwepo na walimwona akitoa mawaidha, akiongea na Waislamu. Kwa hiyo suala la Kamanda wa Pwani kupewa taarifa na yule wa Tanga kwamba kuna majambazi yanakuja kama Afande Ernest anavyodai halipo. Ni uwongo. Lakini Kishki alikuwa na Masheikh kutoka Yemen na Yemen ni nchi ya magaidi kama ilivyo Pakistan na Afghanistan. Na hii si kwa mujibu wa taarifa za kiusalama za akina Ernest na wanausalama wetu wa Ta n z a n i a k w a u j u m l a . Lakini kwa mujibu wa maelezo tunayopewa kutoka Washington na kwa mujibu wa False Flag Terror Attacks zinazoendelea kutekelezwa katika nchi hizo. Nina wasiwasi, na nina haki ya kuwa na wasiwasi, kuwa udhalilishaji waliofanyiwa Masheikh wetu pale Bagamoyo, hayakutokana na taarifa za kikachero za Polisi wetu. Japo waliotekeleza ni wao, na hawawezi kuepuka lawama, lakini inavyoonekana walikuwa wakitekeleza maelekezo kama yale waliyopewa wakawakamata Watanzania wenzetu wasio na hatia wakati akija Bush. Inavyoonekana Polisi wetu waliomgaragaza Sheikh Kishki, walishindwa kukataa kutekeleza maelekezo waliyopewa kama ambavyo walishindwa kuzuiya mbwa wa Marekani kumdhalilisha Mheshimiwa Benjamin William Mkapa na kama walivyoshindwa kuwazuiya makachero wa Marekani kupanda darini Ikulu nchini mwetu. Kwa hiyo, pamoja na hasira ambazo watakuwa nazo Waislamu hivi sasa, lakini binafsi naona badala ya kukasirika, pengine ingekuwa vema zaidi kuwaonea huruma

na kugaragazwa sakafuni kama majambazi. Hata hivyo taarifa zinaeleza kuwa taarifa zilipelekwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mwantum Mahiza ili kuja kuingilia kati tukio hilo kufuatia askari waliowakamata mashekh hao kuendelea kushikilia msimamo wao wa kuwadhalilisha. Shuhuda mmoja wa tukio hilo alieleza kuwa kufuatia Mkuu wa Mkoa kupewa taarifa hiyo, alijibu kuwa tayari amemwagiza OCD wa Wilaya ya Bagamoyo kuchushughulikia mkasa huo hivyo Waislamu wavute subra OCD huyo hadi atakapoka mkuu huyo katika kituo cha polisi Bagamoyo ambako ndiko Sheikh Kishki na wenzake wanashikiliwa. Wakati Mkuu huyo wa Polisi Wilaya akisubiriwa, Waislamu walishamiminika kituoni hapo kujua hatma ya Masheikh hao.

Maandamano makubwa kufanyika nchi nzima


Kufuatia umati kuwa mkubwa, polisi waliamuru Waislamu kuondoka mara moja kituoni hapo lakini waligoma na kusisitiza kwamba hawawezi kuondoka hadi wafahamu sababu ya kukamatwa Masheikh hao na kujua hatma yao. Hata hivyo baada ya polisi hutakiwa kueleza ni kwa nini wamefikia kuwadhalilisha Masheikh hao bila kuwa na udhibitisho wa makosa, polisi walidai kuwa wao wamepata taarifa (information) kutoka Ta n g a k w a m b a k u n a majambazi wanakuja. Hata hivyo hawakufafanua zaidi. Akizungumzia katika tukio hilo, Sheikh Nurdin Kishki alisema kuwa tukio hilo limewadhalilisha sana Mashekh hao na viongozi wa Waislamu na Waislamu kwa ujumla hivyo amemtaka Inspekta Janerali wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema kufanya uchunguzi mapema

na maosa waliowadhalilisha wachukuliwe hatua mara moja. Alisema udhalilishwaji huo kamwe hautakaliwa kimya. Alisema hata kama maosa hao wa polisi walikuwa wanawashuku, hawakustahili kuwaburuza na kuwalalisha chini kama wahuni. Kama wametushuku na walikuwa wamekusudia kufanya uchunguzi dhidi yetu, wangetuhoji kistaarabu hapo kituoni kwao na kama hawakuridhika, basi wangetuhifadhi kistaarabu kwa kuwa tayari tulikuwa kituoni, naamini kama wangekuwa ni Mapadri udhalilishwaji huu usingefanyika hata kama wangeshukiwa ujambazi. Lakini kwa kuwa Kishki amevaa kanzu ana koa na kilemba, basi hao ndio, wa kulazwa chini, kupigwa, kufanyiwa kejeli, tena tukiwa na wageni wetu kutoka nje ya nchi, hili latosha kuwafanya Waislamu watambue kuwa

Hakudhalilishwa Kishki pekee Hata Mkapa alishadhalilishwa


hawa akina Ernest maana wakati mwingine wanakuwa hawajui walifanyalo. Kama tutatanguliza hasira, tutakosa huruma kwa wenzetu hawa halafu tutashindwa kuwasaidia na hasara itakuwa pia juu yetu na kwa nchi yetu kwa ujumla. Wakati tukitafakari kadhia hii ya kudhalilishwa Sheikh wetu Kishki, ndio nikasema tukumbuke pia kile kisa cha kudhalilishwa aliyekuwa Rais wetu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa pale Arusha ambapo mbwa wa polisi wa Marekani walinusa gari lake ili kuhakikisha kuwa hapakuwa na gaidi ndani au bomu la kigaidi ambalo lau lingelipuka, lingemdhuru Bwana Mkubwa kutoka Marekani, Bill Clinton! Katika tukio lile, akina Ernesti wetu walikuwepo na hata vyombo vya usalama vya nchi yetu, lakini hawakuweza kumsaidia Rais wetu asidhalilishwe. Ukitaka kujua uzito wa jambo hili, hebu jaaliya raki Inaendelea Uk. 10

4
Na Azza Ally Ahmed
WA I S L A M U a c h e n i kukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kufuata mkumbo wa vunja jungu. Ndugu zangu Waislamu, dhana ya vunja jungu inabeba mambo machafu kama uzinzi, unywaji pombe, miziki na mengineyo. Wenye tabia hii ya vunja jungu ni wale wanaokusudia kurudi upya katika maovu baada ya mwezi wa Ramadhani kuisha. Yaani wale wanaoifanyia mzaha Dini ya Allah. Nikinukuu hadithi ya Anas isemayo, walikuwa Waislamu kila ukikaribia kuingia kwa mwezi wa Ramadhani wakisoma sana Quran na wale wenye uwezo kimali wakitoa mali zao kuwapa maskini ili kuwapa nguvu za kuingia katika mfungo hali yakuwa wana uhakika (Kujiandaa na mfungo wa Ramadhani). Mwenyezi Mungu ( s . w. ) a n a t u f a h a m i s h a kwamba: Enyi mlioamini m m e l a z i m i s h w a kufunga (swaumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu. (Qur. 2:183). Maneno haya matukufu yana mafunzo makuu matatu. Kwanza, kufunga ni amri wala si jambo la hiari. Pili, kutokana na maslahi yanayopatikana katika funga, maslahi ambayo ni muafaka kwa maumbile ya binadamu, amri hii pia inawahusu wanadamu waliokuwepo kabla yetu. Tatu, tunafahamishwa kuwa, kwa kuitekeleza amri hii tutalikia lengo la kuumbwa kwetu. Lengo ambalo tusingelifahamu bila ya kuelimishwa na Mwenyezi Mungu (s.w.) pale alipotuambia kuwa: Sikuwaumba majini na wanaadamu ila wapate kuniabudu (Quran 51:56) Ni vipi Mwenyezi Mungu (s.w) anatutaka tumuabudu katika mwezi wa Ramadhani? Je, hii ina maana kuwa katika miezi mingine ya mwaka mzima hatutakiwi kumuabudu au kumtii Mwenyezi Mungu (s.w.)? J i b u n i Tu n a t a k i w a kumuabudu au kumcha Mwenyezi Mungu (s.w.) kwa masaa yote 24 ya kila siku na katika kila kipengele cha maisha yetu kwa mwaka mzima. Pili tunatakiwa kumcha Mwenyezi Mungu kwa juhudi zetu zote mpaka

Makala/Tangazo

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012


malengo bora zaidi kwa mwaka ujao. Endapo utakuwa umebahatika kuifahamu tunu hii na kuitekeleza ni kheri kwako. Endelea na ongeza juhudi. Na endapo utakuwa huifahamu tunu hii, basi hujachelewa bado, wakati ni huu; utumie na usiupoteze. Tahadhari kwa ndugu zangu Waislamu: Tusijiwekee malengo mengi ambayo yatatushinda kutekeleza. Tujiwekee malengo makuu mawili au moja ili tutakapofanikisha tupate motisha ya kujiongezea mengine. Tutie nia ya kutorudia tena kwenye maasi. Mtume wa Allah (s.w.) amesema: Yeyote anayedhamiria kufanya jambo jema lakini hakufanikiwa kulifanya jambo hilo, Allah anamwandikia malipo (kama aliyefanya). (Bukhari na Muslim). Tujenge uhusiano mwema na Ndugu jamaa na majirani zetu ambao tulikhitalifiana kati yetu kwa mambo mbali mbali ya kimaisha. Tufuatilie kalenda ya Kiislamu ili siku ya kuanza kufunga isitukute kwa mshtuko mkubwa na kutokujiweka tayari katika hilo. Kwa kifupi tujiandae kwa kutekeleza yale yote yanayomfurahisha Mwenyezi Mungu; na tujiepushe kabisa na yote yasiyompendeza Allah (s.w.)

AN-NUUR

Vunja jungu

mauti yatukute tukiwa Waislamu wa kweli. Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha; wala msife isipokuwa mmekwisha kuwa Waislamu kamili. (3:102) Na katika kumtii Mwenyezi Mungu tunatakiwa tusichague baadhi ya mambo ya kufanya kwa kuwa tu tunayapenda na kuacha mengineyo ambayo hatuna mapenzi nayo, bali, ni kufuata amri zote au kwa maneno mengine ni kutii kila kipengele kilichopo katika maisha yetu. Enyi mlioamini! Ingieni katika hukumu za Uislamu zote, wala msifuate nyayo za shetani; kwa hakika yeye kwenu ni adui dhahiri. (2:208) Kama utaratibu wa kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w.) ndio huu, inakuwaje Allah (s.w.) atuamrishe kufunga Ramadhani ili tupate kumuabudu? Kuna hekima gani katika mwezi wa Ramadhani tofauti na miezi mingine? Ni kuwa, katika mwezi wa Ramadhani tunapewa au tumetunukiwa nafasi ya pekee. Nafasi ambayo kama tutaitumia ipasavyo itatusaidia kulikia lengo la kuumbwa kwetu. Kuhusu kheri zinazopatikana ndani ya mwezi wa Ramadhani,

Nabii Muhammad (s.a.w.) anasema: Mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa Mwenyezi Mungu ambao ameujaza Rehma, Baraka na Msamaha. Na pia ni ukweli usio na shaka kuwa, kwa kutokuzingatia taratibu

Inawatangazia Waislamu wote kuwa imeandaa safari ya Hijja na Umra mwaka 2012 kwa dola (US) $ 3375 tu. Mambo yatakayogharamiwa. Semina za Hijja, Huduma za Afya, Airport charge na Tiketi za ndege, Nyumba za kulala Makka na Madina, Ihram na Kuchinja kwa ajili ya Tamaa-tuu, Chakula wakati wote, Usari na ziara Makka na Madina, Mahema Mina na Arafa. KUHIJIWA ni DOLA US $ 1450. Fomu zinapatikana. 1 Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam- Magomeni Mtaa wa Dosi na Mkadini Nyumba namba 26 Mkabala na Show Room ya Magari Tel: 0713 730 444 au 0773 804101 au 0785 930 444 au 0773 930 444. 2. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar RahaLeo Tel: 0777 484982, 0777 413987. 3. Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar Es salaam Tel: 0784 453838. 4. Abdallah Salehe Mazrui ( Hoko) Dar es salaam Tell. 0715 72 4444. 5. Salim Is-haq Dar es Salaam Tell: 0754 286010, 0774 786101. 6. Dukani kwa Mohamed Hadh Mazrui Wete Pemba Tel: 0777 482665. 7. Sheikh Daudi Khamis Sheha Tel: 07776 79692. 8. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar Tel: 0777 417736. Wahi mapema kulipia ili ushughulikiwe mapema, kama utalipia kwa Account No 048101000030 NBC piga simu kwanza 0774 412975. Kumbuka kikundi cha Ahlul Daawa ni cha Bei nafuu zaidi na huduma zake ni bora zaidi ya vikundi vingine.

Ahlul Daawa Hajj and Travel Agency

za mwezi wa Ramadhani tutakuwa ni wenye kuipoteza tunu adhimu ambayo imetoka kwa Allah s.a.w, kwa wenye hasara kubwa duniani na akhera. Mwezi wa Ramadhani unatupa nafasi ya kuanza maisha mapya na kujiwekea

Kimataifa/Tangazo

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012

AN-NUUR

Tantawi kuendelea kuwa Waziri wa Ulinzi Misri


CAIRO Kiongozi wa Baraza Kuu la Kijeshi nchini Misri, (SCAF) Mohammad H u s s e i n Ta n t a w i , ataendelea kuwa Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo kwenye serikali mpya inayotarajiwa kutangazwa na Rais mteule, Mohammad Morsi. Hayo ni kwa mujibu wa Meja Jenerali Mohamed Assar, asa wa ngazi za juu kwenye baraza hilo. Assar ameiambia televisheni ya CBC kuwa Tantawi, atakuwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Misri sambamba na kuendelea kushikilia wadhifa wake kama Waziri wa Ulinzi. J e n e r a l i Ta n t a w i amekuwa akishikilia wadhifa huo kwa zaidi ya miaka 20 chini ya utawala wa kiimla wa Hosni Mubarak aliyepinduliwa na wananchi mwaka uliopita. Wakati hayo yakijiri, mahakama moja nchini Misri imemhukumu aliyekuwa Waziri wa Nishati kifungo cha miaka 15 gerezani kwa makosa ya ubadhirifu wa mali ya umma pamoja na ulaji rushwa. Mahakama hiyo imesema kwamba Sameh Fahmy, aliuuzia utawala haramu wa Israel gesi kwa bei nafuu ambapo mkabala wake alipokea fedha na zawadi zingine kutoka Tel Aviv.
MAAFISA usalama wa Marekani wakiwakamata waandamanaji nchini humo.

Marekani mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu


WASHINGTON Sarah Flanders, ambaye ni miongoni mwa wakurugenzi wa kituo cha kimataifa cha kupinga vita na ubepari cha The International Action Center (IAC) anaamini kwamba Marekani ndiyo mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu duniani. Televisheni ya Press imemnukuu Sarah Flanders, akisema kuwa hii leo Marekani ndiyo mkiukaji mkuu wa haki za binadamu duniani ndani ya nchi na katika medani ya kimataifa. Kituo cha The International Action Center (IAC) kinakusanya pamoja

Waislamu wasusia Coca Cola, Pepsi Cola


WAISLAMU wa Ufaransa wameanza kususia vinywaji vya Coca Cola na Pepsi Cola baada ya kufichuliwa habari kwamba watengenezaji wa vinywaji hivyo wanatumia kileo katika utengenezaji wake. Kituo cha Press Tv kimeripoti kuwa jarida la Kifaransa la 60 Million Consumers limechapisha ripoti ya uchunguzi ambao umebaini kuwa makampuni ya Coca Cola na Pepsi Cola yanatumia kileo katika utengenezaji wa vinywaji hivyo, suala ambalo limeifanya Jumuiya ya Waislamu wa Ufaransa itoe taarifa ikitangaza kuwa imeanza kususia bidhaa hizo. Kwa mujibu wa uchunguzi wa Taasisi ya Taifa ya Watumiaji (National Consumer Institute (INC)), mada 19 zinazotumiwa katika utengenezaji wa vinywaji vya Coca Cola na Pepsi Cola zimefanyiwa utati na kuonesha kuwa kuna kileo cha miligramu 10 katika kila lita moja ya vinywaji hivyo. Baada ya kushuhudia matokeo ya uchunguzi huo, tunahisi kwamba tumehadaiwa. Makampuni makubwa yanaelewa k w a m b a Wa i s l a m u wanatumia vinywaji vya Pepsi na Coca Cola na hatua ya kutoandikwa kiwango cha alkoholi kilichomo ndani ya vinywaji hivyo ni sawa na kuwahadaa

Rais mteule wa Misri, Mohammad Morsi.

wanaharakati wanaopinga vita na siasa za kibepari za Marekani. Flanders amesema kuwa harakati ya kuteka Wall Street ni mfano wa yale yanayotendeka mara kwa mara nchini Marekani. Amesema kuwa kutiwa mbaroni kwa wingi watu wasiokuwa na hatia, kutolewa taswira isiyokuwa sahihi kuhusu vyombo vya habari na kuwatambua vijana wanaopigania haki zao kuwa ni wahalifu, ni mifano ya wazi ya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na serikali ya Marekani.

Waislamu. Alisema Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ufaransa, Muhammad Bishari. B w. B i s h a r i p i a amezilaumu taasisi nyingine za Kiislamu nchini Ufaransa kwa kunyamazia kitendo hicho na kusema kuwa taasisi muhimu za Kiislamu zinapaswa kutekeleza majukumu yao katika suala hilo.

Habari

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

AN-NUUR

Na Bakari Mwakangwale kauli ambayo haikuwa na shura kwa kuzishirikisha UMOJA wa Wanazuoni taasisi zingine kama wa Kiislamu Tanzania ilivyokuwa awali. (Hay-Atul-Ulamaa), Kwa upande wake u m e s e m a , M u f t i w a Maalim Ally Baswaleh, Bakwata Sheikh Shaaban akijibu swali nani msemaji S i m b a , a m e k h a l i f u wa Waislamu kutokana Uislamu kwa kubatilisha na matamko kutoka na kauli na msimamo wa msimamo tofauti, alisema pamoja ya Waislamu kwa hali ilivyo ni sawa kutoshiriki Sensa. na vyama vingi vya siasa, Hayo yamebainihwa kila mmoja anamwaga na Umoja huo, Jumatano sera zake hivyo mwenye wiki hii wakiongea na sera yenye mashiko ndie Waislamu katika Hoteli atakayefuatwa. ya Tansoma, Kariakoo Awali akisomo tamko Jijini Dar es Salaam, la Hay-Atul-Ulamaa, juu wakisisitiza msimamo ya ushiriki wa Sensa kwa wa Waislamu kutoshiriki Waislamu alisema, msima Sensa inayotarajia kuanza wao unabaki palepale Agosti 26, mwaka huu. na kuwataka Waislamu Aidha umoja huo pia kutoshiriki zoezi hilo umesema, kuwa msimamo mpaka pale Serikali itakapo kwa Waislamu ni ule tekeleza matakwa yao ulioshirikisha Jumuiya na ya kuingizwa kipengele Taasisi zote za Kiislamu cha dini katika dodoso la baada ya kukaa Shura Mjini Sensa yatakapotimizwa. Dodoma muda mfupi baada Alisema, Hay-at, inataka ya kikao cha viongozi wa ieleweke, si kwamba Dini na Serikali, ambapo Waislamu wanapinga Sensa Serikali ilikataa maombi au hawaelewi umuhimu ya Waislamu na kukubali wake, bali wanalichukulia zoezi hilo katika mambo ya Maaskofu. Kwa hiyo, kama Mufti yanayoendana na Sunnah a l i o n a k u n a h a j a y a ya Mtume (s a w), kwani kubadili msimamo, basi baada ya kuhamia Madina, angelirejesha suala hilo aliagiza ifanywe hesabu katika Shura liangaliwe ya idadi ya wakaazi wote wa mji huo, ili kuweza upya. kuwapatia huduma za Wa k i j i b u m a s w a l i kijamii. kutoka kwa waandishi Kutokana na kuelewa w a h a b a r i w a l i o t a k a vyema umuhimu wa sensa kujua Waislamu wafuate kwa maendeleo ya jamii, msimamo gani baada kamwe hawezi kupinga, ya Mufti kutoa tamko la lakini imebidi waisusie kuwataka kushiriki Sensa, kutokana na kupuuzwa Sheikh Abdallah Bawazir, madai yao ya msingi. amesema kiitikadi Mufti Alisema Maalim Bassaleh S i m b a , a m e k h a l i f u akisoma tamko lao. Alisema, upo umuhimu Uislamu. mkubwa wa kuelewa Akisherehesha nukuu ya idadi ya Watanzania kwa aya Qur an 4:115, alisema mujibu wa dini zao kwani kwa kuzingatia aya hiyo, kama hakuna umhimu Waislamu walishafanya huo, vipi Televisheni ya Shura yao na wakatoa njia Taifa-TBC1, itangaze yao ya kufuata, ambayo takwimu kama hizo kisha ni kutoshiriki katika zoezi ije kuomba radhi. lijalo la sensa, sasa Mufti Kutokana na utata huo, amekengeuka katika njia alisema Maalim Basaleh, hiyo ya Waislamu. ndio maana Waislamu Alisema, tamko la awali watoa rai kwa Serikali yao lilijumuisha Taasisi zote kuwa kipengele cha Dini za Kiislamu ikiwemo kirejeshwe kuonyesha Bakwata, hivyo Waislamu katika kuanzia sensa ya wasiyumbe kutokana na mwaka huu, ili zipatikane

Mufti Bakwata amekosea Wasema Wanazuoni Dar


takwimu rasmi na sahihi. Alisema, wale wanao dai kuwa sensa kwa dini haina faida yoyote kwa taifa, lakini hawahoji na kuuliza kuwa dodoso za kuhoji idadi ya Misikiti na Makanisa, zinafaida gani, na vipi basi pasiwe na ulazima na faida ya kujua idadi ya waumini watakao zitumia nyumba hizo. Alisema, ni dhahiri kuwa Waislamu hawatoshiriki

zoezi hili la Sensa Agosti, na hata za miaka ijayo mpaka pale kipengele cha dini kiwekwe katika dodoso la sensa na usimamizi wake uwe wa uwiano baina ya dini zote.

Madaktari Waislamu wafungua kituo cha afya Dar


Na Abdulkarim Msengakamba

DAKTARI bingwa wa magonjwa ya wanawake Dkt. Muzdalifa Abeid (aliyekaa katikati) akiwa na baadhi ya madaktari wenzake wa MSV)

JUMUIA ya Wataalam wa Afya wa Kiislamu nchini, Muslim Sunshine Volunteers (MSV) imefungua kituo cha afya jijini Dar es Salaam. Kituo hicho cha utabibu kiitwacho SMV Maternity and Child Care kimefunguliwa Ilala mtaa wa Kigoma na Bukoba jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Kituo hicho kimeanza kutoa huduma ya afya kwa wanawake na watoto chini ya miaka mitano. Akizungumza katika

haa ya uzinduzi wa kituo hicho, daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake Dkt. Muzdalifa Abeid, alisema kituo hicho kitakuwa kinatoa huduma za matibabu na kuwashauri wanawake na watoto chini ya madaktari bingwa wa kada hiyo. Jumuia hiyo yenye w a j u mb e mad ak tar i 13, ilianzishwa mwaka 2007 nia kubwa ikiwa ni kuufikishia umma huduma ya afya kwa karibu kwa misingi ya Kiislamu. Siku ya ufunguzi wa kituo hicho, madaktari hao waliendesha huduma mbalimbali kwa akina

mama ikiwa ni pamoja na kuwafanyia uchunguzi wa magonjwa ya saratani ya matiti na stula. Aidha wataalam hao walitoa elimu kwa ujumla kwa akina mama juu ya maradhi hayo ambapo walifunzwa namna ya kujichunguza, kutambua dalili, hatua za kuchukua na namna ya kuendea tiba ya maradhi hayo. Kabla ya kufungua kituo hicho, MSV imekuwa ikiendesha huduma mbalimbali za kitabibu katika sehemu mbalimbali nchini, i k i w e m o Wi l a y a n i Ikwiriri, kupima afya za akina mama mkoani Morogoro.

7
Na Omar Msangi
ALIWAHI kusema msemaji mmoja kwamba japo Uislamu na Ukristo zote ni dini, lakini kuna tofauti kubwa sana kati ya dini hizo. Katika kutoa ufafanuzi akatoa maelezo yafuatayo: Anasema, Yesu amezaliwa mamilioni ya miaka baada ya kuumbwa dunia. Yesu amezaliwa maelfu ya miaka baada ya kuumbwa Adam na Hawa. Na Yesu amezaliwa na mama. Amezaliwa na mama anayejulikana kwa jina. Ni Binti Fulani. Mtoto wa fulani. Na kwamba hata ngariba aliyemtahiri siku ya siku saba baada ya kuzaliwa, anajulikana kwa jina. Lakini Yesu huyo huyo tunaambiwa kuwa ndiye Mungu Mkuu! Anasema, hoja hizi hizi katika Uislamu ni kinyume chake. Zinatumika KU-REASON, kujenga hoja kuonyesha kuwa mtu mwenye sifa hizo hawezi kuwa Mungu. Katika jumla ya mambo ambayo yamepigiwa zumari sana katika nchi hii na kuonekana kana kwamba ndio ukweli wenyewe, ni suala la udini. Kila anayesimama katika jukwaa la kisiasa na kila anayeandika na kuzungumza katika vyombo vya habari, ataimba wimbo huo huo. Kwamba nchi hii haina udini. Kwa nini? (eti) Mwalimu Nyerere alipigania utaifa akaondoa udini na ukabila. Na kwa maana hiyo hiyo, watendaji na viongozi serikalini hufanya kazi kwa kujali masilahi ya taifa. Hawana upendeleo. Huu ndio msingi wa nasaha za Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dr. Alex Malasusa pale alipowaomba Watanzania kujihadhari na tabia ya udini aliyodai kuwa inaanza kuchipua nchini. Kwamba udini huo ukiachwa kuota na kuchanua itakuwa sababu ya kuleta machafuko ya wenyewe kwa wenyewe nchini. Askofu Malasusa alitoa nasaha hizo katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa Sinodi ya 12 wa kanisa hilo. Hotuba hiyo ilisomwa kwa niaba yake na Askofu Paul Akyoo wa Dayosisi ya Meru, Arusha. Anachosisitiza hapa Askofu Malasusa katika nasaha zake ni kuwa Tanzania kulikuwa hakuna udini, ila sasa ndio kuna watu wanaotaka kupanda mbegu hiyo. Kwa hiyo anataka Watanzania wasiipe nafasi mbegu hiyo kumea. Yupo Mbunge mmoja kutoka Zanzibar Alhamisi iliyopita aliongea maneno mazito sana bungeni, lakini kwa bahati mbaya yamepotea bure. Yeye alishangaa kuona wabunge wengi kusimama kudai nao wapate mgao wa chenji ya rada. Chenji ya rada ni zile fedha za rushwa na usadi zilizorejeshwa na serikali ya Uingereza. Anasema, watu wanagombea fedha hizo utadhani kuna biashara ilifanyika sasa imezaa faida nzuri. Kwamba suala la msingi ilikuwa kujua nani alihusika na usadi ule na kuhakikisha kuwa anachukuliwa hatua. Lakini watu wamengangania kupata mgao wa pesa ya ufisadi iliyorejeshwa. Sasa hawa ni wabunge. Na huko ndani ya serikali kwenyewe kinachosikika ni kupanga namna ya kuzitumia pesa hizo. Kwamba zikanunulie madawati na vitabu shule za msingi naSuala nani alihusika na usadi ule na achukuliwe hatua, hiyo haimo. Sasa inapofikia hali kama hii utajua kuwa tatizo hapa sio Asa au Waziri aliyehusika kutoa tenda ya

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012


kodi za Watanzania kuwalipa vizuri madaktari na kuboresha huduma za afya Muhimbili, inachukua zaidi ya asilimia 54 ya Bajeti katika Wizara ya Afya kuimarisha hospitali za Kikristo huku ikiwaongezea na pesa kupitia misamaha ya kodi. Udini ambao unaifanya serikali ione kuwa heri na bora wagome madaktari jambo linaloweza kusababisha vifo kwa wagonjwa kwa kukosa huduma, ilimuradi tu ibakishe pesa za kuwapa maaskofu waimarishe taasisi zao! Wanachoimba akina Malasusa hivi leo na wanasiasa wetu, ni ile kasumba na bangi walilovutishwa Wa t a n z a n i a n a M w a l i m u Nyerere. Nyerere ambaye wakati akikaa faraghani na maaskofu aliwahakikishia kuwa atalipa kanisa fursa nzuri ya upendeleo, hadharani anajitakasa na kujifanya kamanda wa kupiga vita udini. Lazima nikubali hapa kuwa Waislamu wengi walilewa bangi hili na hata hivi sasa yapo mabaki ya Waislamu waliosalia na kasumba hiyo kichwani. Nakumbuka wakati huo akiwa Mkurugenzi wa NSSF, Mheshimiwa Mustafa Mkullo alikataa kuwapa Waislamu kiwanja walichoomba kupanua shule yao ya sekondari akidai kuwa ataonekana anapendelea Waislamu. Hawa akina Mustafa ni tofauti kabisa na akina Jenifa ambao Bungeni hupigania hospitali za Kanisa zifanywe ziwe za rufaa na serikali imimine hela katika hospitali hizo za kanisa badala ya kuboresha Mawenzi, Bombo, Temeke, Kitete na hospitali nyingine za serikali. Labda kwa kumalizia nimkumbushe Askofu Alex Malasusa jambo moja. Mwaka 1992 maaskofu waliwekeana makubaliano ya kiitifaki na serikali ambapo serikali inachota fedha za walipa kodi na kuwapa Wakristo kujiimarisha. Kwamba katika kulipa kodi, wanalipa Watanzania wote, Waislamu, Wakristo, Baniani, wenye ibada za mizimu n.k. Lakini serikali ikishakusanya fedha hizo, hukaa pembeni na maaskofu na kuwapa mgawo wao pekee huku wengine ikiwanyima. Sasa yawezekana katika msingi ule ule wa Imani kwamba mtu aliyezaliwa na mama anaweza kuwa Mungu Mkuu, inawezekana ndio huo huo unawafanya Maaskofu na Wakristo kuamini kuwa serikali inayochota fedha katika Hazina ya nchi na kuwapa Wakristo pekee, haina udini. Wa n a c h o p a s w a k u f a h a m u maaskofu na wanasiasa wetu ni kuwa amani ya nchi hii imefikia hapa ilipo kwa sababu ya subra ya Waislamu kwa upande mmoja na kwa upande mwingine kuchukua muda mrefu Waislamu kuzinduka kutokana na bangi walilovutishwa na Nyerere wakajiona wanajenga nchi kumbe wanajenga na kuimarisha mfumokristo. Sasa wakitambua hilo, wajue kuwa kauli hizi za udini wakimaanisha kuwa kanisa liendelee kufaidi ile better chance waliyopewa na Nyerere, hazitasaidia kuepusha vurugu katika nchi hii. Njia pekee ni kwa maaskofu na wanasiasa kutambua kuwa waliodhulumiwa wametambua kuwa wanadhulumiwa. Wanataka haki. Haki ikisimama, serikali ikafanya uadilifu, hakutakuwa na sababu ya kuwa na hofu kwamba kutakuwa na machafuko.

AN-NUUR

Hivi sasa tunavuna matunda ya udini

Askofu Alex Malasusa

Ndalichako asingekua Joyce nchi ingetikisik Kanisa livunje mfumokristo amani itadumu Likitegemea bangi la Nyerere, lisha-expire
kuwa na Baraza la Mitihani bovu lisiloaminika, linalotoa matokeo ya kuchakachua, haionekani. Sasa nashindwa kujua hii ni kutokana na ukweli kwamba tangu hapo misingi ya Imani za dini hizi mbili ni tofauti. Kwamba Waislamu wanatakiwa kuhoji na kujenga hoja katika kuamini au ni kwa sababu gani wengine hawaoni uzito wa tatizo hili. Lakini kwa upande mwingine najaribu kufikiria, kama badala ya Joyce angekuwa Hajat Profesa Fatma na waliolalamika ni Wakuu wa Shule za Kikristo, na madudu yawe ndio haya ya Dr. Ndalichako, hali ingekuwaje! Katika Tamko lao kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jumuiya na Taasisi za Kiislamu wametoa mifano mbalimbali kuonyesha jinsi ambavyo Baraza la Mitihani na majopo mbalimbali ya uteuzi wa wanafunzi kuendelea na masomo walivyokuwa wakihujumu vijana wa Kiislamu. Mifano imetajwa ikiwa ni pamoja na kutaja majina ya vijana wa Kikristo waliokuwa wamefeli wakapewa majina ya vijana wa Kiislamu waliofaulu. Mkristo aliyefeli akaendelea na masomo, aliyefaulu akarudi mitaani. Leo yeye na kizazi chake wanatukanwa kwamba hawataki kusoma! Jambo hili lilikuwa jepesi sana. Ilikuwa iundwe Tume ichunguze, na kwa bahati vijana walioporwa nafasi zao wapo au rekodi zao zinaweza kupatikana shuleni walikosoma. Lipo pia lile ambapo aliyekuwa Waziri wa Elimu Kighoma Ali Malima alibadili mtindo wa kuchagua wanafunzi kwa majina ikawa kuchagua kwa namba, idadi ya wanafunzi Waislamu waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza ikaongezeka kwa asilimia 40. Wizara ipo, rekodi Wizarani zipo. Lakini badala ya jambo hilo kutizamwa positively inaonekana kwamba wanaoleta madai haya wanaleta udini. Na ndio hao wanatuhumiwa na akina Askofu Malasusa kwamba wanapanda mbegu ya udini. Watu hawa hawaleti udini, wanapinga udini ambao umefanya Baraza la Mitihani kuwa na vitengo vya siri vya kuwachinjia watoto wa Kiislamu. Wanapinga udini ambao umefanya Baraza la Mitihani kuwa kama Parokia badala ya kuwa na sura ya kitaifa. Wanapinga udini ambao umefanya serikali badala ya kutumia

Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dr. Alex Malasusa
ununuzi wa rada ile, bali ni tatizo la kimfumo. Mfumo uliopo unaruhusu usadi na kulinda masadi na kwa mtindo huu nchi haiendi kokote. Zipo taarifa kuwa baadhi ya wazazi na wanafunzi wanakusudia kuishitaki serikali kutokana na kufuta matokeo yao ya mitihani ya kidato cha nne ya mwaka jana. Lakini wakati huo huo, bado haujapatikana ufumbuzi juu ya madai ya Wakuu wa Shule za Kiislamu waliotuhumu Baraza la Mitihani Tanzania kuhujumu matokeo ya shule zao. Wakuu hao walitoa mfano wa somo moja tu la Islamic Knowledge ambapo walisema kuwa wana wasiwasi kwamba madaraja yaliyotolewa hayatokani na alama walizopata wanafunzi katika usahihishaji. Bahati nzuri haukupita muda Baraza la Mitihani likakiri kwamba lilifanya makosa. Likasema limesahihisha. Na usahihishaji wenyewe ilikuwa kuzidisha alama zilizotoa madaraja ya awali kwa factor ya 1.5. Hata hivyo mara tu baada ya kutolewa matokeo ya pili, Wakuu hao waliandika tena barua Wizara ya Elimu wakisema kuwa hata matokeo hayo ya pili yamekosewa. Kwamba hakuna mjumuiko wowote wa kihesabu unaoweza kuzaa matokeo ya pili ukitumia factor ya 1.5 katika yale matokeo ya awali kama Baraza lilivyodai. Hii maana yake ni kuwa matokeo ya pili yalikuwa ya kubuni tu au ya kuchakachua kama yalivyokuwa ya kuchakachua yale ya awali. Kwanza tukubaliane kuwa hili ni Baraza la Mitihani. Hiki ni moja ya vyombo nyeti nchini. Lakini tizama jambo hili lilivyochukuliwa mpaka sasa. Maadhali waliolalamika ni Wakuu wa Shule za Kiislamu walioona ubovu huo katika Baraza la Mitihani, limefanywa ni la Waislamu, sio suala la kinchi. Inachukuliwa kama siasa kali fulani wanaleta tu ghasia katika nchi. Ile hatari ya

8
Na Mwandishi Maalum WAPO watu wanasema kuwa kutekwa na kisha kupigwa sana Dr. Steven Ulimboka ilikuwa jambo jema kwake. Kwamba heri ya madhara aliyopata kwa kipigo hicho, kuliko shari iliyokuwa ikimsubiri mbele kama asingepata watu wa kumnusuru kwa njia hiyo ya kipigo. Lakini pengine kabla ya kuchambua kauli na maoni hayo, kwanza niungane na Watanzania wote kulaani kitendo cha kinyama alichofanyiwa Dr. Steven Ulimboka huku nikitaraji kuwa vyombo vya dola vitafanya kazi yake kwa makini kuhakikisha kuwa wahusika wanapatikana na kupewa stahiki yao kwa mujibu wa sheria. Lipo fundisho katika Uislamu ambapo waumini wanaambiwa kuwa sio kila jambo linaloonekana kwa sura yake ya nje kuwa ni zuri, basi ni jema kwao. Linaweza kuwa ni shari iliyojificha katika uzuri. Kwa upande mwingine wanaambiwa kuwa sio kila jambo baya linalowapata, basi ni shari kwao, inaweza kuwa ni heri iliyoajia kwa sura ya ubaya. Katika namna ya aina yake, ndivyo Mbunge wa Viti Maalum na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya alivyoitizama kadhia ya kupigwa Ulimboka, hapana shaka bila kujua kuwa hiyo ni katika moja ya mafundisho ya Kiislamu. Akizungumza Bungeni Jumatatu wiki hii, Mheshimiwa Stella Manyanya alisema kuwa kipigo alichopata Dr. Ulimboka ni mpango wa Mungu wa kumuokoa asiendelee kuongoza mgomo wa madaktari. Kwamba, lau Dr. Ulimboka asingepata kipigo hicho, basi angeendelea kuwa kinara w akuongoza mgomo wa madaktari jambo ambalo lingesababisha madhara mamkubwa kwa wagonjwa ikiwa ni pamoja na vifo. Sasa kwa kufa watu hao an kwa kuteseka wagonjwa wasio na hatia, hapana shaka Dr. Ulimboka angepata sehemu ya madhambi yanayotokana na mateso

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

AN-NUUR

Nani alimpiga Ulimboka?

DKT. Steven Ulimboka. ya waja hao wa Mwenyezi Mungu wasio na hatia. Ni kwa mantiki hiyo, Stella Manyanya anaona kuwa bado Mungu anampenda Ulimboka ndio maana akamnusuru kubeba dhambi kama alizobeba Adolf Hitler aliyesababisha Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ukiacha maoni hayo ya Manyanya, wiki hii kumekuwa na hali ya kurushiana maneno na tuhuma baina ya Wabunge wa CCM na wale wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) juu ya nani anahusika. Wapo wabunge waliosema waziwazi bila ya kutafuna maneno kuwa CHADEMA ndio wanaohusika kuchochea mgomo wa madaktari na huenda pia ndio wanaohusika na kupigwa Dr. Ulimboka. Kwa upande mwingine, wapo wabunge wa CHADEMA wanaotuhumu kuwa kupigwa Ulimboka ni mpango uliopangwa na serikali (ya CCM). Labda swali ni je, kama ni serikali (CCM), ilifanya hivyo ili ipate nini? Na kama ni CHADEMA au mtu mwingine yeyote, ikiwa ni pamoja na watu bianfsi au taasisi za kijamii na hata za kidini; ilisuka mpango huyo, lengo nini? Pengine kama kuchangamsha tu bongo zetu, tujaribu kuchambua makundi yote hayo tuone mizani inaelemea wapi. Ila nitahadharishe hapa kuwa huu ni uchambuzi tu wa kuchangamsha bongo, taarifa za uhakika ni zile zitakazotokana na uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola. Akijibu tuhuma, hisia na uvumi kuwa serikali inahusika, Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda alisema Bungeni kuwa serikali itakuwa ni ya ajabu sana kama itakuwa imefanya jambo lake. Hoja yake ilikuwa kwamba wamekuwa na Ulimboka kwa muda wote wa mgogoro kati ya serikali na madaktari na iliofanya hivyo huku ikijua kuwa Dr. Steven Ulimboka sio daktari mtumishi wa serikali. Sasa leo wamdhuru ili iwe nini? Kauli kama hiyo ilitolewa pia na Mheshimiwa Rais Kikwete katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Jumapili wiki iliyopita. Natambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka. Mimi nimeshangazwa sana na hisia hizo kwani siioni sababu ya Serikali kufanya hivyo. Dkt. Ulimboka alikuwa mmoja wa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na Madkatari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali. Kama nilivyoeleza, mazungumzo yalienda vizuri na mafanikio makubwa yamepatikana. Yapo maeneo machache na hasa eneo la mshahara ambalo hatukuweza kukubaliana. Hapo tulipofikia si pabaya na tulikubaliana sote kurudi kwenye mkondo wa Sheria kusaidiwa. Kwa nini Serikali imdhuru Dkt. Ulimboka? Na, kuhusu mgomo, Mahakama Kuu imekwishatoa amri ya kusitisha mgomo. Anayekaidi amri ya

Mahakama ananunua ugomvi na mhimili huo wa dola ambao wenyewe una mamlaka ya kumtia adabu mtu huyo. Hivi baada ya kuka hapo Serikali iwe na ugomvi na Dkt. Steven Ulimboka kwa sababu ipi na jambo lipi hata iamue kumdhuru? Hiyo ndiyo kauli ya serikali. Ukitizama mgomo huu wa sasa utaona unatofauti kubwa sana na ule wa awali. Katika mgomo wa awali, serikali ilikuwa imekaa mahali pabaya sana. Madaktari, wanaharakati na vyombo vya habari, vilifanikiwa kuwateka wananchi kwa kiwango kikubwa wakawa upande wa madaktari, wagonjwa na uhai wao wakakosa mtetezi. Ilie haki yao ya kusihi ikaonekana kuwa ni collateral damage inayostahiki kutolewa ili madaktari wapate mshahara wao wa milioni saba na ushei waliokuwa wakidai. Katika mgogoro wa sasa, kwanza wanaharakati wamesita kujitokeza haraka haraka, kwa uwazi na kwa nguvu kabisa kushabikia mgogoro na kuwaunga mkono madaktari. Hawakuonekana wakitamba katika vyombo vya habari mpaka ile siku baadhi yao walipokuwa ndani ya gari la wagonjwa lililokwenda kumchukua Ulimboka huko alikokuwa ametupwa baada ya kupigwa. Wakaonekana tena pale Uwanja wa Ndege na mabango yao wakisubiri kumpokea na kumsindukiza Ulimboka akipelekwa nje ya nchi kutibiwa. Ni vivyo hivyo kwa upande wa vyombo vya habari. Kwa kiwango kikubwa vilishindwa kushabikia suala hili kama vilivyofanya kjatika mgomo wa awali. Mi nadhani walishaona kuwa saikolojia na msimamo wa wananchi ulikuwa katika kuwalani madaktari. Ni wachache wal;iohojiwa walijitokeza waziwazi, akiunga mkono madaktari. Wengi waliwalani wakiwataka waache mgomo. Wapo waliohoji wakisema, kabala madaktari hawajagoma, wafikirie lau polisi na wanajeshi wao wanagoma Inaendelea Uk. 9

Makala/Tangazo

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012 Sasa japo haiwi kuwa ni sababu ya kuivua katika tuhuma, lakini hoja ya serikali kuwa, kwa nini sasa na sio wakati ule?, inakuwa na nguvu za kimantiki. Ila kuna jambo moja alilisema Rais Kikwete. Alisema, Kama kuna mtu wa Serikali kafanya, itakuwa kwa sababu zake binafsi na siyo za Serikali au kwa kutumwa na Serikali. Binafsi sioni kwa nini serikali itoe kauli kama hii, labda ituambie kuwa ina wasiwasi kuwa kuna mapandikizi ndani ay serikali. Kuopigwa Ulimboka hivi sasa kumebadili kabisa sura ya mgogoro huu na serikali imejikuta ikiwa ikilazimika kujitetea wakati ilikuwa kazi ni kwa madaktari kutaka kuwashawishi wananchi na wagonjwa wanaokufa na

AN-NUUR

Nani alimpiga Ulimboka?


Inatoka Uk. 8 wan chi. Na kwamnba hadhani kwamba wanajeshi hao wanafanbya kazi hiyo kwa sababu wanapata masilahi makubwa bali ni kwa sababu ya uzalendo wao. Ufupi wa maneno, katika mgomo wa sasa, wananchi walikuwa pamoja na wagionjwa na kwa maana hiyo, serikali ilikuwa

hali itakuwaje. Nakumbuka mwananchi mmoja akitoa maioni yake katika kipindi cha Baragumu (Chanel Ten) alisema kuwa wapo asikari wa JWTZ ambao wapo katika mahandaki na katika mazingira magumu kabisa ya kikazi wakijitoa muhanga kwa ajili ya ulizni

mahali pazuri wakati katika mgomo wa awali ilikuwa katika wakati mgumu sana. Na kama ni kufanya jambo, kwa hakika ingeshawishika kufanya wakati ule ikiwa ni pamoja na kutaka Dr. Steven Ulimboka asiwepo kama kiongozi wa madaktari kwa sababu yeye si Dakitari mtumishi wa serikali.

kuikosa huduma kwamba, hawatetei mishahara minono ila namna nzuri ya kuwatibu. Kwa kitendo hiki cha kupigwa Ulimboka, huruma sasa inahamia kwa madaktari kwa kiasi fulani. Hawezi kufanya jambo hili, ila yule anayetaka kuihujumu serikali. Sasa kama yupo mtu ndani ya serikali kaagiza jambo hili lifanywe, japo Mheshimiwa Rais Kikwete anasema kuwa Kama kuna mtu wa Serikali kafanya, itakuwa kwa sababu zake binafsi na siyo za Serikali au kwa kutumwa na Serikali, lakini hiyo ni ishara pia kuwa ndani ya serikali si salama. Serikali imevamiwa na mapandikizi. Mapandikizi wanaolipwa mishahara na kuhudumiwa na serikali, lakini wakiihujumu serikali ndani kwa ndani, sasa hii ni hatari kubwa zaidi. Mtu unaweza kusema, afadhali hata iwe ni serikali yenyewe ilifanya kuliko kufanywa na watu ndani ya serikali kwa nia ya kuihumu. Ukija kwa watu walio nje ya serikali, iwe ni vyama vya siasa, watu binafsi, taasisi za kijamii na hata za kidini; mi sioni ni kwa sababu gani kwa mfano CHADEMA ipange mpango wa kumdhuru Dr. Steven Ulimboka, labda kama utapatikana ushahidi kwamba bado wana nia na lengo la kutaka serikali ifikie mahali isitawalike kama walivyowahi kusema baadhi ya viongozi wao siku za nyuma. Mara tu baada ya kutangazwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu mbayo CHADEMA walidai kuwa yalichakachuliwa na taarifa zao kupambwa sana katika vyombo vya habari, palitokea kutolewa kauli kwamba na baadhi ya viongozi wa chama hicho wataendesha maandamano nchi nzima na kuhakikisha kuwa nchi haitawaliki. Sasa kama yupo mtu bado ana nia kama hilo, huyo unaweza kumtilia shaka kwamba anaweza kufanya lolote ilimuradi lengo hilo litimie. Vinginevyo, itakuwa ni suala tu la kurushiana madongo ya kisiasa na bora tusubiri vyombo vya usalama vitaibuka na taarifa gani.

10

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

AN-NUUR

Udhalilishaji unaofanywa na vyombo vya Dola Tanzania dhidi ya Waislamu


Na Mohamed Said
M WA K A 2 0 0 6 R a d i o Tehran walipendekeza jina langu kwa Wizara ya Mambo ya Nje Iran wanialike katika hawli ya Imam Khomeni. Sababu ya cha mie kualikwa ni kuwa mara kwa mara nilikuwa nikifanya mahojiano na Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili kuhusu siasa za Tanzania hususan wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 na ikatokea kuwa yale mahojiano yangu yakawa yanapendwa na wasikizaji wa Afrika ya Mashariki na Kati sehemu za Emirati. Nilikwenda Iran na waalikwa walikuwa kutoka dunia nzima na wa kila aina, waandishi, wahadhiri wa vyuo vikuu, wasomi wa kawaida, mawaziri wa serikali kutoka nchi tofauti na watu wengine wengi. Msafara wetu wa wageni kwenda mahali ulikuwa ni msururu wa mabasi zaidi ya kumi yakisindikizwa na kimulimuli cha polisi. Kutoka Tanzania nilikuwapo mimi pamoja na waandishi kutoka Daily News na Kituo Cha TV cha Channel Ten. Nikiwa Tehran niliingia Studio za Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili na tukafanya mahojiano na mtangazaji wao mashuhuri Abdulfataa Mussa na wenzake na vilevile kurekodi vipindi vingi kuhusu hali ya Waislamu Tanzania. Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza. Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo. Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule asa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama. Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri. Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maosa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadharati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado, ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina. Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa. Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo

Mkasa Wangu wa Kukamatwa Uwanja wa Ndege wa Mwl. Nyerere, Dar es Salaam Mwaka 2006
yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imeka siku yangu. Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kukiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu. Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila Inaendelea Uk. 13

Muoneeni huruma Kamanda Ernesti


Inatoka Uk. 3
na jamaa zao walipokuwa wakifuatilia wajue kulikoni, walichoambulia ni kuambiwa kuwa watu hao hawataachiwa mpaka Bush aje aondoke. Na baadhi ya Polisi wakafikia mahali pa kusema kuwa hata kama jamaa hao wangekwenda kwa IGP au Wazairi wa Mambo ya Ndani, asingeweza kusaidia labda waende Ubalozi wa Marekani. Waliokamatwa walikuwa Watanzania wanaofahamika, walipozaliwa, wanapokaa, shughuli zao za kila siku na wengine walikuwa watumishi wa serikali wa ngazi za juu. Kwa hiyo serikali inawajua vizuri na vyombo vyetu vya usalama vinawajua vizuri sana maana wasingepata vyeo bila ya kuwahakiki tabia na mienedo yao. Lakini maadhali waliambiwa kamata hao magaidi wakawakamata kama amri ilivyo kuja. Sasa tunapotafakari suala la kudhalilishwa Sheikh wetu Kishki, tusilitizame suala hili kwa ufinyu. Tuliangalie kwa uzito wake na kwa mapana yake ili tujue tutaisaidiaje nchi yetu maana tulipofikishwa ni pa baya. Bila shaka tutakuwa tunakumbuka lile zogo lililoibuka baada ya Dr. Idiss Rashid kutoa ushauri kuwa serikali inunue iliyokuwa mitambo ya kufua umeme ya Dowans. Ni mitambo hiyo hiyo waliyosema akina Samwel kuwa ni mibovu, ndio Wamarekani hivi sasa wanatukamua watakavyo ambapo vinginevyo mitambo hiyo ingekuwa ya kwetu. Husikii tena kelele za wanaharakati, vyombo vya habari wala akina Samweli Sitta wakisema kuwa mitambo hiyo mibovu. Si ajabu hata kama Symbion ya Marekani watapandisha bei ya umeme watakavyo, usiwasikie wakilalamika wala kuhoji! Hii ndiyo hali. Ni Msiba. Sasa hata kama Waislamu wataamua kufanya maandamano kutaka serikali ikome na isirudie kuwadhalilisha Masheikh na kumtaka Kamanda wa Polisi aombe radhi; lakini ijulikane kuwa kuna kazi kubwa zaidi ya kuwanasua akina Ernesti katika kitanzi hiki kinachowafanya wapokee maelekezo kutoka kwingine bila ya kuhoji wala kwa kutumia taaluma yao ya kipolisi.

yako anakuja nyumbani kwako halafu anakunusisha mbwa wake aliokuja nao ili kujihakikishia kuwa ndani mwako hakuna bomu au gaidi na wewe unakubali! Si umwambie tu kwamba kama anahisi nyumbani kwako hakuna usalama asije? Lakini pale Arusha Akina Ernest wetu hawakuweza kumsaidia Rais wetu kwa sababu vichwani mwao washajiaminisha kuwa wenye akili ya kukiri na wanaojua jambo zuri ni FBI, CIA na watu kama hao. Na maelekezo yao hayapingwi. Hawakuweza kumsaidia Mkapa kwa sababu walishakishwa mahali ambapo hata kama wangeambiwa kuwa baba yake aliyemuacha kule nyumbani akija kazini ni gaidi, basi angeamini na angekwenda kumkamata kama angeamriwa kufanya hivyo na FBI. Na hivi ndivyo walivyofanya alipofika nchini hapa kwa mbwembwe George W Bush. Tutakumbuka kuwa kiasi wiki mbili kabla ya Bwana Bush kuingia nchini wapo Watanzania wenzetu walikamatwa wakawekwa ndani. Ndugu

Kwa mahitaji ya viroba bora vipya kabisa kwa matumizi mbalimbali sasa unaweza kupata kwa bei ya jumla na rejareja kwa saizi zote kwa bei nafuu zaidi, kwa BANDO. Tupo mtaa wa Likoma na Pemba Kariakoo, Dar es Salaam (nyuma ya Msikiti wa Idrisa). Kwa mawasiliano zaidi wasiliana kwa simu: 0557 800999/0683 800999.

VIROBA MURUA

11
Na Rashid Mtagaluka TOKEA ulimwengu ushuhudie mauaji ya kinyama ya Daktari bingwa Alhaji Jumbe Mohammed Maphingo (46), sasa ni mwaka mmoja na mwezi mmoja. Vilevile leo ni siku ya sita tokea ulimwengu huu pia ushuhudie kitendo cha kiharamia kilichofanywa na watu wasiojulikana cha kumteka, kumpiga na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Ta n z a n i a D k S t e v e n Ulimboka. Kimsingi hii yote ni misiba na maafa yasiyoweza kusahaulika katika jamii. Isipokuwa nianze na wa Dk Maphingo Jumbe ambaye siku ya Mei 22, 2011 majira ya kati ya saa 3:30-4:00 za usiku akiwa nyumbani kwake Bulongwa, alivamiwa na wanafunzi wa chuo cha utabibu cha hapo na kumshushia kipigo kilichosababisha kifo chake! Asubuhi yake taarifa za kifo hicho zikasambaa kwenye vyombo mbalimbali vya habari vya hapa nchini, chini ya kichwa cha habari kilichosomeka Wanafunzi Makete wadaiwa kuua Daktari. Maelezo yaliyomo kwenye habari hiyo ndiyo yaliyonishawishi mimi na wenzangu tufunge safari hadi huko Bulongwa kwa lengo la kuipa jamii taarifa kamili ya kile kilichotokea, badala ya zile zilizoonesha kujaa mapungufu yaliyogubikwa na utata usioelezeka. Kwa mujibu wa Afisa Utawala wa hospitali ya Bulongwa inayomilikiwa chuo hicho ambacho marehemu Dk Maphingo alikuwa mkufunzi wake Bwana Edward Masavella, Dk Jumbe alifikwa na umauti huo baada ya kuvuja damu nyingi zilizotokana na kipigo cha maharamia hao wasio na huruma. Sio lengo langu kuwatonesha ndugu, jamaa na maraki msiba wa mpendwa wetu huyo, la hasha! Bali nataka kuweka kumbukumbu sawa tu kufuatia hili tukio la hivi majuzi. Afisa huyo wa utawala alitueleza mimi na wenzangu wawili tulioongozana hospitalini hapo kwamba, Daktari alikuwa akitarajiwa kupandishwa cheo na kuwa Mganga Mkuu wa hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini Kati. Alisema kabla ya

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012


Daktari huyo siku ya Jumanne Juni 26, 2012, bali nataka tuangalie pande zote mbili za matukio haya yanayokaribia kufanana, kwamba kama ni kutetea haki ya uhai na kutetea haki za kibinadamu, mbona tunabagua? Kama alichofanyiwa Ulimboka kinapaswa kulaaniwa na kutolewa matamko, kwanini hayo hayakusikika wala kuonekana pia pale alipouliwa Dk. Maphingo? Hivi ninavyoandika makala haya tayari Jumuiya ya Madaktari nchini imeshasema haina imani na tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuchunguza unyama aliofanyiwa Dk. Ulimboka huku wakisisitiza kuwepo kwa chombo huru zaidi. Hili hatukulisikia kabisa mwaka jana kuzungumzwa na Jumuiya hiyo utadhani Daktari Jumbe alikuwa haishi hapa nchini na hivyo hajulikani! Licha ya kutaka tume huru, madaktari hao wamesema wataendelea na msimamo wao wa kuhakikisha wanatetea maslai yao pamoja na mazingira magumu ya kufanyia kazi yanayowakabili kwa sasa. Akizungumza na waandishi wa habari nje ya jengo la MOI Katibu wa Jumuiya hiyo Dk. Edwin Chitage alisema madaktari nchini wanahitaji chombo kilicho huru kitakachochunguza tukio hilo kwa undani zaidi kuliko Jeshi la Polisi. Swali langu liko hapo. Kwa nini Dk. Chitage anaonekana kuguswa zaidi na majeraha ya Dk. Steven Ulimboka na wala hakuonekana kuguswa na mauaji ya kinyama ya Dk. Alhaji Jumbe? Leo mpaka vyama vya siasa navyo vimeingia katika mtego huo, na baadhi ya wanasiasa wamekwenda mbali sana kwa kutishia kulala barabarani iwapo Ulimboka atakufa! Hivi roho moja ya Dk Ulimboka na mamia ya roho za Watanzania zinazokufa kila kukicha kutokana na kukosa huduma ya matibabu katika hospitali za serikali zipi zenye thamani? Kwa nini wanasiasa hawa kama kweli wana uchungu wasiwahamasishe Watanzania kulala barabarani kupinga mgomo wa madaktari unaosababisha madhara hata kwa wasio husika? Mgomo tunaambiwa una lengo la kuishinikiza serikali kuwapa mafao na marupurupu stahiki madaktari, sasa hawa watoto wadogo na wazee wanaoachwa bila hata kupokelewa mahospitalini Inaendelea Uk. 14

AN-NUUR

Kwanini matamko haya hatukuyasikia alipouawa kinyama Dk. Maphingo Jumbe?

BI. Helen Kijo Bisimba. marehemu kufikwa na kadhia hiyo, mwanafunzi mmoja wa kike aliyemtaja kwa jina alitoka katika mabweni yaliyo jirani na nyumba aliyokuwa akiishi Dk Maphingo na kwenda kumgongea ili akabidhi barua ya kujieleza kwanini usiku uliopita hakulala chumbani kwake. Mbali ya kuwa daktari katika hospitali hiyo, pia marehemu alikuwa akifundisha utabibu katika chuo hicho, na uongozi ukampa cheo cha mkuu wa nidhamu. Hata hivyo cha kushangaza kuwa muda huo sio wa kawaida kwa mwanafunzi yeyote kuwa nje ya bweni na haikujulikana wapi alikopata ruhusa ya kutoka na kwenda kwa Dk Maphingo, alisema Masavella kwa uchungu katika mahojiana hayo. Jambo hilo lililozusha shaka na maswali kibao sio tu kwa uongozi wa hospitali ya Bulongwa, lakini hata kwa ndugu jamaa na maraki wa marehemu, lilipelekea hata sisi kuwa katika taadhari kubwa wakati wote tuliokuwapo kijijini hapo kwa ajili ya kazi hiyo. Taarifa za awali kutoka kwa Afisa utawala huyo ziliendelea kufahamisha kwamba, binti huyo alipoingia tu nyumbani kwa Dk alivua kanga yake aliyokwenda nayo hapo na kuanza kupiga kelele za kubakwa na mara kundi la wanafunzi wa kiume likavamia na kuanza kumsulubu Daktari huyo mpole kwa magongo na mawe mithili ya mtu auavyo nyoka aliyeingia ndani ya nyumba yake hadi walipohakikisha hawezi tena kunyanyuka ndipo nao wakatawanyika. Kinachostaajabisha katika tukio hilo ni kuona vijana hao walivyoka kwa haraka eneo la tukio wakati ambapo liliko bweni lao ni mbali sana ukilinganisha na nyumba ya daktari mwenziwe ambaye hata hivyo hakutokea kutoa msaada. Baada ya hapo tukadhani labda asasi mbalimbali za wanaharakati na zile za kutetea haki za binadamu zingetumia fursa hiyo kulaani na kukemea kitendo hicho cha kinyama kwa daktari bingwa ambaye ni hazina kwa Taifa letu. Aidha, si Jumuiya ya Madaktari kupitia kwa Mwenyekiti wake Dk. Steven Ulimboka, Katibu wake Dk. Edwin Chitage wala chama cha madaktari ambacho kilithubutu angalau kulaani tu mauaji ya daktari mwenzao huyo ambaye alikuwa ni mwanachama hai katika Jumuiya hiyo. Pia si rais wa MAT Namala Nkopi, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa wakati ule, Waziri Mkuu Pinda wala Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu Bi Hellen Kijo-Bisimba waliojitokeza kupanua midomo yao kulaani tukio hilo. Hatukusoma, kusikia na kutazama tena kwenye vyombo vya habari wakilishupalia suala la mauaji ya Dk. Maphingo kama tunavyoshuhudia hivi sasa kufuatia tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk. Ulimboka kama vile Dk. Jumbe hakustaili kuishi! Kinyume chake Dk. Ulimboka ambaye ni kinara wa kuhamasisha migomo ya madaktari katika hospitali za serikali chini ya mwavuli wa Uenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, aliyekutwa akipata vilevi katika klabu ya viongozi (Leders Club) maeneo ya Kinondoni na kutekwa na watu wasiojulikana ndiye anaonekana mwenye haki ya kutetewa na kuonewa huruma zaidi! Nisieleweke vibaya kwamba huwenda kwa kusema hivi pengine naunga mkono kitendo alichofanyiwa

12

Mashairi

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012

AN-NUUR

NDUGU msomaji, assalaam alaykum. Mnamo tarehe 30 June 2012 imeadhimishwa miaka 35 tangu Jumuia ya Afrika Mashariki ilipouawa kutokana na chuki binafsi aliyokuwa nayo Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania mnamo mwaka 1977. Rais wa Uganda wa wakati huo Idd Amin Dadaa na Mwanasheria Mkuu wa Kenya aliyeitwa Charles Njonjo ambaye alikuwa hana uhusiano mzuri na Mwalimu, na katika kikao cha wakuu wa nchi wanachama wa Jumuia hiyo iliyoanzishwa mwaka 1967 ikazaliwa kutokana na East African High Commission nayo ilijikita sana kwenye uchumi na ilikuwa na mashirika yafuatayo: Makao makuu, shirika la reli, shirika la ndege, shirika la Bandari, shirika la Posta, kampuni ya kupakia na kupakua mizigo melini. Nikiwa mmoja wa watumishi wa iliyokuwa Jumuia hiyo kwa upande wa kampuni ya kupakia na kupakua melini na ambayo hadi sasa bado tunapaza sauti za kilio cha kutolipwa mafao yetu kufuatana na sheria zetu za Jumuia hiyo, ila tunashuhudia jinsi serikali inavyozidi kuwa na ubabaishaji wa kukataa kutulipa kwa misingi ya Jumuia hiyo ya mwaka 1967-1977. Tabu hii imetupata sisi Watanzania tuliokuwa watumishi wa mashirika hayo sita. Jambo la kushangaza ni kwamba wenzetu waliokuwa watumishi wa upande wa Uganda walilipwa na serikali yao na wala hawana mgogoro na serikali. Kwa upande wa Kenya kadhalika nao hawana mgogoro wowote na serikali yao kwani nao walishalipwa mapema. Pamoja na kwamba uongozi wetu kwa upande wa Tanzania walituelekeza kuwa tuwaite wakenya kuwa ni manyangau (neno hili ni la Kijaluo, kwa Kiswahili ni masi) na

Miaka 35 ya kifo cha iliyokuwa Jumuia ya Afrika Mashariki


sisi ni waungwana, lakini ajabu ni kwamba upande huo huo wa waungwana wanaendelea kupaza sauti za vilio vya kudhulumiwa mafao yao kila uchao na kuishi katika mazingira magumu, lakini kwa upande wamanyangau wao walishalipana kistaarabu na kumalizana mapema. Wengi wameshafariki wakidai na wengine wanaendela kufariki na kupata taabu za uzee bila hata kufaidi wenyewe jasho la utumishi wao kwenye Jumuia. Mzee Ramadhani Kyaka anaeleza kuwa enzi zao pamoja na kwamba walikuwa ni wafanyakazi wenye nidhamu na uaminifu wa hali ya juu, hata pale ilipovunjwa Jumuia hiyo mwaka 1977, bado mashirika hayo sita yaliendeshwa vizuri bila hata kutegemea wageni (TX). Hadi pale serikali ilipoanza kuwaengua wale wote waliokuwa viongozi wa mashirika hayo sita na kuwaweka wanasiasa chini Scorpo na kuleta sheria na muundo uliofanya mashirika hayo kuanza kufa kifo cha mende hadi leo tunashuhudia. Rasilmali za Jumuia zilikuwa kama ifuatavyo: Majengo ya osi, makazi ya watumishi (majengo), maghala, karakana, vyuo kwa watumishi wa kada na fani mbalimbali, majengo ya burudani na viwanja vyua michezo, zahanati kila palipokuwa na watumishi. Rasilmali nyingine ni magari aina mbalimbali, treni (Injini na mabehewa ya uzito na aina mbalimbali) cranes, winches, folk lift, matrekta ya aina mbalimbali, meli, boti, targu za aina mbalimbali, ndege za aina mbalimbali. Inakumbukwa kwamba mwaka 1977, rubani mmoja aliyekuwa akiendesha ndege za iliyokuwa jumuia hiyo, Capteni Mapunda, alithubutu kutorosha ndege aina ya D.C 9 kutoka uwanja wa ndege wa Embakasi Nairobi hadi Dar es Salaam ikiwa ni kuonyesha mapenzi kwa nchi yake (uzalendo). Aliweza kuvunja amri ya wakuu wake wa kazi mara alipotakiwa aipaki vizuri ndege hiyo. Visa vya namna hii ni vya kizalendo kwa nchi na vilikuwa vingi kwani ilikuwa ni fahari kufanya hivyo. Lakini ajabu ni kwamba viongozi wetu wa Kitanzania hawawataki watu wa aina hii. Ndio kwanza wanazidisha kuwadhulumu, kuwatisha watumishi hawa wa iliyokuwa Jumuia ya Afrika Mashariki. Tangu kuvunjwa Jumuia, kila waliokuwa wafanyakazi wanapojaribu kudai mafao yao kutokana na utumishi wao uliyoyajenga vizuri 67 na hatimaye kufikia bilioni 117. Hapo wastaafu waliamua kurudi mahakamani kudai mapunjo. Hata hivyo Mzee Kyaka anaeleza kuwa wana wasiwasi kuwa serikali kwa makusudi haitaki kuwalipa kwani inawatumia maosa wa Osi ya Mwanasheria Mkuu kukwamisha malipo. Katika moja ya vikao mbele ya Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani alimkaripia mwanasheria kutoka Osi ya Mwanasheria Mkuu kwa kuwawekea wastaafu pingamizi mahakamani yasiyo na maana na kupigwa marufuku asijihusishe na jalada namba 95/2003. kulisoma vizuri wakaiagiza mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam itoe hati amri ya mahakama (court oder) ili hazina iwalipe wastaafu hao. Hata hivyo inatarajiwa kuwa Osi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ataweka kikwazo cha pingamizi kama ilivyo ada na kukaidi agizo la Jaji ili wenye haki yao wasilipwe. Ombi letu kwa Mhe. Rais Jakaya Kikwete, amrejee Mwenyezi Mungu ambaye amekataza dhulma, pia arejee ahadi aliyoitoa Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa katika sherehe ya May Day mwaka 2005 kule Songea. Tunamtaka awe na tahadhari na hawa maosa wake kwani wanaonekana ni miongoni mwa wale wasiomtakia mema katika uongozi wake. Inasikitisha kuona kwamba Rais aliyetangulia aliona kuna haki ya wafanyakazi hawa wa iliyokuwa jumuia ya Afrika Mashariki walipwe mafao yao lakini aliyemrithi aone hakuna haki hasa ikizingatiwa wote hao ni wa chama kimoja kinachotawala, sera moja na katiba ya chama chao ikiwa ni moja. Moja ya sababu ya nchi kuwa na neema ni kuwaenzi wazee kwa kuwapa haki zao na kuwatunza ili wasiwe na manunguniko. Mwenyezi Mungu anachukizwa na dhulma dhidi ya raia. Leo wako wapi Daniel Yona, Basil Mramba, Mustafa Mkulo, Aggrey Mgonja, Zakia Meghji. Je, sio Mwenyezi Mungu amechukizwa na vitendo vya dhuluma dhidi ya raia hususan wazee? Wa z e e w a n a o m b a mamlaka za serikali ya Tanzania na viongozi wake kubadilika kwa kuwaheshimu wazee. Waachane na tabia ya kuwadharau na kuwapuuza pale wanapodai haki zao. Basi ni vyema hima ikafanyika wakalipwa. Abdallah Ramadhani Kyaka 0654145288

Je! Una maoni, barua au Mashairi? Tuandikie: Mhariri AN-NUUR, S.L.P. 55105, Dar es Salaam au tutumie kwa Barua pepe E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk
mashirika hayo kabla ya kuvunjwa Jumuia, wameishia kupuuzwa, kudharauliwa na hata kuambulia virungu vya polisi. Watumishi hao jumla yao ni 30,000 pamoja na familia zao, lakini inasikitisha kuona hata pale ilipofunguliwa kesi ya madai namba 95/2003 mwaka 2005 na kushinda chini ya Jaji Urio wa Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam bado hakuna malipo yaliyofanyika. Pia Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa aliahidi kuwa alitenga shilingi 450,000,000,000,000 kwa ajili ya kuwalipa wastaafu wa Jumuia hiyo na kueleza kuwa hizo ni za kuanzia tu na kwamba Rais ajaye atamalizi kulipa. Pamoja na dhamira ya Rais wa awamu hiyo ya kulipa, tulipatwa na mshangao pale ambapo Waziri wa Fedha wa wakati huo aliposema ametenga bilioni 50., alipoona kakosea aliongeza bilioni Pamoja na hayo, wastaafu hao waliendela kudai court oder kama alivyoagiza Jaji Mkuu Augustino Ramadhani lakini mpaka sasa majaji wawili wameshakutana nao na bado wanaendelea kupokea pingamizi kutoka serikalini kwa maana ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu. Badala ya kutekeleza agizo la aliyekuwa Jaji Mkuu, na kwa kuwa madai wa wastaafu kwa serikali ni mapunjo ya mafao yanayotokana na utumishi wa iliyokuwa Jumuia ya Afrika Mashariki kwa msingi wa sheria zake za mwaka 1977. Pamoja na kufanya maandamano mengi, juhudi zote hizi wadawa walitumia jeshi la polisi kuwaadhibu wanaodai. Ndipo Jaji mstaafu Ramadhani alipoamua kuliitisha jalada la civil case namba 95/2003 ili aweze kujiridhisha. Akaona bora aungane na majaji wanne wa mahakama ya Rufaa. Walipoliona jalada na

13

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012

AN-NUUR

Udhalilishaji unaofanywa na vyombo vya Dola Tanzania dhidi ya Waislamu


naponzwa na dini yangu. Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu. Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa. Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisa sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa. Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha osini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na audio cassette nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniuliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania? Maana mimi hata nyumbani kwangu hii leo mkika nina vitabu vya Khomeni na wanafalsafa wengine kama Karl Marx ambao nimesomeshwa pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Sasa hapo ikaja kejeli. Ala wewe mtu wa Kariakoo lakini umefika hadi Chuo Kikuu! Sikujibu kitu. Awali waliponitia mbaroni waliniuliza kwetu na nikawaeleza kuwa nimezaliwa Kariakoo. Hawakunipa jibu kuhusu kuingiza vitabu na cassette za Khomeni. Ikawa sasa kama vile wameishiwa maswali. Nikaona kuwa sasa ni zamu yangu nami kuwapiga maswali. Yule aliekuwa akinihoji nikamwambia, Mimi wewe nakufahamu vizuri sana kwa sababu ukicheza mpira Simba Sports Club na mie ni mpenzi wa Club hiyo toka utoto wangu wakati huo ikiitwa Sunderland na mmoja wa baba zangu alikuwa mchezaji marufu wa Club hiyo katika miaka ya 1950 akaikia hadi kucheza Kombe la Gossage. Nilihisi amepata mfadhaiko kidogo akanambia,Unanifananish a yule aliyekuwa akicheza Simba ni ndugu yangu. Alikuwa anasema uongo lakini mie nikamkubalia. Hapo nikajua kuwa nishampata sasa hana nguvu tena ya kuuliza maswali. Kusema uongo ni dalili ya kujihami. Nikamrushia kombora lingine, Sasa tuhuma za madawa ya kulevya zimekwisha tuko katika kwa nini naingiza vitabu vya Khomeni nchini? Akanijibu kinyonge, Tumeridhika huna madawa. Kufika hapa tukawa tumemaliza mahojiano. Wa k a t i h u o s a s a n i usiku wa manane na nishapeleka SMS kwa sahib yangu mmoja bingwa wa mambo ya mtandao wa kompyuta kumjulisha kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege kwa tuhuma za uongo za kuvusha mihadarati na yeye ile kuipata tu ule ujumbe wangu akaifahamisha dunia kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege nikitokea mkutanoni Iran na nimebambikiziwa tuhuma za kuingiza nchini mihadarati. Waliponitia mbaroni tu walinionya kuhusu kutumia simu yangu ya mkononi lakini bahati nzuri hawakuninyaganya. Aliyenipa onyo hili alikuwa Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Uwanja wa Ndege. Huyu raki yangu akawa kanisaidia sana maana hadi kumekucha wapenzi wangu wote ndani na nje ya nchi pamoja na vyombo vya habari vinavyonifahamu walikuwa na taarifa za kukamatwa kwangu. (Kwa kipindi takriban miaka ishirini nyuma kwa nyakati fofauti nimekuwa nifanya mahojiano na radio zote muhimu kama, BBC, VOA, Sauti ya Ujerumani, Sauti ya Iran nk.). Nikawaomba wale watu wa Usalama waniachie basi nende zangu kulala nyumbani nirudi hapo kesho asubuhi kwa kuwa sikuwa nimebeba madawa ya kulevya. Wa k a n i a m b i a , I t a b i d i tukulaze hapa hadi asubuhi wakubwa wetu watupe amri ya kukuachia. Maana amri ya kukukakamata wewe imetoka juu. Sasa hapo ikawa nimelipata jingine. Kumbe wauza unga hawakamatwi hadi amri itoke juu. Sasa kama amri haikutoka ndiyo muuza unga atapita aingize sumu zake mitaani? Hili likazidi kunidhihirishia kuwa kukamatwa kwangu hakukuwa na uhusiano wowote na vita dhidi ya mihadarati bali ni vita vile vile vikongwe dhidi ya Uislamu. Nikawa pale usiku kucha. Sasa wakati niko pale wakidhani nimelala. Wakawa wenyewe kwa wenyewe wanazungumza kuhusu hii operation neno walilotumia ni kuwa leo tume-dial wrong number. Wakawa wanasema, Huyu bwana mbona hakuelekea kama muuza unga tena huyu mtu bwana kasoma kweli kweli Wanadhani mie nimelala kumbe ni macho nawasikiliza. (Vipi utalala katikati ya michongoma?). We umeona jinsi alivyokuwa akijibu na kuchambua mambo. Hilo ndilo likawa gumzo lao wakinisia kwa ufasaha na mantiki lakini wakizungumza kwa sauti ya chini kabisa. Hapa ikanidhihirikia kuwa hawa vijana walikuwa wanatimiza wajibu wao wa kazi tu, lakini kiini khasa cha kukamatwa kwangu hawakuwa wanakifahamu. Walionikamata walikuwa vijana kama wanne na wote walijitambulisha kwa majina ya Kiislamu. Nilijua ni waongo kwa kuwa Muislamu anaonekana katika uso na katika matumizi ya lugha. Lakini yule mchezaji wa Simba ni Muislamu na yeye ndiye aliyekuwa mkubwa pale akiongoza ile shughuli yote tena kwa kujidai na kujifaharisha sana. Kisa kile kile cha mtumwa anayelimishwa na yule anaefanya kazi za ndani nyumbani kwa bwana. Ila kitu kimoja lazima nikiri. Wale vijana walikaa na mimi kwa wema na hawakunibughudhi hata kidogo. Hata nilipokuwa nakwenda msalani kijana alienisindikiza alinitaka radhi akasema, Nakusindikiza kwa sababu ni sheria lakini sisi tunakustahi kwa hiyo utuwie radhi kwa kukufuata hadi msalani. Asubuhi wakubwa wakaja kazini lakini hakuna aliyenikabili. Walikuwa wakinichungulia kutoka mlangoni kama simba ndani ya kizimba kwenye zoo, nami nikawa najifanya siwaoni. Ndipo akaja mkubwa mmoja tena akaniita kwa jina langu na kwa heshima na bashasha sana, Bwana Mohamed tuwie radhi sana pamekuwa na makosa kidogo tuwie radhi sasa hivi tutakuruhusu uende nyumbani. Akatoka nje akawa akipiga simu. Kisha akarudi ndani akaamrisha nibebewe mizigo yangu na gari la polisi linirudishe nyumbani. Kistaarabu kabisa nikakataa gari ile huku nikifanya maskhara kuwa naogopa gari ya polisi asijepiga simu akasema mrudisheni huyo mtuhumiwa. Ofisi nzima ikacheka. Hapo ndipo wale wakamataji wangu wa usiku wakabeba mizigo yangu nami nafuata nyuma tunatoka nje ya uwanja. Kisa hasa cha kukamatwa Kilichobaki sasa ni kueleza sababu ya mimi kukamatwa. Mwaka wa 2006 Chuo Kikuu cha Ibadan, Nigeria kilifanya kongamano la kimataifa hapo chuoni kwao kuzungumza kuhusu Ugaidi katika Afrika ya Mashariki na Maendeleo (Conference on Islam, Terrorism and African Development). Mimi nilitoa mada iliyokuwa na anuani hii: Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience. Katika mada hii nilijikita mahsusi katika kuisema Marekani kwa udhalimu wao duniani. Nikaeleza kuwa huo udhalimu wao ndiyo unaopelekea wao kuchukiwa dunia nzima. Hapa ningependa kufahamisha kuwa mkutano huu wafadhili wakubwa walikuwa Iran na Marekani. Saudi Arabia ilikataa kuchangia mkutano ule. Wakati nasema maneno haya ya kuwakanyanga Inaendelea Uk. 14

Inatoka Uk. 10 kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama. Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msarishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya. Nikawauiza, Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli? Wakasema, Ndiyo maana leo tumekukamata. Nikawaambia, Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni Mzungu wa Unga kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya. Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran? Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Amerika na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha. Mbona hamkunikamata wakati ule? Ikawa swali na jibu swali na hivyo. Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislamu sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyanyasa Muislamu? Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa

14

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

AN-NUUR

Inatoka Uk. 13 wenyewe Waamerika wapo hapo mkutanoni. Baada ya kuwalani Waamerika sasa nikaigeukia serikali ya Tanzania na kuishutumu vikali kwa kupitisha Sheria ya Ugaidi. Hapa nikaeleza kuwa Waamerika wasione kuwa Tanzania imepitisha sheria hiyo ya ugaidi kwa haraka kwa sababu Tanzania ina tatizo na ugaidi. Nikaeleza kuwa sheria hiyo imepitishwa kwa sababu Bunge la Tanzania limehodhiwa na Kanisa na kupitishwa kwa sheria hiyo hakuna uhusiano wowote na ugaidi ila Wakristo wamepata fursa ya bure ya kupambana na Uislamu wakitumia serikali ya Marekani kama upawa wao wa kuopolea finyango ya moto kwenye chungu kinachotokota. Nikauchekesha mkutano kwa kuwaambia kuwa Wamarekani wamefanywa wajinga na Kanisa kwa kuchonganishwa na Waislamu

Udhalilishaji unaofanywa na vyombo vya Dola Tanzania dhidi ya Waislamu


wa Tanzania ambao hawana ugomvi nao asilani. Baada ya kusema hayo nikahitimisha kwa kueleza nguvu ya Waislamu Tanzania, kwanza kwa wingi wao na kisha kwa historia yao iliyotukuka iliyodumu takriban miaka mia wakipambana na ukoloni wa Wajerumani kwa silaha (1905 1907), kisha ukoloni wa Waingereza (1929 1961) na kuhitimisha kwa kuleta uhuru na kuanzia 1961 hadi sasa wanapambana na nguvu ya kanisa linalopiga vita Uislamu. Kukia hapa ukumbi ukawa umepata joto. Wanigeria wamesimama kutaka niwaeleze vipi Waislamu watakuwa wamepigania uhuru kisha wako wengi nchini wanaruhusu wao kufanywa raia daraja la pili. Wakashangazwa kuwa hata historia ya mashujaa Waislamu waliopigana Maji Maji na kunyongwa na wakoloni na mashujaa walipigania uhuru wa Tanganyika hawatajwi katika historia ya ukombozi. Nilitoa majibu kadri Allah alivyoniwezesha. Nakumbuka kitu kimoja walichosema wale ndugu zetu Wahausa. Walisema hali hiyo iliyoko kwenu haiwezekani kutokea Nigeria kwa kuwa hiyo itakuwa na sawa na kutangaza vita. Kisha wakanihakikishia kuwa sheria hiyo ya ugaidi haitapitishwa Nigeria hata siku moja. Wapashaji habari wangu wakajanieleza baadae ni hili hitimisho langu ndilo lililosababisha Wamarekani kuleta taarifa Dar es Salaam kutaka taarifa zangu za ugaidi ikawa sasa sababu imepatikana ya mimi kushughulikiwa na vyombo vya dola. Ndipo ikatengenezwa hadithi ya kuku jike na ngombe dume (cock and bull story) kuwa Mohamed Said ni Mzungu wa unga kwa hiyo akamatwe. Mkasa huu ulinika miaka sita iliyopita lakini hadi leo kovu la mkasa ule limebaki katika pasi yangu. Sielewi pasi yangu inaonyesha nini inapotiwa katika compyuta baada ya mkasa huu kwani kama mara tatu husimamishwa kwa muda nakuombwa nitoe maelezo ya ziada kuhusu niendako kila nisaripo nje ya Tanzania. Nimeshuhudia hali hii Uwanja wa Ndege Amsterdam na Detroit, Marekani. Berlin, Ujerumani niliambiwa mzigo wangu umepotea lakini hata kabla sijatoka uwanjani nikatafutwa na kukabidhiwa mzigo wangu na kwa hili sikuwa peke yangu nilikuwa na mwenzangu, jamaa wa Kiarabu kutoka Misri. Sijui kama mizigo yetu ilikuwa imebakishwa nyuma kwa upekuzi zaidi. Amsterdam, Uholanzi baada ya kupita sehemu zote muhimu za upekuzi wakati naelekea kituo

cha mwisho niingie kwenye ndege inayoelekea Detroit, Marekani nikachopolewa kutoka kwenye mstari na nikawekwa pembeni peke yangu kwa usaili wa ziada. New York kadi yangu ya benki ilikataa kutoa fedha kwa siku nzima hadi siku ya pili. Nilikujafahamishwa baadae kuwa system ilikuwa inanichunguza kwanza. Ilikuwa siku ya pili baada ya kuonana na maofisa wa benki ndipo kadi yangu ikaanza kutoa fedha. Geneva, Uswisi kadi yangu ilikataa kutoa fedha katika mgahawa. Sikujua kama ni yale yale au haya yalikuwa mengine. Lakini pasi hii asa wa uhamiaji wa Tanzania alipoiingiza kwenye compyuta yake alimwita mwenzake kuja kutazama kisha wakawa wanacheka. Waliona nini kwenye pasi yangu Allah ndiye ajuaye. (25th February 2008)

Inatoka Uk. 11 wanapokwenda kupata matibabu wana makosa gani? Juzi hapa tumeshuhudia jopo la madaktari, taasisi za kutetea haki za Binadamu wakiwemo kina Hellen KijoBisimba na Ananilea Nkya wakiandamana kumsindikiza Ulimboka uwanja wa ndege wakiwa na msururu wa magari yapatayo nane, wenyewe walipoulizwa kulikoni wakasema eti wanaonesha mshikamano! Mbona mshikamano huu hatukuuona alipouawa Dk Maphingo? Kama si unaki na uabalakala kumbe tusemeje?. Vy a m a v y a C U F n a CHADEMA, ni mfano wa sekta hiyo ya kisiasa ambayo vimelaani kitendo cha kutekwa na kupigwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka, huku vikiitaka serikali kuunda tume huru ya uchunguzi, kauli ambayo hatukupata kuisikia wakiitoa pale alipouawa Dk Alhaji Maphingo Jumbe. Je, dhambi ya Dk Maphingo iliyofikia hata

Kwanini matamko haya hatukuyasikia alipouawa kinyama Dk. Maphingo Jumbe?


viongozi wa serikali Idara ya afya, taasisi za kutetea haki za Binadamu, vyombo vya ulinzi na usalama, watu binafsi na vyombo vya habari kutokusikika wakilaani mauaji ya Dk Jumbe ni kuwa kwake Muislamu? Hivi tumeka mahala nchi hii kuanza kubaguana na kunyanyapaana kwa kutolipa kipaumbele tukio linapomka Muislamu na tukio kama hilo hupewa uzito wa kitaifa linapomka Mkristo? Kama sivyo, basi mniambie nyie mnaojua sababu ya viongozi wote wa juu wa serikali kusikika wakilaani majeraha ya Ulimboka ingawa wana hasira naye kutokana na kuongoza mgomo wa madaktari na wakati huo huo kudharahu kabisa kufanya hivyo kwenye mauaji ya Dk. Maphingo Jumbe aliyeuawa kinyama akiwa nyumbani kwake. Marehemu Dk. Maphingo alizaliwa Juni 30, 1965 mkoani Tanga ambapo elimu yake ya msingi aliipatia katika shule ya Mwakizaro, Tanga kutoka 1975-198, kabla hajenda shule ya sekondari ya Usagara mwaka 1982-1985. Baada ya kuhitimu masomo hayo Alhaji Dk Maphingo Jumbe Mohamed alijiunga na Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya Muhimbili Dar es Salaam kuanzia Januari 1986Februari 1996 na kufanikiwa kupata Cheti cha Teknolojia ya Maabara. Kwa kuwa marehemu alikuwa akijitambua yeye binafsi na kuitambua jamii anamoishi, aliona vema angeongeza elimu kuhusiana na taaluma yake ambapo Septemba 1994-Juni 2001 alifanikiwa kupata Shahada ya kwanza ya udaktari katika Chuo Kikuu cha Kursk State nchini Urusi. Na Septemba 2007- Mei 2009 Dk Maphingo alikuwa ameshahitimu Shahada yake ya Uzamili ya Afya ya Jamii yaani Master of Public Heath (MPH) katika Chuo Kikuu kishiriki cha Muhimbili jijini Dar es Salaam, Tanzania. Mbali na masomo hayo, vilevile Dk Maphingo aliwahi kutunukiwa vyeti mbalimbali katika mafunzo aliyokuwa akihudhuria enzi za uhai wake. Kwa mfano Januari 2007Februari 2009 alihudhuria mafunzo ya wakufunzi wa namna ya kuwahudumia waathirika wa ugonjwa wa UKIMWI ambayo yaliandaliwa na chama cha madaktari nchini Kenya

(KMA) kwa kushirikiana na mtandao wa kuwajengea uwezo, kinga na matibabu waathirika hao yaliyofanyika Nairobi, Kenya. Cheti cha mafunzo ya namna ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu kwa waathirika wa ugonjwa wa UKIMWI ambacho alikipatia Kampala, Uganda Februai 2006. Cheti cha utati juu ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa UKIMWI alichokipata mwaka huohuo wa 2006, Chuo Kikuu cha Makerer, Uganda. Novemba 7-Novemba 15,2005 alihudhuria mafunzo juu ya uangalizi na utabibu wa ugonjwa wa UKIMWI kama yalivyoandaliwa na mpango wa kudhibiti Ukimwi Tanzania (NACP) jijini Dar es Salaam, Tanzania. Pamoja na mafunzo mengine mengi ambayo kutokana na ufinyu wa nafasi sikuweza kuyataja. (Mwandishi wa habari hizi anapatikana kwa simu +255 (0) 718 406 242)

15

Inatoka Uk. 16

Kauli ya Mufti yazidi kupingwa


kudhoosha Uislamu. Akiongea kwa masharti ya kutajwa jina lake gazetini mmoja wa viongozi wa juu wa Bakwata alisema, haelewi imekuwaje Mufti Simba kabatilisha Msimamo wa Bwakata, aliyoito ya kupinga Sensa kwa Waislamu. Kiongozi huyo alishiriki katika Semina ya viongozi wa Dini, Mjini Dodoma Julai 11, 2012, ambapo Serikali iligomea hoja ya Masheikh kutaka kurejesha kipengele cha Dini katika Sensa itakayofanyi mwezi agosti. 2012. Alisema, baada ya hatua ya Serikali, Masheikh wapatao 30, walikutana na kukubaliana kususia Sensa kwa Waislamu, Tamko ambalo lilitolewa katika Makao Makuu ya Bakwata, Kinondoni. Alisema, dalili za Mufti Simba, kubatilisha msimamo huo ambao awali aliuunga mkono na kutolea tamko kabla ya Tamko lililojumuisha Jumuiya na Taaisisi za Kiislamu, aliziona siku moja baada ya tamko hilo la pamoja, ambapo walianza kuhojiwa uhalali wa tamko hilo kutolewa Bakwata. Alidai tamko la Mufti Simba, halielewi wala hakushirikishwa kama alivyoshirikishwa katika tamko la awali. Katika hatua nyingine, kuonyesha kuwa tamko la Mufti, lina walakini hata ndani ya Bakwata, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa ndani ya Bakwata, alimeliambia Gazeti hili kuwa asihusishwe na tamko la Mufti, Simba. Alisema, yeye anabaki na msimamo wake wa awali akiwataka Waislamu kutoshiriki sensa na kupinga kauli ya bosi wake ya kuwataka Waislamu kushiriki sensa, bila kipengele cha dini kuingizwa. Nimekuita nikuambie, siungi mkono kauli ya Mufti, kwa kuwa majumuisho ya madai ya Waislamu kupitia Jumuiya na taasisi yaliafikwa Dodoma, hayajafanyiwa kazi. Sielewi kwa nini alibadilika (Mufti) na kutoa kauli ile pengine alishauriana na wale aliokuwa nao siku hiyo. Alisema Sheikh huyo huku akisema jina lake

Makala

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6 - 7, 2012

AN-NUUR

kwa ujumla hawaamini na hawakubali kuwa Waislamu ni wachache, hivyo anadhani Serikali inashindwa kurejesha kipengele cha Dini ili kuficha ukweli, kwani huenda kutakuja hoja, vipi Waislamu ni wachache Serikalini na sekata zake. Akahoji na kusema kuwa kuna maswali serikali inatakiwa kujibu moja likiwa ni kwa nini nafasi kama za Wakuu wa Wilaya na Mikoa, zimekuwa ni miliki ya Wakristo kwa maana kuwa idadi yao ni kubwa sana ikilinganishwa na Waislamu. Akizungumzia kauli ya Mufti Shaaban Simba, alisema Mufti, amewasemea Bakwata, na sio msimamo wa Waislamu wote. Hili tumelizoea kwa Bakwata kwenda kinyume na maslahi ya Uislamu na Waislamu, hata suala la mwezi wa Ramadhani wametugonganisha sana, tulizuiwa mpaka kuswali kisa Bakwata hawajasema. Lakini imefika mahali Waislamu wameelewa hata wakisema Waislamu wanapima. Alisema Sheikh Barahiyan. Alisema, anasikitishwa na Serikali kila mara kupuuza hoja au ushauri wa Waislamu lakini imekuwa nyepesi kupokea na kuwakubalia Wakristo kwa yale wanayoyataka, akitolea mfano sakata la Maaskofu kuijia juu Serikali baada ya kuondoa misamaha ya kodi kwa asasi za kidini na hatimae Serikali kurejesha misamaha hiyo. Alisema, muda muafaka ukika atautangazia umma, na kwa sasa Mkoani Tanga, wanatumia Misikiti kutoa maelekezo kwa Waislamu kutoshiriki Sensa, ikiwa kipengele cha Dini hakitokuwapo. Wakati huo huo, kufatia taarifa ya Mufti wa Bakwata, kutoa tamko la Taasisi yake, kuwataka Waislamu kushiriki Sensa, imedaiwa kuwagawa wadau wa Taasisi hiyo huku wakimtuhumu Mufti wao kutumiwa na Serikali

Barahiyani azishukia nchi za Kiislamu


Inatoka Uk. 16

lihifadhiwe. Alisema, imeka wakati sasa Bakwata isimamie Waislamu si Serikali ili kuweza kurudisha imani

ya Waislamu nchini, kwani alidai mambo haya ya kuwabadilikia Waislamu ndiyo yanayoondosha imani ya Waislamu kwa Baraza hilo.

kitengo kama hicho lakini misaada yake kwa kiwango kikubwa imekuwa ikitoka kwa masharti ya kufuata itikadi za Kishia badala ya kutizama Uislamu kwa ujumla wake. Ipo haja ya kupiga kelele, vipi watuache tumezungukwa na mabenki yatoayo riba, Saccos zenye mfumo huo. Hali hii inawaacha Waislamu kujiingiza katika dhambi ya riba. Alisema Sheikh Barahiyan. Akaongeza kuwa, misaada inayokuja kutoka nchi za Magharibi (hata

kupitia serikali) hufika na kulenga sehemu zenye Wakristo wengi, akitolea mfano sehemu kama za mkoa wa Tanga kutelekezwa. Alisema, misaada hiyo ingekuwa inafika kutoka nchi za Kiislamu, huenda ingeelekezwa katika mikoa ambayo iko nyuma kimaendeleo, ambayo ni wazi kuwa ni yenye Waislamu wengi. Alisema, Mkoa wa Tanga kuna barabra ya Pangani kuingia Dar es Salaam, njia ambayo ni fupi ukilinganisha na hii iyatumika hivi sasa, lakini

imetelekezwa. Sheikh Barahiyan amesema kuwa lau barabara hiyo ingetengenezwa, ingesaidia kuinua uchumi wa wakazi walio pembezoni mwa njia hiyo ambayo wengi wake ni Waislamu. Kuna Balozi za nchi za Kiislamu, tuzifuate tuwashauri waanzishe vitengo, kama ilivyo kwa Iran. Irani ni Taifa la Kiislamu, lakini linaeneza itikadi za Kishia, sasa hili ni tatizo kumtoa mtu katika itikadi yake kwa ajili ya kumpa msaada tu. Alisema Sheikh Huyo.

KINGDOM OF SAUDI ARABIA COMMITTEE OF DAAWAH IN AFRICA TANGAZO LA MASHINDANDANO YA FAMILIA YA MTUME (S.A.W.)NA MASWAHABA KATIKA QUR-AN NA SUNNAH ZA MTUME (S.A.W.) Kamati ya Da-awah Afrika inawatangazia Waislamu wote kwamba kuna mashindano kuhusu familia ya Mtume (s.a.w.) na Swahaba (r.a. ) kuanzia mwishoni mwa mwezi wa sita hadi tarehe 19/7/2012. Nakala za mashindano hayo zinapatikana sehemu zifuatazo: Tanga: Msikiti wa Alkheir, muone Sheikh Ally M. Kiroboto. Dar es Salaam: ka Msikiti wa Alfurqan, Buguruni Malapa, muone Sheikh Juma O. Poli (0754302082). Unguja: Muone Sheikh Twalib Juma (0777413502), ka osi za Africa Muslims Agency, Mwanakwerekwe. Pemba: Muone Sheikh Yusuph Hamza, Kengeja. Wanaoruhusiwa kuingia katika mashindano hayo ni Waislamu wote; wake kwa waume, kuanzia umri wa miaka 20 ishirini na kuendelea. Mashindano yameandaliwa kwa lugha ya Kiarabu, Kingereza na Kiswahili. Wahi nakala yako mapema kwani muda ni mfupi. Wale watakaokosa nakala halisi (original), wanaruhusiwa kurudufu (kutoa Photocopy). WASHINDI KATIKA MASHINDANO HAYA WATAPATA ZAWADI KAMA IFUATAVYO: -Mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu watazawadiwa safari ya kwenda Hija kwa 2012. -Mshindi wa nne na wa tano watazawadiwa Computer ya mkononi (laptop). -Mshindi wa sita, wa saba na wanane watazawadiwa chombo cha kusomeshea Qur-an tukufu. -Mshindi wa tisa na wa kumi watazawadiwa simu za mkononi. Wabillahi tawq

16

AN-NUUR
16

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

USIKOSE KUSOMA AN-NUUR KILA JUMANNE NA IJUMAA

SHAABAN 1433, IJUMAA JULAI 6-12, 2012

AN-NUUR

Kauli ya Mufti yazidi kupingwa


WAISLAMU kamwe hawato batilisha msimamo wao wa kutoshiriki katika Sensa ya watu na makazi, kufuatia kauli ya Mufti wa Bakwata, Sheikh Shaaban Bin Simba, aliyewataka Waislamu kushiriki Sensa, hata kama Serikali haitaweka dodoso la Dini. Kauli hiyo imetolewa na Sheikh Salum Barahiyan wa Jumuiya ya Ansaar Sunnah nchini. Akiongea na An nuur mwishoni mwa wiki iliyopita, alipinga kauli ya Mufti Simba, huku akiunga mkono msimamo wa Jumiya na Taasisi za Kiislamu nchini ya k u w a t a k a Wa i s l a m u kutoshiriki Sensa iwapo Serikali haitaweka kipenge cha Dini katika zoezi hilo. Sheikh Barahiyan pia ameunga mkono kauli WAISLAMU Tabora wakiwa katika kongamano la kupinga udhalimmu wa Baraza ya Katibu wa Shura ya Maimam nchini, Sheikh al Mitihani la Tanzania lililofanyika hivi karibuni mkoani humo. Ponda Issa Ponda, aliyesema kuwa Mufti Simba si Msemaji wa Waislamu nchini, bali amewasemea Bakwata. Sheikh Barahiyan, aliyekuwa mmoja wa washiriki na mtoa mada katika Kongamano la mwaka la Baraza Kuu la Jumiya za Ansaar Sunnah Tanzania (Basuta), na kushirikisha Jumuiya Na Bakari Mwakangwale B a r a h i y a n , a k i o n g e a husaidia na dini yao ya zake kutoka mikoani, akifafanua kwa nini katika Kongamano la Kikristo. Alisema, huenda hii ni Waislamu wanahitaji MASHEIKH na Baraza Kuu la Jumiya za Wa n a h a r a k a t i w a Ansaar Sunnah Tanzania kutokana na jinsi mfumo kuwepo kipengele cha Kiislamu nchini, (BASUTA), lililofanyika ulivyo wa kitaiafa na Dini, alisema kwanza wamesema ipo haja katika ukumbi wa hosteli kimataifa, hivyo alisema kuondosha utata wa idadi kwa Balozi za nchi za za Chuo Kikuu cha Dar es ipo haja ya kuonana na sahihi ya takwimu za idadi Kiislamu zilizopo nchini, Salaa (UDSM), mwishoni Balozi za nchi za Kiislamu ya wananchi na dini zao, ili k u p e l e k a m a o m b i n a Taifa na wananchi wawe kuanzisha kitengo mwa wiki iliyopita. maalum cha Dini S h e i k h B a r a h i y a n pengine kuuliza kikwazo na takwimu sahihi. Alisema, kujua idadi kwa lengo la kusaidia a l i s e m a i m e k u w a n i ni nini. ya watu na imani zao kwa Barahiyan alisema kuwa Waislamu. kawaida kusikia misaada Hayo yamesemwa k u t o k a k a t i k a n c h i angalau kwa sasa Iran ina Serikali itasaidia katika suala la ujio wa Mahakama na Sheikh Salum za Magharibi, ambazo Inaendelea Uk. 15 ya Kadhi kujua ni eneo

Kiongozi Ansaar asema Waislamu hawashiriki Bakwata wagawanyika, wengine wapinga ya Mufti

Na Bakari Mwakangwale

Barahiyani azishukia nchi za Kiislamu Dar

Ataka ziwe na vitengo vya kusaidia Waislamu

gani lina Waislamu wengi na wapi ni wachache ili kuweza kupeleka huduma hiyo kulingana na idadi ya mahitaji. Alisema, haoni sababu ya Serikali kutaka kujua idadi ya Misikiti na Makanisa, na kukataa kujua idadi ya watu wake wanaotumia nyumba hizo za ibada. Alisema, hivi sasa Serikali imeruhusu kufungua mabenki ya Kiislamu nchini ambazo hufata Sheria za Kiislamu ikiwa ni pamoja na kuepuka riba, hivyo ni vyema kwa Serikali kuwa na takwimu za idadi ya Waislamu ili kuwasaidia wanaotaka kufungua Benki hizo kujua ni wapi penye Waislamu wengi kwa ajili kupeleka huduma hiyo kwa maana mfanyabiashara makini huangalia ni wapi penye wateja wengi wa biashara yake. Sheikh Barahiyani amesema kuwa, wadau wa afya wameonyesha kuwa sehemu ambayo kuna Waislamu wachache kumekithiri ugonjwa wa macho huku zile sehemu ambazo Waislamu ni wengi, ugonjwa huo haupo. Akasema, ingekuwa bora kwa Serikali kupata takwimu sahihi ili kujiridha na kufanya utati sababu ni ipi inayotoa tofauti hizo kiafya. Alisema, pamoja na kuwa Serikali inadai haina dini lakini wananchi wake wana dini, hivyo kujua idadi yao kiimani katika sehemu husika, itaisaidia Serikali kuona ipeleke huduma zake kulingana na mahitaji ya imani ya watu wake na kuepusha dhana ya upendeleo kwa watu wa dini moja. Sheikh Barahiyan anasema kuwa yeye na jamii ya Waislamu
Inaendelea Uk. 15

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

You might also like