You are on page 1of 1

1

STATE HOUSE ZANZIBAR


OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE
Zanzibar 17 . 08 .201 7

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed


Shein , amewaahidi wananchi wa K itogani kuwa uwanja wao utatengenezwa kwa
kiwango ha Kimataifa kitakachoshirikisha michezo ya aina mbali mbali.

Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao wa kijiji cha Kitogani kuwa kijiji chao kitakuwa
eneo la michezo kwani watafika watu kutoka ndani na nje ya n chi kwa ajili ya
kuutumia uwanja wao mpya unaoendelea kujengwa ambao tayari kwa awamu ya
kwanza umekamilika.

Hivyo , amewataka wakaazi wa Kitogani kujiandaa kuwapokea wageni wakiwemo


wanamichezo huku akieleza jinsi Serikali ilovyojiandaa kukijenga kiwanja hicho kuwa
cha kisasa na kuweza kuchezwa michezo kadhaa mbali na mpira wa miguu.

Alieleza kuwa miongoni mwa juhudi zitakazochukuliwa na Serikali anayoiongoza ni


pamoja na kuuwekea mpira wa kukimbilia, majani bandia kama yaliopandwa
halitodumu , taa na kuje ngwa majukwaa ya kukaa pamoja na mambo mengine yote
muhimu yanayopaswa kuwepo kiwanjani hapo.

Dk. Shein alisema kuwa ujenzi wa kiwanja hicho ni utekelezaji wa ahadi aliyowaahidi
wananchi wa Kitogani baada ya wazee kutoa ombi lao la kujengewa uwanja vijana wao
na kusisitiza kuwa juhudi atazifanya katika kuhakikisha kiwanja kinakamilika katika
wakati wake wa uongozi .

Katika maelezo yake, Dk. Shein alisema kuwa nia ya Chama chake cha CCM ni
kuimarisha michezo.

Aidha, Dk. Shein alieleza kuvutiwa kwake na mas hindano ya riadha ya Wilaya
yaliyofanywa mnamo mwaka 2014 na mshindi alitoka Wilaya ya Kati katika kijiji cha
Ndijani na kuyapongeza mashindano hayo .

You might also like