Professional Documents
Culture Documents
1
mwezi june,mwakani hususani katika ujenzi wa daraja la gerezani na
mingineyo
Kwa upande wake Mhe. Dkt Rais Magufuli amemshukuru Rais huyo wa
Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan Bw. Shinichi Kitaoka kwa uamuzi
wake wa kuja Tanzania na amemhakikishia kuwa Tanzania inatambua
mchango mkubwa ambao Japan inautoa katika maendeleo ya Tanzania
kupitia JICA, na kwamba itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano
wake na Japan katika masuala mbalimbali.
Mhe. Rais Magufuli ameishukuru JICA kwa kutoa fedha kwa ajili ya
kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi jijini Dar es Salaam ikiwemo upanuzi wa
barabara ya Mwenge Morocco, utakaoiwezesha barabara hiyo kuwa na zaidi
ya njia nane, ujenzi wa barabara ya TAZARA, ujenzi wa Daraja la Gerezani
njia nne, na barabara ya Bendera tatu hadi Kamata.
Emmanuel Buhohela,
Mwandishi wa Habari,Msaidizi wa Rais,
Dar es Salaam.
21 Agosti, 2017