Professional Documents
Culture Documents
com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1181 SHAABAN 1436, IJUMAA , JUNI 12-18, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Guantanamo Dar!
Aljazeera Ukerewe yazima uzushi wa Jihad John-3
Waalikeni Polisi, 'Task Force' Misikitini wajione!
Mwenzao alisilimu baada ya kutesa Guantanamo
OCD Nansio ajionea. Sasa ahimiza Doria ya Nafsi
MWANASHERIA Mkuu
Wa Zanzibar Saidi Hassan
Tafrani Segerea
Ustadh Salum Ally alala juu ya mti
Amtaka Mwanasheria Mkuu Zanzibar
Sheikh Farid aitwa kuepusha balaa
HAIWEZEKANI Serikali
ya Ta n z a n i a i a c h i l i e
mambo haya yasomeshwe
katika shule za Tanzania.
Vipi mambo haya ya
kipropaganda yenye
khatari kubwa kwa
nchi nzima ya Tanzania
yaendelee kusomeshwa.
Kama nchi hii haina
Udini, muhimu kabisa
ni kupigwa marufuku
usomeshaji wa propaganda
za aina hii na vitabu vyote
vichomwe moto leo kabla
ya kesho. (Soma zaidi Uk. 7, 8)
Na hapo ndipo
watakapoweza kuona kasi
na ghadhabu za nguvu ya
Umma wakati ukifika.
Tu o m b e a m a n i n a
u t u l i v u wa k w e l i n a
uchaguzi huru na wa haki!
(Soma Uk. 16)
Tahariri/Habari
2
AN-NUUR
Karibu Ramadhani
ZIMESALIA siku chache
sana kabla ya mwezi
mtukufu wa Ramadhwani
kuingia.
Huu ni mwezi
wa kufunga kama
ilivyobainisha Qur'an
iliposema:
Enyi mlioamini!
mmefaradhishiwa swawm,
kama waliyofaradhishiwa
waliokuwa kabla yenu ili
mpate kumcha Allah.
Na atakayekuwa
miongoni mwenu
mgonjwa au yumo safarini,
basi atimize hisabu katika
siku nyingine. Na wale
wasioweza, watoe fidia
kwa kumlisha masikini.
Na atakayefanya wema
kwa kujitolea, basi ni bora
kwake.
Na mkifunga ni bora
kwenu, kama mnajua.
Mwezi wa Ramadhaan
ambao imeteremshwa
humo Quran kuwa ni
uongofu kwa watu, na
hoja zilizo wazi za uongofu
na upambanuzi. Basi
atakayekuwa mjini katika
mwezi huu na afunge.
N a m we n ye k u wa
mgonjwa au safarini, basi
atimize hisabu katika
s i k u n ye n g i n e . A l l a h
anakutakieni yaliyo
mepesi wala hakutakieni
yaliyo mazito, na
mtimize hiyo hisabu, na
mumtukuze Allah kwa
kuwa amekuongoeni ili
mpate kushukuru. [AlBaqarah: 183-185].
Ni mwaka jana tu
tulikuwa na mgeni wetu
huyu tunayetarajia
kumpokea tena hivi
karibuni, Mwenyezi
Mungu akitujalia.
Tu l i k a a n a y e s i k u
zisizozidi thelathini na
baadaye akaondoka.
Huenda wengi wetu
mgeni huyo alifika
na akatuacha kama
alivyotukuta. Tulisahau
kuwa mgeni huyu kwetu
ni neema isiyofanana na
kitu chochote. Na kwamba
akija akaondoka bila ya
Muislamu kutakasika, basi
tena huyo yupo katika
hasara kubwa.
L a k i n i k wa h e k m a
zake Mwenyezi Mungu,
kila mwaka neema ya
mwezi wa toba hutufikia
na kupata fursa nyingine
AN-NUUR
muumba.
Shukrani zote ni zake
Muumba wa mbingu na
ardhi aliyetujaalia siku
chache za mgeni wetu
Ramadhan zinazompa
Muislamu nafasi ya
kujisafisha na kuwa Mcha
Mungu.
Tutoe tu indhari kwa
wa f a n ya b i s h a r a w o t e
nchini, hasa wa bidhaa
za vyakula kuwa katika
kipindi hiki cha mwezi
Mtukufu wa Ramadhani,
basi wawape tahfif
Waislamu kwa kuwauzia
bidhaa kwa bei ya haki, ili
kuwawezesha kutekeleza
ibada hii kwa wepesi.
Tukifanya baishara kwa
uadilifu tukitanguliza
mbele ucha-Mungu, utu
na huruma kwa waja wa
Allah, itakuwa na matokeo
bora zaidi kuliko kuweka
mbele tamaa ya kupata
hata kwa kuwakomoa
wafungaji.
Na Bakari Mwakangwale
WA K I L I w a Wa i s l a m u
wenye tuhuma za Ugaidi,
Abubakari Salimu, amesema
Serikali ina nia mbaya dhidi
ya wateja wake kwa kuipiga
danadana kesi hiyo ili wateja
wake waendelee kusota
rumande.
Wakili huyo, ameyasema
hayo Jumatatu wiki hii
akiongea na An nuur, mara
baada ya Mahakama ya
Kisutu Jijini Dar es Salaam,
kuiahirisha kesi hiyo
inayowakabili Sheikh Farid
Had na wenzake 23, mapaka
Juni 18, 2015.
Alisema, kutokana na
mwenendo wa kesi hiyo
unavyo kwenda, wanaona
kama vile kuna nia mbaya
ya kutaka kuichelewesha
kesi hiyo kwa makusudi kwa
kutumia kigezo cha rufaa yao
(upande wa mashitaka) katika
Mahakama ya Rufaa.
Tunaona kama kuna nia
mbaya ya kuichelewesha
kesi hii, wanatumia kigezo
kwamba kwa sababu
wa m e k a t a r u f a a k a t i k a
Mahakama ya Rufaa, ili pia
na mambo mengine huku
yasimame na hawa Waislamu
waendelee kusota rumande.
Alisema Wakili Salimu.
Wakili Salimu, alisema
awali katika kesi hii ya
Masheikh na Waislamu,
Mahak ama Kuu ilisema
kwamba shauri hili lirudi
Mahakama ya Kisutu,
ili litolewe maamuzi, na
kwamba Mahakama isiseme
tu kwamba haiwezi kusema
chochote hivyo ikatakiwa
Inaendelea Uk. 4
3
Na Mwandishi Wetu,
Mwanza
KITUO cha Kiislamu,
Aljazeera kilichopo Nansio,
Ukerewe, kimefungua
milango yake kwa kila
anayetaka kujua ukweli na
kuvunjilia mbali propaganda
chafu za kukibambikia
ugaidi.
Katika hatua hiyo,
iliandaliwa semina ya mwezi
mzima ambapo msimamo
na mafundisho ya Uislamu
juu ya haki na wajibu wa
Waislamu kwa binadamu kwa
ujumla ulifafanuliwa kwa
mapana na marefu.
M a s o m o ya l i y o t o l e wa
katika semina hiyo
iliyowajumuisha washiriki
181 kutoka mikoa ya Kanda
ya Ziwa, inafuta kabisa zile
propaganda na dhana potofu
kuwa Chuo cha Kiislamu
k a m a A l - J a z e e r a , k u wa
kinaweza kutumiwa kwa
namna yoyote kusomesha
na kuhimiza jambo la
kuwadhuru watu.
Ili kuliweka hilo
bayana kwa vyombo vya
Dola, kiserikali na kijamii,
walialikwa pia washiriki na
watoa mada kutoka taasisi
mbalimbali zisizo za kidini
wakiwemo Kamanda wa
Polisi wa Wilaya, Hakimu wa
Wilaya na maofisa wengine
wa serikali.
Huu ni ufunguaji milango
na uwazi ambao kwa hakika
ni wa kuhimizwa ufanyike
katika taasisi zote za
Kiislamu ili kuchoma moto
kichaka wanakojificha watu
wanaopiga propaganda chafu
dhidi ya Uislamu.
Maadhali mafundisho
ya Uislamu sio biashara
ya bangi, basi Waislamu
wasione vibaya kuwaalika
watu wengine, hasa mamlaka
za kiserikali na taasisi za
kijamii kuona wanachofanya
na hata kutoa elimu kama
alivyofanya OCD na Hakimu
wa Ukerewe.
I l i k u wa n i I m a m u n a
Khatibu Mkuu wa Msikiti
Mkuu wa Ijumaa Mwanza
Sheikh Hamza Mansour,
aliyehudhurisha mada
mintarafu muamala au
mahusiano baina ya Waislamu
na wale wasiokuwa Waislamu.
Katika mada hiyo, Sheikh
Hamza alionesha namna
Mtume alivyoamiliana na
wasio kuwa Waislamu kwa
wema kwa kuwafanyia insafu
na adala ya hali ya juu, hata
wale ambao walikuwa maadui
zake wa wazi kabisa.
Ni katika hali hiyo, washiriki
wa semina na Watanzania
k wa u j u m l a wa l i t a k i wa
kujiuliza: kama Mtume (s.a.w)
alikuwa akiwafanyia uadilifu,
hata wale waliomtangazia
uadui, vipi leo Waislamu
watangaziwe ugaidi ambao
tafsiri yake ni kuwadhuru
watu wasio na hatia.
Au vipi Chuo, Madrasa au
shule inayoitwa ya Kiislamu,
inayosomesha Uislamu,
ituhumiwe kuwa inasomesha
ugaidi.
S h e i k h
H a m z a
Habari
AN-NUUR
4
Inatoka Uk. 2
Na Sheikh Al-sayed
Awadh Abduladhim
Shukrani zote anastahiki
Mwenyezi Mungu Rehema
na amani zimfikie Mtume
wa Mwenyezi Mungu.
Kwa hakika wamezingatia
wanachuoni funga kwa
u wa z i k u wa n i m a i s h a
ya kimaumbile hayawezi
kuendelea maisha hayo
isipokuwa kwa funga
kutokana na usawa na Afya ya
maumbile yetu yaliyokamili
n a k wa k i u m b e ye y o t e
hapana budi atakumbana na
ugonjwa ambayo yatamzuia
kula na kama hakufunga kwa
kutaka mwenyewe.
Hapa ndipo tunapoiona
miujiza ya Mwenyezi
Mungu kwa kuweka sheria
ya kufunga kuwa ni ibada,
funga husaidia viungo
katika kuvipumzisha kwa
chakula kidogo pamoja
na kuendeleza maisha
ya kawaida kama ilivyo
elimu ya kidaktari ya sasa
imethibitisha kuwa funga
ni kinga na ni tiba kubwa
ya magonjwa mbali mbali
Habari/Makala
AN-NUUR
na Waislamu hao.
Kwa mujibu wa Wakili
h u y o , Wa i s l a m u h a o
wamedai kurejea Gerezani,
Segerea kwenda kuungana
na wenzao waliogoma kula,
tokea wiki iliyopita jambo
ambalo alidai inaongeza
idadi ya wanaogoma kula
kadiri siku zinavyozidi
kwenda mbele badala ya
kupungua.
Hata hivyo, Wakili huyo
a l i s e m a k u wa H a k i m u ,
amewataka wao kama
Mawakili wa watuhumiwa
hao, wanayo kila sababu ya
kufika gerezani kuwaona
watuhumiwa hao na kupata
uhakika wa kile kinachodaiwa
kugoma kula wakiwa humo
gerezani.
Kutokana na hii hali,
Hakimu ameshauri tutumie
nafasi yetu kwende kuonana
nao na wao kama Mahakama,
wa t a c h u k u a j u k u m u l a
kwenda kuwaona pia maana
k i s h e r i a wa n a r u h u s i wa
mipaka au mapungufu
inasimama dini ya kiislamu
kwa ushupavu kwa ukati
na kati wake uliozoeleka ili
kuleta muongozo wake wa
ukati na kati kwa ajili ya uma
wa kati na kati katika hali
zake zote kama alivyosema
Mwenyezi Mungu mtukufu
na hivyo hivyo tumewafanya
uma wa kati na kati 143 Albakarat anasema mmoja wa
madoktari waislam pamoja
na kukiri kwangu kulikotimia
kama dokta muislam
kwamba funga husaidia
katika tiba katika baadhi ya
magonjwa isipokuwa mimi
Siwezi kuutani kielimu kuwa
ni hakika na ni maalum
wakati wa mtume kabla ya
zama zake kabla ya kuja
mtume na hakuja mtume
(S.A.W) kwa dalili ya wazi
inayojulisha nafasi ya funga
katika tiba na lililozuri na
tuseme kwamba miongoni
mwa hukumu za funga kuwa
zinasaidia tiba baadhi ya
magonjwa kwa masharti ya
kushikamana na mpango wa
chakula cha kiislam na amri
za daktari anayekutibu na
huu ndio muongozo wa ukati
na kati katika kuifanyia kazi
funga na hilo ndilo bora kwa
kufuata na kuepuka kuvuka
mikapa au mapungufu
ambayo hupelekea maadui
wa u i s l a m u k u wa u n a
upungufu na hauna utukufu
pale tutakapo waambia kuwa
katika funga kuna tiba ya
kila magonjwa tunawaambia
hakuna tiba katika funga ya
hivi hivi.
5
Jeshi Lebanon
lawashukuru
Hizbullah kwa
kuwadhibiti
magaidi
KAMANDA Mkuu wa Jeshi
la Lebanon Jean Kahwaji
ametoa shukuran zake za
dhati kwa Wanaharakati
wa Kiislamu wa Hizbullah
nchini humo, kufuatia
juhudi walizozionyesha
katika kukabiliana na
makundi ya kigaidi
wakishirikiana wanajeshi
wa Lebanon katika
operesheni za pamoja katika
maeneo ya mpakani mwa
nchi hiyo na Syria.
Wa p a m b a n a j i wa
H i z b u l l a h wa l i a n z i s h a
operesheni za kuyasafisha
maeneo ya mpakani ya alQalamun yaliyopo katika
ardhi ya Syria tangu wiki
tatu zilizopita, ambapo
wamefanikiwa kuyasafisha
maeneo mengi yaliyokuwa
yamejaa makundi hayo.
K a t i k a h o t u b a ya k e ,
Kamanda Mkuu wa jeshi
la Lebanon Jean Kahwaji,
alisisitizia udharura wa
kuendelezwa mapambano
hayo kwa lengo ya
kuyasafisha kabisa maeneo
ya mpakani mwa taifa hilo,
huku akishiriautayari wa
jeshi la Lebanon katika
uwanja huo.
Kahwaji alisema kuwa
siasa za ndani ya Lebanon
zinaviunga mkono vikosi
vya jeshi hilo, ili liweze
kutekeleza majukumu yake
kwa namna iliyo bora zaidi.
Aidha alisisitizia udharura
wa jeshi la taifa hilo kuwa
makini na kuongeza
kuwa, uchunguzi wa duru
za usalama unaonyesha
kuwa, makundi ya kigaidi
yanakusudia kutekeleza
vitendo vya kigaidi katika
maeneo ya ndani mwa nchi
hiyo kufuatia kushindwa
huko mpakani.
Inaelezwa kuwa baada
ya mapigano makali katika
m a e n e o ya a l - Q a l a m u n
yaliyosababisha kusafishwa
maeneo mengine ya
kimkakati yenye ukubwa wa
zaidi ya kilometa za mraba
300, kwenye miinuko ya
mpakani mwa nchi mbili
za Syria na Lebanon, hali
ya usalama bado ni ya kutia
wasiwasi katika miji na vijiji
vya maeneo hayo kutokana
na uwepo wa wanachama
wa m a k u n d i ya D a e s h
na Jabhatu Nusra katika
miinuko ya miji ya Arsal,
Kaskazini Mashariki mwa
Lebanon ambao wanaweza
kufikiria kulipa kisasi.
Ni katika mazingira hayo,
ndipo Katibu Mkuu wa
Hizbullah, Sayyid Hassan
Nasrullah alisema kutokana
na mazingira nyeti ya sasa
ya taifa hilo la Kiarabu na
eneo zima la Mashariki ya
Kati, aliwataka viongozi na
makundi ya siasa ya nchi hiyo
kutambua mazingira hayo na
kuisaidia serikali na jeshi
katika kutekeleza majukumu
yao ya kuimarisha usalama
nchini.
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
Mikutano ya
Israel imeua watoto 980 Gaza siri Saudia na
Israel ni hofu
JESHI la Utawala wa Israel
limewaua watoto wapatao
kwa Iran?
980 katika hujuma zake
za hivi karibuni katika
Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa Kituo
cha Habari cha Palestina,
i m e k u wa n i j a m b o l a
kawaida kwa utawala
wa Kizayuni wa Israel
kukiuka sheria zote za
kimataifa kuhusu kulinda
haki za watoto katika vita
vyake dhidi ya Gaza.
Taarifa iliyotolewa na
Jumuiya ya Kimataifa
ya Kuwatetea Watoto
Wapalestina, kwa mnasaba
w a S i k u y a Wa t o t o
Wasio na Hatia ambayo
huadhimishwa Juni 4,
imesema kuwa mwaka
2014 ndio uliokuwa
mbaya na mgumu zaidi
kwa watoto wa Gaza,
kwani zaidi ya watoto 530
waliuawa katika hujuma
za katili za jeshi la Israel.
Aidha taasisi hiyo
i l i s e m a k u wa k a t i k a
mwaka huo, kwa wastani
watoto 196 Wapalestina
walikuwa wakikamatwa
kila mwezi na vikosi vya
Israel. Kwa ujumla zaidi
ya Wapalestina 2,100,
wengi wao wakiwa raia,
waliuawa katika hujuma
ya kutisha za utawala wa
Kizayuni wa Israel huko
Gaza mwaka 2014.
Wakati huo huo taasisi
za Umoja wa Mataifa
zimeafikiana na taasisi
za Palestina kuwa idadi
ya kushtusha ya watoto
waliuawa katika hujuma
ya Israel huko Ghaza
mwaka jana. Katika ripoti
ya s i r i ye n ye k u r a s a
22 iliyovujishwa kwa
TELEVISHENI ya Marekani
ya CNN imefichua kuwa,
Wizara ya Mambo ya Nje ya
nchi hiyo imewapa mafunzo
magaidi wa Daesh.
Te l e v i s h e n i h i y o y a
Marekani imesambaza
mkanda wa video kupitia
Intaneti, ambapo ndani ya
mkanda huo anaonekana
Kanali Gulmurod Khalimov,
Mkuu wa zamani wa Jeshi la
Polisi la Tajikistan ambaye
hivi sasa amejiunga na kundi
la la Daesh akisema kuwa,
yeye binafsi ameshiriki mara
tatu katika mafunzo ya kijeshi
ndani ya ardhi ya Marekani
na moja ya mafunzo hayo
ameyapata kwenye jimbo la
Louisiana la Marekani.
Hata Wizara ya Mambo
ya Nje ya Marekani imekiri
jambo hilo. Msemaji mmoja
wa Wizara ya Mambo ya
Nje ya Marekani ameiambia
televisheni ya CNN kwamba
Kanali Khalimov, alipata
mafunzo ya kijeshi katika
vipindi vitano tofauti nchini
Marekani na Tajikistan baina
ya mwaka 2003 hadi 2014.
Alisema, mafunzo hayo
yalitolewa na kusimamiwa na
Wizara ya Mambo ya Nje ya
Marekani kwa kile alichodai
ni kupambana na ugaidi.
Licha ya viongozi wa
Marekani kukiri mara
kwa mara kuwa ndio
waliolianzisha na kulipa
mafunzo kundi la Daesh,
lakini hivi sasa wameunda
muungano wa kulipiga vita
kundi hilo.
Wachambuzi wa mambo
wanasema kuwa huo ni
mchezo wa kisiasa tu wa
TANGAZO
AN-NUUR
Kwa maelezo zaidi piga simu: 0787 188964, 0784 267762 na 0654 613080
Makala
AN-NUUR
Z I N A Z O F U AT A n i
picha nambari 6.10 na
6.11 ambazo zimewekwa
pamoja katika ukurasa
wa 80 wa kitabu cha
History for Secondary
S c h o o l s , F o r m Tw o ,
2012. Kwanza ziangalie
picha zenyewe, ikisha
tutazungumzia juu ya
propaganda iliyotumika:
M a a n a ya m a e l e z o
yaliyoandikwa kwa
Kiingereza chini ya picha
ya kwanza yanasema
Mtumwa akipigwa
mboko na maelezo ya
pili yanasema Mtumwa
anyongwa na aachiliwa
afe.
Kwa mtu yoyote
mwenye kutumia akili
yake, ataelewa moja kwa
moja kuwa kuziweka
pamoja picha hizi mbili si
jambo la sudfa, bali ni la
kukusudiwa. Ya kwanza
inaonesha huyo khabithi
anayemcharaza mboko
mtumwa ni Mwarabu na
kuiweka ya pili ubavuni
m wa k e n i k u m f a n ya
mtazamaji mwenyewe
amalize kwa fikra ya
kwamba waliomnyonga
mbavuni huyo mtumwa
wa Kiafrika na kumwacha
afe kwa maumivu mapevu
ya kikatili, si wengine bali
ni Waarabu Waislamu.
Sasa tuangalie mchezo
mchafu wa kipropaganda
we n ye k u t u m i a d i n i
kama ni kisingiziyo
ulivyochezwa.
Kwanza, inasikitisha
kuona kuwa waandishi wa
kitabu hicho cha historia,
kughushi mchoro wa yale
yaliyotendeka Suriname
Amerika ya Kusini, nchi
ambayo ilikuwa ni koloni
la Wadachi na wala sio
Afrika Mashariki na
wa k h u s i k a wa l i k u wa
Wazungu Wakristo wala si
Waarabu Waislamu. Sasa
Kuadhibu Watumwa
Wa z u n g u Wa k r i s t o .
Imeandikwa kwingi
na hadi kuna kanda za
filamu zinazoonesha na
kuzungumzia ukhabithi
wa Mfalme wa Wabiligiji,
Leopold II (1835-1909).
Mfalme huyu na
Wabiligiji walipoitawala
Kongo, waliwalazimisha
Wa a f r i k a k u wa f a n y i a
Inaendelea Uk. 8
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 7
kazi kama ni watumwa
wa o n a wa n a h i s t o r i a
wanatuelezea kuwa
Wabiligiji waliwauwa
Waafrika wasiopungua
millioni kumi na
k u wa m a u wa j i h a y o
yanatambulikana kama ni
maafa makubwa. Mauwaji
ya k h a l a i k i ya wa t u
ambayo kwa Kiingereza
huitwa genocide.
Iangalie tena picha
ya asili ya kamera
iliyotangulia na utaona
kuwa Mwafrika aliyekuwa
kibaraka wa Kibiligiji,
ndiye aliyetumwa
kumpiga mboko mtumwa
wa Kiafrika. Mzungu
Mkristo haonekani
pichani, kwa hivyo
lawama kubwa anatupiwa
nokoa wa Kiafrika kwa
kutekeleza amri za
Mzungu za kumtendea
mtumwa ukhabithi.
Lakini picha ya kuchora
inaonesha kuwa khabithi
huyo mwenye kumtandika
mboko mtumwa wa
Kiafrika, ni Mwarabu
mwenyewe, ingawa hao
makhabithi wa Kiarabu
pia waliwatuma manokoa
wao kutekeleza amri zao.
Kwa hivyo, katika picha hii
tunapooneshwa moja kwa
moja kuwa ni Waarabu
Waislamu wenyewe ndio
waliowafanzia ukhabithi
watumwa wa Kiafrika,
lawama zetu zinawashukia
Waarabu Waislamu bila ya
kizuizi.
Kama nilivyoelezea,
picha hii ni ya kuchora, si
ya kamera kama ya chini
yake. Kwa hivyo inatokana
na fikra za mchoraji.
Je, unadhani mchoraji
hakukusudia mtazamaji
aone uchungu na ahisi
chuki juu ya Mwarabu
Mwislamu na hatimae
kuwachukia Waislamu
na Uislamu wenyewe?
Kila kitu kimepangwa na
wenye siasa kali za udini
na wachoraji wao. Hakuna
kilichochorwa kwa bahati
mbaya.
Picha na asili
zake tumeziona. Je,
wanapropaganda za
udini walidhani kuwa
k u l e k u g h u s h i k wa o
hakutatambuliwa?
Haisikitishi tu, bali
inaliza kuiona hali
ya masomo ya historia
iliyojaa chuki dhidi ya
Waislamu Tanzania ilivyo,
huku wanajua fika kuwa
Tanzania ina Waislamu
Katika maandishi
yao pia wametumia
propaganda kubwa kwa
mwenye kuelewa lugha
ilivyotumiwa. Kwa mfano,
katika sehemu waliyoiita
The psychological effect of
slavery on its victims yaani:
Athari ya kisaikolojia ya
utumwa kwa waathiriwa,
mna mengi yaliyokusudia
kuficha ukweli na kuleta
chuki, wameandika
Perazia Kaloly na Ferix
Kiruthu yanayofuata:
The Arab slave traders
and the Caucasians slave
owners looked down upon
dark-skinned people.
Ta f s i r i : Wa f a n y a
biashara ya utumwa wa
Kiarabu na Wakaukasian
wamiliki wa watumwa
waliwadharau watu wenye
ngozi nyeusi.
Angalia ibara hio
ilivyoandikwa, kwanza
katajwa Mwarabu kwa
dhambi kubwa ya
k u f a n ya b i a s h a r a ya
utumwa, khalafu katajwa
Caucasian kwa dhambi
ndogo ya kumiliki.
Je, wewe unawafahamu
nani wamekusudiwa kwa
jina la Caucasian?
Hilo ni jina la
kiethonolijia ambalo
halifahamiki kwa wengi
isipokuwa wasomi. Walio
kusudiwa hapo ni wa jamii
9
Na Bakari Mwakangwale
UKIFIKA wanakuambia
k a b i s a k u wa h a p a s i o
Mahabusu. Hapa sio
Gerezani wala hapa
sio Selo ya Polisi. Hii ni
Guantanamo.
Niliwaambia hata
mkiniuwa msidhani kwamba
mtakuwa mmefanikisha
lengo lenu. Sisi mnatukamata
si kwa kuiba, au tumefanya
ovu lolote huko uraiani, bali
mnatutuhumu kwa dhana tu,
labda mseme kosa ni imani
yetu na Uislamu wetu.
WAISLAMU waliokamatwa
kwa tuhuma za Ugaidi,
wa m e f i c h u a k u wa i p o
Guntanamo isiyo rasmi
n c h i n i wa n a y o i n g i z wa
watuhumiwa kuteswa kabla
ya kufikishwa Mahakamani.
Aidha, imedaiwa kuwa
Guantanamo hiyo ipo
chini ya kikosi maalumu
kinachojulikana kama Task
Force ambacho kinafanya
kazi nje ya utaratibu wa
kawaida wa kipolisi.
Hayo yamebainishwa na
mmoja wa watuhumiwa
hao, akiongea na An nuur,
a k i d a i k u wa Wa i s l a m u
wanafanyiwa dhulma kubwa
wa n a p o k u wa m i k o n o n i
m wa wa t u h a o a m b a o
wanajiita Task Force na
kwamba unaweza usiamini
ukielezwa unachofanyiwa
pindi wanapokuhoji watu
hao.
A l i p o u l i z wa k wa n i n i
analeta mfano wa
Guantanamo, alieleza kuwa
ni maafande hao, wanaoitaja
sehemu hiyo kwa jina hilo
mbele ya watuhumiwa, tena
kwa majigambo na kwamba
sehemu hiyo ipo maeneo
ya Mikocheni, Jijini Dar es
Salaam, na wanaeleza wazi
kuwa hapo sio Polisi.
Hili neno ni wao
wanalitamka mbele
yetu, wanapaita hapo ni
Guantanamo, na ukifika
wanakuambia kabisa kuwa
hapa sio Mahabusu, hapa sio
Gerezani wala hapa sio Selo
ya Polisi, bali wanasema hii
ni Guantanamo ya Serikali.
Alisema Muislamu huyo.
Alisema, kabla ya
kukamatwa na aliposikia
madai ya Masheikh
waliofanyiwa vitendo vya
kinyama, ilikuwa ni vigumu
kuamini kama kweli kuna
askari ndani ya Tanzania hii
wanaweza kufanya mambo
hayo.
Lakini anasema, baada ya
kuwa mikononi mwa watu
hao, na mwenendo wao
wa kuwahoji na kuwatesa
watuhumiwa wa ugaidi,
alibaini kuwa hawashindwi
kukufanyia unyama wa aina
yoyote.
Guantanamo
ni
Mahabusu/gereza, lililopo
Marekani, ambalo Taifa
hilo hulitumia kuwahifadhi
watuhumiwa wa ugaidi
kutoka nchi mbalimbali
kabla ya kuchukuliwa hatua
za kisheria.
Alisema, kuwa katika
Makala
AN-NUUR
juu yao.
Remember what Muslims
did to us. Remember who youre
protecting.
Anasema Terry, kuwa hayo
yalikuwa maneno ambayo
kamanda wao aliyekuwa na
cheo cha sergeant alikuwa
akiyarudia mara kwa mara
kama kuwakumbusha kuwa
wanakwenda kukabiliana na
watu waliouwa Wamarekani
4000 katika September 11 na
hivyo hawastahiki kuonewa
hata chembe ya huruma kwa
sababu ni magaidi katili.
So Holdbrooks arrived at
the hot, seared base expecting
hulking killers in every cell.
Anasimulia Campbell.
H a t a h i v y o Te r r y
anasema, alipofika huko na
kila masiku yalivyokuwa
yakienda, alikuja kuona
kuwa aliyokuwa ameambiwa
na makamanda wake na hali
halisi, ni mambo mawili
tofauti kabisa. Ni kama
mbingu na ardhi.
Akitaraji kukutana na
mijitu iliyobobea katika
medani ya kijeshi na kivita,
alisema alikuja kukuta
k u wa wa t u a l i o k u t a n a
nao walikuwa madaktari,
walimu wa skuli na madrasa,
wakulima na wafanya
biashara, maimamu wa
Misikiti, madereva wa tax
(tax drivers) na maprofesa wa
Inaendelea Uk. 10
wanachokuuliza, utasikia
wanasema mpeleke gereji,
huko ndio kuna mateso
m a k u b wa , h u m o g e r e j i
moja ya zana wanayoitumia
k u wa a d h i b u Wa i s l a m u
(watuhumiwa) ni mipini ya
majembe, sio bakora, wala
hupigwi kwa makofi, ni hiyo
mipini na vifaa vingine vizito
ndivyo vinavyotumika.
Kuna watu wa miraba
minne wanafanya shughuli
hiyo, na anapoanza
kukuadhibu anachojoa shati,
anapiga miguuni katika
nyayo, mgogoni mpaka
anatoka jasho kwa kupiga
mwanadamu mwenzake.
Amesema Muislamu huyo.
Alisema, kwa kawaida
ukitoka Sentro, kwenda
Guantanamo, unatoka ukiwa
u n a t e m b e a m we n ye we ,
lakini ukirudi jioni kutoka
huko unaitafutia miguu
pa kukanyaga, kutokana
na kuvimba na wakifika
hapo Polisi, wanakutupa tu
kama mnyama hamna cha
matibabu wala huduma ya
kwanza.
Alisema, mara nyingi
walipokuwa wakirudishwa
Sentro katika hali hiyo
ya maumivu, alikuwa
akiwafariji wenzake kwa
kuwapa mawaidha na
kuwajenga kiimani kutokana
na hali mbaya wanayorudi
nayo kutoka Mikocheni,
jambo ambalo lilisababishwa
kuhamishwa selo na
kupelekwa kituo kingine
cha Polisi.
Anasema, awali akiwa
Guantanamo alipigwa sana
na watu hao wanaojiita Task
Force lakini wakashangaa
hakuwa analia wala kupiga
kelele, jambo ambalo
liliwashangaza na kudai
kuwa yeye ni sugu.
Hata hivyo alidai kuwa
aliwajibu kwamba, wasidhani
n j i a h i y o wa n a y o t u m i a
ya kuwatesa Waislamu ni
kuwakomoa.
Niliwaambia hata
mkiniuwa msidhani kwamba
mtakuwa mmefanikisha
lengo lenu, kama mnadhana
hivyo, muelewe kuwa kwa
Muislamu haiko hivyo,
sisi mnatukamata si kwa
kuiba, au tumefanya ovu
lolote huko uraiani, bali
mnatutuhumu kwa dhana tu,
labda mseme kosa ni imani
yetu na Uislamu wetu.
Najua nipo hapa kwa
ajili ya Uislamu wangu,
kwa hiyo napata faraja
kila mnalonifanyia. Mimi
na Waislamu wenzangu,
kwetu ni kheri zaidi kuliko
mnavyodhania, zaidi
mnatuzidishia imani.
Alisema akirejea kauli yake
mbele ya Task Force.
Alisema, kufuatia kauli
yake hiyo, kuna afande
aliunga mkono, akisema
anachosema huyo Ustadhi
ni sahihi, akiwafafanulia
msimamo wa Waislamu wa
Libya na Palestina, ambaye
alidai amejifunza kutoka
kwao alipokuwa masomoni
Inaendelea Uk. 11
10
Inatoka Uk. 9
Makala
Kosa kulisilimu?
AN-NUUR
11
Makala
AN-NUUR
Mafundisho ya Quran
Fethullah-Gulen
NA wape habari njema
wale ambao wameamini
na wakatenda matendo
mema kwamba wana wao
mabustani inapita ndani
yake mito kila wanapopewa
humo katika matunda
chakula wanasema: Hiki
ndicho tulichopewa huko
nyuma na wanakiletewa
hali ya kuwa kinafanana na
wana wao humo wake walio
takaswa na wao humo ni
wenye kuishi mielele. [AlBararah 25]
Inatoka Uk. 9
katika nchi hizo kwa nyakati tofauti
kuwa Muislamu wa kweli hana
anachopoteza dhidi ya imani yake.
Akielezea aliyohojiwa, alisema
zaidi ilikuwa ni kuhusiana na harakati
zake kwa kujishughulisha katika
masuala ya Waislamu na Uislamu
akihutubia mara kwa mara kuwa
wanaonewa na kudhulumiwa.
Walinieleza kuwa naonekana
kila sehemu katika mikusanyiko
ya Waislamu na katika Misikiti
mbalimbali katika mikoa mbalimbali,
sasa wakataka kujua mimi ni dhehebu
gani, uwezo wa kuwepo huko kote na
upata wapi.
Niliwajibu kuwa uwezo wangu
unatokana na michango ya Waislamu
ndiyo inanifanya niwepo kila
mahali.Alisema.
Alisema, amebaini kuwa
Serikali haipendi kuona viongozi
wanaokubalika kwa Waislamu, hasa
wale ambao wanawaunganisha
Waislamu wawe kitu kimoja katika
jamii.
Akasema, hao ndio huandamwa
kwa kutafutiwa tuhuma zisizo za
kweli na ukitoka inakuwa bahati yako
na sio tatizo kwao kukuzuia kama
unavyoona hali ilivyo kwa Masheikh
wa UAMSHO na wengine.
Alisema, akiwa huko, pia aliulizwa
kuhusu Sheikh Hudhaifa, kwamba
anamfahamu vipi akadai, aliwajibu
kwa kuwaeleza kuwa huyo alikuwa
ni kiongozi wa Taasisi ya Kiislamu
lakini pia alikuwa mwalimu wake.
Lakini pia wakaniluliza
namfahamu vipi Sheikh Qassim
Mafuta, nikawaambia namjua kwa
sababu tumesoma chuo kimoja,
wakaniuliza vipi mawaidha yake,
nikawaambia kwa mazingira ya
sasa kwa Waislamu na Uislamu,
mawaidha yake hayana lengo la
kumtoa Muislamu katika dhulma
inayotukabili hivi sasa Waislamu.
ujuzi uliyokamilika.
Kwa hakika ni kwamba
sisi tunakitazama kila kitu
katika ujumla wake na kwa
sababu hiyo, tutabakia ndani
ya mipaka ya taathira na
makusudiwa yake wakati
wa kusimama kwetu na
uchambuzi na uundaji wa
kifikra. Ila kuna mambo
12
MASHAIRI/MAKALA
MTUKUFU RAMADHANI
Kwa jina lako Rahimu,naanza kusimuliya
Mola wetu Mkarimu,Ya Rabi nijaaliya
Nikadiri kukhitimu, haya nalokusudiya
Niusifu mwezi mwema,mtukufu Ramadhani
Rabi peleka salamu, zende kwa wetu Nabiya
Mtume wetu Adhimu, Muhamadi Hashimiya
Na Swahaba Akiramu, na Isilamu jamiya
Niusifu mwezi mwema, mtukufu Ramadhani
Ya Rabi tupe mwafaka, tufunge bila udhiya
Saumu yenye Baraka, kwako twaitaradhiya
Tuifunge huno mwaka, na mwakani kwa afiya
Tuufunge mwezi mwema, mtukufu Ramadhani
Karibu wetu mgeni, kwa hamu twakungojeya
Ulotukuka yakini, nuru ulivyo eneya
Mtukufu Ramadhani, karibu twakupokeya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mtakatifu adhimu, sote twakukongoweya
Mwezi uliye muhimu, Mola metutunukiya
Twafurahi Isilamu, kila pembe ya duniya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mtukufu mwezi mwema, wa sisi kunyenyekeya
Mwenye kuyatenda mema, bila ya kufanya riya
Tamswamehe Karima, madhambi kumfutiya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mwezi wa nyingi faida, metukuzwa na Jaliya
Mwezi mwema wa Ibada, na imani kutungiya
Huondoka zote shida, nafusi zikatuliya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mwezi huno wa maana, ameusifu Nabiya
Ni bora wajulikana, kwa kheri nyingi kungiya
Mwezi wa neema sana, baraka hutushukiya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mwezi mwema wa swiyamu, wa mema kujichumiya
Milango ya Jahanamu, Rahimu huifungiya
Na ya Janatu Naimu, wazi hutufunguliya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Ni mwezi wa Quraani, mwanzo kuteremkiya
Alipokuja pangoni, Jibirili kwa Nabiya
Ilikiuwa Ramadhan, wahayi alipokeya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mashetani makafiri, wawi wa kuharibiya
Hawawezi kuathiri, wasiwasi kututiya
Huwafungia Qahari, mbali wakatokomeya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Imo Lelatil Qadri, usiku huo kungiya
Bora sana mashuhuri, kuliko elifu moya
Miezi inayo jiri, ya taqwimu Hijiriya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Na hushuka Malaika, mbinguni wakatokeya
Kwa amri ya Rabuka, duniyani kufikiya
Amani hunawirika, hadi swabahi kungiya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Usiku mwema kipita, wakati huo kungiya
Na ukija kukukuta, Ibadani umengiya
Hakika utaipata, Rehema yake Jaliya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Haya basi Isilamu, mgeni ashaingiya
Natutimize saumu, tuifungeni kwa niya
Swala zote tuzikimu, za suna na faridhiya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Mashekhe na masharifu, wahimizeni jamiya
Hima tufungeni safu, Tarawehe kuqimiya
Tumlekee Raufu, kwa kuomba na kuliya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Darasani tuhimize, wenzetu kuhudhuriya
Kwa wakati tufulize, misikitini kungiya
Mawaidha tusikize, atatujazi Jaliya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Haya shime muombeni, Mola kumnyenyekeya
Quraani isomeni, kila siku juzu moya
Mukiweza ongezeni, muzidi kukaririya
Kongo mwezi wetu mwema, mtukufu Ramadhani
Na akhiri nimefika, beti nalokusudiya
Chache naloziandika, tosha kumi na tisiya
Namshukuru Rabuka, shairi limetimiya
La kuswifu mwezi mwema, mtukufu Ramadhani
Amina Rabi Dayani, Dua yetu kubaliya
Ya Ilahi tuauni, tuepushe na udhiya
Tuifunge Ramadhani, kwa furaha na afiya
Twaomba yake neema, mtukufu Ramadhani
SWALEH SUHEIL ABEID
AN-NUUR
Inatoka Uk. 10
na Wazungu Wakristo
na vibaraka wao wa
Kiafrika na kuwatupia
lawama Waarabu na
Waswahili Waislamu.
Hakuna shaka yoyote
kuwa uelekezaji wa
makombora yao wenye
siasa kali za udini
kuwalenga Waswahili
na Waarabu, ambao
ni Waislamu, kuwa
kumefanywa kwa
makusudi. Lengo hili
la kipropaganda za
siasa chafu za udini,
linakwenda vipi na
siasa rasmi za Tanzania
zinazojigamba kila leo
kuwa Tanzania haina
dini?
Haiwezekani
Serikali ya Tanzania
iachilie mambo haya
yasomeshwe katika
shule za Tanzania, ila
pawe na watu wenye
nguvu kubwa ya
kuilazimisha Serikali
kuwaachilia waendelee
kuyasomesha hayo ya
kipropaganda yenye
khatari kubwa kwa
nchi nzima ya Tanzania
katika siku za usoni.
La muhimu kabisa
ni kupigwa marufuku
usomeshaji wa
propaganda za aina
hii na vitabu vyote
vichomwe moto leo
kabla ya kesho.
Kusema tungoje
mpaka tuchapishe
vingine venye kuelezea
ukweli kamili, ni
kuendeleza usomeshaji
wa kipropaganda na
dhulma kubwa katika
nchi inayojinata kuwa
inaziheshimu dini zote
kisawasawa na haina
mapendeleo.
Wasiyoyazungumzia
wenye
siasa kali za udini
Tanzania
Maudhui haya ya
utumwa na biashara
yake, khasa kukhusiana
na Zanzibar, si mambo ya
kuyafanyia maskhara.
Kwa nini? Kwa sababu
ni moja katika jambo
lililotumiliwa vibaya
sana: Kwanza, na
Wamishinari na wafuasi
wao katika kuupiga
vita Uislamu katika
Afrika Mashariki.
Pili, kama tulivyotaja
kabla, wanasiasa fulani
Waislamu Zanzibar, pia
waliyatumilia vibaya
sana katika majukwaa ya
siasa na kuwanyooshea
vidole Waarabu peke
yao kama kwamba ni
Waarabu peke yao ndio
walioyafanya maovu
yote ya utumwa.
Zilikuwa ni siasa za
chuki zilizopindukia
m i p a k a . H a t i m a ye ,
tumeshuhudia
namna roho za watu
zilivyoangamizwa 1961
na kwa wingi zaidi 1964
na kuendelea.
Ni wajibu wetu
tuzinduane ili tuelewe
vizuri matokeo
yaliyowafikisha
Wa z a n z i b a r i h a p a
wa l i p o . I n a f a a p i a
tusomee zaidi ukweli
u l i v y o wa t a a r i k h i
inayokhusiana na
biashara ovu ya
utumwa ili kuelewa
yasiyokuwa ya kweli
wanayoyakhubiri na
k u ya a n d i k a we n ye
lengo la siasa kali za
udini zisizokhusiana
na mafunzo ya Yesu.
(Hawa wenye) lengo
la siasa zenye kutaka
kuwapiga vita Waislamu
na kuwakhasamisha
na Wakristo katika
Afrika Mashariki na
kwingineko. Na katika
hawa wamo pia wale
Waislamu wenye kupiga
debe bila ya kuujua
mchezo unaochezwa.
Au Wanajua, lakini
wanaona kuwa ni siasa
13
MAKALA
AN-NUUR
'VUNJAJUNGU', kama
dhana na kwa maana
ninayoikusudia katika
makala haya, ni istilahi
isiyo rasmi inayotokana na
maneno rasmi mawili ya
lugha yetu adhimu na aushi
ya Kiswahili ambayo ni
'vunja' na 'jungu'. Maneno
ambayo yamehulutishwa
a u k u a m b a t i s h wa a m a
kujumuishwa pamoja na
hatimaye kuzalisha istilahi
h i y o i s i y o r a s m i , k wa
muktadha wa makala haya,
ambayo ni 'Vunjajungu'.
Aghalabu matumizi ya
istilahi hii hushika kasi zaidi
katika kipindi hiki cha mwezi
wa nane ujulikanao kwa jina
la Shaaban kwa mujibu wa
Kalenda ya Kiislaamu. Kwa
maneno mengine, istilahi hii
hutamkwa na husikika zaidi
katika mwezi huu kuliko
mwezi mwingine wowote
katika mwaka kupitia
matangazo yarushwayo
na vyombo vya habari vya
umma na vya watu binafsi
na katika mazungumzo
ya kawaida ya baadhi ya
wanajamii.
Ni nadra kusikia neno
hili likitumika au kutumiwa
katika miezi mingine ya
mwaka kama vile Muharram,
Swafar, Rajab, Ramadhaan,
shawwaal kwa kutaja
michache; na pale inapotokea
kutumiwa au kutumika
kwake katika miezi hiyo
niliyoitaja au hata katika ile
mingine ambayo sijaitaja
mbali na Shaaban, matumizi
hayo aghalabu hurejelea ama
kilichojiri au kilichotarajiwa
kujiri katika kipindi cha
mwezi wa Shaaban kwa
kukifungamanisha au
kukihusisha na dhana
yenyewe ya 'Vunjajungu'.
Naam, tukirejelea mada
ya msingi ya makala haya
ya leo neno 'vunjajungu'
japo linaweza; kwa maana
ya kilugha au ya msingi
wa maneno yaliyotumika
kuunda neno hilo; kufasiliwa
kwa maana ya 'haribu chungu
kikubwa' au 'uharibifu wa
chungu kikubwa' ingawa
hii si maana tunayoikusudia
katika makala haya.
Aidha, maana rasmi ya
kikamusi neno 'vunjajungu'
kama kidahizo limefasiliwa
kuwa ni mdudu aina ya panzi
mwenye kiuno chembamba
na macho makubwa na hula
wadudu wadogo.
Maana ninayoikusudia
katika makala haya, si maana
hiyo ya msingi ya neno husika
kama ilivyodokezwa hapo
juu na katika fasili ya kabla
yake bali ni ile ya kimuktadha
au ya kimazingira ambamo
neno hilo hutumika au
hutumiwa hususan katika
kipindi hiki tulichomo.
'Karibuni au Mnakaribishwa
katika disko la 'vunjajungu'
la kukata na shoka!'au 'Njoo
uvunje jungu la mwaka nasi
hadi majogoo!' na kadhalika,
ni sehemu tu ya ya kaulimbiu chache kati ya nyingi
zitumikazo au zitumiwazo
na vyombo vya habari na
magari ya matangazo katika
kuwashajiisha, aina ile ya
Waislamu niliyodokeza huko
nyuma, kushiriki katika
mradi wao huo haramu!
Ni katika kipindi hiki,
kwa machombezo ya
matangazo kama hayo,
ndipo ambapo baadhi ya
Waislamu wasiojitambua
hunasa kirahisi mtego huu
k wa k u g h u r u r i k a k wa
k u j i i n g i z a n a h a t i m a ye
kuzama katika laghwu na
mambo mengine kedekede
ya hawaa nafsi ikiwa ni
pamoja kujiingiza katika
madisko ya 'vunjajungu',
uzinzi pamoja na ulevi kwa
kutaja machache.
Itoshe tu kusema
kwamba maasi au maovu
yanayotendwa kipindi hiki
si hayo tu bali nimeyataja
hayo matatu kwa sababu
aghalabu ndio hukithiri kwa
kiwango kikubwa katika
utukiaji au utendekaji wake
katika kipindi hiki cha
kuelekea mwezi Mtukufu
wa Ramadhani.
Naam, wafungaji-tarajali
wa s wa u m u ya m w e z i
Mtukufu wa Ramadhani
wanaotanguliza mambo
ya hawaa nafsi kama hayo
yaliyodokezwa hapo juu na
mithili yake, ni vigumu sana
kuufurahia ujio wa mwezi
Mtukufu wa Ramadhani;
japo vinywa vyao vinaweza
Mafundisho ya Quran
Inatoka Uk. 11
akhera kwa akili ya akhera.
Wa k a t i h u o u t a w e z a
kufahamu uhusiano kati ya
kusema Subhanallah na
kati ya kuyala matunda ya
peponi, kwa sababu kila kitu
kitapita huko.
Kufuatana na kanuni za
ghaibu na za nyuma ya tabia
(Metaphysical), tunaona na
tutafahamu kwa uwazi wote,
uhusiano wa kisababu kati
ya malipo na neema ambazo
zinapatikana huko na kati ya
kutenda hapa duniani.
Kanuni za uhakika za
Kifizikia zinazopatikana hapa
haziishii hapa, zinafanya
kazi huko. Kwa mfano,
anasema Mtume (s.a.w.)
kwamba swala zetu zitakuwa
mliwazaji wetu na rafiki yetu
katika makaburi yetu na
kwamba mtu ataingia peponi
kupitia milango yake minane
ambayo ni mbalimbali na
kwamba Quran itasimama
ili iwe muombezi wa msomaji
wake.
Hakika neema yoyote ile,
neema hiyo ama ni malipo
ya matendo fulani au ni
kusimama kwa malipo hayo
au ni kwamba uwezesho wa
milele huko. Ni mashuke ya
mbegu za matendo mema
hapa duniani.
Kwa sababu hiyo, hayo
mawili kwa mazingatio haya,
yanafanana katika undani
wake. Ama kwa mazingatio
ya vipeo vya peponi, pana
tofauti kubwa kati ya mawili
hayo. Inakunjuka dunia na
inavuka, kwa sababu moja
lau ni matunda ya uwezo.
Moja lao linabeba sifa ya
umilele na jingine ni la muda.
Vipeo vya ladha ya milele na
jingine vipeo vya mwili. Moja
lao ni wema kwa ngazi ya
jicho la yakini na jingine,
upole wa Mwenyezi Mungu
katika kilele cha Haki ya
yakini.
(Imenukuliwa kutoka
Kitabu: Miyangaza ya Quran
katika mbingu ya hisia,
cha Muhammad Fethullah
Gullen kilichotafsiriwa
kwa Kiswahili na Sheikh
Suleiman Amran Kilemile)
14
Makala
-metaphysical ikiwa
falsafa ya kuchunguza
chanzo cha uhai na
maarifa, udhanifu,
aliathiriwa pakubwa
na kazi za Aristotle
na Plato. Alijisomesha
vya kutosha kuweza
kuelewa juu ya utanzu
wa uhai. Inakadiriwa
a l i t u m i a m u d a wa
mwaka na nusu
akitaabika katika
k u t a k a u e l e wa j u u
ya hili. Huko mbele
tutakuja kuona namna
alivyokuja kuyakamata
ya Aristotle na wengine
kueleza kuwa alikuwa
na imani dhaifu na hata
wengine kufika kusema
alikuwa murtad.
Nitajaribu kuziweka
hoja za wasomi
mbalimbali juu yake
na kufahamu ukweli
wa imani yake ulikuwa
vipi?
Katika falsafa, Ibn
Sina alijaribu kufanya
kila aliwezalo kuiweka
falsafa iende na
mwenendo mzima wa
dini ya Kiislamu na
hapa ndipo kina Imam
Ghazali walipokuwa
hawaafikiani nae.
Maisha yake katika
k u m b u k u m b u
zilizoandikwa na
wanafunzi wake
kama Wahid Juzjani,
kuna maandiko
yanaonyesha namna
alivyokuwa akijadiliana
na wanafunzi wake alMubahathat na hata
yale maandishi ya Ibn
al-Qiftis Tarikh alhukama juu ya historia
ya falsafa. Aidha Zahir
al-Din Bayhaqis katika
Tatimmat Siwan alhikma wamemuweka
wazi
alikuwa
anakwendaje na
ulimwengu wa falsafa.
M s o m i
w a
U l a ya
G u t a s
anatutahadharisha
kuwa ili kuijua falsafa
aizungumzayo Ibn Sina,
inabidi tujifunze falsafa
kisha ndio tumsome na
kumtolea hoja. Farabi
alimvutia mno kwani
kumsoma Al-Farabi
aliweza kuwaelewa
akina Aristotle na
kina Plato na kuweza
kujenga hoja zake
Fatilia
kuandama kwa Mwezi
Leo Ijumaa ni tarehe 24 Shaaban 1436
Ibn Sina
IBN Sina
katika metafizikia
Babake Ibn Sina
a l i k u wa m s o m i n a
inadhaniwa alikuwa
mwenye kufwata
madhehebu ya Ismaili.
Mzee wake huyu
alikuwa mtaalamu kwa
hio alipewa kibarua
cha kuwa Gavana
wa Samanid. Akiwa
na umri mdogo, Ibn
Sina alikuwa na kiu ya
kusoma kwa hio aliomba
ahame na familia yake
na kuelekea Bukhara
na alipofika hapo
alisoma na kufwata
madhebebu ya Abu
Hanifa (Hanafi) chini
ya mwalimu Ismaiil
Zahid. Aidha alisoma
juu ya utibabu kwa
walimu mbalimbali.
Samanid inaaminika
kuwa ilikuwa na
maktaba iliojaza
vitabu vya kila aina na
hapo ndipo Ibn Sina
akenda kujisomea juu
ya taaluma ya utibabu
na kuwa anajisomesha
mwenyewe na kujaribu
kuyatumia yale
alioyasoma.
Alianza kujulikana
alipotimu umri wa
miaka 18 kutokana na
kuwa ashabobea katika
taaluma mbalimbali
ikiwemo ya utabibu na
hilo likamfanyia wepesi
kuweza kupata kibarua
katika mahkama ya
Samanind ikiwa chini
ya kiongozi Nuh
ibn Mansur na hapo
alikuwa akifanya kazi
ya kutibu wagonjwa.
Alipofariki baba
ya k e a l i p a n d i s h wa
cheo lakini Samanid
h a k u m u w e k a
aliondoka na kuhamia
Gurganj iliopo
K h a wa r z a m , k i s h a
akarudi Bukhara katika
mwaka wa 999 ambako
alikutana na aliokuja
k u wa m wa n a f u n z i
wake Juzjani. Baada
ya m wa k a a k a f i k a
Buyid na kupata kazi
ya utabibu na kuandika
kitabu kwa lugha ya
Kifursi Danishnama-yi
AlaI ikiwa ni kitabu
cha maarifa.
Wa s o m i
wa
nyakati hizo walipata
misukosuko mingi
kutokana na kupewa
kazi na watawala
na
watawala
wa n a p o b a d i l i k a a u
kuondolewa na wao
hujikuta matatani. Ibn
Sina katika maisha
yake ya mji wa
Hamdan kulikuwa na
mapambano makali
baina ya dola ya Isfahan
na Hamdan. Hapa Ibn
Sina akufungwa baada
ya Isfahan kushinda Ibn
Sina alibaki Hamdan
kwa muda lakini
baadaye alikimbilia
Isfahan. Kwa muda
wa miaka 10 hadi 12,
Ibn Sina alibaki katika
utumishi wa Amiri wa
Isfahan, Abu Yafar
Alaa ad-Dawlah akiwa
daktari wake.
Somo la uanzilishi
ndio lilomsumbua
sana Ibn Sina na kufika
kusema kuwa dunia
haina muumba na haina
mwanzo, hapo alikuja
kugombana na wasomi
we n g i n e k u m we k a
kuwa murtad. Lakini
juu ya hayo, Ibn
Sina baadaye alikuja
kuandika kuthibitisha
kukuwepo kwa Mungu,
huku kulimchukua
katika mkondo mmoja
kisha ukamvuta katika
mkondo mwengine, juu
ya hayo bado wasomi wa
wakati wake na wakati
huu bado wanamuona
Ibn Sina kateleza na
kumhesabu ndani ya
hukumu zao kuwa ni
Murtad na kumuelezea
zaidi kuwa akipenda
pombe na mabibi.
Starehe hizi
zilimfanya apatwe na
ugonjwa wa msokoto
wa t u m b o a m b a y o
inafikiriwa ndio
aliomfanya aage dunia.
Hapa ndipo nitajaribu
kupatizama zaidi
kuwa jee tunaweza
kumhukumu mja
au mja uhukumiwa
na Allah? Ibn Sina
katika nyakati tafauti
alishauriwa aache anasa
AN-NUUR
na kila akikatazwa
kushikamana na anasa
akisema :
Napendelea maisha
mafupi ya upana kuliko
membamba yenye
urefu.
M a r a d h i
ya l i v y o m z i d i h u k u
akiwa kitandani alijuta,
a k a t o a v i t u v ya k e
kwa masikini, akatoa
vitu alivyopata kwa
Jee Unajua?
1.
Maji yaliokuwa sio salama yanauwa watoto
wafikao 200 kila saa duniani kote.
2. Takwimu za duniani zinaonyesha kuwa
wanawake wanakuwa na umri mrefu kuliko
wanaume, wastani wa umri wenye kikomo kwa
wanawake ni miaka 69 na kwa wanaume ni miaka
64.
3. China ndio nchi yenye idadi kubwa ya
watu, ikifwatiwa na India. China ina idaidi ya watu
wafikao bilioni 1.35 huku India ikiwa na idadi ya
watu wafikao bilioni 1.21. Nchi ya China na India
kwa pamoja ukizichanganya zina idadi ya watu
wafikao asilimia 37% ya wakazi wote waliopo
duniani.
4. Inasemekana vita vilivyopiganwa kwa
muda mfupi vilipiganwa katika mwaka wa 1896
wakati Ufalme wa Zanzibar uliposalimu amri kati
yake na mkoloni Muiengereza, vita baina ya pande
mbili hizo vilichukua dakika 38.
5. Mabomu yaliozikwa kwenye ardhi
huchukua roho za watu 24,000 kila mwaka.
6. Nchi moja peke yake duniani isiokuwa na
jeshi wala matumizi ya kijeshi nchi hio ni Iceland.
7. Mabara ya Asia na Pacific ndio yanaongoza
kwa utapio mlo ikiwa na idadi ifikiayo watu milioni
553 na nchi ambazo zinaongoza ni Indonesia na
Philippines.
8. Katika nchi zilizo kusini ya jangwa la
Sahara ina idadi ya watu wafikiao idadi ya milioni
227 wapo katika hali ya kukosa chakula zikiwemo
nchi za Ethopia, Niger na Mali.
9. Wasiwasi na kuogopa ni khulqa ya
mwanadamu, hata mwanadamu akiwa ana ushujaa
wa aina gani huwa ana kitu anaogopa, kwa mfano
Napoleon, Mussolini na Hitler walikuwa na
ugonjwa ujulikanao kwa kimombo Ailurophobia
ikiwa ni khofu ya kuogopa paka.
10. Inaaminika kuwa mwanadamu anatumia
asilimia 33% ya maisha yake akiwa amelala, hio ni
sawa na miaka 25.
M
F
A
2
E
F
G
N
A
N
A
U
D
9
A
N
H
D
Y
T
K
T
R
O
O
K
A
I
L
A
K
A
U
I
E
I
P
O
A
R
A
R
1:3
3
U
R
A
T
A
S
I
A
0
P
O
N
A
U
W
M
N
S
R
S
H
A
F
L
E
A
A
D
D
F
O
T
U
Q
H
D
D
3
3
Y
U
I
O
A
E
I
A
1
0
Z
C
B
I
D
P
N
K
F
C
V
B
N
M
R
H
A
U
1.
Taja Sura inayoelezea mwezi wa Ramadhani.
2.
Vita gani Waislamu walipigana katika mwezi
wa Ramadhan.
3.
Ratio baina ya Waislamu na Makafiri katika
vita vya mwanzo waliopigana Waislamu ilikuwa 1:3,
1:6, 2:9.
4.
Sala gani inayosaliwa katika mwezi wa
Ramadhani tu.
5.
Katika mwezi wa Ramadhan kuna milo miwili
inatakiwa kuliwa moja jua linapokuchwa na mwengine
kabla ya kuingia alfajiri, milo hio ni :,
6.
Ramadhani una usiku mtukufu unaitwaje?
7.
Mwezi wa Hijra huandama biana ya na
8.
K u f u n g a k wa m w e z i wa R a m a d h a n
kulifaradhishwa katika mji gani?
9.
Asio balighi ana wajibika kufunga? Ndio au
Hapana.
10. Ramadhani humtakasa mja ..
15
TANGAZO
AN-NUUR
16
MAKALA
AN-NUUR
RA I S J a k a ya M r i s h o
Kikwete.
17
Na Ben Rijal
NENO mazingira
limechukua nafasi kubwa
katika maisha yetu ya kila
siku, mazingira yamepewa
umuhimu mkubwa
kutokana na maisha
yetu yote yanategemea
mazingira na kila mazingira
yakichafuka na kuharibika
mwanadamu na viumbe
m b a l i m b a l i v i n a k u wa
katika matatizo na shida.
Tujiulize kwanza nini
m a z i n g i r a ? M a i s h a ya
viumbe na mwahali
wanapopatikana tutasema
mazingira au tutasema
mazingira ni maingiliano
baina ya viumbe hai na vile
vilivyowazunguka yaani vitu
vilivyokuwa sio hai, ikiwa
udongo, mchanga, milima,
mazingira ni viumbe hai na
yale yote yaliowazunguka
n.k.
Mazingira yanachafuliwa
kwa kila namna mfano, ukataji
wa misitu, umwagaji wa
maji machafu kwenye mito,
maziwa na bahari, utowaji
wa moshi usiochujwa kutoka
viwandani na kuelekea
angani, kunyesha kwa mvua
ya tindi kali, kutosafishwa
kwa maji machafu na
kuachiwa kuingia katika
bahari na mito, kuvunjwa
kwa matumbawe kwa njia
mbalimbali ikiwa pamoja na
kutumia uvuvi haramu wa
kutumia mabomu n.k.
Uislamu unafunza utunzaji
wa mazingira na uhifadhi wa
mazingira kupitia kitabu
kitukufu Quran na Hadithi
za Mtume SAW.
Quran inatufunza kuwa
maisha yote yapo katika
uwiyano, mizani na Allah
amejaalia uwiyano huo,
huku mwanadamu anakuwa
mstari wa mbele katika
kuyachafua mazingira.
Kwa hakika Sisi
tumekiumba kila kitu kwa
kipimo. (54:49).
Allah amejalia kila kitu
kuwemo kwenye mizani na
mizani hio haina shaka na
ni yeye Allah aliokamilisha
kuiweka dunia katika mizani
iliokamilika.
Mwenyezi Mungu
anajua mimba abebayo
kila mwanamke, na
kinacho punguka na kuzidi
matumboni. Na kila kitu
kwake ni kwa kipimo. (13:8).
Katika vyote alivyoumba
Allah na kumleta duniani
mwanadamu, Allah
aliikamilisha mizani.
Na mbingu ameziinua,
na ameweka mizani. (55:7).
Tunapoiangalia dunia,
tunakuta kuna vitu vya
kila aina na kila kimoja
kinakuwepo kutokana na
kushikamana na kengine.
Maisha yetu yanategemea
jua kwa kuwa jua ndio
linaungana na majani katika
miti na kufanya chakula
na wanadamu na viumbe
mbalimbali kutegemea
vyakula kutokana na miti,
ingawa kuna wanyama hawali
majani lakini wanakula wale
wanyama wanaokula majani.
Hapa unaiona dhana nzima
ya kitu kimoja kuungana
na kutegemeana na kitu
chengine. Maisha yote
yanashikana na sehemu moja
ya mazingira. Allah ndio
yeye mwenye kuviendesha
na hakuna kitu kimoja
MAKALA
AN-NUUR
Mazingira yanayopendeza
Mazingira yalioharibiwa
kinachojiendea wenyewe bila
ya uwezo wa Allah. Hapa mja
anatakiwa kuwa mwangalifu
kwa kujuwa kaumbwa na
aliomuumba ameviweka
vitu tuvitumie kama vile
alivyoviweka katika mizani
yake.
Je! Huoni kwamba
Mwenyezi Mungu
vinamtakasa vilivyomo
katika mbingu na ardhi, na
ndege wakikunjua mbawa
zao? Kila mmoja amekwisha
jua Sala yake na namna
ya kumtakasa kwake. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kuyajua wayatendayo.
(24:41).
Tu j u w e k u w a A l l a h
ameumba kila kitu kiwe
alama na maana kamili na
kuweza kufahamika utukufu
wake na sababu ya kuviumba
vitu hivyo.
Ambaye amekufanyieni
ardhi kuwa tandiko, na
akakupitishieni humo njia,
na akakuteremshieni kutoka
mbinguni maji. Na kwa hayo
tukatoa namna mbalimbali za
mimea. (20:53).
Kuleni, na mchunge
wanyama wenu. Hakika
katika hayo zipo ishara kwa
wenye akili. (20:54)
Allah ameiumba dunia
sio kwa bahati nasibu au
kwa kukosea, bali ameiumba
dunia tupate mazingira yalio
salama na yalio endelevu.
Na hatukuziumba
mbingu na ardhi na
vilivyomo baina yake kwa
mchezo. (44:38)
Hatukuviumba hivyo ila
kwa Haki, lakini wengi wao
hawajui. (44:39)
Quran inatufahamisha
na inatuongoza kuelewa
kuwa Allah ameviumba
a l i v y o v i u m b a k u wa n a
thamani ndani yake na hivyo
alivyoviumba ameviumba
viweze kumtumikia
kwa kuwa ni yeye Allah
ameviweka kuwa kila
kimoja kati ya alivyoviumba
viwe vinategemeyana na
kisha baada ya kuviumba
mwishowe hutoweka, kisha
akatoa vitu kutokana na
nje ya uhai kisha vitu hivyo
vikawa ndio uhai autegemayo
mwanadamu.
Hakika Mwenyezi Mungu
ndiye mpasuaji mbegu na
kokwa, zikachipua. Humtoa
aliye hai kutoka maiti, naye
ni mtoaji maiti kutokana
na aliye hai. Huyo ndiye
Mwenyezi Mungu. Basi vipi
mnageuzwa? (6:95)
Allah ameumba mauti na
atampa jaza yule ambaye
kati ya wanadamu akatenda
mema. Allah ameumba
uhai na mauti kwa sababu
zake na ufisadi autendao
mwanadamu afahamu
kuwa katika maisha ya
baadaye hatokuwa katika
waliofuzu. Kwa mantiki hii
mwanadamu anatakiwa
mara zote awe mwangalifu
katika maisha yake ya kila
siku kwa viumbe vyengine
na rasilimali ziliomo kwenye
mazingira anayoishi.
AMETUKUKA ambaye
mkononi mwake umo
Ufalme wote; na Yeye ni
Mwenye uweza juu ya kila
kitu. (67:1).
18
Na Alhaj Abdallah
Tambaza
MWEZI kama huu miaka
minne iliyopita, Rais Jakaya
Kikwete ilibidi akatishe
ziara nchini Botswana na
kurudi nyumbani kuongoza
maelfu ya waombolezaji
jijini Dar es Salaam katika
mazishi ya mmoja wa watu
mashuhuri kupata kutokea
katika ukanda wa Afrika
Mashariki na Kati. Alikuwa
bingwa wa usomaji Quran;
bingwa wa unajimu; bingwa
wa tiba asilia; mtaalamu wa
nyota (horoscope) na pia
mwanasiasa nguli. Endelea
na sehemu ya tatu ya makala
haya.....
Katika utabiri, alianzia
kwenye kutabiri mpira kabla
ya kutoa utabiri wa nyota
magazetini, wakati huo
ambapo hakukuwa na mtu
mwengine aliyeijua fani hiyo
hapa nchini.
Kwa mara ya kwanza,
tulimshuhudia Sheikh
Yahya akitabiri mpira katika
m a s h i n d a n o m a k u b wa
ya Sunlight Cup (baadaye
Taifa Cup) yaliyokuwa
yakishindanisha timu za
mikoa yote ya Tanzania Bara.
Vipeperushi vyake
alivyokuwa akivitawanya
k a b l a ya m c h e z o p a l e
uwanja wa Karume, si tu
kwamba vilionyesha ni
timu gani itaibuka mshindi,
bali pia nambari za
wachezaji na dakika mabao
yatakapofungwa.
Nakumbuka mwaka
mmoja kwenye miaka
ya 1960s, mashindano ya
Gossage (sasa Challenge
Cup) kwa nchi za Afrika
M a s h a r i k i , ya l i f a n y i k a
jijini Dar es Salaam. Sheikh
alikuwa akitoa utabiri wa
michezo ile kadri ilivyokuwa
inaendelea.
Siku moja kulikuwa na
mchezo baina ya Kenya
na Uganda na hapo
aliitabiria timu ya Kenya
kuibuka mshindi akitaja pia
dakika na idadi ya mabao
yatakayopatikana.
Alibashiri pia wachezaji
wa Kenya Joe Kadenge,
Chege Ouma, Livingstone
Madegwa na John Ambani
n d i o w a t a k a o n g a r a
mchezoni.
Wa t u wa K e n ya ,
wakiwamo viongozi wa nchi
ile, walianza kumfuatilia
k wa k a r i b u ; h a s a p a l e
alipotabiri Kenya ndiyo
wa t a k a o c h u k u a k o m b e
mwisho wa mashindano.
Utabiri ulipotimia;
aliletewa mwaliko maalumu
na Serikali ya Kenya kwenda
Nairobi kwenye sherehe za
ushindi.
Huo ukawa ndio mwanzo
wa Sheikh Yahya kufungua
ofisi katika jiji la Nairobi,
wa t e j a wa k e wa k u b wa
wakiwa wanasiasa na
viongozi mashuhuri nchini
Kenya.
Kadri siku zilivyoenda,
Sheikh alipanuka na
a k a wa n a o f i s i k u b wa
KUMBUKUMBU
AN-NUUR
s e h e m u t a k a t i f u h a ya
nenda zako,alisema.
Niliondoka zangu na
kuyaacha nyuma matabiri
yale ya Sheikh Yahya. Wakati
huo sikuwa najua nchi au
mji wowote zaidi ya Nairobi
na Dar es Salaam kwetu
nilikozaliwa.
Miji kama vile Tanga na
Morogoro kwangu ilikuwa
ni miji ya mbali tu. Lakini
miaka kadhaa baadaye,
nilikuja kugundua tayari
nimeshatembelea sehemu
nyingi duniani na hivyo
kujiuliza, ala kumbe utabiri
ule umetimia!
Kwa schorlaship kutoka
ICAO, yaani Shirika la
Umoja wa Mataifa la Usafiri
wa A n g a , m wa k a 1 9 8 4
nilipelekwa katika Chuo cha
Usalama wa Anga (LENAC)
kule Toulouse, Ufaransa.
Nilipokuwa huko, nilipata
fursa iliyoniwezesha kufika
kwenye kituo kikubwa
cha setelilaiti duniani
kilichojulika kama SARSATCORPAS (Search and Rescue
Satelite).
Nilipanda pia ule mnara
wa kihistoria jijini Paris,
unaoitwa le Tourefel na pia
kuyashuhudia maonyesho
m a k u b wa ya m a d e g e
duniani ya Le Burget Air
Show.
Kama hiyo haitoshi,
mwaka 1988 mwandishi
alipata nafasi ya kujiunga na
Chuo Kikuu cha California
pale Los Angeles, na hivyo
kufika sehemu nyingi
maarufu kule California
ikiwamo Hollywood,
Beverly Hills, Las Vegas
pamoja na DisneyLand.
Nilikuwapo pia pale Rose
Bowl Stadium, Pasedina
kushuhudia fainali za
kihistoria za Kombe la Dunia
baina ya Brazil na Italy na
kumwona Robberto Baggio
akipaisha juu penati.
Inatoka Uk. 17
Ikiwa Waislamu tutaweza
kushikana na upandaji
wa miti, tutaiokoa dunia
pakubwa na janga la
mabadiliko ya tabianchi
kutokana na idadi yetu ya
watu bilioni 1.2 robo ya
idadi hii ikishikamana na
upandaji wa miti tutakuwa
tumeitendea haki dunia.
Khalifa wa Nne katika
Uislamu Syd Ali ibn AbiTalib katika kuuhisha maisha
na kujali mazingira aliwataka
waumini waungane naye
katika kuihuisha ardhi
i l i o k u wa h a i z a l i s h i n a
k u i g e u z a k u wa y e n y e
kuzalisha na kuwa endelevu.
Katika kulifanikisha
hilo alisema maneno haya
Shiriki kwa furaha ikiwa
wewe ni mwenye kufaidika
na matumizi ya rasilimali,
usiwe mwenye kufisidi
kuwa mwenye kupanda
vipando wala usiwe mwenye
kuangamiza.
Uislamu umesisitiza
p a k u b wa m a t u m i z i ya
rasilimali na mazingira
19
MAMBO
matatu
yanapendekezwa kwa
mwenye kufunga: La
Kwanza, kuharakisha
kufuturu, baada ya
k u h a k i k i s h a k u wa j u a
lishatua. Hii ni kwa qauli ya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
" Wa t u h a w a t a a c h a
kuwa katika kheri wakiwa
wanaharakisha kufuturu".
(Imehadithiwa na Al
Sheikhan).
Na ameeleza Ibnu Hibbaan
kwamba:
"Alikuwa (Mtume wetu
Mpenzi s.a.w.) akiwa
kafunga, hasali mpaka
apelekewe tende mbichi
au maji, ale (tende-mbichi)
au anywe maji, ikiwa siku
za baridi; hasali mpaka
tumpelekee tende au maji".
Kutokana na Hadithi
hii, inapendekezwa siku za
baridi kufungua kinywa kwa
tende au maji, na siku za joto
kwa tende-mbichi au maji.
Hivi ni kwa vile kitu kitamu
kinatia nguvu mwilini na
maji yanasafisha mwili.
Na amesema Al Rauyany:
"Asipopata tende, basi kwa
kitu kitamu chochote kwani
Saumu inapunguza nguvu
za macho, na tende hurejesha
nguvu za macho, basi kitu
kitamu huwa mahala pa
tende".
La Pili, kuakhirisha
(kuchelewesha) kula daku.
Hivi ni kwa Hadithi ya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
"Hakika kuakhirisha daku
ni miongoni mwa sunna za
Mitume". (Imehadithiwa na
Ibnu Hibbaan).
Na imepokewa pia
kwamba:
"Hautaacha umati wangu
kuwa katika kheri wakiwa
wanaharakisha kufuturu na
wanaakhirisha kula daku".
(Imehadithiwa na Ahmad).
Hikma ya kuakhirisha
kula daku ni kumpa mtu
anaefunga nguvu za kufanya
ibada, katika kutafuta riziki
na ibada nyengine za kutwa.
Na Mussa Ame
RAMADHAN huingia
kwa kuonekana mwezi 29
Shaaban au kumaliza siku
thelathini za Shaaban.
Amesimulia Ibnu Umar
(r.a) kutoka kwa Mtume
(s.a.w) amesema, Msifunge
mpaka uonekane mwezi na
msifungue mpaka uonekane
mwezi (Muttafaq SB 1906
SM 1080).
Hadithi Muttafaq ni ile
iliyokubaliwa na Bukhari
kwa kuwemo katika Sahihi
Bukhari (SB) na Muslim
kwa kuwemo kwenye Sahihi
Muslim. (SM).
Amesimulia Abii Hurayra
(r.a) amesema Mtume (s.aw.),
Fungeni kwa kuonekana
mwezi na fungueni kwa
kuonekana mwezi, na kukiwa
na mawingu timizeni siku
thelathini (SM1081).
Amesema Ibnu Hajari
Asqalaany katika sherhe ya
Makala
AN-NUUR
na siku ya 'Idi-l-adh-ha".
Kufunga katika siku
mbili hizi ni haraam, sawa
ikiwa ni Saumu ya fardhi,
au ya sunna, au ya kafara,
au ya nadhiri. Vilevile
imeharamishwa kufunga
siku za (tashriiq), nazo ni
siku tatu baada ya siku ya
kuchinja. Siku ya kuchinja
ni mwezi kumi wa mfunguo
tatu. Kwa hivyo siku za
"tashriiq" ni mwezi kumi na
moja, kumi na mbili na kumi
na tatu wa mfunguo tatu.
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.
amekataza kufungu siku
hizi kwa sababu hizi ni siku
za furaha (siku za idi), siku
za kula, kunywa na kuzidi
kumtaja na kumshukuru
Mwenyezi Mungu Mtukufu
kwa nema zake juu yetu.
Kwa yule mtu aliefanya
(Hija tamatu'i) ni mtu
kufanya 'Umra kisha akatoka
katika ihraam akapumzika,
kisha akahirimia Hija. Huyu
anatakiwa atoe sadaqa kwa
kuchinja, akiwa hana uwezo
wa kuchinja afunge siku
tatu wakati yuko Makka na
siku saba akirejea nchini
kwao. Yeye inajuzu kufunga
katika hizi siku za tashriiq
kama ilivyokuja kwa Qauli ya
Mwenyezi Mungu Mtukufu:
", basi mwenye
kujistarehesha kwa kufanya
Umra kisha ndio akahiji,
basi achinje mnyama aliye
mwepesi kumpata. Na asiye
pata, afunge siku tatu katika
Hija na siku saba mtakapo
rudi, hizi ni kumi kaamili
". (Al Baqara : 196).
Na katika Hadithi za Imam
Al Bukhary r.a. kutokana na
Hadithi ya Sayyidah 'Aisha,
Mama wa Waumini r.a. na
Ibni 'Amri r.a. wamesema:
"Haikuruhusiwa kwenye
siku za tashriiq kufunga
isipokuwa kwa yule aliyekosa
mnyama wa kuchinja".
Kuingia Ramadhani
Bukhari hadithi (SB 19061911).
Wa m e k h i t a l i f i a n a
Maulamaa kuhusu watu
wa nchi za mbali kufunga,
kwa kufuata muandamo wa
nchi nyengine Kundi moja
limesema kila nchi wauone
mwezi wa mji wao nao ni
Kassim, Ikrimah, Salim na
Ishaaq. Na ameitoa hadithi
Imamu Tirmidhy ya kisa cha
Qurayb inayotoa ushahidi
wa hoja hiyo, pale Abdillah
Ibni Abbas(r.a) alipokataa
mwandamo wa mwezi wa
Sham yeye akiwa Madina,
na akasema hivi ndivyo
tulivyoamrishwa (SM1087
D 2332 T 693).
Na kundi jengine ni
kundi la Malik , Ahmad bin
Hambal, baadhi ya watu
wa Shafiy, Imaam Qurtubiy
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Tafrani Segerea
AN-NUUR
E-mail:info@hajjtrust.or.tz
Na Bakari Mwakangwale
K AT I K A h a l i i s i y o ya
kawaida, mtuhumiwa wa
kesi ya Ugaidi, Ustadh
Salum Ally, amepanda
juu ya mti mrefu uliopo
eneo la ndani ya gereza la
Segerea, Jijini Dar es Salaa
na kugoma kushuka.
Haikuweza kufahamika
mara moja iwapo lengo la
mtuhumiwa huyo lilikuwa
kujirusha afe au nini.
Hata hivyo alipoulizwa
alisema kuwa haoni tena
sababu ya kuishi katika
mgongo wa ardhi kutokana
na mambo machafu
aliyofanyiwa akiwa
mikononi mwa vyombo vya
Dola.
Mtuhumiwa huyo aliye
m s h i t a k i wa n a m b a 1 4 ,
amechukua uamuzi huo
Jumanne wiki hii majira ya
mchana na kuleta tafrani
ndani na nje ya gereza hilo
kufuatia taarifa kuenea
kupitia simu na mitandao
ya kijamii.
Akiongea kwa njia ya
simu akiwa eneo la tukio
hilo, Katibu wa Kamati
ya M a a f a ya S h u r a ya
Maimamu, Ustadhi Ally
Mbaruku, alisema juhudi
za kumshawishi ashuke
z i l i g o n g a m wa m b a n a
kwamba mpaka anaondoka
eneo hilo majira ya saa 12,
jioni alikuwa bado hajashuka.
Ust. Mbaruku, alisema
u s h a w i s h i wa k u m s i h i
ashuke kutoka juu ya mti
s i k u h i y o ya J u m a n n e ,
ulishindikana na kuamua
kumuacha na kusubiri
majaliwa yake atakapoamua
mwenyewe.
Naye mjumbe wa Kamati
hiyo, Ust. Hassan Kayagali,
alisema, walifika gerezani
hapo katika kawaida yao
ya kuwapelekea mahitaji
Waislamu hao, lakini hali
waliyoikuta hapo iliwastua.
Tulipofika tuliambiwa
mmoja kati yao, Salum Ally
Salum, ameamua kupanda
juu ya mti uliopo ndani ya
eneo la Gereza la Segerea, hali
ambayo imewastua na juhudi
za kumshusha kwa kutumia
nasaha zimeshindikana.
Alisema Ust. Kayagali.
Alisema, mtuhumiwa
huyo, amekuwa akisema
kuwa hana haja ya kuendelea
kuishi katika mgongo wa
ardhi kutokana na mambo
aliyofanyiwa na namna kesi
yao inavyocheleweshwa bila
sababu za msingi.
Kwa mujibu wa Ust.
Mbaruku, ameelezwa
gerezani hapo kuwa huenda
Ust. Salum, ameamua
kuchukua hatua hiyo ikiwa
ni muendelezo wa migomo
inayoendelea miongoni
m wa wa t u h u m i wa h a o
kushinikiza madai yao
mbalimbali ambayo tayari
wameshayatoa.
Hata hivyo imeelezwa
kuwa Ust. Salumu, ameshuka
Jumatano (wiki hii) kufuatia
juhudi za Sheikh Farid Hadi,
kufanya kazi ya ziada ya
kumnasi ashuke mtini baada
ya kupewa fursa ya kwenda
katika eneo la mti huo.
Ni kwamba, Ustadhi
Salum, alilala juu ya mti, jana
(jumanne) aligoma kabisa
kushuka, lakini asubuhi ya
leo (Jumatano) ameshuka,
baada ya Sheikh Farid,
kumnasihi sana. Alisema
Ust. Mbaruku.
Alisema, wakati anashuka,
Ust. Salum, alieleza kuwa
anashuka kwa heshma ya
kiongozi wake ambapo
baada ya kushuka, Sheikh
Farid aliwanasihi Waislamu
kuendelee kuwa na subra,
nasaha ambazo ziliungwa
mkono na Mama mzazi
wa Ustadh Salum, ambaye
alifika mapema asubuhi
Gerezani hapo.
M a m a ya k e a l i k u j a
gerezani asubuhi na
a l i k u t a n a n a m wa n a e ,
ambapo alimnasihi kwa
kumtaka awe na subira
kuliko kuchukua maamuzi
ya kujidhuru, kwani Allh
(SWT) yupo pamoja naye.
Alisema, Ust. Mbaruku,
akirejea nasaha za mama
Salum.
Ust. Mbaruku, alisema
miongoni mwa madai
wanayodai Waislamu hao
n i k u p a t i wa m a t i b a b u
sambamba na kufanyiwa
uchunguzi wa kina wa afya
zao kutokana na mambo
wa l i y o f a n y i wa wa k i wa
MWANASHERIA Mkuu
Wa Zanzibar Saidi Hassan
VIONGOZI wa Dini ya
K i i s l a m u wa m e i o m b a
serikali kutenda haki na
uadilifu katika kutoa haki
k wa wa n a n c h i b i l a ya
ubaguzi wa aina yoyote.
Wa m e s e m a k w a m b a
amani haipatikani bila ya
haki, hivyo basi ni wajibu
haki kupewa nafasi yake
kwani kutambua haki na
wajibu walionao raiya kwa
nchi yao, ni moja katika sifa
muhimu za viongozi.
Viongozi wa Dini ya
Kiislamu Pemba wanaiomba
S e r i k a l i ya M a p i n d u z i
Zanzibar kuwapatia
wananchi haki zao za msingi
ikiwemo vitambulisho vya
Mzanzibari Mkaazi, na haki
ya kushiriki katika kupiga
kura ili kuepusha dhulma
kwa wanao stahiki.
Hayo yameelezwa katika
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.