You are on page 1of 4

MAPENDEKEZO YA NDG: JOEL NANAUKA KUHUSU OIL AND GAS REVENUE

MANAGEMENT ACT,2015 INAYOJADILIWA BUNGENI SASA.


Ingawa sikubaliani na utaratibu wa kulazimisha miswada 4 iliyoletwa bungeni kwa
hati ya dharura na serikali,napendekeza miswada hii isubiri bunge la 11 ambapo
wabunge tutapata nafasi nzuri ya kujadili kwa undani miswada hii yenye umuhimu
mkubwa kwa Taifa letu kwa kizazi cha sasa na kile kijacho.
Kwa wakati wowote miswada hii itakapowakilisha nimetoa maoni yangu ya
maandishi kwa kuanza na muswada wa Mapato ya Gesi na Mafuta wa Mwaka
2015 kama ifuatavyo.
ARTICLE 12-(1-3)
Imeeleza kuwa kutakuwa na wajumbe 4 wenye uwezo ,uzoefu na ustadi katikia
eneo la uwekezaji katika mambo ya fedha na sheria ya uwekezaji-wajumbe hawa
wote watapendekezwa na Rais.
Maoni:Kuwe na guidelines za kujitosheleza hasa kuweka uwakilishi thabiti wa
taaisi muhimu kwa Taifa letu mfano: kutajwa kabisa mjumbe mmoja kutoka
TPSF(Tanzania Private Sector Foundations),Tanzania Foundation for Civil Societies
na taasisi muhimu itakayokuwa haina influence ya kisiasa Zaidi.Napendekeza
wajumbe wa kutoka taasisi maalumu wawe 3 na watakaoteuliwa na Rais wawe 2.
Hii itasaidia kuweka uhuru wa kimawazo katika mijadala lakini pia itazuia Rais
kuchagua watu kwa vigezo vya jumla na hivyo kujikuta bodi ikijaza wanasiasa
watiifu tu kwa Rais na kutokuwa na watu wa kutoa changamoto.Mfano mzuri
unaweza kupatikana kutoka chad ambako wajumbe wa bodi waliwakilishwa pia
na watu kutoka taasisi zisizo za kiserikali.

ARTICLE 13-(a-c);16(1-6)
Maeneo ya matumizi yameelezwa kwa kutajwa vipengele mbalimbali.Hata hivyo
napendekeza kuwe na sekta za kipaumbele za matumizi ya pesa
inayokusanywa(priority sectors) inayolandana na mpango wa miaka 5 wa

maendeleo wa Taifa.Hii itasaidia kutoruhusu mipango mingine mipya


inayotugharimu kwa kutapanya nguvu na rasilimali zetu.
Vipaumbele vyetu vinaweza kurejewa na kubadilika kila baada ya miaka mitano
ambapo tunarejea upya mpango wetu wa maendeleo wa Taifa.Hii itasaidia kuwa
specific katika maeneo tunayotaka kuwekeza ili kuzuia pesa hizi zisitumike katika
maeneo tusiyoyataka.
Napendekeza sheria ilazimishe umaalumu wa sekta vipaumbele;mfano isiwe
elimu tu bali iwekwe wazi katika miaka mitano matumizi yatakuwa katika elimu
na hasa kulipa madeni ya walimu na kununua vitabu.Hii itasaidia kuondoa
mwanya wa matumizi mabaya kwani vipaumbele hivi vitakuwa vimepitishwa na
bunge na hivyo vitasimamiwa na bunge.

ARTICLE 17( C )(ii)


Hapa imeeleza jinsi ambavyo pesa zilizowekwa kwenye akaunti ya kutunza
mapato(Revenue Saving Account) zinaweza kuchukuliwa(drawn) kama mapato ya
gesi na mafuta yameshindwa kufikia kiwango cha 3% ya Pato letu la Taifa.Hapa
napendekeza litumike neno-should be borrowed(zitakopwa) ili kuwe na utaratibu
wa kurudisha pesa hizo ambazo ni maalumu kwa kizazi kijacho.
Bila kufanya hivyo inaweza kutokea pesa nyingi ikachukuliwa katika miaka tofauti
na hata miaka ambayo mapato ni mazuri zisirudishwe hivyo dhumuni la kwanza la
kuweka pesa hizo kwa ajili ya kizazi kijacho likapotea kabisa.
Sheria itamke kuwa pesa zozote zitakazochukuliwa kutoka katika akaunti
maalumu kwa kizazi kijacho(Revenue Savings Account) itatakiwa kurudishwa mara
pato la mafuta na gesi litakapoweza kurudia ukubwa wake wa Zaidi ya 3% ya
Taifa.
Kwa maneno Mengine Pesa ikishaingia katika mfuko wa kizazi kijacho sio yetu
tena hatuwezi kuamua tu kuichukua,ila tunakopa na tutalazimika kuirudisha
baadaye.

ARTICLE 17(2-A,B)
Muswada unapendekeza pia kususpend fiscal rules za pesa zinazotokana na
mafuta na gesi pale ambapo kutakuwa na matukio ya majanga na baadaye
kuripoti katika bunge matumizi hayo.
Hii ni hatari sana kwa kuzingatia kuna scandal nyingi sana zimetokea hapa nchini
kwa pesa kutumika vibaya kwa visingizio vya usalama waTaifa na hata majanga ya
njaa.Kuripoti bungeni sio njia nzuri ya kudhibiti matumizi haya bali kudhibiti nani
anaidhinisha ndio njia nzuri Zaidi.Hata kama majanga huwa ni ya dharura
napendekeza kamati ya bunge mojawapo(mfano:ya huduma za jamii) ndio ipewe
mamlaka ya kujadili na kupendekeza jambo flani kuwa limekidhi kigezo cha kuwa
janga na kukubali matumizi yafanyike.
Bila kufanya hivyo ni kutoa mwanya kwa matumizi mabaya na baadae zitaletwa
ripoti zilizojaa ufundi wa kupikwa na pesa zitakuwa zimeshaliwa wakati huo na
pekee kitakachofanyika ni kujiuzulu kwa viongozi wakati Taifa litakuwa
limeshapata hasara kubwa sana.

ARTICLE 18(4,5)
Taarifa zimeeleza zitachapishwa katika gazeti la serikali na pia kupatikana katika
mitandao ya serikali na wizara ya fedha.Ni muhimu kuwa wazi kuwa taarifa hizi
zitachapishwa kila baada ya muda gani au wakati gani mfano:Kila mwisho wa
mwaka wa fedha au kila baada ya miezi mitatu baada ya bodi kukutana.
Bila kufanya hivyo ni kutoa mwanya wa kisheria kwani hata wakikaa mwaka
mzima hawajachapisha na wakaisoma bungeni tu mwananchi wa kawaida
ananyimwa nguvu ya kudai taarifa hiyo.Tukumbuke kuwa kufichwa kwa taarifa
ndio imekuwa nguzo kuu ya kuficha maovu hapa nchini.Sheria iweke muda
maalumu wa kuchapishwa taarifa hizo ili wananchi tuweze kuzidai.

ARTICLE 20(1-5)
Napendekeza utaratibu wa ukaguzi wa mahesabu uhusihe kamati ya PAC pia.Hii
itasaidia kama kamati maalumu ya bunge kupata nafasi ya kupitia kwa undani(to
scrutinize) mapato na matumizi hayo kabla hayajafikishwa bungeni.Kuwasilishwa
ukaguzi huo mara baada ya kupitia kwa waziri peke yake ni kutoa muda finyu wa
kujadili na kupata mambo kwa undani.
Napendekeza kutokana na umuhimu wa mapato haya ripoti yake ipitie utaratibu
kama wa mashirika ya umma kwa kuzingatia kuwa hizi ni pesa za umma
zinazotokana na rasilimali zetu.Kamati ya PAC ihusike na yenyewe ndio iwasilishe
taarifa hiyo bungeni na sio waziri husika kama ilivyo katika utaratibu wa
uwasilishwaji wa hesabu za mashirika ya umma.
Naomba Kuwasilisha,

Joel .A. Nanauka


Mwanachama CHADEMA-Mtwara
0688 67 79 68
jnanauka@gmail.com

You might also like