Professional Documents
Culture Documents
Mahindi: Uzalishaji Bora Wa
Mahindi: Uzalishaji Bora Wa
mahindi
Chapisho hili ni pato kutoka mradi unaofadhiliwa na AGRA nchini Tanzania uitwao:
Scaling up Minjingu phosphate utilization for balanced fertilization of crops in Tanzania
Mradi wa kukuza matumizi ya mbolea za Minjingu fosfati na matumizi sahihi ya mbolea mbalimbali, Tanzania
na msaada kutoka Africa Soil Health Consortium ambayo inaratibiwa na CABI
Udongo
Udongo una rutuba ya asili yaani virutubisho katika udongo, mboji (organic
matter), na viumbe mbalimbali vinavyoishi kwenye udongo. Rutuba ya udongo
inategemea sana hali ya udongo kikemia, kibiolojia na kifizikia.
Makundi ya udongo
Kuna makundi makuu matatu ya udongo, kutokana na ukubwa wa
chengachenga za udongo:
Kichanga (Sand soil) - una uwezo mdogo wa kuhifadhi maji na
unyevunyevu. Hivyo, hukauka upesi.
Tifutifu (Loam soil) - unahifadhi maji vizuri na upatikanaji wa maji na
virutubisho kwa mimea ni mkubwa.
Mfinyanzi (Clay soil) - unahifahdi maji mengi zaidi, bali upatikanaji
wa maji na virutubisho kwa mimea ni mdogo.
Vipimo vinavyoonyesha hali ya rotuba ya udongo ni:
Tindikali ya udongo
Kiasi cha mboji
Kiasi cha Naitrojeni, Fosfati, Potashi, Salfa, Chokaa (Calcium) na
Magnesium. Vilevile kiasi cha zinki, shaba, manganese na boroni
vinapimwa.
Mbolea
Mbolea ni chakula cha mimea, ambayo ni mchanganyiko wa virutubisho
mbalimbali vinavyoongezwa kwenye udongo au vinavyowekwa moja kwa moja
kwenye mimea ili kuongeza ukuaji na uzalishaji wa mimea.
Virutubisho hivyo ni pamoja na madini muhimu kama vile naitrojeni, fosfati na
potashi. Madini mengine ni pamoja na salfa, chokaa (calcium), magnesium,
boroni, shaba, chuma, manganese, molybedenum na zinki. Haya madini kwa
asili, yanapatikana katika udongo kwa viwango tofauti. Yanapopungua
kutokana na kilimo, inabidi yaongezwe kwa kutia mbolea.
Aina za mbolea
Minjingu Phosphate
Ina kiwango cha fosfati (P2O5) asilimia 29 na inatumika zaidi kwa kutoa
kirutubisho hiki. Lakini inaongeza vilevile kirutubisho cha chokaa (calcium)
ambacho kipo kwa kiwango cha asilimia 40. Chokaa inasaidia vilevile kukabili
tindikali (acidity) ya udongo.
Minjingu Mazao
Hii ni mbolea mpya inayotokana na Minjingu Phosphate lakini imeongezwa
virutubisho vingine vitano ambavyo ni naitrojeni (10%), salfa (5%), zinki (0.5%),
shaba (0.5%), boroni (0.1%), pamoja na chokaa (25% CaO) na magnesium
(1.5% MgO). Virutubisho vilivyoongezwa hususani naitrojeni na salfa ni vile
ambavyo vinakosekana katika aina nyingi za udongo.
Zinki, shaba na boroni vimeongezwa kwa tahadhari kwa sababu vinaonyesha
dalili za upungufu katika baadhi ya maeneo. Minjingu Mazao iko katika hali ya
chengachenga.
Dalili ya upungufu wa
virutubisho mbalimbali
1. Upungufu wa naitrojeni (Nitrogen)
B
7
2. Kupanda
Mbegu bora
Matumizi ya mbegu bora ni muhimu katika upatikanaji wa mavuno mengi na
bora. Kuna makundi mawili makuu ya mbegu ambayo ni:
i). Mbegu za asili: Ni zile ambazo zimetumika miaka mingi katika historia
ya kilimo
ii). Mbegu zilizoboreshwa: Hizi ni zile zilizoboreshwa kutoka mbegu za
asili. Kundi hili linagawanywa kwenye makundi mawili - composite
varieties na mbegu chotara (Hybrids).
9
Ushauri wa matumizi ya mbegu zilizoboreshwa unatofautiana kutoka eneo moja na lingine kwa
sababu ya:
i). Mwinuko kutoka usawa wa bahari
ii). Kiasi cha mvua katika eneo husika
iii). Muda unaotumia mbegu hadi kukomaa
Mbegu za mahindi zilizoboreshwa ni kama TMV1, TAN 250, TAN 254, Staha, Situka na zingine zote
zinazoanza na herufi H kama vile H 250, H 251 na H 615.
kupandia
kwa hektari
kwa ekari
DAP
Minjingu fosfati
Minjingu Mazao
10
Muda wa kupanda
Muda wa kupanda unatofautiana kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na majira ya mvua. Kwa
mfano katika wilaya ya Morogoro tarehe za kupanda ni kuanzia februari 15 hadi Machi 15. Mkulima
anashauriwa afuate kalenda ya muda wa kupanda kama anavyoshauriwa na bwana shamba wake.
Kupanda kwa nafasi
Kupanda kwa nafasi ni kati ya njia bora za kilimo inayomwezesha mkulima kupata mazao bora. Hivyo
ni muhimu sana kuzingatia kupanda kwa mistari na kufuata nafasi zinazoshauriwa na wataalamu wa
kilimo. Kwa mfano nafasi zifuatazo zinaweza kutumika katika upandaji wa mahindi:
Nafasi
90 sm X 30 sm
90 sm X 25 sm
90 sm X 50 sm
11
3. Kupalilia
Ni muhimu shamba lipaliliwe baada ya mimea kuota ili kuondoa magugu. Magugu ni mimea hivyo
hushindana na mimea iliyopandwa na mkulima kwa kunyonya virutubisho ardhini. Magugu yanaweza
pia kuhifadhi wadudu na magonjwa yanayoweza kushambulia mimea iliyopandwa na hivyo
kupunguza mavuno.
Mbolea za kukuzia
Ni mbolea zinazotumika baada ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza mimea ili itoe mavuno bora.
Mara nyingi mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni. Mbolea maarufu za kukuzia katika soko la
Tanzania ni kama:
AIna ya mbolea
Urea
46%
23%
21%
12
Urea inakirutubisho cha naitrojeni (N) kwa kiwango kikubwa na watu wengi wanauzoefu nayo. Vilevile
bei yake ni nafuu ikilinganishwa na mbolea zingine za kukuzia. Mbolea hii iko katika hali ya
chengachenga za mviringo (granules) za rangi nyeupe. Kiwango cha urea ni nusu kizibo cha soda kwa
kila shina.
Mbolea hizi hazidumu kwenye udongo kwa muda mrefu kwa hiyo huwekwa shambani wakati mimea
inapokuwa na mahitaji makubwa ya kirutubisho cha naitrojeni na wakati udongo una unyevunyevu na
shamba halina magugu.
Mbolea za kukuzia huwekwa kuzunguka kila shina la mimea au pande mbili au tatu au nne za kila
shina. Cha muhimu ni kwamba mbolea isirundikwe sehemu mmoja.
13
Idadi ya mifuko ya
Urea
CAN
SA*
Viwango
* Kiwango kilichowekwa hapa ni kwa ajili ya kupata kirutubisho cha salfa kinachosha - ambacho ni kilo 20 ya salfa kwa hektari. Na kupata sehemu
ya mahitaji ya naitrojeni ambyao ni kilo 21. Hii ina maana kwamba kilo 39 za naitrojeni inabidi ziwekwe kama Urea au CAN.
14
15
Ili mkulima aweze kupata mazao mengi na bora inashauriwa kutumia dawa za
kuzuia magonjwa na wadudu washambuliao mimea na njia zinginezo.
16
Kukausha
Kama mahindi hayajakauka vizuri hukaushwa zaidi katika juani siku 3-4 ili
kupunguza unyevunyevu kufikia kiwango kinachofaa kwa kuhifadhi (14%). Ni
muhimu mahindi yakauke vizuri ili yasioze yakiwekwa ghalani.
Ili kujua kama mahindi yamekauka vizuri, tia mahindi kadhaa kwenye chupa ya
soda iliyokauka na uongeze kiganja kimoja cha chumvi. Tingisha chupa halafu
uwache itulie kwa dakika tatu. Chumvi ikikwama kando ya chupa, basi mahindi
haijakauka vizuri.
Kusafisha
Mahindi yaliyokauka vizuri hupepetwa na vilevile mahindi mabovu huondolewa.
Kuhifadhi
Mahindi safi huchanganya na dawa za kuua wadudu kama vile Actellic Super
ambayo ni vumbi nyeupe na kisha kuhifadhiwa kwenye ghala.
17
Manufaa ya matumizi
ya mbolea
i). Kuongeza mavuno
ii). Ubora wa mazao
iii). Kuhifadhi rutuba ya udongo
iv). Kuongeza kipato kutokana na mavuno mengi na bora
Ni muhimu kutumia mbolea za viwandani katika kilimo cha mahindi ili kumuwezesha mkulima kupata
mavuno mengi. Lakini ikumbukwe kwamba matumizi ya mbolea ni lazima yaambatane na matumizi ya
mbinu nyingine bora za kuzalisha mahindi, kama vile:
Kuandaa shamba
Matumizi ya mbegu bora
Kupalilia
Kupiga madawa ya kuzuia na kuua wadudu na magonjwa
Kuvuna kwa wakati unaostahili
Kuhifadhi vizuri mahindi
18
Jedwali 1. Tafsiri ya matokeo ya vipimo vikuu vine vya upimaji wa udongo kwa ajili ya kilimo
Kipimo
pH ya udongo
Naitrojeni (N)
(%)
Kiwango
Ufafanuzi/tafsiri
Tindikali kali
Nyongo ya watani
Nyongo kali
Kiasi kidogo
Kiasi kikubwa
Ndogo kuliko 15
Kiasi kidogo
15 hadi 25
Kubwa kuliko 25
Kiasi kikubwa
Kiasi kidogo
Kiasi kikubwa
Fosfati
(mg/kg)
Potashi
(cmolc/kg)
Mapendekezo/Ufafanuzi
19
Chapisho hili ni pato kutoka mradi unaofadhiliwa na AGRA nchini Tanzania uitwao:
Scaling up Minjingu phosphate utilization for balanced fertilization of crops in Tanzania - (Mradi wa AGRA - 2009 SHP 016)
Mradi wa kukuza matumizi ya mbolea za Minjingu fosfati na matumizi sahihi ya mbolea mbalimbali, Tanzania
na msaada kutoka Africa Soil Health Consortium ambayo inaratibiwa na CABI
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo,
Idara ya Sayansi ya Udongo
P. O. Box 3001, Morogoro, Tanzania
Tel.: +255 23 260 4 649
ISBN 978-9987-9673-5-3
Kufanya kazi kwa pamoja na wadau/wabia kutayarisha taarifa zinazohusu mbinu husishi za afya ya udongo
20