Professional Documents
Culture Documents
Untitled
Untitled
1) Hali ya Uchaguzi
Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015 kama
zilivyo chaguzi nyengine unakwenda sambamba na Uchaguzi Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Chaguzi hizo mbili zinafanyika
katika vituo sawa kwa kutumia utaratibu, ulinzi na usimamizi ulio sawa.
Kwa hivyo, siku ya uchaguzi mkuu mwananchi wa Zanzibar ndani ya
kituo kimoja anapiga kura tano (5) badala ya tatu (3) anazopiga
mwananchi aliyepo Tanzania Bara. Kura ambayo mwananchi wa
Zanzibar anapiga ni:
a)
b)
c)
d)
e)
MGOMBEA KURA ZA
MGOMBEA
DR. ALI
182,011
MOHAME
D SHEIN
ASILIMIA
46.28%
207,847
52.84%
IDADI YA
KURA HALALI
393, 323
MAALIM
SEIF
SHARIF
HAMAD
ii.
10
11
12
13
14
15
16
17
18
MGOMBEA
DR. JOHN
POMBE
MAGUFULI
EDWARD
NGOYAYE
LOWASSA
KURA HALALI
194,317
ASILIMIA
46.5%
211,033
50.50%
IDADI YA KURA
HALALI
417,882
19
20
ii.
21
22
Kwa kuzingatia sababu zote hizo, ni wazi kuwa Hoja ya kurudiwa uchaguzi
haina uhalali, haina msingi na ni chachu ya kuiweka nchi katika utawala
usiokuwa halali na kusababisha fadhaa kubwa kwa wananchi. Ni hoja
ambayo inaweza kuzaa fujo na vurugu katika nchi na kupelekea mzozo
mkubwa zaidi wa kikatiba na kisheria. Sidhani kama tunataka tuifikishe
huko nchi na tuwafikishe huko wananchi tulioapa kuwatumikia na
kuwalinda.
5. MAZUNGUMZO YANAYOWAHUSISHA WAGOMBEA URAIS
WA CUF NA CCM PAMOJA NA MARAIS WASTAAFU WA
ZANZIBAR
Kufuatia jitihada kubwa nilizozifanya kwa njia ya simu na hatimaye
kufikisha maombi yangu kwa maandishi kumtaka Dk. Ali Mohamed Shein
akutane na mimi, hatimaye alikubali na kupendekeza tuwashirikishe
viongozi wengine wastaafu wa Zanzibar.
Hadi sasa tumeshafanya vikao vinane, cha kwanza kikiwa ni kile cha tarehe
9 Novemba, 2015.
Wengi wenu mmehoji kwa nini nikakubali kushiriki vikao ambavyo niko
peke yangu kutoka CUF wakati CCM wako watano. Nilikubali hivyo kwa
kutumia msingi wa kuwashirikisha Marais wastaafu wa Zanzibar lakini pia
nikiamini kwamba tungeongozwa na busara na kuheshimu Katiba na Sheria
badala ya utashi wa vyama vyetu.
Tokea mazungumzo hayo yaanze, wananchi wengi wamekuwa wakitaka
tuwaeleze kinachoendelea. Mimi binfasi niliamua kubaki kimya kwa
kuheshimu msingi tuliojiwekea kwamba taarifa ya mazungumzo hayo
itolewe kwa pamoja baada ya mazungumzo kukamilika. Hata hivyo,
inasikitisha kuona wakati mimi nikiheshimu hilo na kuwa kimya kipindi
chote hicho, viongozi wenzangu kutoka upande mwengine wamekuwa
wakiliuka hilo na kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikiwachanganya
wananchi.
Kutokana na mwenendo huo, nimeona kuna haja na mimi kuwaeleza
wananchi ukweli wa kile kinachoendelea.
23
Rais John Pombe Magufuli amefanya kazi kubwa ya kututia moyo ili
tukamilishe mazungumzo hayo kwa ufanisi na kwa kuzingatia matakwa ya
Katiba na Sheria. Alikutana na mimi na baadaye akakutana na Dk. Ali
Mohamed Shein. Hata hivyo, inasikitisha kwamba hata yeye Rais Magufuli
hakuachwa kufitinishwa na wananchi wa Zanzibar pale Balozi Seif Ali Iddi
alipodai hadharani kwamba eti Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania katutaka turudi Zanzibar tukakamilishe taratibu za kurudia
uchaguzi, jambo ambalo si kweli.
Ukweli ni kwamba katika vikao hivyo vinane bado Dk. Ali Mohamed Shein
na Balozi Seif Ali Iddi wanangangania kurudia uchaguzi huku wakimtetea
kwa nguvu zote Jecha Salum Jecha, na mimi nimesisitiza haja ya kuheshimu
matakwa ya kikatiba na kisheria na maamuzi ya wananchi wa Zanzibar
waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015 katika uchaguzi ambao waangalizi
wote wa ndani na nje na hata Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar walisema kwamba ulikuwa huru, wa haki na uliofanyika katika hali
ya amani.
Kwa hakika hadi jana, ukiangalia tovuti ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
utaona taarifa zinazosema kwamba uchaguzi hadi hatua ya kuhesabu kura
ulifanyika kwa utulivu nchi nzima.
Kutokana na kutofikia muafaka pamoja, tulikubaliana kuandaa taarifa ya
pamoja ambayo ilielezwa kwamba ingeandaliwa na Katibu wa vikao hivyo
lakini sasa ni zaidi ya wiki mbili, hakuna kikao kilichoitishwa. Nimeandika
barua kuhimiza kikao cha kupokea taarifa hiyo na kuipitisha lakini bado Dk.
Shein anasema wanahitaji muda.
Ni wazi kwamba Dk. Ali Mohamed Shein hakuwa na nia njema katika
mazungumzo haya na amepoteza sifa ya kuongoza vikao hivyo.
6. NJAMA ZA CHINI KWA CHINI ZA KUHUJUMU UTAFUTAJI
WA UFUMBUZI WA HAKI
Wakati Dk. Ali Mohamed Shein akikwepa kwa makusudi kuitisha kikao cha
kupokea taarifa ya mazungumzo hayo, tumegundua kwamba lengo halisi ni
kuisindikiza Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kutangaza tarehe ya uchaguzi
wa marudio ili baadaye itolewe hoja kwamba suala hilo limeshaamuliwa.
24
25
26
HITIMISHO
Zanzibar imepita katika siasa za dhoruba na machafuko kwa zaidi ya miaka 50.
Dhoruba na machafuko hayo yalifikia hadi kugharimu maisha ya watu. Ni kwa
sababu ya kuchoshwa na siasa za aina hiyo na migogoro isiyokwisha ndiyo
maana mwaka 2009, mimi na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Amani Karume,
tulichukua maamuzi ya kijasiri ya kuleta MARIDHIANO ambayo yaliituliza
Zanzibar. Kila mmoja wetu ni shahidi kwamba kwa miaka sita iliyopita Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ilipumua kujibu hoja zisizokwisha kuhusu hali ya
27
28
tayari kushirikiana nao kuitetea haki yao na maamuzi yao ya kidemokrasia kwa
nguvu zetu zote.
Nawashukuru kwa uvumilivu wenu na kwa kunisikiliza.
Ahsanteni sana.