You are on page 1of 1

1

STATE HOUSE ZANZIBAR


OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE
Zanzibar 15.06.2017

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed


Shein amesema kuwa utamaduni wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China wa
kuendelea kuleta Madaktari kila baada ya miaka miwili ni hatua muhimu katika
kuimarisha sekta ya afya hapa Zanzibar sambamba na kukuza uhusiano na
ushirikiano mwema kati ya nchi mbili hizo.

Dk. Shein aliyasema hayo leo Ikulu mjini Zanzibar katika mazungumzo kati yake na
Madaktari wapya pamoja na wale wanaomaliza muda wao kutoka Jamhuri ya Watu wa
China, wakiongozwa na Balozi Mdogo wa nchi hiyo anayefanya kazi zake hapa
Zanzibar Balozi Xie Xiaowu.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alieleza kuwa utamaduni wa nchi hiyo wa kuleta
Madaktari kwa ajili ya kutoa huduma za afya hapa Zanzibar ni wa kihistoria ambao
umeanza tokea mwaka 1964 na kuendelea hadi hivi leo ambapo China ilianza kuleta
wataalamu wake mbali mbali hapa Zanzibar wakiwemo Madaktari.

Dk. Shein alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wa


Zanzibar wanathamini na wanazipenda huduma zinazotolewa na Madaktari kutoka
nchini China ambao wamekuwa wakishirikiana vyema na Madaktari wazalendo kutoa
huduma hizo kwa ufanisi mkubwa hapa Zanzibar.

Pia, Dk. Shein, alitumia fursa hiyo kueleza uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya
China na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo Zanzibar huku akiahidi
kuendelezwa na kudumishwa na kusisitiza kuwa China imeweza kutoa mchango
mkubwa katika mafanikio ya sekta ya afya na sekta nyengine mbali mbali hapa
Zanzibar ikiwemo sekta ya viwanda, elimu,kilimo, michezo, habari na nyengienzo.

Dk. Shein aliwakaribisha Madaktari hao wapya hapa Zanzibar na kuwaaga wale
waliomaliza muda wao huku akieleza matumaini yake makubwa kuwa madaktari hao
wapya kuwa watafanya kazi kwa ufanisi mkubwa zaidi kama wenzao wanao ondoka
ambao wamefanya kazi vyema katika kutoa huduma za afya.

You might also like