Professional Documents
Culture Documents
Stori Ubungo
Stori Ubungo
OFISI YA RAIS
Simu Na: +255 (026) 2963630 Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Nukushi: +255 (026) 2963629 na Utawala Bora,
Barua Pepe: ps@utumishi.go.tz Jengo la Taaluma Na. 1,
Tovuti: http://www.utumishi.go.tz Chuo cha Masomo ya Biashara na Sheria,
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),
Barabara ya Mkalama,
S.L.P. 670,
40404 DODOMA.
Mhe. Kairuki amesema mwajiri anapoomba kibali cha kuajiri watumishi ni vema
akazingatia mahitaji kulingana na majukumu yaliyopo ili kuondoa ziada ya
watumishi wa umma wasio na kazi kuendana na fani walizosomea kwa lengo
la kuwa na utendaji mzuri.
Waziri Kairuki amesema katika vibali 10,184 vilivyotolewa hivi karibuni na Ofisi
ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa Mamlaka
za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala za Serikali, pamoja na
Taasisi na Mashirika ya Umma ili kujaza nafasi zilizoachwa na watumishi wa
umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, Halmashauri ya Manisapaa ya
Ubungo imetengewa jumla ya nafasi 140.
Mhe. Kairuki yuko katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Dar es salaama kwa
lengo la kukutana na watumishi wa umma na kusikiliza malalamiko, ushauri na
changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili kuweza kuzifanyia
kazi na kuleta mabadiliko katika Utumishi wa Umma nchini ili kufikia malengo
yaliyopangwa na Serikali.