Anuani ya Simu MKUUPOLISI Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734 Makao Makuu ya Polisi, Fax Na. (022) 2135556 S.L.P. 9141, Unapojibu tafadhali taja: DAR ES SALAAM .
18/ 07/ 2017
TAARIFA YA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Saimon Sirro, amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga.
Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kinondoni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Suzan Salome Kaganda amekuwa Mkuu wa kitengo cha Mafao na Fidia Makao Makuu ya Polisi, na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo ambaye alikuwa kamanda Polisi Mkoa wa Shinyanga.
Aidha, Nafasi ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga
imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Sylverius Haule, ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu wa Polisi wa Mkoa wa Mara.
Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la
Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.
Imetolewa na: Barnabus D. Mwakalukwa - ACP Msemaji wa Jeshi la Polisi. Makao Makuu ya Polisi.