You are on page 1of 22

Makala ya Habari kwa Umma

HABARI KWA UMMA


Kipeperushi Na. 2

MAELEZO MUHIMU KUHUSIANA NA


MFUKO WA UMOJA (UMOJA FUND)

Mei, 2005
Makala ya Habari kwa Umma
UTANGULIZI

Mfuko wa Umoja umeanzishwa ukiwa ni mfuko wa kwanza wa uwekezaji wa pamoja


ambao unatoa nafasi kwa Watanzania wengi kuwekeza na kunufaika na ubinafsishaji
(take a stake in privatization), na vilevile kushiriki katika Masoko ya Mitaji na kupata
faida (pato) kutokana na uwekezaji wao. Ni mfuko wa kwanza wa uwekezaji wa pamo-
ja kuanzishwa nchini Tanzania.

Katika Kipeperushi Na.1 cha Habari Kwa Umma, zilitajwa faida mbalimbali za mifuko
ya uwekezaji wa pamoja. Faida hizo ni pamoja na ukusanyaji rasilimali, kutawanywa
kwa hatari za uwekezaji, kupunguzwa gharama za uwekezaji na kuwezeshwa wawekeza-
ji wadogo wadogo.

Mfuko wa Umoja ni mfuko wa uwekezaji wa pamoja ambao pia unajulikana kama


mfuko wa kikundi cha amana (unit trust scheme). Mfuko huu umeanzishwa kwa kufua-
ta Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ya mwaka 1994 (kama ilivyorekebishwa) na
Kanuni/taratibu za mifuko ya uwekezaji wa pamoja za mwaka 1997.

Mfuko huu umebuniwa kuwezesha ushiriki wa Watanzania wa aina zote yaani mtu
mmoja mmoja na taasisi mbalimbali za kijamii ( zilizosajiliwa nchini na wanufaika wake
wote ni Watanzania) iwe kipato chake ni kidogo au kikubwa na vilevile kwa Watanzania
walioko ndani au nje ya nchi.

MAMBO MUHIMU YA MIFUKO YA UWEKEZAJI WA PAMOJA

Kama ilivyokwishaelezwa, Mfuko wa Umoja utakuwa ndio mfuko wa kwanza wa


uwekezaji wa pamoja kuanzishwa nchini Tanzania. Hivyo basi, ni muhimu kufahamu
sifa zake za msingi. Vilevile kuna tofauti ya mifuko kama hii na kampuni na ubia (part-
nership) ambazo zimekuwa ni njia zilizozoeleka za kuendesha biashara nchini mwetu.

MIFUKO YA UWEKEZAJI WA PAMOJA INAPOLINGANISHWA NA


KAMPUNI

Kampuni kwa kawaida inaundwa kwa watu kununua hisa kwa mujibu wa katiba ya kam-
puni (Memorandum and Articles of Association). Kampuni inasajiliwa na Wakala wa
Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Baada ya kampuni kusajiliwa inakuwa kama
mtu kisheria hali inayoitofautisha na wana hisa wake. Mali ya kampuni si mali ya wana
hisa. Mali hiyo ni ya kampuni. Wana hisa wanazo haki zao kufuatana na katiba ikiwa
ni pamoja na haki ya gawio kutokana na faida, kuhamisha [kuuza] hisa, kupiga kura, na

1. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
kupata/kugawana rasilimali iwapo kampuni itafilisiwa au kufungwa. Bodi za
Wakurugenzi huchaguliwa na wanahisa. Kwenye mfuko wa uwekezaji wa pamoja mali
ya mfuko ni mali ya walionunua vipande vya mfuko.

Awali ya yote, kupata gawio kutoka kwenye kampuni inategemea mambo mawili; kwan-
za gawio linatolewa iwapo kampuni imepata faida na pili gawio linapatikana kulingana
na sera ya gawio (Dividend Policy) kama inavyokuwa imeamuliwa na Bodi ya
Wakurugenzi wa kampuni. Inawezekana kwa mfano; Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni
kuamua kuwa faida ibakizwe ndani ya kampuni kwa ajili ya kukuza shughuli za kam-
puni fulani.

Jambo la pili muhimu ni kwamba, kwenye kampuni Bodi ya Wakurugenzi ndiyo yenye
wajibu na madaraka ya kuendesha kampuni. Kwa hiyo, Bodi ya Wakurugenzi ndiyo
inayoteua watendaji wa kila siku wa shughuli za kampuni na yenyewe kubakia na wajibu
wa kutoa na kuratibu sera za kampuni.

MIFUKO YA UWEKEZAJI WA PAMOJA INAPOLINGANISHWA NA


UBIA (PARTNERSHIP)

Ubia (Partnership) ni makubaliano ya watu wasiozidi ishirini waliokubaliana kuchanga


mtaji kwa ajili ya biashara na kugawana faida inayotokana na ubia huo. Ubia unaundwa
na Waraka wa ubia (partnership deed) ambao unaelezea wajibu wa wabia pamoja na
taratibu mbalimbali za ubia huo.

Inawezekana mmoja wa wabia kuwekwa kusimamia biashara ya ubia. Faida inay-


opatikana inagawanywa kulingana na mchango wa kila mbia.

Ubia ukilinganishwa na mfuko/mpango wa amana ya kikundi (kama Mfuko wa Umoja)


kuna tofauti kubwa. Aina ya makubaliano ya kuanzishwa kwa vyombo hivi vya
uwekezaji wa pamoja ni tofauti. Mpango wa uwekezaji wa pamoja huanzishwa kwa
waraka wa makubaliano kati ya mwanzishaji na kampuni ya uangalizi inayotakiwa kuwa
ni benki (Custodian). Wawekezaji vilevile huingia kwenye waraka huu mara tu
wanapowekeza. Tofauti na ubia wa kawaida, uwekezaji kwenye mipango ya uwekezaji
wa pamoja huthibitishwa na hati ya kumiliki vipande ( Unit Certificate).

MUUNDO WA MIFUKO YA UWEKEZAJI WA PAMOJA.

Muundo wa Mfuko wa uwekezaji wa pamoja ni tofauti na muundo wa kampuni. Mfuko


wa uwekezaji wa pamoja unaanzishwa na mwanzishaji ambaye anaweza kuchukua

2. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
majukumu ya kuendesha mfuko au kukodi Meneja mtaalamu kuendesha mfuko huo. Vile
vile mwanzishaji huyo anatakiwa kuteua Mwangalizi (Custodian) ambaye kazi yake
kubwa ni kutunza mali za mfuko na kuhakikisha kuwa mfuko huo unaendeshwa kwa
mujibu wa Sheria. Meneja na Mwangalizi wanakuwa na waraka wa makubaliano ambao
unasajiliwa na Msajili wa Dhamana.

Ijapokuwa mfuko wa uwekezaji wa pamoja pia unasajiliwa kama Dhamana, majukumu


juu ya mfuko yanaangukia kwa pande mbili ambazo ndizo waanzilishi wake ambao ni
Meneja na Mwangalizi. Meneja na Mwangalizi wanawajibika moja kwa moja kutimiza
masharti ya waraka wa makubaliano. Waraka wa makubaliano unataja majukumu ya
Meneja na Mwangalizi. Waraka huu ni mkataba kisheria na hivyo utekelezwaji wake
unaweza kusimamiwa kwenye vyombo vya sheria kama mahakama.

Moja wapo ya tofauti ya wazi kati ya kampuni na mpango wa uwekezaji wa pamoja ni


utaratibu wa kumiliki mali. Mali ya mpango wa uwekezaji wa pamoja ni ya wenye kumi-
liki vipande kwenye mpango huo. Wanamiliki mali kulingana na vipande wanavyomili-
ki katika mfuko wakati mali ya kampuni inamilikiwa na kampuni na sio wanahisa.

Baada ya kuanzishwa, mpango wa uwekezaji wa pamoja unatakiwa kuendeshwa kwa


mujibu wa sheria iliyotajwa hapo juu. Mfumo wa mpango umeelezwa kwa muhtasari
katika Kielelezo Na.1.

Licha ya kuwa mwangalizi wa mpango wa uwekezaji wa pamoja anapaswa kumteua


Mkaguzi wa Mahesabu (Auditor) ambaye hufanya shughuli zake kwa kulingana na tarat-
ibu zilizowekwa bayana kisheria, mwekezaji yeyote anayenunua vipande katika mpan-
go wa uwekezaji wa pamoja anakuwa sehemu ya waraka wa makubaliano kama vile ali-
tia sahihi kwenye waraka huo hapo mwanzo. Katika mazingira haya mwekezaji
anakuwa amewezeshwa kudai kutekelezwa kwa waraka wa makubaliano akiwa na haki
zote za kisheria. Hii ni muhimu kwa sababu inaweza kujitokeza swali kuwa ni kwa vipi
wenye vipande watakavyoweza kudai haki zao dhidi ya Meneja na Mwangalizi kama
hawa watavunja mkataba. Kwa sababu hiyo waraka wa makubaliano ni mojawapo ya
nyaraka ambazo zinatakiwa kuwepo kisheria kwa ajili ya kukaguliwa na wanaotaka
kuwekeza kwenye mfuko.

MCHANGO WA SERIKALI KATIKA MFUKO WA UMOJA

Kama sehemu ya sera zake za uwezeshaji, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa


Tanzania ilianzisha Dhamana ya Uwekezaji Tanzania na kuipa hisa za makampuni mbal-
imbali kwa lengo la kuwezesha umiliki mpana wa hisa hizo miongoni mwa jamii ya

3. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
Watanzania wakiwemo wawekezaji wadogo wadogo na kukuza utamaduni wa kuweka
akiba.

Serikali imesaidia kuanzishwa kwa Mfuko wa Umoja kwa njia zifuatazo:


• Kuanzisha Dhamana ya Uwekezaji Tanzania;
• Kutoa mtaji kwa ajili ya Mfuko wa Umoja;
• Kuruhusu punguzo la bei kwenye mauzo ya mwanzo ya vipande vya Mfuko wa
Umoja;
• Kusaidia matayarisho mbalimbali yenye kuhusiana na kuanzishwa kwa Mfuko wa
Umoja.

MTAJI KWA AJILI YA MFUKO WA UMOJA

Serikali imekubali kutoa asilimia mbili (2%) ya hisa za Kampuni ya Bia Tanzania na asil-
imia moja ( 1%) ya hisa za Kampuni ya Sigara Tanzania kama mtaji kwa ajili ya Mfuko
wa Umoja. Thamani ya hisa hizo zote hapo tarehe 08 Machi, 2005 ilikuwa kiasi cha shs.
11,571,609,600/=

PUNGUZO LA BEI KWA RAIA WA TANZANIA

Licha ya kukubali kutoa hisa zake kwenda kwenye Mfuko wa Umoja, Serikali pia imepi-
tisha uamuzi wa kutoa punguzo la asilimia thelathini (30%) kwenye thamani ya mwan-
zo ya vipande vya Mfuko wa Umoja. Thamani ya mwanzo ya vipande vya Mfuko wa
Umoja ni shs. 100/= kwa kila kipande. Lakini, kwa ajili ya punguzo linalotolewa na
serikali la 30%, mauzo kwa kila kipande yatakuwa kwa bei ya shs 70/=.

Kiwango cha chini cha vipande ambacho mtu anaweza kununua katika kipindi cha
mauzo ya awali ni 50 amabvyo vitamwezesha mwekezaji kuweza kuingia kwa kiwan-
go cha chini cha shs. 3,500/=. Hakuna kiwango cha juu. Hata hivyo maombi yote
yatatathiminiwa na Meneja kulingana na malengo ya mpango kwa kutumia vigezo
vitakavyopitishwa na Mamlaka.

Ili kuhakikisha kuwa punguzo la bei linawanufaisha Watanzania pekee, watu na taasisi
zilizotajwa hapa chini ndio wanaoruhusiwa kuwekeza wakati wa kipindi cha toleo la
kwanza la Mfuko wa Umoja.

(a) Watanzania wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea wanaoishi nchini au nje
ya nchi.

4. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
(b) Wazazi au walezi kwa niaba ya Watanzania wenye umri chini ya miaka 18
walioko ndani au nje ya nchi.

(c) Makampuni yaliyosajiliwa Tanzania na ambayo wamiliki wake ni Watanzania.

(d) Mifuko ya Pensheni au Mifuko ya hifadhi ya jamii iliyosajiliwa Tanzania


ambayo wanufaika wake ni Watanzania.

(e) Vyama vya Ushirika, Taasisi za Kijamii, Taasisi za Misaada, Taasisi za Kidini
na Vyama/vikundi vya uwekezaji viliyosajiliwa Tanzania ambavyo wanufaika
wake wote ni Watanzania.

Wasio Watanzania na wawekezaji wengineo ambao hawaangukii kwenye makundi yaliy-


otajwa hapo juu wanaweza kuwekeza baada kipindi cha kizuizi kinachoishia tarehe 31
Julai 2006.

SERA YA UWEKEZAJI YA MFUKO WA UMOJA

Mfuko wa Umoja ni chombo maalum cha uwekezaji,. rasilimali zitakazokuwa kwenye


mfuko kwa wakati wote zitakuwa ni kwa ajili ya uwekezaji. Mojawapo ya majukumu ya
Meneja (ambaye ni Dhamana ya Uwekezaji Tanzania) ni kuwekeza rasilimali hizo kwa
maslahi ya wenye vipande vya mfuko.

Kama ilivyokwishaelezwa hapo awali, Serikali tayari imekwishatenga hisa kwa ajili ya
Mfuko wa Umoja. Uwekezaji utafanywa kwenye dhamana za serikali, hatifungani za
makampuni, akaunti za muda maalum na hisa nyinginezo zitakazokuwa zimeorodhesh-
wa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam. Kiwango kitakachowekezwa kwenye hisa
hakitakiwi kuwa zaidi ya asilimia thelathini (30% ) ya mseto mzima wa uwekezaji wa
mfuko.

Uwekezaji wa mfuko ni wa mizania (balanced portfolio), ikizingatiwa kuwa Mfuko wa


Umoja ni mfuko wa wazi, Meneja wa mfuko atatakiwa kuwa na kiasi cha fedha cha
kutosha kwa wakati wote kumwezesha kununua vipande kutoka kwa wawekezaji
watakaokuwa wanajitokeza kurudisha/ kuuza vipande vyao kwa Meneja (Dhamana ya
Uwekezaji Tanzania).

Mali ya mwanzo ya Mfuko wa Umoja ni kama ilivyoonyeshwa kwenye Kielelezo Na.2.


Vile vile chanzo cha mali/mtaji na uwekezaji wake umeonyeshwa katika Kielelezo
hicho.

5. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
KIELELEZO I

AINA ZA UWEKEZAJI ZILIZOPO KWA WAWEKEZAJI WA MFUKO WA


UMOJA

Mfuko wa Umoja unazo aina mbili kubwa za uwekezaji ambazo zinalenga kukidhi
malengo ya wawekezaji, aina hizo ni mpango wa mapato (income distribution) na mpan-
go wa kukua (Re-investment).

MPANGO WA MAPATO

Chini ya mpango huu, wawekezaji watakuwa wanagawiwa sehemu ya mapato ya mfuko.


Utaratibu huu unafanana na ule wa malipo ya gawio la faida unaofanywa na makampuni.

6. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
KIELELEZO II

MPANGO WA KUKUA

Chini ya mpango wa kukua hakuna gawio litakalotolewa, badala yake mapato yatabak-
izwa kwenye mfuko na wawekezaji watapewa vipande vya nyongeza, idadi ya vipande
itapatikana kwa kuchukua gawio alilotakiwa kupata mwekezaji na kugawa kwa thamani
halisi ya kipande kwa wakati wa mgao. Wawekezaji vijana wanashauriwa kufuata utarat-
ibu huu kwani unawawezesha kukuza rasilimali zao katika uwekezaji kwa ajili ya maisha
ya baadaye.

UWEZEKANO WA KUBADILI KUTOKA MPANGO WA MAPATO KWENDA


KWENYE MPANGO WA KUKUA (AU KINYUME CHAKE)

Wenye vipande wanaruhusiwa kubadili kutoka mpango wa mapato kwenda kwenye


mpango wa kukua katika muda na tarehe kama itakavyokuwa imetangazwa na Dhamana
ya Uwekezaji Tanzania. Swala muhimu hapa ni kuwa mwekezaji anaweza kubadili kuto-
ka kwenye mapango wa mapato kwenda kwenye mpango wa kukua. Vielvile mwekeza-
ji anaweza akawa na sehemu ya uwekezaji wake kwenye mpango wa mapato na sehemu
kwenye mpango wa kukua.

Mazingira haya yanaongeza urahisi kwa wawekezaji kubadili kutoka utaratibu mmoja
kwenda mwingine.

7. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
MASHAKA YATOKANAYO NA KUWEKEZA KWENYE MFUKO WA UMOJA

Wawekezaji wanashauriwa kuwa kuwekeza kwenye mfuko kunaweza kuathiriwa na


mambo mbalimbali na hivyo kufanya thamani ya mfuko kupanda au kushuka kutege-
meana na sababu mbalimbali zinazoathiri soko la dhamana. Ufanisi wa nyuma wa
dhamana yoyote ile inayonunuliwa na mfuko si lazima ikawa ishara ya ufanisi wa siku
za usoni.
Wawekezaji wanatakiwa pamoja na mambo mengine kufahamu mambo yafuatayo:

• Ufanisi wa kampuni ambazo hisa zake zimenunuliwa na kushikiliwa na mfuko


unaweza kushamiri (improve) au kudorora (deteriorate).

• Ukiachilia dhamana za Serikali, hatifungani zilizotolewa na makampuni zinaweza


kukumbwa na hali ya kushindwa kulipa madeni.

• Mabadiliko ya viwango vya riba yanaweza kuathiri dhamana zenye mapato


maalum (fixed income securities) ambako mfuko umewekeza.

• Mfumo wa kodi unaweza kubadilika na hivyo kuathiri mapato ya mfuko na


mgawanyo wa mapato.

• Mambo mengine ambayo hayategemewi yanaweza kuathiri uwekezaji uliofanywa


na mfuko na hivyo kuathiri thamani ya vipande vya Mfuko wa Umoja.

• Mabadiliko kwenye urahisi wa kuuza na kununua dhamana (ukwasi) kwenye Soko


la Hisa la Dar es Salaam yanaweza kuathiri thamani ya dhamana hizo na hivyo
kuathiri thamani ya vipande vya Mfuko wa Umoja.

SURA YA UENDESHAJI WA MFUKO WA UMOJA

Kama ilivyokwishaelezwa, hisa zilizotolewa na Serikali kama mtaji na fedha zitakazoku-


sanywa kutoka kwa wawekezaji zitawekezwa kwenye mseto wa dhamana. Mtiririko wa
matukio yafuatayo umeonyeshwa kwenye Kielelezo Na. III ambacho kinatoa sura ya
shughuli za Mfuko wa Umoja.

Hatua ya 1: Kutoka kwenye mseto, mfuko utapata gawio na riba;

Hatua ya 2: Gawio na riba vinawekezwa mpaka kipindi cha mgao wa mapato


wakati gharama za lazima zinapoondolewa;

8. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
Hatua ya 3: Baada ya kuondoa gharama za lazima, kiasi kinachobaki
kinawekwa kwenye akaunti ya mgawanyo;

Hatua ya 4: Meneja anaweza kuwekeza sehemu ya mapato kama itaonekana


kuwa uwekezaji huo ni kwa maslahi ya wawekezaji.

Hatua ya 5: Fedha kwenye akaunti ya mgawanyo zitagawanywa kufuatana na


uchaguzi wa mwekezaji kama ifuatavyo:

(a) Wale waliochagua mpango wa kukua watapata vipande vya


nyongeza.

(b) Wale waliochagua mpango wa mapato watapokea fedha taslim.

Hatua 6: Kwa kuwa Mfuko wa Umoja ni mfuko wa wazi wawekezaji


wanaweza kuuzia mfuko vipande vyao au kununua vipande zaidi
kutoka kwenye mfuko.

KIELELEZO III
SURA YA SHUGHULI ZA MFUKO WA UMOJA

9. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
UPATIKANAJI WA VIPANDE

NI WAKATI GANI MTU ANAWEZA KUNUNUA VIPANDE KATIKA MFUKO


WA UMOJA?

Kuna njia mbili ambazo vipande vya Mfuko wa Umoja vinaweza kununuliwa. Vipande
vinaweza kununuliwa wakati wa kipindi cha toleo la kwanza (yaani vinapouzwa kwa
mara ya kwanza - IPO) na hivyo kufaidika na punguzo la asilimia thelathini (30%).
Vilevile vinaweza kununuliwa wakati wowote baada ya kipindi cha kizuizi cha mwaka
mmoja kinachoishia tarehe 31 Julai, 2006. Hii ni kwa sababu Mfuko wa Umoja ni mfuko
wa wazi unaoruhusu wawekezaji kuuza vipande vyao kwa Dhamana ya Uwekezaji
Tanzania na kuvinunua tena wakati wowote wanapokuwa na fedha za kuwekeza.

Baada ya kipindi cha kizuizi, vipande vinaweza kununuliwa (siku za kazi) katika kipin-
di cha mwaka mzima isipokuwa kipindi kisichozidi siku saba ambapo daftari la wana
vipande litakuwa limefungwa.

NI WAPI MWEKEZAJI ANAWEZA KUNUNUA VIPANDE KWENYE MFUKO


WA UMOJA?

Mauzo ya Vipande katika kipindi cha Mauzo ya Awali (IPO).


Maombi kwa ajili ya mauzo ya awali yanaweza kufanyika katika sehemu zifuatazo:-

(a) Matawi ya; CRDB Bank Limited, National Microfinance Bank, Shirika la
Posta, Benki ya Posta (Tanzania Postal Bank) na Akiba Commercial Bank
Limited.

(b) Ofisi za madalali wa Soko la Hisa la Dar es Salaam.

Mauzo ya Vipande baada ya Kipindi cha Kizuizi cha Mwaka Mmoja


Maombi kwa ajili ya mauzo baada ya kipindi cha kizuizi yanaweza kufanywa katika
sehemu zifuatazo:

(a) Matawi ya wakala atakayeteuliwa

(b) Ofisi za Dhamana ya Uwekezaji Tanzania

10. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
NI KWA VIPI MWEKEZAJI ATAFANYA MALIPO KWA AJILI YA MANUNUZI
YA VIPANDE?

Malipo kwa ajili ya ununuzi ya vipande katika kipindi cha mauzo ya awali na baada ya
kipindi cha kizuizi yanaweza kufanywa kwa fedha taslim, au hundi za benki kupitia kwa
wakala yoyote kati ya waliotajwa. Hundi iandikwe “ Mfuko wa Amana ya Kikundi cha
Umoja” (Umoja Unit Trust Scheme). Wawekezaji wanatahadharishwa kwamba malipo
ya kununua vipande vya mfuko yasifanywe kwa mtu au taasisi nyingine zaidi ya
mawakala waliotajwa ambao wanatambulika na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania.

WENYE VIPANDE KWENYE MFUKO WA UMOJA WANA HAKI ZIPI?

Wenye vipande vya Mfuko wa Umoja wanazo haki zifuatazo;


(a) Haki ya kufaidika na rasilimali za mpango na gawio la mapato kulingana na
walichokiwekeza katika mpango.

(b) Haki ya kupata taarifa kuhusu uwekezaji wa mpango kutoka Dhamana ya


Uwekezaji Tanzania kama ilivyoainishwa kwenye waraka wa makubaliano.

(c) (i) Haki ya kutumiwa muhtasari wa taarifa ya mwaka kuhusiana na mfuko


katika kipindi kisichozidi miezi minne tangu siku ya kufunga mwaka wa
fedha wa mfuko.

(ii) Muhtasari huo pia unatakiwa uwepo kwenye Ofisi za Dhamana ya


Uwekezaji Tanzania na matawi ya wakala kwa ukaguzi.

(iii) Taarifa za nusu mwaka zinatakiwa zitumwe kwa wenye vipande si zaidi
ya miezi miwili ya vipindi husika.

(d) Ili mtu akubali kuwekeza kwenye mfuko, inabidi taarifa muhimu zenye
kuhusiana na mfuko huo ziwe zimetolewa kwake. Taarifa hizo ni pamoja na
mambo ya msingi yahusuyo mfuko, sera ya uwekezaji, n.k. Mabadiliko yoyote
ya msingi kuhusiana na taarifa hizo yataweza kufanyika iwapo tu wawekezaji
watakuwa wameruhusiwa kuuza vipande vyao kwa thamani ya wakati huo na
taarifa hizo kuwa zimewekwa kwenye magazeti ya Kiswahili na kiingereza
yenye mzunguko mkubwa hapa nchini.

(e) Haki ya kukagua nyaraka zifuatazo kwenye ofisi za Dhamana ya Uwekezaji


Tanzania;

11. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
(i) Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ya mwaka 1994 kama
ilivyorekebishwa mwaka 1997

(ii) Kanuni za mwaka 1997 za Masoko ya Mitaji na Dhamana (Mifuko ya


Uwekezaji wa Pamoja)

(iii) Waraka wa Makubaliano wa Mfuko wa Umoja ambao ndio waraka rasmi


unaoanzisha Mfuko huo.

KUNA USHAHIDI GANI WA KUMILIKI VIPANDE?

Vipande vinavyonunuliwa kutoka kwenye mfuko wa uwekezaji wa pamoja ni mali ya


waliovinunua. Ushahidi wake ni hati za vipande (unit certificate). Hati hii ni karatasi
inayofanana na hati ya hisa inayotolewa na kampuni.

(a) Wenye vipande wote wana haki ya kupata hati za kumiliki vipande kulingana na
idadi ya vipande walivyonunua.

(b) Wawekezaji walioko kwenye mpango wa kukua watatumiwa taarifa ya


akaunti ikionyesha vipande wanavyomiliki kwenye mfuko. Hii ni kama taarifa
ya akaunti itolewayo na benki.

MAPATO YA MPANGO WA UMOJA YANAGAWANYWA VIPI?

Mgao wa mapato utafanywa iwapo kutakuwa na mapato ya ziada kama itakavyokuwa


imepitishwa na Bodi ya Wadhamini ya Dhamana ya Uwekezaji Tanazania. Kwa kuanzia
itakuwa mara moja kwa mwaka na baadaye kama itakavyoamuliwa na Bodi ya wad-
hamini.

(a) Mwenye vipande ambaye jina lake limesajiliwa kwenye daftari la mpango siku
itakayotangazwa kuwa ya kugawa mapato, na ambaye hayuko kwenye mpango
wa kukua atakuwa anastahili kupata mgao wa fedha taslim.

(b) Mgao wa mapato utafanywa kwa kuhamisha fedha kwenda kwenye akaunti za
wawekezaji ambao watakuwa wametoa taarifa kwa Dhamana ya Uwekezaji
Tanzania mahali akaunti zao zilipo au kwa kutoa hawala za fedha.

(c) Kuweka fedha kwenye akaunti na kutuma hawala ya fedha kutafanywa katika
kipindi kisichozidi siku tano za kazi.

12. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
(d) Wenye vipande walioko chini ya mpango wa kukua hawatapokea fedha taslim
kama mgao. Mapato ambayo yangetumwa kwao yatatumika kununulia vipande
zaidi kwenye mfuko kwa ajili yao kwa thamani halisi ya wakati huo.

(e) Wenye vipande walio katika mipango yote miwili ya kukua na mapato
watapata taarifa ya akaunti kwa ajili ya vipande vilivyoongezeka na fedha
taslim kutokana na mgao wa mapato.

(f) Katika kipindi kisichozidi siku kumi baada ya tarehe ya mgao wa mapato,
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania itatuma taarifa za akaunti kwa wenye vipande
ambao watakuwa wamepata vipande kutokana na kuwekezwa mapato yao.

KUHAMISHA MILIKI YA VIPANDE VYA MFUKO AU KUWEKWA REHANI.

Vipande vinavyotolewa chini ya Mpango wa Umoja vinahamishika (transferable). Pale


inapotokea kuhamisha kukahitajika, kunaweza kutekelezwa kwa kujaza fomu maalum
(Transfer form).

Vipande vya Mfuko wa Umoja vinaweza kuwa dhamana au rehani (pledged or mort-
gage)

(a) Utumiaji wa vipande kama dhamana au rehani unaruhusiwa kwa benki au


taasisi za fedha tu. Mwenye vipande anaweza kuweka vipande vyake
vikashikiliwa na benki au taasisi za fedha kama dhamana ya kupewa mkopo.
Vipande vinaweza kuwekwa dhamana kwa kujaza fomu ya kuomba vishikiliwe
na kutimiza taratibu nyingine kama itakavyohitajika. Baada ya Dhamana ya
Uwekezaji Tanzania kupata fomu husika, itaweka kumbukumbu kuwa vipande
kiasi fulani vya mwekezaji fulani vimezuiliwa kwa ajili ya taasisi fulani ya
fedha iliyotoa mkopo na hivyo anayevimiliki hawezi kuviuza au kuvihamisha
mpaka kuwe na ushahidi kuwa amelipa deni na vipande vyake kufunguliwa.

(b) Benki au taasisi ya fedha itakuwa na madaraka kamili ya kuuza au kuhamisha


vipande hivyo baada ya kutoa ushahidi/kuihakikishia Dhamana kuwa mkopaji
ameshindwa kulipa mkopo husika.

(c) Kuhusiana na vipande vilivyozuiliwa, hakutakuwa na uwezekano wa kuuzwa,


kuhamishwa au kubadilishwa kutoka kwenye mpango wa kukua kwenda
mpango wa mapato au kinyume chake mpaka kutakapotolewa hati ya kuruhusu
kuachiliwa vipande vilivyoshikiliwa kutoka kwa mkopeshaji.

13. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
HALI ITAKUWAJE IWAPO MWENYE VIPANDE ATAFARIKI?

Iwapo itatokea mwenye vipande amefariki, madai ya mirathi yatakuwa kama ifuaatavyo;

• Iwapo vipande vinamilikiwa na watu wawili kwa pamoja basi mrithi atakuwa ni
yule aliyebaki.

• Iwapo vipande vilikuwa vinamilikiwa na mtu mmoja, na marehemu aliacha


ameteua mrithi, vipande vitahamishiwa kwenye jina la mrithi huyo kama mmiliki.

• Pale ambapo vipande vilikuwa vinamilikiwa na mtu mmoja na marehemu


akawa hakuchagua mrithi basi vipande vitahamishiwa kwenye jina la msimamizi
wa mirathi.

UTHAMINI WA MALI YA MPANGO.

Thamani ya kila kipande inaweza kupatikana kwa kugawanya idadi ya vipande vya
mfuko kwa wakati huo ambayo kama ilivyotamkwa awali, mfuko wa Umoja utakuwa ni
mseto wa mizania wenye rasilimali za aina tofauti. Kwa wakati wowote ule, rasilimali
hizo lazima thamani yake ijulikane. Kwa kufanya hivyo, thamani ya rasilimali zote
kwenye mfuko zitajulikana. Madeni ya mfuko inabidi yatolewe ili kupata thamani halisi
ya mpango (Net Asset Value). Kwa hiyo, thamani halisi ya mpango inapatikana kwa
kuchukua thamani ya rasilimali za mfuko na kutoa madeni ya mfuko na wakati huo huo
bila kusahau mapato ambayo yameishajulikana japo hayajapokelewa na gharama
ambazo zinakisiwa (accruals and provisions)

Licha ya kufahamu thamani ya mfuko mzima, thamani ya kila kipande pia inaweza kuta-
futwa, thamani ya kila kipande inapatikana kwa kugawana thamani ya Mfuko kwa idadi
ya vipande vya Mfuko kwa siku hiyo ambayo hesabu hizo zinafanyika.

Ni wazi kuwa uthamini wa mali za Mfuko ni shughuli ngumu na yenye kuhitaji utaalam
; pamoja na hayo, mwongozo uliopo ni kuwa uthamini unafanyika kwa kuzingatia
thamani zinazotambulika kutoka kwenye soko.

Ili kuwawezesha wananchi na wawekezaji kufahamu thamani ya mfuko na thamani ya


vipande vyao, thamani ya Mfuko wa Umoja itatolewa kwa vyombo vya habari kwa ajili
ya kutangazwa kila siku ya Ijumaa wakati wa kipindi cha kizuizi na baada ya hapo
itakuwa ni kila siku ya kazi. Thamani halisi ya vipande itatangazwa kwenye magazeti
yenye kuuzwa kwa wingi nchini Tanzania. Thamani halisi ya vipande vilevile itakuwa

14. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
inapatikana kwenye tovuti ya Dhamana ya Uwekezaji Tanzania. (www.utt- tz.org)

MAMBO YA KUZINGATIA

a) Thamani ya mwanzo ya kipande kwenye Mpango huu ni sh 100/= (shilingi mia


moja tu).

b) Kuna “kipindi cha kizuizi” (lock-in-period) cha mwaka mmoja. Baada ya kipindi
hicho cha kizuizi, mfuko utaweza kuuza na kununua vipande kutoka kwa
wawekezaji. Bei ya kununulia na kuuzia itategemea thamani halisi ya wakati huo
(Net Asset Value) baada ya kutoa au kuongeza gharama ya huduma ambayo ni
asilimia moja (1%)
.
c) Kiwango cha chini cha kuwekeza wakati wa toleo la mwanzo ni sh 5,000/=
(shilingi elfu tano tu) kwa ajili ya kununua kiwango cha chini cha vipande
hamsini. Kutokana na punguzo la bei lililotolewa na Serikali, wawekezaji
wanaweza kuingia kwenye Mfuko wa Umoja kwa gharama ya sh. 3,500/=
. Wawekezaji hawatatozwa gharama zozote wakati wa mauzo ya mwanzo.

d) Mauzo yatakayofuata baada ya kipindi cha kizuizi yatakuwa katika mafungu ya


vipande kumi kumi.

e) Mwekezaji aliyebakiwa na vipande kumi anakubalika kuendelea kuwa mwana


mfuko. Iwapo mwekezaji huyo ataamua kuuza baadhi ya vipande vyake na
kufanya salio lake kuwa chini ya vipande kumi atalazimika kuuza vyote.

f) Mkataba wa kuuza vipande kwa Dhamana ya Uwekezaji Tanzania utachukuliwa


kuwa umekamilika “tarehe ya kupokelewa” isipokuwa pale ambapo maombi
yatakataliwa na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania.

g) Mauzo na manunuzi yatakuwa wazi kila siku ya kazi isipokuwa wakati wa kipindi
cha kizuizi (lock-in-period) na kipindi ambacho daftari la orodha ya wanavipande
litakuwa limefungwa kama itakavyotangazwa na Dhamana ya Uwekezaji
Tanzania.

h) Maombi yote ya kuuza au kununua vipande yatakayopokelewa na kukubaliwa


kwenye Ofisi za Dhamana ya Uwekezaji Tanzania baada ya saa sita kamili mchana
yatafanyiwa hesabu kulingana na thamani ya mpango (Net Asset Value) ya siku ya
kazi inayofuata.

15. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
i) Manunuzi ya vipande vinavyorudishwa na mwekezaji yatafanyiwa kazi iwapo
yatakuwa yameambatana na hati ya kumiliki vipande na fomu ya maombi
yakurudisha vipande ikiwa imejazwa kikamilifu (Re-purchase Form) na nyaraka
nyingine kama zitahitajika kulingana na maelekezo yatakayotolewa na Ofisi ya
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania.

j) Malipo kwa ajili ya vipande vya wawekezaji vitakavyokuwa vinanunuliwa na


Dhamana ya Uwekezaji Tanzania yatatumwa kwa wauzaji (wawekezaji) katika
muda usiozidi siku tano za kazi kuanzia siku ya kupokelewa kwa maombi ya kuuza
vipande hivyo kwenye ofisi za Dhamana ya Uwekezaji Tanzania fomu husika ziki
wa zimejazwa kikamilifu.

k) Inaruhusiwa kwa mwekezaji kuuza sehemu ya vipande vyake ili mradi salio la
vipande atakavyokuwa anamiliki wakati wowote lisiwe chini ya vipande kumi.
Manunuzi vile vile yatafanyika katika mafungu ya vipande kumi.

l) Hakutakuwa na riba itakayolipwa kwa mwenye kuuza vipande kwa kipindi amba
cho muuzaji atakuwa hajatumiwa fedha zinazotokana na mauzo ya vipande vyake.

m) Kwa vyovyote vile, Dhamana ya Uwekezaji Tanzania haitalazimika kufanya


yafuatayo:

(i) kununua vipande katika kipindi cha kizuizi kinachoishia tarehe 31 Julai,
2006;

(ii) kuuza au kununua vipande kwa siku ambazo Ofisi za Dhamana ya


Uwekezaji Tanzania zitakuwa zimefungwa kwa sababu maalum;

(iii) katika kipindi kisichozidi siku saba kwa wakati mmoja, au vipindi vingine
kama itakavyoamuliwa na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania wakati ambapo
daftari la orodha ya wenye vipande litakuwa limefungwa.

KODI

Kodi ni sehemu muhimu katika shughuli za uwekezaji, kwa hiyo ni muhimu kwa
wawekezaji kwenye Mfuko wa Umoja kufahamu baadhi ya masuala ya kodi. Taarifa
inayotolewa katika kipeperushi hiki ni kwa ajili ya ufahamu wa jumla .Inashauriwa
kwamba wawekezaji wawasiliane na wataalam mbalimbali wa maswala ya kodi ili
kufahamu kodi watakazolipa kutokana na kushiriki kwao kwenye Mpango huu.

16. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


Makala ya Habari kwa Umma
Hadi siku kipeperushi hiki kinapotolewa sheria za kodi zilizopo zina maelekezo yafu-
atayo:

• Mapato ya mfuko yanatozwa kodi kwa kiwango cha kawaida cha makampuni.

• Gawio la faida kutokana na hisa zilizonunuliwa na mfuko ambazo


zimeorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam linatozwa kodi ya
aslimia tano (5%) badala ya kiwango cha kawaida cha aslimia kumi (10%)

• Mgawanyo wa mapato unaolipwa kwa wenyevipande haukatwi kodi.

17. Dhamana ya Uwekezaji Tanzania


MAANA YA MANENO

Mawakala wa Kupokea
Hizi ni taasisi ambazo katika kipindi cha mauzo ya awali zitashiriki; kutoa fomu za
maombi, kusaidia wawekezaji kujaza fomu na kuchukua fedha kutoka kwa wawekezaji
ili kuziwasilisha kwenye Dhamana ya Uwekezaji Tanzania.

Mpango wa Kukua
Ni mojawapo ya utaratibu ambao wawekezaji wanaweza kuufuata ili badala ya kupokea
fedha taslimu (kama gawio la faida) wapewe vipande vya nyongeza kwa thamani ya
wakati huo.

Punguzo
Hiki ni kiasi cha pesa kinachopunguzwa kutoka kwenye thamani ya mwanzo ya vipande
vya Mfuko wakati wa kipindi cha mauzo ya awali

Mauzo ya Awali
Mauzo ya vipande au hisa yanayofanywa na mpango wa uwekezaji wa pamoja au kam-
puni kwa mara ya kwanza.

Mauzo ya Mwanzo
Hii ni sawa na mauzo ya awali ila hutumika kutofautisha zoezi lenyewe na mauzo ya
baadaye ya vipande ambayo kwa utaratibu wa Mfuko wa Umoja yatafanywa baada ya
kipindi cha kizuizi cha mwaka mmoja.

Mseto wa Uwekezaji
Huu ni mchanganyiko wa dhamana/rasilimali ambazo mfuko wa umoja utawekeza.

Kipindi cha kizuizi


Hiki ni kipindi cha mwaka mmoja kinachoishia tarehe 31 Julai, 2006 wakati ambapo
mfuko hautakuwa unaendesha zoezi la kuuza na kununua vipande.

Thamani Halisi ya Mfuko (Net asset Value - NAV)


Hii ni thamani ya mfuko inayofikiwa baada ya kutoa madeni yote na kuzingatia mapato
yanayotegemewa ambayo hayajapokelewa na gharama zinazokisiwa.

Hawala ya Fedha (Postal Money Order)


Ni njia ya malipo inayotumiwa na Shirika la Posta Tanzania
Kurudisha (Re-Purchase)
Hii ni pale ambapo mfuko unanunua vipande kutoka kwa wawekezaji ambavyo hapo
awali viliuzwa na kushikiliwa nao.

Mauzo
Haya ni mauzo ya vipande yanayofanywa na mfuko. Inawezekana yakawa ni mauzo ya
awali au mauzo yanayofuata baada ya kuisha kwa kipindi cha kizuizi.

Mdhamini
Mdhamini ni taasisi inayoanzisha Mpango, kwenye Mfuko wa Umoja, mdhamini ni
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT).

Taarifa ya Akaunti
Hii ni aina maalum ya taarifa ya akaunti inayotolewa na mfuko kwa mwenye vipande
ikionyesha idadi ya vipande anavyomiliki kwenye mfuko. Ni kama taarifa ya akaunti ya
benki ambayo huonyesha salio kwenye akaunti ya mteja.

Mauzo Baadaye
Kama ilivyoelezwa hapo juu, haya ni mauzo ya vipande vya mfuko baada ya kipindi cha
kizuizi (lock –in –period)

Waraka wa Makubaliano
Huu ni waraka unaothibitisha kusajiliwa kwa dhamana ambayo ni mpango wa uwekeza-
ji wa pamoja. Waraka wa Makubaliano unatamka kuanzishwa kwa Mpango, wajibu wa
pande zinazohusika (Meneja na Mwangalizi), haki za wenye vipande n.k. Waraka wa
Makubaliano kwa kuanzia unawahusisha Meneja na Mwangalizi. Kila mwenye kipande
anakuwa sehemu ya Waraka wa Makubaliano anapojiunga na mpango.

Kipande
Hiki ni kipande kinachotolewa na mfuko kikiwakilisha haki alizonazo mwenye kipande
kutokana na mali na mapato ya mfuko kulingana na uwekezaji wake. Ni kama hisa
kwenye kampuni ingawa haki za wenye hisa zinatofautiana kiasi fulani na haki za wenye
vipande kama ilivyoelezwa katika kipeperushi hiki.

Hati ya Vipande
Hii ni hati anayopewa mwenye vipande ikiwa ni ushahidi wa kumiliki vipande katika
mfuko.

Mwenye Kipande
Ni mtu au taasisi inayokubaliwa na mfuko kama mmiliki halali wa vipande vya mfuko.

You might also like