“Kamwe sitatikisika! Ee Mungu, kwa fadhili yako,* Umeniimarisha kama mlima mkubwa. Lakini ukajificha mbali nami,* Nami nikaogopa. Nilikulilia wewe, Ee Mungu,* Nilikusihi wewe Mungu. “Je, nikifa utapata faida gani?* Kuna faida gani nikishuka shimoni? Je, waliokufa wanaweza kukusifu?* Je, wanaweza kutangaza wema wako mkuu? Usikie, Ee Mungu, unihurumie,* Ee Mungu, unisaidie!” Wewe umegeuza ombolezo langu* Kuwa ngoma ya furaha. Umeniondolea huzuni yangu,* Ukanijalia furaha tele tele. Basi, sitakaa kimya,* Bali nitakuimbia sifa. Ee Mungu, Mungu wangu,* Nitakushukuru milele.