You are on page 1of 1

Lakini asubuhi husikika sauti ya furaha.

Mimi katika usitawi wangu, nilisema,*


“Kamwe sitatikisika!
Ee Mungu, kwa fadhili yako,*
Umeniimarisha kama mlima mkubwa.
Lakini ukajificha mbali nami,*
Nami nikaogopa.
Nilikulilia wewe, Ee Mungu,*
Nilikusihi wewe Mungu.
“Je, nikifa utapata faida gani?*
Kuna faida gani nikishuka shimoni?
Je, waliokufa wanaweza kukusifu?*
Je, wanaweza kutangaza wema wako mkuu?
Usikie, Ee Mungu, unihurumie,*
Ee Mungu, unisaidie!”
Wewe umegeuza ombolezo langu*
Kuwa ngoma ya furaha.
Umeniondolea huzuni yangu,*
Ukanijalia furaha tele tele.
Basi, sitakaa kimya,*
Bali nitakuimbia sifa.
Ee Mungu, Mungu wangu,*
Nitakushukuru milele.

You might also like