Professional Documents
Culture Documents
Maombolezo Ya Ashura
Maombolezo Ya Ashura
ASHURA
Toleo la Kwanza
Kimekusanywa na:
Musabah Shaban Mapinda
Kimetolewa na Kimechapishwa na
Bilal Muslim Mission of Tanzania
S.L.P. 20033
Dar es Salaam - Tanzania
Haki za kunakili imehifadhiwa na:
Bilal Muslim Mission of Tanzania
Majlis ya Kwanza
Hali ya Bara Arabu kabla ya Uislamu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 1
Majlis ya Pili
Makundi matatu: Muumini, Mwislamu na Mnafiki . . . . . . . . . . . . . 7
Majlis ya Tatu
Kosa kubwa limetendeka . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .13
Majlis ya Nne
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah . . . . . . . . . . . . . . . . . . .18
Majlis ya Tano
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah . . . . . . . . . . . . . . . . . . .23
Majlis ya Sita
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah:
Mtume Kuhamia Madina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 29
Majlis ya Saba
Kisasi cha Banu Umayyah dhidi ya Mtume (s.a.w.w.) . . . . . . . . . . 34
Majlis ya Nane
Fathu Makka . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .38
Majlis ya Tisa . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 44
Majlis ya Kumi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 48
Kwa hiyo basi, kila unapoisoma tarekh, unakuta kuwa, katika nchi
ya Hijaz ambako ndiko uliko anzia Uislamu, kulikuwa na mvutano
au mapambano kati ya koo mbili za ki-Quraish; yaani ukoo wa Banu
Hashim na ukoo wa Banu Umayyah.
1
Vita vya mara kwa mara baina yao, na mauwaji hasa ya watoto wa
kike, yalikuwa ni mambo yaliyoenea sana huko bara Arabu. Hayo
na mengine mengi yaliifanya hali ya eneo hili kuwa kama kituo cha
maovu.
Imam Ali bin Abi Talib (a.s.) ameieleza hali ya waarabu hao
ilivyokuwa kabla ya kuja kwa Uislamu amesema: “Nanyi enyi
wa-Arabu mlikuwa na dini mbaya mno, na mlikuwa (mkiishi)
katika eneo baya mno.” (ufafanuzi wa hali ya waarabu, na dini zao
unahitajika). (Qur’an, 81:8) Na mtoto mwanamke aliyezikwa hai
atakapoulizwa.
2
Kwa muda mrefu nafsi za watu zilikuwa zikisubiri kwa hamu
mkombozi dhidi ya madhila yaliyokuwa ndani ya jamii yao.
Dhulma, utumwa, mauwaji na maovu mengine mengi yalipata
ufumbuzi baada ya kuja Uislamu.
Kuomboleza kifo cha Sayyidina Husein bin Ali bin Abi Talib
(a.s.), kwa kuyakumbuka mateso yaliyompata, ni sunna ya Mtume
Muhammad (s.a.w.w.). Wanachuoni wa somo la historia ya
3
Ki-Islamu wamenukuu matukio kadhaa yanayo onesha kwamba
Mtume Muhammad (s.a.w.w.), aliomboleza kifo cha mjukuu wake
huyu muda mfupi tu baada ya kuzaliwa kwake.
4
na nikampakata mapajani mwangu, kama alivyosema Mjumbe wa
Mwenyeezi Mungu (s.a.w.w.).”
5
Kuna riwaya nyingi mno zinazohusu kitendo hiki cha bwana Mtume
kuomboleza kifo hiki cha Sayyidina Husein (a.s.), kiasi kwamba si
rahisi kuzitaja zote. Lakini hazipungui riwaya kumi na tisa ambazo
baadhi yake bwana Mtume (s.a.w.w.) alilieleza jambo hili ndani
ya nyumba zake, na kuna wakati mwingine alilieleza mbele ya
Maswahaba wake. Na katika kila mara alipolieleza, hakuwacha kulia
kwa huzuni kutokana na kitendo kitakacho fanywa na umma wake
baada yake dhidi ya watu wa nyumbani mwake.
6
Majlis ya Pili :
Makundi Matatu: Muumini, Mwislamu na Mnafiki
7
Ni jambo lililo wazi, ya kwamba: Mafunzo ya Mtume (s.a.w.w.)
yalilenga kuwapata watu watakao kuwa tayari kutoa kila kilicho
chao, kuanzia mali hadi nafsi zao kwa ajili ya kupambana na
udhalimu na uovu uliyokuwa ukitawala enzi hizo kabla ya kuja dini
ya ki-Islamu. (Mfano urejewe kwa sahaba Amri bin Jumuuh).
Aya hii kwa ujumla wake inakusudia kutonesha kundi la pili katika
Uislamu. Hili ni kundi la Waumini.
8
Uislamu kadhalika una sehemu kuu mbili ambazo moja ni ile ya
dhahiri, na nyingine ni ile ya ndani au tuseme kuwa ndiyo imani ya
kweli iliyoko moyoni.
Wanafiq:
Wanafiki ni wale watu ambao imani kamwe haikupta nafasi ya
kuingia katika roho zao. Ukweli wa mambo watu wa aina hii kamwe
hawakukubali Uislamu, bali wanautumia Uislamu kwa maslahi yao
na tamaa zao binafsi.
9
Kwa mukhtasari ni kwamba: Daraja ya muumini iko juu zaidi
kuliko daraja ya mwislamu. Na ama unafiki; wenyewe pia ni siyasa
ya shetani. Kumbuka vita ya Siffin, na kunyanyuwa mishafu.
10
Nukuu ya kwanza: “Nabii Yaqub bin Is-Haqa bin Ibrahim (a.s.)
alimlilia mwanawe Yusuf (a.s.) kwa muda wa miaka mingi.
Kilio hiki cha Nabii Yaqub (a.s.) hakikuwa ni kwa sababu ya kuuliwa
kwa mwanawe, bali Nabii Yusuf bin Yaqub alitoweka tu machoni
mwa baba yake.
Qur’an inaeleza kuwa Nabii Yaqub alilia mpaka macho yake yakawa
meupe. “... Oooh! Majonzi yangu kwa Yusuf!!! Na macho yake
yakawa meupe kwa huzuni, naye alikuwa amejawa na huzuni.”
(Qur’an, 12:84)
11
Siku ya qiyama kila jicho litalia isipokuwa lile jicho lililolia kutokana
na masaibu ya Husein, jicho hilo litakuwa lenye furaha kwa neema
ya peponi.”4
12
Majlis ya Tatu :
Kosa Kubwa Limetendeka
13
Banu Umayyah tangu hapo zamani walisifika kwa maovu ndani ya
jamii ya wa-Arabu huko Hijaz.
Hadithi ya Karbala:
Mnamo mwezi wa Rajabu mwaka wa sitini hijiriya, khalifa wa Ki-
Banu Umayyah kwa jina Muawiyah bin Abi Sufiyan alifariki dunia.
Wakati Muawiyah anafariki dunia, mwanawe aliyekuwa akiitwa
Yazid, alikuwa huko Hauraan.
14
Ili kukifahamu vyema kisa cha Sayyidina Husein bin Ali (a.s.) na
yaliyompata huko Karbala katika nchi ya Iraq, ni vizuri tukaeleza
maandalizi yaliyofanywa na Muawiyah bin Abi Sufian katika suala
la kumrithisha ukhalifa Yazid bin Muawiyah.
Hadithi ya Karbala:
Jinsi Yazid alivyourithi Ukhalifa kutoka kwa Muawiyah:
Mughira bin Shu’bah alikuwa gavana wa Basra katika zama za
ukhalifa wa Muawiyah bin Abi Sufiyan. Kuna wakati Muawiyah
alikusudia kumuondoa madarakani Mughira bin Shu’bah. Taarifa
za kuuzuliwa ugavana wa mji wa Basra zilipomfikia Mughira,
alifunga safari kwenda Shamu ili kuomuona Muawiyah bin Abi
Sufiyan. Alipofika huko alikaribishwa na kisha akatoa rai kwa
Muawiyah kwamba, hakuna mwenye kustahiki ukhalifa baada ya
yeye Muawiyah ila ni Yazid mwanawe.
15
zinaendea ukingoni, alimwita na kuwambia Yazid kwamba: “Ewe
mwanangu! Nimekuandalia mambo vizuri na maadui nimekwisha
kuwadhibiti kwa ajili yako. Na waarabu nimewafanya wawe watiifu
kwako na nimekukusanyia mambo ambayo hakuna mtu yeyote
aliyewahi kuyakusanya.”
Si hivyo tu, bali alimtaka mwanawe huyu awe mkarimu kwa watu
wa hijazi kwani huko ndiko kwenye asili yake. Kadhalika alimuasa
mno kutokana na watu wa Iraq akamwambia: “Endapo watu wa
Iraqi watakutaka kumuuzulu gavana (yeyote yule) kila siku basi
fanya hivyo, kwa sababu kumuuzulu gavana ni jambo jepesi mno
kuliko kukabiliwa na mapanga laki moja.”
16
Maelezo haya ni kwa ufupi sana kuhusu maandalizi yaliyofanywa
na Muawiyah bin Abi Sufiyan kumrithisha mwanawe Yazid
ukhalifa juu ya wa-Islamu. Insha Allah majlis ijayo tutaona ni
hatua gani alizochukua Yazid kujiimarisha mwanzoni tu mwa
utawala wake baada ya kifo cha baba yake.5
17
Majlis ya Nne :
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah
Amma Harb bin Umayyah, naye ni kama baba yake kwa maovu.
Bwana huyu alipanga njama za mauaji dhidi ya myahudi mmoja
aliyekuwa jirani ya Abdul-Muttalib.
Ibn Athiir ndani ya kitabu chake cha tarekh anasema kuwa: “Abdul-
Muttalib alikuwa na jirani yake myahudi kwa jina akiitwa Udhyah.
Myahudi huyu alikuwa ni mfanya biashara na alikuwa na mali
nyingi. Kutokana na utajiri wa myahudi huyu Harb bin Umayyah
aliingiwa na chuki kubwa dhidi yake.”
18
Ibn Athiir anaendelea kueleza anasema: “Harb alikodi vijana wa
ki-Quraish ili kumuuwa yule myahudi na kuchukuwa mali zake.
Amir bin Abdi Manaaf bin Abdid-Daar na Sakhru bin Amri bin
Ka’bi At-Taimi (babu yake Abu Bakr) ndiyo waliyomuuwa yule
myahudi. Kwa bahati mbaya Abdul-Muttalib hakufahamu ni nani
aliyemuuwa jirani yake, lakini alifanya uchunguzi na hatimaye
alifahamu kuwa vijana wale ndiyo waliyo muuwa.
Hadithi ya Karabala:
Majlis iliyopita, katika hadithi ya Karbala, tulieleza namna
Muawiyah alivyompa nasaha Yazid juu ya mambo kadhaa ikiwemo
jinsi yeye Muawiyah alivyofanikiwa kuwadhibiti maadui zake, na
kwamba hakuna kiongozi aliyefanikiwa kumuandalia mrithi wake
kama alivyofanya yeye kwa mwanawe huyu.
19
lolote toka kwa adui yako, basi waombe msaada. Na ukishapata
ushindi mara moja warudishe watu hawa mjini kwao, kwani
endapo watakaa katika mji usiyokuwa wa kwao, mwenendo wao
utabadilika.”
20
ambao hapo kabla walikataa kumbai Muawiyah bin Abi Sufiyan.
Ndipo Yazid alipomwandikia barua Walid kumueleza habari ya kifo
cha Muawiyah.
21
Abdallah bin Zubair alimwambia Husein (a.s.) kwamba: “Kuna nini
kwa mtu huyu kutuletea ujumbe saa hizi, ambapo hana kawaida
ya kuwa na vikao katika nyakati kama hizi?” Imam Husein bin Ali
(a.s.) akamjibu Bin Zubair akasema: “Nadhani kwamba yule muovu
wao amekufa, na hapana shaka ametuita ili atulazimishe kula kiapo
cha utii kabla habari za kifo hiki hazijaenea miongoni mwa watu.”
Abdallah bin Zubair naye akasema: “Nami pia sidhani kama kuna
jambo jingine lisilokuwa hili, sasa je! Utafanya nini?” Imam Husein
(a.s.) akasema: “Sasa hivi mimi nitawakusanya vijana wangu kisha
nitakwenda kwake. Vijana wangu nitawakalisha mlangoni halafu
mimi nitaingia ndani.”
22
Majlis ya Tano :
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah
Miongoni mwa sababu zilizofanya Uislamu uwe hivi ulivyo leo hii,
Banu Umayyah wamechangia kwa asilimia kubwa mno.
Kuna wakati walimtuma Abdallah bin Abi Rabia‘ na Amr bin Al-
A’as waende kwa Najjaashi, yule mfalme wa Uhabeshi, ili kumtaka
awafukuze waislamu waliyohamia huko kukimbia mateso ya
Maquraish.
23
ndiyo wale waliyofanya mateso makubwa dhidi ya waislamu
wanyonge kama vile; Bilal (mwadhini wa Mtume (s.a.w.w.)),
Ammaar bin Yaasir na baba yake na mama yake na wa-Islamu
wengine wengi.
24
Watu hao walikuwa wengi, kama ifuatavyo: Utbah na Shaibah
ambao ni watoto wa Rabia‘, Uqbah bin Abi Muiit, Abu Sufiyan na
Al-Hakam bin Abil-A’s. Wengine ni Al-A’s bin Waail As-Sahmi
ambaye ni baba wa Amr, na watoto wa ami yake ambao ni Nabiih
na Manbah.
Hadithi ya Karbala:
Katika majlis iliyopita ndani ya hadithi ya Karbala, tuliona jinsi
Sayyidina Husein (a.s.) alivyokuwa na tahadhari kutokana na
madhara yanayo weza kutokea kwenye kikao baina yake na gavana
wa Madina, Walid.
Kwa hali hiyo basi, Sayyidina Husein (a.s.) alipofika mlangoni kwa
Walid aliwaambia wafuasi wake kuwa: “Mimi naingia ndani, basi
nitakapokwiteni au mkisikia sauti yangu imepaa juu ingieni nyote
kwa pamoja, vinginevyo bakiyeni hapa mpaka nitoke.”
25
Walid bin Utbah aliitumia fursa hiyo kumsomea Sayyidina Husein
(a.s.) barua kutoka kwa Yazid inayoeleza habari za kifo cha
Muawiyah bin Abi Sufiyan, kisha akamtaka Sayyidina Husein (a.s.)
ale kiapo cha utii mbele yake kwa niyaba ya Yazid.
26
kamwe hutampata. Usimruhusu kutoka mpaka kwanza ale kiapo, na
akikubali hakuna neno, lakini akikataa mkate shingo yake.”
27
Ndani ya kisa hiki cha Sayyidina Husein bin Ali (a.s.), kuna watu
wengi wanahusika kutajwa kwa namna hii au ile. Tuonavyo sisi si
muhimu sana kuendelea kuwataja watu hao kila hatua inayoendelea
katika kisa hiki, japokuwa hapo mwanzoni tuliwataja. Watu hawa
ni kama vile Abdallah bin Zubair na Abdallah bin Umar ambao pia
waliendelea kupelekewa wajumbe ili waonane na Walid kwa ajili ya
kula kiapo cha utii.
28
Majlis ya Sita :
Kizazi cha Hashim na Kizazi cha Umayyah :
Mtume Kuhamia Madina
29
na mkawalilia kwa kusoma mashairi (ya maombolezo) mtaondosha
hasira zenu na chuki zenu, na kwa hali hiyo hamtakuwa tena na ua-
dui dhidi ya Muhammad na masahaba wake.”10
Hadithi ya Karbala:
Tumeona ndani ya majlis yetu iliyopita kwamba Sayyidina Husein
(a.s.) aliondoka kwenye ile baraza ya Walid moja kwa moja
akaelekea nyumbani kwake. Alibakia hapo Madina usiku ule,
ambao ulikuwa ni usiku wa kuamkia siku ya Jumamosi mwezi
ishirini na saba Rajab, mwaka wa sitini hijiriyyah.
30
kwamba: “Ewe Baba Abdillah! Mimi ninayo nasaha kwa ajili yako,
nakuomba unitii (katika nasaha hiyo).” Sayyidina Husein (a.s.)
akasema: “Ni nasaha gani hiyo, hebu sema nisikilize?”
Basi pale pale Sayyidina Husein (a.s.) alijibu akasema: “Innaa lillahi
wa Innaa Ilaihi rajiuun! Sasa Uislamu tuuage (kwa heri ya kuonana),
kwa hakika ummah umepata mtihani kwa kuwa na kiongozi mfano
wa Yazid.” Mazungumzo kati ya wawili hawa yalikuwa marefu kiasi
kwamba Marwan aligeuka akaondoka hali ya kuwa amekasirika.
31
akaanza kuomba kwa kusema: “Ewe Mwenyeezi Mungu! Hili ni
kaburi la Mtume wako Muhammad (s.a.w.w.). Bila shaka Wewe
Unayafahamu mambo yote yaliyonifika. Ewe Mwenyeezi Mungu!
Mimi nayapenda mema na ninayachukia maovu. Ewe Mola
uliyetukuka! Nakuomba kwa utukufu wa kaburi hili na yule
aliyemo, Unichagulie maamuzi ambayo Wewe Mwenyewe na
Mjumbe wako Mtayaridhia.” Kisha baada ya maombi haya,
Sayyidina Husein (a.s.) akalia sana.
32
Alijiandaa na akatoka mjini Madina usiku wa kuamkia Jumapili
kuelekea Makka akiwa na wanawe na baadhi ya ndugu zake. Ndani
ya msafara huo watoto wa Sayyidina Hasan bin Ali bin Abi Talib
walikuwa miongoni mwa watu aliofuatana nao.
33
Majlis ya Saba :
Kisasi cha Banu Umayyah dhidi ya Mtume (s.a.w.w.)
Katika vita hii ya Uhud, Hind binti Utbah, mke wa Abu Sufiyan,
alikuwa mhamasishaji mkubwa wa chuki dhidi ya Mtume na
waislamu. Na ni mwana mke huyu ndiye aliyemkodi Wahshi kwa
ajili ya kumuuwa Sayyidina Hamza, ami yake Mtume (sa.w.w.).12
Hakutosheka na kumuuwa tu, bali alimpasua na kula ini lake.
34
Badri. Vita hii ilikuwa baina ya washirikina wa Makka na waislamu,
na ilipiganwa mnamo mwaka wa tatu wa hijra.
Hadithi ya Karbala:
Baada ya kueleza sababu zilizomfanya Sayyidina Husein bin Ali
(a.s.) akatae kula kiapo cha utii kwa Yazid, sasa turejee tena Ma-
dina na tuyaone mazingira ya safari yake kutoka Madina kuelekea
Makka. Vile vile tutaeleza hali ya mambo ilivyokuwa hapo Makka
baada ya kuwasili kwake.
35
alipo elekea upande wa Madyan alisema: Huenda Mola wangu Mlezi
ataniongoza njia iliyo sawa.”
36
hakufanya haraka kuwaadhibu, bali baadaye aliwaadhibu kwa
adhabu kali. Basi muogope Mwenyeezi Mungu ewe baba Abdur-
Rahman na wala usiwache kunisaidia.”
37
Majlis ya Nane :
Fathu Makka
38
unathamini mno udugu! Namuapa Mwenyeezi Mungu, bila shaka
jambo hilo nimekwisha kulitambua, kwani lau angekuwepo Mungu
mwingine asiyekuwa yeye, basi angetusaidia.”
Nukta Muhimu:
Ibn Hisham ndani ya kitabu chake Siraatun-Nabiyyi ameandika
hivi: Al-Harth bin Hishaam na Abu Sufiyan walipomsikia
mwadhini anasoma adhana; Hisham alimwambiya Abu Sufiyan:
“Ama Wallahi kama mimi ningekuwa najua kuwa Muhammad ni
Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu, basi bila shaka ningemfuata.” Abu
Sufiyan alijibu akasema: “Mimi sisemi kitu.....”
Ama Hind, mke wa Abu Sufiyan, huyu naye alisilimu kwa kukosa
budi kama mumewe. Mama huyu alipofika mbele ya Mtume
(s.a.w.w.) ili asilimu, Mtume alimwambiya: “Nipe baia ya
kwamba hutawauwa watoto wako.” Hind alijibu akasema: “Ama siye
tuliwalea watoto wetu walipokuwa wadogo, walipokuwa wakubwa
wewe ukawauwa siku ile Badri.” Mtume akasema: “Na unipe baia
ya kwamba hutazini.” Hind alijibu akasema: “Hivi kweli mwanamke
aliye huru atazini?” Mtume (s.a.w.w.) alimgeukia Abbas bin Abdil-
39
Muttalib, akatabasamu. Kwa nini Mtume alimtazama Abbas bin
Abdil-Muttalib kisha akatabasamu?
Mazingatio:
Abu-Talib baba yake Imam Ali (a.s.), na Abu Sufiyan, nani
mwislamu?
Hadithi ya Karbala:
Bila shaka bado tunakumbuka jinsi Sayyidina Husein (a.s.)
alivyoshindwa kuendelea na ibada ya hijja pale Makka na
ikamlazimu kuutoka mji huo wa amani hali ya kuwa anangojea nini
kitamtokea.
40
Watu hawa walipokamilika, Suleiman bin Surad Al-Khuzzai
alisimama akawaambia: “Kwa hakika Muawiyah amekufa, na
Husein bin Ali amekataa kuwatii wale waliojitwalia mamlaka na
amekwisha kuondoka Madina na sasa hivi yuko Makka.”
Wale watu walijibu wakasema: “Sisi tuko tayari kutoa nafsi zetu kwa
ajili yake na tutampiga adui yake.”
Baada ya ahadi hii kutoka kwa jamaa hawa, bwana Suleiman bin
Surad Al-Khuzzai aliwaambia: “Basi mwandikieni.”
41
Hapana shaka kwamba, huyu Nu’maan (liwali wa hapo mjini Kufah)
hatushirikiani naye kwenye ibada ya Ijumaa wala hatutoki pamoja
naye kwenye swala ya Idi.
42
Sababu ya pili ni kwamba, waislamu walikuwa bado wanakumbuka
ule mkataba kati ya Muawiyah na Sayyidina Hasan (a.s.) kuhusu
ukhalifa. Mkataba huo ulikuwa unasema kuwa:
“Ikiwa Sayyidina Hasan (a.s.) atatangulia kufa basi Muawiyah
aurudishe ukhalifa ndani ya nyumba ya Mtume (s.a.w.w.).”
43
Majlis ya Tisa
Kipindi hiki cha miaka sabini na nne tangu kuja kwa dini ya
ki-Islamu, kilikuwa ni kipindi cha misuko suko mingi ikiwemo
upinzani wa Maquraishi wakiongozwa na Banu Umayyah dhidi ya
Mtume na waislamu. Kadhalika Banu Umayyah walifanya mateso
mengi na mauwaji ya wafuasi wa dini hii tukufu.
44
uchache wao kwa idadi, lakini walipata ushindi mkubwa dhidi ya
maquraish.
Hadithi ya Karbala:
Majlis iliyopita tulisoma barua ya watu wa mji wa Al-Kufah kwenda
kwa Sayyidina Husein bin Ali (a.s.), na tukaona ahadi yao ya kutaka
kushirikiana naye ili awaongoze, na kwamba wako tayari kujitolea
nafsi zao kwa ajili yake.
Baada ya siku mbili tena, watu wa mji huu walimtuma Hani bin
45
Hani As-Subai na Said bin Abdallah Al-Hanafi waende Makka kwa
Sayyidina Huseina (a.s.), kumpelekea barua ambayo ilikuwa na
maneno yafuatayo:
Bismillahir-Rahamanir-Rahim.
Kwa Husein bin Ali (a.s.), barua kutoka kwa wafuasi wake miongoni
mwa waumini na waislamu. Amma baada ya salaam: “Njoo haraka;
kwa hakika watu wanakusubiri, hawana rai nyingine isipokuwa
wanakusubiri wewe. Basi fanya haraka tena haraka sana.”
46
barua zenu. Wao wamefika mwisho miongoni mwa wajumbe wenu
mliowatuma.
47
Majlis ya Kumi
48
hawakujali wala kukumbuka tangazo la Ghadir. Waligombea
uongozi ule wakaacha nidhamu aliyoiweka Mtume (s.a.w.w.).
Walipitisha maamuzi yao na kumuweka Abu Bakri kuwa khalifa
baada ya Mtume (s.a.w.w.).
Hadithi ya Karbala:
Tumekwisha kuona jinsi barua nyingi kutoka mji wa Al-Kufah
zilivyokuwa zikitumwa kwa Sayyidina Husein (a.s.) wakati akiwa
mjini Makka. Na barua zote zilikuwa zinamtaka aende huko ili
akawaongoze watu wa mji ule.
49
Watu hawa kila wanapokusanyika ndani ya nyumba alimofikia
Muslim bin Aqil, yeye huwasomea barua ya Sayyidina Husein (a.s.),
jambo ambalo lilikuwa linawaliza. Bila shaka walikuwa wakilia
kutokana na shauku yao juu ya Sayyidina Husein (a.s.).
50
“Hakika Muslim bin Aqil amefika hapa Al-Kufah, na watu tayari
wamekula kiapo cha utii kwake kwa niyaba ya Husein bin Ali. Basi
iwapo wewe unaitaka nchi hii ibakie mikononi mwako, mlete mtu
imara atakayesimamia maslahi yako na atafanya vile ambavyo wewe
unamfanyia adui yako. Huyu Nuuman ni mtu dhaifu au pengine
anajifanya dhaifu.”
51
Majlis ya Kumi na Moja
Umar bin Khatab alipoiona hali ile alifanya haraka kumpa mkono
wa baia Abu Bakr, na akawataka waliyo hudhuria kikao kile
wamuunge mkono.
Wakati yote haya yanatendeka, Imam Ali bin Abi Talib (a.s.) na watu
wa nyumba ya Mtume walikuwa wameshughulika kuandaa mwili
wa Mtume (s.a.w.w.) kwa ajili ya maziko.
52
walimtaka Imam Ali (a.s.) awe khalifa, lakini hakuwakubalia
akasema: “Niwacheni; tafuteni mwingine asiyekuwa mimi.”
Baada ya Imam Ali (a.s.) kukubali uongozi, kwa bahati mbaya sana
alikabiliana na upinzani mkali uliyokuwa unaongozwa na Banu
Umayyah.
Wote hawa kila mmoja kwa wakti wake alizusha vita dhidi ya
Sayyidina Ali (a.s.), kiasi kwamba kipindi cha miaka minne ya
uongozi wake kiliandamwa na vita na upinzani wa kila aina.
53
Kama ilivyokuwa katika zama za Mtume (s.a.w.w.), Banu Umayyah
walijaribu kuuangamiza Uislamu wakiwa nje ya dini wakashindwa,
na walipojisalimisha pia wakashindwa. Katika kipindi hiki lilikuwa
ni jaribio jengine la kutaka kuungamiza Uislamu wakiwa ndani ya
dini.
Hadithi ya Karbala:
Majlis iliyopita tumeeleza kuwasili kwa mjumbe wa Imam
Husein (a.s.) bwana Muslim bin Aqil mjini Al-Kufah na jinsi
alivyopokelewa na watu wa mji ule.
54
habari kwamba Nuuman ni mtu dhaifu, na vile vile kauli yake
si nzuri.” Kisha alimsomea barua zile, halafu akamwambiya: “Je!
Unayo maoni gani, nani nimpe uliwali wa mji wa Al-Kufah?”
55
Tabari anaeleza kwamba: Kabla ya hapo, Sayyidina Husein (a.s.)
aliwaandikia barua watu kadhaa wa mji wa Basra, na akaeleza humo
haki aliyo nayo kuhusu uongozi wa dini ya Mwenyeezi Mungu.
56
Majlis ya Kumi na Mbili
57
Muawiyah alikamilisha ufisadi wake kwa kumtawalisha mwanawe
Yazid mlevi na muuwaji kama baba yake, na muovu wa wazi wazi.
Hadithi ya Karbala:
Yaliyo tokea Al-Kufah baada ya Ubaidullah bin Ziyad
kufika hapo:
Ubaidullah bin Ziyad aliingia mjini Al-Kufah usiku, na watu wa mji
ule walidhania kuwa ni Sayyidina Husein bin Ali (a.s.) amewasili
na kwa hali hiyo walifurahi na kumsogelea. Ama walipotambua
kwamba mtu huyo alikuwa ni Ubaidullah bin Ziyad, walitawanyika
wakamwacha wakaenda zao.
58
Kulipokucha alitoka akaanza kuonya na kuwatishia kwa ukali watu
wote wanao muunga mkono Muslim bin Aqil. Habari za vitisho
vya Ubaidullah bin Ziyad zilipomfikia Muslim bin Aqil, alichelea
usalama wake na ikambidi aende nyumbani kwa Hani bin Ur-wah
ambapo alipewa hifadhi.
Kutokana na hali hii, Muslim bin Aqil bila matarajio aliingia ndani
ya kipindi kigumu, kwani kilikuwa ni kipindi cha mateso na tishio
la kuuwawa. Watu waliyo muahidi kumsaidia na kumhifadhi
walimtelekeza.
Bila shaka Muslim bin Aqil alifikwa na mtihani unao wafika watu
wema, ambapo naye alivumilia hali ya kuwa anangoja matokeo ya
vitisho vya panga za maadui zake.
59
Baada ya kugunduwa hivyo, Ibn Ziyad aliwaita mabwana Hani bin
Ash-A’th, Hasan bin Asma bin Khaarijah na A’mru bin Al-Hajjaaj
akawaambia: “Ni kitu gani kinachomzuwiya Hani asije kwetu?”
60
Watu hawa waliendelea kujadiliana naye mpaka wakamshinda.
Hani bin Ur’wa aliagiza mavazi yake akavaa kisha akaomba aletewe
nyumbu wake, akapanda na wakaondoka.
Ibn Khaarijah akasema: “Ewe ami yangu! Mimi sina hofu yoyote
ile juu yako, basi usianze kujitia mashaka mwenyewe.” Inasemekana
kuwa kwa bahati mbaya huyu Hasan alikuwa hafahamu dhamira na
malengo ya Ibn Ziyad dhidi ya Hani.
61
ISBN: 9987 620 55 8