OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA
FURSA ZA MASOMO YA SHAHADA ZA UZAMILI (MASTER’S) KUPITIA UFADHILI
WA “QUEEN ELIZABETH COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS” KWA MWAKA 2020/21
Watanzania wenye sifa wanaalikwa kuomba fursa za masomo ya Shahada za Uzamili
(two-years Master’s Degree) kwa ufadhili wa Mfuko wa Udhamini wa Malkia Elizabeth II wa Jumuiya ya Madola kwa mwaka 2020/21.
Maelezo zaidi kuhusu nafasi hizo za masomo na jinsi ya kuwasilisha maombi
yanapatikana kupitia tovuti ifuatayo:- (i) https://www.acu.ac.uk/qecs
Tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ni 09/07/2020.
ANGALIZO: Kwa wote watakaopata ufadhili wa fursa hizi za masomo itategemea na
Miongozo na Maelekezo mbalimbali iliyotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nchi zingine (mfano:- makatazo ya kusafiri baina ya nchi na nchi) kuhusu ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya CORONA.