Professional Documents
Culture Documents
Natural Chicken Book
Natural Chicken Book
• Shukrani
• Tahariri
• Yaliyomo
• Shirika la Mitamba Tanzania (Heifer)
• Nguzo Kuu za Heifer International
Utangulizi:
Heifer International (Shirika la Mitamba Duniani) ni taasisi isiyo ya kiserikali ya huduma za kibinadamu
iliyojitoa kumaliza njaa na umasikini duniani na kutunza ardhi kwa kugawa mifugo, miti, mafunzo na
rasilimali nyingine kusaidia familia masikini ulimwenguni kuweza kujitegemea na kuinua kiwango chao
cha maisha. Heifer International ilianzishwa mwaka 1944 huko nchini Marekani mara baada ya vita kuu
ya pili ya dunia. Mwasisi wake alikuwa mwinjilisiti Dan West. Leo hii, kazi zake zinafanyika katika nchi 125
duniani na majimbo 38 ya Marekani.
Mwaka 1973, Heifer International iliamua kuingia Afrika na Tanzania ikawa ndiyo nchi ya kwanza
kuanzisha miradi na kazi za Heifer katika bara la Afrika. Uamuzi wa kuingia Tanzania ulifuatia mualiko
uliofanywa na Serikali ya Tanzania kwa lengo la kuboresha maisha ya wakulima walioko vijijini kwa
kugawa mitamba katika vijiji vya Ujamaa wakati vinaanzishwa. Lakini baadae, Heifer iliona kuwa
uwezekano wa kulifikia lengo utakuwepo iwapo tu italengwa familia moja moja, badala ya jamii kwa
ujumla.
Mwaka 1981, Heifer International – Marekani ilishauriana na serikali kuanzisha utaratibu mpya wa
kuwasaidia wakulima wadogo wadogo ambao ndio walio wengi kwa kutumia mfumo na falsafa ya Heifer
ya dhamana ya ‘Kopa ng’ombe lipa ng’ombe’, ikilenga kuboresha maisha ya familia moja moja zenye
kipato cha chini.
Kuanzia hapo, Heifer International Tanzania, imekuwa inatekeleza miradi kwa kutumia mikakati thabiti
ambayo, si tu inayolenga katika utoaji wa mitamba, bali kukuza na kutoa aina mbali mbali za wanyama
ikiwemo, ng’ombe na mbuzi wa maziwa, mbuzi wa nyama, nguruwe, kuku wa kienyeji, punda na ngamia.
Miradi mingine ni ya ufugaji nyuki, ufugaji wa samaki na nyuki na utunzanji wa mazingira. Heifer pia
huchangia juhudi za ulimwengu katika masuala mtambuke ya jinsia na kupunguza kasi ya maambukizi
ya Virusi vya UKIMWI (VVU) na kutoa huduma kwa wale wanaoishi na VVU na UKIMWI, mayatima na
wajane.
Kazi zote za Heifer zinafanyika kwa ushirikiano mkubwa kati yake na serikali, taasisi za kidini na taasisi za
kijamii katika juhudi za kusaidia familia duni kwa kuwapatia mifugo, mafunzo na ushauri wa kitaalamu ili
kupunguza makali ya umasikini na njaa.
Utume wa Heifer:
Kushirikiana na jamii kutokomeza njaa na umasikini pamoja na kuitunza ardhi
Dira ya Heifer:
Jamii ya ulimwengu inayoishi pamoja kwa amani na uwiano mzuri wa mgawanyo wa rasilimali za sayari
yenye utajiri mkubwa.
Falsafa ya Heifer:
Toa Zawadi kwa Wengine’ ni mkakati na mhimili mkuu wa falsafa ya Heifer katika utekelezaji wa
shughuli za maendeleo endelevu – kadiri watu wanavyogawana uzao wa mifugo yao, ikiambatana na
kubadilishana maarifa, rasilimal na stadi zao, kunajengeka mtandao imara wenye matumaini, heshima na
moyo wa kujitegemea unaosambaa ulimwenguni kote
Maeneo ya Kipaumbele:
1. Uimarishaji wa taasisi ya Heifer Tanzania
2. Usawa wa Jinsia na elimu ya VVU na UKIMWI
3. Mandeleo ya kibiashara ya kijamii
4. Kukuza ushirikiano na wadau wengine pia mitandao mbalimbali
5. Kukuza utunzaji wa mazingira
6. Kuboresha hali za maisha ya wahitaji wenye kipato cha chini
Tunafanyeje kazi:
Katika juhudi za kutimiza adhima zake, Heifer International Tanzania inafanya kazi zake kwa ushirikiano
mkubwa na serikali ya Tanzania kupitia wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na Halmashauri za
wilaya na wadau wengine. Heifer inatoa wanyama na mafunzo na halmashauri zinachangia wafanyakazi
wa ugani wa mifugo na wadau wengine wanajitoa kudhamini na kusimamia utekelezaji wa miradi kwa
kushirikiana na kamati za miradi.
Familia duni zimekuwa zinawezeshwa kwa kupewa wanyama mbalimbali. Hadi leo Heifer International
Tanzania inajihusisha na utoaji wa wanyama wafuatao:
• Ng’ombe wa maziwa
• Mbuzi wa maziwa
• Mbuzi wa nyama
• Nguruwe
• Kuku wa kienyeji
• Punda
• Ngamia
• Nyuki
• Samaki
• Miche ya miti
Heifer International Tanzania inatekeleza miradi katika mikoa yote 21 ya Tanzania bara na 5 Tanzania
visiwani. Kati ya wilaya 127 nchini, Heifer inayo miradi katika wilaya 96 sawa na asilimia 76 na vijiji 1,103.
Nini kinafanya Heifer kuwa ya kipekee?
‘Toa Zawadi Pia’, ni mfano wa kipekee ambapo familia moja inayopata mfugo na ujuzi, inakubali kutoa
uzao wa kwanza wa mfugo ambao ni jike kwenda kwa familia nyingine inayo hitaji. Mlolongo huu
huendelezwa na kuwasaidia maelfu ya familia wahitaji na kuwapunguzia makali ya maisha.
Lakini pia, ubora wake wa hali ya juu ni ule utokanao na urahisi na ufanisi wake. Kwa kifupi ni ule
utekelezaji wa kimkakati endelevu wa ‘Familia moja kwa wakati mmoja’. Hali hii imepelekea taasisi nyingi
kuiga na kuanza kutumia mfumo huu. Hali hii imeweza kutoa changamoto kubwa kwa taasisi mbalimbali
zinazolenga kuwezesha jamii kujitegemea.
Mkakati wenye matokeo mazuri unaowezesha kupunguza utegemezi katika miradi ya Heifer, hususani,
wataalamu wa ugani na wafadhili, ni ule wa kujengea uwezo wakulima rika na wahudumu wa afya
za wanyama vijijini. Watu hawa ambao ni wa kujitolea, wapo katika kila eneo la mradi na wanasaidia
kupunguza kwa kiasi kikubwa magonjwa yanayoweza kuzuilika.
Matokeo ya miradi inayofadhiliwa na Heifer yanaonekana wazi nchini. Miradi imewezesha familia nyingi
kuboresha afya na kipato chao. Kutokana na kipato, familia nyingi zimeweza kuboresha nyumba zao
na hata kujenga za kisasa, kulipia watoto wao ada za shule, kulipa huduma za afya na hata mahitaji
mengine muhimu ya kifamilia. Pia , miradi hii imewezesha kutoa ajira vijijini na kupunguza uhamiaji mijini,
imeboresha mazingira na uzalishaji wa mazao ya chakula na ya biashara.
Heifer itaendelea kutumia mkabala wa jumla wa maendeleo kuwawezesha wanajamii waliopo vijijini
katika kuboresha maisha yao binafsi. Familia walengwa, wanawezeshwa kutambua mahitaji na
changamoto zao, kuamua miradi inayowafaa, kupanga na kutekeleza miradi itakayoboresha maisha yao.
Nguzo za Heifer:
Iwapo utawauliza wadau wa Heifer, ‘ni nini kanuni za msingi ambazo kwazo zinajenga maisha yao?’ wengi
watasema ‘nguzo za Heifer.’ Nguzo hizi zina sisimua hekima za makundi na mtazamo binafsi na kuweka
moyo, akili na matendo yenye muelekeo na matunda.
Nguzo hizi zinafafanua maneno ‘TOA ZAWADI PIA’ ambayo yanatoa mwanga unaofanya Heifer kuwa ya
pekee na miradi yake kuwa ya kudumu. Nguzo hizo ni:
Onyesha Uwajibikaji:
Walengwa huamua matakwa yao wenyewe, hupanga mipango ya miradi, huchambua walengwa,
hutekeleza miradi kama inavyotakiwa, hufuatilia maendeleo yake, hutunza kumbukumbu, hutoa taarifa za
maendeleo yake na kutathmini mradi kwa kushirikiana na wadau wote.
Heifer hutoa mifugo kama njia mojawapo ya kuboresha mazingira kwa kushawishi kuwa na mifugo michache
iliyo bora na kufugia ndani. Haya hufanyika katika juhudi za kuzuia mmomonyoko wa ardhi, kusisitiza
matumizi ya samadi kurutubisha udongo, kufanya usafi, kutunza misitu ili kupata kuni, mbao, kivuli na
kutunza wanyama pori pamoja na vyanzo vya maji.
1.0: Utangulizi.
Kuku wa kienyeji ni wale ambao wamekuwepo hapa nchini kwa miaka mingi na damu yao haijachanganyika
na ya kuku wa kigeni. Kuku hawa wana rangi na maumbo mbali mbali. Idadi ya kuku wa kienyeji hapa
Tanzania inakadiriwa kufikia milioni 27. Kati ya kaya milioni 3.8 zinazojishughulisha na kilimo nchini, kaya
milioni 2.3 hujishughulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji. Ufugaji wa kuku wa kienyeji hapa nchini kwetu
Tanzania, kwa kawaida, hufanywa na wafugaji wadogo wadogo wanaoishi kando kando ya miji na wale
wanaoishi vijijini. Kuku hawa hufugwa huria {free-range}, yaani hufungiwa ndani nyakati za usiku na
hufunguliwa asubuhi ili wajitafutie chakula.
Kuku hawa hutoa mazao machache sana yaani nyama na mayai, kwa mfano kuku mmoja hutaga kiasi cha
mayai 40-60 kwa mwaka badala ya 100-150 iwapo ataimarishwa na kutunzwa vizuri. Pia uzito wa kuku hai
ni wa chini sana, wastani wa kilo 1.0 – 1.5 katika umri wa zaidi ya miezi 6 badala ya kilo 1.8 – 2.5 iwapo
atatunzwa vizuri.
Pamoja na sifa hizi ni muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri, wawekwe kwenye mabanda mazuri,
wapewe maji na chakula cha kutosha.
Kutokana na mwingiliano wa vizazi, maumbile hayo yanaweza yakajitokeza kwenye aina mbalimbali za
kuku, kwa kuku mmoja kuwa na kabila moja au zaidi kwa mara moja. Hivyo aina za kuku zifuatazo zinaweza
kutambuliwa kama ndiyo kabila za kuku wa kienyeji kulingana na maumbile yao na maeneo wanakotoka.
Muhimu: Mkulima akifanya uchaguzi vizuri kutoka kwenye aina hii ya kuku na kutoa matunzo mazuri kwa
hao kuku waliochaguliwa, hakika anaweza kupata kuku walio bora wenye uzito wa kutosha na wenye
kutaga mayai mengi na makubwa.
(iv) Singamagazi
Ni aina ya kuku wakubwa wa kienyeji wanaopatikana zaidi maeneo ya Tabora, kuku hawa wana utambulisho
maalum kutokana na rangi zao, kwani majogoo huwa na rangi ya moto na mitetea huwa na rangi ya nyuki.
Uzito - Majogoo wastani wa kilo 2.9, Mitetea wastani wa kilo 2.0, Mayai wastani wa gramu 56
(v) Mbeya
Kuku hawa wanapatikana Ileje mkoani Mbeya, asili hasa ya kuku hawa ni kutoka nchi jirani ya Malawi na si
wa kienyeji asilia bali wana damu ya kuku wa kisasa aina ya “Black Australorp” Rangi ya manyoya ya kuku
hawa ni nyeusi au blue iliyokolea.
Uzito – Majogoo kilo 3
Mitetea kilo 2
Mayai gramu 49
Uwezo wao wa kuatamia mayai na kuangua ni mdogo sana ukilinganisha na kuku wengine.
(vi) Pemba
Kuku hawa wanapatikana maeneo mbalimbali ya kisiwa cha Pemba. Wana maumbo ya wastani na miili yao
ni myembamba. Rangi ya manyoya yao ni mchanganyiko, panga na vilemba vyao ni vidogo.
Uzito - Majogoo wastani wa kilo 1.5
Mitetea wastani wa kilo 1.0
Mayai wastani wa gramu 42
(vii) Unguja
Kuku hawa wanapatikana maeneo mbalimbali ya kisiwa cha unguja, hawana tofauti kubwa sana na wale wa
Pemba isipokuwa panga / vilemba vyao ni mchanganyiko kati ya vidogo na vikubwa.
Uzito – Majogoo wastani kilo 1.6
Mitetea wastani wa kilo 1.2
Mayai wastani wa gramu 42
Kuku hawa wa Unguja na Pemba wanashabihiana sana na Kuchi isipokuwa kuku hawa (Unguja na Pemba) ni
wadogo
Faida Zake:
1. Gharama ndogo za ujenzi wa banda.
2. Gharama za chakula hupungua kwani kuku huokota wadudu na kula baadhi ya majani.
3. Gharama za kujenga uzio hazihitajiki.
Hasara zake:
1. Uwezekano mkubwa wa kuku kuliwa na vicheche, mwewe, kuibiwa mitaani au kukanyangwa na magari.
2. Kuku hutaga popote na upotevu wa mayai ni mkubwa.
3. Kuna usimamizi hafifu wa kundi la kuku.
4. Ni rahisi kuku kuambukizwa magonjwa.
5. Utagaji unakuwa si mzuri kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa.
6. Uwekaji wa kumbukumbu si mzuri na mara nyingi kumbukumbu si sahihi.
7. Si rahisi kugundua kuku wagonjwa na utoaji wa tiba na kinga ni mgumu.
Faida zake:
1. Sehemu ndogo ya kufugia hutumika kuliko ufugaji huria.
2. Utunzaji wa kuku ni rahisi ukilinganisha na ule wa huria.
3. Ni rahisi kutibu na kukinga maradhi ya milipuko kama mdondo (Newcastle disease).
4. Upotevu wa kuku na mayai ni mdogo sana ukilinganisha na mfumo Huria.
5. Uwekaji wa kumbukumbu ni rahisi.
Hasara zake:
1. Unahitaji gharama za banda na uzio.
2. Gharama za chakula zitakuwa kubwa ukilinganisha na ufugaji huria.
3. Matumizi ya muda mrefu ya eneo husika laweza kuwa na minyoo au vimelea vingine vyovyote vya
magonjwa.
Faida zake:
1. Mfumo huu unahitaji eneo dogo la kufugia hivyo ni mzuri kwenye maeneo yenye uhaba wa ardhi.
2. Uangalizi wa kuku ni mzuri na rahisi.
3. Hakuna haja ya kufagia vinyesi vya kuku kila siku.
4. Joto litokanalo na mtandiko lina uwezo wa kuuwa baadhi ya vimelea vya maradhi.
5. Kuku wanakingwa na hali ya hewa mbaya na maadui wengine.
6. Ni rahisi kukinga na kutibu maradhi ya kuku.
7. Uwekaji wa kumbukumbu ni rahisi.
Hasara zake:
1. Uwezekano wa kuku kudonoana ni mkubwa.
2. Gharama za ujenzi wa mabanda zinahitajika.
Muhimu: Kutokana na uwezo mdogo wa uzalishaji kimaumbile kuku hawa hawataleta tija kwa mfugaji
iwapo atatumia mfumo huu.
Banda la kuku linaweza kujengwa kwa kutumia raslimali za misitu zinazopatikana kwa urahisi kwenye
eneo husika; vifaa kama miti, nyasi, mabati, makuti, fito, udongo, mabanzi ya miti, cement na vifaa vingine
mbalimbali vya ujenzi vinafaa kutumika kwa ujenzi wa banda la kuku.
Kuku wanaofugwa kwa mfumo wa nusu ndani nusu nje wanastahili eneo la mita moja mraba kwa kuku 4
- 5. ili kuruhusu nafasi ya vyombo vya chakula na maji.
Aina za Mabanda
Muhimu: Idadi ya viota vya kutagia mayai viwe robo tatu ya idadi ya kuku waliofikia umri wa kutaga.
Ni muhimu pia kuweka viota vya kutagia sehemu iliyojificha (sehemu ya faragha). Yenye kiza kiasi. weka
maranda au majani makavu ndani ya kiota ili kuku aanze kutaga.
◊ Mitetea
Sifa:
• Umbile la mwili na jinsi aonekanavyo (umbile kubwa).
• Uwezo wa kutaga wakiwa na umri mdogo (miezi 6).
• Wenye uwezo wa kustahimili magonjwa.
• Uwezo wa kukua haraka.
• Wawe na uwezo wa kutaga mayai mengi (zaidi ya 15).
• Uwezo wa kuatamia na kuangua vifaranga wengi na kuwalea.
◊ Jogoo
Sifa:
• Mkubwa wa umbo.
• Miguu imara na yenye nguvu
• Awe na kucha fupi.
• Awe mwenye nguvu
• Awe na machachari.
• Upanga / kilemba kikubwa
• Awe na uwezo wa kuitia chakula mitetea.
• Awe na tabia ya kupenda vifaranga.
Njia zitumikazo katika kuchagua:
• Kwa kuangalia kuku wenyewe kulingana na sifa zilizotajwa hapo Juu.
• Kwa kufuatilia kumbukumbu za wazazi wa kuku unaotaka Kuwachagua.
• Kwa kuangalia kumbukumbu za familia (wazazi, kaka na dada)
Umri wa kupevuka
• Mitetea huanza kutaga wakiwa na umri wa miezi 6~8.
• Jogoo huanza kupanda akiwa na umri wa miezi 7 lakini mbegu zake huwa bado kukomaa, hutoa
mbegu zilizokomaa anapofikia umri wa miezi 10.
Ni vizuri jogoo atumike si zaidi ya miaka mitatu ili kuepuka mchanganyiko wa damu kwa wenye nasaba moja
ambayo husababisha uzalishaji duni.
Kwa kawaida kuku wa kienyeji anapofikia umri kati ya miezi sita hadi minane huanza kutoa mlio (kutetea)
unaoashiria kwamba yuko karibu kuanza kutaga mayai, hivyo ni vema viota viandaliwe mapema wakiwa na
umri wa miezi minne au mitano ili waanze kuvizoea.
Kuku anapoanza kutaga, akifikisha mayai matatu, mfugaji anashauriwa kuondoa kila yai linalozidi hayo
matatu kila siku linapotagwa na kuliwekea alama ya tarehe au namba kwa kutumia kalamu ya risasi
(pencil) ili kumfanya kuku aendelee kutaga kwa lengo la kufikisha mayai 15 – 20. Mayai yanayoondolewa
yahifadhiwe kwenye chombo kikavu chenye kupitisha hewa kama tray, box lililowekwa mchanga au hata
chungu kilichojazwa mchanga.
Njia yoyote utakayochagua inahitaji maandalizi ya kina, hususani ya uchambuzi wa mayai yatakayoweza
kutotolewa. Ni vizuri kuchagua mayai ya kuatamia ili mayai yasiyofaa yaweze kuuzwa au kutumika nyumbani
kwa chakula
Kazi hii ya kumuandaa kuku anayetaka kuatamia ni muhimu ikafanyika wakati wa usiku.
Mwisho wa utagaji kuku huanza kuatamia, hivyo mfugaji anashauriwa kumuwekea mayai 12-15 kulingana na
umbile au ukubwa wa kuku husika.
Kwa kawaida kuku hulalia mayai yake kwa muda wa siku 21 ndipo vifaranga huanguliwa.
Muhimu: Mayai ya kuatamia yasishikwe kwa mkono ulio wazi, kwani kwa kufanya hivyo yanaweza kupata
harufu kama za mafuta ya kuijipaka, mafuta ya taa au manukato, na hii hupelekea kuku kuyakata. Hivyo
hakikisha umenawa mikono kwanza kisha jipake jivu mikononi, hapo unaweza kuyashika mayai.
Mfugaji anaweza kutambua mayai yaliyo na mbegu na yasiyo na mbegu siku ya saba baada ya mayai
kuatamiwa iwapo atapima mayai kwa kutumia box lililotengenezwa maalum pamoja na tochi yenye mwanga
mkali ndani ya chumba chenye kiza. Hii itamuwezesha mfugaji ayatumie mayai yasiyo na mbegu kwa chakula
cha familia au kuyauza.
Baada ya siku 21 kuku wote waliowekewa mayai Watakuwa wametotoa kwa pamoja
10 Uleaji wa Vifaranga:
Kuna njia mbili za uleaji wa vifaranga ambazo:
1. Uleaji wa vifaranga kwa njia ya kubuni
2. Uleaji wa vifaranga kwa njia ya asili
Kama utalea vifaranga kwa njia ya asili, basi ni vizuri kumtenga kuku mwenye vifaranga na kumuweka
kwenye chumba cha pekee ili vifaranga visishambuliwe na kuku wengine hali kadhalika kuwalinda na
wanyama na ndege wanaoshambulia vifaranga kama vile vicheche na kunguru.
i. Kutunza vifaranga kwenye mzingo (mduara) ndani ya chumba na kuvipatia joto kwa kutumia taa
ya kandili (chemli), taa ya umeme, au jiko la mkaa. Kwa njia hii unaweza kupima joto katika mzingo kama
linatosha au la kwa kuangalia hali ya usambaaji wa vifaranga ndani ya mzingo kama ifuatavyo:
2) Vifaranga kuwa pembeni mbali kabisa na kifaa cha jotona tena wanalia sana, ni dalili kuwa JOTO
LIMEZIDI na ni kali sana. Hali hii siyo nzuri kwa ustawi wa vifaranga, hivyo mfugaji anashauriwa apunguze
nguvu ya joto.
3) Vifaranga kurundikana upande mmoja au mafungu mafungu inaashiria kuwa upepo ni mkali. Upepo mkali
siyo mzuri kwa ustawi wa vifaranga kwani wanaweza kufa kutokana na baridi kali.
4) Vifaranga kukusanyana na kukisogelea karibu kifaa cha joto na huku wanalia sana, ni dalili kuwa JOTO
HALITOSHI
Brooder hii huwa kwenye umbo la mduara (mviringo) na hutumika ikiwa ndani ya chumba ili lisipigwe
upepo, jua, isilowane na mvua na iweze kuhifadhi joto. Kwa kutumia kifaa hiki kuku wanaweza
kunyang’anywa vifaranga vyao mara tu baada ya kutotoa na kuviweka kwenye hii Bruda na hao kuku
wakaachwa bila vifaranga vyao , baada ya majuma mawili, kuku hao huanza tena utagaji na kuendelea na
uatamiaji hadi kutotoa tena. Kwa mtindo huu kuku anaweza kutotoa mara 5~6 badala ya mara 2~3 kwa
mwaka kama ilivyo sasa.
Vifaranga vikae ndani ya Bruda hii kwa muda wa majuma 3~4 kulingana na hali ya hewa,baada ya hapo
fungua milango ya brooder kuruhusu vifaranga vitoke na kuzunguuka chumbani bila kuvitoa nje kwa kipindi
cha mwezi mmoja au zaidi kutegemeana na mazingira.
Vifaranga wanapopiga kelele sana (kulia) ndani ya Bruda yoyote inaashiria kwamba :
• Joto limezidi au kupungua mno
• Kutokuwepo maji au chakula
• Usumbufu (wadudu,unyevunyevu unaosababishwa na maji kumwagika na au msongamano wa hewa)
Mafanikio:
Majaribio yamefanyika Katika chuo kikuu cha Sokoine Morogoro kwa vifaranga wa kisasa na wa kienyeji na
kupata mafanikio mazuri yaani asilimia 100.
Muhimu: Kwa sehemu zenye baridi sana tumia jiko la mkaa lililotengenezwa maalum kwa kazi hii ambalo
hutumia mkaa mchache kwa nyakati za mchana na nyakati za usiku bila kutumia jiko, Yaani mchana Bruda
huifuniki bali jikolinakuwa juu katikati ili kusambaza joto, na nyakati za jioni unaondoa jiko na unafunika
Bruda na kufunga madirisha ya Bruda yote mawili.
• Vifaranga hukaa ndani ya hii Brudakwa muda wa juma moja au mawili kutegemeana na mazingira
pamoja na afya ya vifaranga vyenyewe.
• Baada ya hapo weka uzio wa upana wa futi moja kuzunguuka Bruda kwa kutumia hardboard.
• Weka maranda ndani ya uzio uliozunguusha
• Weka vyombo vya maji na chakula ndani ya uzio
• Fungua milango yote minne iliyo chini pembezoni mwa Bruda ili kuruhusu vfaranga vitoke nje kila
asubuhi na kuvirudisha ndani ya Bruda kila jioni hadi vifaranga vitakapofikia umri wa majuma manne.
Muhimu: Muda wote huu hakikisha kuwa uzio unaupanua kila unapoona nafasi haitoshi(wanabanana).
• Baada ya majuma manne au sita vifaranga wanaweza kuachiwa ndani ya chumba chote.
Matundu yaliyoko kwenye mbao za inchi 2x2 yanayounganisha nje na ndani ya Kinondoni Bruda ni kwa
ajili ya kupitisha hewa safi pamoja na kutoa hewa chafu.
Kumbuka:
- Ukosefu wa vitamini A hujitokeza baada ya kiangazi kirefu
- Macho ya kuku huharibika
- Ugonjwa hautibiki dalili zikionekana
- Husababisha vifo hasa kwa kuku wanaokua
Vyakula vilivyotajwa hapo juu hupatikana kwa wingi zaidi wakati wa mvua na mavuno, na mara baada ya
kipindi hiki kunakuwepo na upungufu mkubwa ambao huchangia katika ukuaji taratibu na utagaji hafifu.
Utafiti umeonyesha kuwa kiasi cha chakula wanachojitafutia wenyewe kwa siku huwa hakiwatoshi.
Inakadiriwa kuwa wakati wa mavuno kuku anaweza kujitafutia asilimia 50-70 tu ya mahitaji yake ya chakula
kwa siku na wakati wa kiangazi asilimia 30-50 tu ya mahitaji yake ya chakula.
Kwa kawaida kuku wa kienyeji hutumia zaidi ya 90% ya masaa ya siku katika umbali wa mita 110-175 ili
kujitafutia chakula.
Kuku aliyepevuka anayefugwa huria anahitaji gramu 80 za chakula cha ziada kwa siku. Hivyo, ili kuku waweze
kuzalisha wafikie uwezo wao ni muhimu wapewe chakula cha ziada. Chakula cha ziada kitokane na vyakula
vinavyopatikana kwa urahisi katika mazingira anapofugia mfugaji na ambacho hakina ushindani na mfugaji.
Hivyo kilo moja ni Tshs. 210 (Machi 2008). Aidha bei hizi huweza kuongezeka au kupungua kutegemea
upatikanaji wa malighafi, kama kunapatikana dagaa au mabaki ya samaki kama sangara unaweza kuongeza
kilo moja na kupunguza pumba kilo moja. Katika mchanganyiko huu mfugaji anaweza kutumia malighafi
mojawapo au zaidi kutegemeana na upatikanaji katika eneo husika.
Hakikisha wakati wote chakula cha kuku kiandaliwe na kuhifadhiwa kikiwa kikavu {kisilowe maji} ili
kisiharibike kwani chakula kilichovunda kinaweza kuleta madhara kwa kuku. Pia kisitengenezwe chakula
kingi kitakachokaa muda mrefu bila kutumika kwani hupoteza ubora wake.
Mfano wa kiasi cha chakula kwa kulisha kwa siku kuku wa kienyeji watano na vifaranga kumi na tano:
Jogoo mmoja – 1 x 65 gm = 65 gm
Mitetea - 4 x 65 gm = 260 gm
Vifaranga - 15 x 25 gm = 375 gm
Jumla 700 gm
Kuku wawekewe maji kwenye vyombo safi chini ya vivuli vya miti wakati wote muda wa mchana.
Pamoja na mdondo pia yafutayo ni baadhi ya magonjwa yanayoshambulia kuku hawa hapa nchini:
• Ndui ya kuku (Fowl pox)
• Mafua ya kuku (Infectious coryza)
• Homa ya matumbo (Fowl typhoid)
• Kuhara damu (Coccidiosis)
• Minyoo na wadudu kama viroboto, chawa, utitiri na kupe wa kuku
Magonjwa muhimu:
1. Mdondo, Mdonde au Kideri (Newcastle Disease)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi (Virus) na hushambulia kuku wa umri wowote kuanzia vifaranga hadi
kuku wakubwa, pia hushambulia bata, bata mzinga, kanga, kwale na ndege wengineo.
Jinsi unavyoambukiza:
• Kuku mzima kuvuta hewa yenye virusi vya ugonjwa huu toka kwa kuku mgonjwa.
• Upepo huweza kuhamisha virusi vya ugonjwa huu toka sehemu hadi sehemu.
• Watu huweza kuhamisha ugonjwa huu wanapotembea toka sehemu hadi sehemu.
• Kuku wazima wakikaa pamoja na wagonjwa.
• Ndege wanaokula mizoga kama kunguru huweza kusambaza mabaki ya mizoga yenye ugonjwa huu.
• Vyombo vya usafiri toka kwenye eneo lenye ugonjwa.
Dalili zake:
i. Kuku kukohoa au kutopumua vizuri
ii. Kuku kupoteza hamu ya kula na kunywa maji
iii. Kushusha mabawa au kichwa
iv. Kupooza, wengine huzunguka na kuzungusha kichwa na kurudi kinyumenyume.
v. Kuharisha kinyesi cha kijani kibichi
vi. Shingo kupindaa
vii. Kupunguza utagaji hadi 0%
viii. Vifo kufikia hadi 100%
ix. Kuku kutaga mayai yenye matuta, matepe tepe au yenye gamba hafifu.
Kinga ya ugonjwa:
• Kutoa chanjo ya mdondo kwa mtindo wa siku 3, wiki 3 na miezi mitatu au siku 4 wiki 4 kwa miezi 4.
• Hivi sasa kuna chanjo inayotengenezwa hapa hapa nchini inayostahimili joto.
• Usichanganye kuku wako na kuku ambao hujui taarifa zao za chanjo.
Kuku wakipewa chanjo ya mdondo
Kumbuka:
• Mdondo au kideri ni ugonjwa tishio ambao huweza kuua kuku wote.
• Mdondo ukitokea vifo huwa vingi, kuku hupumua kwa taabu hupooza na wengine huzunguka na
kuzungusha kichwa.
• Mdondo huweza kuzuiwa kwa chanjo kila baada ya miezi mitatu.
2. Ndui ya kuku
Ugonjwa huu husababishwa na virusi na hushambulia kuku wa umri wowote lakini zaidi huwapata sana
vifaranga wenye umri kuanzia mwezi mmoja na kuendelea, pia hushambulia ndege wengine. Ndui ni
ugonjwa wa hatari kwenye kuku hasa kwenye maeneo ambayo mdondo umedhibitiwa.
Jinsi unavyoambukiza:
- Ugonjwa huu huambukizwa kwa kupitia kwenye jeraha iwapo
kuku ana jeraha virusi vya ugonjwa huu ndipo hupita.
- Mbu huweza kuambukiza anapomuuma kuku mgonjwa na halafu
akamuuma kuku mzima
Kuku mwenye ndui
Kumbuka kwamba katika ugonjwa huu:
• Dalili ni kuvimba sehemu za ngozi zisizo na manyoya kama ionekanavyo pichani
• Ndui ya kuku huzuiwa kwa chanjo ya sindano.
Dalili zake:
i. Vidonda vya rangi ya kahawia huonekana sehemu za wazi za uso, upanga, mashavu, macho, midomo na
wakati mwingine utando mweupe ndani ya koo.
ii. Kuku kupoteza hamu ya kula
iii. Kuku kupungua uzito
iv. Kuku watagaji kupunguza utagaji.
Matibabu: Hakuna
Kinga
Kutoa chanjo ya ndui wakati vifaranga wakiwa na umri wa miezi miwili na kabla kuku hawajaanza kutaga.
Chanjo hii hutolewa kwa kupitia kwenye utando wa bawa.
Ndui ya hujitokeza wakati wa msimu wa mvua pawapo na wadudu wengi, hivyo kabla ya kuanza mvua
chanja kuku wako kuepusha ndui.
Muhimu
Ili kupunguza kasi endapo ugonjwa huu umeisha washika kuku, sugua majeraha au vipele kwa pamba
iliyochovywa kwenye dawa ya madini joto (Iodine) na baadae paka mafuta mazito (Petrolium jelly) Hii si
kutibu ugonjwa bali unawasaidia kuku kulainisha ngozi ili wapate kuona chakula na maji.
3. Homa ya Matumbo (fowl typhoid)
Ugonjwa huu husababishwa na bakteria (Bacteria) na huwapata kuku wa umri wowote.
Jinsi unavyoambukiza:
• Kuku mzima kula vimelea vya ugonjwa kupitia kinyesi cha kuku mgonjwa
• Kuku mgonjwa huweza kurithisha vifaranga wake kupitia mayai aliyotaga
• Watu na vyombo vya usafiri wanaweza kuhamisha ugonjwa kutoka sehemu hadi sehemu.
• Vyakula vya kuku kutoka sehemu yenye ugonjwa kwenda kusiko na ugonjwa
• Mizoga ya kuku yenye ugonjwa ikipelekwa sehemu isiyo na ugonjwa.
Dalili:
i. Vifo vya ghafla kwa kuku ambao hawajaonyesha dalili. Vifo vinaweza kuwa zaidi ya 30%
ii. Kuku kuzubaa na kutokuwa na hamu ya kula pia hunywa maji sana
iii. Mapanga na mashavu kuonyesha kutokuwa na damu
iv. Kuku huharisha kinyesi cha majimaji cha njano
v. Upumuaji huweza kuwa wa haraka haraka na joto kupanda
vi. Manyoya ya sehemu ya tundu la kutolea kinyesi huchafuka
Matibabu:
Dawa za aina ya antibiotic, sulfa na vitamini zinaweza kutibu ugonjwa huu lakini kuku wanaopona hubaki
bado wanaishi na vijidudu vya ugonjwa huu hivyo ni rahisi kuambukiza kuku wengine au vifaranga wao
wanapototoa.
Jinsi unavyoambukiza:
• Kuku mzima kula na kuvuta hewa yenye vimelea vya ugonjwa huu
• Kuku wazima wanapochanganywa na wagonjwa
Dalili:
i. Kuvimba uso chini na nyuma ya jicho
ii. Kupumua kwa matatizo na hata kukoroma
iii. Macho kuvimba
iv. Kushindwa kula
v. Kutoka makamasi puani
vi. Kutoa usaha unaonuka
vii. Kuchafuka mbawa
Dalili:
• Kuku huharisha kinyesi cha damu au damu kabisa.
• Manyoya husimama
• Hulala na kukosa hamu ya kula.
Tiba:
Dawa za Sulfa, vitamini na madini
Kuku hushambuliwa na wadudu wa aina mbalimbali ambao wamegawanyika katika makundi makuu mawili
kama ifuatavyo:
Wadudu hawa humnyonya kuku damu na kumfanya adhoofike, kupata magonjwa kwa urahisi na hatimaye
kifo.
Dalili za minyoo:
• Upungufu wa hamu ya kula
• Kudumaa kwa kuku wanaokua
• Kupungua kwa utagaji
• Minyoo mingine husababisha kupumua kwa shida
• Kuku hupungua uzito
Dalili
• Kujikuna na kujikung’uta.
• Manyoya kuwa hafifu na dhaifu.
• Rangi ya upanga kuwa hafifu kutokana na upungufu wa damu.
• Kukosa hamu ya chakula.
• Ngozi kuwa nene, ngumu na yenye magamba yanayodondoka kama unga mweupe.
• Kukonda na kupungua uzito.
• Kuku anayeatamia hatulii kwenye kiota.
• Kupungua au kukoma kwa utagaji.
• Fuata kanuni za chanjo hasa ugonjwa wa mdondo, ndui na dawa ya minyoo
• Tenga kuku wagonjwa wakae mbali na kuku wazima
• Kuku wageni watengwe kwa muda usiopunguwa majuma mawili kabla hawajachanganywa na kuku
wenyeji.
Faida za kumbukumbu:
a. Zinamwezesha kugundua makosa na kuweka mpangilio wa masahihisho ya makosa
b. Ni namna ya kuongeza na kuendeleza uwezo wa usimamizi na uongozi wa mfugaji.
1. Kumbukumbu za uzalishaji:
Hizi zitamwezesha mfugaji kujua kiasi cha mayai yanayotagwa na vifaranga waliototolewa pia kujua idadi ya
kuku wanaokufa kwenye banda lake hivyo aweze kuchukua tahadhari.
Mfano wa kumbukumbu
Mada 9. Tiba za Asili
Madawa ya asili yatokanayo na mimea yanayosaidia katika tiba na kinga za maradhi mbalimbali ya kuku.
• Kideri/Mdondo/Mdonde/Chikwemba
• Gumboro (Huathiri kuku wenye umri wa wiki 3-6)
• Ndui
• Kuhara
(9) Mwembe:
Majani magao mawili, ponda chemsha ndani ya lita 6 za maji hadi ibaki lita1. Wape kwa siku moja. Mwembe
hutibu:
• Tumbo
• Mafua
• Kinga ya Kideri/Mdondo
(10) Mpira
Chemsha majani au mizizi. Mpira hutibu:
• Tumbo
• Vidonda na majipu