Professional Documents
Culture Documents
Justification
Justification
Parishi ya Mwananyamala
Dhambi iliingia dunia kupitia kwa Adamu na Eva, ambao waliasi kwa kutomtii
Mungu. Kwa sababu ya Kuasi kwao (kutokutii) Adamu na Eva walianguka na
kuchafuka na dhambi na miili yao, asili yao ya kibinadamu ikafanyika kuwa na
dhambi (Mwanzo 3:1-6, Rumi5:12).
Dhambi ni kitu chochote kinachofanywa au fanyika kinyume na Mungu au mapenzi
yake na sheria zake. Kutenda dhambi ni kuvunja au kutokutii sheria au mapenzi ya
Mungu.
Yakobo 1:14-15 inafafanua wazo hili vizuri, “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa
yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaaikiisha
kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambiikiisha kukomaa huzaa mauti”
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuwa na dhambi ( asili ya dhambi) na kutenda
dhambi. Wale wanaotenda dhambi ni wale walio amua kwa hiari yao kufanya
dhambi - hawako tayari kuacha dhambi.
1 Yohana 3:8 “atendaye dhambi ni wa Ibilisi, kwa kuwa ibilisi hutenda dhambi
tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi
za Ibilisi.”
2
Kanisa la Pentekoste Kijitonyama
Parishi ya Mwananyamala
Yakobo 1:15 “halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile
dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”
Tunapoyatoa maisha yetu kwa Yesu, tunaanza kutmbea kama yeye alivyotembea.
Tunakuwa tumejitoa na kuamua kwa hiari kuanza kuyafanya mapenzi ya Mungu na
kuacha kufanya au kuishi maisha ya dhambi. Tunakuwa tumetangaza vita dhidi ya
dhambi na kuanza kuishi maisha mapya ndani ya Yesu (2Korintho 5:17)
Ebrania 4:15 “Kwa kuwa hakuna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika
mambo yetu ya udhaifu; bali alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila
kufanya dhambi”
1 Petro 2:21 “ Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili
yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake”
Usitende dhambi!
“Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama
mtu akitenda dhambi tunaye mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki”
Ebrania 4:15 “Kwa kuwa hakuna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika
mambo yetu ya udhaifu; bali alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila
kufanya dhambi”
Rumi 8:3-4 “Maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu
kwa sababu ya mwili, Mungu kwa kumtuma mwananwe mwenyewe katika mfano
wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika
mwili; ili maagizo ya torati yatimizwe ndani yetu sisi tusioenenda kwa kufuata
mambo ya mwili, bali mambo ya roho”.
Rumi 12:2 “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa
upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya
kumpendeza na ukamilifu”.
DHAMBI
Kufanya Dhambi ni kufanya jambo au kitu kisichompendeza Mungu.
3
Kanisa la Pentekoste Kijitonyama
Parishi ya Mwananyamala
Kila mtu anayezaliwa Duniani ni mwenye Dhammbi. Zaburi 51:5.
Maisha ya kawaida bila Yesu ni ya Dhambi kwa sababu yamejaa ubinafsi. Mfano
Mtoto mdogo.
Matokeo ya Dhambi.
1. Ina mchukiza Mungu. Mwanzo 6:5-7.
2. Inaleta hatia. Zaburi 51:1-3.
3. Inaleta utumwa. Rumi 6:17.
4. Upofu wa kiroho. 2kor 4:4.
5. Kifo cha Roho. Efeso 2:1
6. Inaondoa Tumaini. Efeso 2:12.
7. Tito 1:15, Yakobo 5:12.
Maneno kadhaa katika biblia yenye maana ya Dhambi.
Biblia inatumia zaidi ya neno moja kuieleza na kufafanua dhambi.
Kuacha njia au kuwa tofauti na kiwango:
Chattah kutolenga shabaha au kwenda kinyume. Waamuzi 20:16, Zaburi 51:4
Avon Kupinda au kupotosha. Hii ina maana ya kuamua kufanya kwa makusudi lile
ambalo si sahihi. Ayubu 33:27.
Shagah kukosea au kupotoka. Ayubu 19:4. Lawi 4:13.
Parabasis Kuiacha njia iliyonyooka, kuvuka mpaka au kwenda kinyume na mpaka.
Rumi 4:15, Galatia 3:15.
Harmatia kutolenga shabaha. Mathayo 1:21, Rumi 6:23.
Paraptoma Kuchukua hatua isiyo sahihi, kukosea. Kolosai 2:12, Efeso 2:5.
Kuelezea hali, hii ni hali ya jinsi mwanadamu alivyo:
Rasha mwovu. Zaburi 1:6, Zaburi 37:28
Asham kuwa na hatia kukosea. Mwanzo 26:10, Lawi 5 :15-16.
Uasi wa makusudi
Hii ni hali ambyo watu wanadhani wanaweza kuendelea na kufanya mambo yao
bila kumhitaji Mungu.
Persha kumpiga ngumi Mungu. Isaya 1:2, 1Falme 12:19.
Anomia kutokuwa na sheria ukaidi uasi. 2Kor 6:14,IYohana 3:4.
Matendo maouvu au dhamira mbaya.
4
Kanisa la Pentekoste Kijitonyama
Parishi ya Mwananyamala
Marah mkaidi, Zaburi 78:8
Ra’ah kuwa mwovu kufanya tendo mahsusi la uovu. Mwanzo 19:7.
Wazo la dhambi linaambatana na uhalisi na ukweli kwamba kuna kitu fulani
kimepotea, potoshwa au haribiwa.
Dhambi inatutenga na kutuweka mbali na Mungu, inasababisha matatizo kati ya
watu na hatimaye humharibu mtu binafsi.
Wajibu wetu.
Rumi 14:12., Ezekieli 18:20-23,Yohana 3:5-7.
Maswali ya kujadili
1. Kutokuwa na shabaha au kutoweza kulenga shabaha ni maana sahihi ya
Dhambi. Jadili
2. Kwanini Mungu alimpa mwanadamu hiari wakati alifahamu kwamba
mwanadamu atatenda dhambi?
3. Kwanini kujisikia hatia ni tatizo la watu wengi