Professional Documents
Culture Documents
NDANI YA IDARA
GODWIN CHILEWA
GOSTCH Publishers
Sponsored By Veritas Gospel Ministries
www.veritasgospel.org
Houston, Texas
© 2020 by Godwin Chilewa. All rights reserved.
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kunakili, kuiga, kuchapa, kuchapisha sehemu
ya kitabu hiki katika mtandao, au kutumia sehemu yoyote ya kitabu hiki kibiashara
bila kupata ruhusa ya maandishi kutoka kwa mwandishi, kama inavyoagizwa na
sheria ya haki miliki. Hata hivyo inaruhusiwa kutumia nukuu za mafundisho
yaliyomo kuwaelimisha watu wengine neno la mungu, kuwafariji waliopatwa na
matatizo, na kutangaza habari njema za ufalme wa Mungu bila kudai malipo.
Maandiko matakatifu yamenukuliwa kutoka
Biblia takatifu –Swahili SUV na KJV
GOSTCH Publishers
ISBN:
TUKUZO
Uinuliwe mwenyezi Mungu wetu mfalme Jehova – El-Shaddai
muumba wa mbingu na nchi, kwa wingi wa neema,
rehema, na Fadhili zako kwetu.
Hakika unastahili kuabudiwa.
YALIYOMO
UTANGULIZI .................................................................................................................... 1
BOMU UBALOZINI ........................................................................................................ 5
IDARA (TISS)…………………………………………………………..…..…43
KIKOSI KAZI (TANBOMB)........................................................................................ 55
FUNUNU ........................................................................................................................... 80
BEGA KWA BEGA NA FBI ....................................... Error! Bookmark not defined.
26 FEDERAL PLAZA NEW YORK ........................ Error! Bookmark not defined.
MBELE YA GAIDI........................................................ Error! Bookmark not defined.
JASUSI................................................................................ Error! Bookmark not defined.
WITO.................................................................................. Error! Bookmark not defined.
USHUHUDA WANGU NI AMINI ......................... Error! Bookmark not defined.
MAREJEO ........................................................................ Error! Bookmark not defined.
FALIHISI .......................................................................... Error! Bookmark not defined.
SHUKRANI
i
GO DW IN C H IL EWA | ii
SHUHUDA ZA JASUSI
NDANI YA IDARA
GODWIN CHILEWA
GOSTCH Publishers
Sponsored By Veritas Gospel Ministries
www.veritasgospel.org
Houston, Texas
GO DW IN C H IL EWA | iv
UTANGULIZI
_______________
M
aneno yaliyoandikwa hapo juu kwa kawaida hutumiwa na
mahakama, ofisi za serikali, na taasisi nyingine zinazotoa
huduma za kisheria kama kiapo cha kusema kweli. Kimsingi
mtu anayeapa mbele ya hakimu au afisa yeyote wa serikali
hujifunga kusema ukweli mtupu, pasipo kupindisha maneno. Kama
baadaye ikibainika kuwa maelezo yaliyotolewa na muhusika baada ya
kuapa ni ya uongo, mamlaka husika huweza kuchukua hatua za kisheria
dhidi yake ikiwa pamoja na kumfungulia mashitaka ya jinai, kumnyima
stahiki alizoomba, kumpiga faini, au kumtupa gerezani.
Ingawa kitabu hiki si nyaraka ya serikali inayonifunga kula kiapo
kabla ya kutoa maelezo yangu, na wala mimi siamini katika kuapa
(Yakobo 5:12), nimeona vema kuanza kutoa shuhuda zangu kwa ahadi
hiyo kwa sababu kuu tatu: Kwanza kwa kuwa nataka kusimulia
matendo makuu ambayo Mungu amenitendea katika maisha yangu.
Yamkini kila mtu mwenye imani huyaona matendo makuu ya Mungu
kwa namna yake, na kuyapokea kivyake. Lakini mlolongo wa matukio
na miujiza niliyopitia katika maisha yangu ni ya kipekee, ya
kushangaza, na kusisimua mno. Nina hakika kama matukio hayo
yangetengenezwa filamu, bila shaka ingeweza kushinda tuzo la Oscar
la nchini Marekani.
1
GO DW IN C H IL EWA |2
BOMU UBALOZINI
I
likuwa siku ya ijumaa, tarehe 7 August 1998 saa moja na nusu
asubuhi, eneo la Ilala Boma, Dar es salaam. Mimi pamoja na
maafisa wenzangu kumi na wawili tulikuwa tumekusanyika ndani
ya chumba namba 102, kilichokuwa kwenye jengo la ofisi ya mkuu
wa mkoa wa Dar es salaam kwa ajili ya kikao cha dharula. Chumba hiki
kilikuwa mojawapo ya ofisi nyingi za idara ya usalama wa Taifa
zilizozagaa jijini Dar es salaam na mikoa yote ya Tanzania.
Kikao kilikuwa kimeitishwa na mama Inviolata Murusuli, ambaye
wakati huo alikuwa ndiye mkuu wa usalama wa Taifa wilaya (District
Security Officer) Ilala, mkoa wa Dar es salaam. Wakati huo mambo ya
‘Kanda maalum za kipolisi’ yalikuwa hayajaanza. Mama huyu alikuwa
akiheshimika mno kwa uwezo wake mkubwa wa kusimamia
operesheni, kuhamasisha maafisa walio chini yake kufanya kazi kwa
bidii na weledi, na kutoa ushauri bora kwa viongozi wa juu. Sifa hizo
pamoja na nyingine nyingi ndizo zilizofanya akabidhiwe dhamana ya
kusimamia usalama wa wilaya maarufu, na ngumu kuliko zote nchini.
Kama ungekutana na mama Murusuli mitaani wakati ule, bila shaka
usingeamini kuwa ni mmoja wa watu muhimu mno katika idara ya
usalama wa Taifa. Sura yake nzuri, iliyoambatana na urefu wake wa futi
tano inchi nane, na umbo lake la kuvutia, iliwafanya wanaume wengi
kumuona kama mfanya biashara tajiri, muhadhili wa chuo kikuu, au
mwanasiasa maarufu wa taifa kubwa. Mama Murusuli alizitumia vema
sifa hizi katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku, akiiwakilisha
vema idara ya usalama wa Taifa kila mahali alipokwenda.
5
GO DW IN C H IL EWA |6
6
7 | SH U HU DA Z A J A SU SI – NDA NI YA IDAR A
7
GO DW IN C H IL EWA |8
ilikuwa kuwavutia wananchi kufika mahali hapo kwa wingi ili hatimae
waweze kusikiliza hotuba za viongozi zilizojaa maagizo ya utekelezaji
wa sera za chama na serikali yake.
Ilipofika saa tatu na nusu hivi mheshimiwa Yusuf Makamba
(aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam wakati huo) akawasili na
kupokelewa kwa shangwe na vifijo. Wakati huo Mimi na maafisa
wenzangu tulikuwa tumeshalivinjali eneo la uwanja wote kwa muda wa
kutosha, na hatukuona dalili zozote za maandalizi ya vitendo vya kiadui
au uvunjifu wa amani. Hali ilikuwa shwari.
Wakati sherehe zikiendelea ghafla ukasikika mshindo wa mlipuko
mkubwa mno upande wa kaskazini mashariki ya mahali tulipokuwa.
Mshindo huo ulikuwa haufanani kabisa na kishindo cha kupasuka kwa
tairi ya gari, bunduki, au muungurumo wa radi. Ulikuwa mshindo
mkubwa na mzito kuliko muungurumo wa Rocket Propelled Grenade
(RPG), silaha inayotumiwa na wanajeshi kulipua vifaru vya adui vitani.
Ingawa eneo tulilokuwepo lilikuwa na kelele nyingi na za kila aina, kila
mtu aliweza kusikia mlipuko huo kwani ulitikisa kila mahali.
Bila kupoteza muda nikainua mkono wangu wa kushoto kuitazama
saa niliyokuwa nimeivaa. Mishale ya saa hiyo ilinionesha ilikuwa
imetimia saa nne na nusu (juu ya alama) asubuhi. Mojawapo ya mambo
muhimu anayopaswa kufanya afisa usalama wa Taifa anapokuwa
kazini, ni kujua na kutunza muda sahihi wa kila tukio linalotokea.
Kufanya hivyo husaidia sana katika uchunguzi utakaofanywa baadae,
hususan katika kuunganisha nukta, kujumlisha moja na moja kupata
mbili, kupunguza idadi ya watuhumiwa, na hata kutambua sababu na
lengo lililopelekea tukio husika kutokea au kufanywa katika muda huo.
Huku nikiendelea kutafakari mshindo wa mlipuko huo, nikatembea
haraka haraka kumfuata Morgan aliyekuwa upande wa pili wa uwanja
akizungukia mkusanyiko wa watu. Ingawa umati wa watu ulikuwa
mkubwa mno sikuwa na shaka yoyote ya kutomuona kwani nilijua
atakuwa ameshafika kwenye kituo, yaani mahali tulipokubaliana
kukutana kama ikitokea dhalula. Utaratibu huu ambao ni wa kawaida
kwa maafisa wa idara husaidia sana kujipanga upya inapotokea dharula
ya kuwafanya mpotezane.
Wakati nikikaribia kituoni, kwa mbali nikamuona Edward (EL)
akiwa ameshafika. Macho yetu yalipogongana nikanyanyua mkono
wangu wa kushoto na kugusa upande wa kulia wa ncha ya kola ya shati
niliyokuwa nimeivaa kumuashiria kuwa mambo si shwari. Bila kusita
naye akanijibu kwa kugusa sikio lake la kushoto kuashiria kuwa hata
8
9 | SH U HU DA Z A J A SU SI – NDA NI YA IDAR A
9
GO DW IN C H IL EWA | 10
10
11 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
11
GO DW IN C H IL EWA | 12
12
13 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
2
Ubalozi wa Marekani ulikuwa eneo la Kinondoni, nyumba namba
36 Laibon, iliyokuwa kwenye makutano ya barabara ya Ali Hassan
Mwinyi na mtaa wa Laibon. Ilinichukua dakika chache tu kutoka ofisi
ya RSO hadi kufika ubalozini hapo. Mbele ya jengo niliwakuta
wanajeshi wa Marekani (Marines) waliovaa mavazi ya kivita (combat gear)
huku bunduki za kivita aina ya M4 Carbine na Machine gun zikiwa
mikononi mwao, tayari kwa mapambano. Moto mkubwa ulikuwa
ukiwaka upande wa mashariki ya jengo, karibu kabisa na mahali
ilipokuwa ofisi ya mapokezi. Mbele kidogo, kiasi cha mita kumi na
tano hivi kutoka lango kuu kulikuwa na mioto mingine mikubwa
iliyokuwa ukiendelea kuteketeza magari yaliyokuwa yameegeshwa
katika eneo hilo. Upande wa kusini, kwenye ukuta wa wigo unaotazama
barabara ya Ali Hassan Mwinyi, kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa
wakijitahidi kupanda ukuta huo ili waruke nje, kujinusulu na dhahama
iliyokuwa ikiendelea katika jengo hilo. Baadhi ya watu waliweza
kupanda na kusalimika lakini wengine hawakuweza kufanya hivyo
kutokana na majeraha waliyokuwa nayo, na au mshituko waliopata
kutokana na mlipuko mkubwa wa bomu. Wakati huo watumishi wa
balozi nyingine na wananchi wa maeneo ya jirani walikuwa wameanza
kumiminika katika eneo hilo kuangalia nini kilichokuwa kimetokea na
kutoa msaada kwa majeruhi.
Huku moyo ukinidunda nilitembea kwa kasi kumfuata kiongozi wa
wanajeshi (Marines) aliyekuwa upande niliotokea. Aliponiona
nikimfuata akashika vizuri bunduki yake na kunifuata huku akiwa
amenielekezea mtutu. Sikushituka, kwani nilikuwa nikitegemea kitu
kama hicho kutokea. Ukiwa umepitia mafunzo ya kijeshi, na au
kushiriki katika mapambano ya kivita unaweza kuhisi hatua anazoweza
kuchukua mpiganaji katika hali ya hatari kama iliyokuwapo wakati huo;
Kwa hiyo nilikuwa nimejiandaa ki mwili na kisaikolojia.
Nilipomkaribia, kiasi cha umbali wa mita kumi hivi nikanyoosha
mkono wangu wa kulia kumuonesha kitambulisho changu “Tanzania
government officer” nilimwambia kwa kujiamini huku nikimpa nafasi ya
13
GO DW IN C H IL EWA | 14
14
15 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
15
GO DW IN C H IL EWA | 16
16
17 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
17
GO DW IN C H IL EWA | 18
18
19 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
19
GO DW IN C H IL EWA | 20
20
21 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
21
GO DW IN C H IL EWA | 22
22
23 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
Sikuwa na mazoea ya kuja katika ofisi hii mara kwa mara kwani
hakikuwa kituo changu cha kazi. Ingawa miaka ya nyuma niliwahi
kufanya kazi kadhaa zilizonifanya nifike makao makuu mara kwa mara,
bado sikujenga mazoea yoyote na watu wa hapa. Tofauti na idara
nyingine za serikali, idara ya usalama wa Taifa ina utaratibu maalum
unaowazuia maafisa wake kwenda kwenye ofisi zisizo vituo vyao vya
kazi bila sababu ya msingi. Utaratibu huu huwahusu maafisa wote bila
kujali vyeo vyao, au idadi ya miaka waliyoitumikia idara.
Kwa ujumla hata kama ofisi ya kitengo kimoja iko kwenye jengo
moja na kitengo kingine, maafisa wa vitengo hivyo hawaruhusiwi
kutembeleana ofisini bila ruhusa au sababu za msingi. Endapo afisa
atalazimika kwenda katika ofisi nyingine, nje ya kituo chake cha kazi
kwa dharula au sababu nyingine yoyote hutakiwa kuomba kibali (gate
pass) ya kumruhusu kufanya hivyo. Vinginevyo anaweza kulazimika
kubaki kwenye ofisi ya mlinzi. Utaratibu huu uitwao compatimentation
huisaidia idara kutunza siri, kuendesha operesheni zinazojitegemea, na
kuwazuia maadui wa taifa kujipatia taarifa muhimu kwa urahisi (endapo
watapenyeza mtu wao ndani ya idara).
Idara imeweka kanuni na taratibu hizi ili kulinda nyaraka na siri za
idara, na pia kujenga nidhamu ya maafisa wake. Kwa ujumla kila afisa
anajua kwamba muda wowote katika ajira yake anaweza kuwa
anafuatiliwa nyendo zake kwa sababu mbalimbali. Aidha kwa lengo la
kuthibitishwa uwezo na umakini wake ili apandishwe cheo na kupewa
madaraka makubwa, au kwa kutiliwa mashaka. Kutokana na utaratibu
huu, hakuna afisa yeyote, wa mahali popote na au cheo chochote (hata
mkurugenzi mkuu wa idara –DGIS) anayeweza kujisifu kuwa anajua
kila kitu kinachotendeka ndani ya idara ya usalama wa Taifa.
Tulipofika sehemu ya maegesho, DOI akasimamisha gari na
kuzima injini. Sote wawili tukateremka na kutembea sambamba
kuelekea ndani ya jengo lililokuwa mita chache mbele yetu. Hali katika
ofisi hii ilikuwa nzuri kuliko ile niliyoikuta katika ofisi ya RSO Dar es
salaam. Baadhi ya vioo vya madirisha vilikuwa vimepasuka kutokana
na mshindo wa bomu lakini jengo lilionekana kuwa imara. Maafisa
wote walikuwa katika hali ya tahadhari kubwa ingawa walishaambiwa
mahali ulikotokea mlipuko. Walinzi wa kumbi (coridol) walionekana
kuwa na msongo zaidi. Kila kumbi tuliyopita walinzi walikuwa imara,
wameshikilia silaha kubwa za kivita tayari kwa mapambano. Tangazo
maalum lilikuwa limeshatolewa kuwajulisha maafisa hao kwamba
magaidi wamelipua ubalozi wa Marekani, na haijulikani kama
23
GO DW IN C H IL EWA | 24
24
25 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
25
GO DW IN C H IL EWA | 26
26
27 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
3
Siku ya jumatatu tarehe 10 August, 1998 nilifika ofisini, Ilala Boma,
mapema kuliko kawaida. Pamoja na kuwahi huko ofisini nilimkuta bosi
wangu, mama Murusuli na maafisa wengine wote wakiwa wameshafika,
wameketi kuzunguka meza ya mkutano, tayari kwa SITREP. Bila
kupoteza muda niliwajulia hali na kuketi katika kiti kilichokuwa wazi.
27
GO DW IN C H IL EWA | 28
Kikao cha asubuhi hii kilikuwa muhimu sana, na cha aina yake.
Kwa maafisa wapya hiki kilikuwa kikao cha kwanza baada ya tukio
kubwa la kigaidi nchini hali iliyowafanya wawe na mchecheto wa aina
yake. Mimi pia nilikuwa katika hali isiyo ya kawaida. Matukio ya siku
mbili zilizopita yalinionesha wazi kazi, na hatari iliyokuwa mbele yetu.
Wakati huo ilikuwa imepita miaka tisa tu tangu nilipotoka kwenye
mapambano na magaidi wa RENAMO. Kwa mama Murusuli mambo
yalikuwa magumu zaidi. Yeye ndiye aliyekuwa katibu wa Kamati ya
Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Ilala. Kamati iliyokuwa na jukumu la
kuhakikisha wilaya ya Ilala, (ambayo ndiyo kitovu cha Dar es Salaam)
inakuwa salama. Kutokana na wadhifa huo alipaswa kuwasiliana na
mkuu wa wilaya (ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati) ili kuitisha kikao
cha dharula. Kikao kilitakiwa kufanyika mara tu baada ya SITREP ili
kuweka mikakati ya ulinzi na usalama wilayani.
Kama kawaida DSO ndiye aliyefungua kikao kwa kutoa maelezo
mafupi kuhusu hali ya usalama nchini. Tofauti na siku nyingine
ambapo masuala ya uchumi, siasa na huduma za kijamii yalitawala zaidi,
siku hiyo agenda kuu ilikuwa suala la ugaidi. Kwa dakika kumi hivi
DSO alitusomea taarifa maalum iliyotolewa na makao makuu kuhusu
shambulio lililotokea katika ubalozi wa Marekani. Taarifa hiyo ilieleza
kuwa watu 10 raia wa Tanzania, walikuwa wameshapoteza Maisha yao,
na wengine 72 walikuwa wamejeruhiwa. Wahanga hawa walikumbwa
na umauti wakiwa ndani ya ubalozi wa Marekani kwa shughuli za
kiofisi, au nje ya ofisi hizo kwa shughuli binafsi na biashara. Wengine
ni pamoja na wafanyakazi wa balozi za Nigeria na Ufaransa zilizokuwa
jirani na ubalozi wa Marekani, na wapita njia.
Kufuatia tukio hilo siku ya Jumapili, tarehe 9 August, rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mheshimiwa Benjamin Mkapa
alitembelea eneo la tukio kujionea hali halisi ilivyokuwa. Akizungumza
ubalozini hapo rais Mkapa alisema wahalifu waliolipua ubalozi huo
hawautakii mema uhusiano mzuri uliokuwepo kati ya Tanzania na
Marekani, na kusisitiza kuwa “Adui wa Marekani ni adui wa Tanzania” na
kuahidi kuwa serikali ya Tanzania itashirikiana na Marekani katika
kuwasaka wahalifu waliohusika. Pamoja na kutembelea ubalozi huo
rais Mkapa pia alitembelea hospitali ya Muhimbili ambako Watanzania
63 walikuwa wamelazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Majeruhi
wengine 18 walikuwa katika hospitali ya Agakhan.
Taarifa hiyo pia iligusia hali ilivyokuwa jijini Nairobi, nchini Kenya
kufuatia tukio la kigaidi lililofanyika sambamba na hili. Watu mia moja
28
29 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
na saba (107) walikuwa wamepoteza Maisha yao, kati yao nane wakiwa
raia wa Marekani. Waokoaji walikuwa wakiendelea kuwatafuta
Wamarekani wengine watano waliokuwa bado wamefunikwa na
kwenye kifusi. Watu zaidi ya elfu mbili na mia mbili (2200) walikuwa
wamejeuhiwa, wengine wakiwa mahututi.
Taarifa hiyo pia iligusia uwepo wa cell ya kigaidi nchini. Uchunguzi
wa awali ulionesha magaidi waliohusika na shambulio la ubalozi wa
Marekani hawakuwa wababaishaji; bali watu wenye uzoefu wa hali ya
juu katika kupanga, na kutekeleza mashambulizi makubwa ya kigaidi.
Hii iliashiria uwepo kwa cell za kigaidi nchini, zinazofanya kazi kwa
ushirikiano au maelekezo ya kundi kubwa zaidi. Baadhi ya makundi
yaliyowekwa katika orodha ni Alqaida, linaloongozwa na Osama bin
Laden, Egyptian Islamic Jihad, Hizbollah, na Hamas. Idara ilipaswa
kuelekeza nguvu zake zote katika ukusanyaji wa taarifa za kiintelejensia
ili kuvitambua vikundi hivyo, washirika wake, wafadhili wake, na jinsi
vinavofanya kazi.
Baada ya maelezo hayo mama Murusuli alitoa nafasi kwa maafisa
kujadili taarifa hiyo kabla ya kuanza utekelezaji wake katika medani.
Morgan ndiye aliyekuwa wa kwanza kunyoosha mkono wake juu,
kuashiria kuwa anataka kuzungumza.
“DSO nakushukuru sana kwa taarifa uliyotupa” Morgan alianza
baada ya kupewa nafasi ya kuongea. “ Kusema kweli taarifa ya makao
makuu imegusia vitu vingi na vya msingi kwa ujumla wake. Lakini
mkuu, sisi tumebahatika kidogo. Mmoja wa maafisa waliofika katika
ubalozi wa Marekani mara tu baada ya tukio ni mwenzetu wa hapa
ofisini; na kwa bahati nzuri asubuhi hii tuko naye hapa. Nafahamu hilo
kwa sababu mimi ndiye niliyemuagiza kwenda kufuatilia mlipuko
tuliousikia. Kwa hiyo naomba kama inawezekana, umruhusu Chilewa
naye atueleze kwa kina mambo aliyoyashuhudia. Naamini maelezo
yake yatatupa picha nzuri zaidi, na tutakapoanza kudadavua tutakuwa
katika nafasi ya kufanya hivyo kwa mapana” Morgan alimalizia.
Hoja hiyo iliungwa mkono na maafisa wengine waliokuwa katika
SITREP. Maafisa hao walionesha shauku kubwa ya kutaka kujua
reaction ya wanajeshi wa Marekani (Marines) waliokuwa wakilinda
ubalozi, na hali halisi ilivyokuwa katika ofisi ya RSO Dar es Salaam
iliyokuwa umbali mfupi tu kutoka ubalozini.
“Nakubaliana nawe Morgan, Chilewa ana maelezo mazuri sana”
Alijibu mama Murusuli. “Hata hivyo taarifa yake haiwezi kuwa sehemu
ya SITREP hii, maana imeshawasilishwa makao makuu. Ila kwa faida
29
GO DW IN C H IL EWA | 30
ya maafisa mliopo hapa, namruhusi awaeleze kwa kifupi ili nanyi mjue
hali halisi ilivyokuwa” Mama Murusuli alimaliza maelezo yake huku
akiniashiria nianze kuzungumza.
Kwa kirefu nikawaeleza jinsi mambo yalivyokuwa tangu
nilipoachana na akina Morgan, hadi nilipoondoka ubalozini kurudi
nyumbani. Nilijitahidi sana kuwapa maelezo ya kina, ili kuwapa picha
halisi ya mfululizo wa matukio bila kugusia mawasiliano yangu na DOI
wala taarifa nilizokuwa nimeziwasilisha makao makuu. Mambo hayo
yalishaingia katika utaratibu wa usiri sambamba (compatimentation) hivyo
sikupaswa kuyaeleza kwa maafisa wengine.
Baada ya maelezo yangu tuliendelea na SITREP kwa dakika
zisizopungua arobaini na tano hivi, kujadili kila suala tuliloona ni
muhimu kufuatia hali tete iliyokuwepo nchini. Kubwa kuliko yote
lilikuwa suala la kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo
yaliyokuwa yakituhusu. Kwa bahati mbaya mpaka wakati huo tulikuwa
hatujapata fununu ya watu waliofanya tukio la kigaidi. Hatukujua
walikuwa wamekusudia kufanya matukio mangapi, maeneo gani, na
kwa wakati gani. Kwa sababu hiyo ulinzi wa hali ya juu ulihitajika katika
maeneo yote muhimu tuliyokuwa tukiyasimamia.
Maeneo tuliyoyapa kipaumbele zaidi ni pamoja na majengo ya
serikali, hospitali za Muhimbili, na Agakhan, masoko na sehemu
maarufu za biashara, mahoteli ya kitalii, stesheni na vituo vya mabasi,
shule maarufu hasa za mjini kati, kumbi za starehe, mitaa yenye
mikusanyiko ya watu wengi, na madaraja muhimu. Uimarishaji ulinzi
ulipaswa kufanyika kwa kushirikiana na jeshi la polisi, idara ya
Uhamiaji, na jeshi la wananchi wa Tanzania.
Jambo lingine tulilolitazama kwa kina, ni suala la wahamiaji
haramu waliokuwa wamejazana nchini. Suala hili lilikuwa nyeti kwa
sababu maafisa wengi walihisi magaidi waliolipua ubalozi wa Marekani
walikuwa raia wa kigeni, au watanzania waliofundishwa na kupewa
msaada na wageni walioingia nchini kutoka ughaibuni. Wakati huo
kulikuwa na idadi kubwa ya wakimbizi kutoka Rwanda, Burundi,
Somalia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na Ethiopia.
Ongezeko la wageni hawa lilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mauaji ya
kimbali yaliyotokea nchini Rwanda, na mapigano yasiyokwisha katika
nchi za Kongo, Burundi, na Somalia. Wengi wa wahamiaji hawa
walitokea katika makambi ya wakimbizi yaliyokuwa kaskazini mwa
Tanzania, au waliingia nchini kwa njia za panya.
30
31 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
31
GO DW IN C H IL EWA | 32
32
33 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
33
GO DW IN C H IL EWA | 34
4
Ilinichukua dakika arobaini na tano tu, kukabidhi kazi zangu zote kwa
DSO. Mama Murusuli alinipongeza mno kwa kazi nzuri niliyoifanya
siku ya ijumaa kiasi cha kuuridhisha uongozi wa juu wa idara.
“Umefanya kazi nzuri iliyotujengea heshima sisi sote. Nilipoongea na
DOI amenipongeza sana. Amesema mama Murusuli unafanya kazi nzuri
mno. Vijana wako wana weledi wa hali ya juu. Hili si jambo dogo kwangu,
ni sifa kwangu binafsi na kwa maafisa wote walio chini yangu”
Aliniambia mama huyo aliyekuwa akinipenda na kunisaidia kama
mwanawe. Nami kama ilivyo ada nilimshukuru kwa kunipa majukumu
34
35 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
35
GO DW IN C H IL EWA | 36
36
37 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
37
GO DW IN C H IL EWA | 38
38
39 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
(RSO) jambo hilo halipo. Pili mimi nina majina ya maafisa wote
wanaotakiwa kuwepo hapa. Jina lako Chilewa halipo.”
Nikabaki kimya, maana sikuwa na jibu lolote.
“Kwa hiyo Chilewa sasa hivi ondoka. Rudi kwenye kituo chako cha
kazi. Na ukifika tu, andika maelezo kwa nini umekuja kwenye kazi
inayohusisha wageni (FBI) bila kibali. Halafu maelezo yako mpe DSO,
mama Murusuli aniletee ofisini kwangu kesho asubuhi. Umenielewa?
Alimaliza huku akinitazama kwa ukali.
“Nimekuelewa mkuu” Nilijibu huku nikihisi jasho jembamba
likitiririka usoni kwangu. Kwa aibu nikageuka na kuondoka taratibu
kuelekea lango kuu. Vishindo vya hatua zangu vilisindikizwa na
vicheko, miguno, na minong’ono ya maafisa wenzangu, waliokuwa
wakinishangaa kwa kitendo nilichofanya.
Morgan alikuwa akijiandaa kuondoa gari kurudi ofisini.
Aliponiona nikitembea haraka haraka kumfuata, akanisubiri ili
anipeleke ninapotaka kwenda.
“Vipi Chilewa, kulikoni? Mbona sura imekubadilika?”
Aliniuliza mara tu nilipofungua mlango wa Pajero na kujirusha katika
kiti cha abiria.
“Turudi ofisini” nilimwambia huku sauti yangu ikiwa na mitetemo.
“Kazi hamuanzi leo? Au mnakutana baadae?
“Hapana, RSO mzee Zuberi amenifukuza” Nilimwambia huku
nikijaribu kutabasamu kuzuia hasira iliyokuwa imeanza kunipanda.
“Amekufukuza? Una maana gani? Aliniuliza kwa mshangao.
Bila kuficha nikamueleza mambo yote tangu mwanzo hadi mwisho.
“Unasema ulimwambia kuwa DOI amepiga simu yeye mwenyewe
kumpa maagizo DSO ? Morgan aliniuliza kwa mshangao
“Nimemwambia kila kitu”
“Na bado akasisitiza uondoke?
“Ndiyo”
“Siamini” Morgan alijibu kwa mshangao.
“Wakati tunazungumza maafisa wote walikuwepo, kwa hiyo siwezi
kupunguza wala kuongeza neno” Nilimwambia kwa kusisitiza baada ya
kuona haniamini.
“Siyo sikuamini, nashangaa kwamba RSO amekataa maagizo ya
DOI mbele ya maafisa wote hao. Anajipalia makaa ya moto”
“Labda kuna mabadiliko. Inawezekana DOI alibadili uamuzi wake
baada ya kuongea na mama Murusuli. Au pengine kuna jambo
tusilolijua”
39
GO DW IN C H IL EWA | 40
5
Ofisini tuliwakuta maafisa wenzetu wakiwa wamesharudi kwenye
madawati yao. Maafisa hao walishangaa mno kuniona, kwani walikuwa
na hakika kazi niliyokuwa nikienda kuifanya ingechukua muda mrefu
kuikamilisha. Hata hivyo hatukuwa na sababu ya kuwaeleza
kilichotokea. Sote wawili tukaenda moja kwa moja ofisini kwa DSO.
Tulimkuta Mama Murusuli akiwa bado ameketi mahali palepale,
akisoma mojawapo ya mafaili yaliyokuwa mezani kwake. Alipotuona
tukiingia, akafunga faili hilo na kutugeukia
“Vipi?” aliuliza kwa mshangao
“RSO amenirudisha” Nilimjibu huku nikivuta kiti na kukaa.
Morgan naye akazunguka na kukaa katika kiti kilichokuwa upande wa
pili wa meza.
“Una maana RSO Zuberi? Aliuliza kwa mshangao.
“Ndiyo”
“Yeye kakurudisha kama nani?
“Nadhani yeye ndiye anayeongoza task force. Sina uhakika, maana
sikupewa utambulisho wowote”
“Ulimwambia kwamba DOI ndiye ameagiza uende?
“Nimwambi” Nikamueleza kila kitu kilichotokea tangu nilipofika hadi
mahali hapo hadi tulivyoondoka. Sikuishia hapo tu, nikamueleza pia
jinsi nilivyojisikia kwa kudhalilishwa mbele ya maafisa wenzangu.
“Usijisikie vibaya Chilewa. Mzee Zuberi ndivyo alivyo, ana
misimamo ya ajabu. Sisi tumeshamzoea. Wewe ulikuwa hujaingia
kwenye aanga zake ndiyo maana umeshituka hivyo” Mama Murusuli
alijaribu kunipooza huku akicheka.
“Ngoja nimpigie simu nimfahamishe kuwa DOI ndiye aliyeagiza
uwepo kwenye hiyo task force” alimalizia.
“Samahani mkuu” Morgan alidakia “Kwa mujibu wa maelezo ya
Chilewa, inaonekana RSO hakufurahishwa na kitendo cha DOI
kupigia simu moja kwa moja kwako, badala ya kumpigia yeye. Kwa
hiyo ukimpigia, mnaweza msielewane vema. Maana hata kule
kumwambia Chilewa aandike maelezo, halafu akupe wewe uyapeleke
40
41 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
41
GO DW IN C H IL EWA | 42
__________
42
43 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
SURA YA PILI
IDARA (TISS)
T
ukio la kulipuliwa kwa ubalozi wa Marekani jijini Dar es
salaam, lilikuwa kama kengele ya tahadhari kwa vyombo vya
ulinzi na usalama vya Tanzania. Kwa miaka mingi nchi hii
ilikuwa ikisifika kama kisiwa cha amani katika Afrika, hali
iliyoifanya kuwa kimbilio la wakimbizi. Wakati Kongo DRC, Rwanda,
Burundi, Uganda, na nchi nyingine jirani zikikumbwa na migogoro ya
kisiasa, au vita vya wenyewe kwa wenyewe, watanzania waliendelea
kuwa wamoja, watulivu, na wavumilivu hata pale walipokosa sukari, au
mchele wa kuwalisha watoto wao. Utulivu huo ulichangiwa kwa kiasi
kikubwa na misingi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea, iliyoasisiwa
mwaka 1967 na baba wa taifa, mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Misingi hiyo iliyojulikana kwa jina la Azimio la Arusha, pamoja na
lugha ya Kiswahili vilijenga umoja wa kitaifa na kuimarisha heshima ya
ki utu isiyojali kabila, lugha, wala udini.
Pamoja na utulivu huo, idara ya usalama wa Taifa (TISS) chini ya
mkurugenzi mkuu Emilio Mzena ilikabiliwa na changamoto za kila
namna. Baadhi ya changamoto hizo zilitokana na uchanga wa Taifa
kisiasa na ki-uchumi. Tanzania ilipata uhuru wake mwaka 1961 kutoka
43
GO DW IN C H IL EWA | 44
44
45 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
45
GO DW IN C H IL EWA | 46
46
47 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
47
GO DW IN C H IL EWA | 48
48
49 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
2
Mashambulizi ya mabomu katika ofisi za ubalozi wa Marekani
jijini Dar es Salaam na Nairobi Kenya yalifanyika wakati asilimia kubwa
ya raia wa Marekani wakiwa usingizini. Ingawa jijini Dar es salaam
muda huo ilikuwa ni saa nne na nusu asubuhi, jijini Washington DC
ilikuwa ndiyo kwanza imetimia saa tisa na nusu alfajiri. Muda muafaka
wa kuchapa usingizi. Hata hivyo mamilioni ya wamarekani wanaofanya
kazi za usiku (night shift) viwandani, katika majumba ya starehe,
mahospitalini, na idara nyingine nyeti walikuwa macho kushuhudia
kituo cha televition cha CNN international kikirusha matangazo yake
mubashara kuelezea janga lililotokea.
Kati ya watu waliopata taarifa mapema zaidi, walikuwa Louis
Free, mkurugenzi mkuu wa idara ya ukachelo ya Marekani Federal
Bureau of Investigation (FBI) yenye makao yake makuu jijini Washington
DC na Richard Alan Clarke aliyekuwa mratibu wa usalama wa Taifa,
49
GO DW IN C H IL EWA | 50
50
51 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
51
GO DW IN C H IL EWA | 52
3
Masaa machache baadae, maafisa wa juu wa serikali ya Marekani
walifanya kikao cha dharula na viongozi wa serikali ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania. Mazungumzo hayo yalilenga kuweka mikakati
ya pamoja katika kusaidia wahanga wa bomu, kuimarisha uhusiano wa
kirafiki, na kushirikiana katika mapambano dhidi ya ugaidi. Kwa miaka
mingi ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani ulikuwa kubabaisha tu
kutokana na tofauti za kisiasa zilizokuwepo kwa zaidi ya robo karne.
Kulegalega kwa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani
kulichangiwa kwa kiasi kikubwa na msimamo wa Tanzania katika
kupigania ukombozi wa kusini mwa Afrika. Wakati Tanzania ikiwa
mwenyekiti wa nchi tano zilizo mstali wa mbele katika ukombozi wa
kusini mwa Afrika, Marekani na Uingereza walikuwa ndiyo washirika
wakubwa wa serikali ya makaburu wa Afrika ya kusini, iliyokuwa
ikongozwa na P.W Botha na washirika wake.
Ili kukwamisha harakati za ukombozi wa Afrika ya kusini, shirika
la ujasusi la Marekani (CIA) lilifanya hujuma nyingi, na propaganda za
kila namna zilizolenga kuiyumbisha Tanzania kiuchumi. Baadhi ya
hujuma hizo zilifanikiwa, nyingine zilibainika na kuzimwa kimya kimya,
na nyingine zilitumiwa kama propaganda ya kupinga ubeberu wa
Marekani na washirika wake. Kwa mfano, katika miaka ya mwishoni
mwa 1970 Tanzania iliituhumu Marekani kwa kuzalisha, na kusambaza
wadudu wa mazao waitwao viwavi jeshi. Wadudu hao, kama lilivyo
jina lao, walikuwa wakitokea kwa makundi makubwa (kama ya nzige)
kushambulia mazao ya chakula hususan mahindi yaliyokkuwa
mashambani. Tofauti na nzige ambao walipotokea (miaka ya nyuma0
wananchi walikuwa wakiwakamata na kuwala, viwavi jeshi walikuwa
hawaliki, wala hawatamaniki. Sambamba na viwavi jeshi, pia waliibuka
wadudu wanaoshambulia mahindi yaliyokaushwa, na kuhifadhiwa
ghalani. Wadudu hawa waliojulikana kama dumuzi waliharibu kwa kiasi
52
53 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
53
GO DW IN C H IL EWA | 54
_______
54
55 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
SURA YA TATU
KIKOSI KAZI
(TANBOMB)
55
GO DW IN C H IL EWA | 56
56
57 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
2
Saa sita mchana ilinikuta nikiwa na maafisa wengine kumi na nne
walioteuliwa kushiriki katika kikosi kazi. Maafisa hawa walikuja kutoka
kwenye ofisi na vitengo mbalimbali vya idara. Nusu ya maafisa hao
nilikuwa nikifahamiana nao vema kwa sababu mbalimbali; Aidha
57
GO DW IN C H IL EWA | 58
58
59 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
uzito maelezo yake, Romeo alianza kwa kusisitiza kwamba kila afisa
aliyeteuliwa kushiriki katika task force alikuwa amewekwa kwenye
mizani, na kuonekana anafaa kwa kila hali. Kwa sababu hiyo
mkurugenzi mkuu ana uhakika wa kuona kazi ikitendeka kwa weledi
na kwa kufuata misingi na kanuni za idara.
“Wengi wenu itakuwa mara yenu ya kwanza kufanya kazi na
mawakala wa nje (FBI) na pia kufanya uchunguzi wa mlipuko wa
bomu; hata hivyo, idara imewaamini kuwabebesha jukumu hilo. Ni
wajibu wenu kujifunza na ku adapt mbinu na mazingira ya kazi
mnayokwenda kuifanya haraka iwezekanavyo ili msiwe mzigo kwa
wageni. Kumbukeni, mawakala wa FBI na wengine wote watakuwa
wakifuatilia utendaji wenu kwa ukaribu zaidi kuliko wenzenu wa idara
ya upelelezi wa makosa ya jinai. Hii ni kwa sababu idara ya usalama wa
Taifa ndiyo kipimo cha ukamilifu wa uwezo na ufanisi wa vyombo vya
ulinzi na usalama nchini” Alieleza kwa hamasa.
“Jambo la pili mnalotakiwa kufanya kwa weledi wa hali ya juu ni
kuangalia nyendo za wageni wote mtakaofanya nao kazi. Kama
mjuavyo serikali ya Marekani imeleta mawakala kutoka idara, vitengo,
na mashirika yake yote ya ukachelo na ujasusi. Mawakala hawa
wamekuja kwa lengo moja lililo wazi, kuchunguza tukio la mlipuko wa
bomu. Lakini kama ilivyo kawaida ya mashirika yote ya kijasusi, kila
unapopatikana mwanya wa kuingia katika nchi nyingine, huwa ndiyo
nafasi ya kufanya kila linalowezekana. Kwa hiyo ingawa tunashukuru
kwamba wageni hawa watatusaidia kuwatafuta magaidi waliohusika na
unyama huu, na kuvunja mtandao wao, ni lazima pia tuangalie mambo
gani mengine watakayo onesha interest. Ni jukumu letu kufanya hivyo,
na kwa umakini wa hali ya juu ili tusichezwe shere nyumbani kwetu.
Kwa hiyo kila afisa atawajibika kuangalia kwa makini nyendo za
mawakala atakaokuwa nao. Jua wanafanya nini, wapi na kwanini. Kama
wanakutana na mtu sikiliza wanauliza maswali gani, Je, maswali hayo
yanahusiana moja kwa moja na tukio la bomu, au yanalenga kukusanya
taarifa tofauti kwa malengo mengine? Kama wana interest ya kujua vitu
tofauti fuatilia kujua ni vitu au habari za aina gani, kutoka kwa watu wa
aina na kariba gani, na nini muitikio wa watu hao” Alisisitiza
Jambo lingine tunalotakiwa kufuatilia kwa makini, ni uwezekano
wa mawakala hawa ku recruite watoa habari katika idara, jeshi la polisi
na idara nyingine za serikali. Kumbukeni CIA ni mabingwa wa kuajiri
watoa habari duniani, na kwa bahati mbaya katika timu ya wapelelezi
waliokuja hatuna hakika wakala yupi ni FBI hasa, na yupi ni wakala wa
59
GO DW IN C H IL EWA | 60
60
61 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
3
Kazi ya uchunguzi ilianza rasmi baada ya kikao cha pamoja kati
ya maafisa wa Tanzania na mawakala wa FBI na washirika wake. Kikao
hicho ndicho kilichoweka msingi wa jinsi kazi itakavyofanyika. Maafisa
wote wa idara walioteuliwa kushiriki katika operesheni hii walihudhuria
kikao hiki. Maafisa wa idara ya upelelezi wa makosa ya jinai pia
walikuwepo wakiongozwa na msaidizi wa mkurugenzi wa makosa ya
jinai (DCI) kamisha mwandamizi msaidizi wa polisi (Senior Assistant
61
GO DW IN C H IL EWA | 62
62
63 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
63
GO DW IN C H IL EWA | 64
64
65 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
65
GO DW IN C H IL EWA | 66
66
67 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
67
GO DW IN C H IL EWA | 68
68
69 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
69
GO DW IN C H IL EWA | 70
70
71 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
71
GO DW IN C H IL EWA | 72
72
73 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
73
GO DW IN C H IL EWA | 74
74
75 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
75
GO DW IN C H IL EWA | 76
76
77 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
77
GO DW IN C H IL EWA | 78
78
79 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
_____________
.
.
79
SURA YA NNE
FUNUNU
W
iki zilipita kwa kasi kama kufumba na kufumbua. Wingi
wa majukumu na kashikashi zake ulitufanya tulazimike
kusahau maisha ya uhuru na starehe tuliyokuwa
tumeyazoea. Kila siku ilikuwa na mambo mapya,
muhimu, na ya kuumiza kichwa kuliko siku iliyotangulia. Kila saa mbili
asubuhi tulikutana kwenye eneo la tukio, au ofisini kwa msaidizi wa
mkurugenzi wa makosa ya jinai Senior Assistant Commissioner of Police
(SACP) Robert Manumba kupeana taarifa (briefing) ya maendeleo ya
uchunguzi. Taarifa hiyo ilikuwa muhimu sana katika kupanga namna
ya kufuatilia leads zilizopatikana toka vyanzo mbalimbali. Kwa ujumla
kazi yetu ilikuwa imeanza kuzaa matunda, na muelekeo wa upelelezi
ulikuwa umeanza kujipambanua.
Katika kipindi hicho pia tulipata fursa ya kutembelewa na
aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la ukachero la Marekani (FBI).
Bwana Louis Free. Mkurugenzi huyo aliwasili nchini tarehe 20 August
1998 kujionea madhara yaliyosababishwa na shambulio la bomu na pia
kututia moyo maafisa wa kikosi kazi (Task Force) tuliokuwa tukifanya
kazi ya kuwasaka magaidi husika ili waweze kuchukuliwa hatua za
kisheria. Akiwa jijini Dar es Salaam mkurugenzi Louis Free alipokea
taarifa ya uchunguzi kutoka kwa viongozi wetu, na akashiriki katika
kupanga mikakati ya kuimarisha ulinzi, na kutanua wigo wa upelelezi
Yapo mambo mengi ya kutia moyo yaliyokuwa yameshafanyika
kufikia wakati huo. Jambo la kwanza lilikuwa mafanikio ya uchunguzi
wa eneo la tukio. Baada ya kazi ngumu ya siku kadhaa, wataalam wa
uchunguzi wa milipuko (Bomb Squad) wakishirikiana na timu ya
uchunguzi wa eneo la tukio (Forensic experts) walifanikiwa kupata
80
81 | SH U H U DA ZA J A SU SI – NDA NI YA IDA RA
81
GO DW IN C H IL EWA | 82
baadae yalipatikana majibu kuwa chasses hiyo ilikuwa ya roli dogo (truck)
aina ya Nissan Atlas lililotengenezwa nchini Japan. Ili kupata taarifa
zaidi kikosi kazi kilituma namba hiyo kwenye ofisi za Interpol na
mawakala wengine ili waweze kufuatilia kiwanda kilichotengeneza gari
hiyo kujua iliuzwa wapi na kwa nani. Haikuchukua muda mrefu
tukaletewa ujumbe kuwa gari hiyo iliingizwa nchini Tanzania na
kampuni iitwayo JABA Tanzania Limited. Kampuni hii ilikuwa
ikifanya biashara ya kuagiza magari toka sehemu mbalimbali duniani
na kuyauza kwa wateja wao kwa fedha taslimu. Mengi ya magari hayo
yalikuwa yaliyotumika (used cars) hivyo yaliuzwa kwa bei nafuu iliyovutia
watu wa kipato cha kawaida.
Bila kupoteza muda siku hiyohiyo waliteuliwa maafisa watano
kutoka miongoni mwetu kuifuatilia kampuni ya JABA. Lengo la
ufuatiliaji huo lilikuwa kujua kama kampuni hiyo bado ilikuwa mmiliki
halali wa gari hiyo iliyotuhumiwa kubeba bomu. Kama JABA ilikuwa
mmiliki halali basi ilipaswa kueleza gari hiyo iilikuwa wapi wakati huo,
na kama liliuzwa lilinunuliwa nani, na kwa utaratibu gani. Pamoja na
hayo maafisa hao walipaswa kuwatambua wamiliki wa kampuni hiyo,
kujua taratibu za uendeshaji wa kampuni hiyo, na kama ina uhusiano
wowote na vikundi vya kigaidi na au washirika wake.
Jambo la tatu kwa umuhimu likuwa matokeo ya uchunguzi wa
mawasiliano ya simu za watuhumiwa. Baada ya safari nyingi kwenye
ofisi zote za makampuni ya simu nchini, hatimaye tulifanikiwa kupata
namba za simu kadhaa zilizoonesha dalili ya kutumiwa na watuhumiwa
wa ugaidi. Namba ya kwanza ilikuwa 6880488
. Lorem ipsum dolor sit abet, constitutor despising alit. Prion sod
mi id ligula truism moles tie. Pelletize critique frangible augur, id
laborites’ pursue. Crams dui mi, macules egret rises id, sagittal pharetra
nigh. Present varies molls nulled. Present consequent magna a pharetra
ornate. Sid magna ulna, cangue vitae torpid a, blander dipygus eras.
Varmus gravida semper null, varies molies risks susceptive evet. Fusc
tempos risks ague, majestic a junto dictum non. Duisk vet puros
convallis, modesties eques utricles, Bibendum veldt. Nam quam nisi,
gravida vet subscript sod, plenitude sit abet sem. Pharsalus au dictum
orca. Pelletize in pharetra libero. Sid a ornate nisi, diapaus effector
82