You are on page 1of 1

Muswada wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi

malengo yake kwa mujibu wa Sheria hii.

Kamati za Bodi 10. Bodi inaweza, kwa madhumuni ya kutekeleza


majukumu yake kwa ufanisi, kuunda na kuteua kutoka miongoni
mwa wajumbe wake, kamati zozote kadri itakavyoona inafaa.

Uteuzi wa 11.-(1) Kutakuwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume


Mkurugenzi
Mkuu ambaye atateuliwa na Rais.
(2) Mtu atateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu ikiwa ana
sifa zifuatazo:
(a) amehitimu katika chuo kikuu kinachotambulika na
ana angalau shahada ya kwanza katika nyanja za
TEHAMA, uhandisi, sheria, uchumi, fedha au
utawala;
(b) ana uzoefu wa utumishi usiopungua miaka kumi
katika angalau moja ya nyanja zilizotajwa katika
aya (a); na
(c) ana ujuzi au utaalamu katika nyanja ya ulinzi wa
taarifa.

Muda wa 12. Mkurugenzi Mkuu atashika madaraka kwa kipindi


kuhudumu wa
Mkurugenzi cha miaka mitano na baada ya kipindi hicho kumalizika,
Mkuu anaweza kuteuliwa tena kwa kipindi kingine kimoja.

Watumishi wa 13.-(1) Tume, kwa kuzingatia sheria za utumishi wa


Tume
umma, itaajiri watumishi kwa idadi itakayohitajika kwa
madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu ya Tume.
(2) Tume inaweza kuteua washauri na wataalam katika
taaluma mbalimbali kwa kuzingatia vigezo na masharti
yatakayowekwa na Tume.

SEHEMU YA TATU
USAJILI WA WAKUSANYAJI NA WACHAKATAJI WA TAARIFA
BINAFSI

Usajili wa 14.-(1) Mtu hatakusanya au kuchakata taarifa binafsi


wakusanyaji na
wachakataji bila kusajiliwa kama mkusanyaji au mchakataji chini ya Sheria
hii.
(2) Mtu anayekusudia kukusanya au kuchakata taarifa
atawasilisha maombi ya usajili kwa Tume.
(3) Tume inaweza, katika muda utakaoainishwa katika
kanuni, kukubali au kukataa maombi yaliyowasilishwa kwa
mujibu wa kifungu kidogo cha (2).

11

You might also like