Professional Documents
Culture Documents
KIJITABU CHA SHERIA YA NDOA BY Mapabha Laban Abas
KIJITABU CHA SHERIA YA NDOA BY Mapabha Laban Abas
UTANGULIZI .............................................................................................vii
REJEA ........................................................................................................... ix
10. Ni kesi zipi zinazohusishwa na maana ya ndoa chini ya sheria hii? ....... 3
12. Ili ndoa iwe halali, ni mambo gani yanapaswa kuzingatiwa? ................. 3
13. Je, kabla ya muislamu kufunga ndoa anatakiwa afuate taratibu zipi? .... 5
i
14. Je, kwa upande wa wakristo wanatakiwa kufuata taratibu zipi wakati
wa kufunga ndoa? ...................................................................................... 6
15. Je ndoa isipofuata utaratibu wote ulioelezwa hapo juu itakuwa halali? . 6
18. Nani mwenye uwezo wa kupinga kuwa hakuna ndoa bali kuna dhana ya
ndoa? .......................................................................................................... 7
19. Mtu yeyote mwenye kupinga kuwa hakuna ndoa bali kuna dhana ya
ndoa anapaswa kuwa na ushahidi gani? .................................................... 7
20. Je, kwa ndoa zinazofungwa kimila ambazo hazihitaji kufanyika kwa
sherehe wala hakuna cheti cha ndoa kinachotolewa, sheria inasemaje ? . 7
21. Mtu anayesema kuwa wanaodhaniwa kuwa hawana ndoa halali wana
ndoa halali, anapaswa kuwa na ushahidi gani? ......................................... 7
ii
26. Ni mambo gani ambayo mahakama itayazingatia wakati wa
kubatilisha/kutengua ndoa iliyo batili toka mwanzo wa ufungaji wa ndoa
hiyo? .......................................................................................................... 9
32. Je, pindi ndoa inapofungwa, wanandoa wana haki na wajibu gani? ..... 13
36. Je, ni kesi zipi zingine zinazohusu ndoa ambazo mtu anaweza kupeleka
mahakamani? ........................................................................................... 16
iii
37. Mahakama inapofanya tathmini ya kutoa adhabu au fidia kwa mtu
aliyezini nje ya ndoa, itazingatia mambo gani?. ..................................... 17
42. Kwa nini Cheti kutoka bodi ya usuluhishi ya ndoa ni muhimu? .......... 18
44. Je, kila kesi ya ndoa ni lazima ipitie bodi ya usuluhishi ya ndoa?. ....... 19
50. Bodi itatumia utaratibu upi wa kumuita mtu aje ajibu shitaka? ............ 21
iv
51. Endapo mtu aliyeitwa kujibu mashtaka amekataa wito, bodi itafanya
nini?. ....................................................................................................... 21
54. Kwenye ndoa mtu yeyote anayo haki ya kuomba mahakama imfanyie
mambo yafuatayo; .................................................................................. 22
56. Mtu yeyote anayo haki ya kudai taraka, je mahakama itazingatia sababu
zipi ili iweze kutoa taraka kwa wanandoa? ............................................. 24
57. Endapo mwenza mmoja amefariki na wana ndoa halali, Je, mwenza
aliyebaki anaweza kuolewa au kuoa mtu mwingine bila kuomba
mahakama itoe amri ya kutambua kifo cha mwenza huyo na kubatilisha
ndoa hiyo?. .............................................................................................. 25
58. Kwa nini ni muhimu kuomba mahakama itoe amri ya kutambua kifo
cha mwenza kabla ya kufunga ndoa nyingine? ....................................... 25
61. Nini dhana ya taasisi hizi kupewa mamlaka ya kutoa taraka? .............. 27
v
62. Kwa ndoa za kiislamu kuna utaratibu tofauti na ndoa za dini zingine au
ndoa za kimila linapokuja suala la kutoa taraka?.................................... 27
64. Baada ya amri ya taraka ni kuvunjika kwa ndoa. Je, ndoa inapovunjika
nini athari zake? ....................................................................................... 28
vi
UTANGULIZI
Ndoa ni saklamenti kwa upande wa wakristo (Roman catholic), kwa
upande wa waislam ndoa ni mkataba. Kwa upande mwingine ndoa ni
muunganiko kati ya mwanaume na mwanamke waliokubali kuishi
pamoja kwa muda wote wa maisha yao.
vii
Baada ya kupitia jarida hili msomaji atapata uelewa mkubwa kuhusu
nini maana ya ndoa pamoja na mambo mengi yanayohusu ndoa na
baadae atajua utaratibu wa kufuata pindi ndoa yake inapofika mwisho au
kutoendelea tena kwa ndoa hiyo ikiwemo namna mahakama inapaswa
kugawa mali, kuuza, kutoa amri ya taraka na matunzo ya watoto (kama
walipatikana)
Shukrani za kipekee zimwendee Madam Mwasi Mbegu mhadhiri toka
Chuo Kikuu Cha Mt. Agostino Mwanza, yeye ni mtaalam wa sheria ya
ndoa ambaye amechangia kwa kiasi kikubwa mimi kuwa na ufahamu
mpana wa sheria ya ndoa na hatimaye kupelekea kuandaa kijitabu hiki
kwa ajili ya jamii.
viii
REJEA
Dhana” kuamini kuwa jambo fulani au kitu fulani ni sahihi kabla ya
kutokuwa sahihi kwa jambo au kitu hicho.
Ibara” ni maneno yapatikanayo kwenye katiba yaliyotengwa kwa
namba kwa ajili ya ufafanuzi wa jambo fulani la kikatiba
Kifungu” ni maneno yapatikanayo kwenye sheria husika yaliyotengwa
kwa namba kwa ajili ya ufafanuzi wa jambo fulani la kisheria.
Kuasili” kitendo cha kumtunza au kumchukua mtoto ambaye si wako na
kumfanya wa kwako.
No 13” sheria ya mtoto ya mwaka 2009 marekebisho ya 2019.
No 29” sheria ya ndoa ya mwaka 1971 iliyofanyiwa marekebisho
mwaka 2019.
ix
1. Maana ya familia kisheria ni nini?
Maana ya familia kisheria hutofautiana kulingana na jamii na jamii au
koo, pia maana hubadilika kutokana na mambo yanayotokea katika
jamii na maendeleo yake.
Kutokana na sheria ya mtoto ya 2009 inasema familia ni baba, mama,
watoto pamoja na ndugu wa karibu kama Babu, mjomba, shangazi,
binamu, wapwa na wajukuu wanaoishi pamoja.
1
5. Kundi la kisasa ni lipi?
Ni kundi ambalo hujipatia familia nje ya utarabu wa kawaida mfano,
mtu mmoja anaweza kumuomba mtu mwingine amzalie mtoto bila hata
kushiriki tendo la ndoa.
7. Ndoa ni nini?
Ndoa haina maana moja, ina maana kulingana na jamii inavyoipa
tafsiri. Pia inategemeana na chaguo la mtu kwa namna ambavyo
angependa kuitafsiri ndoa.
2
8. Maana ya ndoa chini ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971
iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 imetafsiriwaje?
Ni muunganiko wa hiari kati ya mwanaume na mwanamke ambao
wamekubali kuishi pamoja kama mke na mume kwa kipindi cha maisha
yao yote. (kifungu cha 9 cha no 29)
4
• vii. Kama ni muislam na ndoa inayofungwa ni ya mke wa pili na
kuendelea ni lazima mke au wake wa ndoa za awali waweke hiali.
(kifungu cha 38(1) (j) cha no 29).
• Wanaofunga ndoa ni lazima wawepo wote kimwili siku ya kufunga
ndoa. (kifungu cha 38(38)(1)(a) cha no 29)
• Ni muhimu wanandoa kufanya sherehe. Mfano;
• Ndoa ya bomani au ya kiserikali sherehe ishuhudiwe na msajiri
wa ndoa wa halmashauri ambayo ndoa ilifungiwa.
• Ndoa ya kimila, hii itasherehekewa kimila.
• Ndoa ya kikristo, isherehekewe katika kanisa wanakoabudu
wanandoa na ifungwe na mtu ambaye ana cheti au mamlaka ya
kufungisha ndoa.(kifungu cha 30(1) cha no 29)
• Ndoa ya kiislam, hii itasherehekewa kwa mujibu wa taratibu na
imani za kiislam. Sherehe au ndoa itafungwa na KADHI au afisa
ambaye ni muislam.(kifungu cha 23(3)(a) na 30(3) cha no 29)
5
14. Je, kwa upande wa wakristo wanatakiwa kufuata taratibu zipi?
• Kila dhehebu la kikristo lina utaratibu wake kuhusu hatua za
kufuata kabla ya ndoa.
• Ndoa ifungwe na padre au mchungaji aliyepewa kibali au mamlaka
ya kufungisha ndoa. (kifungu 23(3) (b) cha no 29).
6
18. Nani mwenye uwezo wa kupinga kuwa hakuna ndoa bali kuna
dhana ya ndoa?
Ni mtu yeyote mwenye mashaka na ndoa hiyo.
19. Mtu yeyote mwenye kupinga kuwa hakuna ndoa bali kuna
dhana ya ndoa anapaswa kuwa na ushahidi gani?
• Anapaswa kuthibitisha kuwa watu hao wanaodhani wana ndoa
halali hawakuwahi kufanya sherehe ya ndoa na hawana cheti cha
ndoa.
• Kama ni ya kiislam haijafuata utaratibu wa kiislam
• Kama ni ya kikristo haijafuata utaratibu wa kikristo
• Kama ni ya kiserikali haijafuata utaratibu wa kiserikali
• Kama ni ya kimila haijafuata utaratibu wa kimila
7
22. Ni matokeo gani ya kuwa na ndoa dhania?
• Endapo mkitengana mahakama haitatoa taraka
• Mali mlizopata kwa aina hiyo ya ndoa zitagawanywa kwa misingi
ya matunzo ya mwanamke na watoto tu. (kifungu cha 160(2) cha
no 29)
8
25. Je, mmojawapo kati ya wanandoa anaweza kubatilisha ndoa bila
kwenda mahakamani?
Hapana hana mamlaka hayo na haya ndiyo makosa ambayo watu
wengi wamekuwa wakifanya. Anamuacha mwenza wake
kinyemela na kufunga ndoa nyingine kabla ya kwenda
mahakamani kuomba mahakama itengue ndoa ya awali kwanza.
9
• Endapo mmoja kati ya wanandoa hakuwepo eneo la tukio bila
ridhaa ya mashahidi kukubali kutokuwepo kwake.
• Kuwepo kwa mashahidi wasio na sifa. Mfano chini ya miaka 18
• Endapo ndoa hiyo imefungwa kwa mkataba wa muda mfupi au
kwa kipindi cha muda fulani. Maana sheria ya ndoa inatambua
kuwa ndoa ni ya milele.
• Endapo mtu ana ndoa ya kikristo au kiislam baadae akifunga ndoa
nyingine kimila au kikristo. (kifungu cha 38 (1) (a) – (j) cha no
29)
• Endapo ndoa ni ya jinsia moja.(kifungu cha 9(1) cha no 29)
• Kukosekana kwa ridhaa ya mke endapo mume kama ni muislam
anataka kuongeza mke mwingine
10
• Endapo mmoja kati ya wenza anasumbuliwa na magonjwa ya
kuambukiza au ya kurithi kama siko seli
• Endapo mke atazaa na mwanaume mwingine tofauti na mume
wake. Isipokuwa mwanamke hataomba mahakama ibatilishe ndoa
kwa kigezo cha mume wake kuzaa na mwanamke mwingine. Hapa
sheria iliweka upendeleo kwa upande wa mwanaume
• Endapo mmoja kati ya wanandoa atakataa kufanya tendo la ndoa
na mume wake
• Endapo mmoja kati ya wanandoa hajapata ridhaa kutoka kwa
wazazi wake au amri ya mahakama ya kumruhusu kuolewa endapo
yupo chini ya umri wa miaka 18. (kifungu cha 39 (a) i-iv) (b) na
(c) cha no 29)
• Maumbile kuwa makubwa au madogo tofauti na kawaida.
Isipokuwa kama kuna uwezekano wa kufanyiwa upasuaji na tatizo
likaisha haina haja ya kuomba mahakama ibatilishe ndoa hiyo.
11
28. Je, ni jambo gani litapelekea mahakama kutobatilisha ndoa
iliyofungwa halali hata kama kukitokea jambo linalopelekea
kubatilishwa kwa ndoa hiyo?
Endapo mwanandoa ataendelea kuvumilia mapungufu au kosa la
mwenzake linalopelekea ndoa kuvunjika na asichukue hatua
yoyote ya kuomba mahakama ibatirishe /ivunje ndoa hiyo.
12
• Mahakama haitahalalisha vitu ambavyo vilifanyika haramu na
kuharamisha vitu ambavyo vilifanyika halali wakati wa ndoa.
• Maamuzi ya mahakama hayatozuia wanandoa hao kuwa mashahidi
kwa jambo lolote lililofanyika kipindi cha ndoa yao.
• Deni alilokopa mwanaume kipindi cha ndoa kwa ajili ya familia
litalipwa na wote
14
33. Haki za wanandoa kwa watoto ni zipi?
• Haki ya watoto kuishi na wazazi wote. (kifungu cha 57 cha no 13)
• Haki ya kutunzwa na wazazi wote wawili hata kama wameachana.
(kifungu cha 129 (1) cha no 13)
35. Je, maslahi ya watoto ni kama yapi?. (Kifungu cha 26 cha no 13)
• Elimu
15
• Chaguo lao la ni mzazi gani ambaye wamemchagua kuishi naye na
lifanywe na mtoto mwenye umri wa miaka 8 na kuendelea.
(Kifungu cha 125(2) cha no 13)
• Maoni ya mahakama kuwa ni mzazi yupi ambaye ana uwezo wa
kuwatunza watoto yatazingatiwa.
• Kuwatembelea wazazi wote wanapotaka kufanya hivyo.
36. Je, ni kesi zipi zingine zinazohusu ndoa ambazo mtu anaweza
kupeleka mahakamani?
• Kesi ya kuomba fidia endapo mtu amevunja ahadi ya kukuoa au
kuolewa. (kifungu cha 69 (1) cha no 29)
• Kesi za kuomba zawadi ulizozitoa kwa mtu ambaye amekataa
kukuoa au kuolewa kukiwa na ahadi kwamba mtakuja kuoana.
(Kifungu no 71 cha no 29)
• Kesi za kuomba haki ya kulipwa fidia endapo mwenza au
mchumba amekamatwa ugoni au kuna ushahidi wa kutosha wa
yeye kufanya uzinzi. (Kifungu cha 72 (1) cha no 29). Isipokuwa
endapo mlalamikaji ndiye aliyepelekea wewe kufanya hivyo, au
endapo maombi ya fidia yameambatanishwa kwenye maombi ya
taraka, hgaiana haja ya kuomba fidia.
16
Angalizo, adhabu hii haitampata mtu aliyeshiriki uzinzi na mke au
mume wa mtu, endapo mtu huyo hakujua au hana taarifa kama mtu
aliyezini naye ameoa au kuolewa.
17
40. Je, endapo bodi ya usuluhishi imesuluhisha wanandoa kitu gani
kitaendelea?
Kesi itakuwa imeishia hapo na hakutakuwa na haja ya kwenda
mahakamani tena.
18
44. Je, kila kesi ya ndoa ni lazima ipitie bodi ya usuluhishi ya ndoa?.
• Hapana, sheria imesema kuna mazingira ambayo si lazima kesi
ipitie bodi ya usuluhishi ya ndoa. Mazingira hayo ni kama
yafuatayo; (kifungu cha 101 cha 29)
• Endapo mleta maombi ana uhakika kuwa, mke au mume hajulikani
alipo
• Endapo mjibu maombi yupo nchi ya nje na hana uwezekano wa
kufika kwenye bodi kwa kipindi cha miezi sita (6)
• Endapo mjibu maombi kwa hiali yake amekataa kufika kwenye
bodi ya usuluhishi ya ndoa
• Endapo mjibu maombi amehukumiwa kifungo cha maisha au
hukumu ya miaka mitano (5) au amewekwa kizuizini kwa muda
unaozidi miezi 6
• Endapo mleta maombi amedai kuwa mjibu maombi anasumbuliwa
na ugonjwa wa akili
• Pale ambapo mahakama itagundua kuwa, kuna mazingira yasiyo
ya kawaida kwa bodi ya usuluhishi ya ndoa kuendelea kusikiliza
maombi hayo.
19
46. Bodi ya usuluhishi ya ndoa inapaswa kuwa na wajumbe
wangapi?.
Inapaswa kuwa na wajumbe Sita (6)
(kifungu cha 103 (1) cha no 29)
20
ANGALIZO, kesi za kidini zianzie kanisani au msikitini, kesi za
kuanzia kwenye bodi ni zile za ndoa za kijadi au kimila.
50. Bodi itatumia utaratibu upi wa kumuita mtu aje ajibu shitaka?
Itatumia utaratibu wa wito wa kawaida wa maandishi. (kifungu
cha 104(2) cha no 29)
21
• Mahakama kuu
• Mahakama ya hakimu mkazi
• Mahakama ya wilaya
• Mahakama ya mwanzo.
ANGALIZO, mahakama zote hapo juu zina mamlaka sawa za
kusikiliza kesi za ndoa isipokuwa mahakama ya mwanzo imepewa
mamlaka ya nyongeza ya kusikiliza kesi za ndoa zinazohusisha ndoa za
kijadi au kiislam endapo kesi ya msingi inahusiana na uzinzi.
Pia mahakama hizo zitakuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi zote za
ndoa zenye sifa zilizoanzia bodi ya usuluhishi ya ndoa.
23
56. Madhara ya kutengana ni yapi?
• Huondoa wajibu wa kutimiza majukumu yote ya kindoa
• Ni utengano tu siyo taraka
• Ni makubaliano kati ya wanandoa japo kuna mazingira ambayo
mahakama huamua hivyo
• Haiondoi uwajibikaji wa kuwatunza watoto
• Haizuii mwenza mmoja kuwaona watoto mahali walipo na mzazi
mwenzie
• Kutengana ni kwa muda wanandoa wanaweza kurudiana.
(Kifungu cha 113 (1) cha no 29)
26
62. Nini dhana ya taasisi hizi kupewa mamlaka ya kutoa taraka?
• Ili kusaidia mahakama kufikia uamuzi sahihi wa kuvunja ndoa
zilizofungwa kwenye taasisi hizo.
29
70. Je, kwa dhana ya kujifungua tu mtoto inatosha kuthibitisha
kuwa yeye ndiye mama halali wa mtoto?.
• Ikitokea kuna mabishano kuhusu mama halali wa mtoto basi mtu
yeyote au kwa amri ya mahakama, itaamuliwa kipimo cha
vinasana yaani DNA.
30
• Endapo jina la mtoto litakuwa ndio jina lililopo kwenye cheti cha
kuzaliwa cha mtoto
• Baba aliyekutana na mwanamke siku ya tarehe ya kutungwa kwa
mimba, huyo ndiye atakayekuwa Baba wa mtoto.
• Endapo wana ndoa wamefunga ndoa halali chini ya sheria hii
• Endapo Baba amesherehekea kuzaliwa kwa mtoto
• Kutangaza kwa umma kuwa wewe ndiye Baba halali wa mtoto
• Endapo vipimo vya DNA vimethibitisha kuwa, wewe ndiye Baba
halali wa mtoto. (kifungu cha 35 (a) to (e) cha no 13)
31
75. Masharti gani yamewekwa kabla ya mtu kutaka kupima
vinasaba?
• Vinasaba hupimwa kabla mtoto hajazaliwa
• Mtoto akizaliwa hakuna vipimo vya vinasaba hadi atakapofikisha
umri wa miaka 18. Japo kuna mazingira ambayo sheria au
mahakama itaruhusu kufanyika kwa vipimo vya vinasaba hasa pale
ambapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.
• Vipimo vya vinasaba hufanyika kwa amri ya mahakama
32