Professional Documents
Culture Documents
WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu ya mdomo: 255 22 2460 735/2460 706-8
Nukushi: 255 22 2460 735/700
Barua pepe: met@meteo.go.tz
Tovuti: www.meteo.go.tz
S.L.P. 3056
DAR ES SALAAM
4 Septemba, 2014
inaweza kujitokeza.
B:
Katika msimu uliopita wa mvua za Masika Machi hadi Mei, 2014. Maeneo mengi ya nchi yalipata
mvua za wastani hadi juu ya wastani isipokuwa maeneo machache ya mikoa ya Mwanza, Singida
na Dodoma ambayo yalipata mvua za chini ya wastani. Matukio ya vimbunga hususan Kimbunga
Hellen kilichotokea katika Rasi ya Msumbiji kusini magharibi mwa bahar ya Hindi kilisababisha
ongezeko la mvua katika eneo la Pwani ya kaskazini.
Maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka:
Kanda ya Ziwa Victoria: Viwango vya mvua vilivyopimwa katika vituo vya Bukoba na Musoma
vilikuwa juu ya wastani. Kituo cha Shinyanga kilipima mvua kiwango cha wastani wakati katika
kituo cha Mwanza kiwango cha mvua kilikuwa chini ya wastani.
Nyanda za juu kaskazini mashariki: Vituo vya Arusha, Lyamungo na Kilimanjaro vilipima mvua
juu ya wastani ilihali vituo vya Moshi na Same kiwango cha mvua kilikuwa cha wastani.
Pwani ya kaskazini na visiwa vya Unguja na Pemba: Vituo vya Dar es Salaam, Morogoro na
Pemba vilipima mvua za juu ya wastani na vituo vya Zanzibar, Amani, Kizimbani pamoja na Tanga
mvua zilikuwa wastani.
Maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka:
Nyanda za juu kusini magharibi: Vituo vya Mbeya, Tukuyu, na Mahenge vilipima mvua juu ya
wastani na kituo cha Sumbawanga kiwango cha mvua kilikuwa cha wastani.
Kanda ya magharibi: Mvua juu ya wastani ilipimwa katika kituo cha Kigoma ilihali vituo vya
Kibondo na Tabora mvua zilikuwa ni za wastani.
Pwani ya kusini: Kituo cha Kilwa kilipima mvua juu ya wastani na vituo vya Mtwara pamoja na
Naliendele mvua zilikuwa za wastani.
Kanda ya kati: Vituo vya Singida na Dodoma vilipima mvua chini ya wastani na kituo cha
Hombolo mvua za wastani.
Kanda ya kusini: Kituo cha Songea kiwango cha mvua kilichopimwa kilikuwa juu ya wastani.
C: MIFUMO YA HALI YA HEWA
Katika kipindi cha miezi ya Oktoba hadi Disemba, 2014 hali ya joto la bahari katika maeneo ya
magharibi na kusini -magharibi mwa bahari ya Hindi inatarajiwa kuwa juu ya wastani, upande wa
mashariki mwa bahari ya Hindi hali ya joto la wastani inatarajiwa. Hali hii inatarajiwa kusababisha
upepo wenye unyevunyevu kutoka bahari ya Hindi kuelekea katika eneo la Pwani ya Africa
Mashariki. Aidha, hali ya joto la chini ya wastani katika eneo la mashariki mwa bahari ya Atlantiki
(Pwani ya Angola) inatarajiwa kusababisha ongezeko la hewa yenye unyevunyevu kutoka katika
misitu ya Kongo kuelekea katika maeneo ya magharibi na kusini Magharibi mwa nchi.
Hali ya joto la juu ya wastani katika eneo la Tropikali ya bahari ya Pasifiki linatarajiwa kuendelea
kwa kipindi cha miezi ya Oktoba hadi Disemba, 2014. Hali hiyo inatarajiwa kuchangia ongezeko
la mvua katika baadhi ya maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua. Hali ya joto la juu ya
wastani katika eneo la kusini magharibi mwa Bahari ya Hindi linaashiria kuwepo kwa matukio ya
vimbunga katika msimu wa mvua za Vuli kuanzia mwezi Novemba, 2014.
D:
MWELEKEO WA MVUA OKTOBA - DISEMBA 2014:
Kutokana na mwelekeo wa mifumo ya hali ya hewa inayotarajiwa, mvua za kipindi cha Oktoba
2
shughuli za kilimo. Hata hivyo, kwa maeneo machache ya kusini mwa nchi (hususan Mkoa wa
Ruvuma) vipindi vya upungufu wa mvua vinatarajiwa mwanzoni mwa msimu na hivyo kuathiri
kiwango cha unyevunyevu wa udongo. Hali ya unyevunyevu wa udongo kupita kiasi
inayoambatana na vipindi vya mvua kubwa inaweza kusababisha ongezeko la magugu, matumizi
makubwa ya pembejeo, hivyo kuongeza gharama za uzalishaji. Wakulima wanashauriwa kuandaa
mashamba na pembejeo mapema pamoja na kuzingatia ushauri wa wataalam wa kilimo kwa
matumizi sahihi ya ardhi na mbegu.
Malisho na maji kwa ajili ya mifugo na wanyama pori
Hali ya malisho na upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo na wanyama pori inatarajiwa kuwa
nzuri katika maeneo mengi nchini. Hata hivyo, wafugaji wanashauriwa kuzalisha malisho na
kuyahifadhi kwa matumizi wakati wa kiangazi. Aidha, wafugaji wanashauriwa kufuata maelekezo
ya wataalam wa ugani katika maeneo yao hususan matumizi ya maji na malisho na kukabiliana na
magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza. Kutokana na hali ya mvua inayotarajiwa, matukio
ya migogoro inayosababishwa na mifugo, wanyamapori na shughuli za binadamu na kilimo
hayatarajiwi kujitokeza kwa kiasi kikubwa.
Maliasili na Utalii
Mamlaka za usimamizi wa shughuli za utalii na hifadhi za wanyamapori zina shauriwa kuchukua
hatua stahiki katika kuzuia uharibifu wa miundombinu kama barabara na madaraja ndani ya
hifadhi dhidi ya adhari za mvua kubwa na za juu ya wastani katika maeneo husika. Aidha,
wawindaji, wapiga picha za kitalii na makampuni ya kitalii yanashauriwa kuchukua tahadhari ya
uwepo wa mafuriko kutokana na mvua zinazotarajiwa.
Maji na Nishati
Mtiririko wa maji katika mito na vina vya maji katika mabwawa vinatarajiwa kuongezeka katika
maeneo mengi ya nchi kutokana na mvua za msimu wa Vuli. Pamoja na matarajio ya kuwepo kwa
mvua za juu ya wastani inashauriwa kuwa maji yatumike kwa uangalifu na kuzingatia taratibu za
uvunaji, uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali maji.
Mamlaka za Miji
Inashauriwa kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa mifumo na njia za kupitisha maji
zinafanyakazi katika kiwango cha kutosha kuhimili mvua zinazotarajiwa ili kuepusha maji
kutuama na kusababisha mafuriko na uharibifu wa miundombinu, upotevu wa maisha na mali
katika maeneo husika.
Sekta ya Afya
Ushauri unatolewa kwa jamii na sekta husika kuchukua hatua stahiki katika kuzuia milipuko ya
magonjwa yanayosababishwa na kutuama kwa maji na utiririshaji wa maji taka usiodhibitiwa
katika maeneo yao.
Menejimenti ya Maafa
Mamlaka za maafa na wadau wengine wanashauriwa kuchukua hatua stahiki katika utunzaji wa
mazingira, upatikanaji wa maji safi na salama, na usambazaji wa madawa, maji na chakula ikiwa ni
hatua za kujiandaa na kukabiliana na majanga yanayoweza kutokea kutokana na vipindi vya mvua
kubwa na mvua za juu ya wastani zinazotarajiwa.
Vyombo vya habari
Vyombo vya habari vinashauriwa kufuatilia, kupata na kusambaza taarifa sahihi za mienendo ya
hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kutumia wataalam wa sekta
husika katika kuandaa na kufikisha taarifa za masuala mtambuka ya hali ya hewa kwa jamii. Aidha,
5
jamii nayo inashauriwa kufuatilia na kuzingatia taarifa sahihi za hali ya hewa na mirejeo yake
kupitia vyombo vya habari.
Angalizo: Mwelekeo wa mvua uliotolewa hapa umezingatia zaidi kipindi cha msimu (miezi
mitatu) na hali ya mvua katika maeneo makubwa. Hivyo, viashiria vinavyochangia mwenendo
wa mifumo ya mvua na mabadiliko ya muda mfupi katika maeneo madogo utazingatiwa katika
uchambuzi wa utabiri wa muda wa kati na mfupi. Watumiaji wa taarifa za utabiri huu
wanashauriwa pia kufuatilia tabiri za saa 24, siku 10 pamoja na wa mwezi kama zinavyotolewa
na Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Itaendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya hali ya
hewa na kutoa taarifa za mwelekeo wa mvua nchini.