You are on page 1of 3

Na Emmanuel Ghula

MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA),


imezindua klabu ya wanafunzi ijulikanayo kama Sumatra Club
itakayotoa mafunzo na mbinu zitakazowawezesha wananfunzi kutambua
haki zao katika huduma ya usafiri.
Klabu hiyo itaongozwa na kauli mbiu isemayo, Mtetezi wa haki, maslahi
na wajibu wa abiria.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa klabu hiyo uliofanyika kwenye
viwanja vya sabasaba, mwenyekiti wa Baraza la watumiaji wa barabara
na aliyekuwa mgeni rasmi kwaniaba ya mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam,
Ayoub Omar amesema kuanzishwa kwa vilabu vya Sumatra mashuleni
kutasaidia kutoa elimu kwa wanafunzi ili wajue haki zao katika huduma
ya usafiri.
Sumatra imeamua kuanzisha vilabu hivi mashuleni ikiwa na lengo la
kutoa elimu kwa wanafunzi watambue haki zao katika huduma ya usafiri
na wajue namna ya kutatua matatizo wanayokumbana nayo katika
vyombo vya usafiri, alisema Omar.
Aliongeza kuwa, Kwa muda mrefu wanafunzi wamekuwa wakipata tabu
kwenye vyombo vya usafiri na kunyanyaswa na madereva na makondakta
wasio waadilifu. Lakini kupitia vilabu hivi watapatiwa mafunzo
yatakayowapatia mbinu ya kupambana na changamoto hizo kisheria.
Alisema hadi sasa wameshazindua vilabu vya Sumatra katika mikoa nane
na mkoa wa Dar Es Salaam ni mkoa wa tisa ambayo tayari wanafunzi
wake wataanza kupata mafunzo hayo ya haki ya mtumiaji wa vyombo vya
usafiri nchi kavu na majini.

Wanafunzi wamekuwa wanungunikaji kwa muda mrefu lakini sasa


tunataka wawe walalamikaji kwa kufuata sheria na haki walizonazo
katika huduma za usafiri. Tunaimani kuwa vilabu hivi vitakuwa suluhisho
la wanafunzi kupata tabu na kunyimwa haki zao katika vyombo vya
usafiri, alisema Omari.
Kamanda wa polisi kikosi cha usalama barabarani Taifa, Johansen
Kahatamo amesema jeshi la polisi kwa kushirikiana na Sumatra pamoja
na wanafunzi wenyewe wataweza kumaliza changamoto ya usafiri kwa
wanafunzi kama vilabu hivi vitasimamiwa vizuri.
Tatizo la usafiri kwa wanafunzi litapungua na kuisha iwapo tutasimamia
vyema vilabu vyetu. Niwaombe wanafunzi wawe waadilifu na watiifu wa
sheria, msiwe chanzo cha vurugu kwenye vyombo vya usafiri. Kuweni
watatuzi wa matatizo, alisema Kahatamo.
Aliahidi kuwa jeshi la polisi litamshughulikia mtu yeyote atakayevunja
sheria au kuwanyanyasa wanafunzi. Mtu atakayevunja sheria lazima
tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria. Kama wanafunzi mtakumbana na
matatizo chukueni namba za magari husika na kuripoti kwa polisi kupitia
kwa wazazi wenu. Wazazi wapige namba ya polisi 0682 887722 na jeshi
la polisi litachukua hatua za kisheria kufuatilia gari husika, alisema
kahatamo.
Uanzishwaji wa vilabu hivi imeelezwa kuwa ni moja ya mbinu iliyobuniwa
na baraza la watumiaji wa barabara ili kukabiliana na changamoto ya
usafiri kwa wanafunzi. Kila mkoa utakuwa na vilabu vyake vya Sumatra
kwa utaratibu utakaowekwa na mikoa husika.

Kwa upande wao wanafunzi wameeleza kuridhishwa na uanzishwajki wa


vilabu mashuleni na kusema vitasaidia wao kuthaminiwa katika vyombo
vya usafiri kama abiria wengine.
Mathias Kondrad mwanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya
sekondari Kibasila amesema, Nimefurahi sana kuanzishwa kwa vilabu
hivi, tunaimani nasi sasa tutathaminiwa kama abiria wengine. Tumekuwa
tukichelewa shule kwa kukataliwa na hata kupigwa na makondakta ili
tusipande magari yao. Lakini sasa hivi tutatumia sheria kudai haki yetu
ya msingi kama abiria, alisema Kondrad.
Mwisho.

You might also like