Professional Documents
Culture Documents
Maelezo Binafsi Ya Mhe. Zitto Zubeir Kabwe
Maelezo Binafsi Ya Mhe. Zitto Zubeir Kabwe
Maelezo Binafsi Ya Mhe. Zitto Zubeir Kabwe
1)
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa fursa
uliyonipa kutoa maelezo yangu binafsi katika Bunge lako
Tukufu leo. Ninatoa maelezo haya kwa mujibu wa Kifungu
cha 50 (1) cha Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili,
2013 kinachosema kwamba,Mbunge yeyote anaweza, kwa
idhini ya Spika, kutoa maelezo binafsi Bungeni yanayolenga
kufafanua kuhusu jambo lolote linalomhusu na lililoifikia
jamii
2)
Mheshimiwa Spika, Nilijiunga na Bunge lako Tukufu kwa
mara ya kwanza Mwaka 2015 nikiwa na lengo kuu la kupaza
sauti ya vijana kwenye masuala yanayohusu nchi yetu na
kutetea maslahi ya Watanzania hususani Wananchi wa Jimbo
la Kigoma Kaskazini na Mkoa wa Kigoma, na Watanzania kwa
ujumla. Nilichaguliwa na wananchi wa Kigoma Kaskazini kwa
tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Wananchi wa Kigoma Kaskazini walinichagua tena Mwaka
2010 kupitia tiketi ya CHADEMA.
3)
Mheshimiwa Spika, kupitia fursa ya ubunge niliyopewa
na wananchi wa Kigoma Kaskazini kwa udhamini wa
CHADEMA, nimejifunza mengi hapa Bungeni na nje ya Bunge
hili. Nimeijua nchi yangu, nimejua siasa na nimejulikana
ndani na nje ya Tanzania. Muhimu zaidi ni kwamba nimepata
fursa adhimu ya kutoa mchango wangu katika kutunga
sheria na sera mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi