Professional Documents
Culture Documents
1
zinatumika kudhibiti na kukagua uingizaji wa mifugo na mazao yake
katika maeneo ya mpakani, bandarini na viwanja vya ndege;
(ii) Sheria ya Nyanda za Malisho na Rasilimali ya Vyakula vya Wanyama
(Grazing-land and Animal Feed Resources Act) Na. 13 ya mwaka 2010
ambayo inasimamia nyanda za malisho na ubora wa malighafi za
kusindika vyakula vya mifugo;
(iii) Zuio (quarantine) la uingizaji ndege na mazao yake nchini la mwaka
2006, kutokana na uwepo wa ugonjwa hatari wa Homa ya Mafua
Makali ya Ndege katika nchi mbalimbali duniani. Ugonjwa huo
umejitokeza kwenye nchi jirani ya Uganda mwanzoni mwa mwaka
2017 na hivyo kuiweka nchi yetu katika hatari ya kuambukizwa
ugonjwa huu iwapo zuio hili litakiukwa. Zuio hilo halijaondolewa hadi
leo.
(iv) Ukweli kwamba katika Jumuiya ya Afrika Mashariki mifugo na bidhaa
za mifugo zinavuka mipaka kwa utaratibu maalum kupitia kwenye vituo
vya mipakani ambapo maofisa mifugo kutoka pande zote za mipaka
hufanya shughuli ya udhibiti.
Utekelezaji wa sheria na makubaliano haya hufanyika bila ubaguzi wa uraia
wa mwingizaji wa mifugo au nchi inakotoka mifugo hiyo. Nchi zote duniani,
zikiwemo nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, zinadhibiti
uingizwaji wa mifugo na mimea katika nchi zao. Udhibiti huu hufanyika
katika viwanja vya ndege, bandari na vituo vya mipakani. Kwa mfano, katika
Kituo cha Huduma za Pamoja Mpakani cha Namanga, wapo maofisa wa
mifugo na kilimo kutoka Kenya na Tanzania wanaodhibiti uingizwaji wa
mifugo na mimea kwenye nchi zao.
2
Hata hivyo, wapo wamiliki wachache kutoka nchi za jirani waliokaidi agizo
hilo na hivyo ngombe wapatao 1113 walikamatwa katika Wilaya ya
Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro na kupigwa mnada baada ya wamiliki wake
kushindwa kujitokeza. Katika mkoa huo wa Kilimanjaro wapo ngombe 74
ambao wamiliki wake walijitokeza, wakalipa faini kwa amri ya mahakama na
kuondoka na ngombe wao. Katika Mkoa wa Kigoma ngombe 324 ambao
wamiliki wake hawajajitokeza wamekamatwa na hatua stahiki
zinachukuliwa. Aidha, katika mkoa huo wa Kigoma ngombe 728
walikamatwa na wamiliki wao walijitokeza na kulipa faini kutokana na
maamuzi ya Mahakama. Katika mkoa wa Kagera jumla ngombe 1,536
ambao wamiliki wake bado hawajulikani wanashikiliwa na vyombo vya ulinzi
na usalama na sheria itachukua mkondo wake.
Kwa takwimu hizi ni wazi kwamba zoezi hili halijalenga nchi yeyote, kwa
sababu sio nchi moja tu imeathirika. Zoezi hili limelenga kutekeleza sheria
na kanuni za nchi yetu ili kulinda mazingira na kupunguza uwezekano wa
kusambaa kwa magonjwa ya mifugo. Hili suala halipaswi kusababisha
mgogoro wa kidiplomasia na nchi yeyote, labda tu mtu aamue kwa
makusudi yasiyo mema kupotosha na kuchochea mgogoro.
Aidha, tarehe 24 Oktoba, 2017 jumla ya vifaranga vya kuku wa mayai 6,400
vilikamatwa katika Mkoa wa Arusha kwa kuingizwa nchini bila kufuata sheria
na kanuni. Vifaranga hivyo vilikuwa kwenye maboksi 60 vikiwa kwenye gari
lenye namba za usajili T 285 BAY. Mmiliki wa vifaranga hivi alidai kwamba
ameviingiza nchini kutokea Kenya. Vifaranga hivi viliteketezwa kutokana na
msafirishaji wa vifaranga hivi kutokuwa na kibali cha aina yoyote kutoka
mamlaka husika ya udhibiti wa magonjwa ya mifugo hapa nchini ambayo ni
Idara ya Huduma za Afya Mifugo katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Pia,
mmiliki huyu alishindwa hata kuonesha kibali cha Serikali ya Kenya
kumruhusu kusafirisha vifaranga hivyo kutoka Kenya kuvileta Tanzania
pamoja na kwamba mmiliki huyu alidai kwamba vifaranga hivyo amevitoa
Kenya. Ni muhimu ikafahamika kwamba nchi zote duniani, ikiwemo
Kenya, hufuata miongozo ya WTO na Shirika la Afya ya Wanyama
Duniani (OIE) kwa kutoa vibali (export permit) kwa mtu yeyote
anayetaka kusafirisha mifugo nje ya nchi. Kosa jingine kubwa ni kwamba
vifaranga hivi havikupitishiwa kwenye vituo rasmi vya Ukaguzi wa Mifugo na
Mazao yake mipakani (zoosanitary border posts) kwa mujibu wa sheria na
kanuni husika.
3
Pamoja na yote haya, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Tanzania alimpigia
simu Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (Director of Veterinary Services) wa
Kenya kutaka kujua kama Mamlaka za Kenya zina habari kuhusu vifaranga
waliokamatwa na kama Kenya itakubali kuruhusu vifaranga hivyo
virudishwe Kenya. Mkurugenzi huyu wa Kenya alisema hana taarifa
kuhusu vifaranga hivyo na kwamba Kenya haiko tayari kuruhusu
vifaranga hivyo kurudishwa nchini mwao kwa sababu havina nyaraka
kulingana na miongozo ya kimataifa.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
19 Novemba, 2017