Professional Documents
Culture Documents
JUNI, 2015
Mratibu
1. Seleman Pingoni
2. Kaleb Gamaya (CEO-TLS)
3. TEPHEN mSECHU (PO-RPA
4. Selemani Pingoni (M & E Officer)
Mirathi Ni nini?
Wosia Ni Nini?
Faida za wosia
Sheria ya Mila
Mwaka 1963, serikali ilitoa tamko la kuzitambua sheria za mila
za urithi na wosia kupitia Tangazo Rasmi la Serikali Namba
Daraja la Kwanza
Cheo hiki hushikwa na warithi wafuatao;
• Mtoto wa kiume wa kwanza kutoka katika nyumba ya
kwanza (kama ilikua ndoa ya wake wengi), au;
• Mtoto wa kiume aliyezaliwa kwanza kutoka nyumba
yoyote, iwapo marehemu hakuacha mtoto wa kiume katika
nyumba ya kwanza.
Daraja la pili
Cheo hiki hushikwa na watoto wote wa kiume waliosalia ambao
hurithi sehemu kubwa kuliko watoto wa kike ambao huhesabika
kama daraja la tatu.
Daraja la Tatu
Cheo hiki ndio cha mwisho na kinajumuisha watoto wa kike wote
bila kujali tofauti ya umri na nafasi ya mama zao katika ndoa.
Hawa hupata sehemu ndogo kuliko watoto wa kiume. Kama
watoto wa kiume hawapo basi watoto wa kike huongezewa
urithi.
Nafasi ya mjane
Utaona kuwa katika sheria ya kimila ambayo iko katika Tangazo
la Serikali Namba 436 la Mwaka 1963, wajane hawaruhusiwi
kurithi mali za marehemu waume zao. Sheria hiyo inasema kuwa
mjane mwenye watoto inabidi aishi kwa kutegemea watoto
wake. Mjane ambaye hana watoto atabaki katika nyumba ya
marehemu na kupewa asilimia 20 ya nusu ya mali ya marehemu
na kuitumia wakati wa uhai wake. Akifariki au akiolewa na mtu
mwingine nje ya ukoo mali hiyo na nyumba aliyokuwa anakaa
hugawiwa kwa warithi halali wa marehemu mume wake. Sheria
hii pia inasema, mume hawezi kurithi mali ya mke wake katika
urithi usio na wosia, isipokuwa pale tu ambapo mke hakuacha
watoto na hakuacha kabisa mtu yoyote katika ukoo wake.
Sheria hii kwa sasa inakosa uhalali wa Kikatiba kwa kuwa haki
za binadamu zinataka usawa bila ya ubaguzi.
Sheria ya Kiislamu
Sheria ya Kiislamu ya Mirathi ni kama ilivyoanishwa katika
vifungu mabalimbali vya Kuruani Tukufu na kufafanuliwa
katika Makala mbalimbali za wanazuoni wa Kiislamu. Hapa
Tanzania Bara, Sheria ya Kiislamu ya mirathi imeanishwa katika
Tamko la Sheria za Kiislamu la mwaka 1967 (The Statements of
Islamic Law, GN 222 of 1967). Tamko hili pamoja na kwamba
halijawahi kutumika rasmi, ni mwongozo mzuri wa hizo sheria.
Kama mirathi yeyote ile, mgawanyo wa mali ya marehemu kwa
mujibu wa Sheria ya Kiislamu, huzingatia mambo muhimu
matatu yafuatayo,
Kwamba:
i. Mwenye mali awe alishakufa (maut al–muwarith)
ii. Pawepo na warithi halali wa marehemu (hayat al-warith),
yaani watoto wa marehemu ndugu wengine wa marehemu.
Warithi hawa ni lazima wawepo na wawe ni warithi hakika
wanaotambulika kisheria wakati wa mauti ya marehemu
iii. Marehemu ameacha mali (al- tarikah I al–mauruth)
iv. Urithi utokane na mali halisi na halali za marehemu na sio
nje ya hizo.
Maana ya Wosia
Wosia ni kauli inayotolewa na mtu wakati wa uhai wake kwa
hiari yake kuonyesha nia yake jinsi gani angependa mali yake
igawanywe baada ya kufa kwake.
Wosia wa Mdomo
Wosia wa mdomo lazima;
• Ushuhudiwe na mashahidi wanne (wawili wa ukoo na
wawili watu baki);
• Muusia awe na akili timamu;
• Kama mashahidi watakufa kabla ya muusia kufa, basi wosia
hautakubalika na urithi utagawanywa kadri ya mpango wa
urithi usio wa wosia. Mwenyewe kama anataka kuusia mali
zake, atoe wosia mpya;
• Mashahidi wawe wamechaguliwa na muusia mwenyewe.
Kubatilishwa Wosia
Wosia waweza kubatilishwa ikiwa itathibitika kwamba muusia
amepungukiwa akili kwa sababu ya wazimu, ugonjwa, ulevi au
hasira ya gafla. Ni muhimu kukumbuka kwamba ni wahusika tu
Faida za wosia
Wosia una faida zifuatazo;
a. Mwosia anapata fursa ya kufanya mgawo wa mali yake
kwa kadri anavyotaka kabla ya kufariki.
b. Mwosia anapata fursa ya kuamua ni nani awe msimamizi
wa mirathi yake.
c. Wosia huepusha ugomvi wa wanafamilia na kuimarisha
amani miongoni mwa warithi na wanandugu halali.
d. Wosia ni chombo cha kuhakikisha kwamba urithi
unakwenda kwa watu ambao marehemu aliwaridhia.
2. Namchagua ……......……………………………………………..
wa S.L.P. …………………………………………………............
Simu………………………………………………………………
ambaye anaishi ………………….kuwa msimamizi wa
mirathi yangu.
a) ………………………………………......………………....…
S.L.P………………………………………………………….
Simu …………………………………………………………
Shahidi wa Kwanza
Jina: ……………………………………………………………………
Saini: ………………………………………………………….….……
Anuani: ……………………………………………………………….
Kazi: ……………………………………………………….…………
Shahidi wa Pili
Jina: ……………………………………………………….…….….….
Saini: ……………………………………………………………….….
Anuani: …………………………………………………………….…
Kazi: ……………………………………………………………….…..
Mbele ya …………………………………………………..…..........…
Mshuhudi viapo/Saini : ………………………………………………