Professional Documents
Culture Documents
Bashiru Ally
Saida Yahya-Othman
Issa Shivji
NYERE
RE
DA CHA T
A
GO
KI
U
IM
AL
A CHA M
W
UM
AL
NYERE
RE
DA CHA T
A
GO
KI
U
IM
AL
A CHA M
W
UM
AL
ISBN 978-9987-9418-2-7
YALIYOMO
Dibaji
11
Sura ya Kwanza
Azimio la Arusha la 1967
23
Sura ya Tatu
Mwongozo wa CCM wa 1981
55
Sura ya Pili
Mwongozo wa TANU wa 1971
43
Sura ya Nne
Maamuzi ya Zanzibar ya 1991
116
Sura ya Tano
Miongozo Miwili ya Chama na tabaka lililopindua Ujamaa
Issa Shivji
MIONGOZO MIWILI
132
DIBAJI
Kitabu hiki kimeandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere
kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya matukio muhimu katika historia
ya nchi yetu tangu Uhuru. Kuna nyaraka nne katika kitabu hiki: Azimio
la Arusha la 1967, Mwongozo wa 1971, Mwongozo wa 1981 na Maamuzi
ya Zanzibar ya 1991, ambayo ni hotuba ya Mzee Ali Hassan Mwinyi. Kwa
nini tumechagua nyaraka hizo na sio nyengine? Kwa sababu kila nyaraka
ina muhula wa kihistoria wa kuhadithia. Muongo mmoja kati ya 1971
na 1981 ni kipindi cha uzalendo wa hali ya juu, uzalendo wa mrengo wa
kushoto, uliozaliwa na itikadi ya Umajumui wa Afrika (Pan-Africanism).
Kipindi hiki kilipewa jina rasmi la kipindi cha Ujamaa na Kujitegemea.
Mwongozo wa 1981 ni waraka wa kipekee ambayo inafanya uchambuzi
wa miaka 14 ya Azimio kwa mtazamo wa kitabaka, ambao, lazima tukiri,
haukuwa mtazamo wa Chama wala Mwalimu.
Muongo wa 1981 mpaka 1991 ni kipindi cha mpito kutoka muhula
wa kizalendo na kuingia muhula wa uliberali mambo-leo. Maamuzi ya
Zanzibar ya 1991 (kwa msamiati wa kisiasa huitwa Azimio la Zanzibar),
ni hotuba ya Rais wa Awamu ya Pili, inayoelezea na kuhalalisha mtazamo,
mwelekeo, itikadi na sera za uliberali mambo-leo.
Baada ya kuchagua nyaraka hizi, tukamuomba Mzee Kingunge Ngombale
Mwiru, kutuandikia Utangulizi wa Miongozo Miwili. Mzee Ngombale
anajulikana kwa sifa yake ambayo anaistahili - ya kuzungumzia itikadi
na nadharia ya Chama kwa ufasaha, na kwa undani; ni kingunge hasa
wa itikadi ya Chama. Yeye amekuwa mwanaitikadi (ideologue) wa Chama
kwa miongo kama minne hivi. Umahiri wake wa kiitikadi unadhihirishwa
vema na ukweli usiopingika kwamba amekuwa msemaji mkuu wa itikadi
ya Chama katika awamu zote za utawala wa kisiasa nchini kuanzia
awamu ya Mwalimu, ambayo ilikuwa awamu ya kizalendo; kupitia awamu
ya Mzee Ali Hassan Mwinyi ambayo ilikuwa awamu ya mpito kuelekea
kwenye uliberali mambo-leo; ikifuatiwa na awamu ya Mheshemiwa
Benjamin William Mkapa, ambayo ilikuwa awamu ya kuiimarisha bila
vikwazo misingi mikuu ya uliberali mambo-leo, au kwa msamiati wake
4
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
Mwongozo wa 1971
Mwongozo wa 1981
MIONGOZO MIWILI
Hitimisho
Shukrani
MIONGOZO MIWILI
UTANGULIZI
UJIO NA UZITO WA
MIONGOZO MIWILI
Kingunge Ngombale Mwiru
Ujio wa Mwongozo
Kitendo hiki cha uhasama kutoka kwa nchi jirani kilihitaji kupatiwa
jibu la haraka na la kimkakati. Ndipo nilipoitwa Ofisini kwa Makamu
MIONGOZO MIWILI
11
MIONGOZO MIWILI
13
Mwongozo wa 1981
Ujio wa Mwongozo
MIONGOZO MIWILI
15
MIONGOZO MIWILI
17
MIONGOZO MIWILI
Mapokezi na utekelezaji
19
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
21
22
MIONGOZO MIWILI
SURA YA KWANZA
AZIMIO LA ARUSHA
Ujamaa na Kujitegemea
(Lilipitishwa na Halmashauri Kuu ya TANU, mwezi Januari 1967, na
kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa TANU)
(Lilitolewa rasmi tarehe 5 Februari 1967)
SEHEMU YA KWANZA
IMANI YA TANU
Siasa ya TANU ni kujenga nchi ya Ujamaa. Misingi ya Ujamaa imetajwa
katika Katiba ya TANU, nayo ni hii:
Kwa kuwa TANU inaamini:
MIONGOZO MIWILI
23
MADHUMUNI YA TANU
MIONGOZO MIWILI
SEHEMU YA PILI
SIASA YA UJAMAA
(a) Hakuna Unyonyaji
Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi: haina ubepari wala
ukabaila. Haina tabaka mbili za watu: tabaka ya chini ya watu wanaoishi
kwa kufanya kazi, na tabaka ya juu ya watu wanaoishi kwa kufanyiwa
kazi. Katika nchi ya Ujamaa kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye
kufanya kazi hufanya kazi, na kila mfanyakazi hupata pato la haki kwa
kazi aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbalimbali hayapitani
mno.
Katika nchi ya Ujamaa kamili watu peke yao ambao huishi kwa jasho
la wenzao, na ni haki yao kuishi kwa jasho la wenzao, ni watoto
wadogo, wazee wasiojiweza, vilema na wale ambao, kwa muda, Jumuia
imeshindwa kuwapatia kazi yoyote ya kujipatia riziki kwa nguvu zao
wenyewe.
Njia kuu za Uchumi ni: kama vile ardhi, misitu, madini, maji, mafuta na
nguvu za umeme; njia za habari, njia za usafirishaji; mabenki, na bima;
biashara na nchi za kigeni na biashara za jumla; viwanda vya chuma,
mashini, silaha, magari, simenti, mbolea; nguo, na kiwanda chochote
kikubwa ambacho kinategemewa na sehemu kubwa ya watu katika
kupata riziki zao au kinachotegemewa na viwanda vingine; mashamba
MIONGOZO MIWILI
25
Nchi haiwi ya Ujamaa kwa sababu tu njia zake kuu au zote za uchumi
hutawaliwa na humilikiwa na Serikali. Sharti Serikali iwe inachaguliwa na
kuongozwa na Wakulima na Wafanyakazi wenyewe. Serikali ya Makaburu
wa Rhodesia au Afrika ya Kusini ikitawala au kumiliki njia zote za uchumi,
hiyo itakuwa ni njia ya kukomaza Udhalimu siyo njia ya kuleta Ujamaa.
Hakuna Ujamaa wa kweli pasipo na Demokrasi ya kweli.
SEHEMU YA TATU
SIASA YA KUJITEGEMEA
Tunapigana Vita
TANU ina vita vya kulitoa Taifa letu katika hali ya unyonge na kulitia
katika hali ya nguvu; vita vya kuwafanya wananchi wa Tanzania (na
26
MIONGOZO MIWILI
27
Mwaka hata mwaka kila Wizara na kila Waziri hufanya makadirio yake ya
matumizi yaani fedha wanazohitaji mwaka huo kwa kazi za kawaida na
mipango ya maendeleo. Waziri mmoja tu na Wizara moja tu hushughulika
pia kufanya makadirio ya mapato. Ni Waziri wa Fedha. Kila Wizara ina
mipango mizuri sana ya maendeleo. Wizara zinapoleta makadirio yao ya
matumizi huwa zinaamini kwamba fedha zipo ila mkorofi ni Waziri wa
Fedha na Wizara yake. Na kila mwaka lazima Waziri wa Fedha na Wizara
yake awaambie Mawaziri wenzake na Wizara zao kwamba hakuna
fedha. Na kila mwaka Wizara zote huinungunikia Wizara ya Fedha kwa
kupunguza Makadirio yao ya matumizi.
MIONGOZO MIWILI
Na kusema kuwa Serikali haina fedha maana yake ni nini? Maana yake ni
kuwa Wananchi wa Tanzania hawana fedha. Kiasi walichonacho hutozwa
kodi, na kodi hiyo ndiyo inayoendesha shughuli za Serikali hivi sasa na
maendeleo mengine ya nchi. Tunapotaka Serikali ifanye shughuli zaidi
za maendeleo kwa fedha tunataka Serikali itumie fedha zaidi. Na kama
Serikali haina fedha zaidi tunataka izipate, yaani iongeze kodi.
Ukidai Serikali itumie fedha zaidi unataka izipate; na njia ya kuzipata
ni kodi. Kudai Serikali itumie fedha nyingi zaidi bila kukubali kodi zaidi
ni kudai Serikali ifanye miujiza; ni sawa na kudai maziwa zaidi bila
kutaka ngombe akamuliwe tena. Lakini kukataa huku kukiri kwamba
tunapodai Serikali itumie fedha zaidi nia yetu ni kutaka Serikali
iongeze kodi kunaonyesha kuwa tunatambua ugumu wa kuongeza kodi.
Tunatambua kuwa ngombe hana maziwa zaidi; kwamba hata kama
ngombe mwenyewe angependa ayanywe maziwa hayo au yanywewe na
ndama wake au yauzwe yamfae yeye na jamaa yake; utashi huo hauwezi
kuondoa ukweli kwamba hana maziwa zaidi.
29
Hizo ndizo njia tatu kubwa za kupata fedha kutoka nje ya nchi yetu. Kuna
mazungumzo mengi ajabu juu ya jambo hili la kupata fedha kutoka nchi za
kigeni. Serikali yetu na viongozi wetu wa makundi mbalimbali hawaachi
kufikiria njia za kupata fedha kutoka nje. Na tukizipata au japo tukipata
ahadi tu ya kuzipata mara magazeti yetu, au radio zetu na viongozi
wetu hutangaza jambo hilo ili kila mtu ajue kuwa neema imekuja au iko
njiani inakuja! Tukipata msaada hutangaza; tukipata mkopo hutangaza;
tukipata kiwanda kipya hutangaza; tukiahidiwa msaada, mkopo au
kiwanda kipya hutangaza. Japo tukianza mazungumzo tu na nchi au
shirika la kigeni juu ya msaada, mkopo au kiwanda, mara hutangaza japo
hatuna hakika ya matokeo ya mazungumzo hayo. Na kisa? Ni kuwajulisha
wananchi kwamba, tunaanza mazungumzo ya neema!
Ni jambo la kijinga kuchagua fedha kuwa ndiyo chombo chetu kikubwa cha
maendeleo na hali tunajua kuwa nchi yetu ni maskini. Ni ujinga vilevile,
kwa kweli ni ujinga zaidi, tukidhani kuwa tunaweza kuondoa hali hii ya
unyonge wetu kwa kutegemea fedha za kutoka nje badala ya fedha zetu
wenyewe. Ni ujinga kwa sababu mbili.
yetu kwa kiasi cha kuiwezesha nchi yetu kutimiza shabaha zake zote za
maendeleo. Nchi zenye dhiki ni nyingi sana duniani. Na hata kama nchi
zote zenye neema zingekubali kuzisaidia nchi zenye dhiki, bado ingekuwa
msaada huo hautoshi. Lakini nchi zenye neema hazitakubali. Hata katika
30
MIONGOZO MIWILI
nchi ileile, matajiri huwa hawatoi fedha zao kwa hiari ili zisaidie Serikali
kuondoa dhiki.
31
Na Viwanda vya wenye raslimali zao je? Ni kweli tunavitaka. Hata tumepitisha
katika Bunge sheria ya kulinda raslimali ya wageni wanaoanzisha mipango
mbalimbali ya uchumi katika nchi yetu. Nia yetu na matumaini yetu ni
kuwafanya waone kuwa Tanzania ni nchi inayofaa kuingiza raslimali zao.
Kwani raslimali yao itakuwa salama italeta faida. Na faida hiyo wenyewe
wataweza kuiondoa bila vipingamizi. Tunayo matumaini ya kupata
fedha za maendeleo mbalimbali kwa njia hii. Lakini hatuwezi kupata za
kutosha. Lakini hata kama tungeweza kuwaridhisha kabisa Wageni hao
na Makampuni hayo mpaka yakubali kuanzisha mipango yote ya uchumi
tunayohitaji katika nchi yetu, hivyo ndivyo tunavyotaka kweli?
Kama tungeweza kushawishi wenye raslimali wa kutosha kutoka Amerika,
na Ulaya kuja kwetu na kuanzisha Viwanda vyote, na mipango mingine
yote ya uchumi tunayohitaji katika nchi hii, hivi kweli tungekubali bila
kujiuliza maswali? Tungekubali kweli kuacha uchumi wetu wote uwe
mikononi mwa wageni kwa ajili ya kupata faida na kuipeleka katika nchi
zao? Hata kama wasingedai kuhamisha faida na kupeleka makwao, bali
faida yote watakayopata wataitumia hapa hapa Tanzania kwa maendeleo
zaidi. Hivi kweli tungekubali jambo hili bila kujiuliza hasara zake kwa Taifa
letu? Huu Ujamaa tunaosema kuwa ndiyo shabaha yetu tungeujengaje?
MIONGOZO MIWILI
makosa kudhani kuwa tutapata fedha kutoka nchi za kigeni. Kwanza, kwa
sababu kwa kweli hatuwezi kupata fedha za kutosha kwa maendeleo yetu.
Na pili, hata kama tungeweza, huko kutegemea wengine kungehatarisha
uhuru wetu na siasa nyingine za nchi yetu.
MIONGOZO MIWILI
33
MIONGOZO MIWILI
WANANCHI NA KILIMO
Maendeleo ya nchi huletwa na watu, hayaletwi na fedha. Fedha ni
matokeo siyo msingi wa maendeleo. Ili tuendelee twahitaji vitu vinne: (i)
Watu; (ii) Ardhi; (iii) Siasa safi na (iv) Uongozi bora. Nchi yetu ina zaidi
ya watu milioni kumi1* na eneo la eka 362,000.
MIONGOZO MIWILI
35
Pia nchi yetu ni nzuri sana kwa ufugaji wa ngombe, mbuzi, kondoo,
kuku n.k. Pia twaweza kuvua samaki katika maziwa, bahari
na mito.
Wakulima wetu wako katika sehemu ambazo zaweza kutoa mazao haya,
kama si yote walau mawili matatu au hata zaidi. Kila mkulima wetu
aweza akaongeza mazao haya ili ajipatie chakula kingi zaidi au fedha
nyingi zaidi. Na kwa sababu nia kubwa ya maendeleo ni kupata chakula
zaidi na fedha zaidi kwa ajili ya kujipatia mahitaji yetu mengine, ndiyo
kusema kuwa jitihada ya kuongeza mazao ni jitihada, na kwa kweli ndiyo
jitihada peke yake, ambayo italeta maendeleo, yaani chakula zaidi na
fedha zaidi kwa kila mwananchi.
MASHARTI YA MAENDELEO
(a) Juhudi
Kila mwananchi anataka maendeleo, lakini si kila mwananchi anaelewa
na kukubali masharti ya maendeleo. Sharti moja kubwa ni JUHUDI.
Twendeni vijijini tuzungumze na wananchi kuona kama inawezekana au
haiwezekani wananchi kuongeza juhudi.
Kwa mfano, katika miji, mfanyakazi wa mshahara hufanya kazi kwa saa
saba na nusu au nane kutwa kwa muda wa siku sita au sita na nusu kwa
juma. Tuseme saa 45 kwa juma, kuondoa majuma mawili au matatu ya
livu, katika mwaka mzima. Ndiyo kusema mfanyakazi wa mjini hufanya
kazi ya saa 45 kwa juma kwa majuma 48 au 50 kwa mwaka.
Katika nchi kama yetu muda huu ni mdogo kwa kweli. Nchi nyingi hata
zilizoendelea kutuzidi hufanya kazi kwa muda mrefu zaidi kuliko saa 45
kwa juma. Si jambo la kawaida nchi changa kuanza na muda mfupi kama
huo. Jambo la kawaida ni kuanza na muda mrefu zaidi na kuupunguza
kila nchi inavyozidi kuendelea. Sisi kwa kuanza na muda mfupi huu na
tunapodai muda mfupi zaidi kwa kweli tunaiga nchi zilizoendelea. Na
kuiga huku kunaweza kukaleta majuto. Lakini hata hivyo wafanyakazi wa
mishahara hufanya kazi ya saa 45 kwa juma; livu yao kwa mwaka haizidi
majuma manne.
36
MIONGOZO MIWILI
37
MIONGOZO MIWILI
(a) Ardhi
Kwa kuwa uchumi wa Tanzania unategemea na utaendelea kutegemea
kilimo na mifugo, Watanzania wanaweza kuyaendesha maisha yao
barabara bila ya kutegemea misaada kutoka nje kwa matumizi bora
ya ardhi hiyo. Ardhi ni ufunguo wa maisha ya binadamu kwa hiyo
Watanzania wote waitumie ardhi kama ni raslimali yao kwa maendeleo
ya baadaye. Kwa kuwa Ardhi ni mali ya Taifa, Serikali ni lazima iangalie
kuwa ardhi inatumiwa kwa faida ya Taifa zima na wala isitumiwe kwa
faida ya mtu binafsi au kwa watu wachache tu.
Ni wajibu wa TANU kuona kuwa nchi yetu inalima chakula cha kutosha
na kutoa mazao ambayo yataleta fedha nchini kwa kuuzwa katika nchi
za ngambo. Ni wajibu wa Serikali na Vyama vya Ushirika kuona kuwa
wananchi wanapatiwa vyombo, mafunzo ya uongozi unaohitajika katika
kilimo na ufugaji wa kisasa.
(b) Watu
Kuiwezesha siasa ya kujitegemea itekelezwe vizuri, wananchi ni budi
wajengwe moyo na shauku ya kujitegemea. Wajitegemee katika kuwa na
chakula cha kutosha, mavazi ya kufaa na mahali pazuri pa malazi.
Katika nchi yetu kazi iwe ni kitu cha kujivunia. Bali uvivu, ulevi na
uzururaji uwe ni jambo la aibu kwa kila mwananchi. Katika upande
wa ulinzi wa Taifa, wananchi wawe macho na vibaraka waliomo nchini
ambao wanaweza kutumiwa na maadui wa nje wenye nia mbaya ya
kuliangamiza Taifa hili na wawe tayari kulilinda Taifa inapolazimika
kufanya hivyo.
(c) Siasa Safi
Msingi wa siasa ya kujitegemea lazima uambatane na siasa ya Ujamaa
ya TANU. Ili kuzuia unyonyaji ni lazima kila mtu afanye kazi na aishi kwa
MIONGOZO MIWILI
39
SEHEMU YA NNE
UANACHAMA
MIONGOZO MIWILI
SEHEMU YA TANO
AZIMIO LA ARUSHA
Kwa hiyo basi, Halmashauri Kuu ya Taifa iliyokutana katika Community
Centre ya Arusha kuanzia tarehe 26/1/67 mpaka 29/1/67, inaazimia
ifuatavyo:
A. Viongozi
1. Kiongozi wa TANU au wa Serikali sharti awe mkulima au
mfanyakazi na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au
kikabaila.
2. Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
MIONGOZO MIWILI
41
C. Uanachama
Wanachama wafundishwe kwa ukamilifu imani ya TANU ili waielewe, na
wakumbushwe wakati wote umuhimu wa kuishika imani hiyo.
42
MIONGOZO MIWILI
SURA YA PILI
MWONGOZO WA TANU WA 1971
TUMECHOKA KUCHEZEWA
1.
Mabeberu wathubutu
Kujifanya mbwa-mwitu,
Au kujifanya mwewe,
Kwa kuachia wenyewe
Tudhaniwe tu makoo
Ya kuku au kondoo.
Linalia la mgambo,
Lisikike hadi ngambo:
Tumechoka kuonewa!
Tumechoka kuchezewa!
Tunasema: sasa basi
Ubeberu na uasi!
8. Vijana wa Afrika,
Siku yenu imefika!
Siku yenu ndiyo leo,
Siku ya kufunga teo:
Tumechoka kuonewa!
Tumechoka kuchezewa!
9. Shime, Onyesheni njia,
Vijana wa Tanzania:
Wapigeni wanyonyao,
Pamwe na vijibwa vyao;
Mabeberu makaburu,
Wapigeni kwa uhuru.
10.
Wamezidi kutughasi
Kwa kudhani ndiyo basi:
Semeni: leo ni leo,
Twali tukisuka teo!
Kimbieni, tumefika:
Iacheni Afrika!
43
(Azimio la Arusha)
UTANGULIZI
1. Bara letu la Afrika leo ni kiwanja cha mapambano makali ya
ukombozi. Mapambano hayo ni kati ya wale ambao kwa karne
nyingi wamekuwa wakinyonya utajiri wa Afrika, na kuwatumia
wananchi wa bara hili kama vyombo vyao, kama watumwa wao, na
wananchi wa Afrika ambao, baada ya kutambua hali ya unyonge na
kunyonywa, wameamua kuingia katika mapambano ya kujikomboa.
Mapambano haya ni magumu na ya muda mrefu. Wakati mwingine
huwa ya kimya kimya, mara yalipuke kama baruti; wakati mwingine
mafanikio huenda kwa wananchi, halafu punde si punde mafanikio
yakawaponyoka wananchi. Hiyo ndiyo historia ya Afrika mpaka
mwaka 1960, ambapo nchi nyingi za Afrika zilipata uhuru wao wa
bendera. Tangu mwaka huo mpaka leo Serikali nyingi za Afrika
zimeangushwa kwa nguvu, na Serikali mpya kuundwa. Hivi juzi
mabadiliko ya ghafla na ya mabavu yametokea Uganda, ambako
Kibaraka Amini na kikundi cha wanajeshi wenzake waasi wameiasi
Serikali ya Kimapinduzi ya U.P.C inayoongozwa na Raisi Obote.
Wanajeshi walio wengi hawakubaliani na maasi hayo, na wengi
wao, hasa maafisa wakubwa wameuawa na vibaraka hao. Ni dhahiri
kuwa wanaofurahia maasi ya vibaraka hawa ni wale waliokuwa
wakipinga siasa ya U.P.C ya kuleta Umoja na Ujamaa, na kuondoa
ukabila na Unyonyaji. Ndiyo maana Chama chetu kina wajibu
wa kuifafanua shabaha kuu ya mapinduzi yetu na ya Afrika, na
kuwatambua maadui wa mapinduzi haya, ili kutayarisha mipango
44
MIONGOZO MIWILI
45
MIONGOZO MIWILI
SIASA
Chama
11. Wajibu wa kuongoza Umma na vyombo vyake mbali mbali katika
juhudi ya kulinda uhuru, ili mapinduzi ya ukombozi wa Mwafrika
yaendelee, ni wa Chama. Wajibu wa Chama cha Kijamaa ni kuongoza
shughuli zote za Umma. Serikali, Mashirika, Vyama vya Umma, n.k,
ni vyombo vya kutekelezea siasa ya Chama. Historia yetu fupi ya
uhuru inaonyesha matatizo yanayoweza kutokea wakati Chama
hakiongozi vyombo vyake. Sasa wakati umefika wa chama kushika
barabara hatamu na kuongoza shughuli zote za Umma.
47
48
MIONGOZO MIWILI
49
ULINZI NA USALAMA
Katika upande wa ulinzi wa Taifa, wananchi wawe macho
na vibaraka waliomo nchini ambao wanaweza kutumiwa
na maadui wa nje wenye nia mbaya ya kuliangamiza Taifa
inapolazimika kufanya hivyo.
(Azimio la Arusha)
MIONGOZO MIWILI
51
UCHUMI NA MAENDELEO
Maendeleo ya nchi huletwa na watu
(Azimio la Arusha)
Maendeleo ya Watu
28. Kwa watu ambao walikuwa watumwa, au ambao walikuwa
wakionewa, wakinyonywa, na kunyanyaswa kwa sababu ya Ukoloni,
Ukabaila au Ubepari, maendeleo maana yake ni ukombozi.
Kitendo chochote kinachowapa uwezo zaidi wa kuamua mambo yao
wenyewe, ni kitendo cha maendeleo, japo kama hakiwaongezei afya
wala shibe. Kitendo chochote kanachowapunguzia uwezo wao wa
kuamua mambo yao wenyewe na kutawala maisha yao wenyewe,
si kitendo cha maendeleo, ni kitendo cha kuwarudisha nyuma,
japo kama kitendo chenyewe kinawaongezea afya na shibe kidogo.
Kwetu sisi maendeleo ya maana ni yale yanayotuondolea kuonewa,
kunyonywa, kunyanyaswa na mawazo ya kufungwa, na kutuongezea
uhuru na utu wetu. Kwa hiyo katika kufikiria maendeleo ya Taifa
letu, na katika kupanga mipango ya maendeleo, wakati wote mkazo
mkubwa utiliwe kwenye maendeleo ya WATU na siyo ya vitu. Ili
maendeleo hayo yawe ya watu, watu wenyewe lazima washiriki
katika kufikiria, kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo yao.
Chama chetu kazi yake si kuhimiza wananchi kutekeleza mipango
iliyoamuliwa na wataalam na viongozi wachache. Chama chetu kazi
yake ni kuona kuwa viongozi na wataalam wanatekeleza mipango ya
maendeleo kama ilivyoamuliwa na wananchi wenyewe. Uamuzi huu
wa wananchi unapokuwa unahitaji ujuzi ambao walio nao ni viongozi
na wataalam, ni wajibu wa viongozi na wataalamu hao kufikisha
ujuzi huo kwa wananchi ili waweze kujifanyia uamuzi wao; lakini
52
MIONGOZO MIWILI
29. Ili wananchi wawe na ari ya kulinda nchi yao, lazima Serikali ya
TANU kwanza itilie nguvu sana hali ya Uchumi wa wananchi.
Mtindo wa Uchumi tuliorithi kwa wakoloni, ambao umewatupa
wananchi wengi nje ya uchumi, lazima ubadilishwe bila kukawia,
na kuanzisha mipango ya kuongeza matumizi na kutumbukiza
rasilimali katika Wilaya zote. Kwa mfano, Mpango wa Fedha za
Maendeleo Mikoani umeonyesha kusaidia kuamsha shughuli za
kiuchumi na kuleta manufaa ya wazi wazi kwa wananchi, na itafaa
mpango huo utiliwe mkazo kwa kuongeza fedha hizo na kufanya
matumizi hayo yawe ya mwanzo katika makisio ya fedha za Serikali.
Chama kitilie mkazo kushirikisha watu katika kazi mbali mbali za
kujenga Taifa.
Akiba
Uchumi wa Kitaifa
31. Katika kuimarisha Maendeleo ya watu, hivi sasa ipo haja kubwa ya
kujenga na kustawisha uchumi wa ndani ya Taifa letu. Ingawa jambo
hili limegusiwa katika Mpango wa Pili wa Miaka Mitano, halikutiliwa
mkazo katika utekelezaji, na matokeo yake hayajaonekana. Kadhalika,
vitu ambavyo vinatengenezwa nchini mwetu lazima vilindwe na
mashindano yasiyo ya lazima kutoka nchi za nje.
Biashara ya Nje
53
Mashirika ya Umma
Ziada
54
MIONGOZO MIWILI
SURA YA TATU
MWONGOZO WA CCM WA 1981
YALIYOMO
DIBAJI
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
SEHEMU YA PILI
SEHEMU YA NNE
MIONGOZO MIWILI
55
DIBAJI
Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, katika Mkutano wake uliofanyika
mjini Dar es Salaam kuanzia tarehe 23 Novemba, 1981 hadi tarehe 7
Desemba, 1981 ilipitisha MWONGOZO WA CHAMA CHA MAPINDUZI
wa 1981. Halmashauri Kuu ya Taifa ilifikia uamuzi huu baada ya
kuzingatia na kuchambua hali halisi ilivyo hivi sasa nchini katika
masuala ya siasa, uchumi na maendeleo ya jamii, na kuona kuwa
kuna haja sasa ya kutoa msukumo mpya wa ujenzi wa Ujamaa, pamoja
na utekelezaji sahihi wa maamuzi mengine mbalimbali yaliyokwisha
kutolewa. Shabaha ya Mwongozo wa 1981 ni kufafanua kwa upana zaidi
nadharia ya Chama juu ya masuala muhimu na ya msingi ya Siasa yetu
katika fani mbalimbali, pamoja na kutoa maelekezo yaliyo wazi zaidi
kuhusu mbinu sahihi za utekelezaji wa siasa hiyo.
Katika kipindi kilichofuatia kutangazwa kwa Azimio la Arusha, Chama
kilitoa maandishi muhimu kadhaa yanayochambua na kufafanua fani
mbalimbali za Siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea, pamoja na kuelekeza
njia sahihi za utekelezaji wa siasa hiyo. MWONGOZO WA TANU wa mwaka
1971 ni miongoni mwa matamko hayo muhimu ya kipindi hicho.
56
MIONGOZO MIWILI
SEHEMU YA KWANZA
Utangulizi
1. Historia ya Watanzania kwa vile ni sehemu tu ya historia kubwa
zaidi ya Waafrika kwa jumla lazima wakati wote ichambuliwe na
kueleweka katika mazingira ya umoja wa Afrika na watu wake.
Waafrika wamepitia vipindi na karne za fanaka na maendeleo ya
jamii na pia vipindi na karne za misukosuko mikubwa na hata
unyonge kitaifa.
2.
3.
57
MIONGOZO MIWILI
59
MIONGOZO MIWILI
61
22. Katika hali hiyo ambapo Chama kilianza kuona kuwa Serikali
yake inashindwa kutosheleza matazamio ya wananchi kwa jumla
na badala yake kukabiliwa na ongezeko la misuguano ya kijamii
mijini na vijijini, na ambapo kilianza kuingiwa na mashaka na
kutoridhika na matokeo ya utekelezaji wa mipango ya uchumi wa
taifa uliotegemea rasilimali toka ngambo kuwa ndiyo msingi wa
maendeleo, Chama kiliwajibika kujiuliza maswali juu ya usahihi wa
siasa ambayo kimeifuata na kuitekeleza tangu nchi ijipatie uhuru.
Siasa ya uchumi ya kipindi hiki ilikuwa na sura mbili: kujenga nchi
kwa msingi wa ubebari na kwa kutegemea rasilimali toka ngambo.
Funzo tulilopata kama Chama ni kuwa siasa hiyo ya uchumi ilikuwa
imeshidwa kwa maana mbili: Kwanza ni kuwa badala ya kusaidia
kuimarisha umoja wa Taifa ulioanza kujengwa wakati wa kupigania
uhuru ilizalisha migongano ya kijamii na kuanza kukifarakanisha
Chama na umma. Pili, Siasa hiyo ya uchumi wa kibepari
unaotegemea rasilimali toka ngambo kama msingi wa maendeleo
hayo pia ilishindwa maana utekelezaji wake hakuleta vuguvugu
la maendeleo ya kiuchumi yaliyotegemewa na wala hakukuwa na
mtiririko wa rasilimali za kutosha toka ngambo kuingia nchini.
62
MIONGOZO MIWILI
C. AZIMIO LA ARUSHA
23. Tangu nyakati za kupigania uhuru Chama kiliweza wakati wote
kuelewa na kutambua mwenendo wa hali ya mapambano nchini
na duniani kwa jumla na kuchukua hatua sahihi kwa wakati
unaofaa ili kuimarisha na kuendeleza mapambano ya wananchi.
Kuna maamuzi kadhaa katika historia ya Chama chetu, ambayo ni
pamoja na uamuzi wa kuunganisha nchi za Tanganyika na Zanzibar
yanayoonyesha kinaganaga uwezo huo wa Chama kukua na nyakati.
63
26.
Tungeweza kuendelea kukariri mafanikio yaliyopatikana
nchini kutokana na utekelezaji wa siaisa ya Chama ya Ujamaa
na Kujitegemea. Lakini jambo la kuzingatia ni kuwa hatua
tulizozichukua katika kutekeleza Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea
ni za awali tu na kwamba kubwa zaidi tulilofanikiwa ni kujichorea
barabara tunayodhamiria kufuata katika kulijenga Taifa letu la
watu sawa na huru ambalo lengo lake ni maendeleo kwa wote.
SEHEMU YA PILI
MIONGOZO MIWILI
29. Sasa, bei za mafuta na bei za bidhaa za viwanda vya nchi zilizoendelea
zimepanda sana katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Tanzania
sasa inawajibika kutumia asilimia sitini ya mapato yake yote ya
fedha za kigeni kununulia mafuta ambapo mwaka 1972 ilitumia
asilimia kumi ya fedha za kigeni kununua kiasi hicho hicho cha
mafuta. Wakati huo huo, kwa kutumia mbinu za kupandisha
bei za bidhaa zao za viwanda na kushusha bei za mazao ya nchi
changa, nchi zilizoendelea zimefaulu kuupunguza kabisa uwezo
wetu wa kununua bidhaa za viwanda vyao zinazohitajika sana na
nchi changa. Kwa mfano, miaka kumi iliyopita Tanzania iliweza
kununua trekta moja toka ngambo kwa thamani ya tani tano za
chai iliyouzwa ngambo. Leo Tanzania inahitaji tani kumi na saba za
chai ili kununua trekta la aina ile ile. Hali hii lazima iwe na matokeo
mabaya kwa uchumi wa Taifa letu.
30. Nchi yetu pia imepatwa na matatizo ya ndani ambayo pia
tusingekuwa na uwezo wa kuyazuia na yote yameathiri hali
yetu ya uchumi. Matatizo hayo ni pamoja na vita vya kujihami
tulivyolazimika kupigana dhidi ya majeshi ya uvamizi wa Iddi Amin,
mafuriko makubwa ya 1978/79 na hali ya ukame katika baadhi ya
mikoa.
65
33. Pili kuna suala la utengenezaji mali wa kijamaa. Laiti kama Chama
kingeongoza, kusimamia, kuhimiza na kusaidia utekelezaji wa
Ujamaa Vijijini vizuri tangu Azimio la Arusha hadi sasa, tungeweza
kuwa na sekta kubwa ya ujamaa katika kilimo vijijini ambavyo
ingetuwezesha kutoa ziada ya mazao ya chakula na biashara kuliko
ilivyo sasa. Kama wastani wa ekari za ujamaa wa kila kijiji nchini
ungekuwa angalau ekari mia kwa kila kijiji wakati huu basi sekta
ya Ujamaa vijijini katika kilimo ingekuwa na ekari zipatazo laki
sita. Ekari laki sita za ujamaa zingeweza kuongeza ziada ya mazao
yanayotolewa na Taifa kwa kiasi kikubwa.
MIONGOZO MIWILI
36. Aidha, kuna matatizo ya kijamii kama vile kuongezeka kwa rushwa,
hujuma za kiuchumi, wizi, ujambazi na uharibifu wa mali ya
umma, mambo ambayo yanatupunguzia nguvu zetu za kiuchumi
na kudhoofisha dhamira ya umma ya kujenga ujamaa. Haya yote
yamo katika uwezo wa Chama, Serikali na wananchi kuyapiga vita
na kuyashinda.
67
MIONGOZO MIWILI
43. Vyuo vya chama ambavyo ndivyo ingebidi viwe mahala pa kuandaa
wanachama hasa viongozi wa Chama vimeendelea kuwa vyuo
vya Elimu ya Siasa kwa jumla. Ni kweli kuwa Chama chochote cha
kijamaa halisi lazima kiwe na mipango thabiti ya kutoa elimu ya
siasa ili kuwahamasisha wananchi kwa jumla na hasa makundi ya
taasisi mbalimbali kama vyuo, shule, majeshi, vijana, wafanyakazi,
wakuu wa kazi na kadhalika. Lengo la elimu ya siasa kwa taasisi hizi
ni kuinua mwamko wao wa siasa na kuwapa wahusika mwelekeo
wa kisiasa kwa kulingana na shughuli zao katika nchi. Lakini
wanachama wanahitaji mafunzo ya siasa ya Chama ili kuongeza
MIONGOZO MIWILI
69
MIONGOZO MIWILI
71
MIONGOZO MIWILI
73
MIONGOZO MIWILI
75
MIONGOZO MIWILI
77
SEHEMU YA TATU
MIONGOZO MIWILI
79
MIONGOZO MIWILI
81
80. Mapinduzi ya kilimo vijijini katika nchi yetu ni kilimo cha kijamaa
na cha kisasa ambacho kina sifa zifuatazo: Kwanza ni kilimo cha
mashamba makubwa ya kijamaa ya vijiji, pili ni kilimo kinachotumia
pembejeo, zana za utaalamu na tatu ni kilimo kinachotekelezwa
kwa utaratibu bora wa kazi unaoleta ufanisi.
81. Sifa moja ya kilimo cha kisasa duniani kote ni kuwa ni kilimo cha
mashamba makubwa. Tofauti iliyopo ya mashamba hayo ni katika
umilikaji. Katika nchi za kibepari mashamba hayo makubwa ni
mali ya mabepari, wakati katika nchi za kijamaa mashamba hayo
makubwa ni mali ya Taifa au ni mali ya ushirika wa wanavijiji.
Hali hiyo imeanza kujitokeza pia katika kilimo cha kisasa nchini
Tanzania.
82. Mantiki iliyokisukuma kilimo cha kibepari cha kisasa kiwe cha
mashamba makubwa ni ile ile iliyokisukuma kilimo cha kijamaa cha
kisasa kiwe cha mashamba makubwa. Kilimo cha kisasa ni kilimo
cha zana, na ukishavuka kilimo cha plau za maksai na kuingia
katika matrekta na mashine nyingine za kupandia na kuvunia,
basi ni hasara kubwa kuzitumia zana hizo katika vishamba vidogo
vidogo vya ekari kadhaa tu. Ufanisi wa hali ya juu unapatikana
wakati zana hizo zinatumika katika maeneo makubwa. Wakati huo
huo ni kuwa zana hizi za kisasa ni aghali na haiwezekani kwa kila
mkulima mwenye ekari chache kupata uwezo wa kuzinunua hata
katika nchi za kibepari. Hivyo, katika nchi za kibepari ni wakulima
wakubwa tu ndio wenye uwezo wa kumiliki zana hizi na katika
mashindano hayo, wakulima wadogo wamelazimika kutoa nafasi
kwa wakulima wakubwa. Katika nchi za kijamaa uwezekano wa
kumiliki zana hizi ni kwa kupitia Serikali (Mashamba ya Taifa) na
ushirika wa wakulima vijijini.
83. Uwezekano wa kuanzishwa kwa mashamba makubwa ya ujamaa
vijijini ni mkubwa katika Tanzania maana mafanikio yaliyopatikana
mpaka sasa katika vijiji vilivyotekeleza ujamaa vijijini yameufungua
macho umma wa Wakulima vijijini. Wakati huo huo maeneo ya
kuanzisha na kupanua mashamba ya ujamaa hayana matatizo katika
82
MIONGOZO MIWILI
86. Wakati huo huo Chama kihakikishe kuwa serikali inaagiza matrekta
toka ngambo kwa kuzingatia uwezo na uzito unaolingana na umuhimu
wa kilimo kwa maendeleo ya Taifa letu. Kupanga ni kuchagua. Hivyo,
kama kwa mfano, ni kuchagua kati ya magari madogo na matrekta,
basi uzito uwe kwenye matrekta. Lakini, kwa kuzingatia hali halisi
ya uchumi wetu (upungufu wa fedha za kigeni na kwamba hatuna
viwanda vyetu vya chuma na vya matrekta), itachukua muda wa
miaka mingi kabla ya kilimo cha trekta kuwa ndicho kilimo cha vijiji
vyetu. Kwa sasa mbinu ya kutufikisha huko siyo kungoja matrekta
bali ni kutumia majembe ya mkono na plau za maksai katika kilimo
cha kijamaa na cha binafsi vijijini ili kuongeza ziada ya mazao kitaifa
ambayo ndiyo ufunguo wa kulipatia Taifa uwezo wa matrekta zaidi
na kukuza uwezo wetu wa kuanzisha viwanda mama na vinginevyo.
MIONGOZO MIWILI
83
MIONGOZO MIWILI
85
(4) Viwanda
Jambo la kusisitiza linahusu hali ya utengenezaji mali katika viwanda
vilivyopo nchini hivi sasa ambapo vilivyo vingi havitengenezi mali kwa
kadiri ya uwezo vilivyo nao. Chama itabidi kijihusishe na matatizo
ya viwanda hivi na kuhakikisha kuwa vinapata misaada yote ili viweze
kutengneza mali kwa kadiri ya uwezo wake. Licha ya matatizo ya vipuri
na utaalam, viwanda hivi vinakabiliwa pia na matatizo ya kisiasa kama
vile upungufu wa mwamko wa siasa na utovu wa nidhamu.
Viwanda vingi tulivyonavyo nchini hutoa makapi ambayo yangeweza
kutumika kwa utengenezaji wa bidhaa nyingine, lakini jitihada hiyo
haijafanywa. Viwanda kama vya sukari, mafuta, mbolea, nyama na vya nguo
ni miongoni mwa viwanda vya aina hiyo. Kuanzia sasa Serikali itawajibika
kuandaa mipango ya kuyatumia makapi yatokanayo na viwanda vya aina
hiyo ili kutengeneza bidhaa zinazoweza kutengenezwa.
86
MIONGOZO MIWILI
87
C . MAENDELEO YA JAMII
91. Katika kipindi kinachoanzia sasa Chama kitatilia mkazo suala la
ujenzi wa tabia na maadili ya kijamaa nchini. Pamoja na jitihada
iliyofanywa ya kutoa elimu na kuunda vyombo vya umma, jamii
yetu bado inazo mila, tabia na maadili yaliyo kinyume na maadili
ambayo yanafanana na misingi ya siasa ya ujamaa tunayosukudia
kuijenga.
MIONGOZO MIWILI
vya Chama vyenyewe. Wakati huo huo, bado kuna mabaki ya tabia
ya kupuuza elimu ya shule kwa watoto na badala yake kuna wazazi
wanaopendelea watoto wao wachunge mifugo au hata kuolewa
badala ya kuendelea na shule.
89
(d) Hali ya vijiji vingi ingali duni kwa ustawi wa jamii na utamaduni.
Chama kitalishughulikia suala la kuleta mapinduzi ya mazingira
vijijini katika fani hiyo.
(e) Kuhusu walemavu, Chama kitahimiza serikali kuchukua hatua
za kuimarisha na kuvipanua vifaa muhimu kwa walemavu kama
baiskeli, viatu, magongo, na kadhalika.
(2) Elimu
Chama kuanzia sasa kitajihusisha zaidi na shughuli za elimu nchini
hasa kwa upande wa maandalizi ya waalimu na maendeleo yao na ya
shule na vyuo maana waalimu wana mchango mkubwa wa kutoa katika
kumjenga Mtanzania mpya. Katika lengo hilo, Chama kitafanya tathmini
ya mafanikio tuliyoyapata katika kuielewa na kuitekeleza falsafa ya
Chama ya Elimu ya Kujitegemea.
Aidha, Chama kitalitazama upya Agizo la Musoma katika vipengele vyake
vyote. Kwa sasa imedhihirika kuwa utekelezaji wa Azimio hilo kuhusu
utaratibu wa kuingia Chuo Kikuu unahitaji mabadiliko ya msingi.
Pamoja na mafanikio tuliyoyapata katika Elimu ya Watu Wazima
Chama kitaendelea kuhimiza wananchi na hasa wanaCCM na viongozi
kujiendeleza kwa elimu kwa kadiri ya uwezo wao na kujenga tabia ya
kusoma kama sehemu ya maisha yao.
(3) Afya
Kazi moja muhimu ambayo ni ya Chama katika miaka ijayo ni kuhimiza
kuenezwa kwa elimu ya kinga ya maradhi pamoja na kuongoza
mapambano dhidi ya tabia na mila zisizo nadhifu. Hali ya afya ya
wananchi wengi vijijini inaathiriwa na tabia na mila ambazo zinapingana
na maendeleo ya jamii kama vile tabia ya kutotumia vitanda, tabia ya
kuishi katika nyumba moja na mifugo, tabia ya kutotumia vyoo, tabia ya
kunywa maji yasiyochemshwa, miiko mbalimbali, na kadhalika. Wakati
huo huo Chama kitatilia mkazo suala la usafi wa mazingira mijini na
vijijini pamoja na umuhimu wa kuwepo kwa vyoo vya umma mijini.
90
MIONGOZO MIWILI
(5) Nishati
Suala la nishati ni la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu. Pamoja na
kuendelea kutafuta mafuta, Chama kitahakikisha kuwa serikali inazidisha
mipango thabiti itakayoliwezesha Taifa kuanza kutumia nguvu za maji,
makaa, upepo na jua. Pamoja na miradi mikubwa ya nguvu za maji
kuna haja ya kutia maanani miradi midogo midogo ya nguvu za maji.
Suala la kuni itabidi lipewe umuhimu mkubwa kwa kuwa na mipango
kamambe ya kupanda miti vijijini na miradi ya Mikoa na Taifa. Chama
kiihimize Serikali kuendelea na kutafuta mbinu za kutumia makaa ya
mawe tuliyonayo kusukuma uchumi wetu. Umuhimu wa suala la nishati
utahitaji sera maalum.
(6) Msimamo juu ya kuendeleza sayansi na teknolojia
Mpango wa miaka Ishirini unatoa mwelekeo wa maendeleo ya sayansi na
teknolojia, kwani sayansi na teknolojia ni msingi muhimu kwa maendeleo
ya kisasa. Chama kijihusishe zaidi na mipango ya kuwapata wanasayansi
na wanateknolojia wenye uwezo wa viwango mbalimbali vya utaalamu na
msimamo sahihi wa siasa. Wakati huo huo, Chama kishughulikie ustawi
wa wataalamu na mabingwa tulionao hivi sasa nchini ili kuhakikisha
kuwa wanaishi katika mazingira yanayowawezesha kutoa mchango wao
kwa ukamilifu katika ujenzi wa Taifa letu. Kutokana na kukosa msimamo
sahihi wa kuwashughulikia wataalamu wetu kumewafanya baadhi ya
MIONGOZO MIWILI
91
D. ULINZI NA USALAMA
MIONGOZO MIWILI
100. Chama pia kina kazi ya kuchambua tena na kwa makini nafasi ya
Jeshi la Kujenga Taifa katika kusukuma mapinduzi ya ulinzi na ya
uchumi wa Taifa. Pamoja na kwamba madhumuni ya awali ya J.K.T.
bado hayajakiukwa na wakati, Chama kitazame namna ya kulipa
J.K.T. na J.K.U. uwezo wa kuwa chombo cha kukabili kazi za ujenzi
MIONGOZO MIWILI
93
94
MIONGOZO MIWILI
95
SEHEMU YA NNE
CHAMA NA MAPINDUZI YETU
Chama tunachokiunda tunataka kiwe chombo madhubuti
katika muundo wake na hasa katika fikra zake na vitendo
vyake vya kimapinduzi vya kufutilia mbali aina zote
za unyonyaji nchini, na kupambana na jaribio lolote lile
la mtu kumwonea mtu, au shirika au chombo cha nchi
kuonea au kudhalilisha wananchi, kudhoofisha uchumi au
kuzorotesha maendeleo ya Taifa.
(Katiba ya CCM)
104. Chama chetu, Chama cha Mapinduzi, ni Chama chenye historia
ya kipekee katika Afrika. Historia yake ni ya mafanikio na ushindi
katika fani mbalimbali za utekelezaji wa malengo ya siasa yake.
Wanazuoni watakapokuja andika historia ya Chama chetu wataweza
kuyachambua kwa kina na mapana mafanikio hayo yasiyo na kifani.
105. Chama cha Mapinduzi ni Chama cha kijamaa. Kazi kubwa ya CCM
ya sasa ni kuziunganisha nguvu zote za kijamaa na za kimaendeleo
nchini na kuziongoza katika mapambano ya kujenga ujamaa
Tanzania na kujenga ushirikiano wa kimapinduzi wa wajamaa
na wapenda maendeleo wote katika Afrika na Dunia katika
mapambano dhidi ya ukoloni, ukoloni mambo leo, ubepari na
ubeberu.
106. Chama cha Mapinduzi ni chombo kikuu na cha pekee cha uongozi
wa taifa letu. Kuongoza ni kuonyesha njia. Kwa hiyo, Chama chetu
ni mwanga unaotumulikia njia katika hali ngumu ya mapambano
ya wakulima na wafanyakazi kuelekea kwenye ujamaa. Uhalali wa
uongozi wa Chama chetu una misingi ya kihistoria ingawa historia
peke yake haitoshi kuelezea uhalali wa Chama cha Mapinduzi kwa
sasa kuongoza Taifa. TANU na ASP vilijijengea uhalali machoni
mwa wananchi kwa kuwadhihirishia kuwa vinastahili kuongoza
kutokana na usahihi wa siasa na mbinu zao katika mapambano
96
MIONGOZO MIWILI
A. CHAMA NA SERIKALI
97
110. Kuhusu suala hili, Chama cha Mapinduzi kina kazi mbele yake ya
kujumlisha tuliyojifunza tangu tupate uhuru na hasa baada ya
Azimio la Arusha juu ya hatari zinazoweza kutokea kwa siasa ya
Chama na kwa taifa wakati madaraka muhimu ya Chama, Serikali
au Mashirika ya Umma wanakabidhiwa watu ambao kisiasa ni
chui katika ngozi ya kondoo.
MIONGOZO MIWILI
huduma bora kwa umma. Chama kione pia kuwa mifumo iliyopo
Serikalini na katika Mashirika ya Umma inamwezesha mfanyakazi
kushiriki katika uongozi wa kazi mahali alipo na kwamba kwa
kushirikiana na wenzake anapata nafasi anayostahili ya kulijenga
na kulitumikia Taifa lake.
99
118. Wakati huo huo, Chama kitafanya uchambuzi ili kupata njia za
kuimarisha madaraka ya umma tangu vijijini hadi Taifa kwa
jumla. Chama kitayarudia maamuzi yake ya nyuma kuhusu suala
hili tangu tupate uhuru hadi sasa ili kujipa msingi wa kubuni
utaratibu wa kujenga madaraka ya umma yatakayotuelekeza
kwenye demokrasia ya kijamaa, katika jitihada hii, Chama
kitaepuka jaribio la kurudisha mifumo ya tawala za kizamani,
badala yake Chama kitajifunza toka mifumo ya zamani na hata ya
nchi nyingine ili kubuni mfumo mpya utakaolingana na mahitaji
ya maendeleo ya kidemokrasi na ya ujamaa ya Tanzania ya leo na
ya kesho. Hivyo, Chama kitayashughulikia masuala ya madaraka
ya miji, wilaya na vijiji pamoja na suala la vyama vya ushirika
katika msimamo huo.
119. Kwa hiyo, Chama pia kina wajibu wa kuhakikisha kuwa wananchi
katika fani zote za maisha wanashiriki kwa ukamilifu katika ujenzi
wa taifa lao. Katika nchi yetu wakulima na wafanyakazi ndio
msingi wa mfumo wa jamii yetu na siasa ya ujamaa ya Chama ni
siasa ya tabaka hili. Hivyo harakati za kujenga ujamaa ni harakati
100
MIONGOZO MIWILI
101
MIONGOZO MIWILI
103
MIONGOZO MIWILI
134. Katika hali hii, hatua inayofuata ni kwa kila Tawi la Chama
kuchukua hatua ya kuwajadili wanachama wake mmoja mmoja ili
kuamua kama bado wanastahili kuendelea na uanachama au la.
Kwa kuwa wazembe, wazururaji, wezi na majambazi watakuwa
wamefichuliwa katika vikao hivi, kwa kuwa wapinga ujamaa
kiitikadi na kwa vitendo watakuwa pia wamefichuliwa, basi hii
ndiyo nafasi ya kukitakasa Chama. Matawi yapendekeze kwenye
vikao vya juu hatua za kuwachukulia wanachama watakaodhihirika
kuwa hawatimizi masharti na wajibu wa wanachama. Azimio la
Arusha linasisitiza juu ya ubora wa wanachama badala ya wingi wa
wanachama. Vuvuvugu hili la mijadala ya wanachama wenyewe tu
litasaidia kuunda hali itakayowezesha kupiga hatua za mwanzo za
kuelekea kwenye lengo hilo la Azimio la Arusha.
105
MIONGOZO MIWILI
107
MIONGOZO MIWILI
109
151. Hata hivyo, kazi kubwa ya Chama katika sehemu ya kazi itafanywa
na tawi la Chama la mahali pa kazi panapohusika. Kazi ya Chama
katika Taifa, Mkoa na Wilaya ni kuunda hali itakayoliwezesha Tawi
la Chama kutekeleza wajibu wake wa uongozi. Ili kuhakikisha
kuwa Chama katika sehemu ya kazi kinashika nafasi yake ya
uongozi kuna masuala kadhaa ya kutia maanani.
153. Jambo la pili ni kuwa vyama vya kijamaa halisi haviongozi kwa
mabavu bali kwa kuelimisha, kushawishi, kuelekeza na kwa
chama chenyewe kuonyesha njia kwa vitendo. Kwa hiyo, kazi ya
Chama katika sehemu za kazi itakuwa kuwajenga wana CCM kujua
namna ya kuwashirikisha wafanyakazi wenzao katika kutekeleza
malengo na wajibu wa kazi kutokana na mfano wao wenyewe
wa kutekeleza wajibu kwa makini na kwa ari na uwezo wao wa
kushawishi, kushauri na kuwashirikisha wafanyakazi.
MIONGOZO MIWILI
156. Suala linarudia pale pale tulipoanzia. Kwa Chama cha Mapinduzi
kuongoza mapinduzi katika sehemu za kazi, kazi ya msingi ni
kuwaandaa wanachama na viongozi wa matawini kwa mafunzo
thabiti ya siasa ya Chama; ni kwa Chama kuhakikisha kuwa katika
kila sehemu ya kazi viongozi wa Chama waliopo na wanachama
kwa jumla wanapata miongoni mwao kada wa Chama wenye
uwezo wa juu wa uchambuzi na mbinu watakaosaidiana nao
katika mawimbi ya harakati. Hii ndiyo kazi kubwa ya Chama
katika siku zijazo.
111
MIONGOZO MIWILI
113
167. Katika hali hii Jumuia za wananchi zinaweza kuwa vyombo muhimu
vya mapambano ya Chama na kuwa nguvu zake za akiba. Katika
kipindi kinachoanzia sasa, Chama kitajitahidi kuzijenga jumuia
kwa kushirikiana nazo ili ziweze kuwa nguvu thabiti za mapinduzi
ya kujenga ujamaa. Papo hapo, Chama kitahakikisha kuwa Jumuia
za wananchi zinapata msaada utakaoziwezesha kushirikiana na
Chama bila ya kupoteza uwezo wao wa kuziendesha shughuli zao
wenyewe bila ya kuingiliwa.
114
MIONGOZO MIWILI
MWISHO
MIONGOZO MIWILI
115
SURA YA NNE
MAAMUZI YA ZANZIBAR, 1991
(Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Ali Hassan Mwinyi wakati
akizungumza na wazee wa chama, viongozi wa taifa, mashirika ya umma
na watu binafsi juu ya ufafanuzi wa maamuzi ya Halmashauri Kuu ya
Taifa katika kikao chake cha Zanzibar: Diamond Jubilee Dar es Salaam,
tarehe 25/2/1991)
Kabla ya yote, labda niseme kwamba kwa kuwa tumo katika mwezi wa
pili tokea kuanza kwa mwaka mpya, nami sijapata nafasi ya kukutana
nanyi wazee, ni vyema nitumie nafasi hii kwanza kukutakieni heri ya
mwaka mpya, na baraka zote za mwaka 1991. (Makofi). Ninakuombeeni
uzima, nguvu, baraka na mafanikio.
Pili, tuna kawaida katika nchi yetu, kwamba kila linapotokea jambo
muhimu katika Taifa, tunatafuta nafasi ya kukutana nanyi na kukuelezeni.
Hivyo, leo napenda kuzungumza nanyi wazee wa Dar es Salaam na, kupitia
kwenu, iwe ninazungumza na Wazee wenzenu wa Tanzania nzima. Kwa
hiyo, hayo nitakayokuambieni nyinyi, ninawaambia pia Wazee wa Taifa
letu wote kwa jumla.
Hivi karibuni Halmashauri Kuu ya Taifa ilifanya kikao chake cha
kawaida Zanzibar, ambacho kilijadili mambo mbalimbali. Kikao hicho
kilimalizika kwa kutoa maamuzi maalum. Maamuzi hayo yana uzito
mkubwa. Inaelekea baadhi yetu, pamoja na Vyombo vyetu vya Habari,
hatukuyaelewa vizuri maamuzi hayo. Kwanza, nataka nivivue lawama
Vyombo vyetu vya Habari. Maana hatukuwa nao huko. Kwa hivyo
walitangaza vile walivyoelewa. Kwa sababu hiyo nimeona ni vyema
116
MIONGOZO MIWILI
117
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
119
MBINU ZA KUJITEGEMEA
MIONGOZO MIWILI
Ili tujitoe, kitaifa, kwenye shimo la utegemezi tulimo hivi sasa, mbinu
bora ni kutoa uhuru kwa kila mwananchi wa kila Kaya, wa kila Kata, wa
kila Tarafa, wa kila Wilaya na wa kila Mkoa kutumia nguvu zake zote
katika kuzalisha. Matokeo ya hatua hii ni kumwezesha kila mtu katika
Kaya, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa kujitegemea. Tukifika hapo ndipo
Taifa litapokuwa limeondokana na hali ya sasa ya uchumi tegemezi.
KUPANGISHA NYUMBA
121
Sisi tunaamini kwamba baada ya kipindi kirefu cha utumishi, mtu aweze
kuwa na nyumba ili, hata akiwa kipofu angalau aweze kupapasa kuta
zake na kusema: Hii ni nyumba yangu niliyoipata kwa jasho langu la kazi
ya miaka 30. Tunataka awe na kitu. Lakini, Ndugu Wazee, bahati nzuri
wanachama wa CCM, kama wananchi wengine, wanaruhusiwa kukopa.
Wanaweza kukopa kwenye benki zetu wakajenga nyumba za kukaa. Sasa
jamani tukisema kwamba hata mtu aliyekopa asiipangishe nyumba hiyo
atalipia nini huo mkopo?
Vinginevyo tutakuwa tunamfanyia mzaha mtu huyo. Maana
atachukua mkopo, ajenge nyumba, kisha ashindwe kulipa huo mkopo.
Waliomkopesha wataikamata hiyo nyumba na kuiuza ili kurudisha
fedha yao. Katika hali hiyo mwana-CCM gani atakayekuwa na nyumba
122
MIONGOZO MIWILI
123
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
125
Lakini ikiwa watu pale pale wenyewe wana hisa katika kampuni au
shirika - mfano TANESCO [au] kuwa Mkurugenzi katika kampuni ya
Kibepari. Napenda suala hili lieleweke vizuri ili kujibu fikra zilizojengeka
kuwa uamuzi huo umevunja Azimio la Arusha.
MIONGOZO MIWILI
127
Katika hali hiyo, kulikuwa hakuna ulazima wa kufanya kazi ya pili. Afanyae
kazi zaidi ya moja huonekana ni mlafi au ana tamaa. Kwa mshahara huo
huo niliweza kudunduliza pesa na mwishowe kununua gari mpya kabisa.
Gari hilo lilinigharimu pesa nyingi kwa wakati huo - shilingi 13,000/=!!
Wakati huo bei ya mafuta nayo ilikuwa shilingi tatu tu kwa galoni zima.
Katika mazingira ya aina hii mshahara mmoja ulimudu kukidhi mahitaji
ya wafanyakazi wengi ukiacha walevi.
128
MIONGOZO MIWILI
HALI IMEBADILIKA
Lakini leo mambo yamebadilika. Gharama ya maisha imepanda sana.
Serikali yenyewe imeungama waziwazi kuwa haina uwezo wa kumlipa
mfanyakazi wake mshahara unaomwezesha kumudu gharama za
maisha. Kutokana na hali hiyo, wafanyakazi wengi, wanashindwa kukidhi
mahitaji yao muhimu. Ndio maana Chama na Serikali yake vimekuwa
vikiwahimiza wafanyakazi kufanya shughuli nyingine za halali, baada
ya saa za kazi, ili kujiongezea mapato. Mfano wa kazi hizo ni kama vile:
kutibu, kuandika vitabu, kuandika mradi, kutoa ushauri wa kitaalamu,
kufundisha, overtime, useremala, ufundi bomba, ufundi umeme, ufundi
cherahani, kilimo, ufugaji, kuziba mipira ya magari, kuteka maji ya kuuza,
kupiga matofali, kutengeneza baiskeli na kadhalika.
129
Kwa hiyo kama siku moja tulimtia mwenzetu msukosuko kwa kuwa
na shamba kubwa, mbuzi 18 au kuku 500, sasa Chama kimekua katika
falsafa yake. Falsafa ya sasa inatia maanani hali halisi ya wakati wa sasa.
Ndio maana kule Zanzibar tukaruhusu kiongozi awe na shamba lisilozidi
hekta 20, hasa kama shamba hilo limo katika eneo la kijiji.
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
131
SURA YA TANO
Miongozo Miwili ya Chama na
Tabaka Lililopindua Ujamaa*
Issa Shivji
132
MIONGOZO MIWILI
Mambo haya yote mawili ni wazi yalikuwa tishio kwa Tanzania. Tanzania
pia ilikuwa na wasiwasi wa kuvamiwa na jeshi la Wareno. Ndio maana
chama na serikali waliamua kuwa na jeshi la wanamgambo. Jambo hili
ni la kwanza linalozungumziwa katika Mwongozo wa Tanu wa 1971.
Pia, Tanzania ilikuwa haipendwi na mabeberu kutokana na siasa zake
za kijamaa.
Pamoja na mambo haya, sifa moja ya Mwongozo ni uchambuzi wake wa
radikali wa hali halisi ambao unaufanya Mwongozo kuwa nyaraka ya
kimapinduzi zaidi kuliko zote zingine zilizoandikwa wakati wa enzi za
Azimio la Arusha. Mfano mmoja tu unatosha kudhihirisha hili.
Mapinduzi ni mabadiliko ya haraka katika jamii,
mabadiliko ambayo yanawanyanganya wachache
madaraka ambayo walikuwa wakiyatumia kwa manufaa
yao (na ya wanyonyaji wa nje), na kuyaweka madaraka
hayo mikononi mwa wengi ili kuendeleza maslahi yao.
MIONGOZO MIWILI
133
Katika hotuba ya Mei Mosi (ya mwaka wa 1974) yenye kichwa cha habari
Ukigoma unamgomea nani? Mwalimu aliwashutumu wafanyakazi, jambo
134
MIONGOZO MIWILI
Kwa upande mwingine, sera ya Chama juu ya vijiji vya ujamaa pia
ikatekwa na wenye jazba na wapiga debe katika Chama. Mtazamo
wa Ujamaa Vijijini ambao ulisisitiza kwamba vijiji vya ujamaa viwe
chaguo la hiari la wakulima wenyewe ukageuzwa. Sera ukawa vijiji vya
maendeleo na wanakijiji wakalazimshwa, mara nyingine chini ya ulinzi
na mabavu ya FFU (Field Force Unit) kuhamia katika vijiji vya maendeleo.
Jambo hili lilifanya wakulima waanze kupoteza imani na Chama. Kwa
ufupi basi, matabaka ya wafanyakazi na wakulima wakafarakanishwa na
kutenganishwa na Chama, na kwa kiasi fulani Mwalimu mwenyewe. Kwa
upande mwinigine, kuvunjika kwa nguvu za wavujajasho, kukasafisha
njia kwa warasimu na wamangimeza wa Chama na Serikali, kuendelea
kujilimbikizia madaraka (na hata mali angalau kwa kificho) na kujijenga
MIONGOZO MIWILI
135
136
MIONGOZO MIWILI
Kwa hakika matamko haya yalikuwa ni kukiri wazi wazi kwamba sera
za Ujamaa zilikuwa zimehujumiwa na viongozi wenyewe waliopewa
jukumu la kuongoza ujenzi wa Ujamaa kutokana na maslahi yao ya
kitabaka ya kibepari.
Hapa tunashuhudia kwa mara ya kwanza, Chama kikikiri kwamba kuna
mapambano au harakati za kitabaka dhana ambayo kila mara Chama, na
hasa Mwalimu mwenyewe, alikuwa anaikanusha. Kinadharia na kiitikadi
Mwalimu hakukubaliana kabisa na dhana ya mapambano ya kitabaka.
Hata hivyo ibara ya 50 ya Mwongozo inaenda mbali zaidi kwa kueleza
kwamba:
Kuielewa vema jamii ya Tanzania ya leo kunataka
uchambuzi wa hali ya juu pia. Uchambuzi huu
ukiwezeshe Chama kuielewa migongano ya maslahi ya
tabaka ambayo imejitokeza nchini. Migongano hii ina
mizizi katika mgongano wa msingi kati ya Ujamaa na
ubepari, kati ya maslahi ya wakulima na wafanyakazi
kwa upande mmoja, na ya ubinafsi, ubwanyenye na
ubepari ambao umekuwa ukijengeka tangu Azimio la
Arusha kwa upande mwingine.
137
138
MIONGOZO MIWILI
MIONGOZO MIWILI
139
Marejeo
Mapolu, Henry. (mh.), (1976), Workers and Management, Dar es Salaam,
Tanzania Publishing House.
Shivji, Issa G., (1970), Tanzania: The Silent Class Struggle (Cheche 1970)
na kuchapishwa tena katika Issa G. Shivji (mh.) na wengine: The
Silent Class Struggle, (1972), Tanzania Publishing House.
140
MIONGOZO MIWILI