Professional Documents
Culture Documents
WIZARA YA AFYA
MWONGOZO WA KUUSHUGHULISHA
MWILI DHIDI YA TABIABWETE
TANZANIA 2022
OKTOBA 2021
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA
MWONGOZO WA KUUSHUGHULISHA
MWILI DHIDI YA TABIABWETE
TANZANIA 2022
OKTOBA 2021
MWONGOZO WA
KUUSHUGHULISHA MWILI
NA KUEPUKA TABIABWETE
Mwongozo Wa ushuhulishaji mwil na kuepuka
ii tabibwete Tanzania 2022
i. Dibaji
Mwongozo huu wa kuushughulisha mwili na kuepuka tabiabwete ambao unatokana na
mwongozo wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wa mwaka 2020 unakusudia kutoa
mapendekezo na miongozo ya kuushughulisha mwili na mazoezi hatimae kujenga afya kwa
makundi tafaouti yakiwemo watoto, vijana, watuwazima, wazee, walemavu, wajawazito, na
wenye maradhi sugu yasiyoambukiza. Mwongozo huu unaeleza namna ya kuushughulisha
mwili, muda unaotakiwa, kiwango sahihi na kipi kifanyike kwa rika lipi. Mwongozo pia
unaelezea kinachohitajika ili kuleta faida za kiafya na kupunguza athari zitokanazo na
madhara ya kutoushughulisha mwili.
Wizara ya afya maendeleo ya jamii, wazee jinsia na watoto inapongeza kitengo chake cha
maradhi yasiyombukiza kwa kushirikiana na wadau sekta binafsi, na wizara mbalimbali kwa
namana moja ama nyingine zina husika na ushuhulishaji mwili aidha kisera ama kimuondo
mbinu kwa juhudi za kufanikisha uwepo wa mwongozo huu uliotoa mapendekezo muhimu ya
kiafya kwa watu warika tofauti kuanzia miaka 5 hadi 64 na zaidi, bila kujali tofauti ya jinsia,
utamaduni, au hali ya kiuchumi, pamoja na wale wenye maradhi sugu au ulemavu, wajawazito
na waliojifungua. Hawa wote wanapaswa kufuata mapendekezo haya kadiri inavyowezekana.
Pia shukrani ziwaendee Muchi Juma Ameir, wa Idara ya miundombinu na mipango miji
na vijiji Wiziara ya Ardhi na Maendeleo ya makazi Zanzibar, Imelda Mwaluko kutoka
wizara ya elimu sayansi na teknolojia, Dr. Bakari Salimu TAMISEMI, Eliufoo A. Nyambi
kutoka wizara ya habari sanaa utamaduni na michezo, Elysa P. Haji wizara ya habari
utamaduni vijana na michezo Zanzibar na Yahya Said wizara ya ujenzi na usafirishaji.
Shukrani pia ziwaendee wale waliotoa michango yao kutoka kwa taasisi binafsi na
Jumuiya mbali mbali zinazojihusisha na ufanyaji mazoezi kutoka pande zote za mbili
za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kama vile Mathew J. Shayo, Mkuu wa
kitengo cha fiziotherapia KCMC, Moshi, Amina Talib Ali, Katibu wa ZABEZA Zanzibar,
Abdulhakim Cosmas Chasama, Zanzibar Athlete Association (ZAA) na Zanzibar
National Sports Council, Salimu Abdullah Mbonde, Tanzania Jogging Association
(Tanzania Bara), Joel Senny, Cycling Association of Tanzania, Lugmaan K. Mbululo,
Fitness Instructors Association of Tanzania na Meja Mbuya kutoka UMMA WA
WAPANDA BAISKELI (UWABA).
Mwisho kabisa napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wale wote ambao hatukuwataja
ila jitihada zao ziliwezesha kufanikisha kukamilika kwa Muungozo huu wa kuushughulisha
Mwili dhidi ya Tabia Bwete.
Uwezo wa utendaji
kazi Inajumuisha ujenzi kama vile: kumbukumbu ya kufanya kazi,
(Executive function) kubadilika kwa utambuzi (pia huitwa kufikiria kubadilika) na udhibiti
wa vizuizi (ambayo ni pamoja na kujidhibiti) Inajumuisha ujengaji
kama: kumbukumbu ya kufanya kazi, kubadilika kwa utambuzi (pia
huitwa kufikiria kubadilika) na udhibiti wa vizuizi (ambayo ni pamoja
na kujidhibiti
Utimamu wa mwili Kipimo cha uwezo wa mwili kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi katika
(fitness) kufanya kazi fulani, kufanya mazoezi au michezo mbalimbali.
Inauhusisha pia afya bora na uwezo wa moyo, mfumo wa mishipa ya
damu na ule wa upumuaji kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi.
Transport domain
physical activity
Kiwango cha juu cha Kwa kiwango kamili, nguvu ya nguvu inahusu shughuli za mwili
mazoezi au ambazo hufanywa kwa 6.0 au METS zaidi. Kwa kiwango
kushughulisha mwili kinachohusiana na uwezo wa kibinafsi wa mtu, mazoezi ya nguvu ya
nguvu kawaida ni 7 au 8 kwa kiwango cha 0-10.
Vigorous-intensity
physical activity
Transport domain
physical activity
Kiwango cha juu cha Kwa kiwango kamili, nguvu ya nguvu inahusu shughuli za mwili
mazoezi au ambazo hufanywa kwa 6.0 au METS zaidi. Kwa kiwango
kushughulisha mwili kinachohusiana na uwezo wa kibinafsi wa mtu, mazoezi ya nguvu ya
nguvu kawaida ni 7 au 8 kwa kiwango cha 0-10.
Vigorous-intensity
physical activity
1.1 Muhtasari
Mwongozo huu unawalenga watunga sera katika ngazi mbalimbali, taasisi na sekta zote
zenye mchango wa kuimarisha afya ya jamii kama vile wizara za afya, wizara za elimu, vijana,
michezo, miundombinu, mipango miji, ustawi wa jamii pamoja na maofisa wa serikali wenye
dhamana ya kuendeleza mipango ya kitaifa ya kukabiliana na maradhi yasiyoambukiza. Lengo
ni kuhamasisha vitendo vya kuushughulisha mwili na kupunguza tabiabwete katika makundi
ya watu mbalimbali wanaofanya kazi serikalini, katika mashirika binafsi pamoja na watu wote
kwa ujumla.
Mwongozo huu umetoa mapendekezo muhimu ya kiafya kwa watu wa rika tofauti, kuanzia
miaka 5 hadi 64 na zaidi, bila kujali tofauti ya jinsia, utamaduni, au hali ya kiuchumi. Aidha, kwa
wale wenye maradhi sugu au ulemavu, wajawazito na waliojifungua wanapaswa kufuata
mapendekezo hayo kadiri inavyowezekana.
10
Mapendekez Miaka 5 - Miaka 18 - 64 65 + Wajawazito na waliojifungua Wenye maradhi sugu (Miaka Watoto na Watu wa zima na wazee
o 17 18 na zaidi) vijana wanaoishi na Ulemavu
wanaoishi na
Ulemavu
(miaka 5 – 17)
Kuushughulis Dakika Dakika 75 – 150 za uzito Dakika 75 – 150 za uzito Wajawazito na wanawake Dakika 75 – 150 za uzito Watoto na watu wazima wenye ulemavu
ha mwili 60 kila wa juu wa juu walio jifungua kama hawana wa juu vijana wenye wanshauriwa kuushughulisha
siku Dakika 150 – 300 za uzito Dakika 150 – 300 za uzito matatizo yeyoyte ya kiafya Dakika 150 – 300 za uzito ulemavu mwili mara kwa mara
wa wastani wa wastani wanashauriwa wa wastani wanashuriwa
kuushughulisha mwili. washughulish
e mwili mara
kwa mara
Mapendekez Dakika Dakika 150 – 300 za kasi Dakika 150 – 300 za kasi Angalau dakika 150 za kasi ya Dakika 150 – 300 za kasi Dakika Dakika 150 – 300 za kasi
o ya Aerobiki 60 kwa ya wastani AU ya wastani AU wastani kwa wiki ya wastani AU 150 – 300 ya wastani AU
siku za Dakika 75 – 150 za kasi ya Dakika 75 – 150 za kasi ya Dakika 75 – 150 za kasi ya za kasi ya Dakika 75 – 150 za kasi ya
kasi ya juu juu juu Vyote kwa pamoja wastani juu
wastan AU mchanganyiko sawa AU mchanganyiko sawa kwa wiki nzima AU AU mchanganyiko sawa
i wa kasi ya wastani na ya wa kasi ya wastani na ya AU mchanganyiko sawa Dakika 75 wa kasi ya wastani na ya
mpaka juu ya kuushughulisha juu ya kuushughulisha wa kasi ya wastani na ya – 150 za juu ya kuushughulisha
wa kasi mwili kwa wiki nzima mwili kwa wiki nzima juu ya kuushughulisha kasi ya mwili kwa wiki nzima
ya juu mwili kwa wiki nzima juu
AU
mchanga
nyiko
sawa wa
kasi ya
wastani
na ya juu
ya
kuushug
hulisha
mwili kwa
wiki
nzima
11
Mwongozo wa ushuhulishaji mwili na kuepuka tabibwete Tanzania 2022
Tabiabwete Punguza Punguza muda Punguza muda Punguza muda Punguza muda Punguza muda Punguza muda
12
muda unaotumia kubweteka unaotumia kubweteka unaotumia kubweteka unaotumia kubweteka unaotumia unaotumia kubweteka
unaotumi Kujishughulisha/kufan Kujishughulisha/kufan Kujishughulisha/kufan Kujishughulisha/kufan kubweteka Kujishughulisha/kufan
a ya mazoezi (hata yale ya mazoezi (hata yale ya mazoezi (hata yale ya mazoezi (hata yale hususani ya mazoezi (hata yale
kubwetek ya kasi/nguvu nyepesi) ya kasi/nguvu nyepesi) ya kasi/nguvu nyepesi) ya kasi/nguvu nyepesi) muda ya kasi/nguvu nyepesi)
a kama mbadala wa kama mbadala wa kama mbadala wa kama mbadala wa unaotumia kama mbadala wa
hususani kubweteka kuna faida kubweteka kuna faida kubweteka kuna faida kubweteka kuna faida kwenye skrini kubweteka kuna faida
muda nyingi za kiafya nyingi za kiafya nyingi za kiafya nyingi za kiafya za vifaa vya nyingi za kiafya
unaotumi Jaribu Jaribu Jaribu kieletronika, Jaribu
a kwenye kujishughulisha/kufan kujishughulisha/kufan kujishughulisha/kufan kama vile sim kujishughulisha/kufan
skrini za ya mazoezi ya kiwango ya mazoezi ya kiwango ya mazoezi ya kiwango una runinga ya mazoezi ya kiwango
vifaa vya kinachozidi kile kinachozidi kile kinachozidi kile kinachozidi kile
kieletronik kinachoshauriwa. Hii kinachoshauriwa. Hii kinachoshauriwa. Hii kinachoshauriwa. Hii
a, kama inaleta faida zaidi za inaleta faida zaidi za inaleta faida zaidi za inaleta faida zaidi za
vile sim kiafya mwilini kiafya mwilini kiafya mwilini kiafya mwilini
una
runinga
2.1 Usuli
Ndani ya miongo kadhaa iliyopita, tabia ya kuushughulisha mwili na mazoezi kwa wa
Tanzania, imekuwa ikipungua kwa kiasi kikubwa sana. Hii imeendana kwa karibu sana na
kuongezeka kwa tatizo la uzito uliokithiri na maradhi sugu yasiyoambukiza(Kavishe et al.,
2015). Ushahidi wa kisayansi unaonyesha kwamba kushiriki katika mazoezi na
kuushughulisha mwili mara kwa mara kunasaidia katika kuboresha afya na kujikinga na
maradhi mbalimbali (Lee et al., 2012).
Kwa zaidi ya miezi sita, Tanzania kupitia wizara zake zinazohusika na Afya kwa kushirikiana na
wadau mbalimbali walitathimini sera, sheria, kanuni na miongozo iliyopo kuhusu
kujishughulisha, ufanyaji wa mazoezi, michezo, miundombinu, elimu na kadhalika. Tathimini
hiyo ilibaini changamoto mbalimbali zinazoikabili Tanzania katika ushughulishaji mwili
zikiwemo za kisera, kisheria na kimiundombinu. Mwongozo huu ni wa kwanza kuandaliwa
nchini kwa kufuata mchakato ambao unaakisi mwongozo wa mpango mkakati wa dunia wa
kupunguza kutoshughulisha mwili(Cooper, 2018). Mwongozo huu umeandaliwa na kamati ya
kitaalamu ya pamoja kati ya Zanzibar na Tanzania bara.
Kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2012 uliofanywa na Wizara ya Afya ya Tanzania (Mashili et
al., 2018), asilimia 26 ya Watanzania hawashughulishi miili yao ipasavyo, asilimia 30 ya watu
wazima wana uzito mkubwa, asilimia 9 wana ugonjwa wa kisukari na asilimia 26 wana
shinikizo la damu. Kwa upande wa Zanzibar, asilimia 3.7 walikua na ugonjwa wa kisukari,
asilimia 33 walikua na ugonjwa wa shinikizo la damu, asilimia 18 walionekana
hawaishuhgulishi miili yao na asilimia 14.3 walibainika na uzito uliokithiri.
Tafiti za hivi karibuni pia zimeonesha kuongezeka kwa tatizo la shinikizo la damu kwa asilimia
5, pamoja na tatizo la kuongezeka kwa uzito mkubwa kwa watoto wa shule.
Hata hivyo, inaaminika kuwa aina nyingine za kuushughulisha mwili mijini na vijijini
zimedorora kutokana na maendeleo ya teknolojia na ongezeko la vyombo vya usafiri karibu
na jamii. Hali hizo kwa pamoja zimechochea uanzishwaji wa mwongozo wa kuushughulisha
mwili. Lengo ni kukabiliana na ongezeko la uzito uliokithiri na kupunguza maradhi
sugu(Mashili et al., 2018). Kuushughulisha mwili mara kwa mara kunapunguza hatari ya
kupata maradhi sugu na kuimarisha afya kwa ujumla. Kuushughulisha mwili inajumuisha
sayansi na sanaa katika kuzuia maradhi, kurefusha maisha na kuimarisha afya ya jamii kupitia
juhudi za pamoja zinazounganisha jamii, sekta za umma, sekta binafsi, mashirika mbalimbali
yanayosaidia jamii na wananchi.
Hivyo basi, Miongoni wa majukumu ya mwongozo huu itakuwa ni kutoa kipaumbele katika
kuzuia maradhi yatokanayo na athari za kutoushughulisha mwili na tabiabwete sambamba na
kuwahamasisha wananchi kukuza tabia ya kuushughulisha mwili kama kipengele cha msingi
cha afya na ustawi wa jamii katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha mwongozo
utasaidia kupunguza vikwazo vinavyowakabili wananchi hao kutoishughulisha miili yao.
afya, elimu, kazi, makaazi au afua za kijamii za kudhibiti maradhi katika kipindi chote
cha maisha.
iii. Maafisa wa serikali ambao wana jukumu la kuandaa mipango ya kitaifa, mkoa au
kupunguza tabiabwete.
iv. Watu wanaofanya kazi katika mashirika yasiyo ya kiserikali, mashirika ya elimu na
v. Watu wanaofanya kazi katika huduma za afya na wale wanaotoa ushauri na miongozo
juu ya afya kwa jamii na familia kama vile wauguzi, wahadhiri wa vyuo vikuu au
mwongozo huu, yanapaswa kutumiwa kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa huduma za afya,
Vitendo vya kuushughulisha mwili vina athari zake zikiwemo majeraha na ajali. Watoto, vijana
na wajawazito wako katika hatari zaidi ya kupata madhara kwani wao wameonekana zaidi
kushiriki vitendo vya kuushughulisha mwili pasi na kuzingatia miongozo ya kitaalamu ikiwemo
kukosa mbinu na ujuzi sahihi na udhaifu wa misuli. Majeraha na ajali nyingi zinazotokana na
3.1 Methodolojia
Mchakato wa kuandaa mwongozo huu ulianza kwa kuunda kamati ya pamoja ya Zanzibar na
Tanzania bara. Kamati hiyo, ilizishirikisha sekta mbalimbali kutoka Zanzibar na Tanzania Bara
kupitia mradi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoitwa Global Recap Programme. Kamati
ilikuwa na jukumu la kupitia sera, sheria, miongozo, kanuni na machapisho ya kisayansi.
Hatua za kupokea mwongozo wa kidunia juu ya ushaghulishaji mwili dhidi ya tabiabwete
zilipitia utaratibu ufuatao.
ii. Uchambuzi wa hali halisi juu ya sera, sheria, kanuni na miongozo iliyopo juu ya
kuushughulisha mwili kutoka sekta mbalimbali ulifanyika. Uchambuzi huo ulibaini
kuwepo kwa shughuli mbalimbali za kuushughulisha mwili lakini pia uliibua
changamoto ambazo zinaweza kuwa ni vikwazo katika utekelezaji wa mwongozo huo.
iv. Kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupitia rasimu ya mwongozo na kutoa maoni.
Hatua hii ilifanyika kupitia mikutano ya pamoja ya kawaida na kwa njia ya kimtandao
ambapo ushauri na maelekezo mbalimbali yaliafikiwa.
.
3.2 Umuhimu wa Mwongozo huu
Wizara ya Afya ya Tanzania bara na Zanzibar kwa pamoja zimeweka mwongozo imara wa
taifa unaoeleweka kirahisi na kutafasiriwa kutoka kwenye lugha ngumu ya kisayansi mpaka
kuja kwenye lugha nyepesi itakayo eleweka kwa urahisi. Katika kila sura, kwenye
mapendekezo ya miongozo muhimu imefafanuliwa kirahisi sana ili mtu yeyote iwe rahisi mno
kuelewa.
Mapendekezo katika mwongozo huu yamewekwa kwa mujibu wa makundi rika na tabia
(kuushughulisha mwili na tabiabwete). Kwa kila pendekezo lililotolewa kwa kila kundi rika,
maelezo mafupi yanayoeleza faida za kiafya zitokanazo na kuushughulisha mwili na athari za
kubweteka zimeelezwa. Maelezo ya kina yametolewa kwaajili ya kufafanua ni namna gani
mapendekezo hayo yanaweza kufikiwa salama na kundi rika linalolengwa. Kuweka ufahamu
mkubwa kupitia mwongozo huu, waandishi wameweka majedwali matatu yenye umuhimu
mkubwa sana juu ya dhana nzima ya ushuhulishaji mwili na maana ya ufanyaji wa mazoezi,
usalama wa mazoezi, uzito, aina ya shuhuli na mazoezi. (jedwali 1-3)
Jedwali 1
Kikoa Aina
Asili ya Kazi Shuhuli za kikazi: zinahusisha kazi za kutumia
mikono, kutembea, kusimama wima, kubeba na
kunyanyua vitu
Kazi za Nyumbani Kazi za nyumbani, kusafisha na kulima bustani,
kumuhudumia mtoto, kwenda kununua bidhaa
sokoni, kupika na kufua nguo.
usafiri na vyombo vya usafiri Sababu yeyote ya kwenda mahali; kutembea,
kuendesha basikeli, kupanda na kushuka ngazi,
kutumia usafiri wa umma, kusimama ukiwa kwenye
chombo cha usafiri
Muda wa burdani Shuguli zozote za burdani: Michezo, mazoezi, kazi
za kujitolea,
Aina za Mazoezi
Jedwali 3
Uwanda wa ushughulishaji mwili: Aina, mara ngapi (siku, wiki) Muda na Uzito
Maelezo Nuhimu
Kwa Watoto na vijana, kwa kiasi kikubwa tabiabwete zinahusishwa na madhara ya kiafya
yafuatayo: ongezeko la mafuta mwilini; afya dhaifu ya ufanyakazi wa moyo, udhaifu wa
utimamu wa mwili, udhaifu wa tabia ya kushirikiana; kulala kwa muda mfupi.
Zingatia:
Inapendekezwa kufanya vitendo vya kuongeza nguvu misuli kwa kiwango cha kati au zaidi
ambavyo vitajumuisha makundi yote ya misuli mikuu angalau siku mbili kwa wiki kama vile
“push ups”, “pull ups”, kulima, kupanda ngazi n.k.
Dondoo za kiafya:
Watu wanatakiwa kuushughulisha mwili kwa kufanya vitendo vya kuimarisha upumuaji
kwa kiwango cha kati kwa zaidi ya dakika 300 au kwa kufanya vitendo vya kiwango cha
juu kwa zaidi ya dakika 150 ili kuimarisha upumuaji au kufanya shughuli mchanganyiko
zinazowiana kwa wiki nzima.
Maelezo muhimu:
Kuushughulisha mwili ni bora kuliko kubweteka
Iwapo watu wazima hawatofikia kiwango cha kuushughulisha mwili
Madhara ya kubweteka
Kwa watu wazima, kiwango kikubwa cha tabiabwete kinahusisha madhara ya kiafya
yafuatayo: kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa ya moyo, shinikizo la damu, saratani na
kisukari.
Zingatia
Punguza muda unaotumia kubweteka, hasa muda wa kutazama televisheni.
Badili tabia
Shughulisha mwili kama mbadala wa kubweteka kwa kiwango chochote kwa kufanya
shughuli nyepesi za mwili.
Ili kupunguza athari mbaya za kiafya zinazotokana na tabiabwete, inapendekezwa watu
wazima washughulishe mwili kwa kiwango cha kati hadi kiwango cha juu.
Wazee wanatakiwa kuushughulisha mwili angalau siku mbili kwa wiki kwa kufanya vitendo vya
kuongeza nguvu ya misuli kwa kiwango cha kati au zaidi. Vitendo hivi vinatakiwa kujumuisha
makundi makuu ya misuli kama misuli ya mikono, miguu, mapaja na kadhalika.
Kama sehemu ya kuushughulisha mwili kwa wiki, wazee wanatakiwa kufanya vitendo mbali
mbali vya kuushughulisha mwili, hii itapelekea wao kuhimili miili yao na kuipa nguvu kwa
kiwango cha kati au zaidi. Hii ifanywe kwa siku tatu or au zaidi kwa wiki ili kuwawezesha
wazee kuhimili miili yao na kuepuka kuanguka.
Dondoo za kiafya:
Wazee wanatakiwa kuushughulisha mwili kwa kufanya vitendo vya kuimarisha
upumuaji kwa kiwango cha kati kwa zaidi ya dakika 300 au kwa kufanya vitendo vya
kiwango cha juu kwa zaidi ya dakika 150 ili kuimarisha upumuaji au kufanya shughuli
zinazowiana kwa wiki nzima.
Wazee wanaweza kuongeza kufanya vitendo vya kuimarisha upumuaji kwa kiwango
cha kati kwa zaidi ya dakika 300; au kwa kufanya vitendo vya kiwango cha juu kwa
zaidi ya dakika 150 ili kuimarisha upumuaji; au kufanya shughuli mchanganyiko za
Madhara ya kubweteka
Kwa wazee, kiwango kikubwa cha tabiabwete kinahusishwa na madhara ya kiafya yafuatayo:
kuongeza vifo vitokanavyo na maradhi ya moyo, shinikizo la damu, saratani na kisukari.
Zingatia
Punguza muda unaotumia kubwetekaWazee wanapaswa kupunguza muda wa
kubweteka. Tumia muda unaojibweteka kwa kuushughulisha mwili kwa kiwango
chochote ikiwemo shughuli nyepesi nyepesi za mwili ambazo huleta faida za kiafya.
badili tabia
Shughulisha mwili kama mbadala wa tabiabwete kwa kiwango chochote ikiwemo
kuushughulisha mwili kwa kufanya vitendo vyepesi. Ili kupunguza athari mbaya za
kiafya zitokanazo na tabiabwete, inapendekezwa wazee kuushughulisha mwili kwa
kiwango cha kati hadi kiwango cha juu.
Faida hizi ni kwa mama na mtoto akiwa bado tumboni na baada ya kuzaliwa:
Kupunguza uwezekano wa kupata kifafa cha mimba, kisukari cha ujauzito, shinikizo la
damu la ujauzito, kuongezeka uzito wakati wa ujauzito, pia kuzuia tatizo la sonona
baada ya kujifungua
Kupunguza uwezekano wa kupata matatizo wakati wa kujifungua kama vile
kuchelewa kujifungua,
Kupunguza uwezekano wa kuzaa watoto njiti, watoto wenye uzito mdogo au mkubwa
kupindukia, pia kupunguza uwezekano wa mtoto kufia tumboni
Dondoo za afya
maelezo muhimu
Kwa wale wanaoishi na saratani, kuushughulisha mwili na kufanya mazoezi mara kwa
mara, husaidia kuzuia vifo vinavyosababishwa na saratani, magonjwa mengine
pamoja na kuzuia kujirudia na kuendelea kwa saratani
Kwa wale wanaoishi na tatizo la shinikizo la damu na ugonjwa wa kisukari,
kuushughulisha mwili na kufanya mazoezi mara kwa mara, husaidia kuzuia vifo
vitokanavyo na magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, kupunguza shinikizo la damu,
kuzuia kuendelea vibaya kwa ugonjwa na kudumisha ubora wa maisha kwa ujumla.
Kwa wale wanaoishi na virusi vya UKIMWI, kuushughulisha mwili na mazoezi husaidia
kudumisha utimamu wa mwili na kuzuia msongo wa mawazo.
Watu wazima wanaoishi na magonjwa sugu wanashauriwa kuendelea kujishughulisha
au kufanya mazoezi mara kwa mara
Dondoo za afya
Isipokatazwa, watu wazima na wazee wenye magonjwa haya sugu wanaweza
kuongeza mazoezi ya mwili kwa kiwango cha wastani kwa zaidi ya dakika 300; au
kufanya zaidi ya dakika 150 ya mazoezi ya mwili ya kiwango cha juu; au
mchanganyiko sawa wa shughuli na mazoezi ya kiwango cha wastani na cha juu
kwa wiki nzima ili kupata faida za ziada za kiafya
• Kama hawawezi kufikia mapendekezo hapo juu, watu wazima walio na hali hizi
sugu wanapaswa kulenga kushiriki katika mazoezi ya mwili kulingana na uwezo
wao.
• Watu wazima walio na magonjwa haya sugu wanapaswa kuanza kwa kufanya
mazoezi kidogo ya mwili na polepole kuongeza kiwango na muda wa mazoezi
• Watu wazima walio na magonjwa haya sugu wanashauriwa kuwasiliana na
mtaalam wa mazoezi ya mwili au wataalamu wa afya kwa ushauri juu ya aina na
kiwango cha shughuli na mazoezi yanayoendana na: mahitaji yao, uwezo,
mapungufu ya kiutendaji / shida, dawa, na mpangilio wa jumla wa matibabu.
• Usaidizi wa kitaalamu kuhusu mazoezi kwa ujumla hauhitajiki kwa watu wasio na
katazo la kiafya kabla ya kuanza mazoezi ya mwili yaliyo mepesi ambayo hayazidi
kutembea kwa haraka na shughuli za kawaida za maisha
Madhara ya kubweteka
Kwa watu wazima, pamoja na waathirika wa saratani na watu wanaoishi na shinikizo la damu,
aina ya 2 ya ugonjwa wa kisukari na wale wanaoishi na virusi vya UKIMWI, kiwango cha juu cha
tabia ya kukaa na kutokujishughulisha huhusishwa na kuongezeka kwa magonjwa, pamoja na
vifo vinavyosababishwa na maradhi hayo.
Kwa waathirika wa saratani, na watu wazima wanaoishi na shinikizo la damu, aina ya pili ya
ugonjwa wa kisukari na virusi vya ukimwi (VVU) inashauriwa kuwa:
Zingatia
Punguza muda wa kubweteka
Wanashauriwa kujiepusha na muda wa kubweteka ili kupunguza athari zitokanazo na
maradhi.
Badili tabia
Fanya shughuli yeyote ya uzito wa wastani ama wachini. Pia inapendekezwa zaidi pale
wanakuwa na nafasi wafanye shuguli ama mazoezi ya nguvu na kasi zaidi ili kupungunza
athari zitokanazo na maradhi walionayo.
Kuushughulisha mwili na kufanya mazoezi ya kasi kwa kiwango cha juu, pamoja na yale ya
kuimarisha misuli na mfupa vinapaswa kufanyika kwa angalau siku 3 kwa wiki.
maelezo muhimu
Badili tabia
Watoto na vijana wanaoishi na ulemavu wanapaswa kupunguza muda unaotumika
kukaa tu na kutokujishughulisha, hususani muda wa kutizama runinga, simu na
kompyuta
,
Watu wazima wote wanaoishi na ulemavu wajishughulishe na kufanya mazoezi mara kwa
mara
Watu wazima wanaoishi na ulemavu wanapaswa kutumia angalau dakika 150-300 ya mazoezi
ya mwili ya kiwango cha wastani; au angalau dakika 75-150 ya mazoezi ya mwili ya kiwango
cha juu; au mchanganyiko sawa wa shughuli za wastani na zile za nguvu kwa wiki nzima kwa
faida nyingi za kiafya.
Kama sehemu yao ya ratiba ya wiki katika kuushuhulisha mwili, wazee wenye ulemavu
wanashauriwa kufanya shughuli mchanganyiko Pamoja na mazoezi ya kuuwezesha
mwili kujihimili na kuimarisha misuli kwa uzito wa wastani mpaka wa juu kwa siku 3
ndani ya wiki. Hii itaboresha uhimili wa mwili na kuzuia kuanguka.
Dondoo za afya:
Zaidi ya dakika 300 za kasi ya wastani ya mazoezi ya kiaerobiki na zaidi ya dakika 150
za kasi ya juu ya mazoezi ya aerobiki ama muungano wa kasi zote mbili kwa wiki nzima.
Maelezo muhimu:
• Kushughulisha mwili na kufanya mazoezi ni bora kuliko kutokufanya
• Ikiwa watu wazima wanaoishi na ulemavu hawatimizi mapendekezo haya,
kufanya mazoezi ya mwili kutaleta faida kwa afya.
• Watu wazima wanaoishi na ulemavu wanapaswa kuanza kwa kufanya
mazoezi kidogo ya mwili, na polepole kuongeza marudio, nguvu na muda
kadri siku zinavyokwenda.
• Hakuna hatari kubwa kwa watu wazima wanaoishi na ulemavu wanaofanya
shughuli za mwili zinazoendana na kiwango cha shughuli za zao, hali zao
za kiafya na utendaji mwili; na pale ambapo faida zinaongezeka kuliko
athari.
• Watu wazima wanaoishi na ulemavu wanaweza kuhitaji kushauriana na
mtaalamu wa huduma ya afya au mazoezi mengine ya mwili, na mtaalam
wa ulemavu ili kusaidia kujua aina na kiwango cha shughuli zinazofaa
kwao.
Madhara ya kubweteka
Kwa watu wazima, kiwango cha juu cha tabia ya kukaa huhusishwa na kuongezeka kwa
magonjwa pamoja na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo. Magonjwa hayo ni pamoja na
matatizo ya moyo na mishipa ya damu, saratani, aina ya 2 ya ugonjwa wa kisukari,
kuongezeka kwa shinikizo la damu na magonjwa yanayosababishwa na vimelea kama vile
UKIMWI na KORONA.
Badili tabia:
• Watu wazima wanaoishi na ulemavu wanapaswa kupunguza muda unaotumika
kubweteka. Wanashauriwa kuutumia muda huo kufanya shughuli za mwili za
kiwango chochote (hata kama ni kiwango kidogo sana) hii huleta faida za
kiafya.
• Kusaidia kupunguza athari mbaya za viwango vya juu vya tabiabwete kwa afya,
watu wazima wanaoishi na ulemavu wanapaswa kufanya zaidi mazoezi kwa
viwango vilivyopendekezwa vya mazoezi ya mwili ya wastani na ya nguvu.
Wazo kuu katika mwongozo huu, ni kwamba tabia ya kuushughulisha mwili kwa miezi na
miaka kadhaa inatoa faida za kiafya za muda mrefu. Mapendekezo yaliyomo katika
mwongozo huu ni muhimu kwa sababu kuushughulisha mwili kuna tija kwa afya ya
Watanzania ambapo tabia zilizojengeka za kutojishughulisha kimwili kunawaweka katika
hatari za kiafya zisizo za lazima. Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kudhibiti Maradhi
Yasiyoambukiza (2016-2020) umeweka malengo ya kuongeza kiwango cha kuushughulisha
mwili nchini Tanzania. Ingawa taarifa zinaonyesha, kuna mafanikio kadhaa katika viwango vya
kuushughulisha mwili kati ya watu wazima wa Kitanzania, ni asilimia 36 tu ya wanaume na
wanawake walioripotiwa kufanya shughuli za kutosha kufikia kiwango husika cha MET (Utafiti
wa STEPS 2012).
Tabia ya kushughilisha mwili, hasusani kwa vitendo vya kiaerobi, kwa watoto na vijana yana
matokeo chanya ya kiafya haswa kwenye mfumo wa moyo, mishipa yad amu na mzunguko
Kuushughulisha mwili huimarisha mifumo yote ya mwili ambayo hupelekea kupata faida ya
muda mfupi na mrefu ya kupunguza maradhi ya moyo na mishipa ya damu.
Kulingana na ushahidi huu, ilikubaliwa kwamba viwango vya juu vya wastani hadi viwango vya
juu vya kuushughulisha mwili vinavyotumia nguvu nyingi inapaswa kushauriwa kwa wale
watu ambao wana tabia ya kujibweteka zaidi kwa kiwango cha juu ili kupunguza athari
zitokanazo na tabia hii.
Tafiti juu ya uhusiano uliopo kati ya tabiabwete na athari zake kiafya ni eneo jipya katika afya
ya jamii, lakini tabia hili imekuwa kwa kiwango kikubwa sana miaka hii ya hivi karibuni na
linachangia kwa kiasi kikubwa sana kwenye sababu ya vifo haswa vitokanayo na maradhi
yasio ambukiza.
Ushahidi unaonyesha kuwa viwango vya juu vya kuushughulisha mwili baada ya kugundulika
kuwa na saratani inapunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo hasa saratani ya matiti,
saratani ya utumbo mpana na saratani ya tezi dume.
Kuushughulisha mwili kwa watu wanaoishi na VVU unaimarisha mfumo wao wa moyo na
mapafu.
Kuushughulisha mwili ni bora kuliko kubweteka. Iwapo watu hawajafikia kiwango cha
kuushughulisha mwili kinachopendekezwa, kuushughulisha mwili kwa kiasi fulani ni muhimu
kwa afya zao. Hivyo wanapaswa kuanza hatua kwa hatua kuushughulisha mwili na kuongeza
taratibu idadi, kiwango na muda.
Katika miongo kadhaa iliyopita tabia za kuushughulisha mwili miongoni mwa watanzania
yamepungua. Ambapo imeonekana kuna ungozeko la uzito uliokidhiri pamoja na maradhi
sugu. [utafiti wa STEPS 2012 [1]. Kuwa na tabia na utaratibu wa kushughulilisha mwili
kunapunguza hatari ya kupata maradhi sugu na kunachngia kuimarisha afya ya mwili.
Mahitaji ya utafiti
Kutokana na upembuzi yakinifu uliofanyika imebainika kuwa bado kuna mapungufu kuhusu
upatikanaji wa taarifa za kisayansi za kitaifa ili kuweza kupata uhalali wa mapendekezo
kwenye muuongozo huu.
Tafiti zaidi zinahitajika kwenye eneo hili. Utafiti haswa utakao kuwa na misingi ya makundi
mbalimbali ya umri na matokeo ya kiafya juu ya tabia za kuushuhulish mwili dhidi ya
tabiabwete. Tafiti pia zijikite kwenye makundi ya kuushuhulisha mwili, ujumbe sahihi kwa
jamii kwenye maeneo juu yalio na utata na chanagamoto na kuleta matokeo ya kuimarisha
misingi na mikakati katika kutengeneza miongozo ya kutatua changamoto hizo. Kwa mujibu
wa utafiti wa kisera uliofanyika ambao ni sehemu ya mchakato wa muongozo huu,
umeonesha mapungufu na vikwazo vya watu kushiriki katika shughuli za kimazoezi haswa
kwenye mipango miji, barabara, usalama, na maeneo ya kazi.
Tafiti zaidi zinahitaji zinazohusiana na shughuli zote za mazoezi pamoja na kushulisha mwili.
Pia, kuandaliwa kwa miongozo na taarifa za kurahisisha jamii kuushughulisha mwili na
mazoezi
Hakuna mapitio hata moja, adha yalio chapishwa ama yasio chapishwa yana kinzana ama
yanatoa majibu ya moja kwa moja juu ya muoongozo huu. Utafiti wa kisera juu ya
kuushuhulisha mwili na mpango mkakati wa miongozo wa kuushuhulisha mwili (GAPPA)
uliofanyika unatoa muongozo wa kufanya marekebisho na mikakati ya usimamizi wa
muongozo huu. Uchambuzi utakao fuatia utatupa muongozo wa kina na kutuba dira iliyo bora
juu ya vikwazo vilivyo jitokeza kwenye utafiti wa kisera wa awali juu ya kuushughulisha mwili.
Licha ya kuwa na wingi wa data zinazoonesha ongezeko la watu kujishughulisha mwili bado
kunaongezeko za tabia za watu za kujibweteka. Tabia mambazo zinaleta madhara katika afya
Inaoneka kwamba bado kuna tafiti chache kuhusu ufanyaji wa mazoezi na kujishughulisha
mwili katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati, makundi ya watu wanaoishi na ulemavu,
maradhi suguna kaya masikini. Pia, Tafiti nyingi hazijafanywa kuonesha athari za kiafya
zinazopatika kulingana na kijamii, umri, jinsia, rangi, kabila, hali ya uchumi.
Elimu (dissemination)
Lengo la mwongozo wa kitaifa wa kuushughulisha mwili na kufanya mazoezi ni kuwapa
ufahamu au ushauri watunga sera, watekezaji wa mipango ya afya ya jamii, taasisi za elimu,
mahali pa kazi n.k., juu ya mapendekezo ya muda wa kuushughulisha mwili kila siku kwa
watoto, vijana, watu wazima na wazee, na mapendekezo juu ya kupunguza tabiabwete.
Walakini, kuandaa mwongozo huu pekee hakutakuwa na athari kwa jamii bila kusambazwa na
elimu kutolewa na utelezwaji wa mwongozo.
Mwongozo huu wa kitaifa ni sehemu ya msingi ya mifumo ya utendaji ili kuongeza viwango
vya kuushughulisha mwili katika jamii. Mwongozo huu utasaidia katika kupanga mikakati na
vipaumbele vya nchi na kutoa taarifa sahihi katika jamii kwa njia inayofaa.
1. Watunga sera ndani na nje ya sekta ya afya (pamoja na sekta za uchukuzi, mipango,
elimu, sehemu za kazi, michezo na burudani) ili kuongeza:
Hatua zinahitajika kwa mtu mmoja mmoja, makundi na jamii kusaidia Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kuwa wakakamavu. Mazoezi ya mwili yanahitaji kufanywa kwa usalama na
urahisi kwa kila mwananchi. Ili kuongeza viwango vya mazoezi ya mwili kwa ufanisi, mikakati
inayotegemea ushahidi uliothibitishwa na watafiti inapaswa kutumika.
Mapitio ya sayansi yaliyofanywa na Kikosi kazi jumuishi cha kupitia miongozo ya ufanyaji
mazoezi na kuushughulisha mwili umeonesha kuwa mikakati mingi inayotegemea ushahidi
inaweza kutumika kukuza na kuongeza kuushughulisha mwili. Mikakati mingine inajumuisha
Wadau mbalimbali watafaidika na nyenzo tofauti ili kuwasiliana kwa ufanisi, kuzingatia
yaliyomo, muundo, na njia za uwasilishaji kwa wahusika mbalimbali.
Kampeni za kitaifa juu ya kuushughulisha mwili huanzisha kaulimbiu ya kampeni (kwa mfano
"Kuwa na bidii" au "Songa Zaidi"), na uunda vipengee vya muundo au wahusika, ambayo
inaweza kujumuisha ujumbe maalum kwa hadhira tofauti (kama vile watoto wadogo, vijana,
watu wazima au watu wazima wakubwa, wasio na kazi sana, watu wanaoishi na ulemavu au
maradhi sugu). Ujumbe wa kampeni na rasilimali ambazo zimelengwa kwa vikundi maalum
vya idadi ya watu zinaweza kuwa na ufanisi zaidi kuliko ujumbe wa ujumla.
Kampeni za mawasiliano zinapaswa kuzingatia ufikiaji na ufanisi wa vituo vyote vya kijamii
(kama vile televisheni, redio, mabango, rasilimali zilizochapishwa) na vile vile njia za habari za
dijiti (tovuti, simu za rununu, Programu). Kutoa habari juu ya miongozo ya kitaifa katika aina
anuwai pia ni muhimu. Kwa mfano, njia mpya lakini inayozidi kawaida ya kuwasiliana na
miongozo ya shughuli za mwili ni kwa kutumia infographics au video fupi za michoro.
Hatahivyo, ili kufanikisha mabadiliko ya tabia endelevu, vitendo hivi lazima visaidiwe na sera
ambazo zinaunda mazingira ya kuunga mkono ambayo yanawezesha na kuhamasisha watu
kuwa na bidii, pamoja na kuongezeka kwa fursa za kijamii, mwafaka za watu kushiriki katika
mazoezi ya mwili. Sera na mipango lazima izingatie na kubadilishwa kulingana na muktadha
wa eneo hilo, kwa kuzingatia mfumo wa afya na taasisi mbalimbali zenye nia, au fursa ya
kusaidia, kukuza shughuli za mazoezi ya mwili.
Ufuatiliaji na Tathmini
Tathimini itafanyika kwa kutumia dododso la ushungulishaji wa mwili na mazoezi kila baada
ya miaka mitano
Maboresho
kupitia na kuimarisha Mwongozo huu utapitiwa na kufanyiwa maboresho kila baada ya miaka
mitano, na ikitokea mabadiliko katika mifumo ya kiditali inahusisha ufanyaji wa mazoezi na
tabia ya kujibweteka inaweza kupitiwa kabla ya miaka iliyotajwa.