Professional Documents
Culture Documents
wa Madereva
Wanafunzi
ii
Yaliyomo
Dibaji ................................................................................. 1
Utanguluzi ......................................................................... 3
Mambo gani yanayomfanya dereva kuwa mzuri?............... 5
Jukumu lako ktika mfumo wa barabara ............................. 6
Sheria na madereva wanafunzi.......................................... 6
Kujua kuhusu gari lako na jinsi kulidumisha...................... 7
Vijenzi vya msingi........................................................................8
Kulikagua gari ........................................................................... 12
Ushauri kwa madereva wa magari yenye nguvu ya magurudumu ya
mbele na ya nyuma ................................................................... 14
Kuwa katika hali nzuri ya kuendesha............................... 14
Uwezo wa kuona ....................................................................... 14
Uchovu..................................................................................... 15
Kunywa pombe ......................................................................... 16
Kutumia dawa na kuendesha....................................................... 17
Hali na ugonjwa......................................................................... 17
Jinsi ya kuanza, kunyonga, kusimama na kurudi nyuma.. 18
Utangulizi ................................................................................. 18
Kuwasha injini........................................................................... 20
Kunyonga ................................................................................. 21
Kuondoka ................................................................................. 22
Kubadili gia............................................................................... 22
Kuendelea kulidhibiti gari............................................................ 23
Kufunga breki ........................................................................... 24
Kurudi nyuma ........................................................................... 25
Kuliacha gari ............................................................................. 26
Uendeshaji salama barabarani......................................... 27
Kuendesha barabarani................................................................ 27
Mwendo.................................................................................... 31
Kulipita gari jingine .................................................................... 32
Makutano ................................................................................. 36
Ushauri maalumu kwa madereva kwenye sehemu zenye mzunguko. 41
Uendeshaji wa usiku au kwenye hali mbaya ya hewa ..................... 42
Kurudi nyuma ........................................................................... 43
Kuwajali watembea kwa miguu na watumiaji wengine wa barabara
wanaoweza kuathirika ................................................................ 44
Kurudi ulikotoka ........................................................................ 46
Reli Inayokatisha ....................................................................... 47
iii
Kuegesha......................................................................... 48
Uegeshaji wa 900 ....................................................................... 49
Uegeshaji sambamba ................................................................. 50
Uegeshaji wa mshazari ............................................................... 50
Kuegesha kilimani...................................................................... 51
Alama za barabarani ........................................................ 52
Jaribio la udereva ............................................................ 53
Maombi ya kufanya jaribio la udereva .......................................... 53
Kujiandaa kwa jaribio................................................................. 53
Yaliyomo kwenye jaribio ............................................................. 54
Jaribio ...................................................................................... 54
Baada ya jaribio ........................................................................ 56
Kuharibika ....................................................................... 57
Iwapo kuna ajali.............................................................. 58
Muhtasari wa mafunzo ya madereva wa magari madogo
(Leseni za Daraja B & D) ................................................. 59
iv
Dibaji
1
2
Utanguluzi
Seti hii yenye stadi mbalimbali ngumu si kitu unachoweza kujifunza kwa
urahisi kutoka kwa marafiki na ndugu – lazima upate maelezo ya
kitaalamu kutoka kwenye shule ya udereva yenye kibali.
3
“Dereva” maana yake ni mtu yeyote anayeendesha gari au vitu vingine
(pamoja na baiskeli) au anayechunga wanyama barabarani
4
Mambo gani yanayomfanya dereva kuwa mzuri?
5
Jukumu lako ktika mfumo wa barabara
6
kibali cha mafunzo ya udereva. Lazima uonyeshe kasoro zozote au
ulemavu mwilini wakati unaomba leseni ya dereva mwanafunzi.
“Kitabu cha Mwongozo” kwa ajili ya gari lako ni chanzo kizuri sana cha
ushauri wa namna ya kulitumia gari na kulifanya lidumu katika hali nzuri.
Fuata maelekezo haya kwa makini. Kumbuka kuwa gari linalotunzwa
7
vizuri halitakugharimu sana kulitumia, halitaharibika mara kwa mara na
litakuwa salama.
Mfumo wa upozaji. Injini hupata moto sana kwa hiyo lazima kuwe na
mfumo wa kuipoza. Mfumo huu kwa kawaida hufanya kazi kwa kupeleka
maji (kipozeo) kuzunguka injini kupitia mipira na mirija. Angalia kiasi cha
maji kwenye tangi kila wiki na angalia uvujaji kwenye mirija ya maji.
Iwapo mshale kwenye kipimo unaonyesha kuwa joto la injini ni la juu
sana lazima uzime injini kuepuka uharibifu. Maji yatakuwa moto sana na
yanaweza kukuunguza – hivyo, kama unahitaji kujaza tena, subiri hadi
injini ipoe.
1 3 5 1 3 R 1 3
Nyutro Nyutro
Mpango wa pedeli 2 4 2 4 R 2 4
R
Mfumo wa otomatiki:
Mpango wa pedeli
Wenzo wa kichaguzi
Kuegesha
Kurudi nyuma
Nyutro
Kuendesha
2 Breki
L Kichapuzi
9
Breki. Gari lina mfumo wa breki ambao unatumia mafuta ya haidroliki
(kilainishi/mafuta ya breki) kuendesha pedi ambazo hubana
magurudumu na kuyapunguza mwendo. Pedi hizi huweza kuchakaa na
huhitaji kubadilishwa kila baada ya wakati fulani. Breki hufanya kazi kwa
kukanyaga pedeli za breki. Ni muhimu kuangalia kiasi cha
kilainishi/mafuta ya breki kwenye akiba kila wiki. Daima tumia
kilainishi/mafuta halisi ya breki, si mengine ya bei rahisi yasiyo halisi. Ni
muhimu sana kwa usalama wako na kwa usalama wa watumiaji wengine
wa barabara breki kuwa katika hali nzuri, iwapo hazifanyi kazi vizuri na
kwa ubora (gari huenda upande, breki hupiga kelele, au pedeli za breki
kuwa laini na kubonyea) lazima ziangaliwe haraka. Matengenezo ya
mfumo wa breki yafanywe na karakana yenye ujuzi.
Taa za mbele
Indiketa ya kushoto Indiketa ya kulia
80 100 P
FUEL TEMP
H
60 120 F
R
40 140 N
160 D
20 2
0 180 L
km/h E C
Kuendesha
Kipimia joto
Kipimia mwendo
Mahali pa Kipimia Mahali pa
taa ya tahadhari mafuta taa ya tahadhari
Kulikagua gari
Ni muhimu gari lako kufanyiwa matengenezo ya kawaida ya mara kwa
mara na karakana yenye ujuzi, lakini vitu vinaweza kuharibika baada na
kabla ya matengenezo mengine, hivyo ni lazima uendelee kulikagua
mwenyewe.
12
Vitu ambavyo unapaswa kuvichukua kwenye gari:
• Leseni ya biashara, waraka wa usajili wa gari, stika ya leseni ya
barabara, na stika ya bima (vibandikwe ndani kwenye kioo cha
mbele)
• Kisanduku cha huduma ya kwanza
• Tairi la akiba- lijazwe upepo sahihi
• Spana ya gurudumu
• Vibao viwili vya tahadhari vya Pembetatu vyekundu (hivi huhitajika
kisheria)
• Tochi.
13
Iwapo unaendesha umbali mrefu kila siku, au gari lako limechakaa,
fanya uchunguzi wa yaliyoandikwa hapo juu mara kwa mara badala ya
mara moja kwa wiki.
Uwezo wa kuona
Taarifa nyingi anazohitaji dereva humfikia kupitia macho yake. Kwa hiyo
uwezo wa kuona vizuri ni muhimu kwa uendeshaji salama. Lazima uweze
kusoma kibao cha namba za gari kutoka umbali wa kiasi cha mita 20
katika mwanga mzuri wa mchana. Iwapo unahitaji kuvaa miwani (au
lenzi zilizobandikwa kwenye mboni) kuona, lazima uvivae wakati wote
14
unapoendesha. Wakati unaomba leseni ya udereva utatakiwa kuonyesha
cheti kinachoonyesha kuwa uwezo wako wa kuona uko katika viwango
vinavyotakiwa.
Vitu ambavyo moja kwa moja viko mbele yako vinaweza kuonekana kwa
uwazi zaidi, lakini uonaji wako wa pembeni kwa kawaida ni mzuri
kugundua mienendo ya eneo pana kuelekea kwako. Uonaji huu wa
pembeni ni muhimu, kwa sababu unahitaji kuona kitu chochote haraka
(magari, watembea kwa miguu) vinavyokuja kwako kutoka pembeni.
Wakati unaendesha kwa kasi hutaweza kutumia vioo vyako vya pembeni
kikamilifu. Hii inamaanisha kuwa utaikaribia hatari kubwa kabla
hujaweza kuigundua. Kitu kama hicho hutokea pindi ukinywa pombe –
vioo vyako vya pembeni hutiwa ukungu na kuwa vidogo.
Uchovu
Kuendesha kunaweza kukufanya ujisikie usingizi, na hili kwa kiasi
kikubwa hukuongezea hatari ya kupata ajali. Unaweza kuepuka usingizi
kwa kuhakikisha kuwa kuna hewa nzuri ndani ya gari, na umekaa
sehemu nzuri ya kuendeshea. Kitu chochote kinachosababisha ugumu
katika uendeshaji, mfano uchafu kwenye kioo cha mbele, vitakuchosha
kwenye safari ndefu.
15
Inashauriwa kuwa upumzike kwa dakika 30 kila baada ya saa 3 za
kuendesha. Epuka kuanza safari ndefu usiku sana au baada ya saa za
kazi. Usiendeshe kwa zaidi ya saa 9 kwa siku. Madereva wa magari ya
biashara lazima wafuate kanuni za saa za madereva.
Kunywa pombe
Kamwe usinywe pombe kabla ya kuendesha. Pombe hupunguza uwezo
wa mfumo wa akili yako, kupunguza utendaji wako, kuathiri uamuzi
wako wa mwendo unaofaa, umbali sahihi na hatari itakayotokea, na
kukupa hisia zisizo sahihi za kujiamini.
16
Pombe na hatari ya ajali
Hatari kubwa ya Watu wanaoathiriwa
ajali baada ya zaidi na pombe
kunywa pombe
Wanaoathirika
MARA 15 zaidi
KIKOMO Wanaoathirika
KISHERIA kidogo
MARA 5
Hatari ya ajali
bila pombe
0 10 50 80 100 150 200
Hali na ugonjwa
Usiendeshe wakati una hasira, ukiwa na furaha zaidi au kuchanganyikiwa
sana kuhusu jambo fulani. Usiendeshe kama hujisikii vizuri. Iwapo una
tatizo la kiafya litakalokufanya kuelekea kuzimia au kifafa, au kupata
ulemavu wa mwilini lazima umuulize daktari wako iwapo ni salama
kwako kuendelea kuendesha. Iwapo daktari wako atakuambia uache
kuendesha, ipeleke leseni yako Polisi. Fanya hivyo hivyo iwapo uwezo
wako wa kuona utaathirika na kuwa chini ya kiwango kinachotakiwa.
17
Jinsi ya kuanza, kunyonga, kusimama na kurudi
nyuma
Utangulizi
Kabla hujaliendea gari lako ili uendeshe ni muhimu kuwa na tabia ya
kupanga safari yako. Unajua kwa uhakika unakokwenda na namna ya
kufika kule? – Kama hujui, angalia kwenye ramani au pata ushauri
kutoka kwa mtu anayelijua eneo hilo. Unapopanga safari yako fikiria
kuhusu msongamano wa magari, matengenezo ya barabara, hali mbaya
ya barabara, au matatizo mengine.
Kuwasha injini
Kabla ya kuwasha injini, hakikisha kuwa breki ya mkono imewekwa na
kuwa gari haliko kwenye gia – Angali kuwa wenzo uko kwenye
“KUEGESHA” (kwa otomatiki) au NYUTRO ( kwa manyu gia boksi). Pia
angalia kuwa hakuna aliyesimama mbele au nyuma ya gari. Weka
ufunguo kwenye swichi ya kuwashia na iwashe (mahali penye ON) –
dashibodi itaanza kufanya kazi. Zungusha ufunguo wa kuwashia mahali
pa kuwashia na sikiliza sauti ya injini – mara ukishasikia injini imeanza
kuunguruma achia swichi (angalia Kitabu cha Mwongozo kwa ushauri
wowote maalumu wa kutumia pedeli ya kichapuzi wakati wa kuwasha).
Iwapo una gari lenye injini ya dizeli lazima usubiri taa ya indiketa ya
PLAGI INAYONG’AA (kwa kawaida ni ya rangi ya chungwa) lazima kabla
ya kunyonga ufunguo kutoka ON, hadi START.
20
Kunyonga
Mwazoni ni changamoto kufanya vitendo vichache mfano kupinda, na hili
litahitaji umakini wako mkubwa. Kwa kufanya mazoezi na baada ya
muda, utakuwa na uwezo wa kuliongoza gari kirahisi na kwa kujiamini.
Kuzungusha usukani kulia hulifanya gari lako lipinde kulia na kuzungusha
usukani kushoto hulifanya gari lako kupinda kushoto.
Kubadili gia
Maelekezo haya yametumika tu unapokuwa unatumia giaboksi ya
manyu. Kubadili gia bila shida inaweza ikakuchukua muda mrefu
kujifunza.
Kubadili gia (juu). Ili kuongeza mwendo wa gari bila ya kuongeza zaidi
mzunguko wa injini unahitaji kubadili gia. Isikilize injini na usikie wakati
inaanza kuzunguka zaidi; huu ni wakati wa kubadili gia. Hatua ni:
• Kanyaga pedeli ya klachi chini wakati unaachia kichapuzi - klachi
ikanyagwe kwa kiasi cha sekunde kabla ya kuachia kichapuzi (siri ya
kwanza ya kubadilisha gia vizuri).
• Sogeza sehemu ya gia kutoka ilipo hadi kwenye gia mpya (mwanzoni
wakati wa mafunzo hili hasa litahusisha kutoka gia ya kwanza kwenda
ya pili – kupitia nyutro)- usilazimishe mahali pa gia – uweze
kuhamisha taratibu kwenda mahali papya kwa nguvu za wastani.
22
• Iache pedeli ya klachi ipande polepole, na wakati huohuo (au muda
mfupi baadaye) polepole kanyaga pedeli ya kichapuzi kwenda chini
(siri ya pili ya ubadilishaji gia vizuri).
Kuwa makini zaidi kwenye barabara zisizo na lami, kwani matairi yako
yatakuwa yakikamata barabara kidogo, na kukufanya uwe na uwezekano
mkubwa wa kuteleza ikiwa utajaribu kwenda kwa kasi. Mwendo wako
uwe chini ya km 80kwa saa na nyonga usukani taratibu.
23
Kufunga breki
Iwapo unataka kupunguza mwendo wako fanya taratibu, ondoa mguu
wako kwenye kichapuzi. Hii itakufanya upunguze kasi yako. Wakati
unataka kupunguza mwendo haraka funga breki. Wakati mwendo
unapungua unatakiwa urudi kwenye gia za chini.
24
Umbali Halisi wa Kusimama
km 30 kwa saa
Umbali wa
mita 12 kufikiria
au urefu wa magari 3
Umbali wa kufunga
km 50 kwa saa breki
mita 23
au urefu wa magari 6
km 80 kwa saa
mita 53
au urefa wa magari 13
mita 73
Wastani wa urefu wa gari = mita 4 au urefu wa magari 18
Kurudi nyuma
Kurudi nyuma ni hatari zaidi ya kwenda mbele, hivyo usirudi nyuma zaidi
ya inavyotakiwa. Wakati unataka kurudi nyuma kwanza ingiza gia ya
kurudi nyuma – kamwe usifanye hivi mpaka gari lisimame kabisa. Kisha
weka mkono wako wa kulia kwenye usukani mahali ambapo ni sawa na
saa 6 kamili kwenye saa na geuza kichwa chako na sehemu ya juu ya
mwili wako kushoto. Hili litakuwezesha kuangalia kupitia begani kwako
na kupitia kwenye dirisha la mwisho-angalia kielelezo. Endesha polepole
wakati unarudi nyuma. Ikibidi dhibiti mwendo wako kwa kukanyaga
vizuri pedeli ya klachi.
25
mtoto - aliyejificha kwenye eneo fiche. Angalia kwenye mwelekeo wako
lakini angalia pia pande nyingine. Ni vizuri kumpata mtu kusimama
nyuma ya gari kukuongoza. Hili ni muhimu hasa kama unaendesha gari
la mizigo au gari lolote ambalo kuna ugumu dereva kuona eneo la nyuma
ya gari.
Kuliacha gari
Pindi gari lako likisimama weka breki ya mkono. Kwa gari lenye mfumo
wa otomatiki sogeza wenzo wa kichaguzi kwenye kuegesha. Kwa gari la
giaboksi ya manyu peleka wenzo wa gia kwenye nyutro (madereva
wengine hupenda kuyaacha magari yao kwenye gia ya kwanza au ya
kurudi nyuma). Kisha zima injini yako.
26
Uendeshaji salama barabarani
Kuendesha barabarani
Endesha kwa usalama. Sheria inasema USIENDESHE kwa hatari au
kwa uzembe. Hii huelezwa kama tabia ambayo dereva mwenye ujuzi
ataichukulia kama hatari – mfano kulipita gari jingine mahali ambapo
pana kona kali kiasi kuwa huwezi kuona vizuri mbele.
Endelea kutazama
sehemu zote. Usiangalie
sehemu moja kwa zaidi ya
sekunde 2 – endelea
kuhamisha macho yako
sehemu zote kuhakikisha
kuwa hukosi kuona kitu
chochote – angalia mbele
zaidi na kushoto na kulia –
na kila sekunde 5 angalia
kwenye vioo vyako, hata
kama unadhani hakuna magari karibu.
PITA PITA
29
Kuondoka. Kabla ya kuondoka, daima tumia vioo vyako, toa ishara na
tazama nyuma ya mabega yako kuona kuwa barabara haina kikwazo.
Ondoka iwapo umejiridhisha kuwa ni salama kufanya hivyo.
Vioo – alama – kitendo. Tumia vioo vyako daima ili wakati wote ujue
kilichoko nyuma na pembeni yako. Tumia vioo vyako vizuri kabla ya
kupinda au kubadili njia, na kisha toa ishara ifaayo.
Chunguza
katika kioo,
pima, amua
Toa ishara
sahihi
Fanya tendo
30
Usiweke msururu wa magari nyuma yako. USIENDESHE taratibu bila
sababu. Iwapo unaendesha gari kubwa au linalokwenda polepole na kuna
foleni ya magari nyuma yako, LAZIMA utafute sehemu ya kuingilia kwa
usalama na ruhusu magari mengine yakupite.
Endesha kwenye njia. Pale penye njia zaidi ya moja zenye mwelekeo
mmoja, tumia njia ya kushoto kwenda mbele na nyingine kwa ajili ya
kuvipita vyombo vingine, kupinda kulia, au kuyapita magari
yaliyosimama. Usibaki kwenye njia ya kulia muda mrefu zaidi ya
unaohitajika. Wakati wa kubadili njia kumbuka vioo – ishara - kitendo.
Mwendo
Endesha kwa mwendo salama. USIENDESHE kwa mwendo ambao
unaweza kuwa wa hatari kwa wengine. Daima rekebisha mwendo wako
kulingana na mazingira. Kwa mfano, punguza mwendo kama unakaribia
kona, daraja jembamba, au makutano, au eneo lenye watembea kwa
miguu wengi. Chagua gia itakayokuwezesha kulidhibiti gari zaidi.
Endesha polepole zaidi iwapo barabara ina majimaji, au huwezi kuona
vizuri. Endesha polepole zaidi usiku, kwa kuwa ni vigumu kuwaona
watembea kwa miguu, waendesha baiskeli, wanyama, na magari
yaliyoegeshwa au kuharibika.
32
Usilipite gari jingine isipokuwa kama una uhakika unaweza kufanya hivyo
bila ya kusababisha hatari kwa watumiaji wengine wa barabara au kwako
mwenyewe. Iwapo una mashaka usilipite gari jingine.
Unaweza kuvuka
mstari wa katikati
USIVUKE mstari USIVUKE mstari kama ni salama
wa katikati wa katikati kufanya hivyo
33
Sehemu zisizo salama kulipita gari jingine
34
Utaratibu wa msingi wa kulipita gari jingine. Kabla hujaanza kulipita
gari hakikisha kuwa barabara haina vikwazo mbele kukuwezesha kulipita
gari na kurudi kushoto bila ya
kulilazimisha gari jingine
kupunguza mwendo au kupinda
haraka ili kukukwepa.
Kama una shaka – usilipite gari
jingine. Tumia vioo vyako
kuona kuwa hakuna gari
linalokupita. Toa ishara kabla
ya kuanza kutoka [1]. Kuwa
mwangalifu zaidi usiku na
kwenye ukungu au mvua kubwa
wakati inapokuwa vigumu
kuamua kuhusu mwendo na
umbali. Kumbuka: vioo -
ishara - kitendo
Lipite gari lingine upande wa kulia. Daima lipite gari jingine upande
wa kulia, isipokuwa kama:
35
• gari la mbele yako linaonyesha ishara ya kupinda kulia, na kuna nafasi
ya kulipita kwa usalama kushoto (usiendeshe kwenye njia ya waendao
kwa miguu)
• magari yanakwenda polepole kwenye njia, na magari kwenye njia ya
kulia yanakwenda polepole zaidi yako.
Makutano
Kukaribia makutano ya barabara. Kugongana kwingi hutokea kwenye
makutano, hivyo chukua tahadhari zaidi. Angalia makutano yaliyo mbele
yako, na fikiria hatua ipi ya kuchukua, iwapo utatakiwa kufanya hivyo.
Hakikisha kuwa gari lako liko mahali sahihi kwa hatua unayotaka
kuichukua na kuwa unaendesha kwa mwendo unaofaa.
SIMAMA
Simama
na subiri
Simama
na subiri
Pale ambapo una haki ya kupita, nenda mbele kwa tahadhari na uwe
tayari ikibidi kupunguza mwendo na kusimama kuepuka kugongana.
Kupinda kulia
1. Hakikisha usalama kabla ya kupinda kulia, tumia vioo vyako kuona
kuwa magari yaliyo nyuma yako yapo umbali salama
2. Onyesha ishara ya kupinda kulia na anza kwenda polepole
3. Nenda kwenye sehemu ya kushoto ya katikati ya barabara
4. Mara tu panapokuwa na upenyo salama wa magari yanayokuja
mbele yako pinda kulia-usipite njia ya mkato.
38
Kupinda kushoto
1. Hakikisha usalama kabla ya kupinda kushoto, tumia vioo vyako
kuona kuwa hakuna gari linalokuja nyuma yako upande wa kushoto
2. Onyesha ishara ya kupinda kushoto na anza kwenda polepole
3. Kama barabara haina vikwazo pinda huku ukiwa karibu na ukingo wa
upande wa kushoto wa barabara (madereva wa magari marefu
wanaweza kuhitaji kwenda katikati ya barabara ili kuweza kupinda).
Kuwa makini na waendesha baiskeli na pikipiki ambao wanaweza
kutokea kwa upande wako wa kushoto - waache wakupite na angalia
usalama kabla ya kupinda. Kuwa makini na watembea kwa miguu -
iwapo kuna watembea kwa miguu wanaovuka barabara upande
unaopindia, lazima usimame na kuwaacha wavuke.
KAMWE usilipite gari lingine na kisha kupinda kushoto mbele ya gari hilo.
Angalia kwenye
kioo chako kuona
kama pikipiki au
baiskeli zinakuja
upande wako wa
kushoto
Nenda mbele tu wakati taa za kijani zitakapowaka, iwapo njia yako haina
vikwazo, au unajiandaa kupinda kulia.
40
Ushauri maalumu kwa madereva kwenye sehemu zenye
mzunguko
Kabla hujafika kwenye kiplefti hakikisha unapunguza mwendo wako,
amua ni njia ipi unahitaji kupitia, angalia kioo chako, na ingia kwenye
njia sahihi (angalia ushauri hapo chini) ukifika kwenye kiplefti yaruhusu
magari ambayo tayari yako kwenye mzunguko yapite. Angalia kwa
makini waendesha baiskeli na pikipiki, ambao inaweza kuwa vigumu
kuwaona iwapo kuna magari mengi. Kumbuka kuwa pia kunaweza kuwa
na watembea kwa miguu wanaovuka barabara - kutoka kushoto na pia
kulia.
41
4. Onyesha ishara ya kwenda kushoto baada ya kupita njia ya kutokea
kabla ya ile unayohitaji
5. Endelea kwenye njia yako ya kutokea, ukiwa bado unaonyesha ishara
ya kwenda kushoto.
42
Usiwafanye watumiaji wengine wa barabaraa kutoona vizuri. Usiwashe
taa za mavunde au taa nyingine isipokuwa kama kuna mavunde sana au
ukungu.
Kurudi nyuma
USIRUDI nyuma zaidi ya inavyotakiwa.
Kuwa makini hasa wakati unarudi nyuma ili utoke kwenye jengo, uzio,
kiwanja cha nyumba – ukuta au uzio unaweza kuwaziba watembea kwa
miguu ambao wanakaribia kupita sehemu ya kutokea gari. Ikiwezekana,
geuzia ndani, ili uweze kutoka nje kwa mbele.
43
Usirudi nyuma
kamwe kwenye
barabara ndogo
pembeni mwa
barabara kuu. Usirudi
nyuma kamwe
kwenye makutano
makuu. Usirudi
nyuma kamwe
mahali wavukapo
watembea kwa
miguu, au mahali reli
inapokatisha
barabara.
44
Kuwa makini sana kama watoto wako karibu, na wakati unaendesha
karibu na shule. Usiwategemee watoto kutenda kama watu wazima.
Uwezo wao wa kuona na kusikia una ukomo na hawawezi kutambua
mwendo vizuri. Hawako makini, na wanapokuwa hatarini wanaweza
kusimama tuli kwa hofu, badala ya kuondoka mahali hapo. Mahali
ambapo pana watoto punguza mwendo na kuwa makini sana.
45
Ishara zinazoongoza kuvuka kwa watembea kwa miguu. Sehemu
nyingine za kuvukia zinaongozwa na taa za barabarani. Fuata ishara za
taa za barabarani. Watembea kwa miguu wanaweza kuvuka barabara
mbele yako, taa NYEKUNDU ikiwa inawaka.
Kurudi ulikotoka
Reli Inayokatisha
Kwenye reli inayokatisha bila vizuizi, ishara au mtu yeyote anayeongoza
magari, punguza mwendo kabla ya kuingia kwenye reli ili kuchunguza
kama magarimoshi yanakuja. Madereva wa mabasi, na magari
yanayobeba vitu vinavyoweza kuwaka moto, LAZIMA wasimame na
kuangalia kabla ya kuendelea. Sikiliza king’ora cha garimoshi. Kamwe
usishindane na magarimoshi – mara zote yana haki ya kupita. Hakikisha
ni salama kabla ya kuvuka, na uwe makini zaidi pale penye njia za reli
zaidi ya moja.
Kuegesha
USIEGESHE gari:
• bila ya kujali na kuwafikiria wengine
• kwenye alama za pundamilia au mita 5 karibu na alama hizo
• mita 5 ndani ya makutano au mahali reli inapokatisha barabara
• kwenye kituo cha basi au mita 15 toka pande zote za alama ya “kituo
cha basi”
• kwenye njia ya waendao kwa miguu
• mbele ya sehemu ya kuingilia magari
• kwenye barabara yenye mistari myeupe miwili ya katikati, hata kama
moja ya mistari hiyo umekatikakatika
• ambapo haparuhusiwi kuegesha gari kwenye alama ya USIEGESHE
na/au mistari ya njano kwenye ukingo wa barabara.
48
• Pale ambapo gari lako litaziba alama au ishara ya barabarani.
Egesha gari lako kwa unadhifu, kwa uzuri na usalama. Unahitaji udhibtii
mzuri wa mwendo wako na usukani na pia uamuzi sahihi wa nafasi.
Chagua sehemu yako ya kuegesha kwa makini –
• kuna sehemu ya kutosha?
• ardhi inafaa – kuna vikwazo vyovyote?
• gari lako litakuwa salama?
Uegeshaji wa 900
Jaribu na egesha pale ambapo
unaweza kuendesha mbele na
kutoka kwenye maegesho.
Hata hivyo, katika maegesho
mengi utatakiwa kurudi nyuma
- ama mahali pa maegesho au
nje ya hapo. Kwa kawaida ni
vizuri kurudi nyuma kwenye
maegesho, kwa sababu hili
litakuwezesha kwenda mbele wakati unatoka – hali itakayokuwezesha
kuona vizuri magari na watembea kwa miguu. Usiliweke gari lako karibu
sana na gari la jirani kwani dereva wake au abiria atapata taabu kuingia
kwenye gari hilo. Usiegeshe kwenye maeneo yaliyoachwa kwa ajili ya
walemavu isipokuwa kama una uhalali wa kuyatumia.
49
Uegeshaji sambamba
Lazima uwe na uwezo wa kuegesha gari lako kwenye mstari wa wengine
sambamba na ukingo wa barabara – huu huitwa uegeshaji sambamba,
na ni wa kawaida mijini. Angalia nafasi ya kiasi cha mara moja na nusu
ya urefu wa gari lako. Ni vizuri kuingia kwa kurudi nyuma, isipokuwa
kama eneo lenyewe ni refu vya kutosha. Endesha ukipita sehemu tupu
na simama upande wa gari la kwanza baada ya eneo hilo – kiasi cha mita
moja (1) kutoka kwenye gari hilo.
Usiyaguse kamwe magari mengine kwa gari lako. Wakati unarudi nyuma
kwenye maegesho upande wa kulia wa barabara fuata taratibu zilezile za
msingi.
Uegeshaji wa mshazari
Ziko sehemu ambazo utatakiwa kuegesha mshazari kwenye kingo za
barabara. Kuendesha kwenda kwenye maegesho hayo ni rahisi: angalia
vioo vyako na maeneo fiche, ashiria kwenda kushoto, punguza mwendo
taratibu, na kisha nyonga kwa nguvu kuingia eneo hilo. Yanyooshe
matairi na simama pamoja na gari la mbele kwenye ukingo wa barabara.
Kuacha sehemu si kitu rahisi, kwa sababu utatakiwa kurudi nyuma, na
magari mengine yaliyoegesha yanaweza kukukinga kuona magari
yanayokuja. Jaribu kumtafuta mtu wa kusimama nyuma ya gari na
kukuongoza utoke. Rudi nyuma taratibu sana na angalia wakati wote
magari – pindi sehemu ya mbele ya gari lako itakapokuwa sawa na
sehemu ya nyuma ya gari lililoegeshwa kando yako, anza kupinda kwa
50
nguvu – angalia kuwa sehemu ya mbele ya gari lako iwe inapita kwenye
sehemu ya nyuma ya gari la jirani upande mwingine – kisha nyoosha na
simama – kisha utakuwa tayari kuondoka.
Kuegesha kilimani
Unapoegesha kilimani liache gari likiwa matairi ya mbele yamegeuzwa
kwenye upande wa barabara. Iwapo breki za mkono zitashindwa kufanya
kazi gari litakwenda nje ya barabara. Iwapo gari lako linatumia giaboksi
ya manyu liache gari kwenye gia ya kwanza au gia ya kurudi nyuma. Hii
itasaidia kulizuia gari lisitembee iwapo breki za mkono zitashindwa
kufanya kazi.
51
Alama za barabarani
52
Jaribio la udereva
53
Yaliyomo kwenye jaribio
Jaribio
54
• Unakuwa mwangalifu nakuangalia vizuri kabla ya kuingia, au
kukatisha makutano yoyote
• Unaonyesha ufahamu na matarajio kwa vitendo vya watembea kwa
miguu, waendesha baiskeli, na madereva wengine
• Liweke gari lako kwenye njia sahihi barabarani – wakati unaendesha
moja kwa moja na wakati unapinda kwenye makutano.
55
Baada ya jaribio
Iwapo utashindwa lazima usubiri kwa kiasi cha wiki nne kabla ya
kujaribiwa tena. Mtahini anaweza kuongeza kipindi hiki hadi wiki tisa (9)
kama ataona kuwa unahitaji muda zaidi wa kuboresha udereva wako.
56
Kuharibika
57
Iwapo kuna ajali
58
Muhtasari wa mafunzo ya madereva wa magari
madogo (Leseni za Daraja B & D)
1. Gari
Mwanafunzi lazima:
a) Awe na uelewa wa msingi wa jinsi gari inavyofanya kazi
b) Ajue matumizi na kazi za vidhibiti vya gari (mf. Usukani, breki na
gia) injini, mwako na sehemu nyingine za kiufundi
c) Aweze kusoma na kuelewa vifaa vya gari (mf. Spindometa) na
umuhimu wake
d) Kutambua hatari zinazotokana na kushindwa kufanya kazi kwa
sehemu mbalimbali za gari na jinsi ya kugundua hitilafu,
e) Ajue jinsi ya kufanya safari za awali, ukaguzi wa kila wiki na kila
mwezi,
f) Awe na uelewa wa jinsi aina mbalimbali za magari madogo (mf.
Magari madogo ya kawaida, pikapu, magari yenye kutumia
magurudumu yote manne) yanavyokuwa yakiendeshwa na jinsi ya
kuyaendesha kwa usalama.
2. Kufaa kuendesha
Mwanafunzi lazima:
a) Awe na mtazamo sahihi wa uendeshaji:- kuwajibika, kuwa makini,
matarajio, uvumilivu na kujiamini
b) Aelewe jinsi pombe inavyoathiri uwezo wa kuendesha gari, ajue
sheria inasemaje kuhusu kunywa pombe na kuendesha gari na jinsi
sheria inavyotekelezwa
c) Aelewe umuhimu wa kutoendesha gari wakati amechoka na ajue
miongozo kuhusu ni mara ngapi anatakiwa kupumzika
anapoendesha gari
d) Aelewe kwamba baadhi ya dawa zinaweza kuathiri uwezo wa
kuendesha gari na ajue jinsi ya kuzitambua
e) Aelewe jinsi ya kubadilikabadilika na ugonjwa kunavyoathiri uwezo
wa kuendesha gari
f) Aelewe umuhimu wa kuona vizuri na jinsi ya kutambua hali ya
macho.
3. Dereva na Gari
Mwanafunzi lazima:
a) Ajue nafasi inayotaiwa kuendeshea na jinsi ya kuingia sehemu hiyo
59
b) Ajue jinsi ya kurekebisha vioo, kujua ukomo wake na kujua kuhusu
maeneo yasiyo mazuri (“blind zone”)
c) Ajue jinsi ya kurekebisha udhibiti wa kichwa vizuri
d) Aelewe umuhimu wa kufunga mikanda, jinsi ya kuifunga vizuri na
sheria inayohusika
e) Ajue namna nzuri ya kubeba watoto kwa usalama
f) Ajue jinsi ya kubeba mizigo na wanyama kwa usalama.
4. Dereva na Sheria
Mwanafunzi lazima:
a) Ajue sheria muhimu, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusu kusababisha
ajali kutokana na kuendesha gari vibaya na kwa uzembe, kuendesha
wakati mtu amekunywa pombe na dawa za kulevya, kuendesha kwa
kasi n.ik..
b) Awe na uelewa wa msingi wa masharti ya gari kuwa zima
c) Ajue masharti ya leseni ya udereva, ikiwa ni pamoja na yale
yanayowahusu madereva wanafunzi
d) Ajue majukumu ya kisheria ya kuhusu kugongana
e) Ajue masharti ya bima ya gari na umuhimu wa kukata bima inayofaa
f) Awe na uelewa wa msingi wa jinsi sheria za usalama barabarani
zinavyotekelezwa (ikiwa ni pamoja na faini za papo hapo) na adhabu
za makosa ya uendeshaji gari.
5. Udhibiti na uratibu
Mwanafunzi lazima:
a) Aweze kuwasha injini, kuondoka na gari, kuongeza mwendo,
kubadilisha gia, kurudi nyuma, kuendesha kwenye kupanda mlima
na kushuka na kukata kona, na kufunga breki kusimama kwa
usalama bila taratibu na kiumahiri
b) Aweze kusimama na kuondoka kwenye mlima bila tatizo na bila ya
kurudi nyuma
c) Ajue jinsi mtindo wa uendeshaji unavyoathiri matumizi ya mafuta,
starehe na usalama wa abiria.
7. Mwendo kasi
Mwanafunzi lazima:
a) Ajue kuwa hatari ya kugongana inaongezeka kadri mwendo
unavyoongezeka
b) Aweze kuendesha kwa mwendo salama katika mazingira
c) Ajue vizuri jinsi ya kuepuka kuteleza na afanye nini utelezi
unapotokea
d) Awe na uelewa wa jumla wa umbali wa kusimama na jinsi
unavyotofautiana kulingana na mazingira ya barabara na mambo
mengine
e) Ajue mipaka ya mwendo kasi wan chi wa eneo, umuhimu wake na
jinsi inavyotekelezwa
f) Ajue kwamba kikomo cha mwendo kasi hakina maana na kwamba
wakati wote itakuwa ni salama kuendesha katika mwendo huo.
8. Kupita gari
Mwanafunzi lazima:
a) Ajue wakati gain ni salama kulipita gari
b) Ajue maeneo ambayo si salama kulipita gari – na wapi alama za
barabara zinaonyesha ni kosa kulipita gari
c) Aweze kulipita gari jingine katika hali ya usalama na umahiri, bila
kusababisha gari linalotoka katika mwelekeo tofauti kupunguza
mwendo au kubadili uelekeo ili kuepuka kugongana.
61
9. Makutano (tofauti na mzunguko)
Mwanafunzi lazima:
a) Aweze kuendesha gari kwa kupita katika aina zote za makutano
katika hali ya usalama na umakini, ikiwa ni pamoja na yale yaliyo
katika barabara iliyogawanywa sehemu mbili, mitaa ya njia moja na
zile zinazoongozwa na alama za barabarani
b) Ajue umuhimu wa kukaribia makutano kwa mwendo unaofaa,
kuingia katika njia na nafasi sahihi, kutii sheria muhimu kuangalia
vizuri na kutozuia misururu mingine ya magari kutembea
c) Atumie vizuri ishara.
10. Mizunguko
Mwanafunzi lazima:
a) Aweze kupita kwenye mizunguko katika hali ya usalama na umahiri
b) Ajue ni njia gani ya kutumia anapoingia na kukata kona na
kuondoka kwenye mzunguko
c) Atumie vizuri ishara
d) Ajue nani mwenye kipaumbele.
62
13. Kuharibika na dharura
Mwanafunzi lazima:
a) Aweze kutumia breki na gia ili kuweza kusimamisha gari haraka bila
ya kuteleza na bila ya kuzima injini
b) Ajue atafanya nini kama atahusika katika kugongana au kusimama
kutoa msaada
c) Ajue atafanya nini kama ataharibikiwa gari barabarani na hususan
jinsi ya kuepuka kusababisha hatari kwa watumiaji wengine wa
barabara.
16. Maegesho
Mwanafunzi lazima:
a) Aweze kuamua kama ni salama ni sheria na ni busara kuegesha
sehemu yoyote
b) Aweze kuegesha sambamba, maegesho ya 90º, na maegesho
mshazari katika hali ya usalama na umahili kwa usimamizi mzuri,
uelekeo sahihi na uzuiaji mdogo wa magari mengine
63
c) Kuweza kuegesha kwa usalama kwenye mteremko (mwinuko na
mteremko).
64