Professional Documents
Culture Documents
(TAWLA)
MWONGOZO WA TARATIBU ZA
KISHERIA KATIKA UMILIKI WA ARDHI
Kimechapishwa na:
Tanzania Women Lawyers Association(TAWLA)
S. L. P. 9460, Dar es Salaam - Tanzania
Tel: +255 22 2110758, Fax: + 255 22 2110758.
SHUKRANI..................................................................................................i
MUHTASARI..............................................................................................ii
ANGALIZO................................................................................................iii
KUHUSU TAWLA...................................................................................... iv
SURA YA KWANZA:............................................................................... 1
HISTORIA, UMILIKI NA MATUMIZI YA ARDHI TANZANIA.............1
SURA YA TATU:.................................................................................... 24
SHERIA YA ARDHI YA KIJIJI NA.5 YA 1999.........................................24
SURA YA NNE:..................................................................................... 31
SHERIA YA FEDHA NA REHANI...........................................................31
SURA YA TANO:................................................................................... 36
SHERIA YA UMILIKI WA VIPANDE......................................................36
SURA YA SITA:..................................................................................... 42
SHERIA NYINGINEZO ZINAZOHUSIANA NA UMILIKAJI WA ARDHI
..................................................................................................................... 42
SURA YA SABA:.................................................................................... 57
UTATUZI WA MIGOGORO YA ARDHI................................................57
SHUKRANI
Mwongozo huu unalenga kuelezea malengo na mikakati ya TAWLA
ambayo moja wapo ni kuhakikisha haki za wanawake zinazingatiwa
na zinalindwa. Muongozo huu unalengo la kuwaelimisha na
kuwapa ufahamu wanawake juu ya sheria na haki zao katika
masuala mbalimbali yanayohusiana na ardhi. TAWLA inapenda
kutoa shukrani zake za dhati kwa watu wafuatao waliochangia kwa
kiasi kikubwa uandaaji wa mwongozo huu.
TIKE MWAMBIPILE
Mkurugenzi
MUHTASARI
Mwongozo huu umeandaliwa na TAWLA kusaidia katika kuelewa
sheria na taratibu mbalimbali zinazohusiana na masuala ya ardhi
kwa wanawake Tanzania.
ANGALIZO
ILANI
Mwongozo huu umeandaliwa na TAWLA kwa lengo la kusaidia
watanzania wote kupata ufahamu wa kuweza kujua na kufahamu
taratibu mbali mbali za kufuata katika kumiliki kutumia na kutatua
migogoro ya ardhi katika vyombo mbali mbali.
KUHUSU TAWLA
TAWLA ni shirika lisilokuwa la kiserikali, lililoanzishwa mwaka
1990 chini ya sheria ya vyama na moja ya kazi zake ni kutetea na
kulinda haki za binadamu hasa hasa wanawake.
DHAMIRA YA TAWLA.
Ujumbe na dhamira ya TAWLA ni kuwa na nia ya kuendeleza
wanachama wake kitaalamu na pia kukuza haki na usalama bora
kwa wanawake na watoto.
MAONO YA TAWLA
Maono ya TAWLA ni kulenga jamii yenye kuheshimu haki za
binadamu na kuzilinda.
Sura ya Kwanza
HISTORIA, UMILIKI NA MATUMIZI
YA ARDHI TANZANIA
UTANGULIZI
Sehemu hii inaangalia mfumo wa umilikaji ardhi na haki ya
mwanamke kwenye maswala ya ardhi. Inaangalia dhana nzima ya
mabadiliko ya sheria za ardhi hapa Tanzania na jinsi mabadiliko
hayo yanavyomlinda mwanamke. Kwa hiyo sehemu hii pamoja
na mambo mengine inajaribu kuchanganua mapungufu yaliyo
sababisha mabadiliko ya sheria za ardhi pamoja na dondoo muhimu
kwenye sheria za ardhi. Inajaribu pia kufanya mlinganisho wa
masuala yanayowagusa wanawake kwenye ardhi pamoja na jinsi
masuala hayo yanavyo elezewa kwenye sheria za ardhi. Sehemu hii
haiangalii tu jinsi sheria za ardhi zinavyolinda haki za mwanamke
kwenye ardhi bali inaangalia pia jinsi baadhi ya vipengele
vinavyoweza kutafsiriwa ili kulinda haki ya mwanamke katika
masuala ya ardhi.
Sura ya Pili
SHERIA YA ARDHI NA. 4 YA 1999
A. MGAWANYO WA ARDHI
Sheria hii mpya imeigawa ardhi yote ya Tanzania katika
Makundi matatu. Makundi hayo ni:-
i. ARDHI YA JUMLA
Ardhi ya jumla ni ile ardhi yote ambayo siyo ardhi ya
hifadhi au ardhi ya kijiji lakini ambayo inajumuisha
ardhi ya kijiji ambayo haikaliwi wala haitumiki.
ii. Ardhi ya Vijiji
Ardhi ya vijiji ni ile ambayo iko ndani ya mipaka ya vijiji
na ambayo imesajiliwa kwa kufuata sheria zilizoweka
kama vile sheria ya Serikali za Mitaa ya 1982 na sheria
mpya.
iii. Ardhi ya hifadhi
Ardhi ya hifadhi ni ardhi iliyotengwa kwa madhumuni
maalum. Ardhi ya hifadhi inajumuisha aina zifuatazo
za ardhi:-
• Maeneo ya hifadhi na misitu yanayotambulika
kisheria (sheria ya misitu)
• Mbuga za wanyama pori (sheria ya Hifadhi ya
mbuga za wanyama, sheria ya Hifadhi ya eneo la
Ngorongoro.
• Hifadhi za maji (bahari, mito , mabwawa makubwa
na maziwa n.k)
• Ardhi yenye majimaji (kama ile iliyo pembezoni
mwa mito na madimbwi)
• Hifadhi ya barabara
• Maeneo ya wazi (kama yale yaliyotengwa kwa ajili
ya kupumzikia, burudani, michezo na starehe)
I. Rais
Rais ni msimamizi mkuu wa utawala wa ardhi lakini
anaweza kumteua mtu ambaye atashughulikia masuala
ya ardhi. Mtu huyo ni Waziri anayeshughulikia ardhi
na chini yake kuna Kamishna wa Ardhi ambaye
ndiye mtendaji na mshauri mkuu katika mambo yote
yanayohusu ardhi. Kwa maana hiyo Rais ana majukumu
yafuatayo;
o Udhamini wa ardhi yote ya Tanzania
o Kumteua waziri wa Ardhi
o Kumteua Kamishna wa Ardhi
C. KUMILIKI ARDHI
Nani mwenye haki ya kumiliki ardhi?
Mwenye haki ya kumiliki ardhi ni raia yeyote wa Tanzania.
Anaweza kumiliki ardhi kama mtu binafsi au kikundi cha
watu wawili ama zaidi. Watu wanaweza kumilikishwa ardhi
kwa njia zifuatazo:-
1. Kwa kupatiwa hati ya umilikaji kwa mujibu wa sheria
2. Kwa kuitwaa kwa kufuata taratibu za kimila/au kwa
kuikalia na kuitumia ardhi kwa muda mrefu kama vile
kwa miaka kumi na mbili au zaidi.
3. Kwa mujibu wa sheria ya uwekezaji kwa lengo la
kutumia ardhi kwa uwekezaji.
Taratibu za kufuata:
Sheria hii inaeleza taratibu zifuatazo:
1. Maombi yawekwe na kuwasilishwa kwenye fomu maalum
inayoambatanishwa na picha ya mwombaji. Maombi hayo
yawasilishwe wilayani ama wizarani kwa kadri ya sheria na
taratibu zinavyoelekeza.
2. Maombi yaambatanishwe na ada kama inavyoelezwa kwenye
sheria.
3. Fomu isainiwe na mwombaji, mwakilishi au wakala wa
mwombaji.
4. Maombi yaeleze ama yaambatanishe taarifa inaotakiwa
ambayo kamishna ataiomba kwa maandishi.
5. Maombi yaambatanishwe na tamko la mali nyingine
zinazohusiana na ardhi anazomiliki mwombaji kwa wakati
huo.
6. Endapo sheria inahitaji idhini ya mamlaka ya serikali ya
mahali ama mamlaka ya chombo chochote kabla ya kutoa
idhini ya kumiliki ardhi, hatua hizo zifanyike na nyaraka hizo
zisainiwe na mamlaka husika. Mfano kama mashirika ya dini
yatatakiwa kuidhinishwa na kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali.
7. Kama ombi ni la mgeni ama kampuni ya kigeni liambatanishwe
na cheti cha kuidhininishwa na kitengo cha mwekezaji
kulingana na sheria ya uwekezaji ya 1997 au nyaraka nyingine
zitakazohitajika.
8. Kama ombi ni la mgeni ama kampuni ya kigeni na linahusu
haki ya miliki ya makazi, matumizi ya ardhi yalingane na yale
yaliyoidhinishwa na sheria ya uwekezaji.
9. Baada ya kupokea nyaraka na maelezo yote yanayohitajika,
Kamishna ataanza kushughulikia ombi la haki miliki kwa
kufuata sheria inavyoagiza. Hatua ya kwanza ni kusajili ombi
hilo katika kitabu cha usajili wa maombi ya ardhi. Hii inasaidia
kuondoa usumbufu kwa umma kwa visingizio mbalimbali.
Sura ya Tatu
SHERIA YA ARDHI YA KIJIJI
NA.5 YA 1999
Lengo la sheria hii nikuweka masharti ya usimamizi na uendeshaji
wa maswala ya ardhi na vijiji na mambo mengine yanayo husiana
na hayo.
Jedwali Na. 1
Ardhi ya
Ardhi ARDHI pamoja
iliyokaliwa ambayo
na kutumiwa halmashauri
na mtu, ya kijiji
itapendekeza
familia au YA kwa kupitia
kikundi cha mkutano
watu kwa wa kijiji
mujibu wa maeneo na
sheria za KIJIJI makusudio
kimila ya maeneo
hayo
Sura ya Nne
SHERIA YA FEDHA NA REHANI
Sheria ya fedha na rehani imeweka mazingira kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba kwa kutoa hakikisho la kuwalinda wakopeshaji.
Taratibu za uombaji
Sheria hii inatoa mwanya kwa mwombaji kujua asili, masharti
na muda wa haki kusudiwa kabla ya kukubali. Mara mwombaji
anapokuwa amekubaliana na masharti yaliyoainishwa alitakiwa
kusaini barua hiyo ya kukubaliwa na kulipa malipo yanayotakiwa.
MAPUNGUFU YA SHERIA
1. Kifungu hiki kimeegemea zaidi upande mmoja pasipo
kuangalia upande wa familia ya mkopaji lakini pia
kutokuzingatia uwezekano wa hati ya kiapo kugushiwa.
2. Ilipaswa kubaki kuwa jukumu la mkopeshaji kuthibitisha
taarifa zilizo tolewa na mkopaji endapo ni sahihi kabla ya
kutoa mkopo.
3. Pia, marekebisho yameruhusu kubadilishwa kwa kiwango cha
riba kwa mkopeshaji kuandika notisi kwenda kwa mkopaji;
hii inamweka mkopaji katika hali ya mashaka endapo ataweza
kulipa deni pale riba inapopandishwa.
4. Vilevile kama inavyoonekana kigezo kikubwa cha kubadilisha
kiwango cha riba ni kuangalia faida ya soko na sio hali ya
kichumi ya mkopaji.
5. Pia uamuzi wa kupandisha riba ni wa upande mmoja wakati
mkataba wa mkopo ulikuwa wa pande mbili. Mkopaji hana
fursa ya kutoa mtizamo wake.
6. Hata baada ya nyongeza ya kiwango cha riba endapo mkopaji
akashindwa kulipa mali yake inaweza kuchukuliwa na
kuuzwa kulipia deni na kuwaacha mke na watoto wakiteseka.
Wakati inajulikana kwamba mkopaji anaweza kuweka rehani nyumba
ya kuishi ambayo kuna watu ndani au shamba linalotumiwa kwa
ajili ya kilimo, marekebisho yameweka wazi kwamba mkopeshaji
anaweza kuuza ardhi kama mkopaji atashindwa au kuchelewa
kulipa deni kwa wakati. Mauzo yanaweza kufanyika kwa njia
ya mkataba na kwa muda mfupi au mnada wa hadhara ambapo
mkopaji na watu wengine wenye maslahi watapewa notisi ya siku
kumi. Hii kwa vyovyote itaathiri wanawake na watoto inapokuja
kwenye swala la lazima kuondoka kwenye nyumba.
mauzo. Mwanya huu pia unabaki kuwa mlango wazi kwa ajili ya
soko kukanyaga haki za wanyonge hasa wanawake na watoto.
Sura ya Tano
SHERIA YA UMILIKI WA VIPANDE
UTANGULIZI:
Sheria ya umiliki wa vipande ya mwaka 2008, ni Sheria inayoweka
mfumo wa kisheria kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo wa umiliki
pacha Tanzania. Sheria hii japo inalenga kupunguza changamoto za
makazi ambazo ni pamoja na mpangilio hafifu, vikwazo vya kisheria,
kukosekana mikopo ya nyumba ya muda mrefu, udhaifu wa sheria
za ardhi, kuongezeka na kupanuka kwa miji na kukosekana kwa
fedha za kununua au kujenga makazi bora.
Uuzaji wa vipande
• Sheria inaelekeza yakuwa eneo la matumizi ya pamoja
halitauzwa au kutozwa gharama yoyote labda tu kama
linamilikiwa na mtu mmoja.
• Mmiliki ana haki ya kumpa mtu yeyote sehemu yake kwa njia
ya kuuza ,kupangisha, kuzawadia, kurithisha, kuweka rehani
au kwa namna nyingine yoyote iliyoidhinishwa kisheria.
Upangishaji.
• Mmiliki ana haki ya kupangisha kipande chake.
• Mmiliki anayepangisha kipande chake atawajibika kuweka
fedha ya tahadhari chini ya uangalizi wa ushirika na kulipia
gharama zozote za matengenezo, upotevu na manunuzi ya
vitu vitakavyoharibiwa.
• Mmiliki wa sehemu ya vipande ana wajibu kisheria kujulisha
ushirika juu upangishaji wa sehemu yake kwa maandishi
yenye maelezo muhimu na jina la mpangaji ndani ya siku
saba.
Urithishwaji.
• Mmiliki wa sehemu ya vipande anaweza kurithisha sehemu
yake kwa kufata taratibu zilizoainishwa katika sheria ya Usajili
wa Ardhi, sura ya 334.
Rehani.
• Sheria inaruhusu mmiliki kuweka rehani sehemu ya jengo lake
kwa kufuata taratibu zilizoainishwa katika sheria ya Ardhi ya
mwaka 1999 (sura ya 113) ambayo imerekebishwa na sheria
Na 2 ya mwaka 2004 na sheria Na 17 ya mwaka 2008.
• Ushirika unawajibu kisheria kulinda sehemu ya jengo ya
ushirika ilyowekwa rehani kwa kuzingatia taratibu ya Sheria
ya umiliki wa sehemu ya jengo na 16 ya mwaka 2008.
Sura ya Sita
SHERIA NYNGINEZO ZINAZOHUSIANA NA
UMILIKAJI WA ARDHI
SHERIA YA NDOA.
Nyumba ya ndoa katika sheria ya ndoa
o Nyumba ya ndoa ni nyumba ambayo mume na mke wanaishi
wakati wa ndoa inawezekana ikawa mali binafsi ya mke au
mume au nyumba ya kupanga .
o Mke au mume hanaruhusiwi kuuza nyumba hiyo, kuweka
rehani au kumpa mtu mwingine kama zawadi bila makubaliano
ya wanandoa.
o Kama mmoja wa wanandoa anataka kuuza nyumba hiyo bila
kukubaliana na mwenzi wake Yule mwenzi ambaye hakutoa
idhini anaweza kuweka pingamizi (caveat-buyer be aware)
ambayo kimsingi inatahadhalisha mtu yeyote atakaye taka
kujihusisha na mali au ardhi hiyo mfano kwa kununua kuwa
kuna mtu mwingine mwenye maslahi katika ardhi au mali
hiyo.
SHERIA ZA MIRATHI
Mirathi ni Nini?
Ni masuala yanayohusu kukusanya kulipa na kugawa mali pamoja
na kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu. Mojawapo ya mali ni
ardhi, nyumba na vinginevyo ambayo marehemu alikuwa anamiliki,
I. Sheria ya kimila
Sheria hii diyo inayodhaniwa kutumiwa kwa wazawa wote
isipokuwa pale ambapo alikuwa afati mila na desturi husika za
kiafrika.
WOSIA
Wosia ni kitu muhimu sana kwani unaondoa migogoro mingi katika
familia na kuwapunguzia matatizo wale wanaobaki, baada ya mtoa
wosia kufariki hasa kwa wale ambao ni warithi.
Wosia wa maneno
Wosia huu unapaswa kushuhudiwa na mashaidi wasiopungua
wanne na wawili kati ya hao lazima wawe ni wanaukoo wa huyo
mwosia. Wosia wa aina hii unaweza kufutwa kwa wosia mwingine
wa mdomo au wa maandishi.
Wosia wa maandishi
Wosia wa maandishi unatakiwa uandikwe kwa kalamu isiyofutika
au upigwe chapa. Ni muhimu na lazima wosia huu uwe na tarehe.
Tarehe………………………
Mbele yetu sisi wawili kwa wakati mmoja katika muda huu
kutokana na matakwa yake mwenyewe nasi tunaweka majina
na sahihi zetu hapa chini kama mashahidi:-
1. Jina la shahidi……….. 2. Jina la shahidi…………
Sahihi………………….. Sahihi …………………….
Kazi………………….…. Kazi……………………….
Tarehe………..………. Tarehe…………………….
BARAZA LA KATA
Wajumbe wasiopungua 6 wala kuzidi 8
Kazi:- Kutatua migogoro ya ardhi
katika kata husika
Kupokea rufaa toka baraza la ardhi la
kijiji
BARAZA LA KIJIJI
Wajumbe 7 kwa ujumla na kati yao
wanawake wawe watatu au zaidi
Kazi:- Kusuluhisha migogoro ya ardhi
katika eneo la kijiji husika
- Kupokea rufaa toka maamuzi ya
Mwongozo
Mwongozo wa Taratibu
wa Taratibu za KisheriazaKatika
Kisheria
kamati Umiliki Katika
wa Ardhi
ya ardhi
Umiliki wa Ardhi
ya kijiji
57
41
Tanzania women Lawyers Association
Rufani
Kwa mtu ambaye atakuwa hajaridhika na uamuzi wa kamati
ataweza kukata rufani dhidi ya uamuzi huo kwenye baraza la
ardhi la kijiji ndani ya siku thelathini (30) baada ya kutolewa kwa
kumbukumbu.
Sifa za wajumbe.
Mtu hatateuliwa kuwa mjumbe kama:-
a. Si mkazi mwenyeji wa kijiji ambacho Halmashauri inaendesha
kazi zake;
b. Ni mbunge
c. Ni hakimu mwenye mamlaka kwenye Wilaya ambayo ndimo
ilimo Halshauri ya kijiji itakayoendesha shughuli
d. Ni mtu aliye chini ya miaka kumi na nane
e. Ni mtu mwenye matatizo ya akili
f. Ni mtu aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai kuhusiana
na kukosa uaminifu au kukosa maadili
g. Mtu asiye raia wa chi hii
Rufani
Kwa mtu ambaye atakuwa hajaridhika na uamuzi wa Baraza la
Ardhi la Kijiji ataweza kukata rufani dhidi ya uamuzi huo kwenye
baraza la kata.
3. Ni mtumishi wa serikari
4. Ni mwanasheria au mtu yeyote aliye ajiriwa katika idara ya
mahakama
5. Ni mtu ambaye haja timiza umri wa mmiaka 18
6. Ni mtu ambaye ametiwa hatiania kwa kosa la kukosa uaminifu
7. Ni mtu ambaye si raia wa Tanzania
Rufani
Kwa mtu ambaye atakua hajaridhika na uamuzi wa Baraza la Kata
ataweza kukata rufani dhidi ya uamuzi huo kwenye Baraza la Ardhi
na nyumba la Wilaya.
Baraza litaweza kuita shauri toka Baraza la kata kwa ajili ya kupitia
mwenendo mzima wa shauri husika ili kujiridhisha kama uamuzi
wa Baraza la Kata haujakiuka sheria zilizopitishwa na Bunge ama
sheria ndogo. Pia Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya linaweza
kufanya hivyo ili kutazama kama maamuzi ya Baraza la Kata
halijakiuka haki asili au kama uamuzi ulitolewa na Kikao halali.
Pia Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya laweza kufanya hivyo
ili kujiridhisha kama Baraza la Kata halikusikiliza mgogoro ambao
haupo chini ya mamlaka yake.
Rufani
Kwa mtu ambaye atakua ajaridhika na uamuzi wa Baraza hili
ataweza kukata rufani dhidi ya uamuzi huo kwenye mahakama
kuu kitengo cha ardhi ndani ya siku 60 toka siku uamuzi huo
ulipotolewa.
Rufani
Kwa mtu ambaye atakua hajaridhika na uamuzi wa Mahakama hii
ataweza kukata rufani dhidi ya uwamuzi huo kwenye Mahakama
Kuu ya Rufani na taratibu za kukata rufaa kwenye Mahakama ya
Adhabu:-
Mtu atakayetenda makosa yaliyoainishwa hapo juu atahukumiwa
adhabu ya faini isiyo zidi shilingi milioni moja au kifungo cha muda
usio zidi miaka mitatu jela au adhabu zote mbili, yaani faini na
kifungo.
2) Ni kosa la jinai
Kwa mtu bila sababu ya kuridhisha kushindwa kutoa waraka
wowote kama inavyo hitajika chini ya sheria hii.
Adhabu
Mtu akipatikana na hatia kwa kosa hili ata hukumiwa adhabu ya
faini isiyozidi shilingi hamsini elfu au kifungo kisichozidi miaka
mitatu au vyoteiwili.
3) Nikosa la jinai
Kwa mtu kukalia ardhi kinyume cha sheria.
Adhabu
Mtu akipatikana na hatia kwa kosa hili atahukumiwa faini isiyozidi
shilling za kitanzania miatan o kila siku atakayo endelea kufanya
kosa.
4) Nikosa la jinai
Kwa mtu yeyote kwa makusudi kuzuia au kuingilia haki ya njia kwa
Umma, na akashindwa kuondoa kizuizi hicho au kuacha kuingilia
haki hiyo ya Umma ndani ya wakati unao ainishwa katika notisi
yoyote aliyo pelekewa.
Adhabu
Mtu akipatikana na hatia kwa kosa hilo ataukumiwa faini isiyo
zidi shilingi elfu kumi au kama ataendelea kutenda kosa hili
atapata adhabu ya faini isiyo pungua shilingi mia mbili kila siku
atakayoendelea kutenda kosa hili.
5) Nikosa la jinai
Kwa mtu yeyote kwa makusudi atakawiza kuzuia, kuziba,
kuogopesha, au kumpinga mtu yeyote aliye idhinishwa chini ya
sheria hii kuingia na kukagua ardhi kwa zoezi halali la mamlaka
aliyo pewa.
Adhabu
Mtu akipatikana na hatia kwa kosa hilo atahukumiwa faini
isiyopungua shilingi laki moja au kifungo kisicho pungua muda wa
mwaka mmoja au vyote viwili, faini na kifungo.
6) Ni kosa la jinai
Iwapo mtu yeyote ama katika hali ya kawaida au katika kutekeleza
jukumu maalumu au vinginevyo ataingia isivyo halali au kwa
nguvu kwenye ardhi au wakati akikalia ardhi hiyo au kuharibu kitu
chochote cha hasili kwenye ardhi hiyo au kinacho milikiwa na mtu
yeyote anaye tumia ardhi hiyo au kuharibu madhao yaaliyooteshwa
au majengo yaliyoko kwenye ardhi, mtu huyo atakuwa ametenda
kosa la jinai.
Adhabu
Mtu akipatikana na hatia kwa kosa lililotajwa hapo juu atahukumiwa
faini isiyozidi shilingi elfu hamsini au kifungo kisicho zidi miezi
mitatu au vyote viwili, faini na kifungo.
Sura ya Nane
ULINZI WA MWANAMKE DHIDI YA
VIPENGELE VYA KUBAGULIWA
Ni muhimu pia kutambua kwamba haki za kijamii, kiuchumi
na kisiasa zimetambuliwa na kulindwa na Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania. Inatakiwa wakati wa kuangalia haki za
wanawake kwenye maswala ya ardhi kuzingatia katiba ya nchi.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) inatambua haki
ya wanawake kwenye ardhi kwa kuzuia ubaguzi na kutilia mkazo
usawa wa watu wote. Kwenye
MIKATABA YA KIMATAIFA
Tanzania kama mjumbe wa Umoja wa Mataifa (UN) inawajibu
kutoa haki sawa kwa wanawake na wanaume kama ilivyoainishwa
kwenye Katiba ya Umoja huo (UN Charter) na Tamko la Haki za
Binadamu (UDHR)). Mkataba wa kuzuia aina zote za ubaguzi dhidi
Mali ya Familia
Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 pia inatamka kwamba ridhaa ya
mwenzi lazima ipatikane kwenye uhawilishaji wa ardhi kama vile
kuuza, kukodisha, kupangisha au kuweka rehani.
KIMILA
Mali ya wanandoa iliyoko chini ya hati ya kimila ambayo imeingia
kwenye hatari ya kuchukuliwa na mkopeshaji inalindwa na
sheria. Hati ina maana zaidi kwa wanawake kwa jinsi inavyotoa
ulinzi wa baadaye hata pale ambapo haki ya mwanamke kutoa
ridhaa haikuzingatiwa pale awali. Lakini hata pale mali ilipokuwa
inamilikiwa na mwanamke na anaona kwamba masharti hayakuwa
ya haki au wazi wakati wa kuingia kwenye makubaliano anaweza
kupata msaada wa baraza la ardhi la kijiji kuhakikisha kwamba
mali (ardhi/nyumba) haichukuliwi kirahisi. Hata kama ulinzi huu
ulilenga kulinda ardhi ya kijiji na sio mali ya familia ulinzi huo kwa
vyovyote vile utamnufaisha mmiliki wa ardhi familia au mali ya
wanandoa.
2.8 Hitimisho
Inaweza kuonekana kwamba kinadharia mfumo wa kisheria uliopo
umeweka nyenzo zinazohitajika kuhakikisha kwamba haki ya
wanawake kwenye ardhi inalindwa. Inapaswa kuwepo na jitihadi
za dhati kuhakikisha kuna utekelezaji wa sheria zilizopo. Vikundi
vyenye kutetea maslahi ya umma vinapaswa kusimama, kutetea na
kuhakikisha kwamba maudhui ya sheria hizi yanatiliwa mkazo na
kutekelezwa