Professional Documents
Culture Documents
ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kuna mpaka kauli ambazo zinaonesha jinsi tunavyoamini kwenye wingi, kauli
kama WENGI WAPE au PENYE WENGI HAPAHARIBIKI NENO zinaonesha jinsi
jamii zetu zimejengwa kufuata mkumbo.
Pamoja na manufaa makubwa ambayo kufuata mkumbo yanayo, hasa
kuturahisishia kufanya maamuzi, kuna hatari. Wale wanaojua jinsi ya kutumia
silaha hii kushawishi, wanaweza kutengeneza mazingira yanayotufanya tuone
wengi wanafanya kitu fulani hivyo ni sahihi kwetu kufanya na kumbe siyo
kweli. Hapa tunakwenda kuona jinsi silaha hii inatumika kushawishi na jinsi ya
kuepuka kushawishiwa vibaya kwa silaha hii.
Ukweli ni sisi.
Kama umewahi kuangalia vichekesho kwenye tv utagundua baadhi ya
vichekesho vina sauti za kucheka ambazo zinaambatana na vichekesho hivyo.
Sauti hizo zinaweza kuwekwa kwenye tukio ambalo hata halichekeshi, lakini
kwa kusikia sauti zikicheka, unaona hilo ndiyo jambo sahihi kufanya, unacheka
pia.
Wanaotumia njia hii kwenye vichekesho wanajua msingi mkuu wa kijamii
ambao ni kilicho sahihi kufanya ni kile kinachofanywa na wengi. Kwa kifupi,
kwenye jamii ukweli huwa unaonekana kuwa pale walipo wengi. Hivyo
unapokuwa njia panda na hujui kipi sahihi kufanya, huwa unaangalia wengi
wanafanya nini na kufanya hicho pia.
Hata unapoenda ugenini, huwa unaangalia wenyeji wanafanya nini na kisha
kufanya kwao. Iwe ni jinsi ya kusalimia, kula na mengine, huwa tunapata
mwongozo wa kilicho sahihi kwa kuangalia wengi wanafanya nini.
Kwa sehemu kubwa, msingi huu wa kufuata mkumbo una manufaa,
unatupunguzia kufikiri na kufanya maamuzi kila mara hasa kwa uhaba wa
muda na nguvu tulionao. Ukifika mahali ambapo ni mgeni na ukakuta watu
wanafanya au hawafanyi kitu fulani, kuna sababu nyuma yake, kama huna
muda wa kuchunguza sababu hiyo, utakuwa salama zaidi kama utafanya kama
wao kuliko kufanya tofauti.
Lakini hili linatuweka kwenye hatari ya kushawishiwa vibaya na wale ambao
wanatumia msingi huu kutushawishi kukubaliana na kitu, kwa sababu tu
wanatuambia wengine nao wanakubali.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Asilimia 95 ni waigaji.
Mwandishi anamnukuu Cavett Robert ambaye ni mkufunzi wa mauzo ambaye
amekuwa akifundisha kwamba kwenye jamii yoyote ile, asilimia 5 tu ya watu
ndiyo waanzilishi au wabunifu, asilimia 95 iliyobaki ni waigaji. Hivyo watu
wengi huwa wanashawishika zaidi na matendo ya wengine kuliko kile
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Ujinga wa kundi.
Tabia ya kuangalia wengine wanafanya nini ndiyo mtu ajue kilicho sahihi
kufanya, imekuwa inazalisha hali ya ujinga wa kundi. Ambapo unakuta kundi la
watu wanafanya kitu, ila hakuna hata mmoja anayejua kwa nini anafanya. Kila
mtu anakuwa anaangalia wengine wanafanya na yeye anafanya.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
mtu kuona kwamba wengine watasaidia. Lakini kwa kijijini, kunakuwa na watu
wachache, hivyo inapotokea shida ni rahisi kusaidiwa. Chukua mfano nyumba
imevamiwa na majambazi, kwa mjini, mtu anakuwa na majirani wengi, hivyo
hata kama wote watasikia, kila mmoja atajiambia jirani mwingine atakuwa
ameshapiga simu polisi, kinachotokea ni hakuna hata mmoja anapiga simu,
kwa sababu kila mmoja anafikiri mwenzake ameshafanya hivyo. Lakini kwa
kijijini, mtu anakuwa na jirani mmoja ambaye atabeba wajibu na hata
mwingine wa kumtegea. Hivyo wingi wa watu maeneo ya mjini unafanya
msaada kuacha kuwa jukumu la mmoja na kuwa la wengi ambapo hakuna
anayeutoa.
2. Maisha ya mjini yanawafanya watu wanakuwa wametingwa na kuzungukwa
na usumbufu, kitu kinachowafanya washindwe kujua kama kitu ni tatizo kweli
au la. Mfano kama kwa jirani kuna ugomvi, kwa mjini ni vigumu watu kuingilia
kwa sababu wanakuwa hawajui nini kinaendelea. Lakini kwa kijijini, watu
wanakuwa na utulivu wa kujua yanayoendelea na hivyo tatizo linagundulika
haraka.
3. Watu wa mjini hawajuani moja kwa moja kama ilivyo kwa watu wa vijijini.
Majirani wa kijiji kimoja wanajuana vizuri na hivyo inakuwa rahisi kusaidiana.
Watu wa mjini hawajuani kwa undani, watu wanaweza kuwa majirani lakini
wasijuane kuhusu maisha yao, hivyo inakuwa vigumu kusaidiana.
Vitu hivi vitatu vinafanya utoaji wa msaada kwa wenye uhitaji wa hali ya
dharura kuwa mgumu kwenye maeneo ya mjini kuliko maeneo ya kijijini.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
kama kila mtu kwenye kundi hafuati wengine kwa sababu tu ya wingi wao. Hili
litasaidia kuondoa ile hali ya kufuata mkumbo kwa sababu wengi wanafanya,
itakusaidia kujua nini kimewafanya wengi hao wafanye hivyo. Fanya hivi kabla
ya kufikia maamuzi makubwa na muhimu, usiangalie tu kundi kubwa, bali
angalia kundi hilo linajua nini.
Njia hii ya kwanza nzuri kutumia pale unapojikuta njia panda au ukiwa na hali
ya kutokuwa na uhakika. Badala ya kujiunga tu na kundi, jua kundi hilo
linasimamia nini.
Njia ya pili ni kujiepusha na ujinga wa kundi, pale unapoona kuna jambo halipo
sawa, badala ya kujiambia kuna mwingine ameshachukua hatua, wewe chukua
hatua. Jua kila mtu anafikiria mwingine ameshachukua hatua na hivyo hakuna
anayechukua hatua. Wewe vunja hilo kwa kuwa mtu anayechukua hatua na
hata kama mwingine ameshachukua, hakuna unachokuwa umepoteza.
Kwa ujumla, silaha ya kufuata mkumbo huwa inafanya kazi kwa sababu watu
wanafanya mambo yao kwa mazoea. Hivyo kuepuka kuingia kwenye ushawishi
mbaya kwa silaha hii, mara kwa mara hoji, dadisi na kagua kile ambacho
kinafuatwa na kundi kubwa la watu na jua ukweli wake uko wapi. Utaweza
kufanya hivyo kama utajiweka pembeni na kundi kwa muda na kuangalia
ukweli unaosimamiwa na kundi hilo.
Wengi wanaodhurika kwa kufuata mkumbo, kama waliojiua kwa kushawishiwa
na viongozi wa kidini ni kwa sababu wanakuwa hawapati muda wa kufikiri
wenyewe nje ya kundi wanalokuwepo. Kwa kuwa kila anayewazunguka
anafanya, wanaona ndiyo kitu sahihi kufanya. Lakini wewe ukiwa mtu wa
kukaa nje ya kundi kidogo na kufikiri kwa akili yako, utaona jinsi yale
yanayofanyika yasivyokuwa sahihi.
Na kwenye biashara mbalimbali, nunua kitu kwa sababu una uhitaji nacho na
siyo kwa sababu umeambiwa kila mtu ananunua kitu hicho. Hiyo itakuepusha
kusukumwa kununua kwa kufuata mkumbo.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Rafiki mwizi.
Huwa tunakubaliana kwa urahisi na watu tunaowajua na kuwapenda kuliko
watu tusiowajua au kutokuwapenda. Huu ni msingi wa mahusiano wa kijamii
ambao unatupa njia ya kufanya maamuzi haraka bila ya kufikiri sana.
Kama tulivyoona kwenye silaha nyingine za ushawishi, zote ni njia za mkato
kwetu kufanya maamuzi na zimekuwa na msaada mkubwa kwetu.
Chukua mfano kama ingekubidi ukague nia ya kila mtu unayejihusisha naye
kwenye maisha yako, uchunguze kila mtu kabla hujakubaliana naye,
usingeweza kufanya lolote. Itakuchukua muda mpaka uweze kumchunguza
mtu na kumjua kiundani.
Kuondokana na hilo, tumekuwa na njia ya mkato ambao inatusaidia. Kwa wale
tunaowajua, tunakuwa na uhakika kwama lolote wanalofanya ni kwa wema na
wana nia njema na sisi, hivyo tunakubaliana nao bila kuwachunguza sana.
Kwa marafiki, ndugu na jamaa wa karibu, huwa tunakubaliana nao bila hata ya
kuwachunguza kwa sababu tunajua wana nia njema kwetu, hawawezi kufanya
jambo la kutuumiza.
Na hapo ndipo mwanya wa wale wenye nia ya kutushawishi unapotokea,
wanakuja kwetu wakijifanya ni marafiki zetu, tunawaamini na kukubaliana nao
bila kuwachunguza kwa undani.
Biashara ya mtandao.
Biashara zinazoendeshwa kwa mfumo wa mtandao (network/multilevel
marketing) huwa zinatumia nguvu ya urafiki kuwashawishi watu kununua
bidhaa zao.
Mfumo wa biashara hii unamtaka mtu ajiunge na kuwa mteja, kisha
awashawishi marafiki na watu wake wa karibu nao kujiunga na kuwa wateja.
Biashara hizi huwa zinatoa faida kubwa kwa anayejiunga na kulipa kamisheni
pale anapoweza kuwashawishi wengine nao kujiunga.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Inakuwa rahisi kwa kampuni husika kuuza kwa sababu watu wanatumia
mahusiano yao na watu wao wa karibu kuwashawishi.
Kama umewahi kualikwa uhudhurie mikutano ya biashara hizi, utagundua
ulialikwa na mtu wako wa karibu. Na alipokualika hata kama ulikuwa hutaki
kuenda, hukuwa tayari kukataa, badala yake ulikubali kuhudhuria na huenda
hata kujiunga.
Silaha hii ya kupenda ina nguvu kubwa, ni vigumu sana kumkatalia mtu
unayemjua na unayempenda.
Silaha hii kama ilivyo kwa silaha nyingine inatumia udhaifu wetu wenyewe
kutuangusha. Kwa kutumia mfano wa biashara ya mtandao, unaweza kuwa
huna uhitaji na kitu, lakini ukaishia kukinunua, ndani yako utajishawishi
kwamba umemuungisha rafiki yako, lakini hiyo ndiyo mbinu ya kampuni
husika, kutumia uhusiano wa watu kuuza zaidi.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kwa kujua nguvu ya hili, wale wanaofanya mauzo ya nyumba kwa nyumba,
wakikushawishi ununue, iwe utanunua au la, mwisho huwa wanakuomba
uwape jina la rafiki yako ambaye unaona anaweza kunufaika na ofa nzuri
waliyonayo. Wewe utafutahi kutoa jina la rafiki na wao wanaandika na kisha
kumtafuta.
Wanapofika kwa rafiki yako, wanamwambia tulimtembelea rafiki yako fulani
na amekuchagua wewe pia upate ofa nzuri tunayoitoa. Kwa kutaja jina lako na
kueleza kwamba wewe ndiyo umewaelekeza, rafiki yako anashawishika zaidi
kununua.
Mtu akija kwako na kukuambia rafiki yako fulani amekuchagua wewe unaweza
kunufaika na ofa yetu, unajikuta njia panda, ukisema hapana, hujasema
hapana kwa wauzaji tu, bali umesema hapana kwa rafiki yako, na hilo ndiyo
linaipa silaha hii nguvu.
Kwa kutumia njia hii, makampuni ya mauzo yamekuwa yanatengeneza orodha
kubwa ya wateja na marafiki zao na kuitumia vizuri kushawishi watu wanunue
wanachouza.
Njia nyingine ambayo makampuni hayo yamekuwa yanatumia ni kukupa ofa
kwa kutumia jina la rafiki yako. Watakuambia tuko kwenye mpango wa kutoa
ofa na rafiki yako fulani amekuchagua wewe upate ofa hii. Utaona ni jambo la
heshima, katika watu wote rafiki huyo kukuchagua wewe na hapo
utashawishika zaidi. Wakishakushawishi na ukanunua, wanakuomba uchague
rafiki yako ambaye ungependa pia apate ofa. Hapo wanazidi kupata wateja
zaidi na ambao ni rahisi kuwashawishi.
Pale watu walipoanza kufuatilia ili kujua kwa nini wateja wanampenda sana
Girard kuliko wauzaji wengine, ndipo walipogundua siri, alijenga mahusiano ya
urafiki na ukaribu na kila mteja wake. Girard alikuwa na orodha ya wateja wote
ambao wamewahi kununua kwake na wale ambao analenga kuwauzia. Kisha
kila mwezi alituma kadi moja kwa kila mteja wake, aliyoiandika kwa mwandiko
wake na kuweka sahihi yake.
Kila mwezi alitafuta sababu ya kutuma kadi kwa kila mteja, iwe ni siku yake ya
kuzaliwa, iwe ni sikukuu za kitaifa, za kidini au yoyote ile, alihakikisha mwezi
hauishi bila kila mteja wake kupata kadi kutoka kwake. Alikuwa na malaki ya
wateja, lakini wote waliwatumia kadi hizo.
Hilo liliwafanya wateja kumjua na kumchukulia kama mtu wa karibu na pale
walipohitaji kununua gari hawakufikia mtu mwingine bali Girard.
Mfano wa Girard na ambao umekuwa unatumiwa na wengi, unaonesha jinsi
silaha hii ilivyo na nguvu ikifanyiwa kazi vizuri.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
4. Ukaribu na ushirikiano.
Ukaribu na ushirikiano umekuwa unapelekea watu kupendana. Hata pale watu
wanapokuwa wanatofautiana au hawajuani, wakikaa karibu kwa muda na
kushirikiana kwenye jambo lolote mwisho hujikuta wakipendana na
kukubaliana.
Wale wanaotaka kutushawishi huwa wanatengeneza mazingira ya kuleta
ushirikiano, kujiona tuko upande mmoja na hapo tunakubaliana nao zaidi.
5. Hali na Uhusianisho.
Huwa tuna tabia ya kuwahusianisha watu na hali wanazokuwa nazo. Ule usemi
kwamba mjumbe hauawi siyo kweli, mjumbe anapotuletea taarifa ambazo ni
mbaya, huwa tunamuona na yeye ni mbaya, hata kama yeye ameleta tu taarifa
na hahusiani nazo.
Huwa tuna tabia ya kusianisha watu na vitu au hali fulani wanazoendana nazo.
Mfano mzuri ni wasomaji wa utabiri wa hali ya hewa, pale wanaposoma taarifa
kwamba hali ya hewa itakuwa mbaya, watu huwa wanawachukia wao kama
vile ndiyo wameleta hali hiyo mbaya.
Kwa kujua hili, wale wanaotaka kutushawishi huwa wanahakikisha
wanajihusisha na vitu vizuri tu ili tuwapende na kukubaliana nao.
Hii imekuwa inatumika sana kwenye matangazo, bidhaa au huduma
inahusianishwa na kitu ambacho tayari mtu anakipenda.
Mfano mzuri ni wasanii na watu maarufu wanapochaguliwa kuwa mabalozi wa
taasisi au biashara fulani, au wanatumika kwenye matangazo. Kinachofanyika
hapo ni kuwafanya wale wanaowapenda wasanii na watu hao maarufu,
kupenda pia bidhaa ambayo wanaonekana kuitumia. Kwa kuwa unampenda
msanii fulani na kwa kuwa umemuona kwenye tangazo la kitu fulani, moja kwa
moja unakipenda kitu hicho pia.
Hili huwa linafanya kazi hata kama kinachotangazwa hakina uhusiano na
umaarufu wa mtu. Mfano msanii maarufu wa muziki anaweza kuwa kwenye
tangazo la vinywaji, sabuni au chochote na bado tukavipenda vitu hivyo kama
tunavyompenda msanii huyo.
Wanasiasa na washawishi wengine wamekuwa wanatumia nguvu hii ya
uhusianisho kuhakikisha wanaweza kuwashawishi watu. Wanachofanya ni
kutafuta kitu ambacho watu wanakipenda na kisha kutengeneza uhusiano
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Ushabiki wa timu.
Ushabiki wa michezo mbalimbali umekuwa na nguvu kubwa kwa watu. Mtu
anayeshabikia timu huwa anajihusisha na timu hiyo kabisa, hata pale timu
inaposhinda mtu anasema tumeshinda, kama vile alikuwa uwanjani.
Hii yote inatokana na nguvu ya silaha ya kupenda, pale mtu anapokipenda kitu
kutoka ndani ya moyo wake, anakiona kama ni kitu chake au anashiriki moja
kwa moja hata kama siyo kweli.
Kadiri mtu anavyoipenda timu yake, ndivyo nafsi yake inavyojiona kupitia timu
hiyo. Ndiyo maana baadhi ya mashabiki wanaweza kufanya hata mambo
ambayo ni hatari, kwa sababu wanajiona kama vile wao ndiyo timu zao. Wapo
wanaofikia hatua hata ya kujiua, kwa sababu wanakuwa wamemezwa nafsi zao
na timu zao.
Kinachopelekea watu kupenda sana timu au kitu wanachoshabikia ni kwa
sababu ya kutaka kuhusianishwa na mafanikio ya kitu hicho. Iko hivi, washabiki
kindanindaki wa kitu chochote kile, ni watu ambao hawana mafanikio
makubwa kwenye maisha yao. Hivyo mafanikio ya kile wanachoshabikia huwa
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
wanayahesabu kuwa mafanikio yao. Ndiyo maana huwa wanataka sana kile
wanachoshabikia kifanikiwe, maana wanakitumia kupima mafanikio yao.
Kila mtu huwa anapenda kuwa sehemu ya ushindi, hivyo pale ambapo mtu
hana ushindi kwenye maisha yake, anachagua kitu cha nje ambacho anaweza
kujihusisha na ushindi wake na hapo ndipo ushabiki mkubwa unapozaliwa.
Tafiti zinaonesha pale timu inaposhinda, watu wengi zaidi huvaa jezi za timu
hiyo kuliko timu iliyoshindwa. Yote hiyo inaonesha jinsi gani tunapenda
kujihusisha na mafanikio ya wengine.
Hata lugha inayotumika huwa ni tofauti kwenye ushindi na kwenye kushindwa.
Timu inaposhinda mashabiki wake hutumia lugha ya umiliki, husema
‘tumeshinda’ lakini timu inaposhindwa hawatumii lugha ya umiliki, badala yake
wanajitenga na timu kwa kusema ‘timu imeshindwa’ na siyo tumeshindwa.
Tafiti zinaonesha kadiri mtu anavyokosa ushindi ndani yake, ndivyo
anavyotafuta ushindi wa nje wa kujihusianisha nao. Mfano wapo wanaoenda
hatua ya ziada na kununua tiketi za mchezo ambao hawakuhudhuria ili tu kuja
kuwaonesha wengine kwamba walihudhuria mchezo huo. Kitu kama hicho
kinawafanya waonekane nao kuna kitu wamefanikisha, hata kama siyo kweli.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007