Professional Documents
Culture Documents
2
“Ikiwa upo kwenye mitandao ya Kijamii na hujifunzi, hucheki,
huhamasiki na hujengi mtandao na watu, basi unaitumia vibaya.”
~Germany Kent
CHUO KIKUU
CHA
GOOGLE, LINKEDIN
NA
YOUTUBE
MAMBO 10 MUHIMU AMBAYO HUJAWAHI
KUAMBIWA KUHUSU MITANDAO YA KIJAMII
EDIUS KATAMUGORA
3
CHUO KIKUU
CHA
GOOGLE, LINKEDIN
NA
YOUTUBE
4
SHUKURANI
5
Natamani kusoma vitabu na Yusufu Nina
Ndoto na vingine vilivyopo nyuma ya kitabu
hiki.
6
UTANGULIZI
Je umewahi kutamani kuwa mtu wa hamasa
mtandaoni? Kama jibu ni ndiyo kitabu hiki ni
kwa ajili yako? Je unafahamu kwamba kupitia
mitandao ya kijamii unaweza kujifunza mambo
mengi zaidi ya darasani? Wakati naandika
utangulizi huu nilikua nachati na rafiki yangu
mmoja ambaye tumejuana siku za hivi karibuni
mtandaoni, akaniambia yeye anafahamu lugha
ya Kifaransa nikamuuliza ulisoma shuleni,
akanijibu, “Nimesoma vitabu na kujifunza
mtandaoni,” Mitandao ni vyuo vikuu ambavyo
wengi hawajavifahamu. Kama bado hauamini
katika hayo soma kitabu hiki mpaka mwisho.
7
mabadiliko makubwa utayaona katika maisha
yako.
8
nami mara huhitajipo msaada kuhusu kitabu
hiki.
9
TAARIFA MUHIMU
MWANDISHI WA KITABU HIKI
AMECHAGULIWA KUWANIA TUZO
ZA WAANDISHI BORA WA VYUO
VIKUU.
https://www.instagram.com/p/B-
rlirXATeg/?igshid=pmz7cwp549lx
10
1. YAH: GOOGLE, LINKEDIN NA
YOUTUBE NI VYUO VIKUU. ADA
NI BANDO LAKO
Ukisoma kitabu changu cha PUMBA ZA
EDIUS {MAMBO MUHIMU
TUNAYOYACHUKULIA POA
MAISHANI} utakutana na maneno niliyoanza
nayo hapo juu. Maneno hayo niliwahi
kuyaandika facebook ingawa wengi
hawakunielewa.
11
Toka hapo nimekuwa muumini mzuri wa
kuwahasa watu watumie intaneti kwa matumizi
sahihi ingawa bado wengi hawajajua matumizi
yake, wanakuwa kama mimi siku za mwanzo.
Imani yangu kubwa huwa inakwenda na
msemo huu wa kiingereza kuhusu intaneti,
“The Internet is the future,” ni kimaanisha
kwamba intaneti ni wakati ujao au wakati ujao
umebebwa na intaneti.
12
mwanafunzi anayekaa darasani akisubiri
profesa aje kumfundisha.
Tuanze na Google:
“Google kila kitu. Namaanisha kila kitu.
Google ndoto zako, google matatizo yako.
Usiulize swali kabla haujaligoogle, utapata
jibu au utapata swali bora zaidi,” anasema
Austin Kleon mwandishi wa vitabu.
13
na naona wananishangaa lakini vyote hivyo
huwa navitoa google. Nikupe mfano tu
nimejifunza namna ya kutangaza matangazo ya
Facebook na Instagram kwa kutumia google.
LINKEDIN
“LinkedIn leo ni kama Facebook 2012.”
~ Gary Vee
Siku ya kwanza kuandika kuhusu LinkedIN
nilishangaa kuona watu wengi hawaujui
mtandao huo. Kiufupi LinkedIn ni mtandao
wa kijamii kama zilivyo WhatsApp, Twitter,
15
Tiktok na Instagram. Kutojulikana kwa
LinkedIn ni kwamba huo ni mtandao wa watu
wenye kazi (professions) mbalimbali. Ni
mtandao wa wabobezi kwenye sekta
mbalimbali. LinkedIn hakuna vichekesho
huko.
16
Leo hii ni kinyume, ukijiunga tu na facebook
wataanza kukuonesha watu walio kwenye
mawasiliano yako kwanza. Leo karibia kila mtu
yumo facebook.
17
sehemu ya kutafuta watu wa kuwapa kazi basi
ujue kwamba mtandao huo sio wa kitoto.
21
2. KUWA NA WAFUASI WENGI
MTANDAONI HAIMAANISHI
KWAMBA UNAWEZA KUUZA AU UNA
HAMASA KUBWA KWAO
Kitu kikubwa ambacho watu wengi wanalilia
mara nyingi mtandaoni ni kuwa na followers
wengi.
Kuwa na followers wengi hakuna maana
yoyote kama hauwezi kuwabadili hao followers
kuwa wateja wa kazi zao.
Ukweli lazima usemwe, Likes haziliwi,
kuonekana maarufu mtandaoni wakati hauna
pesa mfukoni ni upuuzi.
Watu wengi wana wafuasi wengi mitandaoni
lakini wanashindwa kuwabadili kuwa wateja wa
kazi zao.
Umewahi kusikia mtu aliyekuwa na wafuasi
milioni 2.6 instagram na akashindwa kuuza
22
tisheti 36? Ndiyo wafuasi milioni 2.6 wala
sijakosea.
Arianna Renee aliyekuwa na wafuasi milioni 2.6
instagram anayetumia jina la @arii alishindwa
kuuza brand yake ya Tisheti inayojulikana kama
ERA kwa wafuasi wake hao mamilioni.
Unaweza kujiuliza mtu huyo alishindwaje
kuuza Tisheti hizo chache wakati ana wafuasi
wengi. Jibu ni moja hakuwa mtu anayetoa
thamani (value) kwa watu wake.
Ukitaka kuwa na wateja kupitia mitandao ya
kijamii toa thamani hata ukiwa na watu 1000
wanaoamini kwenye thamani unayoitoa tayari
wewe ni tajiri. Sikuzote unapokuwa unataka
kuwa na wafuasi wengi kwenye mitandao
kumbuka watu wanakufuata kwa ajili ya
thamani unayoitoa.
23
3. MAUDHUI NI MFALME
Katika kipindi hiki tulichomo ambacho kila
mtu anamiliki simu janja (smart phone) ni
muhimu kukumbuka hili Maudhui ni Mfalme.
Maudhui ndiyo pesa.
Kwa wastani mtu mmoja hutumia karibia saa 5
mtandaoni watu hawa huwa wanatafuta
maudhui yaliyobora. Mtu mwenye maudhui
bora ndiye anayepewa jicho kubwa mtandaoni.
Ili upewe jicho kubwa mtandaoni maudhui
(content) yako yanahitaji kuwa ya kipekee.
Ukiwa na maudhui ya kutoa kwa watu wengine
tambua kwamba watu wakijua unakoyatoa
watakimbilia huko.
Amini pia kwenye unachokifanya, kifanye na
watu wanaopenda kitu unachokifanya
watajileta kwako.
24
Nitakupa mfano mdogo nilianzisha kuandika
misemo niliyoipa PUMBA ZA EDIUS katika
mtandao wa facebook mwanzoni watu
hawakunielewa nikapata vipingamizi vingi
kwamba nakosea. Baadaye nikaamua
kutengeneza kitabu, kitabu hicho kwa muda wa
wiki mbili kimewafikia zaidi ya watu elfu 30.
Tena kwasababu nilikuwa natoa kitabu hicho
bure baadhi ya walioomba kitabu hicho ni wale
ambao walinibeza wakisema nakosea. Pointi ya
kuchukua hap ani kwamba amini kwenye kile
unachokifanya.
Jambo jingine la kufahamu kuhusu maudhui ni
kwamba kadri unavyoendelea kuposti ndivyo
watu wanazidi kuvutiwa na wewe ndivyo watu
wanazidi kukufahamu. Usitegemee kuposti kit
umara tat una uache eti watu watajua unafanya
nini, hilo halihitaji miujiza. Miujiza
unaitengeneza kwa kuposti mara nyingi kadri
uwezavyo kama upo kwenye mashindano
25
ukilala wenzako wanaamka. Ukiacha kuposti
watu wanakimbilia kutazama wengine.
Waingereza wanasema, “Consistency is the
key,” yaani kuendelea kufanya kitu bila kuacha
ndiyo ufunguo.
26
4. WHATSAPP NI DUKA
WANALOLITUMIA WACHACHE
Pamoja na kuchelewa kuifahamu na kuitumia
vizuri WhatsApp business mimi ni
mmojawapo wa waliofanya biashara kupitia
whatsapp ya kawaida. Nimeuza vitabu,
masweta, tisheti nimetangaza biashara za watu
na wamepata wateja.
Siku si nyingi zilizopita tuliunda kundi la
whatsapp liitwalo DREAM TEAM katika
kundi hilo tunatangaza biashara ya mtu mmoja
kila siku kwenye kundi kupitia status, hii
imetuwezesha kuwafikia wateja wengi ambao
hata kabla hatukuwahi kutarajia.
Inawezekana unaona sehemu ya status kama
sehemu ya kuposti memes na vichekesho
wenzako wanaona sehemu ya kutangaza
biashara. Amka sasa usisubiri upate fremu
ndipo uanzishe biashara yako nawafahamu
27
wengi ambao kupitia biashara zao
wanazozifanyia nyumbani kwao wameweza
kukuza brand zao kupita mitandao ya kijamii na
kuwafikia watu wengi.
Huwa nashangaa mtu ana views zaidi ya 200
kwenye status za whatsapp na analia njaa.
Kama wewe ni mmojawapo unafanya makosa
makubwa. Kati ya hao watu 200 ukipata walau
wateja kumi wa biashara yako hauwezi kulilia
njaa. Amka sasa anza kufikiria whatsapp kwa
picha ya tofauti. “Ukibadili unavyofikiri
unabadili unavyozalisha,” anasema Askofu
Joel Osteen. Badili leo unavyofikiri kuhusu
Whatsapp.
Nafurahi kuona leo baadhi ya watu wanaweza
kuwa na madarasa katika makundi ya whatsapp
ili mtu ajiunge na makundi hayo na kupata
elimu ya watu hao kuna kiasi anabidi kuchangia
ilia pate huduma hizo. Jiulize wewe unajua nini
28
ambacho unaweza kukifanya kama darasa
mtandaoni?
29
TAARIFA MUHIMU
MWANDISHI WA KITABU HIKI
AMECHAGULIWA KUWANIA TUZO
ZA WAANDISHI BORA WA VYUO
VIKUU.
https://www.instagram.com/p/B-
rlirXATeg/?igshid=pmz7cwp549lx
30
5. Mashabiki 1000 wa Ukweli
Dhana hii ya mashabiki 1000 wa ukweli
inatokana na makala iliyoandikwa na Kevin
Kelly mwaka 2008
Hii ni kwa waandishi, wanamuziki, mabloga,
wanotengeneza video za Youtube, na wote
wanaotengeneza kitu chochote. Ukweli ni
kwamba hauhitaji kuwa na mjomba
atayekukopesha ili uanzishe biashara. Hauhitaji
kuwa na wafuasi milioni ili kuanzisha baishara.
31
Kama ukiamua kutengeneza shabiki mmoja
kila siku itakuchukua miaka 3. Kitu cha
kuzingatia hapa ni kuwa na mawasiliano
endelevu kila mara.
32
6. JINSI YA KUUZA NA
KUTENGENEZA BRAND YAKO KWA
KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII
Zama zimebadilika, mambo yamebadilika.
Ujio wa intaneti umefanya mapinduzi
makubwa katika biashara hasa kwa karne
hii ya ishirini na moja. Utangazaji wa
biashara kupitia magazeti na televisheni
kwa kiasi kikubwa hauna nguvu tena kama
ilivyokuwa hapo zamani.
35
kupata connection kubwa ambazo hata kabla
ulikuwa huzitarajii.
36
3. Kuwa mtu wa watu. Ukiwajali watu
watakujali pia. Unahitaji kuwa mtu wa watu
katika mitandao ya kijamii. Wajibu watu kwa
heshima, tumia maneno kama; kaka au dada
yanasidia sana. Asikwambie mtu watu
wanapendwa kuheshimiwa. Ukiwapa heshima
watakuja kwako.
38
MAMBO YA KUFAHAMU KABLA
KUANZA KUTUMIA MITANDAO YA
KIJAMII KUJITANGAZA:
· MALENGO:
Unahitaji kuanza kwa kuandika malengo yako
kwanini unataka kutumia mitandao ya kijamii
kujibrand na kufanya biashara. Hatupangi
kushindwa tunashindwa kupanga, watu wengi
hawapangi ndiyo maana malengo yao
hayatimii.
· Ni wapi wanapatikana.
Ukijua ni mitandao gani wateja wako
wanapatikana hakikisha unawafata huku. Hapo
utakuwa umelishika soko lako.
39
MAMBO YA KUZINGATIA:
1. Uaminifu.
Kama hautakuwa mwaminifu katika kazi zako
ni bora usifanye biashara kupitia mitandao ya
kijamii. Uaminifu ni nguzo kubwa katika
kufanya biashara kupitia mitandao.
2. Kanuni ya 7/1
Kama katika post unazoziweka katika
mitandao yako ya kijamii hakikisha post 6
zinazungumzia au kuelezea bidhaa zako na
ujuzi wako na post moja ambayo ni ya saba
ndiyo iwe tangazo la bidhaa yako. Ukiwa mtu
wa kutangaza bidhaa tu utawaboa watu na
wataacha kukufatilia. Weka vitu vingi
vinavyowaelimisha na ndipo uweke matangazo
ya bidhaa zako.
3. Kuwa muwazi.
Ukionekana kwenye mitandao ya kijamii
onekena kama mtaalamu. Usionekane kama
40
watu wengine. Kumbuka watu wanhukumu
kava ya kitabu na ni kilicho ndani ya kitabu.
4. Unahitaji kuwa mbunifu. Usifanye mambo
kwa mazoea, kila siku jiulize swali ili:
nitafanyaje kwa ubora Zaidi ya jana? Hilo ni
swali unalopaswa kujiuliza kila siku.
42
7. The Internet Is The Future
Jumanne ya tarehe 22 Julai mwaka 2019 nilipata
fursa ya kufundisha somo linaloitwa
INTERNET IS THE FUTURE katika kundi
la whatsapp lijulikanalo kama CYM
International
43
Njia nzuri ya kuwa kwenye sehemu nzuri ya
kuununua wakati ujao(buying the future) ni
kuwa kwenye intaneti.Nimekua nikiwaambia
watu, na nimeandika sana. Badala ya kuitumia
intaneti yenyewe inatutumia.
44
biashara yako unayoifanya haipo mtandaoni
biashara hiyo haipo. It doesn't exist.
Kuanzia
AMAZON
FACEBOOK
ALIBABA
KIKUU
YOUTUBE
UBER
TAXIFY.
NETFLIX
46
Facebook Twitter na Linkedin. Anayeuza
bidhaa ni rahisi sana Instagram kuliko Twitter.
Unawafundishaje?
51
hebu kaangalie Millard Ayo kwa siku anapost
mara ngapi.
53
TAARIFA MUHIMU
MWANDISHI WA KITABU HIKI
AMECHAGULIWA KUWANIA TUZO
ZA WAANDISHI BORA WA VYUO
VIKUU.
https://www.instagram.com/p/B-
rlirXATeg/?igshid=pmz7cwp549lx
54
8. ENDELEENI KUSEMA FACEBOOK
NI YA WATOTO
55
1. Unatumia facebook?
2. Au ntauliza facebook unatumia jina gani?
56
Jibu ninalokupa leo ni kwamba facebook sio
ya watoto. (Naomba uwatag wote waliowahi
kukuambia majibu kama hayo hapa.)
Je unayajua haya?
57
Leo hii kama facebook ingekuwa nchi,
ingekuwa nchi ya kwanza duniani kwa kuwa
na idadi ya watu wengi. Facebook
inawatumiaji bilioni 2.38 kwa mwezi, wakati
nchi ya China yenye watu wengi inakadiriwa
kuwa na watu bilioni 1.4
58
Watu wengi wanaotumia mtandao huu ni
kuanzia miaka 25-34, ambao ni asilimia 29.7
ya watumiaji.
59
Wastani wa kila mtu kutumia facebook ni
dakika 20.
60
Kupitia facebook unaweza kutangaza biashara
yako kwa bei rahisi, hata kwa kupitia ukurasa
wako na bado ukapata wateja. Leo hii
kutangaza kupitia redio, Magazeti na
televisheni ni mambo yaliyopitwa na wakati.
Kwa kutumia dola moja kwa siku unaweza
kuwafikia zaidi ya watu 5000 kwa kutangaza
biashara yako na ukapata wateja. Jambo
jingine matangazo ya facebook yanakufanya
uwafikie wateja wa mbali zaidi bila ukomo.
Waliokuwa mnasema facebook ni ya watoto,
mnakwama wapi?
61
9. UNAWAJUA KIZAZI Y?
Inawezekana ni neno geni kusomeka au
kusikika masikioni mwako lakini ni vyema
uwafahamu watu hawa. Kwa jina jingine
wanafahamika kama kizazi za milenia kingereza
chake kikiwa Generation Y (Gen Y). Hawa ni
watu waliozaliwa kuanzia miaka ya 1982 hadi
kufikia mwaka 1994. Hawa ni watu muhimu
sana kwa sababu jinsi wanavyounhanishana na
kuwasiliana imeleta mabadiliko makubwa
katika ufanyaji wa biashara.
Kama unaanda mpango biashara ambao
haujalenga kizazi hicho jiandae kupata tabu
sana. Serikali pia inahitaji kuwapa jicho la tatu
watu hawa.
Kama umewafahamu je, unajua tabia zao?
Twende sasa nikupe tabia za kizazi hiki cha
milenia.
Moja, ifikapo mwaka 2025 asilimia 75 ya kizazi
Y ndio watakuwa watendaji kazi, ndio
62
watakuwa wameajiriwa au wamejiajiri. Hawa
ndio watakuwa wameshika mzunguko wa
fedha, ndiyo maana nikasema kuwa na mpango
biashara bila kuwatizama wao jiandalie kifo cha
biashara yako.
Kizazi cha milenia kinatizama TV kwa kutumia
kifaa cha kielectronic zaidi ya kimoja.( Kuna
haja ya kuwa na online TVs kwa wamiliki wa
vituo vya television). Hawatizami TV san ana
hawasomi sana lakini wanasikiliza zaidi kile
marafiki zao wanachokisema.
Kizazi za milenia huwaamini zaidi watu wa
mbali na walipo zaidi ya marafiki wa karibu na
hata familia. Hawa wanaweza kununua kitu
kwa kutizama ni nani kakitumia ambaye ni mtu
maarufu.
Wanaweza kufuata(kufolo) brand mtandaoni
Mara tatu zaidi kuliko kumfuata mtu wa karibu
wa kwenye familia yao. (Ukiwa na brand
iliyosimama watakufuata tu)
63
Asilimia 66 yao wataingia kwenye duka fulani
kununua bidhaa kama watamwona rafiki yao
akiwa humo. (Watanunua bidhaa kama
wataona rafiki yao akitumia bidhaa hiyo)
Kizazi za milenia huamini kuwa watumiaji
wenzao wa bidhaa wanajali zaidi ya
mfanyabiashara anayeuza bidhaa, hivyo
huweka maoni yao mtandaoni kuhusu bidhaa
hiyo. (Kuna wakati kampuni ya Tigo ilianzisha
kampeni ya JAZA UJAZWE. Hawa ndio
walikuwa watu waliokataa kampeni hiyo kupitia
mtandaoni hivyo haikudumu)
Wanatumia sana Facebook na Instagram zaidi
ya watu wengine.
Kizazi Y hupenda “Uzoefu” kwanza
wanapenda wakitumie kitu kwanza ndipo
watakaposema wanakipenda ama hawakipendi.
Ni watu wa kidunia sana kwasababu teknolojia
imekuwa sehemu ya maisha yao.
64
Utauzaje kwa kizazi hiki? Wataalamu wanaodili
na kizazi hiki, yaani kizazi Y wanatoa vigezo
muhimu ili watu hawa wawe wateja wako.
• Gharama ndogo
• Ubora
• Huduma ya haraka (fast service)
• Uzoefu “experience”
Kizazi Y wapo konektedi sana mtandaoni zaidi
ya vizazi vilivyowahi kuwepo au wazazi wao.
Kwa kutumia intaneti wanaweza kujifunza
chochote saa 24 kwa siku.
65
WAFAHAMU PIA KIZAZI Z
Hawa walizaliwa kati ya mwaka 1995-2004.
Usichokijua ni kwamba watu hawa
wanakamilisha asilimia 18 ya watu wa dunia
nzima. Waitwa Generation Z.
Ingawa bado ni wadogo bado wanauwezo wa
kupata teknolojia na vifaa kama simu, iPods,
tablets na kompyuta na teknolojia hii ndiyo
inatoa taswira ya maisha yao.
Hawa ndio kizazi cha digitali. Wamekulia katika
kizazi cha usawa, wanaamini kwamba
wanaume na wanawake wote ni sawa.
69
10. EPUKA KUSHIKA SIMU YAKO
MARA TU UNAPOAMKA
71
Hakikisha walau dakika 30 za kwanza baada ya
kuamka haushiki simu na unajiweka bize na
mambo ya msingi.
73
wa mitandao. Mitandao ya kijamii haikujengwa
ili sisi tuwe walevi wake.
75
TAARIFA MUHIMU
MWANDISHI WA KITABU HIKI
AMECHAGULIWA KUWANIA TUZO
ZA WAANDISHI BORA WA VYUO
VIKUU.
https://www.instagram.com/p/B-
rlirXATeg/?igshid=pmz7cwp549lx
76
KUHUSU MTUNZI
77
Mwandishi amekuwa mkereketwa wa
mabadiliko ya watu katika jamii hivyo
kupitia maandiko yake maisha ya watu wengi
yamebadilika.
78
3. Kijana wa Maarifa
4. Kijana Jithamini (Ameshirikishwa
pamoja na waandishi wengine)
79
5. YUSUFU NINA NDOTO
80
KITABU HICHO HAPO JUU
KINAPATIKANA BURE
81
82
Mawasiliano:
EDIUS KATAMUGORA
0764145476
0758594893 (WhatsApp).
ekatamugora@gmail.com
Instagram:@ediuskatamugora
83
OMBI
MWISHO
84