You are on page 1of 47

NAJIFAHAMU

FURAHA YA KUWA MIMI

Na Mwanagenzi Michael The Great one.

1
YALIYOMO:
1. UTANGULIZI……………………… 3

SURA YA KWANZA.

1. Mimi ni nani?.......................................4-7
2. Ninajengaje fikra njema niwe mwema…8-12

SURA YA PILI.

1. Aina ya vipaji na namna ya kufahamu vipaji vyako….13-16


2. Njia nyingine nzuri za kufahamu vipaji vyako…………17-24

SURA YA TATU.

1. Jenga tabia bora nayo itakujenga kuwa bora….25-29

SURA YA NNE.

1. Misongo mdudu anayekula uhai wa wengi……….30-31


2. Aina ya misongo na namna ya kukabiliana nayo….32-38

SURA YA TANO.

1. Maisha ya mafanikio na furaha………………39-43


2. Viambata vya mafanikio……………………….44-45
3. Mwisho ……………………………………………..47-47

2
UTANGULIZI.

Maisha ya kiumbe pasipo kujifahamu ni sawa na kuishi kwenye lindi la maisha


ya mateso kwakua unaishi kwa kuigiza nje ya uhalisia wako na kwa hakika
utakuwa na nafasi ya kutokufurahia maisha yako, pamoja na kwamba safari
ya kujifahamu ni miongoni mwa safari ngumu ambayo kila kukicha
wanadamu wanapaswa kuifanya ili waweze kuishi uzuri na kuwa na maisha ya
furaha , nimekuandikia kitabu hiki kukupatia hamasa ya kuendelea
kujifahamu na uanze kuishi uzuri wa maisha yako na kuona tumaini kubwa
maishani mwako na uwe kiumbe cha maana sana hapa duniani,wewe ni mtu
bora sana kwenye ulimwengu huu na hakuna mwenye kukufikia kwa uzuri na
ubora wako kama tu utajifahamu.

Karibu nikualike kwenye safari mpya ya kujifahamu na kuanza kuishi wewe


hapa duniani.

3
SURA YA KWANZA

1
MIMI NI NANI?

~Wewe ni matokeo ya fikra zako. ~

K
atika kutambua mzizi wa matatizo yetu, na ukweli wa kuyahusu
maisha yetu kujitambua ni moja ya jambo muhimu sana.

Kiumbe Mwanadamu hata akitambua kuna Mungu wa kweli ama kuna


sayari ngapi? jua nini ?, akatambua pia kuna nyota ngapi?, akajua pia kuna
viumbe wangapi majini na hata akajua Rais aliyefanikisha kupatikana kwa
uhuru wa Tanganyika na akafahamu na nchi yake inazo mbuga ngapi?.

Mambo hayo hayatafaa kitu kama binadamu huyu hatakuwa na utambuzi wa


kuwa yeye ni nani?, Kwakua Hawezi kuwa na hekima na maarifa sahihi juu
ya kitu gani anaweza kutokeza kwenye maisha yake na kwa namna gani
anaweza kutokeza kitu hicho na kuanza kukiiishi na kikayapatia maana
maisha yake na kutoa mguso wa ajabu kwa maisha ya wengine.

Pamoja na kwamba kujitambua ni moja ya mazoezi magumu sana kwa


binadamu kutokana na namna alivyozaliwa na kutengenezwa, lakini ni moja
ya jambo la kutilia mkazo sana sana kwenye safari ya binadamu ya maisha
yake ya kuwepo hapa duniani ikiwa ni pamoja na wewe.

Kujitambua ni moja ya jambo linalohitaji juhudi sana kwakua ni moja ya


jambo litakalokusaidia kutenda mambo yaliyo sahihi na kwa hekima katika
maisha yako.

Mtu anayejitambua na kufahamu kuwa yeye ni nani na yupo hapa duniani kwa
kusudi gani?, atakuwa na ufahamu wa juu kuhusu maisha yake na ya wengine
na kwa kufahamu hilo atakuwa na uchukuaji mkubwa wa hatua za kimaisha.

4
Kuelekea safari ya kujitambua inahitaji kuacha kuamini watu
wanavyokusema na kukuona, bali inahitaji kujitafuta wewe na kuja ukiwa
wewe na kuiambia dunia niiteni kwa jina hili na nitambueni kwa jina hili,
mimi ni huyu futeni yale yote mliyokuwa mkiinita kuwa mimi ni
mshindwaji, kuwa mimi ni asiyejua kitu, kuwa mimi ni mhangaikaji
tu nisiye na maana, kuwa mimi si lolote wala chochote, waambie
wafute hayo majina na waanze kukuona katika muono mpya na muonekano
mpya wenye nguvu zako na wenye uwezo wako wote.

Unahitaji kufahamu mambo muhimu matatu juu yako kuelekea utambuzi wa


juu kukuhusu wewe. Mambo haya matatu yatakupatia maana halisi kuhusu
wewe na kukufanya uwe wa maana, kwakua yatakupatia wewe halisi na mtu
bora sana kwenye jamii hii na kuanza kutokeza makubwa ambayo dunia
inakusubiri tu wewe uanze kuyafanya na kuishi uwezo wako wa juu.

Kumbuka wewe si mwili huo ulio nao, na wewe si jina hilo unaloitwa, wewe ni
zaidi ya hayo na wewe unatambulika kwa mambo haya matatu muhimu;-

i) Akili yako (fikra zako).


ii) Hisia zako.
iii) Matendo yako.

Unahitaji kuifahamu akili yako vyema, na kufahamu akili vyema itatokana na


ufahamu wa mawazo yako unayo yawaza muda mwingi kwenye maisha yako.
Kwamba una mawazo gani ambayo ni zao la fikra zako (akili) huyo ndiye mtu
wa kwanza kumfahamu. Kwamba linapokuja tatizo mtu huyu hujiendesha
kwa namna gani? Hukimbia tatizo na kutafuta visingizio ama huyakabili
matatizo akiwa mwenyekujiamini kuwa anao uwezo wa kutosha kuyaondoa
matatizo yake ya kimaisha yanayomkabili na yeye ndiye mwenye kujiambia
kuwa mimi ndiye majawabu ya matatizo yangu na nipo tayari kuondoa kila
kitu kinachonizuia na ninao uwezo mkubwa sana dhidi ya matatizo yanayo
nikabili kwenye maisha yangu.

Siku moja mchungaji, mhamasishaji mkubwa na tajiri sana marehemu Dr


Myles Munroe alisimulia simulizi la kufurahisha sana juu ya watu
wanavyopaswa kujifahamu ili waweze kuishi maisha bora na maisha yao
halisi na kwakua wanaishi maisha ya kutokujifahamu wamebaki wakifikiri
kuwa wao hawana uwezo wa kuishi maisha mazuri kwakuwa uwezo huo wa
kuishi maisha hayo wanao tena ni mkubwa tu na upo ndani yao.
5
Kwakua hawafamu kama wana uwezo huo wameamua kuishi maisha ya
ajabu ajabu na kupoteza uwezo wao huo mkubwa kwa kutokuufahamu tu,
Dr Myles Munroe anasema siku moja alialikwa kwenda kufundisha kwa
rafiki yake kwenye moja ya nchi za kitajiri sana. Alikwenda kufika huko
walipatiwa huduma zote zilizokuwa zinahitajika kama mgeni waalikwa
moja ya huduma ya kufurahiwa ilikuwa ni kupelekwa kwenye matembezi ya
kutalii na gari kwenye mji mkubwa wa nchi hiyo, anasema walipakiwa
kwenye gari zuri tu lenye hadhi ya juu sana, anasema walipofika kwenye
moja ya barabara zinazoruhusu kuendesha bila kufuata sheria ya spidi
mchungaji Dr Myles alipewa aendeshe gari lile, wakati anaanza kuendesha
alikuwa anaendesha kwa mwendo mdogo na wakawaida, mwenyeji wake
akamwambia ongeza mwendo, mchungaji Dr Myles aliongeza mwendo
kuitikia itikio la mwenyeji wake , mwenyeji wake alimwambia ongeza bado,
ongeza tena, mchungaji Dr Myles akaongeza mpaka ikafikia spidi mia moja
na ishirini anasema gari ilikuwa inakimbia balaa , mwenyeji wake
akamwambia tena ongeza bado, mchungaji Dr Myles akaongeza tena gari
ikaenda kwa kasi sana akashangaa kuona anayapita tu magari mengine na
huku akicheka kwa raha ya mwendo wa gari linavyokwenda kasi zaidi
kuangalia kwenye kioo cha spidi aliona spidi mia moja na themanini,
mwenyeji wake akamwambia bado hajamaliza spidi za gari husika kwa
maana ya uwezo wa gari kwenda mwendo hadi wa mwisho
liliotengenezewa nao kutoka kiwandani , mchungaji Dr Myles
anatushirikisha kuwa toka siku hiyo alijifunza jambo muhimu sana kwenye
maisha yake kuwa maisha tunayoishi kwa kufikiri hatuna uwezo mkubwa
wa kufanya makubwa wakati aliyetuumba toka kiwandani ametupatia
uwezo mkubwa sana na kama tutagundua uwezo huo na kuanza kuutumia
tutashangaa kuona magari (watu) mengine tunayapita tu na wakati huohuo
tunakuwa hatujataka kutumia uwezo wetu wote mpaka mwisho.

Kwa mjibu wa wanasayansi wanasema ubongo wa binadamu una uwezo


mkubwa sana kiasi cha ukubwa wa neva bilioni kumi na nne ambazo zinaweza
kuchukua na kutunza taarifa au mambo mbalimbali ya muhimu kwenye
maisha ya binadamu.

Na kama tu ataamua kujifunza jambo lolote ubongo wake utamwambia ipo


nafasi na hauwezi kuijaza, na inasemekana kuwa binadamu mpaka anakufa
anakuwa ametumia uwezo kidogo sana wa kiuwezo wake.

6
Kwahivyo jambo la kwanza na muhimu sana kwenye safari ya kujitambua
unapaswa kukubali na kukili kuwa unao uwezo mkubwa sana wa kufanya
mambo makubwa na inategemea akili yako ina nini?, maswali ya kujiuliza ni
kuwa unaipatia na kuilisha mawazo gani ? mambo ambayo yanatengeneza
msingi wa kuwa wewe.

Ni wakati muafaka sasa kuanza kuipatia akili mambo mazuri kwa maana ya
kuchunga sana taarifa unazozipokea na ambazo mara kwa mara unaulisha
ubongo wako kwakua hizo ndiyo hugeuka kuwa wewe kwa kujionyesha
kwenye hisia zako na matendo yako. Kwamba hisia zako na matendo yako ni
zao la akili (fikra) zako na kama utakuwa mwenye akili njema basi utakuwa na
hisia njema na matendo mema na mwisho kuwa mtu mwema na mwenye
kujitambua.

7
SURA YA KWANZA

2
NINAJENGAJE FIKRA NJEMA ILI NIWE MWEMA?

U
jengaji wa fikra njema (akili) njema ndiyo jambo muhimu la kufanya
kuelekea ujitambuaji wa juu, safari hii inakutaka kuanza kuondoa
fikra mbovu ambazo kwa hakika zimekufanya kuwa mtu wa ajabu
kwenye jamii na kukupatia maisha ya majuto, maisha ya kujitweza, maisha ya
kukosa uthubutu wa kufanya makubwa, maisha ya kuogopa kila kinachotokea
kwenye maisha yako badala ya kukikabili na kujitengenezea maisha bora,
unaishi ukiwa umekufa angali ukiwa unatembea kwakua kila kitu
kinakuchukua wewe na unakwenda kwa kila mwelekeo moja ya jambo baya
sana kwenye maisha ya binadamu.

Katika kufahamu ni kwa namna gani unaweza kujenga fikra njema na zenye
umuhimu sana kwenye maisha yako kukupatia maisha unayoyataka na
mwisho kuwa mtu mwema mwenye kujitambua ni kwa kufanya mambo haya:-

a) Jitazame kwa mtizamo chanya.

Kujitazama kwa mtizamo chanya kuna maanisha kuwa na uwezo wa kufurahi


na kujikubali jinsi ulivyo kujipenda bila kusubiri wengine wakupende, ni
tamanio la kuwa mtu bora na bila kujisikia vibaya ukiwa mtu bora. Kwa lugha
nyingine ni kuishi maisha uyapendayo ambayo hayakuletei mzigo wa majuto
na mahangaiko ya kiafya kwa kujiharibu wewe mwenyewe kwa kufanya
vitendo vibaya.

Ili kuwa na uwezo wa kuwa na mtizamo chanya kujihusu wewe unapaswa


kufanya mambo haya kwa haraka sana;-

8
1. Jiweke katikati ya makundi ya watu waliofanikiwa zaidi yako, hii
itakutia hamasa, na wivu mzuri, na kukupatia bidii ya kufanya
vizuri zaidi na zaidi.
2. Jitamkie maneno chanya kila siku kuwa utakuwa mtu bora
mwenye uwezo wa juu na mwenye kuutumia uwezo wako wote
kwa ajili ya mafanikio yako.
3. Jiepushe na watu wanaokukatisha tama na waepuke kabisa kwa
kaa nao mbali, na hawa kuwafahamu ni rahisi sana utaona stori
zao ni za kulalamika, kukosoa tu, kuhukumu, na kukatisha tamaa
kwa kila hatua unayotaka kuichukua achana nao hawa
wananyonya uwezo wako wote ni sawa na gari yenye tenki bovu la
mafuta haiwezi kukaa na mafuta kwa ajili ya safari ya mbali.
4. Tafuta mtu wa kukushauri aliyefanikiwa mweke karibu na mtumie
kukushauri.
5. Azimia kuachana na mabaya na uanze kuishi kwenye njia ya
uchanya ama uzuri unaovutia ambao utakuletea watu wazuri na
ambao ulitaka kuwa nao nyakati zote.
6. Azimia kuwatendea wengine kwa uzuri kwa lengo la kuwafanyia
jambo jema na zuri na la heshima bila kutarajia kitu toka kwao.

b) Andika mambo unayoyata kwenye maisha yako (malengo


yako).

Mwandishi nguli na aliyeandika vitabu muhimu sana kwenye maisha ya


kimafanikio ndugu Brian Tracy, anasema alikuwa ana maisha magumu sana
na ya kukatisha tamaa, kwa kuishi kwenye vijumba vya kupanga, maisha ya
kazi za ukibarua kwa kuosha vyombo, kuchunga mifugo, kazi za mashambani,
kazi za kwenye ujenzi, kazi za uvuvi, kibarua kwenye ukorogaji na umwagaji
zege na kuuza bidhaa nyumba kwa nyumba na wakati mwingi bila kupata
wateja.

Anasema siku moja alirudi nyumbani akiwa mwenye uchovu wa hali ya juu
sana kiasi cha kuyakatia tamaa maisha yake na kuona hakuna analoweza
kufanya alikaa chini ndani ya nyumba yake na kujiuliza maswali muhimu na
kujambia kwa mfumo mtazamo chanya juu ya maisha yake kwa kusema
“hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwangu, na hakuna mwenye
dhamana na maisha yangu, yakiwa mabovu kama yalivyo sasa ni mimi

9
mwenyewe , na kama nataka yawe mazuri ni mimi mwenyewe wenye uwezo
wa kuyafanya yawe mazuri” baada ya maneno haya akachukua kikaratasi
akaandika nini anataka kwenye maisha yake anasema kutoka hapo maisha
yake yalianza kubadilika na kuanza kuishi maisha ya mafanikio na sababu ya
kuanza kuishi maisha ya mafanikio ni pale tu alipoamua kuandika mambo
anayoyataka kwenye maisha yake.

Uandikaji wa mambo tunayoyataka kwenye maisha ni jambo ambalo lipo kwa


watu wanaotaka mafanikio na wanaofahamu kwa hakika kuwa maisha
yanataka nini na njia zipi za kuyapata na kuyaishi mafanikio, wasiotaka
kufanikiwa hawajui hata wasiyoyataka kwenye maisha yao na wakati wote
wapo tayari na wanamiliki mawazo ya kushindwa, hawajui kuandika malengo,
wanafanya kazi bila kuwa na mipango na wapo tayari kufanya kazi maisha yao
yote.

Kuandika malengo yako na kubadili mawazo yote ya kushindwa na kuwa na


mawazo chanya, na kuweka mipango ya kufanikiwa na kufanyia kazi mipango
mpaka itimie ndiyo siri kuu ya kujitambua na kuwa mtu bora.

Unahitaji kuandika malengo ya mambo unayoyataka kwenye maisha yako, hii


ndiyo njia iliyowapatia maelefu ya watu duniani nafasi ya kuwa na mafanikio
makubwa kwenye maisha yao, zipo sababu nyingi na muhimu sana za kwanini
unapaswa uandike malengo yako ikiwa ni pamoja na:-

1. Malengo hukufanya upae kama mshale unaokwenda moja kwa


moja kwa kasi mpaka pale ulipolenga na kukita tiii.
2. Malengo hufungua fikra zako mpya na kuachilia mawazo mapya
na makubwa na kukupatia nguvu ya kuyatimiza malengo hayo.
3. Waliofanikiwa duniani wanatabia ya uwekaji malengo na
wanajikita kwenye lengo moja mpaka walitimize na
kulifanikisha.
4. Malengo ndiyo huonyesha wewe ni nani? na una uwezo gani?
Na unautumiaje kuishi wewe na kuwa wewe hapa duniani.

Malengo ni jambo la muhimu sana katika safari yako ya kujitambua na


unapaswa kwa hakika kuweka malengo kama unataka kuwa wewe na mtu bora
sana hapa duniani na hakikisha kuwa unaweka malengo yako kwenye maeneo
sita kwenye maisha yako ikiwa ni pamoja na malengo yako juu ya afya ,
malengo yako juu ya fedha, malengo juu ya akili yako, malengo yako juu
10
mahusiano yako, malengo yako juu ya jamii inayokuzunguka majilani na
ndugu, malengo yako juu ya mambo ya kiroho yaani utambuzi wako wa juu
dhidi ya nguvu umba yaani Mungu.

Na malengo hayo yanaweza kuwa ya muda mfupi yaani kuanzia mwezi mmoja
mpaka mwaka mmoja, ambayo yaweza kuwa kama

 Kuweka fedha akiba.


 Kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
 Kutaka kufanya biashara.
 N.k.

Ama malengo ya muda wa kati yaani kuanzia mwaka mmoja mpaka miaka
mitano na isizidi miaka mitano ambayo yaweza kuwa:-

 Kuanzisha biashara niitakayo.


 Kuwekeza hisa kwenye masoko ya hisa.
 Kujenga nyumba ya kuishi.
 Kujifunza fani niipendayo.
 N.k.

Ama malengo ya muda mrefu haya ni ya zaidi ya miaka mitano mpaka miaka
kumi na yaweza yakawa:-

 Kupanua biashara zako.


 Kuongeza nyumba ama biashara tofauti.
 Kama hauna kazi kutafuta kazi ama kutengeneza kazi.
 Kuwa na akiba ya ustaafu angali ukiwa kijana.
 N.k

Jambo la muhimu unapoandika malengo hakikisha unaandika kulingana


na hali yako, kuandika kwa uhalisia,na kuandika bila kudhamilia sana kiasi
kwamba uje ushindwe kuyatimiza malengo hayo, na mwisho ni kuandika
kwa njia yanayokupatia wepesi kuyafanya kwa mfano mwaka ujao nitaweka
akiba ya Tsh 2000/= kila mwezi na sitaigusa kwa jambo lolote.

Hayo ndiyo mambo muhimu sana kuelekea safari yako ya kujitambua na


kujifahamu na kuanza kuishi wewe na ukiangalia kwa umakini mambo
hayo yanakufungamanisha na wewe unavyotaka kuwa na kutimiza
matamanio yako, matumaini yako na ndoto zako na mwisho kujenga dunia

11
yako inayotokana na matokeo ya fikra zako juu ya mambo muhimu ya
kijamii kama dini yako, saikolojia yako(tabia zako), falsafa yako(yale
unayoyaamini), na mwisho kuwa na mtazamo utakaotoa matendo na kuwa
wewe.

Kwahivyo unajenga ndani yako kwanza kisha ndani yako inatoka nje na nje
yako inaakisi ndani yako ulivyo juu ya mambo unayoyapenda sana na
ambayo unayafanya kwa urahisi sana hata kama wengine wanasema
hawajui na wamechoka kufanya lakini wewe unafanya tu, na kadili
unavyofanya ndivyo kiwango chako cha furaha na utoshelevu ndivyo
kinavyokuwa na kuwa kikubwa sana na mwisho kuwa wewe na watu
wanasimama kukupigia makofi baada ya kufanya kwa ishara ya
kukuheshimu na kukupongeza.

Mambo hayo yaweza kuwa kuimba kwako, kucheza kwako, kuongea kwako,
kuwashauri wengine, kuchora, kufanya mahesabu, kufundisha, kuwatetea
watu, kuongoza tukio fulani kwa uzuri, kuuza, kuwahudumia wengine,
kupika, kubuni, kusaidia wengine, na n.k hayo ndiyo yanayokutambulisha
kuwa wewe ni nani?

12
SURA YA PILI

1
AINA YA VIPAJI NA NAMNA YA KUFAHAMU KIPAJI CHAKO.

V
ipaji ni moja ya injini iliyowafanikisha wengi baada ya kufahamu
wanakipaji cha aina gani? , na baada ya kufahamu hawakubaki kusema
tu kuwa kipaji hiki kitanivusha bali waliingia kukifanyia kazi zaidi na
zaidi katika kukifanya kianze kuishi na baada ya mazoezi magumu ya bila
kuchoka na ya kila siku mwisho dunia ilikuja kuwatambua kuwa hawa ni watu
wasio kuwa wakawaida na wanapaswa kupewa heshima kwa kazi zao nzuri
zilizotukuka kutokana na vipaji, dunia inashuhudia uharibifu mkubwa wa
vipaji vya maana ambavyo vvipo ndani ya watu na watu hao hawafahamu
kama wanavyo vipaji hivyo na wameishia kuishi maisha ya kawaida na yasiyo
na maana kwa jamii, inasadikika kuwa angali binadamu anapokuwa katika
hali yake ya utoto kiwango chake cha kipaji huwa kipo juu sana zaidi ya
asilimia 98% akiwa kwenye umri wa miaka mitano mpaka kumi , baada ya
kutoka hapo mtoto huanza kupoteza uwezo wa vipaji vyake na mpaka kufika
umri wa miaka kumi na nne anakuwa kapoteza uwezo mkubwa wa vipaji
vyake na kuanza kuishi gizani, na sababu kuu zinazotajwa kuchangia uharibifu
huu mkubwa wa vipaji ni malezi ya wazazi , mazingira anayokulia, aina ya
elimu anayopata, mambo haya hudidimiza kabisa tumaini la mtoto kuishi na
vipaji vyake mwisho wa siku anakuwa dubuwasha ama roboti wa kupangiwa
kila kitu, cha kufanya, namna ya kuwaza, namna ya kufikiri, namna ya kula,
namna ya kuenenda, namna ya kufurahi, namna ya kukasirika n.k.

Hali ni mbaya sana makaburi mengi yamebeba miili ya watu waliokuwa


wakuu sana na miili yao ilikufa bila kutimiza mambo makubwa yaliyopaswa
kufanywa na unaambiwa asilimia 95% ya wakazi duniani wanaishi bila
kufahamu vipaji vyao yaani ule uwezo wao wa juu wa kufanya mambo bila
kuchoka na wakati huohuo wakati wanafanya kiwango chao cha furaha na
13
raha kinaongeza sana na kuishi kwa kusudi kunakua sana na hali
inayowafanya kuishi maisha ya maana sana hapa duniani huku nyuso zao
zikiwa na furaha na tabasamu nyusoni kwao na hapo wana nafasi ya kuishi
maisha marefu sana hapa duniani maana wanaishi kwa kutimiza kila kitu
walicho nacho ndani yao na kuifanya dunia kuwa mahali pazuri pa kuishi kwa
lugha nyingine tunaweza kusema wanakuwa na uwezo wa kujimimina zaidi
kwenye yale wayafanyao.

Benjamin franklini aliwahi kusema kuwa watu wengi sana wanakufa wakiwa
na miaka 25 na wanazikwa wakiwa na miaka 75 , kwamba kwenye maisha
kuna aina tatu ya vifo , moja kifo cha kiroho ambapo mtu anakuwa hana
mahusiano ya moja kwa moja na nguvu tenda yaani Mungu katika kumsaidia
kufanya makubwa hapa duniani , na kifo aina ya pili ni kifo cha uwezo wake
wa kufanya mambo kwa njia ya urahisi sana lakini anachokifanya anakifanya
kwa uzuri na wengine wanampongeza kwa kufanya hicho anachokifanya yaani
kifo cha kipaji chake ingawa unaendelea kupumua lakini unaishi chini ya
uwezo wako, kifo cha aina ya tatu ni kifo cha kimwili ambapo hapa unakufa
mwili wako na kuzikwa kaburini habari lako linakuwa limekwisha kama na
hakuacha alama duniani basi unabaki kuwa umeandikwa majina yako ya
utambulisho hapa duniani kwenye kaburi lako tu.

Kifo aina ya pili yaani kufa kivipaji ni moja ya kifo cha hatari sana kwakua
unaishi duniani bila kuwa na kusudi na moja kwa moja hauwezi kuwa na
furaha, kwakua hakuna hata ndoto moja ulizokuwa nazo iliyowahi kutimizwa
, unaishi kwa kukata tamaa, unateswa na mambo ya kupita kama matatizo,
changamoto na umebaki kuwa bingwa wa kusimulia matatizo yako badala ya
kusimulia na kuhubiri mafanikio yako umekuwa unajulikana kwa majina ya
matatizo mbaya sana.

Ndani yako una uwezo mkubwa sana, kama utakubali leo kuanza kuchukua
hatua kubwa kubwa za kujitafuta ndani yako na uanze kuishi wewe ukiwa na
mwenye kila kinachohitajika kwenye maisha yako, wajapani wanaopatikana
kwenye mji mmoja mzuri sana ujulikanao kwa jina la Okinawa , moja ya sifa
ya mji huu ni kuwa wakazi wa eneo hili wanaishi miaka mingi sana duniani, na
ni moja ya eneo ambalo watu wake wanaishi wakiwa na furaha kwa kipindi
kirefu, nyuso zao zinauchangamfu wa kiwango cha juu, huwezi kukosa kutoka
kwao tabasamu, vicheko, kufanya kazi kwa upamoja, kukaa kwa upamoja na
huku wakicheka, utani wa hapa na pale, ulaji wa vyakula vya asili ambavyo
14
hulima kwenye nyumba zao, na ulaji wa mazao ya ziwa na bahari naaam kwa
uzuri mji huu ulifikia hatua mpaka ya kubadilishwa jina na kuwa mji wa
waishi miaka mingi yaani (longevity) kilichokuja kugundulika kutoka kwa
watu hawa ni kuwa ni miongoni mwa watu wanaishi kwa kusudi yaani Ikigai
neno la kijapani lenye maana ya kuishi ~iki kwa kusudi ~Gai na kupatikana
falsafa ya Ikigai ambayo inawasaidia wajapani wengi kugundua
vipaji vyao na kuviishi kwa kutumia kanuni muhimu nne ambazo
ni

1. Kufahamu wito wako wa kuwepo duniani ni nini?

Hii ina maana mambo gani unaweza kuyafanya kwa ajili ya wengine yaani
kufanya kwa ajili ya wengine kujitoa kwa uwezo wako kwa ajili ya wengine
hapa wawajibika kutambua mambo hayo unayoweza kuwafanyia wengine.

2. Kipi unapenda kufanya sana?

Hii ina maana ya mambo ambayo huwa unayafanya ukiwa na furaha sana na
hauchoki kuyafanya hapa wawajibika kuyatambua mambo hayo.

3. Upi ujuzi wako unaokufanya kufanya jambo fulani kwa uzuri zaidi?

Hii ina maana ya kufahamu ujuzi wako na huu waweza kuwa wa kusomea ama
wa kujifunza chini ya mtu mwingine na ukawa na ujuzi huo wa juu na kila
ukifanya wengine wanauliza kwa hamu ya kutaka kujua nani kafanya kitu
hicho na unatajwa kuwa ni wewe.

4. Kipi upo tayari kulipia ili ukifahamu na uanze kukifanyia kazi.

Hii ina maana ya mambo ambayo huenda hauyafahamu na unapenda


kuyafahamu hayo mambo na upo tayari kurudi darasani ama kumtafuta
mwenye kuyafahamu mambo hayo na uanze kuyatumia kwenye maisha yako

Sasa mjumuisho wa mambo hayo yote hukuletea maisha yenye kusudi na


yenye furaha na unawajibika kuanza kufanya kidogo kidogo ukijigundua
ulivyo na uanze kujifahamu wewe na uwe na siri ya kuwa na furaha kutoka
kwenye hayo mazingira yako na ukipata mambo hayo kwa haraka anza
kuyafanyia kazi kila siku bila kuacha kwa lengo la kujiboresha, kwa kufanya
hivyo utakuwa unayapa maana muhimu sana maisha yako.

15
Kurahisisha kujifahamu wewe jiulize maswali hayo na yapatie majibu na
yaandike na ukishayaandika yafanyie kazi kila kukicha na endelea kujiuliza
maswali sahihi na ujiambie ukweli kwa mfano, nini kinanisukuma kuamka
asubuhi na mapema na kitu gani kinanifanya kuchelewa kulala ? kitu hicho
chaweza kuwa kimebeba siri za kufanikiwa kwako na kuanguka kwako gundua
kwa haraka na kama kinakupa mafanikio na furaha endelea kupapalilia
kukifanya na kama kinakupatia maisha ya hovyo anza kuachana nacho mara
moja ili uanze kuishi wewe ujifahamu uzuri wa kuwa wewe.

Kuharakisha ujitambuaji wako kwenye ngazi ya vipaji endelea kukazia fikra


katika kuanza kidogo kidogo ufanye bila kuacha, endelea kujitafuta ndani yako
ujigundue wewe ni nani nje ya jina lako, na endelea kufanya kwa uendelevu
pata furaha kutokana na hayo unayofanya na uliyo nayo, na mwisho hakikisha
unatunza uwepo wako kwenye jambo unalolifanya hakikisha unakuwepo hapo
kwenye kile unachokifanya.

16
SURA YA PILI

2
NJIA NYINGINE NZURI ZA KUFAHAMU VIPAJI CHAKO.

M
wandishi na mwanasakolojia wa chuo kikuu cha Harvad nchini
marekani miaka ya 90 alianidika kitabu kizuri sana kijulikanacho
kama Frame of Mind ndugu Howard Gardner aliandika
kitabu hicho kuashiria kuwa kuna aina ya uwezo mkubwa sana walionao watu
wa kitofauti tofauti baina ya huyu na yule na si kwamba wote tunapaswa kuwa
na aina moja ya uwezo wa juu yaani uginiasi , kupitia kitabu chake anaibua
aina saba ya uwezo wa juu ambao unawatambulisha watu na huenda na wewe
ukajigundua upo kwenye eneo gani.

Howard anasema aina hizo za kuiwezo wa juu kuwahusu watu ni pamoja na

i) Verbal ~linguistic(Uwezo wa juu sana kuhusu lugha)

Uwezo huu unamaana ya kwamba na kwa mara nyingi uwezo huu


hupimwa kwenye taasisi nyingi za kielemu kwa wanafunzi kuwa na
uwezo wa kusoma na kuandika maneno na ni wa muhimu sana wa
kuanza nao ambapo ndiyo ujuzi unamuwezesha binadamu kubadili
maarifa kuwa taarifa watu wanaopatikana kutoka kundi hili ni pamoja
na, walimu, waandishi, wanasheria, wengi wanao ujuzi huu.

ii) Numerical ( Uwezo wa juu sana kuhusu mahesabu na namba)

Uwezo huu una maana ya kuwa watu wenye uwezo huu wana uwezo wa juu
kuhusiana na masuala ya kimahesabu na wanao ujuzi huu kwa asili ama
kwa kujifunza kwa kiwango juu. Watu wanapatikana kwenye kundi hili ni
pamoja na wanamahesabu wakubwa , wanasayansi , madaktari wakubwa ,
wana anga.

17
iii) Spatial (Uwezo wa juu wa kiubunifu na sanaa)

Uwezo huu una maana ya watu wenye ubunifu wa juu kutokeza mambo
mapya ama kuyatokeza kwa namna yake ya kipekee. na watu kutoka kundi
hili ni pamoja na wasanii wakubwa , wachoraji .

iv) Kinestthetic ( Uwezo wa juu kutumia mwili wao vizuri )

Uwezo huu unawahusu watu wenye uwezo wa kutumia uwezo wa miili yao
kutokeza mambo mazuri na makubwa kwa kutumia mwili tu kama
kukimbia , wacheza mziki ,mafundi ujenzi ,mafundi makanika, mafundi
mbao ,na hata wapishi wakubwa. Watu kutoka kundi hili wanasifa kuu ya
kujifunza kwa kutenda yaani (hand on learning)

v) Intra personal (Uwezo wa juu wa kihisia).

Uwezo huu unawahusu watu wenye uwezo wa kuongoza na kudhibiti


mawazo ya kihisia na uwezo wa juu wa kujisemesha wao wenyewe na
wenye ujuzi huu utauona kwa watu wakati wa hasira ama woga , watu
kutoka kundi hili ni pamoja na washauri wakubwa , wameombeaji
wakubwa , wasuluhishi wakubwa .

vi) Interpersonal (Uwezo wa juu kuongea na kuwaliana).

Uwezo huu unawahusu watu wenye wenye kuongea sana , ama kuzungumza
kwa umahili na kuwasiliana na wengine kwa urahisi, na watu kutoka kundi
hili ni pamoja na waimbaji wakubwa , wahubiri wakubwa , wahamasishaji
wakubwa ,wanasiasa wakubwa , waigizaji wakubwa , na wauzaji
wakubwa.

vii) Environment (Uwezo wa juu kuyahusu mazingira).

Huu ni uwezo wa juu wa mazingira jinsi yanavyoweza kutufaidi kwa mfano


kuna watu wamezawadia kudili na kufahamu matumizi ya miti, mimea,
samaki, bahari, wanyama na ardhi, watu kutoka kundi hili ni pamoja na
wakulima wakubwa, wafundishaji wa wanyama, park rangers posses.

Kwahivyo nawe unaweza kujitafuta kutoka kwenye makundi hayo na uache


kujiona mtu wa kawaida bali wewe ni mkuu na jikuze kwenye eneo lako na
uanze kufanya makubwa zaidi na zaidi.

18
Baada ya kuwa umeona aina za vipaji kama hivyo hapo juu, sasa nawe
unaweza pia kufahamu aina ya kipaji chako kupitia ama kwa kutumia njia
kama hizi.

a) Jifanyie tathimini wewe mwenyewe binafsi juu ya vipaji vyako.

Kujifanyia tathimini ni jambo bora sana na hili hutusaidia kujigundua kwa


haraka tulivyo, na kama unataka kujifanyia tathimini wewe mwenyewe juu ya
vipaji vyako jifunze kukaa maeneo tulivu na yenye hewa safi na yenye
kukuhamasisha kufikiri kwa uzuri na kuwa na kalamu na daftari zuri anza
kuchukua mambo kutoka ndani yako na yamwage kwenye maandishi juu ya
uzuri wako kwenye eneo fulani, epuka sana kujidanganya amua kujiambia
ukweli wakati unajifanyia tathimini na usiendeshwe na namna dunia na
walimwengu wanajiendesha kuwa wenye vipaji na waimbaji tu, wacheza mpira
tu, ama wacheza vikapu tu, ama wapiga vyombo vya ala hapana kuna aina
nyingine nje ya vipaji hivyo ikiwepo hata kuwa msomaji mzuri wa vitabu,
kuchanganua semi tata kwenye maandishi ya vitabu, kuongea kwa weledi,
kuwafurahisha kundi la watu, n.k anza kufanya tathimini sasa kwa kujibu
sehemu ya maswali kama haya

i. Wapi nimewahi kufanya vizuri sana kwenye maisha yangu?


ii. Ni masomo yapi nilikuwa nayapenda sana toka utotoni?
iii. Vitu gani nilipenda sana kuchezea angali nipo mtoto?
iv. Ni jambo gani huwa nalifanya kwa uzuri sana na ninaona kama ni
jambo la kunifurahisha huku wenzangu wakiona ugumu juu ya jambo
hilo lakini mimi naliweza?
v. Watu huwa wananizungumzaje mimi juu ya mambo fulani fulani
ninayofanya?

b) Baada ya kuwa umeandika majibu yako kwa uzuri jaribu kuwauliza watu
unaofaana nao sana kisha wao wakwambie wanakuonaje na kisha nenda
ulinganishe na majibu yako ambayo ulikuwa wajichunguza na kujifanyia
tathimini juu ya vipaji vyako, kuna namna fulani utaona kuna kufaana
ama kupata wazo jipya juu yaw ewe.

c) Andika kile kilichosemwa na hao wengine juu yako, ili uanze kuyaona
mambo kwa uhalisia na kuanza kujifahamu.

19
d) Mwisho linganisha majibu yako na kile ambacho wengine wamesema na
kisha fuata hatua inayofuata juu ya kuanza kuishi kipaji chako na
kukitendea haki.

20
SURA YA PILI

3
KUFANYIA KAZI KIPAJI NA KUANZA KUISHI WEWE.

H
aitoshi kuwa na kipaji tu, kisha ukafanikiwa na kipaji hicho kuna
hitajika mambo ya kufanya muhimu sana kukifanya kipaji kikusaidie
kutimiza mengi na yenye mafanikio hapa duniani katika safari ya ya
kujitambua na kuanza kuishi uwezo wako ama wewe, mambo hayo ni pamoja
na kuwa tayari umekifahamu kipaji chako na sasa unataka kuanza kufanyia
kazi basi fanya haya kwa uzuri kabisa utaona ukifanikiwa kutokana na kipaji
chako.

1) Kubali kuonekana mjinga na mpumbavu.

Wakuu wote walianza kwa kuonekana wajinga ama wapumbavu na mwisho


waliheshimiwa na kama unataka kuwa mkuu na mwenye kuheshimiwa kubali
leo kuonekana mpumbavu na mwenye kudhaurika kwenye kutendea kazi
vipaji vyako, Marehemu Ruge Mtahaba aliyekuwa mshirika na mkuu wa
vipindi kwenye kampuni ya CLOUDS MEDIA aliwahi kusema “kama
unachokifanya hakina ukosoaji ama kupingwa basi fahamu
unachokifanya si sahihi badilisha” maana yake ni kuwa kwenye
kuviendea vipaji vyetu na kufanya jambo fulani juu ya vipaji vyetu kuna
namna nyingi tutakutana na vikwazo na kukatishwa tamaa na kwa msingi huo
hatuna haja ya kuacha ama kukata tamaa, lazima tukubali kuonekana wajinga
bila kupoteza utayari wetu na udhubutu wetu katika kufanya mambo
yanayotakiwa na vipaji vyetu, kupingwa tutapingwa san asana ten asana lakini
lazima tukumbuke kuwa wakuu walianza na kudharauliwa na mwisho
wakaheshimiwa.

21
2) Wacha visingizio.

Wengi ya watu wanaacha kufanyia kazi vipaji vyao kwa kujipa visababu na
visisngizio vingi na wanaweza kuorodesha sababu hata mia za kwanini
hawawezi kufanya jambo fulani na ukizingalia kwa umakini na jicho la
mashaka unaweza kulidhia kabisa kuwa watu hawa wapo sahihi kutokufanyia
kazi lakini ukweli wa mambo ni kuwa hata kama zitakuwepo sababu za msingi
za wewe kutokufanyia kazi kipaji chako nakwambia ziweke pembeni na
ziambie naomba mnisubiri hapa kwanza naenda kufanya kwa namna yoyote
ile, kisha jitose kwenda kufanya, washindi wote waliacha kujionea huruma ,
kujipa sababu zisizo na maana juu ya mambo fulani fulani na waliazimia
kufanyia kazi vipaji vyao iwe jua linawaka ama mvua inanyesha.

3) Kipatie muda wa kutosha kipaji chako na kitumikie.

Ukitaka kufanikiwa kwenye jambo lolote hakikisha unatenga muda wa


kutosha juu ya jambo hilo na kwa hakika utaona matokeo ya jambo hilo, watu
wengi wanataka kufanya mambo fulani na kwa wakati mchache tu wanataka
kuona matokeo ya jambo, ndugu yangu dunia na kanuni za asili hazisemi
hivyo inahitaji muda kwa kila jambo kuanza kukua na kupitia vipindi kadha
wa kadha ni kama tu ambavyo mtoto hupatikana ni lazima mambo fulani
yafanyike kwa muda fulani na kisha kupata matokeo ya jambo takiwa,
kwahivyo na kwako pia fanya mazoezi ya kutosha juu ya kipaji chako, tenga
muda wa kutosha kujikomaza kwenye kipaji chako.

Na kwa sababu unao uwezo wa asili anza kufanyia kazi kipaji chako
utajikusanyia mafanikio ya kutosha na mali za kutosha na dhamiria kuwa
hakuna jambo litakuzuia kufanyia kazi kipaji chako, na kama kuna vizuizi njia
za kutatua na kuondoa vikwazo hivyo vitatumika na utafanikiwa.

Makampuni makubwa yaliyofanikiwa yanafahamu nguvu ya muda, kwamba


kwa kuanza tu huanza na kukataliwa kwenye soko, ama hutoa huduma duni
na zisizo na viwango lakini kadili ya muda unavyosonga ndivyo mabadiliko
makubwa hutokea na ushindi hutokea, iwe hivyo na kwako endelea
kujiboresha na kujijenga kwa muda wa kutosha utakuwa mtu bora sana na
mwenye uwezo wa juu sana.

22
4) Endeleza kipaji chako kwa kuwasaidia na wengine.

Wachina wana msemo mmoja muhimu sana juu ya ukuaji wa maendeleo ya


kudumu katika kuweka alama na kubaki kwenye ulimwengu hata baada ya
kuwa mwili umekufa na kuharibika na wao husema “kuwa ukitaka
mafanikio ya miaka kumi panda miti, ukitaka mafanikio ya
mwaka mmoja na miezi panda mpunga, lakini ukitaka mafanikio
ya kudumu na karne na karne panda watu.” Mafanikio utakayoyapata
kutokana na vipaji vyako lazima na ni muhimu yawe ni yanayogusa na
wengine, kuwasaidia na wengine kuona mwanga wa kimafanikio toka kwako,
kuwashika mikono wengine na huko ndiko furaha nyingi hupatikana na
maana ya maisha huwa pana na ya kufurahisha sana sana, basi amua na wewe
kwa namna moja ama nyingine kuona kuna umhimu sana wa kusaidia
wengine na kuwagusa kwa namna moja ama nyingine.

5) Ambatana na watu sahihi.

Tathimini bora na ya muda mrefu kwenye maisha ya wanadamu kutaka


kuwafahamu kwa undnai wao wakoje na wanapenda nini ni kwa kuangalia
aina ya marafiki za mtu huyo unayetaka kumfahamu vyema na kama
utabahatika kufahamu marafiki za mtu huyo ni kwa haraka sana utamfahamu
mtu huyo, kuwa atakuwa mwenye mafanikio ama mwenye kushindwa kwenye
maisha, na kwa mjibu wa tatifiti asilimia 80% ya waliofanikiwa, mafanikio
yao yamechangiwa na aina ya watu walio ama wanao ambatana nao, na kwako
pia kama hautafanya machujio mazuri juu ya watu unaombana nao una nafasi
ya kuwa mwenye kujuta sana badala ya kuwa mwenye uwezo wa kuona fursa
na kupiga hatua muhimu, ili kulitimiza hilo unawajibika kuwa na aina hii ya
watu;-

a) Shabiki wako (cheer leader)

Hawa ni wale wanaokutia hamasa kwenye mambo muhimu unayoyafanya


kwenye maisha yako, na hawa kwa kipindi kingi huwa wako upande wako na
wanakuunga mkono, na maadui zako wakianza kukusema vibaya mashabiki
zako wanakutetea ukiwa haupo hawa ni muhimu sana kuwa nao.

23
b) Mshauri (mentor)

Hawa kazi yao kubwa huwa wanafanyaka kazi kukuonyesha njia kule
unakotaka kwenda na njia hiyo yaweza kuwa kifamilia , kiuchumia au hata
kibiashara, mshauri anakupatia ushauri mwanana ambao unatakuwa
unahitaji sana, anakushirikisha taarifa muhimu na yeye hufurahi wewe
unapofanikiwa na huchukia pale unaposhindwa kuchukua hatua muhimu
zinazohitajika ili kukufanya ufanikiwe.

Ili kuwatunza washauri kumbuka haya kwamba wao wapo kwako si kwakua
wanataka uwalipe ama usaidie wenyewe wapo kwako kukutegemeza kiushauri
kwahivyo kuwa makini na uwatunze na tambua mchango wao kwenye maisha
yako.

c) Rafiki (friend)

Hawa ni wale ambao kwa muda mrefu upo nao na kuna aina fulani ya tabia
mnaendana na kwa hakika anakufaa kwa mchango wake wenye tija kwenye
maeneo yako ya kile unachotaka kufanya.

d) Sahibu (comrade)

Hawa ni wale wanakuja kwenye maisha yako kwa sababu maalumu nayo ni
kwa kuunganishwa na adui ambaye ni adui yako lakini na yeye sahibu
amekutwa adui huyo naye ni adui yake kwahivyo anakuja kuunganisha nguvu
kummaliza adui yenu, akimaliza kumuungamiza adui yenu huyo huondoka
kwenye maisha yenu.

e) Mwenye kufafana na yale unayofanya(peer)

Hawa ni wale ambao kwa namna moja ama nyingine wanafanya


unachokifanya na wanakupenda unavyofanya na wewe, na wapo tayari
kukusaidia kufahamu mambo kadha wa kadha kama hauyafamu, hana choyo
yupo tayari kukuonyesha kinachotakiwa kufanyika.

24
f) Kocha (coach)

Hawa siku zote wanakusukuma kufanya makubwa na wanataka uende mbele


zaidi kutoka hapo ulipo na ufanikiwe zaidi na zaidi, anahakikisha hauridhiki
na mafanikio uliyo nayo, na sifa zao nyingine ni kuwa ni wakali sana
unapokwenda kinyume na huenda akakufokea.

Ni mtu anayejua vipaji vyako ama aina ya uwezo wako fulani ambao wewe
haujaugundua ama hauvijui na yupo tayari kukuambia namna ya kufanya.

g) Mwamini (confidant)

Hawa ni wale watunza siri zako na ambao unaaminiana nao na wanakutunzia


siri zako, na ni watu ambao unaongea nao kwa uwazi bila kuficha jambo lolote
na wao wapo radhi kukutunzia siri hata kama mmegombana au kukorofishana
watakuwa upande wako katika kuhifadhi habari na taarifa muhimu kuhusu
wewe.

Hii ndiyo aina ya watu unaowahitaji kwenye safari yako ya kujitambua na


ujifahamu furaha ya kuwa wewe.

25
SURA YA TATU.

1
JENGA TABIA BORA NAYO ITAKUJENGA KUWA BORA.

~hakuna kitu imara kama tabia~ na von.

K
atika safari ya kujitafuta na kujitambua huwezi kuliacha jambo la
kitabia, tabia ndiyo muhimili wa muhimu katika kuelekea safari yako
ya kujitambua na kuanza kuishi wewe kwa furaha.

Ili kufamu kwanini tabia ni muhimu tufahamu maana yake kuwa tabia ni
pamoja na mambo yote amabayo mtu/kiumbe hufanya kwa kuyarudia rudia
ambayo yanatujenga kwa uzuri ama kwa ubaya na kama ukitaka kuanza
kubadili hatua zako muhimu kimaisha eneo hili ndiyo eneo wa kulipatia uzito
wa juu na kwa umhimu wake unaotakiwa sana.

Hauwezi kuwa chochote unachotaka kuwa kama haujaweza kuwa chochote


unachotaka kuwa kichwani kwako, kisha kutoka kichwani kwako kiwepo
kwenye uhalisia wa maisha yako, kila kitu tunachokiona kwa macho kikiwa
kwenye mfumo wa umbo ama yale yote unayoyamiliki ulianza kuyapatia
nafasi kichwani kikiwa katika hatua ya mawazo ama picha ambayo unaanza
kuijenga fikrani kwako na mwisho inakuwa kama maelekezo kutoka ndani
yako na kuwa nje yako ambayo husukumwa kwa uzuri na tabia ima nzuri ama
mbaya juu ya jambo ulilolitokeza kwenye ulimwengu wa uhalisia kutoka
kwenye ulimwengu wa kimawazo.

Matokeo ya kimaisha yetu ni matokeo ya picha ambazo tulijenga ndani yetu na


kinachotokea nje kwenye maisha yetu ni matokeo ya mwisho ya picha ya picha
hizo na tunazoendelea kuzijenga, kama unataka kubadili maisha yako na
kuyaboresha tunapaswa kubadili kile tunachokijenga ndani yetu na ambacho
wakati mwingi hutusukuma kuangalia yanayofanana na hayo na hapa utakuta

26
unasikiliza nyimbo za aina ileile iliyojengwa kichwani kwako, mikanda ya
video iliyojengwa kichwani kwako, kukaa na aina ya watu waliojengwa
kichwani kwako na vyote hivi vyaweza kuwa chanya ama hasi ni wewe
unayewajibika kufanya mabadiliko yanayotakiwa.

Milango yetu ya fahamu inaingiza taarifa na hizi taarifa zinajenga picha kwa
matendo ya kurudiwarudiwa na hukaa huko na mwisho hukomaa katika akili
isotambuzi na ikishafika huku hushika nguvu na kufanya vitu viende
vyenyewe na hapo sasa ndiyo yanapotokea matabaka ya watu wenye furaha na
wasio na furaha na wenye mafanikio na wasio na mafanikio ni kutokana na
tabia ambazo huwapatia matokeo ya kimafanikio na kiuduni kwa asilimia 99%
, aliyeduni anatabia duni kwa asiliamia 99% na mwenye mafanikio anazo tabia
za kimafanikio kwa asilimia 99%, kwamba matajiri wameshajingea uwezo wa
kuona utajiri akilini mwao na mambo hayo yanafanyika yenyewe pasipo
kutumia nguvu kwakua yameshakuwa akilini mwao na yanathibitishwa na
matendo yao , hivyo hivyo kwa maskini na wenye hali dhoofu kuwa ndani yao
kunakuwa kumejenga umaskini wa kutisha na kinachoonekana nje yao ni
matokeo ya ndani yao.

Mwandishi wa kitabu bora sana kiitwacho The power of Habit ndugu


Charles Duhig anasema kuwa tabia hujengwa na kutengenezwa na mambo
matatu ambayo ndiyo hujenga tabia ya mtu nayo ni;-

i) Kisababishi, sababu inayomfanya kutaka kufanya jambo fulani?


ii) Kurudia ama mazoea kwamba analifanya jambo hilo tena na tena.
iii) Zawadi, hiki ni kile anachokipata baada ya kuwa amefanya jambo
hilo.

Na mwisho jambo hilo hugeuka kuwa tabia ya mtu na litaanza kufanyika bila
yeye kuliwazia ama kulipangia kulifanya na ubongo wake hautakuwa tena kazi
ya kuanza kulifikiria jambo hilo badala yake litajitokeza kwa haraka tu
kichwani na kufanyika.

Sasa katika kutaka kubadili tabia mbaya ni muhimu kubadili mambo mawili
ya juu na na la tatu muhimu kwamba badili kisababishi na kisha badili
mazoea, kwa mfano kama ulizoea kukaa na walalamikaji, wenye kulaumu kila
kitu kinachotokea kwenye maisha yao, basi acha kwenda kukaa nao kaa na
wale wanaokujenga wale wenye mtazamo chanya wenye kuona fursa kwenye
mkingamano wa matatizo na hapo taratibu taratibu jambo hilo litaanza
27
kufutika kichwani kwako kwa kupakiwa jambo jipya mbadala na hilo,
kumbuka kuanza kidogo kidogo bila kuacha kubadili tabia mbaya na mwisho
tabia hizo zitabadilika.

Tunaposema tabia mbaya maana yake halisi ni zile tabia ambazo hazikujengi
badala yake zinakubomoa na kukuacha ukiwa mwenye huzuni kuu, mwenye
kuteseka kihisi, mwenye kubaki na hatia tabia hizo ni kama uvutaji wa sigara,
utumiaji wa madawa ya kulevya, ulevi wa kupindukia na mambo kama hayo.

Miongoni mwa tabia haribifu kwenye safari ya kujitambua na kupata


mafanikio na kuanza kuishi maisha ya furaha ni pamoja na hizi zifuatazo;-

i) Tabia ya ubinafsi, hali ya uchoyo kufanya mambo kwa ajili yako tu.
ii) Tabia ya kuwa na uoga wa kushindwa.
iii) Tabia ya kutokuweka malengo yanayofikiwa.
iv) Tabia ya kughairisha mambo na ukianza haumalizi unaishia njiani.
v) Tabia ya kutokutaka kujifunza.
vi) Tabia ya kutokutenda yale uliyopanga.
vii) Tabia ya kukosa uvumilivu.
viii) Tabia ya kutokuwa na vipaumbele unafanya lolote lile.
ix) Tabia ya kukata tamaa.
x) Tabia hasi kukaa na watu hasi, kulalamika, kulaumu kwa kila kitu ,
kukosoa kwa kila jambo.

Hizo zinaweza kuwa sehemu ya tabia mbaya na haribifu sana kwenye safari
yako ya kimafanikio na katika kujitambua na kujifahamu wewe ni nani na
uanze kuishi uzuri wa maisha uyatakatayo.

Katika kujenga tabia bora ni jambo linaloanza na wewe na kukuza uwezo wa


kujenga tabia bora ni mwanzo bora wa kujipatia mafanikio kwenye maeneo
sita ya kimaisha yako ikiwa ni pamoja na mambo ya kifedha, kiafya, kiakili,
kijamii, kifamilia na kiroho haya yote yanahitaji kuwa na tabia bora na tabia
hizo ni pamoja na;-

i) Kuongea na kujenga mambo chanya kama kujisemea najipenda,


mimi ni mzuri, mimi ni mwenye mafanikio, mimi ni tajiri, mimi ni
mshindi, mimi ni mtu mwema, mimi ni mwenye afya bora , mimi ni
mtu bora sana n.k kwa kufanya hivi unaanza kujenga imani mpya

28
kujihusu wewe na ikifuatiwa na nguvu ya matendo makubwa
yanayoyafanya hayo kujidhihiri wazi kwenye maisha yako.
ii) Kukaa na watu chanya , ikiwa ni pamoja wale unaopenda kuwa kama
wao, wale wanaokuhamasisha kufanya makubwa, wale wenye
kuthubutu, wale wenye kutenda kwa vitendo wanayoyasema
midomoni kwao, wale ambao furaha na tabasamu halikauki kwenye
nyuso zao, wale ambao wana nguvu ya kuona kesho kwa kutenda
vyema leo wakijiandalia kesho yao nzuri.

iii) Kuvuta hisia ya mambo mazuri, hii ni tabia nzuri sana na yenye
nguvu sana katika ujenzi wa mambo makubwa akilini kwako, ona
malengo uliyoyaandika yakitimia, ona dunia yenye utele wa kila aina
ya fursa na mawezekano ya kimafanikio, jione ndani yako ukiwa
vizuri na mwenye nguvu za kufanikisha malengo yako.

iv) Tabia ya ulaji wa vyakula vizuri na bora kiafya, unajengwa na


kuundwa kwa vyakula na vile unavyokunywa kama utaweza kuwa na
utamaduni bora wa kitabia wa kula vyakula bora vyenye virutubisho
bora ikiwa unywaji wa maji mengi, ufanyaji wa mazoezi, kufanya
matibabu kama mwili wako unaumwa na kuangalia maendeleo ya
kifya yako na mwisho kujikinga kwa uzuri na visabisho vya maradhi.

v) Tabia ya kupenda kujifunza, wale wanaoamua kujifunza mambo


mapya wana nafasi kubwa sana ya kujitambua kwa haraka na kuwa
na ufahamu wa mambo mengi ambayo mengi yake yamefichwa
katika mfumo wa kujifunza na kusoma vitabu, kuhudhuria semina za
kidarasa na kimafunzo, ukweli wa mambo ni kuwa tunajua kidogo
sana kama hatutaka kujifunza mambo mengi tutayafanya kwa njia ya
uduni kwa namna isiyotupatia matokeo bora kwenye maisha.
Maaarifa ni nguvu na maarifa ni matokeo ya taarifa sahihi na
mwenye taarifa nyingi sahihi ndiye mwenye maarifa mengi , hii
haiwezi kuja kihivi hivi bali yatakiwa kufanywa kuwa tabia yako ya
kupenda kujifunza na kufanyia kazi kile unachojifunza.

29
vi) Kuza na kuwa na matarajio bora na chanya kwenye maisha yako ,
ikiwa ni pamoja na yale umepanga kuyatimiza kwenye maisha yako
kubali kuendelea kujiboresha kujikuza na kufanikisha yanayotakiwa
kuza imani yako ya kuyaona yakitimia usiache kufanya kile
unachokiweza kukifanya leo.

30
SURA YA NNE

1
MISONGO MDUDU ANAYEKULA UHAI WA WENGI.

~Si misongo inayotuua, ni mijongeo/tafsiri zetu juu ya misingo ndiyo inayo


tuua~ by Hans Selye

M
isongo limekuwa tatizo kubwa sana kwenye ulimwengu wa sasa na
limetokea kuweka vikwazo kwenye mambo mengi katika safari ya
kujifahamu na kujitambua, kwa sababu unapokuwa katika hali hii
hata uwezo wako wa kufikiri na kufanya maamuzi sahihi hupungua, na kwa
kiwango kikubwa msongo umeharibu sana namna ya watu wanavyoishi na
eneo kubwa panapozalishwa misongo aina mbalimbali ni kutokana na
mahusiano, aina ya kazi wanzofanya watu, aina ya starehe wanazofanya watu
kama ulevi wa vinywaji vikali, namna wanavyofikiri na kuyapatia tafsiri
mambo mbalimbali na kwa kiwango cha juu sana msongo mkubwa sani ni
misongo ya kimawazo inayotokana na mahusiano ya kimapenzi na kifamilia,
na hali hii imetokeza ndoa na mahusino machungu na wengi wanaishi bila
kuwa na furaha, mambo mengi hayakamilishwi, tafiti nyingi zinaonyesha
namna ambavyo mahusiano mengi yamevunjika na kushindwa kudumu na
wengine wamejiua.

Si kwamba kuwa na misongo ni jambo baya hapana ni jambo ambalo


linatakiwa na ni jambo ambalo kila siku tunakuatana nalo jambo hili kwenye
maisha yetu, kukutana nalo na kukaa nalo si tatizo, bali tatizo huanzia pale
tunapokuwa kwenye msongo wa aina fulani kwa muda mrefu sana kwenye
maisha yetu na kushindwa kukabiliana nao kiasi ambacho kinakutuoletea
matatizo na maamuzi ya hovyo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha yetu,
kwa mfano ndoo ya maji ya lita ishirini ya maji imeundwa kuchukua uzito wa
lita ishirini za kimiminika na kama itatumika kwa kiwango cha uzito
31
uliopangwa kwa usahihi ndoo hiyo inaweza kudumu kwa muda mrefu sana
tofauti na hapo kama itatumika kinyume na hapo inaweza kupasuka ama
kuvunjika na kutoweka, ndivyo ilivyo kwako pia umeundwa kubeba misongo
ya aina fulani na ambayo kwa hakika unayoweza kukabiliana nayo ikizidi hapo
kuna hatari ya kujitarisha na misongo hiyo.

Ukweli mchungu na mbaya kusikilizwa na wengi ni kuwa hakuna mtu


aliyewahi kupoteza maisha kwa sababu ya msongo wa mawazo, lakini ukweli
ni kuwa mtu anaweza kufikia hata kupoteza maisha kutokana na namna
anavyotafsiri jambo ambalo laweza kuwa msongo hatari ama rahisi kutokana
na tafsiri zake ambazo zimejengwa na tabia zake kuelekea jambo, hali fulani,
na ndivyo hivyo hujenga uhalisia wake wakuona kwa jicho la aina ya
kujiangamiza au kujiponya kutokana na msongo huska na hapa sasa umhimu
wa kuwa na mtazamo chanya unapohitajika.

32
SURA YA NNE

2
AINA YA MISONGO NA NAMNA YA KUONDOKANA NAYO.

1. MSONGO WA MAWAZO/ MENTAL STRESS.

Msongo wa mawazo kwa maana na jina lake lilivyo ni kuwa na hali ya


kuchanganyikiwa kimawazo kunako tokana na taarifa au hali usizokuwa na
ufahamu nazo wa kutosha ama maelezo ya kutosha, hali inayokupelekea
kuwaza jambo hilo mara kwa mara bila kuwa na suluhisho la jambo hilo,
mwisho kunasababisha kuibuka kwa hisia ambazo kama utashindwa
kuzihimili unaweza kujikuta ukiwa katika hali mbaya sana na yenye kutisha,
na kushindwa kujifahamu kunakopelekea uwezo wako wa kuishi na furaha
kupungua ama kutokuwa na furaha tena na mwisho kuishi maisha ya hovyo
hovyo.

Sababu kubwa zinazochangia misongo ya kimawazo kwa kiwango kikubwa ni


pamoja na mambo mbalimbali kama, mahusiano ya kimapenzi, masomo
usiyoyafahamu, matatizo ya kifedha, matatizo ya matukio ya asili kama kifo
cha mpendwa ama magonjwa yasiyo tibika, matetemeko, upepo mkali, njaa ya
kutisha yaliyoleta uharibifu mkubwa ambao kwa namna moja ama nyingine
umeguswa nawe na hauna njia ya kujisadia nayo kwa haraka basi unafikia
kwenye kiwango cha kuchanganyikiwa na kuwa na msongo wa kimawazo
mkubwa wenye kukutesa sana na kama hautafahamu namna ya kukabiliana
nao hali yaweza kuwa mbaya.

Kwa mfano wanawake kwa sasa kwa kiwango kikubwa na wanaume kwa wingi
wanakabiliwa na zimwi la kushindwa kuhimili usaliti wa kimapenzi ama
kukosa uaminifu wa wenzi wao hali inayopelekea kutokeza maamuzi mabaya
na yanayofanya watu kubaki midomo wazi kwa kile ambacho mtu ameamua
juu ya tukio kama hilo, haishangazi tena kuona mwanaume akipiga
mwanamke msaliti mpaka kumuua na yeye kuishia kujiua ama kufungwa jela
33
kwa miaka mingi na kufia jela hukohuko, ama haishangazi kuona mwanamke
akimwekea sumu mwanaume msaliti kwenye chakula na mwanaume huyo
kula na kufa, na mwanamke huyu kufungwa jela ama kuishi maisha ya hatia
akiwepo hapa duniani hali ni mbaya.

Haipiti sekunde arobaini kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO,


linavyosema kuwa kila sekunde arobaini kuna mtu anakuwa amejiua kwa
namna moja ama nyingine huenda ni kwa kutokana na msongo wa kimawazo
wajuu sana, kwahivyo ni muhimu sana kupata njia sahihi ya kuondokana na
msongo wa aina hii kabla haujawa kitu cha hatari kwako.

Namna rahisi ya kuondokana na msongo wa aina hii ni kwa kufanya haya


yafuatayo ili uweze kujisaidia na kurudisha furaha yako ni kwa kufanya haya
yafuatayo kwa uzito na kwa nidhamu ya juu bila kupuuza:-

i. Kuwa muwazi na mwenye utayari wa kutafuta msaada na majibu juu ya


yale yanayokusumbua kimawazo kwa kumshirikisha mtu
unayemwamini jambo ambalo linakutatiza, kufanya hiki si udhaifu bali
ni ujasiri na njia bora ya kujiokoa kama mtu anayejifahamu na mwenye
kuishi yeye.

ii. Kuwa na mtazamo chanya kwa kila hali unayoipitia, fikra chanya ni
kuyaona mambo yaliyojitokeza kuna namna fulani yanasababu za
mambo hayo kutokea na kuwa halisia kuwa si mambo ambayo yanaweza
kudumu kwa muda wote na hata kama yametokea kuna namna bora na
nzuri zaidi ya kuyafanya yaishe na kuondoka kwenye maisha yako,
badala ya kubaki ukijilaumu wewe na kulalamika hali ambazo kwa
hakika huwa haziondoi matatizo badala ya kuyaongeza tu.

iii. Kuza kiwango chako cha kujipenda na kujithamini, watu wakuu


hawakuwahi kujiona duni kutokana na matatizo waliyoyapitia ama
kujikuta kwenye matatizo, mara zote walijiona kuwa wao ni wakubwa
dhidi ya matatizo yanayowakumba kwenye maisha yao, na kwa kufanya
hivi walianza kupita kila kwazo ama kila tatizo walilokabiliana nalo
kwenye maisha yao, waliliona kama fursa ya namna fulani kwamba
wakiitatua basi watakuwa wananafasi nzuri ya kuishi maisha yao.

34
iv. Tumia muda wa kutosha kufanya tathimini kujua wapi umekosea na
nini ufanye kurekebisha ili kosa hilo lisije likajirudia na kukutosa tena
kwenye kuwa na msongo wa kimawazo, kwa mfano umepoteza fedha
zako nyingi na unapofanya tathimini unagundua kuwa haukuwa na
uhifadhi bora wa fedha hizo, kugundua hivyo kunakupatia nafasi ya
kubadili utunzaji wako na kuanza kutunza vizuri ili usije kupoteza tena.

v. Tambua na kubali madhaifu yako pindi unapoona kabisa kuwa upo


tofauti, jambo hili litakufanya kuwa kwenye wakati mzuri wa
kujiimarisha na kuondoa aina za udhaifu wako katika kutaka
kujiboresha zaidi na kuwa huru na msongo wa kimawazo.

vi. Acha kuishi kwa kushindana na wengine, kushindana kumeyafanya


maisha kuwa magumu sana kwa baadhi ya watu kwa mfano kama
utataka kushindana katika kuvaa, nakwambia hauwezi kushindana na
viwanda ambavyo huzalisha mamilioni ya pea za nguo kwa masaa
machache na eti kisa unataka tu kumuonyeshea mbaya wako ambaye
hata naye hana mchango mkubwa sana kwenye maisha yako, badala
yake ni kujiumiza na kufukuza upepo tu, wacha kushindana na watu ishi
ukishandana na wewe kujibadili katika kutoka uduni wako wa nyuma
mpaka ubora wako kwa sasa kwa kufanya ya muhimu yanayopaswa
kufanywa.

vii. Heshimu hisia za wengine hata kama zipo kinyume nawe, kufanya hivi
kutakupunguzia mawazo mengi yasiyo na maana kwenye maisha yako
kutokana na kuishi na wengine, hakikisha unapendezwa na watu
wengine kwa jinsi walivyo, epuka kushauri bila kuombwa ushauri na
mtu husika, epuka kueleza matatizo yako kwa watu unaojua kabisa
hawana msaada juu ya matatizo hayo, epuka kuwakosoa watu,
kuwalalamikia, kuwalaumu na hata kuwahukumu bali sitawisha sifa
nzuri ya kuwasifia kwakua ndicho kitu unapenda wewe na wao
wanapenda pia.

viii. Acha kuishi na mategemeo makubwa bila kuwa na uwezo wa kuyatimiza


hata kwa kuanza kidogo kidogo, kuna watu wanaelewa vibaya kuwa na

35
ndoto kubwa na kuwa na mategemeo makubwa ya kimaisha, kuwa na
ndoto kubwa ni kule kuweka malengo na mipango , mikakati, tarehe ya
mwisho ya kuyatimiza hayo na kuanza kufanyia kazi mara moja bila
kukatishwa tama, lakini kuishi na mategemeo makubwa ni kujitwisha
jambo fulani kubwa kisha ukitegemea fulani atatimiza, na asipotimiza
ndiko kuanguka kihisia na kuwa na msongo wa kimawazo acha ishi kwa
malengo ambayo una uhakika nayo kuyatimiza.

ix. Kubali kwamba si wewe tu unayepitia hali mbaya kama hiyo, maisha
hayapo upande wako tu na ugumu hauko upande wako tu , pia kuna
wengine wanapitia hali mbaya na ngumu hata wakati mwingine kuzidi
hata wewe, nakumbuka simulizi la baba yangu alipokuwa akinisimulia
kuwa kuna siku alikuwa nyumbani kwake amekaa ametulizana akiwaza
namna maisha yanavyomwendea kombo, wakati yupo kwenye lindi la
kimawazo mara ghafula alipita mtu anayemfahamu fika na mtu huyu
kwa sasa amekuwa mtu wa makamo kama yeye lakini amechoka sana
mwenye mavazi chakavu, baba yangu katika kumwangalia vizuri
alimfahamu na kumuita jina lake …….fulani…..ndugu yule aliitika na
kuelekea upande alipo baba na wakaanza kusalimiana naye, na
kukumbushana kipindi cha nyuma waliko wahi kukutana
wakatambuana kuwa wote walisoma shule moja ya msingi huko
Buswelu, anasema baada ya kusalimiana pale yule ndugu aliaga na
kuondoka, baba akawaaambia wale waliokuwa karibu yake kuwa
mnayemuona yule bwana tumesoma naye na alikuwa na akili sana
darasani, watu wakashangaa kwa kusema yule haiwezekani bwana kwa
muonekano huo, baba anasema aliacha na kuwaza juu ya ugumu wake
kuwa eti na yeye maisha yanamwendea kombo akabaki na tumaini jema
kuwa kumbe mimi afadhari.
Hii pia inaweza kukujenga na wewe usione kabisa kuwa wewe ndiye
mwenye kupitia maisha magumu peke yako hesabu baraka zako na si
kushindwa kwako, jikusukume zaidi kutengeneza hali bora maisha bora
yanakusubiri ni wewe tu.

36
x. Jipe nafasi ya kufanya yale unayoyapenda sana, haya ni kutia ndani
unayopenda na ukiyafanya unapata furaha yaweza kuwa kusoma vitabu,
kulala, kufundisha , kufanya mazoezi, kufanya matembezi, kuchora,
kuimba, kusikiliza mziki, kucheka na wengine, kuongea na wengine kwa
aina ya kufurahishana na kuelemishana, kuwasiliana na mtu
unayempenda sana na n.k

xi. Fanya kazi kwa bidii, katika kazi ndiko Mungu ndiyo alikokuwa
anakutana na Adamu kwa mjibu wa simulizi la vitabu vitakatifu, na
wewe kupitia kufanya kazi kutakupunguzia kwa kiasi kikubwa sana
kuwa na mawazo hasi ambayo mengi hukuchochea kuwa na msongo wa
kimawazo, jikite kutafuta majibu ya matatizo mbalimbali na huko ndiko
kiwango kikubwa cha msongo wa kimawazo utapotea.

xii. Wacha kulalamika lalamika, kulalamika ni tabia chochezi ya kuangukia


kwenye msongo wa kimawazo na kukufanya kushindwa yanayopaswa
kufanyika badala yake kughairisha na kutafuta sababu sababu na
mwisho unaweza kuangukia kwenye uvivu ama dhaifu usiyeweza
kutafuta suruhu ya matatizo fulani bali umebaki kuwa mlalamikaji tu na
msongo hauwezi kukuacha utaambana na wewe tu.

xiii. Kula vyakula bora, kula vyakula bora huupatia mwili wako uwezo wa juu
wa kutatua mengi ya matatizo yanayotokana na namna ya kufikiri na
utajipatia nguvu nyingi za kushinda misongo mingi ya kimawazo.

xiv. Kama unahisia fulani kuhusu, mtu fulani mwambie acha kubaki na hisia
hizo na mwisho kujipa msongo usioa na maana, kama kuna mtu
unampenda sana mwambie nakupenda, hakuna kosa kumwambia mtu
hisia zako, na kwa kufanya hivyo ni kwa kujiponya kwa haraka na
kushinda msongo wa kimawazo.

xv. Fanya yale umesema unataka kufanya, wengi wakuwa wasemaji wazuri
tu na mwisho hawafanyi kinachotakiwa kufanywa na mwisho
wamejikuta wakiwa kwenye msongo wa kimawazo juu ya yale walitaka
kuyafanya kwenye maisha yao, kama umesema nataka kufungua

37
biashara weka mipango na namna ya kukuwezesha kuanzisha biashara
itakupatia wakati mzuri wa kuondokana na msongo wa kimawazo.

2. MSONGO WA MWILI/ PHYSICAL STRESS.

Huu ni msongo unaotokana na mwili kuchoka kutokana na kazi fulani


unayoifanya na msongo wa aina hii si mbaya sana kwakua tunataka miili yetu
kuchoka ili kutupatia usingizi bora, maisha marefu, tabasamu la kudumu
usoni, n.k lakini tahadhari usipate uchovu unatokana na kuteswa ama
kupigwa na ukasema huu nao ni msongo salama kwa mwili wako hapana, huo
si msongo salama kwa mwili wako, katika kuondokana na msongo huu ni
pamoja na kuoga maji, kula vizuri, kulala vyakutosha ama kupumzika,
kufanya masaji ya mwili, kunywa maji mengi safi na salama ya kutosha.

3. MSONGO WA DAWA/MEDICAL STRESS.

Huu hutokana na huwapata watu wale wanaougua na kupatiwa dawa ya


kutibu miili yao na kwa namna fulani wanalazimika kupumzika kutokana na
nguvu ya dawa hizo walizopatiwa na kuwa katika hali hiyo wanakuwa kwenye
msongo wa kidawa, kuna aina nyingine ya upatikanaji wa msongo huu kwa
watu wanaofanya kazi kwenye maeneo yenye kiwango kikubwa cha dawa ama
kemikali kali za dawa kama watoa tiba za maji, wanaofanya kwenye vitengo
vya dawa, ama wakulima wanaotumia dawa kali mashambani kuulia wadudu
n.k hawa wote wanakumbwa na msongo wa dawa na wataalamu
wanapendekana kutumia vifaa vizito na muhimu vya kujikinga na majanga
haya ya dawa ikiwemo kukaa eneo la hewa safi, kunywa maziwa ya
kutosha,kutoka eneo la madawa na si kukaa kwa muda mrefu eneo hilo.

38
SURA YA NNE

3
NJIA SALAMA ZA KUKUONDOLEA MISONGO

Mambo mengine muhimu ya kukusaidia kuondokana na misongo aina hii ama


aina zote ni pamoja na kufanya haya:-

a) Kuwa tayari kuwajibika hasa katika eneo linakuhusu, hii ni kuchukua


kwa uzito yale yanayokuhusu kama ni mwanafunzi , soma na jifunze
kwa umakini ili usiwe na hofu ya kimtihani, kama ni mzazi kuza
watoto wako kwa kuwapatia mahitaji stahiki yanayotakiwa n.k

b) Jenga mfumo mzuri wa mawasiliano baina yako wewe mwenyewe


yaani wewe na wewe na watu wengine kuanza kuishi vizuri na kuwa
na furaha.

c) Jifunze kujijali na kujipatia muda wa kwako peke yako kufanya kitu


kinachokufurahisha walau kila baada ya muda fulani.

d) Jifunze kusikiliza na kuelewa kila jambo ambalo watu wanataka


kukuambia badala ya kuwasikiliza ili ujibu, sikiliza kuelewa.

e) Wacha kutaka kufanya mambo yote kwa wakati mmoja bali jifunze
kujipatia ratiba ya mambo mbalimbali na acha kufanya jambo
ambalo halipo kwenye ratiba yako.

f) Kuwa mwaminifu na kwa watu unaowapenda na shikamana nao


watu hao iwe mtaani, kazini kwako, na maeneo mbalimbali.

39
SURA YA TANO.

1
MAISHA YA MAFANIKIO NA FURAHA.

M
aana halisi ya kufanikiwa yaweza kuwa kwa njia rahisi tu nayo ni
kupata kile unachotaka iwe kwenye mtazamo chanya ama hasi kama
umepata kile ulichokuwa unataka unakuwa kwenye fanikio fulani la
jambo unalolitaka na hapo hapo utakuwa na nafasi ya kuwa mwenye furaha
kwakua umetimiza jambo ulilokuwa unalitaka.

Pamoja na kwamba mafanikio limekuwa jambo lenye kuwatesa wengi na kuwa


hanganisha na wengi kutokana na kutafuta kile kinachoitwa mafanikio
wamejichoma vibaya na kusababisha kupoteza kiwango kikubwa cha kupoteza
furaha ya maisha na uzuri wa maisha na kuishia kuishi maisha ya majuto na
yasiyo hata chembe moja ya furaha, muangalie yule anayefanya umalaya kwa
ajili ya kujipatia kipato cha kutaka mafanikio ya kununua nguo, na
kubadilisha milo ama kununua gari bora la kisasa kabisa, na mwisho
kajichoma na gonjwa baya ambalo linaogopesha na limechukua uhai wa
wengi, ama mwangalie yule kijana anayefanya kazi ya kuiba na kupora mali
kwa kutumia nguvu, ambavyo anaishi maisha ya kujifichaficha machoni pa
watu wenzake na mwisho anaishia kuwa jela, mifano inaweza kuwa mingi,
lakini kwa ufupi safari ya kutafuta mafanikio si jambo ambalo linapaswa
kukutosa kwenye lindi la kuishi bila furaha na mwenye huzuni kuu na kukosa
maana ya maisha.

Mafanikio halisi yanapaswa kuenenda na kuiishi kwa furaha na mwenye


amani ya moyo na mwenye uwezo wa kuwa wewe na si mwenye kuendeshwa
na mafanikio kiwango ambacho kinakupelekea kujiuumiza vibaya na kukosa
uhalisia wa maisha, pamoja na kwamba mafanikio hayaji bila kuchukua hatua
fulani muhimu basi kuyakosa napo mafanikio nako ni yanaweza kuwa

40
matokeo ya kuishi maisha yasiyo kuwa na furaha, twawajibika kuwa na furaha
na wakati huohuo tukiwa wenye mafanikio.

Kuna watu wanapoingia kwenye utafutaji wa maisha wamekuwa watu wa


ajabu sana kwa kutaka kupata vitu burebure ama kutaka kuona mambo
yakifanyika tu bila wao kutia juhudi fulani kwenye kuyatafuta mafanikio,
hakuna vya bure, kutaka kupata mafanikio yatakutaka kulipia gharama fulani
na ujitoe kwa ukweli kufanya kazi, na kwakua kuchagua njia ya kupata kwa
urahisi baadaye inaweza kuwa ni moja ya njia ngumu sana kwako yenye kuja
na maumivu mengi sana kwako.

Kuna mambo mengi yanayowafanya watu kushindwa kufanikiwa ikiwa ni


pamoja na haya yafuatayo na kama unaona na wewe yanakugusa kwa namna
moja ama nyingine basi wawajibika kuyabadili mara moja kuanzia sasa ili
uweze kuona mafanikio unayoyataka kwenye maisha yako na uanze kuiishi
maisha ya furaha.

Mambo hayo ni pamoja na:-

a) Kukosa vipaumbele.

Huku ni kule kuwa mtu mwenye kufanya kila kinachokuja mbele yako na kwa
kufanya hivyo unakosa umakini kwenye mambo muhimu yanayopaswa
kufanyika kwa umakini, ana kupoteza rasilimali muhimu za kufanyia mambo
muhimu ambayo yangekupatia mafanikio ya haraka, kitendo cha kuwa na
vipaumbele hutia ndani kuwa na nidhamu ya kufanya jambo linalopaswa bila
kuachana nalo na kufanya mengine kisa unafuata ushabiki wa watu wengine
na hisia, mambo yanayokukosesha uwezo wako wa kuyapata mafanikio
unayoyataka.

b) Kuangalia njia fupi za kufanikiwa.

Mafanikio ya kutafutwa kwa njia fupi huleta madhara mengi kwenye maisha
na hakuna jambo ambalo linaweza kudumu kwa muda mrefu kama
limepatikana kwa njia ya haraka na isiyoeleweka, kwa mfan0 leo ni rahisi
kuwakuta vijana wa makamu na watu wazima wakitafuta mafanikio ya kifedha
kwa kubeti ama kucheza michezo ya kubahatisha, hukuna mafanikio ya
namna hiyo ambapo unaweza kusema umeyapata na kuwa utatudumu nayo,

41
maisha yanataka kujitoa, kufanya kwa viwango vya juu na uwe mtu mwenye
kuwajibika sana.

c) Kukosa kujiamini.

Kama wewe mwenyewe tu haujiamini ni nani unataka akuamini, hakuna uzuri


wa kujiamini katika wewe kwanza unaweza kutokeza ushindi unaohitajiwa,
unapokosa kujiamini na ujasiri utakimbia huku na kule, na utaishia kufanya
mambo ambayo hayakusaidii kwa sababu hauna kujiamini na unafanya
kutaka kukubalika tu, badili mwelekeo kwa kuanza kujiamini sasa na ufanye
kwenye uwezo wako ukiwa na nguvu na ujasiri kutokeza mambo bora.

d) Kukosa malengo na maandalizi ya mafanikio uyatakayo.

Haitoshi kusema tu unataka kufanikiwa na ufanikiwe inahitaji kuweka


malengo na kufanya maandalizi ya kutosha juu ya malengo unayoyataka
kuyatimiza kwenye maisha yako na kwa angalau kuwa na malengo na
maandalizi hukufanya ujiamini na kukusaidia kufanya kwa kiwango cha juu
na mwisho kupata matokeo ya juu.

Maandalizi ni muhimu kwa kila sehemu yanapohitajiwa mafanikio ya aina


yoyote, kujiandaa ni kuona kushindwa kwa uhalisi na haukubali kumezwa na
kushindwa huko unajiandaa na kukabiliana na kushindwa huko, kujiandaa
hutia ndani kujifunza kutokana na makosa na kuyaepuka makosa
yanayokukwamisha usifanikiwe.

e) Kuendeshwa na uoga.

Uoga imekuwa sumu namba moja inayoua vipaji vya wengi na kuwafanya
watu kuishi maisha ya kawaida kisa tu wameendekeza uoga wa aina yoyote na
kuwafanya washindwe kuamua kutaka kufanya makubwa kwenye maisha na
moja ya uoga mbaya wanaokutana nao watu wengi ni pamoja na uoga wa
kushindwa, uoga wa kujiandaa, uoga wa kutokujua na hawataki kujifunza
anabaki kusema sijui, uoga wa kushindwa, uoga wa kukosolewa, uoga wa
kukataliwa, uoga wa mafanikio, na uoga wa kufanya maamuzi na mwisho
kuishia kufanya maamuzi mabaya kwa kuendeshwa na hisia zaidi ama
ushabiki, n.k

Njia ya haraka ya kuondokana na uoga ni kufanya tu kwa namna yoyote


kuanza kufanya lile ulilopanga kulifanya na mwisho kupata uzoefu kutokana

42
na kujaribu huko na kushindwa kwingi ndiyo kunakupatia nafasi kubwa ya
kufanikiwa.

f) Kutokujitambua na kutumia vipaji vyetu.

Kila mtu ana aina yake ya uwezo wa kipekee ambao kutokana na uwezo huo
anaweza kujipatia mafanikio kutokana nao, sasa wengi hatutumii vipaji vyetu
na uwezo huu na mwisho tunakufa tukiwa hatujatumia chochote katika
kuifanya dunia kuwa mahali pazuri pa kuishi, kwa asili binadamu waliotumia
uwezo wa juu wa uwezo wao walionao wametumia kwa asilimia 10% mpaka
12% tu na wamefanya makubwa lakini je kama wangeamua kutumia asiliamia
40%? anatufahamisha ndugu Willium James, amua kwa kutumia njia
zilizoanishwa kugundua vipaji vyako na uvitumi kwa juhudi katika kukusaidia
kufanikiwa.

g) Kutokujiuliza maswali muhimu na kujipatia majibu


sahihi.

Kujiuliza ama kuuliza maswali sahihi imekuwa njia mama ya watu kujifunza
wasioyajua, na njia hiyo imewaokoa katika kufahamu mengi kuliko wale wasio
uliza maswali wameishia kuwa na ufahamu ule ule walio nao, katika
kuendeleza jambo hili zuri la kuuliza maswali basi tunawajibika pia kujiuliza
maswali sahihi na kuyapatia majibu sahihi mfano wa maswali hayo ni pamoja
na:-

1. Je una kusudi linaloeweka kuhusu maisha yako?


2. Je una malengo na mipango ya kutimiza malengo hayo?
3. Je ni juhudi gani unaweka kwenye maandalizi kufanikisha
mafanikio yako?
4. Je ni gharama kiasi gani upo tayari kulipa ili kuyapata mafanikio
unayoyataka?
5. Je ni kwa mwendo gani upo tayari kwenda kuyatimiza mafanikio
yako?
6. Je una uvumilivu unaotakiwa kwenye safari ya mafanikio
kwamba upo tayari kila ukianguka utaamka?
7. Je una kanuni na falsafa zako za kukuwezesha kusimama?
8. Je unatabia zinazotakiwa kwa watu wanaotaka kufanikiwa kama
kuwa na maono na kuwa na kauli ya NAWEZA, NITAFANYA, NI

43
LAZIMA , roho ya kimafanikio kwa mujibu wa aliyekuwa
mwenyekiti wa makampuni ya IPP, marehemu Reginald Mengi?
9. Je wajua kwa hakika mzizi wa matatizo yako ama yenu?
10.Je utaachana na ubinafsi na uroho kuyatafuta mafanikio?

Hayo na mengine mengi yanaweza kuwa njia bora ya kuanza kujiuliza na


kuyapatia majibu stahiki yanayohitajika kwenye maisha yako ili uwe na nafasi
nzuri ya kuanza kufanikiwa kama utaamua kutumia uwezo wako wote na
kujiuliza maswali sahihi na kuamua kutenda.

44
SURA YA TANO.

2
VIAMBATA VYA MAFANIKIO.

B
aada ya kuona sababu zinazowasababisha wengi kushindwa
kupayapata mafanikio ni muhimu sasa kuona viambata muhimu vya
mtu anayetaka kufanikiwa na kuishi maisha ya furaha.

1. Ona picha kubwa akilini mwako kuhusu maisha yako, ona ukifanikiwa,
ona ukiwa mtu mwenye mafanikio makubwa.

2. Usijikatishe tamaa na kujikatisha moyo juu ya uwezo wako.

3. Kuza uwezo wako na nguvu za maarifa kukabiliana kila na gumu.

4. Amua kuwa mtatuzi wa matatizo ishi ukitafuta matatizo na jipe muda na


nguvu ya kuyatua matatizo hayo.

5. Mara zote kuza uwezo wako wa kufikiri na jifunze kufikiri kwa urefu na
kwa ubunifu juu ya kila changamoto.

6. Usingalie kutokuwa na kitu, ona na ishi kwenye dunia yenye kila kitu na
kazi yako ni kwenda kuchukua ama kutafuta na kupata.

7. Ambatana na watu wenye tabia njema na wenye mafanikio.

8. Jifunze kutokana na makosa ya wengine na uyaepuke badala ya


kuyapuuza, kwa mfano mtaani kwako kuna wazee wanaishi maisha

45
magumu na ya tabu inaweza kukupati funzo gani kwako juu yao?
ukipata funzo hilo fanyia kazi.

9. Weka malengo na wajibika kwayo kwa kupanga kufanikiwa na si


kutokufanikiwa.

10.Jipongeze kila hatua unayofikia ambayo imetokana na kujikaza na


kuweka nidhamu fulani, kufanya hivyo kutakuongezea molari ya kutaka
kufanya zaidi na zaidi.

46
~MWISHO~
Ukiwa umesoma sura za kitabu hiki cha “najifahamu furaha ya kuwa
mimi” weka kwenye vitendo angalau hata kwa jambo moja
kubwa ambalo unataka kuriboresha kwenye maisha yako, kila
unapoanguka endelea kujihamasisha kuwa unaweza na
utafanikiwa na mwisho utaondoka duniani ukiwa mtupu na
mwenye furaha kuu na kutokeza kumbukumbu la kukumbukwa
na kila mmoja na hata kusimuliwa kila vizazi ukiwa unaishi hali
ya kuwa mwili wako ukiwa kaburini.

Uwe na usomaji mwema, endelea kujifunza zaidi na zaidi


uwekezaji huo unao fanya hauna hasara kwako utakulipa kwa
namna ya ajabu usiyotarajia.

WASILIANA NA MWANDISHI WA KITABU HIKI KWA


MAWASILIANO YA SIMU 0759880010 ama kwa barua pepe
michaelcharles44@ymail.com.

47

You might also like