Professional Documents
Culture Documents
1
KUBALI HIVI SASA
Hakimiliki zote zipo chini ya ©Elisha Daudi
Mwakalinga
emwakalinga@myfaithlife.co.tz
ISBN: 978-9976-5267-3-8
©2022
Kimechapwa na
Truth Printing
0764 425 704/0692 637 282
geofreymakula@gmail.com
Dar es Salaam-Tanzania
2
YALIYOMO
SHUKRANI ZA PEKEE ..................................................................... 5
WALENGWA ......................................................................................... 6
UTANGULIZI ..................................................................................... 7
Sura ya Kwanza .............................................................................. 10
KUWA MMOJA WAO ..................................................................... 10
Sura ya Pili ....................................................................................... 26
WEKEZA KWA WATU ................................................................... 26
Sura ya Tatu .................................................................................... 34
JENGA TABIA ................................................................................. 34
Sura ya Nne ..................................................................................... 40
KUBALI KULIPA GHARAMA......................................................... 40
Sura ya Tano ................................................................................... 54
USILISHE NJAA LISHA MAONO ................................................. 54
Sura ya Sita...................................................................................... 69
TENGENEZA MFUMO WAKO WA MAOMBI ............................. 69
Sura ya Saba ................................................................................... 74
WATU WAKUU HUANDALIWA SIRINI ....................................... 74
Sura ya Nane ................................................................................... 86
JIBORESHE ..................................................................................... 86
Sura ya Tisa ..................................................................................... 92
UPINZANI NI SEHEMU YA MAISHA UNAPOINGIA HATUA
NYINGINE ........................................................................................ 92
3
Sura ya Kumi ................................................................................... 96
TUMIA UWEZO WAKO WOTE..................................................... 96
Sura ya Kumi na Moja .................................................................. 101
USIOGOPE CHUKUA HATUA.................................................... 101
IKIWA HAUJAOKOKA NA UNATAKA KUMPA YESU MAISHA
YAKO .............................................................................................. 107
4
SHUKRANI ZA PEKEE
Shukrani zangu za dhati ni kwa Mungu Baba wa
Mbinguni aliyeniwezesha kwa msaada wa Roho
Mtakatifu kukamilisha kazi hii mpaka ikatoka.
5
WALENGWA
Walengwa wa kitabu hiki ni watu wote wa kike
na wa kiume ambao wanajua Mungu amewaita
kumtumikia katika nyanja mbalimbali,
watumishi vijana ambao tayari wanaendelea na
huduma, walezi na wazazi ambao wanatamani
vijana wao wafikie ndoto kubwa za kulitumikia
shauri la Mungu. Neno hili limetoka kwa Bwana
nalo ni ajabu machoni petu (Zaburi 118:23)
6
UTANGULIZI
Tangu zamani Mungu amekuwa akiwaita watu
mbalimbali makundi kwa makundi ili wamtumikie
Mungu katika huduma na maeneo mbalimbali. Japo si
wengi wanajua kitu ambacho Mungu ameweka ndani
yao, lakini angalau wanasikia wito wa kutumika. Swali
langu ni hili; Kanisa au jamii imejipangaje kulea,
kutunza na kukuza vipawa hivyo ndani ya watu hasa
vijana? Ni kweli kwamba wana vitu vizuri na vikubwa
ndani yao lakini je! Nani anajali malezi yao ili kesho
waweze kufikia pale walipokusudiwa?
7
Mungu, unahitaji muda wa kutosha wa maandalizi
ambao ndani yake umebeba kukuandaa kimwili, kiroho
na kiakili kusudi utakapoanza kuyatenda uweze
kutenda kwa ubora mkubwa. Lakini pia muda wa
maandalizi ndio unaotengeneza msuri wako na uimara
wako kiasi ambacho utakapoanza safari uweze
kuendelea vizuri pasipo kuyumbishwa njiani.
8
swali lako moja baada ya jingine na kukuwekea ndani
yako msingi mkubwa kuelekea kwenye ndoto na maono
uliyo nayo.
9
Sura ya Kwanza
KUWA MMOJA WAO
K
atika karne hii tuliyonayo, bado Mungu
anatafuta watu wa kufanya nao kazi, watu
ambao atatukuzwa kwa sababu yao, watu
ambao watamfanya Mungu ajulikane. Macho yake yapo
kila mahali kuangalia watu wa namna hiyo. Najua ni
wengi waliookoka lakini walio tayari kutumika kwa
ajili ya Mungu sio wengi, walio tayari kuyatoa maisha
yao jumla kwa ajili ya Mungu na Ufalme wake hawapo
kila mahali, ni kundi dogo sana.
10
akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila
alipopita njia ile, huingia kula chakula. Yule
mwanamke akamwambia mumewe, Tazama,
mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu
mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.”
11
kuiona sifa hii kwanza kwamba wewe ni mtu mtakatifu
wa Mungu.
12
mashuleni na vyuoni, basi kwa sehemu kubwa
tutaokoa kizazi hiki ambacho wengi maisha yao na
ndoto zao zinaishia njiani. Tunahitaji vijana wenye sifa
hii ya utakatifu wa kweli ili kuleta mabadiliko chanya
katika nyanja zote.
13
Mambo yanayosababisha kukosekana kwa
utakatifu wa kweli siku hizi za mwisho.
i. Kukosa nidhamu.
14
ii. Kukosa muda na Mungu.
2. Mtumishi.
15
Yehoshafati akasema, Neno la BWANA analo
huyu.” Huyu Elisha hakuwa tu anamimina maji
kwenye mikono ya Eliya, amewahi pia kufanya mambo
makubwa sana ikiwemo kuyapiga maji ya mto wa
Yordani yakagawanyika huku na huku naye akavuka
akiwa mwenyewe (2 Wafalme 2:14), Wana wa Manabii
walipomwambia kwamba nchi inazaa mapooza,
alifanya ule muujiza wa kuyaponya maji (2 Wafalme
2:19-22) Mwanamke mmojawapo wa wana wa manabii
alipompelekea kesi kwamba watoto wake wanataka
kuchukuliwa utumwani ili kulipa deni ambalo mume
wake aliliacha. Elisha alisababisha muujiza kwa yule
mama (2 Wafalme 4:1-7) pamoja na miujiza mingine
mingi aliyofanya, Elisha alikuwa akijulikana kama
mtu aliyekuwa akimimina maji kwenye mikono ya
Eliya.
16
vivyo hivyo ukitaka kufikia hatma kubwa huna budi
kuvaa roho ya utumishi.
17
3. Mpakwa mafuta wa Mungu.
18
Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko
na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote
walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu
alikuwa pamoja naye.” Tunaweza kuwa na pesa
nyingi, muziki mzuri kwenye makanisa yetu na kila
kitu kinachohitajika, lakini kama tutakosa mafuta ya
Roho Mtakatifu na nguvu zake basi itakuwa ni sawa na
bure. Mafuta ni nguvu za Roho Mtakatifu za
kutusaidia kutimiza kila kusudi lake ndani yetu. Kama
tunaweza kufanya kazi ya Mungu pasipo nguvu za
Mungu ni bora sana kama tukiacha na kutafuta kazi
zingine za kufanya. Tunatakiwa tufike hatua ambayo
hatuwezi kutekeleza chochote katika huduma zetu bila
nguvu za Mungu.
19
Osinachi Kalu Okoro Egbu maarufu kama
Sinach mwimbaji wa nyimbo za kuabudu nchini
Nigeria na duniani alipohojiwa kuhusu siri ya sauti
yake alieleza mambo matano kama siri ya watu
kuguswa na kubarikiwa kila anapoimba. Akiendelea
kuzungumza alisema “Watu wanaweza kukumbuka
wimbo ambao umeimba, lakini hawawezi
kusahau mguso na mtembeo wa nguvu za Roho
Mtakatifu ulipokuwa unaimba, hawawezi
kusahau jinsi Roho Mtakatifu alivyosema nao,
hawawezi kusahau jinsi Mungu
alivyowahudumia kila mmoja kwa namna
mbalimbali” Hili ndilo jambo la msingi sana kwa
waimbaji na watumishi wa Mungu.
20
Wakorintho 4:19-20. Nguvu za Mungu bado zipo ndani
yako?
21
maili 5 ambazo ni kilomita 8. Sasa jumla ya kutembea
kwao siku ile ilikuwa maili 32 ambazo ni sawa na
kilometa 51.
2. Nia safi.
22
Eliya kwa mara ya kwanza na kuanza safari pamoja ya
kumtumikia Mungu, jinsi Elisha alivyojitoa (1 Wafalme
19:15-21) mpaka Eliya anaondoka machoni pa Elisha,
nia yake ilikuwa ni Mungu atukuzwe.
3. Hakuipenda dunia.
23
alipokea ukoma badala ya mafuta ambayo
angeyapokea toka kwa Elisha.
24
mpakwa mafuta wa Mungu. Wakati ulimwengu
unahangaika na namna yake, wewe baki katika
mambo haya, baada ya muda dunia itajua yuko Mungu
ndani yako na watu wataijia nuru yako.
25
Sura ya Pili
M
oja ya mambo yaliyolikumba kanisa, jamii na
mtu mmoja mmoja ni ubinafsi wa kufikiri
ukiwekeza kwa watu basi baadae wanaweza
kukuzidi hivyo unajaribu kuweka wivu. Dr. Paul
Enenche anasema hivi "Ukiwainua watu, baadae watu
hao watakuinua wewe" hivyo hakuna unachopoteza.
Wekeza rasilimali zako kwa watu, muda wako, vipawa
vyako viguse maisha ya watu, haijalishi hata iweje,
huwezi kubaki chini au kuwa mtu wa chini. Kiwango
unachowekeza kwa watu ndio kiwango cha matokeo
utakayokuwa nayo kesho.
26
kwa kufanya hivyo unakuwa umejitengenezea
barabara nzuri ya kuelekea katika mafanikio yako.
27
nne hivi. Kumbuka wakati huo Daudi alikuwa sio
Mfalme bado, lakini kwa kile alichokuwa nacho alianza
kuwekeza kwa hao watu. Kwanza kushughulika na
hali walizokuwa nazo, kisha kuwakusanya wawe kitu
kimoja na kuwa jeshi kubwa na lenye nguvu sana
katika Israeli hakikuwa kitu chepesi. Umewahi kufikiri
kama walikuwa wanakaa pangoni, walikuwa wanakula
nini watu mia nne kila siku? Bila shaka kuna neema ya
Mungu ya ajabu iliyokuwa juu ya Daudi kuwawezesha,
lakini pia hawa watu hawakuwa watu wa kawaida.
Tafiti zinasema, miongoni mwao kulikuwa na askari
wengi wenye uzoefu waliotoroka kutoka makabila ya
mashariki, Benjamini na Yuda ili kuja kujiunga naye.
(I Nyakati 11:10-15)
28
vikosi mbalimbali. Angalia “Haya ndiyo majina ya
mashujaa aliokuwa nao Daudi...” 2 Samweli 23:8.
Watu hawa walimsaidia Daudi alipokuwa amechoka
asiweze kuuawa na adui zake, badala yake
wakasimama kupigana kwa ajili ya Daudi. “Basi
kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli;
Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi
wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye
Daudi akaishiwa na nguvu. Naye Ishi-benobu,
aliyekuwa mmojawapo wa Warefai, ambaye uzito
wa mkuki wake ulikuwa shekel mia tatu za shaba
kwa uzani, naye amejifungia upanga mpya,
alijaribu kumwua Daudi. Lakini Abishai, mwana
wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti,
akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia,
wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi
kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli.”
2Samweli 21:15-17.
29
mbele za Bwana; akasema, Mungu wangu apishe
mbali, nisifanye hivi; je! Ninywe damu ya watu
hao waliohatarisha nafsi zao? Maana kwa hatari
ya nafsi zao wameyaleta. Kwa hiyo hakukubali
kuyanywa. Hayo ndiyo waliyoyafanya wale
mashujaa watatu.” 1 Samweli 11:17-19. Unaelewa
maana yake nini? Hawa watu walikuwa tayari
kuhatarisha na kupoteza maisha yao kwa ajili ya
Daudi.
30
Kwenye maisha yako jitahidi kuwe na mtu angalau
umemwinua toka chini alipokuwa kufika ulipo au hata
zaidi yako. Danieli aliwainua wenzake na akawaweka
kwenye nafasi za juu. “Tena Danieli akamwomba
mfalme, naye akawaweka Shedraka, na Meshaki,
na Abednego, wawe juu ya mambo yote ya Uliwali
wa Babeli; lakini huyo Danieli alikuwa akiketi
katika lango la mfalme.”
31
huwezi sema mabaya juu yake watu wakanyamaza,
lakini pia ameinua walimu wengi sana wa aina yake
ambao sasa ni ushuhuda unaotembea, ameinua
waombaji wengi sana katika taifa hili, ametengeneza
wachungaji, ameimarisha huduma nyingi kwa kile
anachofanya, amegusa maisha ya watu kwa kiasi
kikubwa; Mchungaji Dr. Eliona Kimaro, Mungu
amempa neema ya ajabu sana huyu baba, hakuna
ubinafsi ndani yake, ameinua watu wengi sana kupitia
mikono yake katika kile anachokifanya, amewasaidia
wengi kujitambua, amewaelekeza na kuwaonyesha njia
ya kupita, amefanyika daraja kubwa sana la kuvusha
vipawa na huduma za vijana wengi kufikia kiwango
cha utukufu ambacho walikusudiwa na Mungu,
amewasaidia vijana kiuchumi na kujitegemea. Ninaye
baba na rafiki yangu mtumishi Paul Mwangosi, katika
huduma yake ya uimbaji, huwezi kuzungumza juu ya
huduma ya kusifu na kuabudu nchini Tanzania bila
kumtaja Paul Mwangosi. Amewasaidia waimbaji wengi
hapa nchini, wengine sasa hivi wamekuwa maarufu
lakini walipita katika mikono yake, amewaelekeza njia,
wengine amewapa nafasi ya kuonesha walichonacho na
sasa wamekuwa watu wakubwa; kwa kile Mungu
alichompa amehusika kupanda moyo wa Ibada katika
taifa hili ambapo kuna vitu tunaviona leo ni matunda
yake, amepanda moyo wa Ibada kwenye makundi
mengi ya kusifu na kuabudu yaliyopo makanisani na
32
binafsi, na wengine wengi ambao nisingweza kuwataja
nikamaliza hapa.
33
Sura ya Tatu
JENGA TABIA
N
i dhahiri kwamba kuna vitu vingi kwenye
maisha yako vinategemea tabia yako ili
uvipate, vilevile ili uweze kufikia hatima
njema unahitaji kujenga tabia njema na bora. Samsoni
pamoja na kwamba alikuwa ni mnadhiri wa Mungu na
mtu aliyeitwa na Mungu mwenyewe ili kuja kuwaokoa
Israeli na mkono wa adui zao Wafilisti, bado tabia yake
ya kupenda wanawake ilimwangusha na
kumwangamiza kabla ya wakati wake. Haijalishi una
vipawa vingi na vizuri namna gani kama tabia zako ni
mbovu hautafika mbali, kuwa na vipawa, maono na
ndoto ni jambo moja lakini tabia itaamua umbali
utakaoenda nao katika hivi vyote; lakini pia tabia
itaamua ubakie katika unachofanya kwa ubora na
nguvu ile ile kwa muda gani. Chunguza ndani yako, ni
tabia gani ambayo unaona ni kikwazo kwako? Nenda
nayo mbele za Mungu ili akusaidie kuishinda na
kutengeneza kitu kipya ndani yako.
34
hauna ndani yako basi itakuwa vigumu kuendelea
kubakia katika unachofanya kwa moto na upako ule
ule uliokuwa nao mwanzo. "Maana tu kazi yake,
tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo
mema, ambayo tokea awali Mungu aliatengeneza
ili tuenende nayo." Waefeso 2:10
Tabia ya uaminifu.
35
namna Mungu alikuwa akimtumia Paulo na kumwinua
viwango vya utumishi wake kila wakati, lakini
ukifuatilia utaona ni kwa sababu ya uaminifu.
Anasema “Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana
wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa
mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake;” 1
Timotheo 1:12. Yesu aliona uaminifu ndani yake ndipo
akamuweka katika utumishi, tunaoona matunda yake
yakizalishwa mpaka kesho. Uaminifu kwa Mungu ni
kigezo kikubwa cha kukuinua na kukuweka katika
nafasi ya juu aliyokusudia kwako. Viwango vingine vya
utumishi vinahitaji uaminifu na viwango vingine vya
upako vinahitaji uaminifu ndani yako. Uaminifu wako
kwa watu na kwa Mungu ni ngazi ya kupandia
kuelekea katika ukuu wako.
Kuwa na subira.
36
umeharibu maana wakati wake ulikuwa bado. Mngoje
Bwana kwa Saburi na utulie mbele zake. Hata
ungefika mahali pa juu pa ukuu sana, kama utakosa
subira basi tutashuhudia ukurupukaji katika
maamuzi, kufanya vitu bila kujipanga na kufanya chini
ya kiwango kwa sababu ndani yako kutakosekana si tu
uvumilivu bali utulivu pia. Kumbuka subira ni
uvumilivu wenye utulivu ndani yake.
Tabia ya unyenyekevu.
37
wa Mungu, hautafuti kujulikana wewe katika jambo
ulifanyalo bali Mungu.
Tabia ya utakatifu.
38
neno la Mungu, ni kujitenga na uovu na kuamua kuishi
kwa haki.
39
Sura ya Nne
KUBALI KULIPA
GHARAMA
M
oja ya mambo muhimu na yasiyopendwa na
vijana na watu wengi licha ya kwamba wana
ndoto na malengo ya kufika mbali ni kulipa
gharama. Wengi wanatamani kufanikiwa katika
wanachofanya, lakini hawako tayari kulipa gharama za
kufika huko kwa sababu kulipa gharama ni gharama
kuilipa. Uzuri ni kwamba kila unachokitaka kina
gharama zake za kukipata, na kuna vitu huwezi
kuvipata kwenye maisha isipokuwa umelipa gharama
zitakazokuwezesha kupata unachotaka.
40
Zipo gharama za aina tofauti tofauti ambazo
unapaswa kulipa ili kufikia katika kiwango cha
utukufu ambacho Mungu amekusudia kwa ajili yako
kulingana na ulichopewa. Hapa chini nimekuwekea
baadhi tu ya gharama ambazo ni za muhimu na lazima
kwa mtu yeyote anayetaka kuacha alama duniani na
kuwa baraka kwa kizazi hiki na kijacho.
41
kwenye hatima yako kubwa au yanakubomoa? Kaa
chini jiulize swali hili; katika mambo yote unayofanya,
vitu vyote unavyokimbizana navyo je vinakufaa na
kukujenga? Jiulize marafiki ulionao, je wanakufaa?
Wanakujenga au wanakubomoa? Wanakusaidia kuwa
wewe halisi ambaye Mungu amekusudia uwe au
wanakuondoa katika mpango wa Mungu? hii ndiyo
gharama unayopaswa kuilipa, kukubali kuacha baadhi
ya vitu visivyokufaa na kukujenga ili upate vile
ambavyo Mungu amekusudia kwako.
42
Jitathmini, ni mambo gani ukiyatazama unaona si
kitu kwa ajili ya kitu ulichonacho ndani? Pili; kile
unachokitaka kwenye maisha kinatakiwa kiwe na
nguvu kuliko kitu kingine chochote kwenye moyo wako,
kisha kikutengenezee nidhamu ya kukaa na kutembea
nacho mpaka umekipata. Uzuri usio na kiasi wa
kumjua Kristo Yesu ulimfanya Paulo aone kila kitu
ambacho hakimuelekezi kumjua huyu Yesu kiwe si
kitu. Usianze kukimbizana na kila kitu, acha vingine
vikupite kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kitu
ambacho Mungu ameweka ndani yako. Kubali hivi sasa
maana mbele kuna utukufu mkubwa sana ambao
Mungu ameandaa kwa ajili yako.
43
kiutumishi wanajikuta wanakiona kila kitu si muhimu
kwa wakati huo. Nina rafiki yangu ambaye aliacha
kazi ya ualimu ili aweze kumtumikia Mungu. Kulipa
gharama kwa kukubali kuachana na baadhi ya mambo
hakuna maana kwamba hayo mambo hayana umuhimu
kwako, la hasha! Ila unaangalia kilichoko ndani yako
na kule unapaswa kuelekea.
44
akainuka, akamfuata Eliya, akamhudumia.”
1Wafalme 19:19-21
45
anazolima kwa siku atavuna gunia 120 (Haya ni
mavuno ya shamba alilolima kwa siku moja).
46
Jidhabihu.
47
kuchipuka hata pangekuwa pagumu namna gani
itachipuka tu na itaota na kuzaa matunda, na wale
ambao waliikanyaga ikiwa ardhini watatamani
matunda yake.
Muda.
48
kufika au kuwa. Muda wa saa 24 ni mchache sana
kufanya kila kitu, chagua mambo ya msingi ya kuyapa
muda wako kama tu unataka kufikia malengo na
kufanikisha ndoto yako.
49
tumia muda wako kujifunza kuhusu huduma hiyo,
wekeza katika maombi, mifungo, soma vitabu vya
watumishi mbalimbali, soma neno la Mungu, kaa na
watu ambao wamefanikiwa katika eneo hilo.
50
Mipango.
51
Mwendelezo.
52
Siku moja nilikuwa naongea na mtu mmoja
ambaye Mungu amemuita eneo la Maombi, hasa
kuombea watumishi na kazi ya Mungu, lakini kwa
sababu ya changamoto za maisha na masuala ya kazi
ameacha wito huo, nikaongea naye kwa kirefu na
kumweleza bila kusita kwamba anatakiwa kusimama
tena na kufanya wajibu huo bila kuangalia mazingira
yanasemaje. Muendelezo unahitaji uvumilivu sana ili
uweze kufikia makusudi ya Mungu kwako.
53
Sura ya Tano
K
ulisha njaa ni kufanya maamuzi kwa
kuangalia hali yako ya sasa bila kujali kesho
yako itaathiriwa kwa kiasi gani na maamuzi
unayofanya. Tuna watu wengi sana waliopoteza
mwelekeo, wameacha kufanya vitu walivyoitwa na
Mungu kuvifanya, wameyaacha maono wanafanya vitu
vingine kwa sababu tu walikutana na hali
zilizowalazimisha kufanya maamuzi bila kuangalia
matokeo ya maamuzi yale katika kesho yao.
54
chenye kukufaidisha hata kingeonekana kama
dhahabu, lazima ujifunze kuona kama Mungu aonavyo
ili uweze kuwa salama katika zamani hizi.
55
Kukubali kulisha maono ni gharama sana, njaa ya
muda mfupi inaweza ikakusahaulisha unakoelekea;
njaa ya siku moja ilimfanya Esau auze haki yake ya
mzaliwa wa kwanza na kujikuta maisha yake
yanakuwa tofauti kabisa na vile Mungu alimkusudia.
Jifunze kutokana na makosa ya watu hawa ili usifanye
kama wao;
ESAU.
56
Kuna maswali ya kujiuliza katika habari hii; Mosi,
je! Mama yao (Rebeka) hakupika chakula siku hiyo
mpaka Esau aende kumuomba Yakobo chakula chake?
Pili, Esau hakupata kitu kabisa alikokuwa ameenda
kuwinda ili akifika nyumba ajitengenezee apate kula?
Tatu, Kama alipata mawindo, nini kilimfanya
ashindwe kuvumilia kidogo tu ajitengenezee chakula
chake kuliko kuingia kwenye mtego wa hatma yake?
Nne, Hakujua haki ya mzaliwa wa kwanza kwamba
imebeba baraka kiasi akaidharau na kuitoa kwa
chakula cha dengu? Tano, Wazazi wao walikuwa wapi
wakati hii biashara inafanyika iliyoathiri maisha yao
ya baadae? Majibu utakayoyapata katika maswali haya
utagundua Esau alikuwa na shida kubwa maana
aliidharau haki ya mzaliwa wa kwanza. Kudharau
maono, ndoto na vipawa kwa ajili ya chakula cha siku
moja kunaweza kukugharimu maisha yako yote ya
baadae ambayo Mungu alikusudia kwako.
57
26:35. Sasa ona, kosa moja limegharimu mpaka maisha
yake ya mahusiano. Alioa wake ambao wazazi wake
hawakupenda, si tu kwamba hawakupenda ila Esau
aliwadharau wazazi wake katika suala la kuoa tofauti
na Yakobo ambaye Biblia inasema “Na ya kuwa
Yakobo amewatii babaye na mamaye...” Mwanzo
28:7
58
muhimu kuliko unavyoweza kufikiri. Wakati mwingine
huwa natamani Mungu angemuonesha kila mtu picha
ya maisha yake ya baadae aliyomkusudia, pengine
watu wangeheshimu kile kitu na kuhakikisha
wanatunza kwa namna yoyote ile.
SAMSONI.
59
ujauzito yule mama hakunywa divai wala kileo
chochote ili kulinda maono ya Mungu ndani ya mtoto.
60
jambo lile lile asijue maamuzi hayo yatamgharimu yeye
mwenyewe, familia yake na taifa zima. Unaweza
ukapiga hesabu ya gharama aliyoingia Mungu mpaka
kuhakikisha anapatikana mtu kama Samsoni halafu
baadae anaishia alipoishia. Umewahi kufikiri jambo
hili?
61
Baada ya Samsoni kueleza asili ya nguvu zake
Biblia inasema Delila alimuweka katika mapaja yake
mpaka Samsoni akalala usingizi, kisha akawaita
Wafilisti wakamnyoa nywele zake, “Kisha akasema,
Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika
usingizi wake, akasema, Nitakwenda nje kama
siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya
kuwa BWANA amemwacha. Wafilisti
wakamkamata, wakamng’oa macho;
wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga
kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga
ngano katika gereza.” Waamuzi 16:20-21
62
kufisha maono ndani yako, anatumia njaa ya muda
mfupi kukupofusha macho usiweze kabisa kuona na
kufikia kesho njema aliyoikusudia Mungu kwenye
maisha yako.
63
kila hatua yako ya maamuzi ili uweze kutimiza kila
ndoto njema iliyo ndani yako.
64
kumweleza ujio wao, wakiambatanisha na ahadi ya
Mfalme wao ambayo ilikuwa ni “kumfanyizia heshima
nyingi na kila atakaloliomba kwake atapewa”. Balaamu
akawaambia watu wale akasema, “Kaeni hapa usiku
huu, nami nitawaletea jawabu kama BWANA
atakavyoniambia;” Hesabu 22:8, hii mbinu
ilimuondoa katika mtego mkubwa sana wa Mfalme wa
Moabu. Tunafahamu kwamba baadae alienda lakini
angalia kila hatua yake, ilikuwa kila hatua anaenda ili
asikie Bwana atakalomwambia na msimamo wake
ulikuwa kwamba; SIWEZI KUPITA MPAKA WA
NENO LA BWANA MUNGU WANGU,
KULIPUNGUZA au KULIONGEZA.
65
uthamani. Kama Eva angejua kwamba Shetani
alikuwa anawinda kesho yao na yetu inawezekana
asingeruhusu kabisa kumpa nafasi ya kumsikiliza au
hata kuzungumza naye. Ukijua ulichonacho kwamba ni
cha thamani na Shetani hataki kifanikiwe basi
utatumia kila njia kujilinda ili usiharibu kabla ya
wakati.
66
Unapokuwa katikati ya jaribu au changamoto
inayokuhitaji kufanya maamuzi fulani, chunga
sana aina ya maamuzi unayofanya.
Ningekuwa Samsoni.
67
BWANA, akasema, Ee Bwana MUNGU,
unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu,
nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate
kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya
macho yangu mawili” Waamuzi 16:28
68
Sura ya Sita
TENGENEZA MFUMO
WAKO WA MAOMBI
T
unapozungumzia mfumo wa maombi,
hatuzungumzii tu habari za kuomba, bali kuwa
na utaratibu maalumu na unaoeleweka wa
kuomba. Mfumo huu wa maombi ndio ngazi ya
kupandia juu, kuvuka vikwazo na dhoruba zinazoweza
kutokea katika maisha yako. Usiombe tu kwa sababu
unahitaji kitu fulani toka kwa Mungu, bali omba kwa
sababu ndio mfumo wako wa maisha ya kila siku.
69
kosa aweze kufukuzwa kazi. Walipokosa sababu ya
kumshitaki wakagundua ni mtu wa maombi sana,
ndipo walipokuja na hoja ya kutunga sheria
itakayoenda kinyume na mfumo wake wa maombi.
70
mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa
akifanya tokea hapo.” Danieli 6:10. Nataka
uyaangalie kwa umakini tena maneno haya ya mwisho,
anayosema “Akapiga magoni mara tatu kila siku,
akasali, akashukuru mbele za Mungu wake kama
alivyokuwa akifanya tokea hapo.”
71
atakayeomba kwa Jina la Mungu huyu
tunayemuabudu katika Kristo Yesu, bado utakuwa na
msimamo ule ule wa kuwa na maombi binafsi kwa
Mungu wako na kutokukubali hadhi na heshima ya
Mungu kushindanishwa na wanadamu?
72
wangu watu watetemeke na kuogopa mbele za
Mungu wa Danieli; maana yeye ndiye Mungu aliye
hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme
usioharibika, na mamlaka yake itadumu hata
mwisho. Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara
na maajabu mbinguni na duniani, ndiye
aliyemponya Danieli na nguvu za simba.” Danieli
6:26-27
73
Sura ya Saba
WATU WAKUU
HUANDALIWA SIRINI
V
itu vizuri na vikubwa huandaliwa sirini, watoto
hutungwa na kuzaliwa sirini, upasuaji na
kuokoa maisha hufanyika sirini, Yakobo
alifanyika kuwa Israeli alipokuwa sirini na Mungu.
Ukitaka kukwepa mahali pa sirini umetaka kuwa mtu
asiye na matokeo katika kizazi chako.
74
watu wengi sana wenye vitu vikubwa ndani yao. Musa
alikuwa na kitu sahihi cha Mungu lakini wakati
haukuwa sahihi kwa yeye kuanza kujionesha kwa watu
na kutaka kuwaokoa Israeli. Unapotaka kuchomoka na
kitu katika wakati ambao si wa Mungu, uwe na
uhakika utakiharibu na utashindwa kufika mwisho
mzuri kwa sababu ulikosa muda mzuri wa kuandaliwa.
75
Miaka arobaini sio miaka aliyopoteza, kwa kawaida
unaweza ukaona Musa alisoma vizuri shule ya
darasani alipokuwa akilelewa na Farao kwa hiyo
kusingekuwa na haja ya yeye kupelekwa tena jangwani
miaka 40, kwanza msomi kwenda kuchunga kondoo
lazima watu waliona anapoteza muda, lakini Mungu
alikuwa anajua ni maandalizi ya namna gani ambayo
Musa aliyahitaji kwa kipindi chote hicho.
76
kumsikiliza Mungu na kufuata sauti na maelekezo ya
Mungu. Kuna wakati Mungu alikuwa akimuita Musa
mlimani, anawaacha watu wote kisha anapanda na
Yoshua peke yao kwenda mlimani kwa Mungu, hii
ilikuwa ni ili kumuandaa kuwa kiongozi wa taifa la
Israeli baadae. Angalia “BWANA akamwambia
Musa, Njoo huku juu kwangu mlimani, uwe huku;
nami nitakupa mbao za mawe na ile sheria na
hiyo amri niliyoiandika ili uwafundishe. Musa
akaondoka na Yoshua, mtumishi wake, Musa
akapanda mlimani kwa Mungu. Akawaambia
hao wazee, Tungojeeni hapa, mpaka
tutakaporudi kwenu; na tazameni, Haruni na
Huri wapo pamoja nanyi; kila mtu aliye na neno
na awaendee.” Kutoka 24:12-14. Kwa nafasi
aliyokuwa nayo Musa, ungefikiri asingemuacha Haruni
kwa sababu ya nafasi yake na umuhimu wake, lakini
aliwaacha wote na kumchukua Yoshua mtumishi wake.
77
Unahitaji kutulia sirini ili utengenezwe, usikimbie
kimbie tu, kaa utulie mbele za Bwana ili Mungu apate
kuachilia maelekezo yote ya huduma na utumishi
alioweka ndani yako. Katika kipindi chote ambacho
Yoshua alikuwa chini ya Musa haumsikii akichomoka
na kitu chake mwenyewe licha ya kwamba alikuwa
mtu hodari sana wa vita, alisubiri wakati ulioamriwa
kwa ajili yake, na alipotoka alikuwa mtu mkuu sana.
78
Wana wa Israeli walipokosea, Yoshua alikuwa anaona
na hata hatua ambazo Musa alikuwa anazichukua
Yoshua pia alikuwa anaona. Aliandaliwa kwa kipindi
kirefu sana kabla ya kuitwa na kupewa jukumu la
kuwaongoza Israeli. Alijifunza mema na mabaya ya
wana wa Israeli, uzuri na changamoto za safari ile kwa
ukaribu sana.
79
Alikuwa ni mtu mzuri Biblia inasema alikuwa na
umbo la kupendeza, mwekundu na mwenye macho
mazuri. Zaidi ya yote Bwana alikuwa pamoja naye.
Tunasoma “Ndipo akajibu mmoja wa watumishi
wake akasema, Tazama, nimemwona mwana
mmoja wa Yese, Mbethelehemi, aliye stadi wa
kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa
vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye
BWANA yu pamoja naye” 1 Samweli 16:18
80
kanisa ndio kuna hatari zaidi kwa sababu watu
hukurupuka hata kabla hawajaiva kuwa vile Mungu
aliwataka wawe. Kubali kuandaliwa ili utumike katika
kiwango ambacho Mungu alikukusudia.
Yothamu.
81
wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na
vita, na kurudi Misri; lakini Mungu
akawazungusha hao watu kwa njia ya bara
kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli
wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa
silaha.” Kutoka 13:17-18
Paulo.
82
ukijua ni Shetani amesababisha upungukiwe kumbe ni
Mungu na lengo lake sio baya ni zuri kabisa,
anaruhusu upitie kipindi cha njaa na kukosa mahitaji
muhimu ili tu kukuimarisha.
Eliya Mtishbi.
83
sana. Hatuambiwi baba yake nani, wala mama yake ni
nani, Wala amelelewa katika mji upi; hakuna mahali
wanasema habari hizi lakini tayari ni mtumishi na
nabii wa Mungu aliye hai.
84
bila kupitia mafunzo ya kijeshi. Usiogope kukaa mahali
pa siri. Kuna wakati unataka kusema kilicho ndani
yako na hakuna mtu anataka kusikia hata sauti yako,
usipate shida, wakati unakuja ambapo kila mtu
atatamani kuisikia sauti yako. Unataka kuimba lakini
ni kama watu hawana muda na wewe, una kitu ndani
yako unatamani watu wangekiona ila ni kama vile
haupo maana kila mtu anaendelea na shughuli zake.
Tulia wakati huu wa kuandaliwa, siku zinakuja na
sasa zipo karibu ambapo watu watataka sana
ulichonacho maana kimeandaliwa kwa ajili ya wakati
kama huo.
85
Sura ya Nane
JIBORESHE
I
li uweze kufikia malengo yako ya kuwa mtu fulani
au kufikia hatua fulani kihuduma, kielimu au
kibiashara unahitaji kujiboresha kila siku kusudi
uweze kufikia kiwango unachokusudia kufika.
86
unajua kwamba huwezi kutoa kitu usichonacho, kama
alitaka niandike kitu kila siku basi alitaka kila siku
nisome kitu kipya ili nipate kitu cha kuandika kila
siku.
87
walimu, jinsi alivyokuwa akifundisha. Mafundisho
yake, na namna alivyokuwa anafundisha nilikuwa
nikihisi nguvu za Mungu zikitembea ndani yangu,
wakati anaelekea mwisho wa kozi ile tulimuuliza
anatumia jina gani kwenye mitandao ya kijamii ili
tuweze kumfuatilia huko. Tulishangazwa sana na
majibu yake, alituambia hana mtandao wowote
anaotumia zaidi ya whatsapp, tulipoendelea kumuuliza
zaidi alitueleza kwamba hana muda wa kuwa huko
kwa sababu muda mwingi kama sio wote anautumia
kusoma neno, kuomba, kujifunza mambo mbalimbali
kupitia vitabu na kufanya kazi yake ya Uchungaji kwa
bidii zote. Akaongeza kusema; tunachokiona akiwa
anafundisha wala sio upako, ni vile amesoma na
kusoma na kusoma kuhusu kitu alichokuwa
anatufundisha kiasi ambacho kimemfanya amekuwa
bora.
88
mtu stadi wa kupiga kinubi ili ile roho mbaya
itakapoanza kumsumbua, basi kipigwe kinubi vizuri na
ile roho mbaya itamwacha. Alitafutwa Daudi mwana
wa Yese, angalia maneno haya “Ndipo akajibu
mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama,
nimemwona mwana mmoja wa Yese,
Mbethelehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena
ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa
busara, mtu mzuri, ambaye BWANA yu pamoja
naye” 1 Samweli 16:18
89
Alipotumwa achunge kondoo za baba yake,
alitumia muda huo kujinoa na kujiboresha kupiga
kinubi mpaka akawa stadi wa kupiga kinubi. Mfalme
Sauli alipotafuta mpiga kinubi stadi, hakuonekana
mwingine isipokuwa Daudi mwana wa Yese. Muda
aliokuwa machungani, hakuwa anajilaumu kwamba
familia imemuacha au ameonewa, hakuwa analaumu
kwamba hajapelekwa shule kama ndugu zake, alitumia
muda huo kama fursa kujiandaa na kujiboresha mpaka
akafikia kiwango cha ushujaa; walipotokea Simba na
Dubu kutaka kuwararua wanyama wake aligeuka na
kupambana nao hata akawashinda. Alipoenda
kuwatembelea kaka zake walipokuwa vitani na kukuta
Goliathi yule Mfilisti akiyatukana majeshi ya Bwana,
alijitosa katika vita ile na akamshinda Goliathi kwa
Jina la Bwana (1 Samweli 17:31-51)
90
kuwadhihirishia kwamba unaweza na wala wewe sio
bahati mbaya.
91
Sura ya Tisa
UPINZANI NI SEHEMU
YA MAISHA
UNAPOINGIA HATUA
NYINGINE
F
ahamu jambo hili kwamba; upinzani ni sehemu
ya maisha unapoingia hatua nyingine, inaweza
kuwa katika huduma, elimu, kazi, biashara au
katika ndoa. Barbara Wentroble katika kitabu chake
cha God’s Purpose for your life ameandika hivi; “New
level new devil” akiwa na maana kwamba kila
unapopiga hatua kutoka ulipo kuelekea hatua ya juu
zaidi ya hapo, kuna upinzani utakutana nao ambao
haujawahi kukutana nao au haukuwepo kabisa. Hatua
yoyote ile ina kawaida ya kuja na vikwazo, upinzani na
kila aina ya vizuizi. Mfano mtoto anapotaka kuzaliwa,
licha ya furaha iliyo kubwa kwa mama mzazi, lakini
kuna maumivu mengi anayapitia, uchungu na machozi
kabla ya furaha. Vivyo hivyo mtoto anapoendelea
kukua, anapotoka hatua moja kwenda nyingine pia
huwa sio rahisi kwake, hatua hizo huambatana na
92
maumivu na homa za hapa na pale. Hii ni asili na
kawaida kwa mwanadamu.
93
Walipoendelea kuhubiri huku mafundisho yao
yakibadili maisha ya watu kwa kasi ya ajabu,
Masadukayo wakawatokea na kuwakamata kisha
wakawaweka gerezani hata asubuhi, baadae
wakawauliza, Kwa nguvu gani na kwa jina la nani
ninyi mmefanya haya? Matendo ya Mitume 3:6-7, 4:3-7.
Maswali ya jinsi hii hayakuwepo Petro alipokuwa
mvuvi wa samaki, yalisubiri atokee katika udhihirisho
kamili wa kile ambacho Mungu amemtuma kwacho
duniani.
94
Ukiwa mtu wa kawaida na katika hatua uliyopo ya
kawaida, hautaona maswali, kuhojiwa au hata
kufuatiliwa na watu, lakini pale utakapochukua hatua
ya kusogea kiwango kingine cha utukufu na kutumia
vipawa na karama zilizo ndani yako vyema, utakutana
na upinzani mkubwa kutoka kwa watu wako wa
karibu, rafiki zako, watu wanaofanya kitu kama cha
kwako, wale uliowaamini wangekuwa mstari wa mbele
kukushika mkono na hata kwa watu usiowajua. Hii ni
kwa sababu mioyo ya watu walio wengi haiko tayari
kupokea mabadiliko na kuruhusu wengine waende juu
zaidi ya pale walipokuwa.
95
Sura ya Kumi
E
sau na Yakobo walipokuwa tumboni mwa
mama yao, Mungu alikuwa amewaweka kama
mataifa mawili makubwa, lakini matokeo yake
tunaona Yakobo peke yake anafikia hatua ya kuwa
taifa huku Esau akishindwa kabisa kufikia ndoto hiyo
(Mwanzo 25:23) Kuishi chini ya kiwango au uwezo
uliozaliwa nao kumewafanya watu wengi sana kuishi
nje ya kusudi la Mungu kwenye maisha yao; badala ya
kuwa vile Mungu alivyokusudia toka mwanzo
unajikuta unaishi kama mtu wa kawaida na asiye na
kitu ndani yake.
96
haukugundulika wala kutumika ipasavyo na
ukasababisha hasara kubwa sana kwa taifa la Israeli.
97
Usifukie talanta na kipawa ambacho Mungu
ameweka kwenye maisha yako kama yule mtumwa
aliyepokea talanta moja akaenda akaichimbia chini
akaificha. Si wingi wa talanta unaoweza kukufanya
uzalishe zaidi, bali uwezo wa kujua kwamba
ulichopewa si kwa ajili yako, hivyo kama utatumia
akili na kwa uaminifu kuzalisha kwa kadiri ya neema
ya Mungu na kusudi lake kwako, utapata matokeo
makubwa. Siku ile hatutatoa hesabu kuangalia wingi
au uchache wa matokeo bali kwa kadiri ya makusudi
ya Mungu na kile alichoweka kwako. Ukipewa vingi
kwako vitatakwa na zaidi.
98
yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha,
alifufuka, akasimama kwa miguu yake” 2
Wafalme 13:20-21.
99
hayo, wako watu wengi sana wanayasubiri; usilale na
mawazo ya miradi mikubwa ndani yako; Chochote
ambacho Mungu ameweka ndani yako si kwa ajili yako
bali ni kwa ajili ya watu, tumia kwa kadiri ya nguvu
unazojaliwa.
100
Sura ya Kumi na Moja
USIOGOPE CHUKUA
HATUA
H
ili ndilo jambo ninaloweza kukuambia kijana
na mpendwa wangu. Kubali kuchukua hatua
kuelekea kutimiza ndoto na maono katika
maisha yako. Usisubiri mpaka ufunuliwe kila kitu ili
kujua kama upo tayari kuanza kuchukua hatua au la,
wakati mwingine Mungu huachilia picha ya alichoweka
ndani yako kidogo kidogo, na kwa kadiri ambavyo
utaendelea kuchukua hatua ndivyo ambavyo
ataendelea kuachilia zaidi. Hatua ndogo ndogo nyingi
huzaa kitu kikubwa, hatua ndogo ndogo zilizojaa Imani
na uvumilivu huzaa matokeo makubwa sana siku za
usoni. Usiogope kuchukua hatua.
101
asijue aendako.” Waebrania 11:8. Neno hili
linatuonesha Ibrahimu alipoitwa na Mungu atoke
katika nyumba ya baba yake alitii ile sauti na
akachukua hatua asijue aendako. Hatua ya kwanza ina
nguvu sana kuamua kesho yako.
102
Biblia inatahadharisha juu ya watu waoga kwa
namna ya ajabu sana. Angalia katika kitabu cha
Ufunuo 21:8 anasema “Bali waoga na wasioamini,
na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na
wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo
wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo
moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” Swali
langu, kwanini waoga waende katika ziwa la moto? Hili
jambo limenipa kutafakari sana kwamba kumbe
Mungu anatazama uwoga kama dhambi. Mtu mwoga
anafananishwa na mzinzi, mwasherati, mwabudu
sanamu na mchawi. Tafsiri isiyo rasmi ya woga ni hali
ya kusitasita kuthubutu kufanya mambo fulani kwa
kuangalia mazingira yanayokuzunguka na kuwa na
mashaka juu ya matokeo yatakayotokea.
103
amekupa kufanya kwa kigezo cha kuogopa watu,
Mungu hapendi, kwake hilo jambo analifananisha na
kutoamini.
Wakoma wanne.
104
mjini, mjini mna njaa, nasi tutakufa humo; nasi
tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya! Twende
tukaliendee jeshi la Washami; wakituua,
tutakufa tu. Basi wakaondoka kabla ya
mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha
Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha
Washami, kumbe! Hapana mtu.” Ukiangalia
mazingira waliyokuwa nayo hawa Wakoma wanne
utaona ni halali kwao kama wasingechukua hatua.
Kwanza sheria ilikuwa haiwaruhusu kuingia mjini, pili
walikuwa ni wakoma wasingeweza kuliendea jeshi
wakabaki salama. Walipoangalia mazingira yao
wakaona wakibaki bila kuchukua hatua watakufa kwa
njaa, hata wakitoka kuingia mjini huko nako kuna njaa
watakufa vilevile kwa njaa au kwa kupigwa mawe,
sehemu pekee iliyokuwa imebaki yenye chakula ni
katika jeshi la Washami. Walishauriana wakachukua
hatua kulielekea jeshi la Washami, walipoanza tu
kuchukua hatua, ndipo Bwana akawasikizisha
Washami kishindo cha miendo ya magari na farasi,
kishindo kikubwa mno. Wale Washami wakakimbia,
wakaacha kila kitu kambini. Wakoma wakachukua
nyara za kuwatosha katika hema ya kwanza na ya pili
wakazificha kwa ajili yao kisha wakaenda kuwaambia
mabawabu wa mji na baadae nchi nzima ilipata
chakula.
105
unajiuliza utawezaje lakini kwa sababu umechukua
hatua Mungu amekufanikisha kwa namna ambayo
haukutegemea. Kwenye kuchukua hatua kuna mwanzo
mpya, kwenye kuchukua hatua kuna mafanikio,
kwenye kuchukua hatua iko nguvu ya Mungu
inayovunja nguvu za upinzani mwanzoni mwa jambo.
Kuna watu hata ungeomba vipi hautawaona mpaka
umeanza kuchukua hatua, watajitokeza kukushika
mkono kwa namna ambayo haukuwaza. Kila kitu
ukiangalia unaona ni Mungu amekusaidia. Usiogope.
chukua hatua leo.
106
IKIWA HAUJAOKOKA NA UNATAKA KUMPA
YESU MAISHA YAKO
S
ema maneno haya kwa imani; “Asante Bwana
Yesu kwa kazi ya msalaba uliyofanya kwa ajili
yangu, ninaomba uniokoe, ninakiri dhambi
zangu na makosa yangu yote mbele zako, ninakupokea
wewe ili unisafishe kwa damu yako, ninaitambua
nguvu ya Neema, ambayo kwa hiyo ninapata wokovu
na si kwa matendo yangu. Biblia inasema “kwa moyo
mtu huamini hata kupata haki na kwa kinywa hukiri
hata kupata wokovu” (Warumi 10:10) Nami naamini
kwa moyo wangu wote kwamba wewe ni mwana wa
Mungu na ninakiri kwamba ulikufa msalabani kwa
ajili yangu ili niokolewe. Futa dhambi zangu zote na
unisafishe kwa damu yako. Ninakukaribisha ndani ya
moyo wangu uwe Bwana na Mwokozi wa Maisha
yangu, Amen”
107
Mungu akubariki sana.
Mawasiliano;
emwakalinga@myfaithlife.co.tz
©2022
MAREJELEO.
108
• Nguzo ya Siku by Apostle Shemeji Melayeki
• The world is waiting for You by Gospel Orji
• Disciplines of Godly Man by R. Kent Hudhes
• Disciplines of Godly Young Man by R. Kent
Hughes
• Finding Your Ministry – A study of the fruit and
gifts of the Spirit by Raymond W. Hurn
• God's Purpose for Your Life – Becoming one of
God's Called, Chosen and Faithful Followers by
Barbara Wentroble
109