Professional Documents
Culture Documents
Matangazo ni swala muhimu kwa kila biashara. Tatizo linatokea pale ambapo
biashara inashindwa kumudu gharama za matangazo, hasa matangazo ya
gharama kubwa.
Fuatilia makala hii kwa karibu ili nikufahamishe njia 9 unazoweza kuzitumia
kutangaza biashara yako bure au kwa gharama nafuu sana.
1. Tumia tovuti
Tovuti au blog ni njia rahisi na ya gharama nafuu ya kujitangaza. Ikiwa una
blog au tovuti ambayo inaidadi nzuri ya watembeleaji, unaweza kuweka
tangazo la biashara yako hapo na likaonekana kwa watu wengi zaidi.
Kumbuka hivi leo karibu kila mtu anatumia mitandao ya kijamii. Hivyo
kutangaza biashara yako kupitia kurasa au akaunti zako za mitandao hii ni
rahisi na utawafikia watu wengi zaidi.
3. Tengeneza vifungashio au zawadi ndogo
Siyo lazima uwe na pesa nyingi ndipo utoe zawadi au huduma ya vifungashio
vyenye chapa yako. Unaweza kubuni na kuchapisha vifungashio vyenye jina
na maelezo mafupi kuhusu biashara yako ili kujitangaza.
Unaweza kutoa zawadi ndogo kama vile kalamu au shajara (diary) vyenye
maelezo ya biashara yako.
Naamini njia hii ni nafuu sana kuliko kuweka tangazo kwenye televisheni
wakati wa habari.
8. Endesha shindano
Nani asiyependa kushinda? Naamini hata wewe unapenda kushinda zawadi
fulani.
Kwa njia hii utafahamika na kuwafikia watu wengi zaidi na hivyo kuitangaza
biashara au huduma yako kwa urahisi na kwa gharama nafuu kabisa.
Hitimisho
Naamini hutoumiza tena kichwa kufikiri njia za kupata pesa nyingi kwa ajili ya
matangazo ya gharama kubwa.
SOMO: 2
1. Lugha nzuri
Katika mambo yanayowapotezea wafanyabiashara wengi wateja ni lugha
mbaya kwa wateja. Hakuna mteja anayependa kupokelewa au kujibiwa
vibaya.
Ili kuwavutia wateja unaweza kutoa huduma au vitu vya bure kama vile
kalamu, mifuko, shajara (diary) au hata maji ya kunywa. Kwa njia hii
utawavutia wateja wengi zaidi.
3. Punguzo
Punguzo ni njia bora sana ya kukabiliana na ushindani wa kibiashara na
kupata wateja. Ikiwa mwenzako anauza sabuni kwa shilingi 2,100, wewe uza
2,050. Unaweza usipate faida kubwa kwenye bidhaa moja lakini utapata faida
kubwa kwenye mauzo ya jumla.
Kwa mfano ikiwa faida kwenye sabuni hapo juu ni sh. 100, muuzaji wa
kwanza akauza sabuni 5 kwa sh. 2,100 atapata faida ya sh. 500.
Lakini wewe ukauza sabuni 20 kwa sh. 2,050 utapata faida ya sh. 1,000. Je
huoni kuwa umeuza na kupata faida zaidi kutokana na kuvutia wateja wengi
kupitia punguzo? Weka punguzo sasa.
4. Shindano
Siyo lazima uwe na pesa nyingi ndipo uweze kuendesha shindano. Unaweza
kuendesha shindano lenye zawadi ndogo kama vile vocha, kalamu, mikoba,
shajara au hata vinywaji.
Ukweli ni kuwa blog au tovuti ni muhimu sana kwa ajili ya kuongeza wateja
kwa njia ya kutangaza biashara yako.
7. Matangazo
“Biashara ni matangazo.”
Biashara nyingi hupuuza nafasi ya kujitangaza ili kuongeza wateja na hatimae
kupata faida zaidi. Siyo lazima utumie njia za gharama kubwa kujitangaza
kwani zipo njia nyingi sana.
8. Toa misaada
Je umeshawahi kujiuliza kwanini biashara na kampuni nyingi hutoa misaada
mbalimbali? Je ni kwa kuwa wana pesa za ziada au wanawapenda sana wale
wanaowasaidia?
Ni wazi kuwa hii ni mbinu nzuri sana ya kujitangaza na wala si vinginevyo.
Kwa njia ya kutoa misaada wateja huongezeka zaidi kwani watu huifaahamu
biashara husika, pia huichukulia kama biashara inayowajali zaidi.
9. Lenga changamoto
Watu wananunua bidhaa au huduma fulani ili itatue changamoto zao. Hivyo
kuendesha biashara isiyolenga changamoto za wateja haitapata soko.
Hebu fikiri mtu anaanzisha duka la kuuza dawa za Ebola Kenya au Tanzania,
je atapata wateja kweli? Ni wazi kuwa hatapata wateja kwani tatizo la Ebola
kwa Tanzania na Kenya ni dogo sana.
Hitimisho
Naamini sasa umeona jinsi unavyopoteza wateja na faida bila sababu yoyote
ya msingi. Fanyia kazi mbinu jadiliwa hapo juu nawe kwa hakika utaweza
kuongeza wateja na hatimaye kupata faida zaidi. Je wewe unatumia mbinu
gani kupata wateja?
SOMO: 3
Jinsi ya Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo
Usiogope; kuwa na mtaji mdogo au kutokuwa nao kabisa sio mwisho wako wa
kutimiza malengo yako.
Reginald Mengi
Zipo mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukuwezesha kufanya biashara
hata kama utakuwa na mtaji mdogo. Tafadhali fuatilia hoja jadiliwa hapo chini
kwa ufafanuzi zaidi.
1. Kuwa mbunifu
Moja kati ya mambo ambayo yatakusaidia sana kwenye kuanza biashara kwa
mtaji mdogo ni ubunifu. Kwa njia ya ubunifu utaweza kushinda biashara na
bidhaa zilizoko sokoni kwa urahisi zaidi. Unaweza kufanya haya yafuatayo:
2. Anza na unachokijua
Unapokuwa na mtaji mdogo huhitaji kuhusisha mambo mengi mageni au
yanayotegemea sana watu wengine kwa kuwa huna pesa za kuyagaramia.
Kwa mfano kama unaanzisha biashara ya ushonaji basi anza kutengeneza
mavazi yale unayoyaweza kwa kutumia vifaa ulivyonavyo; kwa njia hii
utajenga mtaji wako kisha baadaye utaweza kuajiri wengine watakao
kuwezesha kutengeneza aina nyingine zaidi.
Unapofanya kile unachokijua gharama huwa haziwi kubwa sana kwani ni kitu
unachokimudu mwenyewe.
Kuwa na matumizi mazuri ya fedha hasa kwa mambo ya msingi tu. Watu
wengi wameshindwa kwenye biashara kwa sababu wameanza biashara kwa
mbwembwe za matumizi badala ya huduma bora zenye ubunifu.
Tumia muda vizuri, pia hakikisha unatoa huduma yenye ubora wa hali ya juu
kwa bei ambayo wateja wataweza kuimudu. Jitese kwa muda mfupi kwa
kipindi cha kuweka msingi wa biashara yako kwani hata kipindi cha kupanda
katika kilimo huwa ni cha taabu.
Tumia fursa kama vile mitandao ya kijamii ili kujitangaza. Pia unaweza
kutumia udhaifu uliopo katika biashara nyingine za watangulizi wako kama
fursa kwani unaweza ukarekebisha udhaifu huo kupitia biashara yako.
7. Jali wateja
Kujali wateja katika biashara ni jambo muhimu sana kama unataka kuona
matokeo chanya. Siku zote ninapenda kusema “wateja hufugwa”. Wateja
hufugwaje? Hufugwa kwa huduma nzuri.
Waheshimu wateja wako pia hakikisha unatimiza na kumaliza haja zao katika
ubora wa hali ya juu. Kumbuka siku zote mteja huja kwanza kabla ya pesa;
hivyo usitangulize pesa kabla ya huduma nzuri kwa mteja.
Ukilifanyia kazi hili utaweza kukuza biashara na mtaji wako kwa muda mfupi.
Hitimisho
Thubutu, nza, fanya bidii, weka nidhamu, mtangulize Mungu na hakika utaona
mafanikio chanya katika biashara yako.
Kuanza biashara kutoka kiwango cha sifuri siyo kazi rahisi. Kama mjasiriamali
utakutana na changamoto nyingi. Hili haliwezi kuwa tatizo ikiwa uko tayari
kujifunza kutokana na makosa na kufahamu njia za kuyaepuka huko mbeleni.
Hivi ndivyo wajasiriamali wengi wanavyojifunza na kukua. Unapokuwa
kwenye biashara ni lazima ufahamu makosa ambayo yanaweza kuathiri
biashara au uwekezaji wako; ili ujitahidi kuyaepuka ama kuyapunguza kadri
iwezekanavyo. Ni dhahiri kuwa wajasiriamali wengi wamekwama kutokana na
kupuuzia au kutofahamu makosa haya 15 ambayo hata wewe unatakiwa
kuyafahamu na kuyaepuka.
Kwa mfano kama kuna tatizo la upatikanaji wa mboga katika mji au eneo
unalokaa, ikiwa wewe utaleta mboga katika eneo hilo ni wazi kuwa watu
watakupa pesa ili uwape mboga. Hivyo ni muhimu kila mara ukatafuta
changamoto ukaitatua, nawe bila shaka utapata pesa za uhakika.
2. Kuwa na maono
Hakuna ujasiriamali bila maono. Kuwa mjasiriamali bila maono ni sawa na
kuendesha gari isiyokuwa na usukani. Maono katika ujasiriamali
yatakuwezesha kukuongoza ufanye nini na kwa muda gani. Ni lazima ujiulize
kuwa unataka kuwa nani, lini na unataka kufanya nini baadaye? Jonathan
Swift alisema maono ni sanaa ya kuona kile ambacho wengine hawaoni. Ni
lazima uwe na lengo na ufanye bidii kulifikia.
“Wajasiriamali waliofanikiwa ni wale walioweza kubadili maono
yao kuwa uhalisia”
Kila mara kumbuka kuwa ushindani ni mkubwa, hivyo jitahidi kuongeza tija na
ubora wa huduma na bidhaa zako.
Naamini kwa kufanya hivi utaweza kujijengea msingi mzuri wa wateja kwa ajili
ya huduma au bidhaa zako kila siku.
Kuna watu, mipango, vitu au hata tabia ambazo zinaweza kukuathiri vibaya
sana kwenye ujasiriamali wako. Hivyo kusema hapana kutakuepusha kwa
kiasi kikubwa na mambo haya.
9. Fahamu soko
Kanuni mojawapo ya kuongeza mauzo yako kama mjasiriamali ni kulifahamu
soko vyema. Hakikisha huduma au bidhaa unayoitoa inakidhi mahitaji na
inafika kwenye soko stahiki.
Kwa mfano ikiwa wewe ni mzalishaji wa mayai, lakini eneo ulilopo soko ni
duni, basi tafuta eneo jingine ambalo soko la bidhaa hii ni nzuri. Ikiwa wewe
huwezi kwenda, unaweza kutafuta mtu kwenye eneo lenye soko zuri
akakuuzia bidhaa yako na ukampa gawio fulani.
Kwa kufanya hivi utaweza kulenga soko na kujiongezea faida zaidi wewe
kama mjasiriamali.
Kwa mfano ikiwa kuna wateja walipata shida kupata huduma au bidhaa yako,
maliza kwanza swala hili kabla ya kuendelea kuweka jitihada za kuuza bidhaa
mpya. Kwa kufanya hivi utaweza kufanya mambo kutokana na umuhimu
wake, jambo ambalo litakuwezesha kukua.
SOMO: 6
Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kuchagua Jina la Biashara
Uteuzi wa jina la biashara ni hatua muhimu kama ilivyo kwa jiwe la pembeni
katika nyumba. Watu wengi wamekuwa hawatilii maanani mambo muhimu ya
kuzingatia wakati wa kuchagua jina la biashara au kampuni.
Hivyo basi tumia huduma kama vile (Whois) kutazama kama unaweza kupata
anwani ya matandao inayoendana na jina la kampuni au laa.
Kumbuka haina maana kampuni kuitwa Moja LTD halafu ikawa na tovuti
inayoitwa “http://mbili.com”; hapa utapoteza watu, hawataweza kuifikia tovuti
yako vyema.
4. Upekee
Kama nilivyoeleza katika hoja zilizopita hapo juu ni muhimu kuhakikisha
unabuni jina lenye upekee kwa ajili ya biashara yako. Epuka kutumia majina
yanayofanana na majina mengine.
Hivyo ni muhimu kuzingatia kuwa jina unalolichagua leo litakufaa pia kwa
upanuzi na matumizi ya baadaye ya biashara yako.
Hitimisho
SOMO: 7
Fahamu Njia 8 Unazoweza Kuzitumia ili Kupata Mtaji
Nifanyeje nipate mtaji? Nina wazo zuri lakini sina mtaji? Haya ni maswali
ambayo nimekuwa nikiulizwa sana na wasomaji wa Fahamuhili.com, pamoja
na watu wengi ninaokutana nao kwenye maisha ya kila siku.
Ingawa mtaji siyo kigezo pekee cha kufanikiwa kwenye biashara au mradi
unaoufanya, mtaji unabaki kuwa kiungo muhimu sana katika kutekeleza wazo
fulani au mradi kwa ufanisi. Kwa kuwa watu wengi huanzisha miradi au
biashara kwa lengo la kupata pesa, huwa vigumu sana kuwa na pesa za
kutosha kuanza utekelezaji wa wazo hilo.
1. Akiba binafsi
“Mtu anayeweka akiba, ni mtu anayewaza kuhusu kesho.”
Mara kadhaa nimekuwa nikieleza kuwa kuweka akiba kuna manufaa
kemkem, ikiwemo kupata uwezo wa kuwahi fursa mbalimbali na kuzifanyia
kazi kwa wakati.
Hivyo basi, unaweza kutunza kiasi fulani cha pesa katika kipato chako
hatakama ni kidogo, ili uweze kupata mtaji wa kuanzisha biashara au mradi
wako.
Kumbuka! Usitake kuanza biashara na mtaji mkubwa sana kwani kuna hatari
ya kuupoteza, jega mtaji wako kidogokidogo; unaweza kuanza na mtaji wa
shilingi 10,000 lakini baadaye ukakua na kuwa mamilioni ya pesa.
Unaweza kuuza vitu vyote ambavyo ukivikosa hutokufa ili uweze kupata mtaji;
kumbuka uwekezaji ni muhimu kuliko maisha ya kifahari na anasa.
Small Starter
Africa Connekt
Iesc
Fuatilia vyombo mbalimbali vya habari pia jiunge na vikundi vya wajasiriamali
wengine ili zitokeapo fursa za mitaji uweze kuzifahamu na kuzitumia.
5. Mikopo ya taasisi za kifedha
Hivi leo ziko taasisi kedekede zinazotoa mikopo kwa ajili ya watu mbalibali;
hivyo, mikopo kutoka kwenye taasisi za kifedha inaweza kutumiwa kama mtaji
mzuri sana wa biashara.
Hakikisha kama unataka kutumia njia hii kupata mtaji wa biashara au mradi
wako, umejipanga vyema na unafahamu wazi njia na mbinu utakazozitumia
kurejesha mkopo wa taasisi husika hata kama mambo yatakwenda mrama.
6. Ubia au uwanahisa
Katika dunia yetu ya leo, wapo watu wengi wenye fedha lakini hawajapata
mahali pa kuwekeza fedha zao; wengi huwa na pesa nyingi lakini hawana
muda wa kuanzisha na kusimamia biashara au mradi.
Unaweza kutumia mbinu hii kupata mtaji, kwa njia ya kuingia ubia au
uanahisa na mtu au watu wengine wenye mitaji wanaotafuta mahali
pakuiwekeza.
7. Mali kauli
Najua umeshajiuliza ‘mali kauli’? Ndiyo, mali kauli ni njia nyingine bora kabisa
unayoweza kuitumia kupata mtaji wa biashara kwa kutegemea uaminifu wako.
Zipo biashara kubwa zenye mali nyingi lakini zina mzunguko mdogo katika
eneo husika; lakini inawezekana wewe unafahamu mahali ambapo mali hizo
zikiuzwa zitauzika vizuri. Unachopaswa kufanya ni kuchukua mali kwenye
biashara husika na kwenda kuziuza kisha unarejesha fedha ya mauzo ya
bidhaa husika na yule mwenye biashara atakupa gawio fulani kwa kazi hiyo.
Ikiwa utakuwa mwaminifu na kufanya kazi hii kwa bidii, ndani ya muda mfupi
utapata mtaji wa kuanzisha biashara yako mwenyewe ambayo imetokana na
kuuza mali za biashara nyingine kubwa kwa kuaminika tu (mali kauli).
8. Mashindano
Je, unajua kuna watu wametoka kimaisha kutokana na mitaji waliyoipata
kutokana na mashindano mbalimbali?
Hitimisho
Naamini hadi kufikia hapa umepata mwanga wa ni njia gani unaweza kuitumia
ili kupata mtaji kwa ajili ya kutekeleza wazo au mradi wako.
Napenda kukukumbusha kuwa mtaji siyo kila kitu na wala siyo kiasi cha pesa;
bali usimamizi na mikakati sahihi kwenye kile unachaokifanya vitakuwezesha
kukuza mtaji wako na kufikia malengo yako.
SOMO: 8
Kwa hakika ujasiriamali ni chaguo muhimu sana kwenye karne hii ya sasa ili
kujipatia kipato. Hivi leo kuna wajasiriamali wengi waliofanikiwa na wengine
hawajafanikiwa.
Kwa hakika wajasiriamali waliofanikiwa wanafahamu na wanaziishi sifa za
wajasiriamali bora. Ni wazi kuwa huwezi kuwa mjasiriamali bora wakati una
sifa za mwajiriwa.
1. Mwenye malengo
Malengo ni mwongozo wa kukuwezesha kufanikisha jambo lolote. Kuwa na
malengo ni sifa muhimu ambayo kila mjasiriamali anapaswa kuwa nayo. Je
umeamua kuwa mjasiriamali kwenye nini? Kwa ajili ya nini?
Malengo yatakuongoza ufanye nini, wapi lini na kwa ajili ya nini. Bila malengo
utafanya mambo bila mwongozo wowote na ni vigumu kufanikiwa.
2. Nidhamu
Nidhamu ni sifa muhimu kwa mjasiriamali kwani itamtenga na mambo mengi
yasiyokuwa na umuhimu. Ni lazima mjasiriamali awe na nidhamu ya maswala
kama vile matumizi ya muda pamoja na pesa.
3. Ujasiri na uthubutu
Ujasiri na uthubutu ni sifa muhimu sana kwa mjasirimali ili aweze kutekeleza
malengo yake. Ujasiriamali ni swala linalohitaji ujasiri na uthubutu wa
kuchukua maamuzi magumu hata kama kuna changamoto au hatari kadha
wa kadha.
5. Uvumilivu
Kila jambo lina changamoto zake. Ujasiriamali una changamoto nyingi
ambazo zinahitaji uvumilivu ili kuzimudu.
Hivyo basi, sifa ya kuwa na uvumilivu ni muhimu sana kwa kila mjasiriamali
anayetaka kufanikiwa. Haijalishi umepata hasara au unakutana na
changamoto nyingi kiasi gani, ni muhimu kuvumilia.
6. Bidii
“Mafanikio huja kwa wale ambao wanafanya bidii kubwa
kuyatafuta.”
7. Kupenda anachokifanya
“Fanya unachokipenda na pesa zitafuata.”
Marsha Sinetar
Watu waliofanikiwa sana duniani, wanafanya kile wanachokipenda.
Unapofanya kile unachokipenda ni rahisi kufanikiwa kwani utakifanya kwa
moyo, bidii pamoja na kutokata tamaa.
Kama uliwekeza pesa zako zikapotea, basi usiache ujasiriamali bali baini ni
nini kilisababisha ukapoteza pesa zako ili ukiepuke mbeleni.
Neno la mwisho
SOMO: 9
1. Weka bajeti
Ni rahisi kusikia watu wakilalamikia bajeti za serekali na kuzikosoa lakini wao
wenyewe hawana bajeti zao binafsi. Unawezaje kukosoa bajeti ya serekali
wakati ya kwako mwenyewe imekushinda? Fikiri tofauti; tambua umuhimu na
jinsi ya kujiwekea bajeti. Bajeti yako binafsi itakuwezesha kufahamu mapato
yako, mambo gani muhimu unayotakiwa kuyafanya na yatakugharimu kiasi
gani cha pesa. Kwa kufanya hivi utaweza kutafuta na kutumia pesa kulingana
na bajeti uliyojiwekea na kuokoa pesa ambazo zingepotea bila sababu.
2. Panga manunuzi kabla
Ni muhimu kupanga manunuzi yako kabla ya kwenda sokoni au dukani. Hili
litakuwezesha kubainisha nini unachotakiwa kununua na kwa gharama gani.
Unapokwenda sokoni au dukani bila kupanga manunuzi yako ni rahisi
ukanunua vitu ambavyo hukuvipanga. Unaweza kuorodhesha vitu katika
kipande kidogo cha karatasi pamoja na bei zake ili uwe ni mwongozo wako
katika manunuzi.
3. Weka vipaumbele
Kuna mahitaji mengi kwenye maisha ya mtu; lakini kuna yaliyo muhimu zaidi
kuliko mengine. Jifunze kubainisha mambo ya muhimu zaidi ili uanze
kuyatengea pesa kwanza. Kwa mfano maswala kama vile eilimu, uwekezaji,
kodi ya nyumba, chakula, ni baadhi tu ya mambo muhimu kuliko gari, pombe,
simu pamoja na mambo mengine ya anasa. Ukijifunza kuwa na mtazamo wa
kutambua vipaumbele utaweza kutenga na kutumia pesa kwenye mambo ya
muhimu kwanza.
Epuka tabia kama vile kuacha taa zikiwa zimewashwa hata wakati wa
mchana bila sababu. Punguza matumizi ya pasi, redio na hata televisheni. Pia
unaweza kununua taa zinazookoa umeme yaani energy servers.
Unaweza ukaokoa maji kwa kutumia maji ya mvua au toka chanzo kingine
badala ya kutumia maji ya bomba kwa kila kitu.
Punguza matumizi ya gesi kwa kuzima jiko pale lisipokuwa na uhitaji. Hakuna
haja ya kupasha maji moto kila wakati huku unaweza kuogea maji ya baridi au
uvuguvugu.
Epuka kupiga simu zisizokuwa na ulazima kwani kwa kufanya hivi unapoteza
pesa bila sababu. Jiunge kwenye vifurushi (bundles) vya muda mrefu kuliko
vya siku moja ili uweze kupata muda wa kutosha kutumia vyema muda wako
wa maongezi.
6. Tafuta punguzo
Mara nyingi vitu huuzwa kwa punguzo, hivyo ni vyema ukanunua vitu kwa
punguzo kuliko kununua kitu katika bei halisi ili kupuguza gharama. Naamini
unafahamu kuwa yapo maduka yanayouza aina fulani ya shati kwa shilingi
laki tatu, lakini shati hilo hilo linauzwa kwa shilingi elfu kumi na tano duka
jingine. Sasa kwanini usinunue kwenye hili duka la pili linalouza shati kwa
shilingi elfu kumi na tano? Epuka sifa na ufahari usiokuwa na sababu, tafuta
na nunua vitu kwa punguzo ili kuokoa pesa ambazo zingepotea bila sababu.
Naamini kwa kufanya hivi utaweza kupangilia pesa zako vyema na hatimaye
kujiwekea akiba.
Neno la mwisho: Pesa siyo kila kitu katika hii dunia, lakini ina nafasi kubwa
sana. Hivyo ukitaka kuwa na utawala mzuri katika maisha yako ni vyema
ukaimarisha misingi ya matumizi yako ya pesa. Epuka tabia za kitoto au za
watu wasiokuwa na busara, ambao hula au kutumia kila wanachokipata.
Naamini njia hizi 10 zilizoelezwa hapa zitakupa mwanzo mzuri wa matumizi
ya pesa.
SOMO: 10
Kama unapenda kuokoa kiasi cha mafuta yanayopotea bila sababu ya msingi
katika gari lako, basi tumia njia hizi 8 zifuatazo.
1. Kabili upepo
Unapoendesha gari upepo hukinzana na gari; hivyo kadri gari linavyokinzana
zaidi na upepo ndiyo pia unavyotumia mafuta mengi zaidi. Hivyo basi,
usipende kuweka mizigo juu ya gari kwa nje (carrier) au kufungua vioo kwani
kutasabisha ukinzani zaidi kati ya gari na upepo.
2. Punguza mwendo
Hakuna haja ya kukimbia wakati huna jambo la haraka unaloliwahi; pia
hakuna haja ya kukimbia ili uwe mbele ya gari linalofuata.
Kufanya hivi kutakupotezea kiasi kikubwa cha mafuta bila sababu yoyote ya
msingi. Endesha mwendo wa wastani kama hakuna ulazima wa kuchochea
mwendo na kupoteza mafuta mengi bila sababu.
3. Zingatia Matengenezo
Gari linahitaji matengenezo ya mara kwa mara. Kutofanyia mifumo kama vile
injini na magurudumu matengenezo kwa wakati kutakufanya kupoteza kiasi
kikubwa cha mafuta.
Unahitajika kuhakikisha mafuta lainishi (oil) yapo katika hali nzuri na katika
kiwango cha kutosha katika injini yako. Pia unatakiwa kukagua ujazo wa
magurudumu ya gari lako; kwani kadri gurudumu linavyokuwa na ujazo
mdogo, ndivo linavyohitaji mafuta mengi zaidi kulizungusha.
4. Punguza uzito
Kadri gari linavyokuwa na uzito mwingi ndivyo linavyohitaji mafuta zaidi
kuliendesha. Ikiwa hakuna haja ya kuongeza uzito usio na sababu kwenye
gari basi upunguze.
Hakuna haja ya kubeba mizigo na vifaa usivyovitumia mara kwa mara kila
ufanyapo safari. Jitahidi kupunguza mizigo isiyo ya lazima katika gari lako ili
kuokoa matumizi yasiyo ya lazima ya mafuta.
5. Zingatia matuta
Matuta huwekwa katika barabara ili kutawala mwendo. Hivyo kufunga breki
ghafla mara ukutapo tuta na kuchochea mwendo ghafla baada ya tuta
kutakufanya utumie kiasi kikubwa zaidi cha mafuta.
6. Zima kiyoyozi
Ufanyaji kazi wa kiyoyozi (AC) katika magari mengi hutegemea nishati
inayozalishwa na kifaa kiitwacho Alternator ambacho huzalisha umeme kwa
msaada wa injini ya gari.
Hivyo basi, kuwasha kiyoyozi kutahitaji mafuta zaidi ili kuendesha kifaa hiki
kiitwacho Alternator. Inashauriwa kuwasha kwa muda au kuzima kiyoyozi pale
ambapo hakina ulazima ili kuokoa matumizi ya mafuta yasiyo ya lazima.
7. Tumia kiongeza mwendo vyema
Matumizi mazuri ya kiongeza mwendo (Accelerator), kutakuokolea kiasi
kikubwa cha mafuta mara uendeshapo gari. Mambo ya kuzingatia katika
swala hili:
Hitimisho
SOMO: 11
Mambo Matano Muhimu ya Kuzingatia Kabla ya
Kuomba Mkopo
Ni vyema ukafahamu gharama hizi ili uone kama utazimudu vyema. Hakikisha
waraka wa mkopo unaopewa unausoma na kuuelewa vyema kabla ya
kuidhinishiwa kupokea mkopo ili kuepusha matatizo yoyote mbeleni.
Neno la mwisho
Kwa hakika mikopo imewasaidia wengi lakini pia imewafilisi wengi kutokana
na kutokufahamu mambo ya muhimu ambayo wangepaswa kuyazingatia
kabla ya kuomba mkopo.
SOMO: 12
Mambo ya Kuzingatia Ili Kuchagua Kichwa Kizuri cha
Kitabu
Ukizingatia haya utaweza kupata msingi mzuri wa kuchagua kichwa kizuri cha
kitabu.
Tumia ubunifu wako kama mwandishi ili uteke fikra na hisia za msomaji
kupitia kichwa cha kitabu chako.
Kwa mfano unaweza kuandika kitabu cha kuwafundisha watu jinsi ya kuwa
matajiri na ukatumia vichwa hivi:
i. Jifunze jinsi ya kuwa tajiri
Hakikisha kichwa cha kitabu chako kinasadifu yaliyomo ndani ya kitabu chako
ili ufikishe ujumbe vyema kwa hadhira lengwa.
Hitimisho
2. Je ni wakati sahihi?
Kufanya jambo lolote nje ya wakati ni kosa kubwa. Hakikisha uamuzi
unaoufanya wa kuacha kazi ni kwa wakati sahihi.
Kuacha kazi bila kufikiri juu ya maswala haya kunaweza kukufanya usipate
kazi tena. Inawezekana wapo watu tele wanaotafuta kazi kama yako, hivyo
kuiacha ni kuipoteza daima.
Kuacha kazi bila kujiuliza swali hili kutakuweka kwenye hali ngumu.
Chukua muda uwatumie watu wengine walioacha kazi kama shule yako ya
kujifunza. Je maisha yao yakoje? Yamekuwa mazuri au mabaya? Tafakari
vyema kabla ya kuchukua hatua.
Usiache kazi bila kuwa na kiasi cha uhakika cha akiba itakayokusaidia wewe
na wale wanaokutegemea.
Neno la mwisho
Earl Nightingale
Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani,
ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu
vitakavyotuhamasisha.
Napoleon Hill
Walt Disney
3. “Usiruhusu jana itawale sana leo.”
Will Rogers
Steve Jobs
Johann Wolfgang
Henry Ford
Hasidic Proverb
Theodore Roosevelt
Buddha
11. “Muda mzuri wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita.
Lakini muda mwingine mzuri wa pili ni sasa.”
Chinese Proverb
Steven Jobs
Vince Lombardi
Christopher Columbus
Frank Sinatra
Aristotle
Arthur Ashe
Japanese Proverb
19. “Mlango mmoja wa furaha ukifungwa, mwingine
unafunguliwa, lakini mara nyingi tunautazama sana ule
uliofungwa na kushindwa kuona ule uliofunguliwa kwa ajili
yetu.”
Helen Keller
20. “Kila kitu kina uzuri wake, lakini siyo kila mtu anaweza
kuuona.”
Confucius
Joshua J. Marine
Booker T. Washington
Bill Cosby
Reginald Mengi
Albert Einstein
26. “Mtu anayesema hawezi kufanya hatakiwi kumwingilia
mtu anayesema ninaweza kufanya.”
Chinese Proverb
George Eliot
Oprah Winfrey
Farrah Gray
Norman Vaughan
Benjamin Franklin
Steve Jobs
Zig Ziglar
35. “Ndoto zetu zote zinaweza kutokea ikiwa tuna ujasiri wa
kuzifuata.”
Wale Disney
Reginald Mengi
Hajulikani
Chris Grosser
Albert Einstein
Eleanor Roosevelt
Kim Garst
42. “Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga
msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na
wengine.”
David Brinkley
Hajulikani
Orarah Winfrey
Reginald Mengi
Steve Jobs
Reginald Mengi
Less Brown
Napoleon Hill
SOMO: 4
6. Tafuta ofisi
Watu wengi wamekuwa wakianzisha kampuni kwa mazoea bila kuzingatia
kuwa ofisi ni muhimu kwa biashara au kampuni zao. Tafuta ofisi utakayo
mudu gharama zake, pia yenye kukidhi mahitaji ya kampuni au biashara yako.
7. Bainisha changamoto
Changamoto zipo kila mahali; hivyo yakupasa kuzifikiria kabla ya kuanza
kampuni au biashara yako. Kama unajidanganya kuwa utafanya biashara bila
kukutana na changamoto yoyote unajidanganya.
Hitimisho:
Naamini makala hii imekupa mwongozo juu ya mambo unayotakiwa
kuyafanya kabla ya kuanzisha kampuni au biashara yako. Naamini ukiyafanya
haya utaweza kuanzisha kampuni au biashara itakayokuwa na mafanikio
makubwa.
SOMO: 15
2. Huimarisha meno
Maziwa ni chanzo bora cha madini ya kalisiamu, hivyo basi maziwa ndicho
kitu halisi kinachohitajiwa na meno yetu. Pia maziwa huzuia kutoboka na
kuoza kwa meno. Kalisiamu hufyonzwa na miili yetu kukiwa na vitamini D;
hivyo jitahidi kunywa maziwa kwani maziwa huwa na vitamini D.
3. Huimarisha mifupa
Ni ukweli usiopingika kuwa watoto wanahitaji kunywa maziwa ili kuimarisha
ukuaji wao. Ni kweli pia watu wazima wanahitaji kunywa maziwa ili kulinda na
kuimarisha mifupa yao dhidi ya magonjwa kama vile udhaifu wa mifupa
(osteoporosis). Maradhi haya huzuiliwa kwa kalisiamu ipatikanayo kwenye
maziwa na ambayo hufyonzwa kutokana na uwepo wa vitamini D.
4. Kujenga misuli
Maziwa yana mchango mkubwa katika ukuaji wa misuli. Hili ni kutokana na
protini zinazopatikana katika maziwa. Wanariadha wengi hunywa maziwa
baada ya mazoezi, hii ni kwa ajili ya kuupa mwili virutubisho vya kutosha kwa
ajili ya kujijenga tena. Maziwa huzuia maumivu ya misuli pamoja na kurudisha
ute ulipotea kwenye misuli wakati wa kazi mbalimbali.
5. Kupunguza uzito
Utafiti unaonesha kuwa wanawake wanaokunywa maziwa hupunguza uzito
zaidi kuliko wale wasiokunywa. Inashuriwa kunywa maziwa wakati wa chakula
cha jioni au unapokula matunda. Pia maziwa yanaweza kutumiwa kama kileta
hamu ya kula yaani appetizer.
9. Huondoa kiungulia
Kiungulia huwasumbua sana watu wengi. Kiungulia husababishwa na asidi
zipatikanazo tumboni. Hivyo maziwa (ambayo si mgando) hutengeneza
utando maalumu tumboni ambao hupambana na asidi hizi.
Hitimisho
SOMO: 16
Ukizingatia haya utaweza kupata kiwanja kizuri kwa ajili ya kujenga nyumba
bora kwa ajili ya matumizi yako.
Ramani mbaya.
Weka makadirio ya gharama za ujenzi ili angalau uandae kiasi fulani cha
pesa.
Nunua baadhi ya vifaa kabla. Unaweza kununua mchanga, mawe, kokoto,
nondo, mabati n.k. Ili kupunguza matumizi ya pesa wakati wa ujenzi.
Weka mipango ya kutunza mahitaji yako mengine ya pesa kabla ya kuanza
ujenzi. Kwa mfano ada za shule, kodi mbalimbali, chakula n.k.
Punguza matumizi yasiyokuwa ya lazima kabla na wakati wa ujenzi.
Ikumbukwe kuwa pesa nyingi zitahitajika kwenye ujenzi.
4. Kutokubainisha mahitaji
Mahitaji ya nyumba hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Hivyo ni
vyema ukabainisha mahitaji yako kwa nyumba husika. Nimeshuhudia watu
wakijenga nyumba na kuzivunja ua kuzifanyia marekebisho kila mwaka
kutokana na kutobainisha mahitaji yao mapema.
5. Kutokuwaza mbeleni
Ni vyema kuwaza mbeleni kwani nyumba ni kitu utakachokitumia muda mrefu.
Ni vyema ukafahamu vitu na mahitaji utakayoyataka kwenye nyumba yako
kwa siku za mbeleni. Hili litakuwezesha kujenga nyumba utakayoitumia na
kuifurahia kwa muda mrefu zaidi.
Hitimisho