Professional Documents
Culture Documents
HAKI ZAKE
JANUARI, 2016
MTOTO NA
HAKI ZAKE
SHERIA KATIKA
LUGHA RAHISI
JANUARI, 2016
KIMEANDALIWA NA:
Chama Cha Wanasheria Tanzania Bara (Tanganyika Law Society)
Kiwanja Na. 391, Mtaa wa Chato
Regent Estate, S.L.P 2148
Dar es Salaam, Tanzania.
Simu +255 22 2775313 / +255 22 5500002
Nukushi +255 22 2775314
Barua Pepe info@tls.or.tz
Tovuti www.tls.or.tz
SHUKRANI ............................................................................... iv
Maana ya Mtoto ......................................................................... 1
Mkataba wa Kimataifa wa Haki za
Mtoto wa mwaka 1989 .............................................................. 1
Mkataba wa Kiafrika wa Haki na Ustawi wa
Mtoto wa mwaka 1990 .............................................................. 3
Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 ................................................ 4
Wajibu wa Mtoto ........................................................................ 5
Wajibu wa Mzazi au Mlezi Kulinda Haki za Mtoto .................... 6
Wajibu wa Jamii ......................................................................... 7
Sheria ya Mtoto na Ajira kwa Watoto ......................................... 7
Mahakama ya Watoto ................................................................. 8
Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 ................................................. 9
Cheti cha Mtoto cha kuzaliwa .................................................... 10
Mtoto aliye kwenye mgogoro na Sheria ....................................... 10
Makosa Ambayo Mtoto Anaweza Kufanya .................................. 11
Ulinzi wa Mtoto na Maslahi Yake Katika Mfumo wa
Haki Jinai .................................................................................... 12
Uthibitisho wa Nasaba ya Mtoto na Matokeo yake...................... 15
Kwanini Uthibitisho wa Nasaba? ................................................. 15
Pili, Shukrani ziende kwa Taasisi ya Legal Service Facility (LSF) kwa
ufadhili na ushauri wa kipekee katika kuandaa kijarida hiki.
Unyonyaji wa Mtoto
Hili ni tatizo kubwa duniani kote ambalo mkataba huu unataka
Kwa mujibu wa sheria hii mtoto ni mtu yeyote mwenye umri chini
ya miaka kumi na nane. Sheria hii inafanunua zaidi kuwa mtoto ni
pamoja na mtoto yatima, mtoto aliye katika mazingira magumu,
mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa, mtoto wa kuasiliwa, na mtoto
anayelelewa katika vituo vya kulelea watoto.
Mahakama ya Watoto
Mahakama ya Watoto imeanzishwa Kisheria ili kuhakikisha mashauri
yote yanayohusu watoto yanasikilizwa na kuamuliwa kwa kuzingatia
taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto. Hivyo;
➣ Mahakama ya Watoto itasikiliza na kuamua mashauri ya jinai
dhidi ya mtoto.
➣ Maombi yanayayohusu matunzo ya mtoto.
➣ Mahakama ya Watoto itaongozwa na Hakimu Mkazi.
➣ Mashauri yataendeshwa kwa faragha.
➣ Ni haki ya mzazi, mlezi au ndugu kuwepo; Ofisa wa Ustawi wa
Jamii atakuwepo wakati wa kuendesha mashauri.
➣ Mtoto atakuwa na haki ya kuwa na ndugu wa karibu au
kuwakilishwa na Wakili.
➣ Haki ya kukata rufaa itafafanuliwa kwa mtoto ili aielewe.
➣ Mtoto atakuwa na haki ya kutoa ufafanuzi na maoni.
➣ Uwepo wa Afisa Ustawi wa Jamii unahitajika katika Mashauri
yote yamhusuyo mtoto.
Wajibu wa Mzazi
Kuasili mtoto