Professional Documents
Culture Documents
1
IMARISHA NDOA YAKO
SURA YA KWANZA
UMOJA UNAOIMARISHWA KUPITIA KUFAHAMU MWONGOZO WA MUNGU KUHUSU
NDOA
Mwanzilishi wa ndoa ni Mungu mwenyewe na hakuna binadamu ambaye anaweza
kubadili kusudi la Mungu la kuanzisha ndoa zaidi ya Mungu mwenyewe. Kila mtu
anatakiwa kutekeleza kusudi la Mungu la kuanzisha ndoa na siyo kuharibu msingi wa
ndoa ambao Mungu ameuweka. Mungu anataka Mwanamume na mwanamke waoane
kwa kufuata utaratibu uliyowekwa.
Mungu ameuweka Mwongozo au katiba ya Ndoa kwa wanandoa hata kabla ya Adam na
Hawa kumkosea Mungu.
Mwongozo wa Ndoa uliotolewa na Mungu umeandikwa katika vitabu vinne tu katika
Biblia Takatifu, umeandikwa mara moja katika Agano la kale kabla ya Adam na Hawa
kutenda dhambi na umeandikwa mara tatu katika Agano Jipya.
Mwongozo huo una hatua tatu ambazo zinatakiwa kufuatwa ambazo ni kuacha,
kuambatana na kuwa mwili mmoja ambazo nitazifafanua vizuri katika kitabu hiki.
Lengo la somo hili ni kumsaidia mume na mke kujifunza wote pamoja kwa ajili ya
kukuza na kuboresha ndoa yao na kujua maana halisi ya kuacha wazazi, kuambatana
mume na mke na kuwa mwili mmoja.
A. Ninavyofahamu mimi katika Biblia Takatifu Mungu ametamka mara nne tu kauli
moja ya kuhusu ndoa au amesisitiza Mwongozo wa Ndoa au katiba ya Ndoa
mara nne katika Biblia Takatifu.
1. Amesema katika kitabu cha mwanzo 2:24, Mathayo 19:5, Marko 10:7, 8 na
Waefeso 5:31, ‘...na kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na
mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili
mmoja’.
2. Mungu ameirudia kauli hii mara nne katika Biblia takatifu, kama nilivyosema
awali aliitoa mara moja katika Agano la kale kabla ya la anguko la dhambi
kwa binadamu (Adamu na Hawa kutenda dhambi) na ameitoa mara tatu
baada ya anguko la dhambi katika Agano la Jipya. Kurudia kwake Mungu
kauli hiyo kuna maanisha kwamba huo ndio Mwongozo wa Mungu kuhusu
Ndoa takatifu kwa binadamu mwenye dhambi na aliyeanguka katika dhambi.
Kwa ujumbe huo au kauli hiyo, Mungu anataka ndoa bora/takatifu na siyo
bora ndoa au ndoa ya takafujo kwa wanandoa.
B. Mwongozo mzuri unaotakiwa katika ndoa nzuri ambayo Mungu anaitaka ni ule
ambao una mpango mkakati au (mradi ujenzi/building project).
1. Leo, wanandoa wengi hawana furaha, wana machungu, wana majeraha ya
ndoa, hawatimiziani au hawatoshelezani mahitaji yao ya ndoa si tu kwa
ndoa za wasio wakristo, hata ndoa za wakristo matatizo hayo yapo.
2
IMARISHA NDOA YAKO
3
IMARISHA NDOA YAKO
4
IMARISHA NDOA YAKO
5
IMARISHA NDOA YAKO
6
IMARISHA NDOA YAKO
7
IMARISHA NDOA YAKO
yao, mateso yao, furaha zao, mawazo yao, uwezo wao, matatizo yao,
mafanikio yao, kushindwa kwao, n.k.
b. Mume na Mke ni timu moja na cho chote atakachofanya mmoja wapo
lazima atambue kuwa anafanya kwa ajili ya mwenzake au angalau sio
lazima awe anazingatia au anajali mahitaji ya mwenzake (Waefeso
5:28; Mithali 31:12, 27).
c. Mume na mke si wawili tena bali ni mwili mmoja. Na hii dhana ya
mwili mmoja lazima ijidhihirishe kwa njia ya matendo siyo kwa
maneno ya mdomoni tu, ielewezwe kwa kuonyesha matendo. Mungu
hakukusudia hiyo iwe dhana tu au nadharia bora, lakini ni dhana
yakinifu (dhana ya ukweli). Urafiki kamili na umoja wa ndani ni
sehemu ya Mwongozo wa Mungu kuhusu ndoa.
3. Urafiki kamili na umoja wa ndani sana, hata hivyo, haumaanishi kuwa ni
wanafanana au wanakuwa sawa kimawazo na kimsimamo katika hali ya
kiroho.
a. Mfano, Mwili wangu umeumbwa na viungo mbalimbali, Mkono wangu
hauwezi ukafanya kazi ya mdomo, moyo wangu hauwezi ukafanya
kazi ya ini na wala masikio hayawezi kufanya kazi ya kichwa.
b. Kila kiungo katika mwili kina kazi yake lakini vina umoja. Viungo
vyangu vya mwili vinaonekana tofauti na vina tenda kazi tofauti,
lakini uhalisi ni kwamba kila kiungo kina fanya kazi kwa manufaa au
kwa faida ya viungo vingine na kiungo kimoja hakiwezi kamwe
kikajaribu kukiumiza kiungo kingine.
c. Kazi za viungo vya mwili ni sawa na kazi za mume na mke ambazo
zinafanyika ndani ya ndoa na wanaweza wakawa wanaoneka tofauti
kwa sura, kimo, kimaongezi, kielimu, kiheshima na hata kiimani
lakini hawatakiwi kuruhusu tofauti zao kuzuia au kuharibu umoja wao
katika ndoa kwa sababu kusudi la Mungu kuhusu ndoa ni kuwa mwili
mmoja, kuwa na umoja kamili.
C. Lakini tambua kwamba kuwa mwili mmoja (umoja kamili-total oneness)
ambako Mungu anataka wanandoa tufikie siyo rahisi sana kufanikiwa kama
hatutazingatia Mwongozo wa Mungu kuhusu Ndoa na kutambua vikwazo
vyake ambayo ni dhambi kupitia milango mbalimbali kama ifuatavyo:-
1. Mojawapo ya kikwazo kikubwa cha kuzuia wanandoa wasiwe mwili
mmoja au kuwa na umoja kamili na wanaendelea kubaki kuwa wawili
badala ya mwili mmoja ni dhambi zetu.
a. Katika kitabu cha Mwanzo 2:25, mara tu baada ya Mungu kuwaambia
Adamu na Hawa kuwa Mume na Mke wawe mwili mmoja na si wawili
tena, Maandiko yanasema, “Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu
na mkewe, wala hawakuona haya”.
b. Kuwa uchi Adamu na Hawa siyo pendekezo la jamii kuwa uchi. Hilo
lilitokea kabla ya watu kuwa wengi au kuongezeka. Adamu alikuwa
binadamu pekee ambaye alimwona Hawa akiwa uchi wa mnyama, na
8
IMARISHA NDOA YAKO
9
IMARISHA NDOA YAKO
10
IMARISHA NDOA YAKO
11
IMARISHA NDOA YAKO
12
IMARISHA NDOA YAKO
5. Kutii hakuna maana kuwa mke ni mnyonge (kiumbe duni au dhaifu) kwa
mume wake. Yesu Kristo hakuwa mnyonge kwa Maria na Yusufu (wazazi
wake), na bado Maandiko yanaeleza kuwa kama mtoto, “Yesu aliendelea
kuwatii” (Luka 2:51). Yesu kwa namna yo yote hakuwa mnyonge kwa Mungu.
Yesu alikuwa na ni Mungu kamili, kwa kila sifa. Bado Maandishi yanaeleza
kuwa kuna utaratibu na Muundo wa Utata mtakatifu (Mungu baba, Mungu
Mwana na Roho Mtakatifu). Yesu anasema, “Mimi siwezi kufanya jambo lo
lote kwa mamlaka yangu mwenyewe. Mimi nahukumu kufuatana na jinsi
Mungu anavyoniambia. Na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti
kufanya nipendavyo, bali nafanya mapenzi yake yeye aliyenipeleka.”
(Yohana 5:30) naye Paulo anasisitiza, “Lakini napenda muelewe kwamba
Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa
cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo” (1 Wakorintho 11:3). Kwa
kweli, haimaanishi kuwa Yesu alikuwa mnyonge kwa Mungu baba. Badala
yake Yesu anatufundisha kwamba kuna mgawanyiko wa kazi na majukumu
katika Utatu mtakatifu. Kwa mtindo kama huo, utii wa mke kwa mumewe
kwa njia yoyote haimaanishi ni udhalilishaji au unyonge. Badala yake,
inafundisha umuhimu wa kufuata utaratibu na muundo wa mgawanyiko wa
majukumu ndani ya nyumba (ndoa). Ukisoma Mwanzo 1:26,27; 2:23 na
Wagalatia 3:28 vyote hivyo vinaeleza hali ya usawa na haki ya mwanamke
na mwanamume.
B. Baada ya kujifunza mtazamo hasi au picha mbaya ya maana ya utii wa mke kwa
mumewe kwa mujibu wa Biblia Takatifu, sasa tuangalie maana halisi ya utii wa
mke katika ndoa yake kwa mtazamo chanya kwa mujibu wa Biblia takatifu;-
1. Maandishi yanaonyesha kuwa ni wajibu wa mke mwenyewe kuwa mtiifu
(kutii): - Hakuna mahali po pote kwenye Biblia ambapo panaeleza kuwa
Mungu amemuagiza mume kumlazimisha mke amtii. Badala yake maandiko
yanaeleza kuwa Mungu amemamuru mke mwenyewe kuwa mtiifu au amtii
mume wake bila kulazimishwa na mtu ye yote kwa kuwa ni agizo la Mungu
ambalo mke anatakiwa kulitekeleza. (Soma Waefeso 5:22 na 1Petro 3:1.)
2. Maandishi yanaonyesha kuwa utiifu wa mke ni lazima uwe endelevu au
usiwe na mwisho ni wa kila siku: - Katika mstari huo unaoelezea kutii kwa
mke katika vifungu vya Biblia kitenzi kipo katika wakati uliopo wa sasa
kikiwa na maana ya kwamba mke kutii ni suala la wakati uliopo wa sasa ni
suala endelevu lisilo na mwisho mpaka kifo kiwatenganishe wanandoa hao.
(Soma Waefeso 5:22 na 1Petro 3:1.)
3. Mke Kutii au kuwa mtiifu kwa mume wake ni lazima, siyo hiari: - Ukisoma
kitenzi cha Kiswahili kinachoelezea mke kutii kipo katika hali ya lazima.
(Soma Waefeso 5:21, 22 na 1Petro 3:1.) Mke kuwa mtiifu au kumtii mume
wake hakupaswi kutegemea namna gani mume anaishi na mke wake au
mume anavyomtendea mkewe. Utiifu wa mke kwa mumewe hakutegemei
kipaji cha mume, uwezo wa mume, hekima ya mume, elimu ya mume, au
hali ya kiroho ya mume. (Soma 1Petro 3:1 na Luka 2:51.)
13
IMARISHA NDOA YAKO
4. Mke Kutii au kuwa mtiifu kwa mume wake ni suala la kiroho:- Suala la
mke kumtii mume wake linafanyika kama kwa Bwana (Waefeso 5:22).
Bwana anamuamuru mke kutii kwa hiyo mke kutokuwa mtiifu au kushindwa
kutii ni kumuasi Mungu mwenyewe. Mungu ndiye aliyetoa amri kwa mke
kumtii mume wake na siyo mume ametoa amri kwa mke wake amtii. Suala
la mke kumtii mume wake ni jaribio la kuona namna gani mke anampenda
Mungu pamoja na mume wake. Kwa hiyo mke anatakiwa aangalie kuwa
mtiifu kwa mume wake kama tendo la kudhihirisha utii wake kwa Yesu
Kristo na siyo kwa mume wake. Yesu alisema, “Mkinipenda, mtazishika amri
zangu” (Yohana 14:15), na moja ya amri zake kwa wake ni, “Wake, watiini
waume zenu kama mnavyomtii Bwana” (Waefeso 5:22). Bado nasisitiza
kuwa suala la mke kumtii mume wake ni sauala la kiroho ambalo mke
ambaye ametakaswa na Yesu Kristo na kujaa nguvu za Roho Mtakatifu
hataona uzito kutekeleza amri hiyo ya kutii (Waefeso 1:1-5:21; 1Petro 1:1-
3, 6.)
5. Utiifu katika dhana nzuri (mtazamo mzuri), na siyo dhana mbaya (siyo
mtazamo mbaya):- Biblia inasisitiza zaidi jambo la mke kutii kuliko jambo
ambalo hatakiwi kutii. Kuna mtumishi wa Mungu Bill Gothard amefafanua
Kutii kuwa ni haki iliyokusudiwa. Anaendelea kufafanua kuwa utiifu ni uhuru
wa kuwa mbunifu katika kutekeleza maagizo ya Mungu. Utiifu wa mke kwa
mume ni kitendo cha mke kuwekeza nguvu zote za vipaja, uwezo,
rasilimali, nguvu yote kwa ajili ya mume wake. Utii wa mke kwa mume
wake ni uwezo wa mke kutekeleza mipango mkakati waliyopanga na mume
wake kwa ajili ya faida ya familia yao pamoja na kumshauri mume mambo
mazuri na kumkataza kufanya mambo mabaya yayoweza kuiingizia hasara
familia au ndoa yake pamoja na kumkosanisha na Mungu. Mke anajua wajibu
wake kama mjumbe mmojawapo katika maamuzi ya mipango ya familia na
mtekelezaji wa maamuzi yanayofanyika katika ndoa na humshauri mume
kwa hekima.
6. Kutii kunajumuisha mtazamo pamoja na matendo ya mke:- Yesu alikuwa
mtiifu kikamilifu kwa baba. Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni
kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma, na kuikamilisha kazi yake”
(Yohana 4:34). Alifanya kazi ya Mungu kwa moyo wa furaha na si kwa
kulazimisha. Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu (Zaburi 40:7, 8).
Ndivyo ilivyo hata kwa mke anatakiwa kumtii mume wake kwa moyo wa
furaha pasipo na chuki wala kulazimishwa na mtu ye yote. Kwa mujibu wa
maandiko, Mungu anamtaka mke kufanya kazi kwa mikono yake mwenyewe
kwa ajili ya kuinua kipato cha familia yake (Mithali 31:13), anatakiwa
atafute mahitaji kwa ajili ya kutosheleza mahitaji ya familia yake na
kutimiza mahitaji ya mume wake. Waefeso 5:33 inaelezea mtazamo kwa
baadhi ya mambo ambayo mke anatakiwa atii kwa mume wake.
7. Utiifu wa mke ni jambo linalotakiwa liangaliwe kwa upana zaidi: - Mke
anatakiwa amtii mume wake pamoja na kanisa la Kristo (Waefeso 5:24).
14
IMARISHA NDOA YAKO
Kristo ni kichwa cha kanisa (Waefeso 1:22) na mambo yote yanafanyika kwa
utukufu wa Mungu mwenyewe (Wakolosai 3:17; Mithali 3:5, 6 na
1Wakorintho 10:31).
Kwa maana nyingine, kutii hakuna maana kwamba mke amtii mume wake
hata kama anamuamuru amkatae au amtukane Mungu, anatakiwa atii amri
za Mungu zote na atekeleze maagizo mume wake kama sehemu ya
mgawanyiko wa mamlaka kutoka katika taasisi ya ndoa ambayo ipo chini ya
Mungu. Mke anatakiwa kukataa maagizo au maelekezo yo yote
yanayotolewa na mume wake ambayo kusudi lake ni kumkosanisha mke na
Mungu, mfano mume anamuagiza mke aiende akaibe au akajiuze kwa
wanaume huko wapate fedha, hayo hatakiwi kufanya kabisa na ikiwezekana
amshughulikie kikamilifu ili amuokoe mume wake katika mikono ya shetani
(Soma Wakolosai 3:18). Mume hana mamlaka ya kumuzuia mke asifanye kile
ambacho Mungu ameagiza afanye na kushindwa kutekeleza amri au maagizo
ya Mungu ni uasi (Matendo 5:28-29).
Utii wa mke kwa mume wake ni tendo lisilo na kikomo, linatakiwa kufanyika
kila wakati, muda wo wote (asubuhi, mchana, jioni na usiku). Mke
anatakiwa kumtii mume wake kwa kila kitu ilimradi hakipingani na Neno la
Mungu. Mke anatakiwa kuwa msaidizi wa mume wake na siyo mpinzani wa
mume wake (Soma Mwanzo 2:18).
15
IMARISHA NDOA YAKO
16
IMARISHA NDOA YAKO
17
IMARISHA NDOA YAKO
18