You are on page 1of 26

 Imeandaliwa na kuwasilishwa na

Dr. Baraka F. Kanyabuhinya


Chuo Kikuu cha Dar es Salaam- Shule kuu ya Sheria
kanyabuhinya@yahoo.co.uk
 Utangulizi na Historia
 Sheria zinazohusika na kulinda Hakimiliki
 Hakishiriki ni nini
 Umuhimu wa kulinda Hakimiliki
 Haki zinazolindwa
 Vigezo vya kazi zinazostahili kulindwa
 Muda wa ulinzi
 Mmiliki wa Hakimiliki ni nani?
 Jinsi ya kunufaika na hakimiliki
 Hakimiliki za kimila
 Vyama vya kulinda hakimiliki na wajibu wake
 Sheria za kimataifa
 Ukiukwaji na adhabu
 Umuhimu wa kurekebisha sheria zinazohusiana na
hakimiliki
 Nini Kifanyike kuimarisha ulinzi wa kazi zenye hakimiliki
 Hakimiliki na hakishiriki ni moja sehemu ya
sheria zinazohusu ulinzi wa kisheria wa miliki
bunifu.
 Hakimiliki kwa upande wake hulinda kazi za
ubunifu za kiuandishi na za wabunifu wa
sanaa (literary and artistic works)
 Sheria huzuia kazi hizi zisinakiliwe,
kuzalishwa au kusambazwa na mtu
mwingine asiye mmiliki wa kazi husika.
 Sheria ya kwanza ya hakimiliki ilitungwa
Tanganyika mwaka 1924 (The Copyright
Ordinance)
 Sheria ya mwaka 1924 ilifutwa baada ya uhuru
hapo mwaka 1966 na sheria namba 61 ya
mwaka 1966.
 Mwaka 1999 bunge la Tanzania lilitunga sheria
mpya ya Hakimiliki na hakishiriki (sura na 218)
ambayo ndiyo inatumika mpaka sasa
 Hakimiliki ni haki ya msingi inayolindwa
kisheria kwa kazi yoyote ya utunzi, ubunifu na
uandishi wa kazi za maandishi na za kisanii.
 Hakishiriki ni haki muambata kwa hakimiliki
apewayo mshiriki katika kazi inayolindwa na
hakimiliki, mfano mtunzi wa mziki anakuwa
mmiliki wa hakimiliki, wachezaji wa jukwaani
wanastahili kutambuliwa kwa hakishiriki.
 Kujenga ari ya ubunifu kwa kuwafaidisha
wabunifu kwa kazi zao
 Kusambaza kazi za ubunifu kwa watumiaji
wengine
 Kufidia jasho na kazi za mbunifu-asiyefanya
kazi na asile
 Kujenga utamaduni na jamii bunifu
 Kutekeleza mikataba ya kimataifa kuhusu
ulinzi wa milikibunifu.
 Haki za kiuchumi na haki za haki za kiutamaduni/hadhi
 Haki za kiuchumi ni zile zinazomnufaisha mmiliki
kiuchumi moja kwa moja –mfano ukiuza kazi,
ukiikodisha, ukiiazimisha kwa malipo, ukimpa haki
mwingine aitumie kwa malipo, kuionyesha katika
umma, kuisambaza, kuitangza katika vyombo vya
habari nk.
 Haki za kiutamaduni/hadhi hulinda hadhi na taswira ya
mtunzi isichafuliwe machoni kwa jamii- mfano inazuia
kuchana kazi ya mtu, kutumia kazi kwa kudhalilisha
mtunzi nk.
 Mifano ni mingi: vitabu, muziki, filamu, sanaa,
uchoraji, uchongaji, ramani, picha za sinema,
mihadhara, hotuba, michoro, ramani za
nyumba, mahubiri picha na katika nchi
nyingine program za komputa.
 Kazi inalindwa kama mtunzi/mwandishi
mtanzania, mkazi wa Tanzania au kama kazi
imechapishwa kwa mara ya kwanza Tanzania.
 Kazi lazima liwe wazo halisi la
mbunifu/mwandishi au mtunzi
(original work of authorship)
 Sheria inalinda mawazo
yaliyodadavuliwa (expressed) na
siyo wazo tu (idea).
 Hakimiliki hulindwa kwa muda wa maisha
yote ya mbunifu/mwandishi kujumlisha miaka
hamusini baada ya kufariki.
 Kama ni kazi imebuniwa pamoja –ni baada
miaka 50 ya maisha ya mbunifu wa mwisho
kuishi.
 Kazi za video/muono-miaka 50 baada ya
kutungwa au kutangazwa kwa umma-hii
inahusu pia kazi amabayo mtunzi hajulikani.
 Mmiliki wa kwanza ni mbunifu/mwandishi
(aliyeibuni kazi husika),
 Anaweza asiwe mmiliki kama ameuza kazi yake
au alikodiwa/alilipwa kuibuni kazi hiyo kwa niaba
ya mtu mwingine,
 Mbunifu hatakuwa mmiliki kama kazi hiyo
ameifanya kama mwajiriwa kwa niaba ya mwajiri.
 Kazi inaweza hama umiliki kwenda kwa mwingine
kwa njia ya leseni/kibali.
 Kama mmiliki una haki ya kipekee kuuza,
kusambaza, kudurufu, kuzalisha nakala,
kukodisha, kuionyesha/kuicheza sehemu za
umma, kutafsiri, kuionyesha katika vyombo vya
habari, kuitumia hadharani nk.
 Mtu mwingine yoyote amezuiliwa kufanya hayo
bila kupata kibali cha mmiliki na mara nyingi
kibali hutolewa baada ya malipo kwa mmiliki.
 Kuitumia bila kibali ukiwa si mmiliki ni kuvunja
sheria na kuna adhabu zake.
 Kazi za uandishi na sanaa za kimila zimelindwa
kisheria(folklore)
 Ni pamoja na nyimbo za kimila,vitendawili,
misemo, methali, michoro, ufinyanzi, vinyago,
mapambo ya mavazi, vifaa vya muziki vya kijadi
nk.
 Sheria inamtaka yoyote anayetaka kutumia kazi
hizi za kimila/kitamaduni kupata kibali kutoka
Baraza la Sanaa la Taifa (National Arts Council)
baada ya malipo yatakayotumika kukuza
utamaduni.
 Ulinzi wa hakimiliki hauhitaji usajiri japo usajiri
una faida nyingi.
 Chama kinachosajiri kazi zenye hakimiliki
Tanzania bara kinaitwa The Copyright Society
of Tanzania (COSOTA), kwa visiwani COSOZA
 Inashauriwa kusajiri kazi zenye hakimiliki kwa
sababu usajiri una faida nyingi.
 Kurahishisha kuthibitisha umiliki wa
hakimiliki ukitokea mgogoro
 Kurahisisha mtu yoyote kujua kazi yako
ina hakimiliki na mmiliki
 Kukuwezesha kulipwa mirahaba kwa
matumizi ya kazi zenye hakimiliki ndani
na nje ya nchi
 Jaza fomu ya maombi COSOTA
 Kazi itachunguzwa kuona kama hakuna
iliyosajiriwa inayofanana
 Ambatanisha nakala mbili za kazi husika, picha
mbili za passport, vitambulisho
 Nakala ya mkataba au nyaraka nyigine
kuthibitisha kazi ni yako au unaimiliki na wengine.
 Kwa badhi ya kazi viambatanisho zaidi vinaweza
kuhitajika mfn kazi ya kwaya orodha ya
wanakwaya wote.
 Kibali cha kumkodisha kazi yako mtu
mmoja tu(ecxlusive licence) ni kama
umeuza haki zako lazima ulipwe
vizuri
 Kibali cha kukodisha wengi (no
exclusive) kinakuacha huru
kukodisha yoyote atakaye kuitumia
kazi yako
 Mkataba wa Berne(WIPO) 1886
 Mkataba wa TRIPS (WIPO)
 Mikataba hii inawezesha mmiliki wa
hakimiliki mtanzania kulindwa katika nchi
yoyote ambayo imeridhia mikataba hii
 Pia inaipa wajibu Tanzania kulinda kazi za
wageni ambao nchi zao ni washirika
katika mikataba hii.
 Haki za kiuchumi na za kihadhi tulizoziona
hapo juu zikitumiwa na mtu mwingine bila
ridhaa au kibali cha mmiliki basi ni ukiukwaji/
uvunjaji wa sheria.
 Mfano ni kunakili kazi ya mtu na kuiuza kama
yako, au kuicheza sehemu za hadhara
 Unaweza kuthibitisha ukiukwaji kwa
kulinganisha kazi mbili, iliyoibwa na
inayotuhumiwa km kazi ya wizi.
 Ukiukwaji ni makosa ya jinai au ya madai
 Faini isiyozidi milioni 5 au kifungo kisichozidi
miaka 3 au vyote kwa kosa la kwanza na km
ukiukwaji ni wa kibiashara
 Faini isiyozidi milioni 10 au kifungo
kisichozidi miaka 5 au vyote kwa kosa la pili
na kwa kiwango cha kibiashara
 Adhabu ya faini bila kifungo ni ndogo na
mkiukwaji anaweza asijutie kutenda kosa
 Mdai anaweza kuomba amri ya
zuio kuzuia uvunjifu kuendelea,
 kuharibu vifaa vinavyohusika na
uhalifu, kuvikamata na
kuvishikilia, nakala za kihalifu
kuletwa kwa mdai,
 akadai fidia
Matumizi ya kazi yanye hakimiliki kwa kazi
zifuatazo hayatachukuliwa km ukiukwaji:
-Kufundishia, utafiti, nukuu katika kuchapisha
makala
-Kuhabarisha
-Kidini
-Kwa matumizi ya maktaba
Cha kuzingatia kusiwe na faida ya kibiashara
 Kuweka adhabu kali
 Kutambua hakimiliki kikatiba
 Kutambua hakimiliki kama mali nyingine
 Kuvipa meno na kuviwezesha vyama vya
wamiliki wa hakimiliki kama COSOTA
 Kutekeleza sheria bila woga au kupuuza
 Kuruhusu vyama mbadala wa COSOTA
kusajiriwa kuleta ushindani
 Kuelimisha wasanii na waandishi kuhusu haki zao
 Kufundisha somo la hakimiliki kuanzia shule za
msingi, sekondari, vyuo vyote
 Msaada wa kisheria kwa wasanii/waandishi
wasioweza kulipa gharama za wakili
 Wasanii/waandishi kutambua umuhimu wa
wanasheria
 Vyama vya kutoa elimu kutambuliwa na
kuwezeshwa.
Asanteni
kunisikiliza.

You might also like