Professional Documents
Culture Documents
Maudhui ya Msingi
1.0 UTANGULIZI
Bendera ya Taifa
b) Lugha ya Taifa na
Mawasiliano Mbadala
(Ibara ya 4)
Nembo ya Taifa
Katika jamii yetu tunao watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali unaoathiri
fursa zao za kupata mawasiliano kimaandishi au kwa alama. Kwa kutambua
hili, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu, Katiba Inayopendekezwa
inataja lugha ya alama kwa viziwi, na lugha ya alama mguso kwa viziwi
wasioona kuwa lugha rasmi za mawasiliano. Hii ni hatua kubwa katika
kuhakikisha kwamba ndugu zetu wenye ulemavu wanapata haki zao za aina
mbalimbali ikiwamo haki ya kuwekewa mazingira imara ya kupata na kufanya
mawasiliano kwa lugha muafaka kwao.
KATIBA INAYOPENDEKEZWA -Maudhui ya Msingi
e) Mamlaka ya Wananchi
(Ibara ya 7)
b)
10
11
wa miongo kadhaa nchi yetu imekuwa na maadili ya miiko ya uongozi katika sura zake
mbalimbali. Wengi watakumbuka kwamba tumewahi kuwa na waraka uliojulikana sana
kama Mwongozo wa TANU; tumekuwa na miiko iliyotokana na Azimio la Arusha; tumekuwa
na taratibu za kiutumishi zinazoainisha miiko ya maadili ya uongozi. Yote haya yanadhihirisha
kwamba nchi yetu na watu wake hawana ugeni katika eneo hili. Ni wazi, hata hivyo, kwamba
taifa letu limekua, misingi ya haki na uhuru imepanuka, mahitaji ya leo, si mahitaji ya jana. Yote
haya yamekuwa na taathira katika kusimamia na kutekeleza miiko na maadili ya viongozi. Katiba
Inayopendekezwa imetambua haya. Hivyo katika Sura ya nne misingi thabiti ya miiko na maadili
inawekwa.
Kuwekwa kwa misingi hii ndani ya Katiba ni jambo muhimu na la lazima. Lakini ni wazi kuwa
kuwekwa kwa misingi hii ndani ya Katiba peke yake, hakutuhakikishii utekelezaji na umadhubuti
tunaoukusudia. Hivyo Katiba Inayopendekezwa inaelekeza kutungwa kwa sheria mahsusi
zitakazoweka kwa kina utaratibu wa kutekeleza misingi hiyo mikuu. Kwa mfano, msingi wa
kikatiba umewekwa kuhusu haja ya viongozi wa umma kuwasilisha serikalini zawadi mbalimbali
wanazozipata wakiwa katika utumishi wa umma. Huu ni msingi mzuri na muhimu. Lakini kwa
taratibu za uandishi wa Katiba, haiwezekani kuweka maudhui ya kina ndani ya Katiba yanayohusu
utekelezaji wa msingi huu. Hivyo pamoja na kuuweka mwiko huu wa maadili ndani ya Katiba
itakuwa muhimu kwa sheria kutungwa ili kuelekeza utekelezaji wake kwa undani. Sheria hii itahitaji
kuainisha aina za zawadi ambazo mtumishi wa umma atapaswa kuzikabidhi serikalini;
kueleza namna ya kusajili na kuweka kumbukumbu za maandishi
za zawadi hizo; kueleza zitahifadhiwa wapi,
na mamlaka gani; utunzaji
wake; matumizi yake baada
ya kukabidhiwa kwenye
mamlaka husika; zitauzwa
au zitatumikaje; ndani ya
muda gani; kwa manufaa ya
nani, na kadhalika. Haya yote
hayawezekani kukaa kwenye
Katiba na ndiyo sababu Katiba
Inayopendekezwa
inataka
maeneo yote haya yaainishwe
vizuri zaidi ndani ya sheria, tofauti
na kuwekwa kwenye Katiba pekee,
kwani asili yake Katiba haiwezi
kuweka maelekezo ya aina hii kwa
kina, haiweki katazo, wala adhabu.
Sheria ndiyo yenye uwezo wa
kufanya yote haya.
12
Kiongozi wa umma
atapaswa kuzingatia
yafuatayo:-
i. Kufanya uteuzi bila ubaguzi
kwa kuzingatia uwezo, sifa na
mwenendo unaofaa,
ii. Kutoa uamuzi bila kujali udugu,
ukabila, udini, rushwa, na
ubaguzi wa aina yoyote.
iii. Kutoa huduma pasipo upendeleo
na kwa kufuata maslahi ya
umma.
KATIBA INAYOPENDEKEZWA -Maudhui ya Msingi
13
i. Hauruhusu kutokea mgongano kati ya
maslahi binafsi na maslahi ya utumishi wa
umma;
ii. Haushushi hadhi ya ofisi anayofanyia kazi;
au hauruhusu matumizi ya ofisi ya umma
kwa maslahi binafsi.
14
uniani kote Sura ya Haki za Binadamu ina umuhimu wa pekee. Kukaa kwake ndani
ya Katiba ni kuhakikisha zinalindwa kama sehemu mojawapo ya wajibu wa dola kwa
raia. Katiba Inayopendekezwa katika Sura hii imebainisha haki zote kama zilivyo
katika Tangazo la Dunia la Haki za Binadamu la Mwaka 1948. Tofauti na baadhi ya watu
wanavyopotosha, haki hizi zinaweza kutiliwa nguvu mahakamani kwa mujibu wa Ibara ya
65(2) ya Katiba Inayopendekezwa. Sura ya pili ya Katiba Inayopendekezwa inataja malengo
muhimu ya taifa. Malengo yamewekwa kwa nia ya kutoa dira kwa Serikali na vyombo vyake
wanapopanga mikakati mbalimbali ya maendeleo. Utekelezaji wa malengo yale ni endelevu
na hivyo Serikali haipaswi kufikishwa mahakamani endapo utekelezaji wake utachelewa. Hii
ni kwa sababu malengo yale yanabainisha azma ya Serikali ya kuyazingatia katika utekelezaji
wa mpango wa maendeleo. Hakuna Katiba yoyote duniani imeweka utaratibu wa kuifikisha
Serikali mahakamani endapo malengo hayatatimia. Hivyo si sawa kusema kwamba katika
eneo lile kuna haki ambazo haziwezi kudaiwa mahakamani.
15
16
17
18
19
20
Vile vile, Katiba Inayopendekezwa
inaelekeza kwamba watu wenye ulemavu
wana haki ya kupata elimu kwa kutumia
vifaa maalum na kushiriki katika nafasi
za uwakilishi na shughuli za kijamii,
kuwekewa miundombinu na mazingira
yanayofaa yatakayomwezesha kwenda
anapotaka, kutumia vyombo vya usafiri,
kupata habari, kutumia lugha ya alama,
alama mguso, maandishi ya nukta nundu,
maandishi yaliyokuzwa, kupata ajira,
kufanya kazi na kupata huduma bora
za afya na uzazi salama. Kutambulika
kwa kundi hili kikatiba ni fursa nzuri
ya kuhakikisha kwamba taifa letu
linaondokana na vitendo ambayo vina
sura ya ukatili, ubaguzi na unyanyapaa, na
badala yake kuwapa fursa ya kujiendeleza
kisiasa, kiuchumi na kijamii.
21
ix.
x.
22
xi.
23
24
a) Mahusiano kati ya
Serikali ya Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania
na Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar (Ibara ya 77)
b)
25
b) Idadi ya Mawaziri
(Ibara ya 115)
26
27
28
29
a) Mahakama ya Juu
(Ibara ya 171 174)
30
a)
Katiba Inayopendekezwa inaanzisha Tume ya
Utumishi wa Umma ambayo itakuwa chombo cha
juu chenye mamlaka ya nidhamu na uratibu wa
mambo yote ya utumishi wa umma katika Jamhuri ya
Muungano. Pamoja na kazi zake nyingine, Chombo
hiki kitahakikisha kwamba kunakuwepo uwakilishi
na uwiano mzuri wa watumishi wa umma kutoka
Tanzania Zanzibar na Bara.
31
32
Mgombea huru
(Ibara ya 216)
Katiba Inayopendekezwa inaanzisha
utaratibu wa kuwa na mgombea huru
katika nafasi mbalimbali za uchaguzi
kwa ngazi zote. Hili ni jambo jipya
linaloonesha kukua na kukomaa kwa
demokrasia katika nchi yetu.
a)
33
SEHEMU YA TATU
3.0 UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA MUUNGANO
Sehemu hii ya waraka ni mahsusi kwa ajili ya kubainisha
namna ambavyo changamoto za Muungano zimepatiwa
ufumbuzi ndani ya Katiba Inayopendekezwa.
34
35
Kwa mujibu wa Hati ya Makubaliano ya
Muungano, Rais wa Zanzibar alikuwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
ya Tanzania. Hata hivyo, kufuatia mabadiliko
mbalimbali yaliyotokea katika nchi yetu,
hususani kurejeshwa kwa mfumo wa vyama
vingi vya siasa mwaka 1992, nafasi ya Rais wa
Zanzibar kama Makamu wa Rais iliondolewa.
Baada ya mabadiliko mbalimbali ya kisiasa na
kikatiba (hususan kwa upande wa Zanzibar,
na uzoefu uliopatikana wa namna bora zaidi
ya kuimarisha Muungano wetu), Katiba
Inayopendekezwa inarejesha nafasi ya Rais wa
Zanzibar kama Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano kupitia Ibara ya 99(b).
36
37
38
39