Professional Documents
Culture Documents
Hii ni TANZANIA
Kwanini hali hii? Hali hii mpaka lini?
Barazani
Darasani
9
11
inaendelea
Ukaguzi wa kina ufanywe na Mkaguzi wa Halmashauri ya Manispaa. Viongozi wa Kijiji, Kata na Shule wasihusike kununua vifaa vya ujenzi badala yake watake taarifa na kutoa ushauri. Kamati ya Shule ndiyo ihusike na ununuzi wa vifaa vya ujenzi na kuhakiki ubora wa kazi ya ujenzi.
12
. Inaendelea ..
Kamati ya Shule ya Msingi Mkonoo A ivunjwe na Kamati nyingine iundwe. Uongozi wa Serikali ya Kijiji na Kata uwe karibu sana na Kamati ya Shule kwa kutoa ushauri kuepusha ubadhilifu. Kuwekwe utaratibu wa kutunza vifaa vya ujenzi na taarifa ya matumizi itolewe kila siku.
13
. Inaendelea ..
Ulinzi wa Shule uimarishwe saa zote kuepuka upotevu wa vifaa vya shule. Elimu ya Kujitegemea ifufuliwe shuleni na iwe na usimamizi pia itoe taarifa kwenye mkutano wa wazazi.
14
Taarifa hii ilitolewa kwa Mkutano Mkuu wa Kijiji na kusambazwa kwa:Ofisi ya Serikali ya Kijiji Mkonoo Ofisi ya Kata Terrat Mratibu Elimu Kata Terrat Mh. Mbunge Jimbo la Arusha Mkurugenzi H/Manispaa Arusha Afisa Elimu H/Manispaa Arusha Ofisi ya MKUKUTA Kijiji cha Mkonoo
15
Inaweka misingi ya Maadili ya Viongozi wa umma ikiwa ni pamoja na Kutoa mara kwa mara tamko la mapato, raslimali na madeni ya viongozi wa umma
Katiba ya JMT
Inawataka viongozi wasiwe na tabia ya udanganyifu, upendeleo, ukosefu wa uadilifu au tabia inayochochea rushwa wakati wanapotekeleza shughuli za umma Inawataka viongozi wa umma wawe waaminifu, wawazi, wenye kuutoa haki bila upendeleo, walinde fedha na mali ya umma Inaelekeza viongozi wa umma iwapo hawatekelezi majukumu yao wafukuzwe au kuondolewa madarakani.
Kujenga na kudumisha imani ya wananchi kwa viongozi wao Kuweka utaratibu mzuri wa uwazi na uwajibikaji Kujenga mazingira bora ya kuwavutia wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo Kupunguza migongano kati ya madiwani, watendaji na wananchi Kuweka bayana maadili yanayotegemewa kwa viongozi katika jamii ya watu Kuibua, kukuza na kudumisha demokrasia
Kwa hiyo diwani anawajibika kuzingatia kiwango cha juu kabisa cha maadili yanayojumuisha tabia yake binafsi na mwenendo wa utendaji wa majukumu yake
Diwani anapaswa
Kuendesha shughuli zake kwa namna itakayojenga imani ya wananchi kwa halmashauri yao Kuheshimu na kuzingatia sheria na kuendesha shughuli zake kufuatana na dhamana aliyopewa na wananchi Kuisaidia Halamashauri yake kwa kadri iwezekanavyo kuhakikisha kuwa inatekeleza wajibu wake kwa kuzingatia maslahi ya jamii nzima Kutotumia nafasi yake kama diwani kwa faida yake mwenyewe, familia yake, maslahi ya kifedha ya marafiki zake Kutotoa upendeleo wa aina yoyote wakati wa kutekeleza majukumu yake
Diwani anapaswa..
Kutojiweka katika hali inayowafanya wananchi kutilia shaka uadilifu wake Kuwajibika ipasavyo kwa wananchi walio kwenyewe eneo la halmashauri yake kutokana na maamuzi na matendo yake Kuwa muwazi katika matendo yake na katika kuchangia maoni yake ili kufikia uamuzi wa pamoja na kwamba ataunga mkono maamuzi hayo na kuyatolea maelezo kwa wadau wengine Kufanya maamuzi bila upendeleo na kulingana na stahili ya jambo bila kushawishiwa. Mfano katika masuala ya ajira Kutoshiriki katika majadiliano ama kupigia kura ktk jambo lolote ambalo ana maslahi nalo
Diwani anapaswa
Kuhakikisha kuwa habari/taarifa zote za siri zinazohusu watu zinahifadhiwa kwa mujibu wa sheria na kwa maslahi ya umma na kutozitumia habari hizp kwa maslahi yake binafsi Kutoa taarifa kwenye halmashauri au kamati ya halmashauri kuhusu maslahi yake binafsi katika jambo lolote linalohusu utekelezaji wa majukumu yake Kuheshimu nafasi na hadhi ya madiwani/watumishi wenzake kwa namna inatakayojenga hali ya kuheshimiana kati ya madiwani na watumishi wa halmashauri
Madaraka ya kisiasa
Mali ya halmashauri zilizo chini ya dhamana ya diwani zitumike kwa madhumuni yaliyokusudiwa (23) Uhuru wa kujieleza katika mikutano ya halmashauri na kamati zakke usivunje taratibu za mijadala zilivyofafanuliwa katika Kanuni za Kudumu (24)
Uhusiano baina ya madiwani na watumishi wa halmashauri (Na. 25 28) Maamuzi, maelekezo, amri na miongozo itatolewa katika vikao vya halmashauri na kuelekezwa kwa Mkurugenzi kwa utekelezaji Diwani akiwa peke yake hatatumia nafasi yake kama mjumbe kumzuia mtumishi au wakala wa halmashauri kutekeleza maamuzi ya halmashauri au maamuzi ya kamati ya halmahsuari (25) Madiwani na watumishi wa halmashauri watatakiwa kujenga uhusiano mzuri utakaohakikisha ufanisi na utendaji bora katika halmashauri, na kuepuka uhusiano wa karibu sana na watumishi wa halmashauri unaoweza kuathiri au kudhalilishanupande wa madiwani au upande wa watumishi wa halmashauri (26)
Uhusiano
Madiwani wasijihusisha na majukumu ya kitaaluma na kitaalam yanayohusu uendeshaji wa shughuli za halmashauri (27) Madiwani wasitoe taarifa za uongo au ushauri mbaya kwa halmashauri hasara (kanuni 28) na hatimaye kumfanya diwani awajibishwe kwa kulipa gharama ya hasara iliyopatikana
Utoaji wa taarifa
Diwani haruhusiwi kutoa taarifa za siri anazozipata kutokana na wadhifa wake ambazo hazitakiwi kutolewa kwa muhjibu wa Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 na kwa mujibu wa kanuni zilizotungwa chini ya sheria hiyo (29)