You are on page 1of 45

1.

0 UTANGULIZI:

1.1 Eneo la Utawala


Ndugu Wajumbe,
Jimbo la Singida Kaskazini lipo Mkoa wa Singida na lina ukubwa wa kilometa za mraba 6053. Jimbo
hili lina tarafa Tatu (3) ambazo ni Mgori, Ilongero na Mtinko. Jimbo pia lina kata Ishirini na moja (21)
ambazo ni Mughunga, Mgori,Ngimu, Itaja, Mrama, Ntonge, Kinyeto, Kinyagigi, Merya, Mughamo,
Msange, Maghojoa, Mwasauya, Ikhanoda, Ilongero,Msisi, Ughandi, Makuro, Mdida, Mtinko na
Kijota na lina Vijiji 84.

1.2 Idadi ya Watu


Kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012, Jimbo la Singida Kaskazini
lilikuwa na watu wapatao laki mbili na Ishirini na Tano Elfu mia tano ishirini na moja (225 521), kati
yao wanawake 113 749 na wanaume 111 772. Kwa sasa Jimbo linakadiriwa kuwa Zaidi ya wakazi
261 584 sawa na ongezeko16%.

Shughuli za kiuchumi za wananchiwa Jimbo la Singida Kaskazini ni pamoja na Kilimo, ufugaji,


uchimbaji wa madini, viwanda vidogo vidogo, uvuvi, ujasiriamali na ufugaji wa nyuki.

1.3 Shukrani
Ndugu Wajumbe,
Kwa heshimanataadhimakabla ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama
Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015/16 hadi 2020/21 katikaJimbo la Singida
Kaskazini,Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Mkoa wa Singida.
Ninayo heshima kubwa kuwashukuru viongozi wangu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,
Mkoa, Wilaya, Kata,Matawi na Mashina kwa ushirikiano mkubwa nilioupata katika kutekeleza wajibu
wangu kwa umma wa watanzania hususa ni kwa Wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini. Ninajiona
mwenye furaha sana kuona wamenipa ushirikiano wa kutosha ulioniwezesha kutekeleza Ilani ya
Uchaguzi yaCCM kwa kasi na mafanikio makubwa hasa katika kipindi nilichoingia madarakani Jan
2018 hadi June 2020. Ninawaahidi kuendelea kutekeleza Ilani ya Chama chetu kwa ufanisi
mkubwazaidi kwa manufaa ya wananchi na Taifa letu pendwa la Tanzania.

Ndugu Wajumbe,
Kwa heshima kubwa sana,ninamshukurusana Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, kwa kukubali
kwake kuniruhusu kugombea nafasi ya uwakilishi katika Jimbo letu toka utumishi wa Serikali na kwa
Miradi mingi na mikubwa ya maendeleo tuliyoipata katika kipindi cha miaka miwili na nusu
tunayohitimisha awamu hii ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya tano. Kwakweli nakosa maneno
mazuri ya kuzungumza juu ya Mhe. Rais zaidi ya kusema asante na kumuombea kwa Mwenyezi
Mungu aendelee kumjalia afya njema ili aendelee kuliongoza Taifa letu.
Pia ninawashukuru sanaMhe. Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania pamoja na Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano wao mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yangu
1
kama Mbunge na kwa Ziara za kikazi walizofanya Jimboni kwa nyakati tofauti katika kukagua miradi
ya maendeleo na kutoa maelekezo yaliyotusaidia kufikia mafanikio haya. Kwa niaba ya wananchi wa
Jimbo la Singida Kaskazini, nasema asanteni sana Viongozi wetu kwa moyo wenu wa upendo.

Ndugu Wajumbe,
Wakati wa uchaguzi mdogo ulioniweka madarakani, nilikabidhiwa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015
– 2020 iliyoweka misingi ya utendaji wangu katika kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Singida
Kaskazini na Watanzania. Natoa pongezi nyingi sanakwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Mzee
Mangula, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally Kakurwa na sekreatrieti ya CCM Taifa,
waliokuwa mstari wa mbele katika kukipatia Chama Cha Mapinduzi Ushindi wa Kishindo. Vilevile
ninawashukuruWajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Wajumbe wa
Halmashauri kuu ya CCM Taifakwa Imani yao kwangu na watendaji wengine wote wa Makao Makuu
ya Chama.

Ndugu Wajumbe,
Nawapongeza Viongozi wa CCM Mkoa wa Singida wakiongozwa na Alhaj Juma Hassani Kilimba
Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Ndugu Yohana Msita (MNEC), Ndugu Alexandrina Katabi Katibu wa
CCM wa Mkoa na Wajumbe wote wa Kamati ya Siasa ya Mkoa na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa
wa Singida kwa juhudi kubwa za kukipatia Chama Cha Mapinduzi Ushindi wa kishindo na
kuhakikisha kuwa Ilani ya CCM inatekelezwa kwa kiwango cha juu sana katika ngazi mbali mbali
hususa ni Katika Jimbo letu la Singida Kaskazini, Singida Guntooo.

Ndugu Wajumbe,
Utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimboni usingelikamilika kama kusingekuwa na ushirikiano na
usimamizi wa karibu wa Kamati ya Siasa na Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Singida Vijijini
wakiongozwa na Mzee William Mwang’imba Nyalandu Mwenyekiti wa CCM Wilaya na ndugu Pili
Mbaga, Katibu wa CCM wilaya ya Singida vijijini . Kwa heshima na taadhima ninawashukuru sana
kwa mapenzi makubwa mliyonayo kwa wananchi wa Jimbo letu na kunisaidia kutekeleza vema Ilani
yetu na ahadi mbalimbali tulizotoa wakati na baada ya uchaguzi. Nasema hongereni sana ndugu zangu
wajumbe na Viongozi wengine wote wa Chama katika ngazi za Kata, Matawi na Mashina bila kusahau
WanaCCM wote, kazi tumefanya, Ilani tumetekeleza, Ahadi tumetekeleza kwa ufanisi, Mungu
awabariki sana.

Napenda kuwashukuru Waheshimiwa Madiwani wote wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri


ya Singida DC Mhe. Elia Digha Mlangi na viongozi wote wa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri,
kwa ushirikiano walioonyesha katika kuitekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi (CCM) tangu
nilipoapishwa kushika wadhifa wa Ubunge tarehe 30 Jan 2018 hadi sasa. Ama hakika wahenga
walisema “Umoja ni Nguvu, Utengano ni Udhaifu” kwa umoja wetu, matunda ya utekelezaji
yamejionyesha katika sekta mbalimbali za kimaendeleo katika Jimbo la Singida Kaskazini.

NduguWajumbe,

2
Kwa moyo wa dhati kabisa nipende kuwashukuru viongozi wote wa Dini katika Jimbo la Singida
Kaskazini kwa kuendelea kuliombea Taifa letu, Jimbo letu na mimi mwenyewe pamoja na familia
yangu na watumishi wenzangu katika ofisi ya Mbunge.Dua na maombi yao yametuwezesha kuwa na
ujasiri wa kupambana na changamoto zilizojitokeza katika utendaji wetu. Kwa ujumla kupitia dua na
sala tunaendelea kuwa na afya njema na Amani na kuendelea kulitumikia Taifa letu. Mungu awabariki
sana.

Mwisho lakini si kwa umuhimu, shukrani za kipekee zimwendee Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Singida
Eng. Pascas Muragili, Kamati ya Ulinzi na Usalama, pamoja na watumishi wote na Serikali Kuu kwa
kuhakikisha kuwa Ulizi wa Wananchi na mali zao umekuwepo wakati wote, umoja na utulivu wa
kisiasa uliotuwezesha kutekeleza wajibu wetu kwa umma wa watanzania. Asanteni sana viongozi.

Kwa namna ya kipekee, ninawashukuru sanawananchi wote wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa
kuniamini kupitia kura zao na kunipa ushirikiano katika kutekeleza kazi zangu kama Mbunge bila
kujali itikati walizonazo za kiimani, kisiasa, kimtazamo. Sina cha kuwalipa zaidi ya kuwaahidi kuwa
nitaendelea kuwa mwaminifu kwao na kusimamia shughuli za maendeleo jimboni kwa niaba yao kwa
uadilifu na uaminifu mkubwa, bila kuyumbishwa kwa maslahi mapana ya wananchi na Taifa letu.

Ndugu Wajumbe,
Kwakuwa siyo rahisi kumtaja mmoja mmoja kwenye taarifa hii naomba kuwatambua na kuwashukuru
sana wadauwote na washirikawa maendeleo Jimboni kwetu na kwa uchache niwataje baadhi yao
wakiwemo shirika la HAPA, CIP, SAVING FRIENDS INTERNATIONAL, MAJI TECH, WADA,
WAENDELEE, CWV na wengine wote waliochangia kwa hali na mali ili kupatikana kwa mafanikio
katika Jimbo letu. Nawaomba wadau wote wa maendeleo, tuendelee kushirikiana kwani umoja wetu
ndio nguvu na ushindi wetu.

2.0 MAJUKUMU YA KIBUNGE


Ndugu Wajumbe,
Kama inavyoelezwa kwenye katiba ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 1977 Toleo la mwaka
2012, Sehemu ya Kwanza ibara ya 5 (7) kwamba, “Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima,
Wafanyakazi na Wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea na hasa kila mtu ana haki
ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake”
Kwa mwongozo huu, ifuatayo ni taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha
Mapinduzi kwa kipindi cha Mwaka 2015/16 hadi2020/21.

Taarifa hii imeonesha mafanikio katika utekelezaji wa Ilani ya CCM, ahadi za Viongozi wakuu wa
Serikali na majibu mbalimbali ya kero tulizokabiliana nazo katika masuala ya Uchumi, Miradi ya
maendeleo, Huduma za Jamii na matukio mbalimbali ya kijamii ambayo kwa kiasi kikubwa ofisi ya
Mbunge imeshiriki moja kwa moja ikiwa ni pamoja nautekelezaji wa ahadi za Mbunge na ziara
mbalimbali Jimboni.Aidha, taarifa hii imeonyesha ushiriki wa Vikao na Mikutano ya Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Vikao na Mabaraza ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya

3
Singida kama sehemu muhimu ya majukumu yangu ya uwakilishi. Pia ushiriki wa vikao vyaChama
cha Mapinduzi katika ngazi za Shina, Tawi, Kata, Wilaya, Mkoa na Taifa.

2.1 Vikao vya Bunge la Jamhuri ya Tanzania


Katika kipindi cha miaka miwili na nusu niliyotumikia kama mwakilishi wa Wananchi, niliweza
kuwasilisha maswali 12 Bungeni yaliyotokana na hoja na mahitaji ya Wananchi ambapo maswali 7
ya Msingi na 26 ya nyongeza yalijibiwa. Pianiliweza kuwasilisha hoja 12 katika Wizara kwa
kuzungumza na 8 kwa maandishi. Maoni ya wananchi, utekelezaji wa Ilani ya CCM na ubunifu ndivyo
vilikuwa msingiwa mawasilisho yote na ninawashukuru sana Wananchi wa Jimbo la Singida
Kaskazini kwa ushiriki wao katika kufanikisha haya.

Ndugu Wajumbe,
Baadhi ya maswali na hoja zilizowasilishwa zimekwishazaa matunda mfano katika Sekta ya Afya,
Elimu, Nishati ya Umeme, Miundombinu ya barabara, Kilimo, Mifugo, Maji na Ziara za Viongozi.
Haya nimafanikio machache kati ya mengi yaliyopatikana wakati wa uwakilishi wangu kama
mtakavyoona mbele katika ripoti hii.

2.2 Vikao vya Baraza la Madiwanina Ziara za Kikazi


Katika kutekeleza majukumu yangu kama Mbunge, nimehudhuria vikao vya kamati na mabaraza
katika kipindi nilipokuwepo Jimboni, nimefanyavikaovya ndani na mikutano ya hadhara Jimboni
pamoja na kufanya ziara za kikazi kama Mbunge za ukaguzi wa shughuli za maendeleo. Vile vile
nilipata nafasi ya kukutana na wadau mbalimbali wakiwemo Walimu kuzungumzia masuala ya
ufaulu na elimu kwa ujumla, Viongozi wa Dini katika kushiriki katika shughuli za kimaendeleo,
Wazee na Walemavu katika kujadili masuala yanayowahusu pamoja na changamoto zao.

Ndugu Wajumbe,

4
Tulifanya jumla ya ziara 157 Jimboni ikiwemo mikutano ya hadhara 75naziara 82 za kukagua
miradi ya maendeleo kwa nyakati tofauti. Pia nilishiriki katika kampeni za uchaguzi mdogo wa
Ubunge Jimbo la Liwale katika kutafuta ushindi kwa Chama Cha mapinduzi, Udiwani kata ya
Kitubuka Jimbo la Liwale na Unyambwa Jimbo la Singida Mjini.

3.0 HALI YA KISIASA


Ndugu Wajumbe,
Hali ya kisiasa katika Jimbo la Singida Kaskazini ni shwari pamoja na vuguvugu la uchaguzi Mkuu
wa mwaka 2020 ambapo baadhi ya watia nia wa vyama mbalimbali wameanza kujitokeza kufanya
ushawishi katika maeneo mbalimbali. Hata hivyo, Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho kina-
choongoza Halmashauri ya Wilaya ya Singida na ndicho kinachoendelea kusimamia utekelezaji wa
Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa 2015-2020. Jimbo la Singida Kaskazini lina waheshimiwa Madiwani 29
ambao kati yao21 ni wa kuchaguliwa na 8 niwa viti maalumu na wote ni madiwani kupitia CCM. Ni
Imani yangu tutaendelea kufuata taratibu na kanuni za uchaguzi ili kupata viongozi bora
watakaolisaidia Taifa letu kusonga mbele tukiongozwa na Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

4.0 HALI YA UCHUMI


Sekta ya Fedha na Biashara
Ndugu Wajumbe,
Katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, mkazo mkubwa uliwekwa
katika kuongeza ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa matumizi ili kuziwezesha Halmashauri
kutekeleza miradi ya maendeleo na kutoa ahuduma bora kwa wananchi. Kazi hii ilifanywa na Watendaji
wa Ofisi ya Mkurugenzi chini ya usimamizi mahiri wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
ya Singida kwa mafanikio yafuatayo;
 Makusanyo ya Halmashauri yameongezeka kutoka Tsh 332,395,242 mwaka 2014/15 hadi
1,139,124,463 mwaka 2018/19. Katika bajeti ya 2019/20 Halmashauri imekwishakusanya Tsh
869,751,270 hadi kufikia April 2020
5
 Jumla ya POS 127 zimenunuliwa na kugawiwa vijiji vyote kwa ajili ya makusanyo ya mapato
 Halmashauri imefanikiwa kuondoa hati zenye mashaka kwenye ukaguzi wa CAG kwa miaka
mitatu mfululizo
 Kumekuwa na ongezeko la viwanda kutoka viwanda 28 mwaka 2015 hadi 43 mwaka 2020
 Ongezeko la viwanda vidogo sana, vidogo na vya kati kutoka viwanda 344 hadi 668 mwaka 2020

5.0 SEKTA YA KILIMO NA USHIRIKA (Ibara 21)


Chini ya maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020 katika ibara ya 22,Chama Cha
Mapinduzi kimeilekeza Serikali kutilia mkazo utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Programu ya
Kuendeleza Kilimo (Agricultural Sector Development Programme – ASDP II) pamoja na miradi
ya Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ili kufikia malengo makuu ya kukifanya kilimo
kuwa cha kisasa na cha kibiashara, chenye tija na ambacho mazao yake yatakuwa yameongezewa
thamani.

4.1 Mafunzo ya Kilimo cha Kisasa


Ndugu Wajumbe,
Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetekeleza maelekezo ya Ilani katika ibara hii kwa kuhimiza
kilimo bora cha mazao ya chakula na biashara katika vijiji vyote 84. Kwa kushirikiana na wadau wa
sekta binafsi mfano Shirika la FaidaMali, Taasisi za Kifedha, Litenga Holding Company pamoja na
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini elimu ilitolewa kwa wakulima, kuimarisha
upatikanaji wa pembejeo na zana za kilimo na kuhamasisha kilimo cha umwagiliaji katika ya Alizeti,
Vitunguu, Mtama, Ulezi, Maharage, viazi vitamu na mahindi.Jumla ya wakulima wapatao
17200walipatiwa mafunzo ya kilimo cha kisasayaliyowawezesha wakulima kuongeza tija na ufanisi
kwa kutumia miundombinu iliyopo ikiwa ni pamoja kilimo mseto na kulima zaidi ya mara moja kwa
mwaka.

Halmashauri pia imeandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi ya kilimo na kuendelea kupima
mashamba ya wakulima na kutoa hati za kimila ambazo zinawasaidia wakulima katika dhamana ya
kupata mikopo.

6
4.2 Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo
Ndugu Wajumbe,
Katika kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao kwa wakulima, Halmashauri ya Wilaya ya Singida
imesimamia vyema upatikanaji wa pembejeo, zana za kilimo kwa wakulima zinazotunza mazingira
na uasili wa udongo na zenye tija kwa mkulima. Kwa kipindi cha miaka 5 ya utekelezaji wa Ilani ya
CCM, chini ya uongozi shupavu wa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,tumehimiza matumizi
bora ya pembejeo na hivyo kuwa na ufanisi katika kilimo. Aidha kilimo hifadhi na kilimo mseto pia
vimetumika kupunguza hasara kwa matumizi ya pembejeo za madawa. Vilevile uhamasishaji wa
mbegu bora na zenye kuleta tija yamesisitizwa na wakulima wamehamasika na kuona manufaa ya
kulima eneo dogo lenye uzalishaji mkubwa kwa kutumia kanuni za kilimo bora.

4.3 Uanzishwaji wa Zao la Kimkakati la Korosho


Ndugu Wajumbe,
Kwa kutambua dhima na muelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano ya kufikia Tanzania ya viwanda
na uchumi wa kati, Halmashauri ya Wilaya ya Singida imefanikiwa kuanzisha kilimo cha korosho
kama zao la kimkakati ili kutunza mazingira, kuwa na chanzo cha uhakika wa mapato cha kudumu na
kuzalisha malighafi kwa ajili ya viwanda.

Uanzishwaji wa zao la kimkakatiumefuata taratibu zote za kitaalamu ikiwa ni pamoja na kushirikisha


taasisi ya utafiti wa zao hilo ya Naliendele iliyofanya utafiti na kuthibitisha kuwa kutakuwa na tija ya
kilimo cha zao hilo katika Halmashauri yetu. Hadi sasa tuna wakulima 796 waliolima jumla ya ekari
1800. Aidha, katika kipindi cha kilimo 2018/2020, Halmashauri ilinunua tani 4 za mbegu za korosho
na zilisambazwa kwa wakulima katika kata 10 navijiji 18. Mbegu hizo zimeoteshwa na kupandwa
kwenye ekari 8,500 hadi kufikia msimu wa 2019/20.Lengo ni kuwa na zao la nyongeza la biashara na
la kudumu pia kupanua kilimo hicho adhimu katika ukuaji wa uchumi na kuongeza pato la Taifa.

4.4 Uboreshwaji wa Huduma za Ugani kwa Wakulima


Halmashauri ya Wilaya ya Singida imeendelea kuboresha huduma za ugani kwa wakulima ili ku-
wawezesha kupata elimu, mbinu na teknolojia sahihi za kukuza uzalishaji wao mashambani.
Hadi sasa Halmashauri yetu imekuwa na jumla ya Maofisa ugani 16 navyombo vya usafiri pikipiki8
zinatumiwa na Maofisa ugani katika utoaji wa huduma za ugani vijijini. Aidha, maafisa ugani toka
kwa wadau wetu wa maendeleo nao wameendelea kutoa huduma kwa mazao wanayoyasimamia kama
Alizeti na Pamba

5.0 SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI(Ibara 23)


Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015-2020 inatambua sekta ya mifugona uvuvi kuwa nguzo
muhimu katika uchumi hivyo Chama Cha Mapinduzikimeielekeza Serikali kuendelea kuboresha na
kuhimiza ufugaji wenye tija, wenye kuwaongezea wafugaji na wavuvi kipato pamoja na kuchangia
kwenye Pato la Taifa.
5.1 Sekta ya Mifugo (Ibara 25)

Ndugu Wajumbe,
7
Kwa kutambua umuhimu huo Halmashauri ya Wilaya Singidana wadau wa maendeleo wameendelea
kusimamia na kuboresha ufugaji wa kisasa wenye kuleta tija na usalama wa chakula. Kwa kipindi
hiki cha awamu ya tano inayoongozwa naMhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli,idadi ya mifugo
imeongezekana ubora wa mifugo pia umeongezeka kutokana na wananchi kutumia kanuni bora za
ufugaji na upatikanaji wa malisho. Aidha, wafugaji wengi (98%)wameendelea kufuga mifugo ya asili
inayofugwa kiasili katika eneo la kilomita za mraba 1423.2na wameshaanza kuboresha mifugo hiyo
kwa kutumia madume bora katika kuongeza upatikanaji wa maziwa na nyama bora. Hali ya malisho
ni ya kuridhisha japo changamoto za malisho hasa wakati wa kiangazi, zinaongezeka kutokana na
kupanuka kwa shughuli za kilimo.Tayari hatua kadhaa ikiwemo elimu ya kilimo cha malisho na
ufugaji wa mifugo bora imeanza kutolewa ili kupunguza idadi ya mifugo itakayoendana na eneo la
malisho.

Katika kuhakikisha huduma bora kwa ufugaji, yapo malambo 33 Jimboni, mabwawa 6 na mito 35
ambayo ni vyanzo vya maji kwa mifugo yetu. Aidha, katika jumla ya majosho 25 yakiyopo Jimboni,
majosho 14 yamekwishafanyiwa ukarabati na kutumika na juhudi zinaendelea kukamilisha ukarabati
ili uogeshaji wa mifugo uweze kusimamiwa vizuri. Hata hivyo uogeshaji kwa pampu za mkono
unaendelea kutumika katika maeneo ambayo huduma ya majosho hazijatengamaa.

Ndugu wajumbe,
Pia kupitia maombi yetu serikalini, Serikali imetenga fedha katika mwaka wa fedha 2020/21 kujenga
Kliniki 10 za mifugo ikiwemo katika Halmashauri yetu sambamba na kuelekeza vituo binafsi
vilivyopo kutoa huduma za uchunguzi wa awali kwa magonjwa ya mifugo vikiwemo 3 katika
halamashauri yetu. Hii ni hatua nzuri katika sekta hii ya mifugo ambayo inagusa maisha ya wananchi
wengi na kuongeza kipato katika Halmashauri yetu.

5.2 Sekta ya Uvuvi(Ibara 27)

Kwa kuzingatia ukubwa wa maeneo na wingi wa rasilimali za uvuvi tulizonazo nchini, Chama Cha
Mapinduzi kiliielekeza Serikali kuiendeleza na kuimarisha sekta ya uvuvi.

Ndugu Wajumbe,
Japo Katika Jimbo letu sekta hii sio kubwa sana, Halmashauri ya Wilaya ya Singida kwa kuzingatia
ibara 27, imechukua hatua mbalimbali katika utekelezaji wa Ilani ikiwa ni pamoja na kuimarisha
hifadhi ya mabwawa yetu ya uvuvi, kurejesha na kuongeza mazalia na makulia ya samaki
yaliyoharibiwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa mazingira. Pia uboreshaji wa
maeneo ya uvuvi kwa kutumia teknolojia rafiki ya mazingira kwa kuwavutia samaki na kuzuia uvuvi
haramu katika mabwawa yetu.

8
Aidha tumeshirikiana kurudishia samaki na kupandikiza samaki kwa lengo la kuongeza wingi wa
samaki. Pia tunaendelea na uhamasishaji wa wananchi kujenga mabwawa ya kufugia samaki ili
kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa samaki kwa matumizi ya ndani na kibiashara.

6.0 SEKTA YA HUDUMA ZA JAMII (Ibara 48)


Huduma bora za Jamii kama Afya, Elimu, Maji na nyinginezo ni nyenzo muhimu katika kuondoa
umaskini na kuharakisha maendeleo ya Wananchi. Katika kipindi 2015-2020, Chama Cha Mapinduzi
kimeelekeza Serikali kuendeleza mafanikio yaliyokwishapatikana ili wananchi waendelee kunufaika
na huduma za Jamiii ambazo ni za msingi katika jitihada za kuboresha maisha yao.

6.1 Sekta ya Afya


Ndugu Wajumbe,
Kwa kuzingatia wananchi wenye afya bora ndio wenye uwezo wa kushiriki katika shughuli za kujenga
uchumi, Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetekeleza ibara ya 50 ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM
kwa kuendelea kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Aidha ilani iliweka lengo la kuwa na
Zahanati kwa kila Kijiji na Kata kuwa na kituo cha afya na Ujenzi wa Hospitali za Wilaya kwa maeneo
ambayo huduma hizi hazijakamilika.
Ninayo furaha siku ya leo kuwajulisha kuwa kwa mapenzi makubwa wa Wananchi wetu, ufuatiliaji
makini wa Mbunge wenu Serikalini na wadau wengine wa maendeleo, tumefikia mafanikio
yafuatayo katika sekta hii.

6.1.1 UjenziwaZahanati yaKijiji cha Lambaimekamilika na inatoa huduma

Kijiji cha Ughandi “B” Zahanati imekamilika inasubiri hatua za kuzinduliwa

9
Hatua iliofikia Zahanati ya kijiji cha Mughanga kata ya MtinkoBado ujenzi wa shimo la choo na nyumba zawatumishi.

Kijiji cha Mwachambia Zahanati imekwishaezekwa na ipo katika hatua za umaliziaji

Mbunge ametimiza ahadi ya bati 143 na mbao 25 zenye thamani ya Tsh 4,600,000/= kwa ajili ya kuezekeza Zahanati ya Mwachambia Kata ya
MAGHOJOA.

7.1 Vituo vya Afya (ibara ya 50(a)i).


NduguWajumbe,
Katika kipindi cha kuanzia Feb 2018 nilipoingia madarakani hadi kufikia Juni 2020, Halmashauri ya
Wilaya ya Singida imefanikiwa kuwa na vituo 3 vya afya ambavyo ni Kituo cha afya Ilongero
ambacho kinaendelea kutoa huduma kwa ufanisi mkubwa,kituo cha afya Mgorina kituo cha afya
Msange ambavyo kwa pamoja vimeongezewa majengo yenye jumla ya Tsh 900,000,000 na vinasubiri
vifaa kuweza kutoa huduma za upasuaji pia.

10
Kituo cha afya kipya kinachojengwa katika kata ya Msange.

Pia Serikali inayoongozwa naMhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli ilitupatia fedha Kiasi cha
shilingi Bilioni moja na milioni mia tano(Tsh 1.5 Bil) kwa ajili ya ujenzi wa Hospitalimpya ya Wilaya
iliyojengwa katika kata ya Ilongero sambamba na kuisajili Hospitali ya St Carolos Mtinko kuwa
Hospitali Teule ya Wilaya. Haya ni mafanikio makubwa sana katika historia ya sekta hii ya afya katika
Jimbo letu.

Hivi sasa tumeomba fedha tena ili kuendelea na ujenzi wa vituo vya afya katika kata za Ngimu na
Makuro ambazo nguvu za wananchi zilikwishanyanyua majengo ya OPD na kuhitaji usaidizi wa
Serikali kuyakamilisha. Pia katika hatua mbalimbali, zahanati na vituo vya afya zimekwishaanzishwa
na wananchi katika kutekeleza Ilani ya CCM. Hongera sana wananchi kwa msukumo huu wa
kiamaendeleo ama hakika kama mwakilishi wenu nimefarijika sana.

9.0 SEKTA YA ELIMU (ibara ya 52)


Kwa kutambu kuwa Elimu ya kisasa na yenye mwelekeo wa Sanyansi na teknolojia ina nafasi ya
kipekee katika ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea, ibara ya 52 ya ilani
ilielekeza kuandaa mfumo, muundo na taratibu za kutoa elimu ya Awali, Msingi na Sekondari kidato
cha 4 bila malipo/ada, kuongeza uandikishaji na udahili, kuboresha ufundishaji na ufaulu, kuboresha
uwiano wa vitabu kwa wanafunzi na kuimarisha miundombinu msingi ya kutolea elimu.

Ndugu Wajumbe,
Yafuatayo yamefanyika katika Sekta ya Elimu Jimboni ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM;

9.1 Ujenzi wa Miundombinu kwa Shule za Msingi


 Ujenzi wa madarasa, ofisi za walimu, matundu ya vyoo, nyumba za walimu katika Shule
mbalimbali za msingi kupitia Michango ya Wananchi, Wadau wa maendeleo nafedha za mfuko
wa Jimbo.

Picha ya jengo la Shule ya Msingi Mkenge kabla na baada ya kujengwa jengo lingine
 Ujenzi wa Shule ya Msingi Mwandumo katika Kata ya Mughamo ili kupunguza idadi ya
wanafunzi katika shule ya msingi Ntunduu na kupunguza umbali wa watoto hasa wa madarasa ya
chini kwa nguvu za wananchi, mchango wa Mbunge na fedha za mfuko wa Jimbo. Mhe mbunge
alichangia mifuko 10 ya sarujina nondo vyenye thamani ya Shilingi laki tatu (300,000).
11
4

 Katika shule ya msingi Njiapanda Kata ya Mughamo Mhe. Mbunge amechangia shilingi laki nne
(400,000) kwaajili ya ujenzi katika shule hiyo.
 Kuchangia mifuko miamoja (100) ya saruji yenye thamani ya Shilingi Milinioni moja na laki nane
(1,800,000) katika Shule ya Msingi Gairo Kata ya Itaja kwa ajili ya ujenzi wa Shule hiyo.
 Kuchangia kiasi cha shilingi milioni tano na laki tano (5,500,000) kwa ajili ya ujenzi wa
kukamilisha vyumba vya madarasa katika Shule ya msingi Misuna, Kata ya Ngimu
 Kuchangia saruji mifuko 50 yenye thamani ya laki Tisa (900,000) katika wa ujenzi Shule ya
Msingi Ngaramtoni ili kukamilisha ujenzi wa darasa

 Ujenzi wa Vyumba 5 vya madarasa katika shule ya msingi Ntunduu kupunguza uhaba wa vyumba
vya madarasa
 Ujenzi wa matundu arobaini na sita (46) ya vyoo (matundu 6 yakiwa ya walimu) katika Shule ya
msingi Ntunduu yenye wanafunzi Zaidi ya 1900 waliokuwa wakitumia matundu nane
(8)yaliyokuwepo awali
 Shule ya msingi Ntondo Mh. Mbunge amechangia mifuko ya saruji ishirini (20) yenye thamani ya
Shilingi laki tatu na elfu Sitini (360,000/=)

 Kuchangia mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya kukarabati darasa mojakatika shule ya msingi
Ntunduu

 Ujenzi wa madarasa mawili, matundu ya vyoo sita katika Shule ya Msingi Mtinko ambapo Serikali
Kuu ilitoa kiasi cha Shilingi Milioni Arobaini na sita na laki sita (46, 600,000)

 Kupitia mfuko wa jimbo, Mhe. Mbunge amechangia Shilingi Milioni moja na laki tano (1,500,000)
kwaajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi Malolo Kata ya Mtinko

12
 Serikali Kuu ilitoa jumla ya shilingi Milioni mia moja tatu na laki mbili(103,200,000) kwaajili ya
ujenzi wa madarasa mawili, nyumba mbili za Walimu na matundu 6 ya vyoo katikaShule ya msingi
Mikuyu Kata ya Makuro.Ujenzi umekamilika kwa ongezeko la matundu mawili ya vyoo.
 Ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa kwa nguvu za wananchi, wadau na Mbunge katika
shule ya msingi Mikuyu

 Ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule ya Msingi Mwangae kata ya Kijota Mh. Mbunge
amechangia mifuko ya saruji thelathini (30), yenye thamani ya Shilingi laki tano na elfu arobaini
(540,000) na kuongeza kiasi cha shilingi milioni mbili na nusu (2,500,000) kwaajili ya ujenzi wa
nyumba ya Mwalimu.

 Mhe. Mbunge amechangia shilingi Laki tano (500,000), kwaajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo
shule ya msingi Msisi na shilingi Laki tano (500,000) kwaajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo
katika Shule ya msingi Nduamughanga.

 Kwenye ujenzi wa shule ya awali Sagara, Mh. Mbunge amechangia Shilingi laki mbili (200,000).
 Katika ujenzi wa darasa shule ya msingi Kinyantundu iliyopo Kata ya Mgori Mh. Mbunge,
amechangia tofali elfu moja zenye thamani ya Shilingi milioni moja (1,000,000).

 Ujenzi wa darasa katika Shule ya Sekondari Mdida Mh. Amechangia kiasi cha Shilingi Milioni
mbili na laki tano (2,500,000).

 Katika ujenzi wa Shule yamsingi Mangida Kata ya Msange Mh. Mbunge amechangia mifuko
sitini ya saruji yenye thamani ya Shilingi Milioni moja na laki tatu (1,300,000) kwaajili ya ujenzi
wa madarasa.

 Shule ya msingi Mbuyuni, Mbunge amechangia kiasi cha shilingi milioni moja na laki tano,
(1,500,000) kwaajili ya ujenzi wa madarasa.

 Katika Shule ya msingi Igauri Kata ya Ntonge Mh. Mbunge amechangia bati arobaini (40), yenye
thamani ya Shilingi laki nane (800,000) kwaajili ya ujenzi.

 Mh. Mbunge amechangia mifuko ya saruji ishirini (20) yenye thamani ya Shilingi laki tatu na elfu
stini (360,000), kwenye Shule ya msingi Migugu Kata ya Mdida kwa ajili ya ujenzi.

 Katika Shule ya Msingi Sekotoure kata ya Ilongero Mh. Mbunge, amechangia mabati yenye
thamani ya shilingi milioni 1 kwaajili ya kuezeka darasa.

 Pia katika Shule ya msingi Mwasauya Mbunge Eng Justin Monko amechangia bati 60 zenye
thamani ya Tsh 1,320,000/=kwa ajili ya kupaua madarasa mawili.

13
Mh Mbunge Eng Justin Monko atembelea shule ya Msingi Mwasauya kata ya Mwasauya na kujionea changamoto
mbalimbali pia ameweza kuchangia bati 60 kwa ajili ya ujenzi wa darasa.

9.2 Ujenzi wa Miundombinu kwa Shule za Sekondari

 Kuchangia ujenzi katika Shule ya Seondari Nyeri katika kuboresha miundombinu iliyopo.

Katibu wa Mbunge Maria Daniel Hungii akikabidhi mifuko Hamsini (50) ya saruji katika Shule
ya Sekondari Nyeri kata ya Kinyagigi.

 Kuchangia Mifuko mia moja ya saruji yenye thamani ya Milioni moja nalaki nane (1,800,000)
katika shule ya Sekondari Mwanamwema Shein, Kata ya Mgori,

 Kuchangia Mifuko 50 ya saruji yenye thamani ya Shilingi laki tisa (900,000) katika Shule ya
Sekondari Merya kwaajili ya ukarabati wa darasa.

 Katika Shule ya Sekondari Maghojoa iliyopo Kata ya Maghojoa Mh. Mbunge amechangia
madawati mia moja thelathini yenye thamani ya Milioni saba na laki moja na nusu (7,150,000).

14
 Ujenzi wa madarasa mapya katika Shule ya Sekondari Maghojoa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani
katika sekta ya Elimu

Muonekano wa madarasa manne Shule ya Sekondari Maghojoa.

 Serikali Kuu imetoa jumla ya Shilingi Milioni Mia Moja (100,000,000) kupitia mpango wa P4R
kwaajili ya ujenzi wa bwalo la chakula kwa wanafunzi katika Shule ya Sekondari Mtinko,

 Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili katika Shule ya Sekondari
Mwanamwema Sheiniliyopo Kata ya Mgori ambapo Mhe Mbunge amechangia kiasi cha Tsh.
Milioni mbili na laki sita (2,600,000) kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara

Picha ya jengo la Bweni la Shule ya Sekondari Mwanamwema Shein Kata ya Mgori

9.3 Utengenezaji wa Madawati kwa Shule za Msingi na Sekondari


Pamoja na uwepo wa vyumba vya madarasa, walimu na miundombinu mingine, suala la madawati
lina umuhimu mkubwa katika kuwafanya wanafunzi kuelewa, kuandika vizuri na kulinda usafi wao
binafsi. Katika kulitambua hili, Halmashauri ya Wilaya ya Singida kwa Kushirikiana na Mbunge na
Wadau wengine wamefanya juhudi kubwa katika kutatua changamoto iliyojitokeza hasa baada ya
kuongezeka kwa uandikishaji wa wanafunzi

15
 Mh. Mbunge amechangia madawati mia moja (100), yenye thamani ya milioni tano na laki tano
(5,500,000) katika Shule ya Sekondari Msisi Kata ya Msisi.

Mh, Mbunge akiwa kwenye ziara katika Shule ya Sekondari Msisi Kata ya Msisina kukabidhi Madawati Mia moja.

 Mh. Mbunge amechangia madawati mia moja (80), yenye thamani ya milioni nne na laki nne
(4,400,000) katika Shule ya Sekondari Mughamo Kata ya Mughamo.

Mh. Mbunge amechangia Madawati Themanini (80) katika Shule ya Sekondari Mughamo yenye
thamani ya Milioni Nne na laki Nne (4,400,000).

Mh. Mbunge amekabidhi madawati ishirini yenye thamani ya Shilingi Milioni Mbili (2,000,000/=)
katika Shule ya Msingi Ntunduu

16
Picha ya mwonekano wa darasa Ntunduu s/m kabla na baada ya kupokea madawati 20

Mh. Mbunge amechangia madawati arobaini katika Shule ya Msingi Munkwae Kata ya Kijota yenye
thamani ya Milioni mbili na laki mbili (2,200,000)

Madawati arobaini (40) yaliyokabidhiwa na Mh. Mbunge katika Shule ya Msingi Munkwae Kata ya Kijota.

Uwiano wa Vitabu kwa Wanafunzi kwa Shule ya Msingi (Ibara ya 52f)


Tunaishukuru Serikali kwa kufanikisha ununuzi na usambazaji wa vitabu vya kiada na ziada ambapo
vitabu vimekuwa vikinunuliwa na kugawiwa katika shule zote hapa jimbonin kwetu na Upatikanaji
huu wa vitabu umesaidia kupunguza uwiano wa kitabu kimoja kwa wanafunzi kutoka wastani wa
kitabu 1 kwa wanafunzi 6 mwaka 2015 hadi kitabu 1 kwa wanafunzi 4 kwa mwaka 2018.
Sekta ya Elimu kwa Jimbo la Singida Kaskazini inaendelea kufanya vizuri na kufikia kiwango cha
wastani. Hivyo nikiwa kama Mwakilishi na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu
wakiwemo walimu pamoja na wazazi nina hakikisha sekta hii muhimu ya elimu inafanya vizuri na
kufika kiwango kizuri ikiwa ni pamoja na kutoa motisha kwa walimu pamoja na shule zinazofanya
vizuri katika mitihani.
Ndugu Wajumbe,
Katika kupunguza changamoto ya vitabu ofisi ya Mbunge imechangia vitabu vya shule ya msingi na
Sekondari vyenye thamani ya Tsh Milioni nane (8,000,000)

17
Mhe. Mwenyekiti,
Aidha Serikali chini ya usimamizi mahiri wa Mhe. RaisDkt John Pombe Joseph Magufuli kwa
kutambua umuhimu wa elimu katika Jimbo la Singida Kaskazini imetoa fedha za P4R kiasi cha
Shilingi milion mia Saba na tisa na laki sita (709,600,000)kwa shule 7 ikiwa tatu ni Shule zaMsingi
na Shule nne za Sekondari huku ikiongeza tena fedha kiasi cha Shilingi Milioni mia tatu
(300,000,000/=) kwa ajili ya kumalizia maboma ishirini na nne (24) katika shule za sekondari ambayo
yamejengwa kwa nguvu za wananchi. Aidha Serikali iliongeza shilingi milioni themanini na saba na
laki tano (87,500,000) kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma katika shule za Msingi jimboni

Katika kuhakikisha kiwango cha elimu kinakuwa kwa Jimbo la Singida Kaskazini Serikali kupitia
EQUIP-T limetoa shilingi million ishirini na Tano na Laki mbili (Tsh 25,200,000/=) kwa ajili ya
ukamilishaji wa Madarasa Shule ya Msingi Mitula na milioni sitini (60,000,000) Shule ya msingi ya
Ngaramtonina kazi tayari zimekamilika

Kiwango cha Taaluma


Hali ya taaluma kwa Halmashauri ya Wilaya ya Singida kinakuwa kwa kasi kutokana na kuwa shule
zimeendelea kufanya vizuri kwa walimu kuongeza bidii katika ufundishaji pamoja na kujiwekea
mikakati na mbinu mbali mbali za namna ya kukuza taaluma katika jimbo letu. Mfano Shule ya Msingi
Kinyamwenda mwaka 2018 iliweza kufaulisha wanafunzi kwa wastani wa Daraja la Kwanza na kuwa
ya kwanza kiwilaya na ya Tatu Kimkoa. Haya ni mafanikio makubwa sana na yenye kutia moyo.
Walimu na wawakilishiwa wa wanafunzi walitembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kama sehemu ya motisha kwa walimu na wanafunzi.

6.0 SEKTA YA MAJI(Ibara 54)


6.1 HALI YA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA
Pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika Serikali ya awamu ya nne, Chama Cha Mapinduzi
kimeielekeza Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha huduma ya maji vijijini kwa kuendelea
kutekeleza miradi ya maji vijijini, kujenga vituo vya kuchotea maji na kuhamasisha ujenzi wa
miundombinu ya kuvuna maji ya mvua.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini ikishirikia na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri


ya Wilaya ya Singida na Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira (RUWASA), zimefuatilia
upatikanaji wa fedha za miradi na utekelezaji wa miradi mbalimbali Jimboni. Chini ya program ya
maji, miradi ya bakaa ya mwaka 2017/2018, pamoja na miradi ya Payment by Results (PbR), miradi
ya Payment for Results (PfR)na miradi iliyotekelezwa na wadau wa maendeleo ikiwemo miradi ya
Wafadhili na wadau wa maendeleo utekelezaji wa Ilani katika sekta hii imetekelezwa kama ifuatavyo.

 Mradi wa maji kijiji cha Mtinko na kijiji cha Ngamu. Pia miradi ya ukarabati na upanuzi katika
vijiji vya Minyaa, Nduu, Nduamughanga, Ng’ongoampoku, Msimihi, Ntondo, Semfuru, Kibaoni,
Mikuyu, Merya, Minyenye, Ntunduu, Ughandi ‘B’, Msange, Sagara, Ikhanoda, na Sughana yote
ikiwa ni miradi ya fedha za PbR. Miradi itakayotekelezwa kwa fedha za PfR kwa kuhusisha ujenzi

18
wa Mradi mpya, upanuzi na ukarabati wa miundombinu katika kijiji cha Mughamo, Msisi, Ngimu,
Matumbo, Mgori, Malolo, Kijota, Ghalunyangu na Sefunga-Mangida.

6.2 UTEKELEZAJI MIRADI KWA KIPINDI CHA MWAKA 2017/2020


Ndugu Wajumbe,
 Malengo ya utekelezaji kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 unazingatia bajeti iyotengwa pamoja na
Miradi ya nyuma itakayoendelea kutekelezwa na kukamilishwa kama ilivyokusudiwa pamoja na
uchimbaji wa visima virefu vitano (5) katika vijiji vya Mitula, Mwighanji, Migugu, Misinko na
Ughandi ‘B’.na tayari vimekamilika na vipo kwenye bajeti ya mwaka 2020/2021 kwa ajili ya ujenzi
wa miundombinu ya Maji. Uundaji wa Jumuiya za Watumia Maji ngazi ya Jamii 13 kwa sheria mpya
ya Mwaka 2019 ulifanyika katika kusimamia miradi ya maji.
Hivyo jumla ya wananchi Zaidi ya 171 352sasa wanapata huduma ya maji safi na salama kati ya
Wananchi 264,433 sawa na asilimia 64.8%toka asilimia 52.09 iliokuwepo awali

Aidha, jumla ya kiasi cha Tsh. 1,925,671,387.62 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya
maji Jimbo la Singida Kaskazini kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

6.3 MIRADI YA MAJI KUTOKA KWA WAFADHILI NA WADAU


Kupitia Wafadhili na Wadau wa maendeleo,kuna visima vipya hamsini(50) vilivyochimbwa na
Shirika la Serving Friends International kutoka Wakorea Kusini katika kutatua changamoto ya maji
katika shule za Msingi, Sekondari na zahanati. Jumla ya shilingi 521,314,500 zilitumika kuchimba
visima na kuweka pump za mkono katika Sekondari 14, shule za msingi 31, Zahanati 3 na makanisa
2.

Pia tumefanikiwa kupata mradi mkubwa wa maji kutoka kwa wadau wa maendeleo waitwaoCarlvic
Family unaotekelezwa katika kijiji cha Mvae kata ya Merya unaogharimu takribani Tsh Milioni mia
nne (400,000,000).

19
Mh Mbunge akitembelea mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa katika kijiji cha
Mvae kata ya Merya.

Mh Mbunge akitembelea miradi ya maji katika kata ya Merya mwezi March 2019 kipindi akifanya Ziara katika tarafa za
Mtinko na Ilongero.

Mh Mbunge Eng Justin Monko akitembelea miradi ya Maji katika Kata ya Kinyagigi mwaka 2019

6.3 Nje na miradi ya maji kutoka kwa wadau mbalimbali ifuatayo ni miradi ya maji kutoka Serikalini;
(i) Mradi Mkubwa wa maji unaoendelea katika kijiji cha Ngamu kata ya Mwasauya
utakaogharimu zaidi ya Milioni 400
20
(ii) Mradi Mkubwa wa maji katika kijiji cha Mughamo kata ya Mughamo unagharimu zaidi
ya Milioni 400
(iii) Mradi Mkubwa wa maji unaoendelea katika kijiji cha Mtinko tayari mabomba
yameshasambazwa katika vijiji jirani na vitongoji vya kijiji cha Mtinko.

Mh Mbunge pamoja na viongozi wa kata ya Kinyagigi wakikagua visima vya maji

MWAKA VISIMA VISIMA VISIMA MATANKI YA PAMPU ZA MABWAWA/MA


WA FEDHA VIREFU VYA KATI VIFUPI MAJI YA MVUA UPEPO LAMBO
2015/16 25 53 160 70 1 11
2019/20 34 87 176 79 1 11

8.0 SEKTA YA MICHEZO (ibara 160)

 Kama ilivyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi tumeendelea kuhamasisha shughuli za michezo


kwa watoto, vijana, akinamama na wazee. Kumekuwepo mafanikio kwani timu za michezo
mbalimbali ya mpira wa miguu ziliundwa kuanzia ngazi ya vijiji. Mnamo mwezi September 2019
Mimi Mbunge wenu niliweza kufadhili Ligi ya mpira wa miguu kwa Jimbo zima na kusimamiwa
na chama cha mpira wa Miguu Wilaya ya Singida SIRUFAna kufanikiwa kupata timu 68 kutoka
vijiji 68 vya Jimbo la Singida Kaskazini ambapo vijiji 16 havikuweza kushiriki hivyo kati ya vijiji
84 vilishiriki vijiji 68 tu. Mashindano haya yaligharimu Tsh 8,600,000(MilionNane na laki sita)

MALENGO YA LIGI YA JIMBO.


 Kuwapata mabingwa Mshindi wa I, II, III wa Wilaya 2018/2020.
 Kuchambua wachezaji bora kuunda timu ya Jimbo.
 Kuwaburudisha wana Singida Kaskazini baada ya kukosa mashindano haya kwa misimu mitatu
mfululizo.
 Kuwawezesha Wachezaji wenye vipaji kutambua fursa za ajira.

21
 Kuongeza umoja na mshikamano kwa vijana na Jamii ya Jimbo la Singida Kaskazini.

MAFANIKIO
 Tumefanikiwa kumaliza ligi salama
 Washindi watatu wamepatikana kwenda kucheza ligi daraja la tatu mkoa nazo ni Ngamu United
Kutoka kata ya Mwasauya, Bodaboda FC Kutoka kata ya Ilongero na Ghata FC Kutoka kata ya
Maghojoa.
 Tumefanikiwa kuwaunganisha vijana kutoka kona zote za Wilaya kwa kuruhusu usajili hadi
fainali.
 Tumefanikiwa kufikia malengo kwa 95%.
 Tumefanikiwa kuwafikia vijana1,496 (wachezaji) waliosainishwa form za usajili zenye nembo
Jina la Mdhamini Monko Cup

Ligi 2019/2020
Kwenye vituo 8 vya kucheza mpira kwa hatua ya awali kabla robo fainali Ofisi ya mbunge imechangia
Tsh 5,440,000/= na kwa hatua za mwisho Ofisi ya Mbunge imechangia Tsh 1,450,000.

10.0 SEKTAYA MIUNDO MBINU YA BARABARA NA MAWASILIANO(ibara 38, 39, na 40).

10.1 MIUNDO MBINU YA BARABARA NA MAWASILIANO

Mhe. Mwenyekiti,
Katika kipindi hiki kifupi tumejitahidi kufanya mengi katika sekta mbalimbali ili kuhakikisha
tunanyanyuka kimaendeleo katika sekta nyeti ambazo zinamgusa mwananchi moja kwa moja.

Tumeweza kuendelea kuzihudumia barabara zetu zilizokuwepo tangu awali kwa kufanya
matengenezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na matengenezo ya maeneo korofi na ya kawaida kama
ifuatavyo.

Moja wapo ya mafanikio makubwa tuliyoyapata upande wa barabara ni pamoja na kuzikarabati kwa
kiwango kizuri na kuzifanya kupitika na hivyo kuwarahisishia wananchi usafiri wao na usafirishaji
wa mazao kuelekea sokoni.

 Barabara ya Msisi–Ughandi inatengenezwa hivi sasa mkandarasi yuko kazini


 Barabara ya Mtinko-Makuro imefanyiwa ufuatiliaji na tayari Mkandarasi amesharipoti na muda
wowote anaanza kazi
 Barabara ya Itaja –Ngimu imefanyiwa ukarabati kwa kuwekewa madaraja na Drift
imeshakamilika na imeanza kutumika

22
 Pia Barabara ya Sagara –Gairu -Pohama ambao umetengewa kiasi cha Shilingi Milioni Moja
na Laki Nane (Tsh mill 1,800,000/=)

Aidha katika mwaka wa fedha 2019/20 barabara zifuatazo zilianza kufanyiwa matengenezo na
zinaendelea baada ya mvua kubwa kuisha. Matengenezo haya ni pamoja na barabara ya;

 Barabara kutoka Manispaa - Ilongero itakarabatiwa na kuwekwa kiwango cha Lami (2.7 Km) na
umembuzi yakinifu na usanifu wa kina unafanyika katika Bajeti ya mwaka huu 2019/20.

MATENGENEZO YA MUDA MAALUMU

 Kinyeto-Darajani- Sagara (4 Km)


 Msikii-Songa-Minyaa (3 Km)
 Njiapanda Merya-Merya (3.72 Km)
 Mtinko-Makuro-Diagwa (3 Km)
 Mudida-Kitwanasi (6 Km)
 Mtinko-Senenemfuru (7 Km)
 Mgori-Nduamughanga (3 Km)
 Itaja-Ngimu (5.4 Km)
 Njiapanda-Mgori (6 Km)
 Kinyawahe-Lamba-Ngimu (8 Km)
 Maghojoa-Murigha-Mwachambia (3.5 Km)
 Merya-Ngamu (8 Km)

MATENGENEZO YA KAWAIDA KUTUMIA NGUVU KAZI (Labour Base technology)

 Igauri-Misinko-Minyenye (2.723 Km)


 Ghata-Maghojoa (2.61 km)
 Mgori-Ngimu (3.001 Km)

10.1.1 Mawasiliano (ibara 46)


Mhe. Mwenyekiti,
Pamoja na kuwa bado tatizo la mawasiliano lipo katika baadhi ya maeneo kama vile Kata ya
Mughunga kwa vijiji vya Nduamughanga, Kijiji kivuli Mukulu, Kata ya Itaja katika kijiji kivuli Gairo,
Baadhi ya maeneo Kata za Makuro, Ughandi, Kinyagigi, Mgori na Mpipiti kata ya Mdida Ofisi ya
Mbunge tumeweza kuwasilisha maombi Wizarani ya kujengewa minara ya simu kupitia mpango wa
mawasiliano kwa wote. Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya mtandao wa intaneti tutaendelea
kuongea kushirikiana na mashirika ya simu nchini ili kuongeza mtandao wa intaneti wenye kasi (3G
na 4G) ili kuwawezesha wananchi kupata huduma ya intaneti. Hali ya mawasiliano ya mtandao wa
simu yamefikia zaidi ya asilimia 65 na tutaendelea kuweka minara maeneo ambayo bado kuna
changamoto ya mawasiliano

23
10.1.2 Sekta ya Umeme (ibara 43)
Mhe. Mwenyekiti,
Katika kipindi cha utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi mwaka 2015-2020 Chama cha Mapinduzi
kimeielekeza serikali kuongeza kwa kiwango kikubwa uzalishaji wa nishati ili kuendelea kukuza sekta
hiyo na kuongeza mchango wake kwenye pato la Taifa.

Kutokana na Ilani yetu inavyosema juu ya umuhimu wa kuongeza bajeti ya Wakala wa Usambazaji
wa Umeme Vijijini (REA) tumeendelea kufuatilia usambazaji umeme katika Jimbo letu la Singida
Kaskaziniukizingatia kuwa mwaka 2015 hatukuwa tumewasha umeme kijiji hata kimoja. Hata

hivyo hadi sasa vijiji 58Vimewasha umeme na vijiji 26 viko kwenye mpango wa kufikiwa na huduma
ya umeme.

Mh. Mbunge na Waziri wa Nishati na madini wakizindua umeme katika Kijiji cha Msikii na
Mughamo Tar. 27 Aprili 2020

10.1.2.1 Jedwali lifuatalo linaonesha mchanganuo wa mradi wa umeme wa katika Jimbo letu la
Singida Kaskazini;

11.0 ULINZI NA USALAMA,(Ibara ya 146)


Mhe. Mwenyekiti,
Kwa kutambua kazi kubwa inayofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama katika kudumisha amani,
usalama na utulivu nimekuwa nikishirikiana na vyombo vya usalama katika kutatua baadhi ya

24
VIJIJI JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI
REA III REA III
JINA LA KIJIJI TANESCO REA II BTIP PHASE1 PHASE 2 MAPENDEKEZO
NGAMU √ UMEME UMEWAKA
√ √
MWASAUYA MRADI BADO KUJENGWA
MDILU √ MRADI BADO KUJENGWA
MJUGHUDA √ UMEME UMEWAKA
IKHANODA √ UMEME UMEWAKA
MSIMIHI √ ITAWASHWA KARIBUNI
ILONGERO √ UMEME UMEWAKA
MADAMIGHA √ ITAWASHWA KARIBUNI
SEKOUTURE √ ITAWASHWA KARIBUNI
MWAHANGO √ BADO KUJENGWA
MRAMA √ UMEME UMEWAKA
ITAMKA √ BADO KUJENGWA
MWAKITI √ BADOKUJENGWA
IDD SIMBA √ UMEME UMEWAKA
MAGHANDI √ UMEME UMEWAKA
KINYAGIGI √ BADO KUJENGWA
MITULA √ UMEME UMEWAKA
KIHINADI √ BADO KUJENGWA
MWANYONYE √ BADO KUJENGWA
MAGHOJOA √ UMEME UMEWAKA
MWACHAMBIA √ ITAWASHWA KARIBUNI
MERYA √ UMEME UMEWAKA
KINYAMWAMBO √ UMEME UMEWAKA
MWARUFYU √ BADO KUJENGWA
MVAE √ BADO KUJENGWA
MSANGE √ √ UMEME UMEWAKA
MANGIDA √ UTAWASHWA KARIBUNI
SEFUNGA √ BADO KUJENGWA
ENDESHI √ BADO KUJENGWA
NTONGE √ ITAWASHWA KARIBUNI
IFOMBOU √ UMEME UMEWAKA
IGAURI √ UMEME UMEWAKA
KINYETO √ ITAWASHWA KARIBUNI
NTUNDUU √ ITAWASHWA KARIBUNI
MKIMBII √ ITAWASHWA KARIBUNI
MINYAA √ ITAWASHWA KARIBUNI
MUGHAMO √ UMEME UMEWASHWA
MSIKII √ UMEME UMEWASHWA
UGHANDI √ BADO KUJENGWA
MISINKO √ BADO KUJENGWA
SENENEMFURU HAKUNA MRADI.
UGHANDI B √ BADO KUJENGWA
LAGHANIDA √ BADO KUJENGWA

25
UMEME UMEWAKA NA KUNA
KIJOTA √ √ MRADI MWINGINE
IKIU √ BADO KUJENGWA
MITONTO √ BADO KUJENGWA
NDUU √ BADO KUWASHWA
MDIDA √ UMEME UMEWAKA
MPIPITI √ ITAWASHWA KARIBUNI
KIBAONI √ BADO KUWASHWA
MIGUGU √ BADO KUJENGWA
MAKURO √ BADO KUJENGWA
GHALUNYANGU √ BADO KUJENGWA
MATUMBO √ BADO KUJENGWA
MKENGE √ BADO KUJENGWA
MWALALA √ BADO KUJENGWA
MUGHUNGA √ BADO KUJENGWA
UNYAMPANDA √ BADO KUJENGWA
NDUA MUGHANGA √ BADO KUJENGWA
MKULU HAKUNA MRADI

UMEME UMEWASHWA NA
KUNAMRADI MWINGINE BADO
MTINKO √ KUJENGWA
MALOLO √ BADO KUWASHWA
NDUGHWIRA V BADO KUJENGWA

UMEME UMEWASHWA NA
KUNAMRADI MWINGINE BADO
MSISI √ √ KUJENGWA
MNUNG'UNA √ √ UMEME UMEWASHWA
NTONDO √ UMEME UMEWASHWA
NGIMU √ BADO KUJENGWA
POHAMA √ BADO KUJENGWA
MISUNA HAKINA MRADI
MWIGHANJI √ BADO KUJENGWA
LAMBA √ BADO KUJENGWA
MGORI √ √ BADO KUWASHWA
MNKOLA √ BADO KUJENGWA
SUGHANA √ BADO KUJENGWA
ITAJA √ BADO KUJENGWA
KINYAMWAMBO √ UMEME UMEWASHWA

ITAHITAJI TRANSFORMER UNDER


GAIRO LINE
MIKUYU √ BADO KUJENGWA
MPOKU √ BADO KUJENGWA

26
MINYENYE √ BADO KUJENGWA
MWAKICHENCHE √ BADO KUJENGWA
MUGHANGA √ BADO KUJENGWA
MPAMBAA √ BADO KUWASHWA
changamoto ikiwemo kusaidia katika kukarabati majengo mbalimbali katika sekta hii, April 2019
nimeweza kuchangia mifuko 20 ya saruji katika kukarabati ofisi za Polisi kata ya Mtinko, pia
nimeweza kuchangia bati 60 katika kukamilisha jengo la dawati la jinsia Mkoani Singida.

Niwapongeze viongozi wote ngazi za Vijiji, Kata, Wilaya pamoja na wananchi kwa kushirikiana na
Jeshi la Polisi kupunguza uhalifu katika jimbo letu la Singida Kaskazini na kuongeza amani katika
eneo letu lote.

11.1 HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA


Mhe. Mwenyekiti,
Katika kuendeleza jitihada za kukuza, kulinda na kuhifadhi Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria
katika ngazi zote za uongozi kama inavyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya
145(a),Ushirikishwaji wa jamii unafanyika kupitia Mikutano ya Baraza la Madiwani kwa ngazi ya
Halmashauri, Kamati za Maendeleo za Kata (WDC) na mikutano mikuu ya vijiji ambapo maoni,
mapendekezo na mahitaji ya wananchi husikilizwa na kupelekwa katika ngazi stahiki kwa utekelezaji
kwa kuzingatia miongozo ya uendeshaji wa mikutano hiyo.

12.0 VIWANDA NA FURSA ZA UWEKEZAJI (ibara 83)


Mhe. Mwenyekiti,
Uchumi wa Viwanda una nguvu kubwa ya kuziwezesha sekta zingine za uchumi kuingia katika
mkondo wa uchumi wa kisasa.
Mkazo mkubwa jimboni umewekwa ili kuwezesha uanzishwaji viwanda na kuanzisha uwekezaji
katika jimbo. Viwanda vidogo vidogo vilivyoanzishwa nipamoja na Viwanda vya kukamua mafuta ya
alizeti ambapo jimbo letu la Singida kaskazini tuna Jumla ya viwanda 27 vya kukamua mafuta na
Kongano lililoko kata ya Mtinko ambapo hukusanya mafuta ghafi na kuyasafisha kwa mara ya pili na
kupata mafuta yenye thamani kubwa zaidi, Tuna kiwanda cha kusindika vyakula kilichopo kata ya
Msange ambapo kilijengwa na Shirika la Mirvafu na kiko chini ya usimamizi wa kikundi cha WERU
GROUP, kutengeneza thamani na mashine za kuunganisha vyuma. Mazingira ya kuvutia wawekezaji
yanaendelea; ikiwa ni pamoja na kuleta umeme, maji, kuzalisha mali ghafi pamoja na kuboresha
miundombinu ya barabara.

KUWEZESHA VIJANA KUJIAJIRI.


Mhe. Mwenyekiti,
Chama cha mapinduzi kinatambua umuhimu wa Vijana ambao ni kundi kubwa la nguvu kazi,
changamoto zinazowakabili ni pamoja na kukosa ajira, Elimu na maarifa ya kisasa katika uzalishaji
mali, mitaji ya biashara na ujasiriamali.

27
 Kwa kuzingatia haya Ofisi ya Mbunge imeweza kusaidia vikundi vya Vijana kupata mafunzo
mbalimbali, juu ya namna ya kujiajiri kama vile mafunzo yaliotolewa na wakala wa Barabara za
mijini na vijijini TARURA, Mwezi Aprili hadi Mei 2019 ambapo Mh. Mbunge amemechangia
Mafunzo hayo kwa Shilingi milioni moja (1,000,000) Mafunzo haya yamewezesha vikundi kupata
tenda za kutengeneza barabara za vijijini kama vile, kuchonga sehemu korofi na kujipatia pesa
kama kikundi.
 Pamoja na hayo, Mh Mbunge amechangia katika usajili wa vikundi vya akina mama juu ya
kujiunga na wakala wa Barabara ya mijini na vijijini kwa kata ya Ntonge kwa kutoa Tsh 100,000/=
Kikundi cha akina mama kata ya Mughamo kwa kutoa Tsh 100,000/= na kikundi cha vijana Kata
ya Kijota kijiji cha Ikiu kwa Tsh 100,000/= hii yote ni kusaidia vikundi vya akina mama na vijana
kujikwamua kiuchumi kwa kujipatia vipato vyao kama vikundi na wao binafsi.

 Halmashauri ya Singida pia inasaidia dhima ya kuwezesha vijana kujiajiri kwani imeendelea
kutenga asilimia 4% kwa Vijana, 4% kwa akina Mama na 2% kwa ajili ya Walemavu, ili kuweza
kusaidia hasa Vijana wanaohitimu masomo yao kuweza kujiajiri.

 Halmashauri ya Singida pia imeweza kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo kama vile
Shirika la Mivarfu, Shirika la Faida Mali, Shirika la Action Aid na Litenga Holding juu ya
kuunda vikundi na kuvijengea uwezo juu ya sekta mbalimbali hususani Kilimo, biashara, ufugaji
na ujasiriamali na namna ya kutafuta masoko ya bidhaa wanazozalisha.

 Pia ameweza kuchangia Fedha taslim Shilingi laki nne na nusu (450,000/=), katika kikundi cha
Vijana kiitwacho I can Youth group kwa ajili ya kuongezea kununua Mashine iitwayo Milk
Separator, hiki ni kikundi cha Vijana kutoka sehemu mbalimbali katika Mkoa wa Singida na
wanafanyia shughuli zao Singida Mjini.

Mhe. Mwenyekiti,
Mh Mbunge ameweza kuchangia mashine za kufyatulia tofali katika jumuiya ya Vijana Jimbo la
Singida Kaskazini kama chachu ya kujiletea maendeleo kwa vijana. Mashine hizi zina thamani ya Tsh
800,000/= (Laki inane)

28
Picha za Mashine za kufyatulia tofali zilizotolewa na Mh. Mbunge kwaajili ya kuwawezesha vijana
kujiajiri Jimbo la Singida Kaskazini kwa mwaka 2020.

13.0 KAZI ZA OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI.


Mikutano ya Hadhara

Kutokana na ziara ambazo nimekuwa nikiendelea nazo katika Jimbo letu la Singida Kaskazini katika kip-
indi cha 2018-2020, yaliulizwa maswali yapatayo 602 katika kata zote 21. Maswali hayo yalionesha kero
zilizokuwepo katika sekta mbalimbali hususani katika idara za Elimu, Afya, Maji, Umeme, Ujasiliamali,
Kilimo, Mifugo,Miundombinu ya barabara na mawasiliano.

Matukio ya kijamii

Ilani ya Chama cha Mapinduzi inasisistiza mahusiano mema na jamii inayotuzunguka. Kuwa na
mahusiano mazuri na jamii wakati wote kwenye harakati za kuleta maendeleo kwa makundi yote.

13.1 SHUGHULI ZIFUATAZO ZILIFANYWA NA OFISI YA MBUNGE

Kushiriki harambee na ufadhili katika Chama na taasisi za Serikali na makundi mengine

Ili kuonesha tuko karibu na wananchi wetu tumeshiriki kikamilifu kwa upande wa ujenzi wa Chama chetu
pendwa Chama cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuunga mkono nguvu za wananchi katika kuchangia
shughuli za maendeleo kama ifuatavyo: -

 Nimeweza kuchangia kiasi cha Tsh 1,000,000(Milioni moja) katika ukarabati wa ofisi ya CCM
Mkoa
 Nimeweza kuchangiaTsh 250,000 (laki mbili na hamsini elfu) katika ununuzi wa vifaa vya ofisi
Katika ofisi ya CCM Wilaya ya Singida Vijijini
 Pia nimechangia Tsh 200,000 kwa ajili ya ziara ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya kwa mwezi
September
 Nimechangia Tsh 150,000 kwenye jumuiya ya Wazazi kwa ajili kufanya mkutano
 Nimechangia Tsh 150,000 kwenye Jumuiya ya Vijana kwa ajili ya Ziara
 Sikuishia hapo nimeweza kuchangia Tsh 150,000 kwenye Jumuiya ya UWT
 Pia nimeweza kuchangiaTsh 100,000 Kwa ajili ya Ziara ya Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya
Singida Vijijini mwezi Augost.
 Tarehe 10 November 2018 ilifanyika harambee kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya CCM Wilaya ya
Singida Vijijini ambapo Mh Mbunge nimeweza kuchangia mifuko 120 ya saruji na pesa taslim
1,500,000(Milion moja na laki tano) kwa ajili ya kusaidia katika ufyatuaji wa tofali kazi
itakayofanywa na kambi ya vijana.
 Licha ya kuchangia mifuko 120 ya saruji na pesa Tsh 1,500,000Katibu wake Madam Maria Daniel
aliweza kutafuta wadau wa maendeleo na kuchangia mifuko 90 pamoja nay eye mwenyewe Katibu
alichangia mifuko 30 ya saruji inayoleta jumla ya mifuko 120 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa
Ofisi ya CCM Wilaya ya Singida Vijijini.

29
 Nimeweza pia Kuchangia bati 24 pamoja na pesa kiasi cha Tsh 250,000 kwa ajili ya ujenzi wa
Ofisi ya Chama katika kijiji cha Kinyamwenda kata ya Itaja.
 Ofisi ya Mbunge imeweza kuchangia Tsh 1,170,000(Milioni moja laki moja na Sabini elfu)
ukatika ujenzi wa ofisi ya CCM tawi la Mnunghuna kata ya Msisi.
 Ilipofika Mwezi wa pili mwaka 2019 Ofisi ya Mbunge tuliamua kutenga kiasi cha Tsh 300,000
(Laki tatu) kila Mwezikwa ajili ya matumizi ya kiofisi.

 Mh Mbunge ameweza kuchangia mashine 2 za kufyatulia tofali kwa Jumuiya ya Vijana UVCCM
Wilaya ya Singida Vijijini zenye thamani ya Tsh 800,000/=
 Mh Mbunge ameweza kununua pikipiki namba MC216, CDG kwa ajili ya Jumuiya ya UWT
Wilaya ya Singida Vijijini yenye thamani ya Tsh 2,200,000/=

Picha ya Pikipiki iliyo tolewa na Mh. Mbunge kwaajili ya Jumuiya ya UWT Wilaya ya Singida
Vijijini

 Mh Mbunge ameweza kununua bati 17 kwa ajili ya kuezeka ofisi ya CCM tawi la Mwenge kata
ya Ikhanoda yenye thamani ya Tsh 340,000/=
 Mh Mbunge ameweza kununua baiskeli 1 kwaajili ya walemavu Kata ya Ikhanoda yenye thamani
ya Tsh 300,000/=.
30
Mhe. Mwenyekiti,
Ofisi ya Mbunge inaahidi kuendelea kushiriki kwa ukaribu katika shughuli za Chama pamoja na
kuchangia kupatikana vitendea kazi maana Chama ndicho kilichotupa dhamana ya kuendelea
kutekeleza Ilani ya uchaguzi.

13.2 MICHANGO KATIKA SEKTA ZINGINE ZA MAENDELEO


 Nimeweza kuchangia Tsh Milion moja (1,000,000) ujenzi wa Bweni katika shule yasekondari
Mwanamwema Shein ambayo ipo kwenye hatua nzuri ya ujenzi.
 Nimeweza kuchangia mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika Shule ya Msingi
Mwangae ilioko kata ya Kijota
 Nimeweza kuchangia Tsh 500,000 (Laki tano) kwa ajili ya kuchonga barabara ya Sagara mpaka
Gairo Kata ya Itaja, hii ni kuunga mkono nguvu za wananchi kwa ajili ya kutatua kero ya Barabara
hii ambapo ni kikwazo cha muda mrefu.
 Nimeweza Kuchangia mifuko 20 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika shule ya Msingi
Kinyeto
 Mapema mwaka 2018 nimeweza kuchangia mifuko 10 ya sarufji na nondo zenye gharama ya
Tsh.300, 000/=katika shule mpya ya Mwandumo kijiji cha Mughamo Kata ya Mughamo, shule
hii ni mpya na sasa madarasa mawili yako tayari na ofisi moja hivyo itaanza kufanya kazi muda si
mrefu.
 Nimeweza kuchangia Tsh 400,000 kwa ajili ya ujenzi wa darasa katika Shule ya Msingi Njiapanda
Kijiji cha Mughamo Kata ya Mughamo, hii pia ni shule mpya itakayosaidia vitongoji vya
Njiapanda na Kinyasatu.
 Nimeweza kuchangia mifuko 20 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika shule
ya Msingi Misuna kata ya Ngimu
 Nimeweza kuchangia mifuko 20 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa darasa katika shule ya Msingi
Ntondo ilioko kata ya Msisi.
 Nimeweza kuchangia mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya ukarabati wa darasa katika shule ya msingi
Ntunduu kata ya Kinyeto
(a) Kushiriki harambee na ufadhili katika taasisi za kidini

31
Mhe. Mwenyekiti,
Katika jitihada zilezile za kuitaka jamii ya wana Singida Kaskazini ikae katika misingi ya kiutu na
tabia njema ambavyo ni msingi wa imani, tumechangia katika shughuli mbalimbali zinazoendelea
katika baadhi ya Misikiti iliyopo Jimboni kwetu na Makanisa mbalimbali yaliopo Jimboni kwetu
Michango yote inalenga kuleta maendeleo katika Taasisi hizo ambazo zinatoa huduma za maendeleo
ya kiroho na kimwili kwa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini.

Katibu wa Mbunge Maria Daniel akikabidhi mifuko 50 ya cement kwa kiongozi wa Msikiti, katika Msikiti wa
Ilongero kwa niaba ya Mh Mbunge kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Msikiti Kata ya Ilongero.

(b) Kushiriki katika maafa mbalimbali yanayojitokeza kwa wananchi wetu

Mhe. Mwenyekiti,
Kwa ushirikiano mkubwa tumeshiriki katika matukio mbali mbali ikiwemo kuwafariji wananchi
katika kata zetu hususani katika misiba, athari za mvua kama vile mafuriko yaliotokea Jimboni mwaka
2018 na kuathiri maeneo ya kata za Merya na Kinyagigi.

13.3 MGAWO WA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO2017/2018 - 2019/20


Mhe. Mwenyekiti,
32
Mfuko wa Jimbo umeendelea kuwa kichocheo kwa wananchi kuchangia maendeleo ya Jimbo la
Singida Kaskazini kama iliyokusudiwa. Jumla ya miradi 26 ilifadhiwa na Mfuko wa Jimbo kwenye
kata zote 21 na kiasi cha jumla ya Tsh 59,100,000 kimetumika kwa ajili ya utekelezaji miradi ya ujenzi
wa madarasa, zahanati, ununuzi wa vitanda shule za bweni, nyumba za watumishi na ujenzi wa vyoo
mashuleni.

14.0 TAARIFA YA MATUMIZI MGAWANYO WA MFUKO WA JIMBO KWA KIPINDICHA


MWAKA 2018/2020. (HALMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA)

Mchanganuowa matumizi ya fedha Tshs. 59,100,000/= ni kama ifuatavyo:

Na Jina la mradi Fedha


zilizotolewa
1 Ukamilishaji wa jengo la Zahanati Zahanati ya kijiji cha Unyampanda Kata 2,600,000.00
ya Mughunga
2 Ukamilishaji wa Ujenzi Shule ya Sekondari Mwanamwema Kata ya Mgori 2,600,000.00
3 Ununuzi wa Tofali 1000 Shule ya Msingi Kinyatundu Kata ya Mgori 1,400,000.00
4 Ukamilishaji wa Ujenzi wa madarasa mawili Shule ya Msingi Misuna Kata 2,500,000.00
ya Ngimu
5 Ununuzi wa mifuko 100 ya saruji Shule ya Msingi Gairu Kata ya Itaja 1,700,000.00
6 Kufungua Barabara kata ya Itaja 1,800,000.00
7 Ujenzi wa Madarasa 3 Shule ya Msingi Malolo kata ya Mtinko 2,000,000.00
8 Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Shule ya Msingi Mwangae kata ya Kijota 2,500,000.00
9 Ujenzi wa Ofisi ya Kijiji cha Laghanida kata ya Ughandi 1,500,000.00
10 Ununuzi wa Solar Zahanati ya Misinko kata ya Ughandi 2,000,000.00
11 Ununuzi wa Vitanda Shule ya Sekondari Ughandi Kata ya Ughandi 1,000,000.00
12 Ujenzi wa Darasa shule shikizi ya Mwangindi kata ya Msisi 1,500,000.00
13 Ukamilishaji wa Madarasa 2 Shule ya Msingi Mkenge kata ya Makuro 2,500,000.00
14 Ununuzi wa Saruji Sekondari ya Mudida kata ya Mudida 2,500,000.00
15 Ujenzi wa Ofisi ya Walimu Shule ya Sekondari Ntonge kata ya Ntonge 2,500,000.00
16 Ujenzi wa Vyoo vya Wanafunzi wa Elimu Maalumu Shule ya Msingi 2,000,000.00
Ilongero kata ya Ilongero
17 Ujenzi wa matundu 16 ya vyoo Shule ya Msingi Mrama kata ya Mrama 2,500,000.00
18 Ukamilishaji wa ujenzi wa Shule Mpya ya Mwandumu kata ya Mughamo 2,000,000.00
19 Ukamilishaji wa Nyumba ya Mwalimu shule ya Msingi Msikii kata ya 2,000,000.00
Mughamo
20 Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Shule ya Sekondari Ikhanoda kata ya 2,500,000.00
Ikhanoda
21 Ujenzi wa madarasa mawili shule ya Msingi Mkimbii 2,500,000.00
22 Ununuzi wa Saruji kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba ya mwalimu shule ya 2,500,000.00
sekondari Nyeri kata ya Kinyagigi

33
23 Ujenzi wa Nyumba za Walimu Shule ya Msingi Kinyamwambo kata ya 3,500,000.00
Merya
24 Ujenzi wa Zahanati ya Mwachambia kata ya Maghojoa 4,000,000.00
25 Ukamilishaji wa Madarasa 2 Shule ya Msingi Sokoine kata ya Mwasauya 2,500,000.00
26 Ununuzi wa madawati 55 shule ya sekondari Madasenga 2,500,000.00
Jumla kuu 59,100,000.00

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO 2019/2020

Matumizi
Idhinishwa Tolewa Tumika Baki Chanzo
Utekelezaji hadi
NA JINA LA MRADI % cha Maoni
301, Desemba 61,138,640 156,3
61,295,000. 61,295,000.00 fedha
60.00
- - - -
Kuwezesha Vyumba 3 vya Upauaji
ukamilishaji wa Maabara 10,000,000.0 umekami
1. 87 0 10,000,000.0 0 CDCF
Maabara sekondari vimepauliwa 0 lika
ya Mrama
Kuwezesha ujenzi Kazi
wa choo cha Ujenzi upo hatua ya inaendele
2. 60 5,000,000.00 5,000,000.00 0 CDCF
Wanafunzi – Itaja lenta 0 a
Sekondari
Kuwezesha Kutenegeneza na Kazi
Ukamilishaji wa kuweka grill 11 za imekamil
Maabara sekondari madirisha, kufunga ika
ya Ntonge madirisha 5 ya
3. Alumium, kuweka 100 0 4,000,000.00 4,000,000.00 0 CDCF
sakafu vyumba 2
pamoja na
utenegenezaji wa
milango 5.
Kuwezesha upauaji Upauaji
Ununuzi wa mabati
wa Madarasa 2, umefanyi
4. na sementi 95 0 7,000,000.00 7,000,000.00 0 CDCF
Shule ya msingi ka
umefanyika
Mwandumo
5. Kuwezesha upauaji Madaras
Ununuzi wa bati
wa madarasa 2 a
vipabde 22, Mifuko
shule ya msingi yameeze
50 ya Sementi,
Misuna na
utengenezaji wa 86 0 4,000,000.00 4,000,000.00 0 CDCF
upigaji
Madirisha 10
wa plasta
pamoja na vioo
umekami
umefanyika
lika
6. Ukamilishaji Ukamilishaji Hatua ya
nyumba ya umefanyika umaliziaj
mwalimu na i
upauaji wa
85 0 7,000,000.00 7,000,000.00 0 CDCF
madarasa 2 shule ya
msingi
Kinyamambo –
Merya

34
Kuwezesha upauaji Madarasa 2 Kazi
wa madarasa 2 yamepuliwa imekamil
7. 100 0 3,700,000.00 3,700,000.00 0 CDCF
shule ya msingi ika
Mwasauya
Kuwezesha upauaji Ununuzi wa bati Kazi ya
wa Madarasa shule pamoja na upauaji
8. 100 0 5,000,000.00 5,000,000.00 0 CDCF
ya msingi Mkimbii misumari imekamil
– Kinyeto umefanyika ika
Kuwezesha ujenzi Nyumba ya choo Ukamilis
wa choo zahanati imejengwa na haji
9 ya Ughandi kuezekwa pamoja 95 0 4,000,000.00 4,000,000.00 0 CDCF unaendel
na kujengelea a
shimo la choo
Kuwezesha Kazi
ukamilishaji wa Ununuzi wa imekamil
10 ofisi ya kijiji cha milango ya grill 8 100 0 1,000,000.00 1,000,000.00 0 CDCF ika
Laghanida – umefanyika
Ughandi
Kuwezeshaja Nyumba
ukamilishaji wa
umaliziaji wa imepauli
nyumba ya
11 nyumba ya 97 0 3,000,000.00 3,000,000 0 CDCF wa
mwalimu umefikia
mwalimu shule ya
hatua ya upauaji
sekondari Mudida
12. Kuwezesha ununuzi Ununuzi
wa Mabati 40 shule wa
Mabati 40
ya msingi 100 0 1,250,000.00 1,250,000.00 00 CDCF mabati
yamenunuliwa
Sekouture umefanyi
ka
13. Kuwezesha ununuzi 0 Ununuzi
wa Mabati 40 shule wa
Mabati 40
ya msingi Igauri 100 0 1,250,000.00 1,250,000.00 CDCF mabati
yamenunuliwa
umefanyi
ka
14. Kuwezesha ununuzi 0 Ununuzi
wa Madawati 40, wa
Mabati 40
S/M Munkwae 100 0 2,000,000.00 2,000,000.00 CDCF mabati
yamenunuliwa
umefanyi
ka
15 Ununuzi wa Ununuzi
sementi mifuko 180 umefanyi
@16,000 kwa ajili Sementi ka
ya shule ya msingi imenunuliwa na
100 0 2,880,000.00 2,880,000.00 0 CDCF
(Ngalamtoni 70, kupelekwa shule
Endesh 30, husika
madamigha50 na
Migugu 30)
16 Kupakia na
Usafirishaji
kushusha mifuko ya 100 0 58,640.00 58,640.00 0
umefanyika
sementi 180
Jumla 0 61,138,640 61,138,640 0

35
15.0 AHADI ZA MBUNGE WA JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI.

MH. ENG JUSTIN MONKO 2018-2020

S/N AHADI IMETIMIZWA KWA ASILIMIA FEDHA MAELEZO


ALIZOTOA

1. AHADI YA KUWEKA UMEME 01 APRIL 2018 TSH 500,000/= 500,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA OFISI YA CCM KATA KWA AJILI YA KUNUNUA
YA MSANGE VIFAA VYA UMEME OFISI YA
CCM KATA YA MSANGE
ZILIKABIDHIWA
2. TAREHE 20 FEB 2018 AHADI 15 APRIL 2018 AHADI YA 300,000 FEDHA BINAFSI
YA MIFUKO 10 YA SARUJI NA MIFUKO 10 YA SARUJI NA
NONDO ZENYE THAMANI YA NONDO ZENYEWE THAMANI
TSH 300,000/= KATIKA SHULE YA 300,000/= ILITEKELEZWA
YA MSINGI MWANDUMO
KATA YA MUGHAMO
3. 10 MARCH 2018 AHADI YA 16 APRIL 2018, 400,000 FEDHA BINAFSI
TSH 400,000 KWA AJILI YA AHADI YA TSH 400,000 KWA
KUCHANGIA UJENZI WA AJILI YA KUCHANGIA UJENZI
DARASA KATIKA SHULE YA WA DARASA KATIKA SHULE
MSINGI NJIAPANDA KATA YA MSINGI NJIAPANDA
YA MUGHAMO ILITEKELEZWA
4. AHADI YA 450,000 KATIKA AHADI IMETIMIZWA TAREHE 21 450,000 FEDHA BINAFSI
KIKUNDI CHA VIJANA I CAN APRIL 2018, FEDHA TASLIM
YOUTH GROUP SINGIDA 450,000 ILIKABIDHIWA KWA
MJINI VIONGOZI WA KIKUNDI
5. AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA, MIFUKO 360,000 FEDHA BINAFSI
MIFUKO 20 YA SARUJI KWA 20 ILIKABIDHIWA KWA MKUU
AJILI YA UJENZI WA DARASA WA SHULE PAMOJA NA MH
KATIKA SHULE YA MSINGI DIWANI KATA YA MSISI
NTONDO KATA YA MSISI
6. AHADI YA TSH MILION MOJA AHADI ILITEKELEZWA, 1,000,000 FEDHA BINAFSI
(1,000,000) KATIKA KANISA TSH 1,000,000/= KWA AJILI YA
KATOLIKI KATA YA MTINKO KUCHANGIA UNUNUZI WA
GARI LA KANISA
7. AHADI YA TSH 500,000 KWA AHADI IMETEKELEZWA, TSH 500,000 FEDHA BINAFSI
CHAMA CHA UIMBAJI WA 500,000 IMEKABIDHIWA KWA
NYIMBO ZA INJILI MWENYEKITI NA KATIBU WA
WILAYA(CHAMWITA) CHAMWITA KATIKA TAMASHA
LA UIMBAJI LILILOFANYIKA
KATA YA MSANGE
8. AHADI YA MILION MOJA AHADI YA KUCHANGIA KIASI 1,000,000 FEDHA BINAFSI
(1,000,000) KATIKA CHA TSH 1,000,000 (MILION
UKARABATI WA OFISI YA MOJA) KATIKA UKARABATI WA
CCM MKOA
36
OFISI YA CCM MKOA
IMETEKELEZWA
9. AHADI YA KUNUNUA VIFAA AHADI IMETIMIZWA KUPITIA 250,000 FEDHA BINAFSI
VYA STATIONARY KATIKA KATIBU WA CCM WILAYA
OFISI YA CCM WILAYA YA NDUGU GRACE SHINDIKA KWA
SINGIDA VIJIJINI TSH KUKABIDHIWA TSH 250,000/=
250,000/=
10. AHADI YA KUCHANGIA TSH AHADI IMETIMIZWA KWA 200,000 FEDHA BINAFSI
200,000 KATIKA ZIARA YA MWENYEKITI WA CCM WILAYA
MWENYEKITI WA CCM KUKABIDHIWA TSH 200,000/=
WILAYA
11. AHADI YA KUCHANGIA TSH AHADI IMETIMIZWA KWA 150,000 FEDHA BINAFSI
150,000 KATIKA JUMUIYA YA KATIBU JUMUIYA YA WAZAZI
WAZAZI KWA AJILI YA KUKABIDHIWA TSH 150,000/=
ZIARA MWEZI JULY 2018
12. AHADI YA TSH 150,000 AHADI IMETIMIZWA KWA 150,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA JUMUIYA YA UWT KATIBU WA UWT
KWA AJILI YA ZIARA MWEZI KUKABIDHIWA 150,000/=
JULY 2018
13. AHADI YA TSH 150,000 AHADI IMETIMIZWA AHADI 150,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA JUMUIYA YA IMETIMIZWA KWA KATIBU WA
VIJANA KWA AJILI YA ZIARA VIJANA KUKABIDHIWA TSH
MWEZI JULY 2018 150,000/=
14. AHADI YA KUCHANGIA TSH AHADI IMETIMIZWA KWA 100,000 FEDHA BINAFSI
100,000 KWA MWENEZI WA MWENEZI KUKABIDHIWA TSH
CCM WILAYA YA SINGIDA 100,000 /= KWA AJILI YA ZIARA
VIJIJINI KWA AJILI YA ZIARA
MWEZI AUGOST 2018
15 AHADI YA KUCHEZESHA AHADI IMETIMIZWA KWA 8,600,000 FEDHA BINAFSI
LIGI YA MPIRA WA MIGUU KUCHEZESHA LIGI YA MPIRA
KATIKA JIMBO LA SINGIDA WA MIGUU KATIKA JIMBO LA
KASKAZINI 2018/19 SINGIDA KASKAZINI KWA
GHARAMA YA TSH 8,600,000/=
16 AHADI YA MIFUKO 30 YA AHADI IMETIMIZWA KWA 600,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI KATIKA SHULE YA MKUU WA SHULE YA MSINGI
MSINGI MWANGAE KATA YA MWANAGAE KUKABIDHIWA
KIJOTA KWA AJILI YA MIFUKO 30 YA SARUJI
UJENZI WA MATUNDU YA
VYOO
17. AHADI YA MIFUKO 10 YA AHADI IMETIMIZWA 200,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI KWA AJILI YA
KUKARABATI DARASA
KATIKA SHULE YA MSINGI
NTUNDUU KATA YA
KINYETO
18 AHADI YA MIFUKO 120 YA AHADI IMETIMIZWA KWA 1,500,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI NA TSH 1,500,000/= KATIBU WA CCM WILAYA
KWA AJILI YA UJENZI WA KUPOKEA MIFUKO 120 YA
OFISI YA CCM WILAYA SARUJI PAMOJA NA TSH
TAREHE 10 NOVEMBER 2018 1,500,000/=
19 AHADI YA KUNUNUA AHADI IMETIMIZWA, PIKIPIKI 2,200,000 FEDHA BINAFSI
PIKIPIKI KATIKA JUMUIYA IMENUNULIWA KWA TSH
YA UWT WILAYA YA 2,200,000 /= NA KUKABIDHIWA
SINGIDA VIJIJINI NA MWENYEKITI WA CCM
MKOA MH JUMA KILIMBA
TAREHE 8 .03.2020

37
20 AHADI YA TSH 300,000/= NA AHADI IMETIMIZWA KWA 300,000 FEDHA BINAFSI
MIFUKO 10 YA SARUJI MKUU WA SHULE
KATIKA SHULE YA KUKABIDHIWA TSH 300,000/=
SEKONDARI MAKURO KATA NA MIFUKO 10 YA SARUJI,
YA MAKURO KWA AJILI YA TAREHE 11 FEB 2020
KUCHANGIA UJENZI WA
VYOO
21. AHADI YA TSH 550,000 550,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA MSIKITI WA AHADI IMETIMIZWA TAREHE 20
BAKWATA KATA YA MERYA JULY 2019
KWA AJILI YA KUCHANGIA
UJENZI WA MSIKITI
22 AHADI YA 200,000/= KATIKA AHADI IMETIMIZWA TAREHE 200,000 FEDHA BINAFSI
SHULE YA AWALI SAGARA 11 DEC.2019
23 AHADI YA TSH 1,000,000/= AHADI IMETIMIZWA 1,000,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA KANISA LA K.L.P.A
KATAYA ITAJA KWA AJILI
YA KUNUNUA VYOMBO VYA
MZIKI
24 AHADI YA 150,000/= KATIKA AHADI IMETIMIZWA 150,000 FEDHA BINAFSI
OFISI YA CCM TAWI LA
MGORI KATA YA MGORI
25. AHADI YA KUNUNUA BATI BATI 24 ZIMEPELEKWA 480,000 FEDHA BINAFSI
24 KWA AJILI YA KUMALIZIA
UJENZI WA OFISI YA CCM
TAWI LA KINYAMWENDA NA
PESA TSH 250,000
26 AHADI YA KUPELEKA TRIP AHADI IMETIMIZWA 600,000 FEDHA BINAFSI
15 ZA MCHANGA ZENYE
JUMLA YA GHARAMA YA
TSH 600,000/=
HOSPITAL YA WILAYA
ILONGERO
27 AHADI YA TSH MILION MOJA AHADI IMETIMIZWA 1,000,000 FEDHA BINAFSI
(1,000,000) KWA AJILI YA
KUCHANGIA KATIKA
MAFUNZO YA VIKUNDI
YALIOANDALIWA NA
TARURA JUU YA
UTENGENEZAJI WA
BARABARA
28. AHADI YA TSH 500,000 AHADI IMETIMIZWA 500,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA MAULIDI YA
WAISLAM KATIKA MSIKITI
WA BAKWATA KATA YA
MRAMA
29. AHADI YA KUCHIMBA AHADI IMETEKELEZWA NA 25,000,000 WAFADHILI
KISIMA KATIKA KIJIJI CHA MAJI YAMESAMBZWA (Wafadhili) KUTOKA
NDUAMUGHAGA KATA YA KWENYE TAASISI ZA MAREKANI
MUGHUNGA KISERIKALI NA WANANCHI WA
KIJIJI CHA NDUAMUGHANGA
WANAPATA MAJI SAFI NA
SALAMA
30 AHADI YA TOFALI 1000 AHADI IMETIMIZWA NA 1,000,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA SHULE YA MSINGI DARASA LIMESHAJENGWA
KINYANTUNDU ILIOKO WANAFUNZI WANASOMA
KATA YA MGORI KWA AJILI
38
YA KUCHANGIA UJENZI WA JUMLA YA GHARAMA NI TSH.
DARASA 1,000,000/=
31. AHADI YA TSH 1,500,000 /= AHADI IMETIMIZWA 1,500,000 FEDHA BINAFSI
KWA AJILI YA KUSAIDIA
KUCHONGA BARABARA YA
SAGARA KWENDA GAIRO
KATA YA ITAJA
32. AHADI YA TSH 1,680,000 AHADI IMETIMIZWA 1,680,000 FEDHA BINAFSI
MABATI 60 KWA AJILI YA
UJENZI WA DARASA KATIKA
SHULE YA MSINGI
MWASAUYA
33. AHADI YA MIFUKO 30 YA AHADI IMETIMIZWA 600,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI KATIKA SHULE YA
MSINGI SEKETOURE KATA
YA ILONGERO
34 AHADI YA MIFUKO 20 YA AHADI IMETIMIZWA 400,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI KATIKA SHULE YA
MSINGI MIGUGU KATA YA
MDIDA
35. AHADI YA MADAWATI 80 AHADI IMETIMIZWA 4,200,000 FEDHA BINAFSI
YENYE THAMANI YA TSH
4,200,000/=KATIKA SHULE YA
SEKONDARI MUGHAMO
KATA YA MUGHAMO
36 AHADI YA MADAWATI 100 AHADI IMETIMIZWA 5,500,000 FEDHA BINAFSI
YENYE THAMANI YA TSH
5,500,000/= KATIKA SHULE
YA SEKONDARI MSISI KATA
YA MSISI
37 AHADI YA KUTOA TSH AHADI INAENDELEA 300,000 FEDHA BINAFSI
300,000 /= KILA MWEZI KWA KUTIMIZWA
AJILI YA MATUMIZI YA OFISI
YA CCM WLAYA YA SINGIDA
VIJIJINI TANGU FEB. 2019
HADI SASA
38 AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA 1,000,000 FEDHA BINAFSI
MAFUTA YA GARI KWA AJILI
YA SHUGHULI ZA
UFUATILIAJI SHUGHULI ZA
UCHAGUZI WA SERIKALI ZA
MITAA 2019 TSH 1,000,000/=
39 AHADI YA KUPELEKA MAWE BADO
KATIKA SHULE YA MSINGI HAIJATEKELEZ
MKIMBII WA
40 AHADI YA MIFUKO 20 YA AHADI IMETEKELEZWA 400,000 FEDHA BINAFSI
SARUJI KATIKA SHULE YA
MSINGI KINYETO KWA AJILI
YA UJENZI WA MATUNDU
YA VYOO
41 AHADI YA KUCHIMBA AHADI IMETIMIZWA NA 15,000,000 MAJI
KISIMA KATIKA SHULE YA MGOGORO UMETATULIWA YAMECHIMBWA
MSINGI KIHUNADI KATA YA NA WAFADHILI
KINYAGIGI NA KUTOKA KOREA
KUSHUGHULIKIA
MIGOGORO YA MIPAKA
KATIKA SHULE HIYO
39
42 AHADI YA KUTATUA AHADI IMETIMIZWA KWA JUMLA YA WAFADHILI
CHANGAMOTO YA MAJI KUTAFUTA WAHISANI KUTOKA VISIMA VIPYA
MASHULENI NA KATIKA MAREKANI NA KOREA KWA MASHULENI,
VIJIJI VILIVYOKUWA NA AJILI YA UCHIMBAJI MAJI ZAHANATI
SHIDA KUBWA YA MAJI MASHULE NA ZAHANATI VITUO VYA
JIMBONI AFYA NA
VIJIJINI
43. AHADI YA VITI 40 KATIKA AHADI ZIMETIMIZWA TAREHE 350,000 FEDHA BINAFSI
OFISI ZA CCM KATA YA 08 MARCH 2020 KWA
MSISI NA KATA YA MSANGE KUKABIDHIWA NA
MWENYEKITI WA CCM MKOA
MH JUMA KILIMBA
44 AHADI YA MABATI 17 AHADI IMETIMIZWA TAREHE 08 425,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA OFISI YA CCM TAWI MARCH 2020 KWA
LA MWENGE KATA YA KUKABIDHIWA NA
IKHANODA MWENYEKITI WA CCM MKOA
MH JUMA KILIMBA
45 AHADI YA KULIPIA USAJILI AHADI IMETIMIZWA 400,000 FEDHA BINAFSI
WA VIKUNDI VYA TARURA
KATA YA KIJOTA TSH
200,000/-, KATA YA NTONGE
100,000 NA KATA YA
MUGHAMO TSH 100,000
46 AHADI YA KUJENGA OFISI AHADI IMETIMIZWA KWA OFISI 2,300,000 FEDHA BINAFSI
YA CCM TAWI LA YA MBUNGE KUCHANGIA TSH
MNUNUGHUNA KATA YA 2,300,000/=
MSISI
47 AHADI YA KUTATUA AHADI IMETIMIZWA KWA 7,150,000 FEDHA BINAFSI
CHANGAMOTO KUBWA YA ASILIMIA 100 AMBAPO, OFISI NI TSH 2,000,000
UKOSEFU WA MADAWATI YA MBUNGE KWA NA 5,150,000/=
NA KUSABABISHA ZAIDI YA KUSHIRIKIANA NA WADAU WA IMECHANGIWA
WANAFUNZI 120 KUKAA MAENDELEO WAMEWEZA NA WADAU WA
CHINI KATIKA SHULE YA KUKABIDHI DAWATI 130 MAENDELEO
SEKONDARI MAGHOJOA ZENYE THAMANI YA TSH KWA
KATA YA MAGHOJOA 7,150,000/= KUHAMASISHWA
NA MH MBUNGE
48 AHADI YA KUCHEZESHA TSH. 4,000,000/= 4,000,000 FEDHA BINAFSI
LIGI YA MPIRA WA MIGUU IMESHATOLEWA NA LIGI
JIMBONI KWA MWAKA 2019 INAENDELEA KUCHEZWA
NGAZI YA KATA
49 AHADI YA KUCHANGIA BATI AHADI IMETIMIZWA NA 4,600,000 FEDHA BINAFSI
140 NA MBA0 25 KWA AJILI ZAHANATI IMESHAEZEKWA
YA KUEZEKA ZAHANATI YA TAYARI, GHARAMA YA BATI
MWACHAMBIA ILIOKO KATA NA MBAO NI TSH 4,600,000/=
YA MAGHOJOA
50 AHADI YA MIFUKO 30 AHADI IMETIMIZWA 600,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA SHULE YA MSINGI
MVAE
51 AHADI YA BATI 40 KATIKA AHADI IMETIMIZWA 1,000,000 FEDHA BINAFSI
SHULE YA MSINGI
MAGHOJOA
52 AHADI YA BATI 50 KATIKA AHADI IMETIMIZWA 1,250,000 FEDHA BINAFSI
MSIKITI WA UGHANDI KATA
YA UGHANDI
53. AHADI YA ZULIA KATIKA AHADI IMETIMIZWA 200,000 FEDHA BINAFSI
MSIKITI KATA YA UGHANDI

40
54. AHADI YA BATI 100 KWA AHADI IMETIMIZWA KWA 3,500,000 FEDHA BINAFSI
AJILI YA KUEZEKA OFISI YA KUKABIDHI BATI 100 ZENYE
CCM WILAYA YA SINGIDA THAMANI YA TSH 35,000,000
VIJIJINI
55. AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA KWA 8,000,000 FEDHA BINAFSI
VITABU MASHULE KUCHANGIA VITABU KWA
SHULE 8 ZA MSINGI NA SHULE
8 ZA SEKONDARI VYENYE
THAMANI YA TSH 8,000,000
56. AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA 200,000 FEDHA BINAFSI
MIFUKO 10 KATIKA
ZAHANATI YA
MWACHAMBIA
57. AHADI YA MIFUKO 10 AHADI IMETIMIZWA 200,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA OFISI YA CCM TAWI
LA IKIWU KATA YA KIJOTA
58. AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA 600,000 FEDHA BINAFSI
MIFUKO 30 OFISI YA WAZAZI
WILAYA
60. AHADI YA KUCHANGIA AHADI IMETIMIZWA 400,000 FEDHA BINAFSI
MIFUKO 20 ZAHANATI YA
IDD SIMBA KATA YA
MRAMA
61. KUCHANGIA SUKARI AHADI IMETIMIZWA KWA 600,000 FEDHA BINAFSI
KATIKA SHULE ZA KUKABIDHI KILA SHULE KILO
NGARAMTONI, 50 ZA SUKARI JUMLA YA TSH
MWIGHANJI,MNUNGHUNA 600,000
NA IKIWU KWA AJILI YA
WALIMU KUPATA CHAI
JUMLA YA FEDHA BINAFSI NI TSH 104,950,000/=

16.0 CHANGAMOTO
Bado tunazo changamoto nyingi ambapo tunaendelea na juhudi za kuzibadilisha kuwa fursa. Changamoto
hizo ni pamoja na kutokuyatambua mafanikio mengi yaliyofanyika, upungufu wa rasilimali kwani
mahitaji ni mengi, changamoto za usalama baadhi ya maeneo, ukosefu wa ardhi kwa ajili ya kilimo na
mifugo, masoko ya mazao yetu ya kilimo, mifugo na mazao ya maliasili Siyo rahisi kuzitaja changamoto
zote. Hata hivyo, juhudi zetu tumezielekeza kuzigeuza changamoto hizo kuwa fursa

17. 0 HITIMISHO
Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi kwa kuendelea kunipa afya njema
ili kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Singida Kaskazini na Watanzania kwa ujumla.
Nami kwa niaba yenu Napenda kuahidi kuendelea kuwatumikia vyema na kwa moyo wa dhati kabisa,
wananchi wa jimbo la Singida kaskazini na watanzania wote kwa ujumla

Tunafahamu kuwa maendeleo yanaenda awamu kwa awamu hivyo nawaomba wananchi wetu wawe na
subiria katika mapinduzi makubwa yanayokuja kwa kasi katika Jimbo letu la Singida Kaskazini.

ENG: JUSTIN JOSEPH MONKO

(MBUNGE JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI)


41
42
43
Mh Mbunge akiwa kwenye picha na wadau mbalimbali katika Jimbo la Singida Kaskazini na nje ya
Jimbo.

44

You might also like