Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1052 SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema iwapo Tume ya Uchaguzi itafanya kazi kwa kujiamini na kuacha kufuata matakwa ya wanasiasa, itajenga imani kwa wananchi juu ya uwezekano wa kuwepo kwa chaguzi huru na za haki na kukidhi matakwa ya wananchi. Maalim Seif ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwake Mbweni Zanzibar, wakati akizungumza na wajumbe wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar-ZEC, waliofika kwa ajili ya kumkabidhi ripoti ya utendaji wa Tume hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, pamoja na kumuaga baada ya kumaliza muda wao wa utumishi ndani ya
SHEIKH Ponda Issa Ponda akiwa katika Mahakama ya Kisutu Jumatau wiki hii. (Picha na Bakari Mwakangwale
Inaendelea Uk. 2
si upotoshaji bali ni vitabu mbalimbali na uhalisia na kwamba, mwenyewe (Nyerere) yale wanayodai kuwa ni hakuwahi kukanusha upotoshaji yamo katika Inaendelea Uk. 4
2
AN-NUUR
Tahariri/Habari/Tangazo
kwa ukubwa huu wa nchini, ni dhahiri kwamba kuna uhaba makubwa ya watu kulingana na ukubwa wa ardhi yetu. China ina watu milioni 1,300, ikiwa na ukubwa wa eneo la km 9,596,960. Malaysia ina ukubwa wa eneo la km 329,847 tu, lakini watu wake ni 26,888,000 kwa kadirio la mwaka 2006. Sensa ya
AN-NUUR
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
MAONI YETU
Inatoka Uk. 1
mwaka 2000 iliyofanyika nchini humo ilionyesha kuwa kulikuwa na idadi ya watu 23,953,136. India yenyewe ina idadi ya watu bilioni 1.2 Utaona kuwa pamoja na kuwa na idadi kubwa ya watu, na nchi nyingine kuwa na ardhi ndogo, bado mataifa hayo yamekuwa ndio tishio kwa sasa katika
mzigo kwa serikali. Hata hivyo, katika mataifa yaliyoendelea na yanayokua kwa kasi kiuchumi, watu wamekuwa mtaji mkubwa wa kiuchumi kwa mataifa hayo. Watu ni soko, watu ni nguvu kazi. China, Malaysia, India, na mataifa mengi ya Bara Asia, yamekuwa yakipiga hatua kwa kasi kiuchumi, nyenzo kubwa ikiwa ni idadi kubwa ya watu. Watu wengi ni kigezo muhimu cha kukua uchumi wa soko na nguvu kazi kwa Taifa lolote lile. Hata wanaofanya biashara, hukimbilia sehemu zenye idadi kubwa ya watu ili kupata soko. Idadi ya sasa ya Watanzania, japo tunaamini wengi hawakuhesabiwa, lakini haiwezi kuzua hofu kwa serikali yeyote yenye mipango mizuri ya kiutawala kwa watu wake. Tuonavyo sisi, hofu ya Rais Kikwete isingekuwepo kama angekuwa na watu waadilifu wa kumsaidia kusimamia mapato namatumizi na rasilmali za Taifa, ili kuijenga nchi kiuchumi na kuiongezea serikali nguvu ya kuwahudumia watu wake. Ukweli ni kwamba, kukosekana kwa viongozi na watendaji waadilifu, ambao wangeweza kusimamia rasilmali za nchi kwa faida, ndio sababu kubwa ya kutiliwa shaka uwezo wa serikali kuhudumia watanzania, sio idadi yao inayokuwa. Hata kukiwa na idadi ndogo ya watu isiyokuwa kwa kasi, lakini waliopewa dhakama na kuongoza na kusimamia mali za watanzania wakikosa uadilifu na kutokuwa watu wa kutosheka, uwezo wa kuhudumia watu hao wacheche hautakuwepo pia. Kukosekana maadili kwa viongozi kumekua chachu ya matumizi mabaya ya rasilmali za nchi, kiasi cha kushindwa kutoa huduma nzuri na bora kwa watu wake. Hulka za wizi, dhuluma, ufisadi, ubinafsi, kukosa uzalendo, ni matokeo ya kukithiri utamadumi mbovu kwa viongozi na watendaji, ambao wameweka uadilifu pembeni na kuvaa ubinafsi na kulitia taifa katika hasara. Ukweli ni kwamba, Tanzania imekuwa ikipata taabu kukia malengo yake ya kuwahudhumia watu wake, kutokana na watu waliopewa dhamana kuliingiza Taifa katika mikataba mibovu na ya kihasara kwa maslahi yao na familia zao, huku watanzania walio wengi wakiachwa kuishi katika maisha ya kilofa. Tunaona kwamba Tanzania ambayo ina eneo la nchi kavu la kilomita za mraba 945,000, ambazo kati ya hizo, Kilomita za mraba 881,000 ni eneo la Tanzania Bara pekee yake na kilomita za mraba 2,000 ni eneo la visiwa vya Zanzibar na Pemba,
Tume hiyo. Hata hivyo, Maalim Seif, amesema Tume hiyo inayomaliza muda wake mwishoni mwa mwezi huu, inaondoka huku ikiacha viporo ambavyo Tume inayokuja inapaswa kuvipa umuhimu wa kipekee. Miongoni mwa mambo ambayo hayakuweza kutekelezwa na Tume hiyo ni pamoja na kushindwa kulifanyia uhakiki daftari la kudumu la wapiga kura kwa vipindi viwili tofauti, jambo ambalo liliahidiwa na Tume hiyo kufanyika kila ikapo mwezi wa Oktoba. Kamishna wa Tume hiyo Bw. Ayoub Bakar Hamad, amesema tatizo hilo lilitokana na ukosefu wa fedha za kuendeshea kazi hiyo na kwamba, kwa sasa Shirika la Umoja wa Mataifa la
zaidi ni kukubali kufuata sharia. alishauri Mwinyichande na kuongeza. Wanasiasa pia mnayo nafasi kubwa ya kuisaidia Tume kwa kuipa maelekezo yanayostahiki, na kufanya hivyo kunaweza kuipa nyenzo bora za kufanyika kazi. Naye Mkurugenzi wa Tume hiyo Bw. Salum Kassim Ali, ameahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika chaguzi zilizopita, ili kuweka mazingira bora zaidi katika chaguzi zijazo. Pamoja na hayo, Maalim seif, alieleza haja ya Tume hiyo kuanzisha mfuko wake, ili mapato ya Tume yaingie moja kwa moja katika mfuko huo na kupunguza usumbufu wakati Tume inapohitaji fedha kwa ajili ya matumizi yake ya kawaida.
ALJEBRA ISLAMIC SEMINARY KIKAO CHA WAZAZI, WALEZI NA WADAU WENGINE WA ELIMU
SHULE YA ALJEBRA ISLAMIC SEMINARY ILIYOPO KIBADA KIGAMBONI DAR ES SALAAM INAPENDA KUKUTAARIFU KUWA IMEANZISHA SHULE YA MSINGI ENGLISH MEDIUM. UKIWA KAMA MZAZI, MLEZI AU MDAU WA ELIMU UNAKARIBISHWA KWENYE KIKAO CHA KUTAMBULISHA SHULE RASMI, KIKAO KITAFANYIKA SHULENI SIKU YA JUMAPILI TAREHE 6/1/2013 KUANZIA SAA 3 ASUBUHI HADI SAA 6 MCHANA. KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU NAMBA: 0715/0752/0688 260241 AU 0655/0768 176700 TAFADHALI ATAKAYESOMA TANGAZI HILI AMTAARIFU NA MWENZAKE WOTE MNAKARIBISHWA WABILLAH TAWFIIQ MKUU WA SHULE
Habari
AN-NUUR
WAKILI wa Sheikh Ponda Issa Ponda, Juma Nassoro akiongea na Waislamu nje ya Mahakama ya Kisutu Jumatatu wiki hii. (Picha na Bakari Mwakangwale)
Wa s h t a k i w a w e n g i n e waliopo nje kwa dhamana, wametakiwa kufika Mahakamani hapo Januari 17, 2013, siku ambayo kesi hiyo itaendelea kwa kusikiliza mashahidi wa upande wa mashtaka. Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Wakili wa Sheikh Ponda, Juma Nassoro, alionyesha kushangazwa na mwenendo wa kesi hiyo kwa upande wa walalamikaji. Alisema, mbali ya mashahidi wanaoanza kukwepa kuka na kutoa ushahidi wao, lakini hata Hadhi, ambaye ndiye mlalamikaji amekuwa haki Mahakamani bila sababu za msingi. Aidha alisikitishwa na kitendo cha upande wa mashtaka kushindwa hata kutaja majina na idadi halisi ya mashahidi, jambo alilodai kuwa si la kawaida kwani hata katika kesi za mauaji, mashahidi huwa wanatajwa tofauti na wale wa kesi ya mteja wake. Alipoulizwa na An-nuur juu ya mustakali wa dhamana kwa wateja wake (Sheikh Ponda na Mukadam), alisema bado Jamhuri inadai kuwa inaona watahatarisha amani endapo watakuwa nje. Hata hivyo alisema, wameandika barua kulalamikia suala hilo kwa DPP lakini bado hawajapata majibu yoyote. Alisema katika barua hiyo, wamemweleza DPP kwamba kuendelea kumshikilia Sheikh Ponda na Mukadam, ni kinyume cha
haki za binadam kwa sababu haiwezekani katika kesi moja washtakiwa wengine wote wapate dhamana na wengine wanyimwe haki hiyo. Alisema kitendo hicho ni cha kukandamiza haki za msingi za binadamu kwa sababu katika mtiririko wa maelezo ya kesi, hakuna hata mmoja anayezungumzia kuvurugwa amani ya nchi, zaidi mashahidi wanazungumzia uhalali au kutokuwapo uhalali wa kuuzwa kiwanja cha Markazi Changombe. Kwamba hakuna sehemu yeyote ambayo inaonyesha kiwanja hicho kinagusa maslahi ya Taifa. Tumeandika barua kwa DPP, Desemba 24, 2012, yenye kumbukumbu namba LJ/CC/245/2012, tumeomba kwamba DPP aondoe pingamizi lake la dhamana kwa sababu kesi na mtiririko wake unavyokwenda, hakuna
lolote linaloonyesha maslahi ya Taifa au usalama wa nchi unaweza kuhatarika kwa Sheikh Ponda na Sheikh Mukadam kuwa nje kwa dhamana. Nao wapewe haki hiyo kama ambavyo wenzao waliopatiwa dhamana katika shauri hilo hilo. Alisema Wakili Nassoro. Wakili Nasoro alisema, ushahidi unaotolewa unaonyesha kabisa kuwa ni mashtaka ya kawaida kwani alidai kwamba, hata maelezo ya Bw. Hadhi, (aliyenunua kiwanja) aliyoyataoa Polisi Changombe akiwa mlalamikaji, hakuna mahala panapoeleza kuna kuhatarisha maslahi ya Taifa au Usalama wa Taifa. Alisema ndio maana a m e m u o m b a D P P, a t o e pingamizi lake ili Mahakama iweze kuweka wazi dhamana kwa washtakiwa ili wapate haki yao ya dhamana.
Vipo Barabara ya Kongowe-Soga Kilomita moja toka barabara ya Morogoro. Simu No.0755 090 754/0715 090 754.
Aidha wamefahamishwa kwamba, inaposemwa kuwa hayati Mwalimu Nyerere alikuwa muasisi wa Mfumokristo, umekuwepo ushahidi kamili hivyo haisemwi kwa kuzusha tu au kumpakazia na kwamba, ndiyo sababu Kanisa Katoliki nchini linataka kumpa utakatifu kutokana na kazi nzuri alilolifanyia Kanisa hilo alipokuwa madarakani. Akihutubia ndani ya Masjid Idrisa, uliopo Kariakoo jijini Dar mara baada ya swala ya Ijumaa wiki iliyopita, Maalim Bassaleh, aliwataka Maaskofu nchini, kueleza kwa uwazi sababu za kubariki utakatifu wa hayati Julius Kambarage Nyerere, wakati hakuwa kiongozi wa dini. Alisema kabla ya kutaka kumkingia kifua Mwalimu Nyerere ambaye aliyekuwa kiongozi wa siasa, ni vyema kwanza wakaeleza misingi ya kumsimika utakatifu mkatoliki ambaye hakuwa kiongozi wa Kanisa. Lakini tuliulize hilo Kanisa Katoliki, kwamba je, Mwalimu Nyerere, alikuwa kiongozi wa dini au kiongozi wa Siasa? Kama wa siasa, vipi Kanisa hilo linataka kumpa cheo cha utakatifu, cheo ambacho kinalihusu Kanisa hilo tu, wakati alikuwa ni kiongozi wa umma na si wa dini. Alisema na kuhoji Maalim Bassaleh. Alisema kwa kawaida, Wakatoliki huwapa utakatifu watu ambao walikuwa nguzo (mihimili) ya Kanisa Katoliki na ambao wamefanya kazi zilizotukuka wakiwa ni Wachungaji au Watawa au watumishi wa kanisa waliowahi kujitolea kwa muda mrefu katika Kanisa. Akinukuu kitabu cha Rais mstaafu wa Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe, ambaye alifanya kazi ya kwa karibu na mwalimu, Maalim Bassaleh alisema katika kitabu chake hicho cha The Partnership, ameeleza kwamba mwalimu Nyerere, alikuja kuimarisha Mfumokristo katika utawala wake kutokana na nafasi aliyokuwa nayo na zaidi alilipendelea Kanisa lake Katoliki. Alisema Alhaji Jumbe, aliyaeleza hayo kwa kutumia
Habari
AN-NUUR
MAALIM Ally Bassaleh akiongea na Waislamu katika viwanja vya Biafra, jijini Dar es Salaam. ushahidi wa Padri Mkristo wa Kikatoliki, Dk. Sivalon, aliyefanya utafiti kuhusu Kanisa Katoliki na siasa za Tanganyika, ambapo kwa uwazi na mapana Padri huyo ameonyesha ni vipi mwalimu Nyerere, wakati wa utawala wake alivyokuwa akilipendelea Kanisa Katoliki nchini. Ufafanuzi wa Maalim Bassaleh umekuja kufuatia yaliyoelezwa katika tamko la Jumuia ya Maaskofu lililotolewa Kurasini Jijini Dar es Salaam siku za hivi karibuni. Katika tamko hilo, pia walijadili hali ya kuzorota kwa mahusiano baina ya dini mbili kubwa hapa nchini, Uislamu na Ukristo, kisha walieleza juu ya hatari inayolinyemelea Taifa kutokana na hali hiyo. Maalim Bassaleh, alisema katika kipengele hicho, amewataka Waislamu kuwapongeze Maaskofu hao kwa kuiona hali hiyo na kisha kutoa wito wa kuyashughulikia haraka yale yanayoashiria hatari sambamba na kuboresha mahusiano mema baina ya Waislamu na Wakristo. Kama ndugu zetu Maaskofu watakuwa wakweli, basi huo ni mwanzo mzuri wa kujenga msingi mwema wa amani ya kweli katika nchi yetu na wala isiwe amani ya kifaurongo (aina ya mti ukiguswa husinyaa baada ya muda huchanua). Alisema Maalim Bassaleh. Pamoja na kuwapongeza Maaskofu kwa kuiona hatari iliyo mbele, lakini alidai makundi hayo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa katika kiini cha matatizo hayo na suluhisho lake. Akichambua tamko hilo, Maalim Bassaleh, alisema makundi hayo yanaanza kuachana pale ambapo Maaskofu hao wanapokataa kuwepo kwa Mfumo Kristo ulioota mizizi katika dola, wakidai kwamba ni dhana potevu. Jukwaa la Wakristo nchini tunakanusha wazi wazi na kuelezea bayana kuwa nchi hii haiongozi kwa Mfumo Kristo, kwa watu walio makini hakuna kicho kuwa viongozi wote waandamizi wa ngazi ya juu serikalini awamu ya sasa asilimia tisini ni Waislamu. Dhana ya kuwepo Mfumo Kristo ni uongo na ni dhana potevu, maneno hayo ni agenda za waamini wenye imani kali na waliojiandaa kwa mapambano maovu. Alinukuu sehemu ya tamko hilo. Akifafanua neno Mfumokristo Maalim Bassaleh, alisema ni mfumo kandamizi dhidi ya Uislamu na Waislamu, japo kuwa kwa misingi ya kiserikali mfumo huo haupo rasmi, lakini kiutendaji mfumo huo umefanywa kuwa ni mila, desturi na utamaduni wa watendaji walio wengi serikalini na katika taasisi zake, ambazo mara nyingi zinatumika kuwakandamiza na kudhulumu haki za Waislamu. Alisema mfumo huo umekuwa kama utamaduni na umeenezwa hadi katika mashirika ya umma na katika Taasisi za kijamii. Mara kadhaa watekelezaji wa Mfumokristo wamekuwa wakikiuka hata Katiba na sheria za nchi, hususani masuala hayo yanapogusa Waislamu na Uislamu. Maalim Bassaleh alisema kwa utaratibu huo, hata kama Maaskofu wamenisha kuwa Rais na watendaji wa ngazi za juu wote ni Waislamu, lakini kutokana na Mfumokristo, wote waliotajwa wanatatizika katika kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Wakijisafisha kuhusu suala la MoU, Maaskofu hao wanadai katika tamko lao kwamba mkataba huo ni baina ya Makanisa ya Tanzania na Makanisa ya Ujerumani na kwamba, serikali ilihusishwa tu. Katika maelezo yao kuhusu MoU, wao wamedai kuwa MoU ya mwaka 1992, ni kwa ajili ya huduma ya kijamii zinazotolewa na Makanisa kwa Watanzania wote, ikiwa ni pamoja na huduma za hospitali, vituo vya afya, zahanati na shule mbalimbali zinazoendeshwa na Makanisa nchini.
Maalim Bassaleh alihoji, ikiwa mkataba huo ni wa Makanisa na kwamba serikali ilihusishwa tu, itahusishwa vipi katika masuala ya dini wakati Serikali yenyewe haina dini? Inafahamika kwamba kwamba hao Maaskofu, wamekuwa wakiigomea Serikali kujihusisha na Mahakama ya Kadhi na suala la OIC kwa Waislamu, wakidai serikali haina dini. Mbona Serikali hiyo inahusishwa katika mikataba ya Makanisa ya Ulaya na yale ya humu nchini, lakini hawataki ihusihwe na OIC, ambayo nayo ikija itatengeneza barabara, madaraja, na watakaopita ni watu wote bila kuangalia waliovaa kofia, kanzu au kilemba, kusaidia taasisi za huduma za kijamii ya watanzania wote bila kujali dini zao kama inavyodaiwa kufanywa na taasisi za makanisa?. Alihoji Maalim Bassaleh. Hata hivyo Maalim Bassaleh alisema maaskofu hawataki kusema kweli juu ya mkataba wao wa MoU kati yao na serikali. Alisema, maelezo wanayoyatoa Maaskofu ni tofauti na mkataba wenyewe ambao unasema, Sisi tuliotia saini zetu ambao ndio wahusika katika maridhiano hayo, kwa kutaja Makanisa yaliyoungana chini ya Baraza la Makanisa Tanzania na Baraza la Maaskofu Tanzania. Ambayo katika mkataba huu yatakuwa yanajulikana kama ni Makanisa kwa upande mmoja na Serikali ya Muungano wa Jamhuri wa Tanzania, itatambulika kama ni Serikali kwa upande wa pili. Alinukuu sehemu ya mkataba huo kati ya serikali na makanisa. Alisema, kutokana na kipengele hicho, inaonyesha makubaliano hayo ni ya pande mbili ambapo upande wa kwanza ni wa Makanisa, ambayo yameungana pamoja na upande wa pili ni wa Serikali. Katika Makanisa yaliyotajwa hapo, hakuna Kanisa la Kijerumani. Alisema kwa kupitia mkataba huo, Makanisa yanatumia pesa za Serikali ambazo ni za walipa kodi wote. Mwaka wa fedha wa 2008-2009, Serikali ilitumia mamilioni ya fedha kwa ajili ya kufadhili Mahospitali na taasisi nyingine za huduma za afya zinazomilikiwa na Makanisa kwa ajili ya kulipa mishahara wafanya kazi.
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
WASHINGTON HABARI kutoka Marekani zinabainisha kuwa, viongozi wa kisiasa wa vyama vya Republican na Democrats, wameendelea kulumbana kutokana na hali mbaya ya uchumi wa nchi hiyo. Mvutano huo umetokea kuhusu juu ya namna gani ya kutatua matatizo ya kiuchumi ili kuweza kuwapunguzia wananchi mzigo wa mgogoro wa kiuchumi. Mkuu wa taasisi ya Centre for Corporate Policy, ya Washington Bw. Charlie Cray, amesema kuwa jamii ya watu wa tabaka la kati nchini Marekani, ndio waathirika wa malumbano ya kisiasa nchini humo. Ameongeza kuwa, hali hiyo imezidisha ongezeko la ukosefu wa ajira na mgogoro wa kiuchumi nchini humo. Mtaalamu huyo wa masuala ya kiuchumi pia amesisitiza kuwa, hali mbaya zaidi inawakabili Wamarekani wenye asili ya Kiafrika na kwamba, kiwango cha ukosefu wa ajira katika tabaka hilo kimekia asilimia 12.4, ambapo wengi wao ni vijana walio na umri wa kati ya miaka 18 hadi 29. Rais Barack Obama amekuwa akishinikiza mpango wake wa kuiongeza kodi kwa matajiri nchini humo, ikiwa nikatika harakati zake za kujaribu kupunguza nakisi ya bajeti ya nchi hiyo na kuongeza pato la serikali.
LONDON LICHA ya kutangazwa kwa propaganda mbaya kama dini ya magaidi, Uislamu unakuwa kwa kasi katika nchi za Magharibi ambazo kwa kawaida wanaishi wakristo wengi. Uingereza imekuwa mfano mzuri wa hali hii ambapo Wakristo wengi wanabadili dini na kuwa Waislamu na kuufanya Uislamu kuwa dini inayokuwa kwa kasi zaidi katika majimbo ya nchi hiyo. Kushamiri kwa Uislamu kumebainika hivi karibuni kufuatia sensa iliyofanyika hivi karibuni Uingereza, ambayo si kwamba imebainisha ukuaji wa haraka wa Uislamu, lakini pia kumeifanya Uislamu kuwa dini ya pili nchini humo. Mmoja wa watathmini
Uislamu unakuwa kwa kasi na idadi kubwa ya wasiokuwa Waislamu wameamua kuufuata, ingawa watu wa Magharibi wanauona kama ni dini ya magaidi na kusambaza propaganda potofu dhidi ya Waislamu.
Makala
AN-NUUR
SHEIKH Farid Had na viongozi wenzake wa UAMSHO wakiwa katika karandinga la Polisi. Na Mwandishi Wetu
WAZUNGU wana msemo wao usemao, Ukitaka kumuua mbwa mpe jina baya. Jambo la kushangaza basi, katika uzoefu wa maisha ya mwanadamu si mara nyingi falsafa na ukweli uliomo katika methali kutumika kama falsafa ya nchi au taifa fulani. Lakini kwa sababu moja au nyengine, kuna misemo miwili mitatu hivi inaonekana kubakia kuwa misemo tu, bali imekuwa kama falsafa inayoongoza maisha na malengo ya watu hapa duniani. Kwa mfano, msemo mkongwe w a Wa z u n g u u t a f s i r i k a o kama wagawe, uwatawale umetumika ipasavyo katika kuzitawala nchi na Jumuiya mbalimbali duniani. Waingereza waliweza kuitawala dunia kwa msemo huu. Na Wamarekani wameweza kufanya watakalo duniani kwa kutumia falsafa hii. Pia Watanganyika wameweza kuitawala Zanzibar kimabavu kwa kutumia fasalafa hii pia. Wametugawa na kututawala. Wakati hubadilisha mambo. Kwa muda wa miongo ipatayo sita (six decades) tangu uhuru, falsafa hii imekuwa ikichwa kutumiwa kwake. Inachwa sio kama haipo, ipo lakini dunia ya sasa ya utandawazi na haki za binadamu, falsafa hii haipati nguvu ya kutembea utupu hadharani tena kama ilivyokuwa mwanzo. Na kwa vile silaha hii imekwisha nguvu, tumeletewa silaha nyengine isemayo, Ukitaka kumuuwa mbwa, mpe jina baya! Zanzibar, katika ramani ya siasa za dunia imekuwa ikifanyiwa kila bidii na njama ili iwe sawa na Palestina, au mataifa mengine ya Kiislamu yaliyoharibiwa na Mayahudi na Manasara kupitia mataifa yao makubwa. Yaani Zanzibar inatakiwa isiwe na utaifa wala utambulisho wowote. Na hilo lilikuwa karibu mno kufanikiwa. Lakini kabla ya kukia hatua hiyo, wazanzibari wameamka. Wakaanza kudai haki zao. Na kwa vile wanzanzibari hawalengwi wala kuthibitikiwa na kuwa na haki ya kudai chao, pao, lao, wala ya kwao, hili limekuwa kosa. Sasa tunabatizwa kwa kila jina baya ili kuhalalisha kuangamizwa kwetu. Tu n a i t w a m a g a i d i n a Waislamu wenye msimamo mkali. Tunaitwa hivi katika kipindi ambacho dunia imejengwa iamini kila Muislamu ni adui asiye na haki ya kuishi katika mgongo wa dunia hii. Kwa kusherehesha mjadala huu, katika siku za hivi karibuni, Zanzibar imekuwa ikiharibiwa sifa na jina lake kwa maksudi na vyombo vitatu. Kwanza, Kanisa ambalo limekuja Zanzibar sio kwa kufanya ibada, bali kuifitinisha Zanzibar mbele ya jamii za Kimataifa. Kanisa lilikuwapo Zanzibar tangu na kabla ya kuja kwa Edward Steere hapa Zanzibar. Kulikuwa kimya ilhali Waislamu walikuwepo, tena na wasomi wakubwa wa enzi hizo wakiwa hai hapa Zanzibar. Ilikuwa kimya na wala hakukuwa na Mzanzibari aliyewahi kuingilia uhuru wa kuabudu kwa wana Kanisa. Na hivi ndivyo ilivyo mpaka leo. Zanzibar ni nchi pekee duniani iliyo na ustahamilivu mkubwa wa kidini (Religious tolerance) kuliko nchi yoyote. Kwa vile wanaonekana Wazanzibari hawapendi ugomvi na wenzao wa Kikristo, la kufanya ni kuwapachika kila aina ya sifa mbovu ili kuwachafua, hata kama hawamchokozi mtu. Kanisa, Zanzibar hufanya kila liwezalo, kuhakisha wanawakorofisha Waislamu ili wajibu mapigo, wawaharabie sifa na malengo yao yatimie. Hili lilishindikana na sasa kuna njama za maksudi za kufanya matukio yao wenyewe kama vile kutia moto baa, makanisa yao, na hata kujeruhiana na kisha wakasingizia Waislamu wa Zanzibar, ambao wengi wao hawana habari na Wakristo waliopo. Wazanzibari wa sasa wametiwa dhiki za maisha kiasi kwamba hata hizo sala tano ni shida kuzisimamisha, seuze kugombana na kanisa. Chombo cha pili ni Serikali, ambayo ili kulinda maslahi ya Muungano, imeifanya Zanzibar kuwa ni eneo la hatari kidini na kisiasa. Na bila kujua athari ya maneno wanayosema mbele ya jamii za kimataifa, serikali imethubutu kuitangazia dunia kuwa Zanzibar kuna magaidi na wanaharakati wa Kiislamu wenye msimamo mkali. Huu ni ubaya ulio dhahiri wa Serikali dhidi ya wananchi wake wenyewe. Serikali haitambui kuwa kufanya hivi sio kuharibu taswira ya Zanzibar na Waislamu tu, bali hata nchi nzima, na kuathiri shughuli nyingi za kiuchumi, lakini nani anakiri hayo. Tupo kisiasa zaidi. Taasisi ya tatu, Mayahudi na Manasara ambao kazi yao ni kuleta tina katika ardhi, hasa hasa ardhi za Kiislamu. Watu hawa ambao wengi ni wazungu, huja hapa kama watalii na baadae
kuanza kupanga hujuma na mitandao ya tina zisizomithilika dhidi ya Waislamu. Baada ya hujuma zao hizo kutimia, ndio utaona wanatumia vyombo vya habari kuitangazia dunia kuwa Zanzibar kuna ugaidi Waislamu wanawaonea wakristo. Hii ni tna tupu. Zanzibar hakuna lolote kati ya hayo wanayoyataja. Na jambo la kushangaza, hakuna kiongozi wetu hata mmoja anayekanusha upuuzi na kasumba hizi. Leo hii Wazungu ndio wanaoongoza kwa kutembea uchi hapa Zanzibar. Waislamu wako kimya. Wao wapo hapa pia kuishawishi nchi hii ikubali ndoa za mashoga. Mambo ambayo huko kwao yameshawashinda, wanatuletea sisi huku. Wazungu ndio walioleta nakama ya mahoteli, kuigiza na kuingiza mikanda ya ngono, na ndio wanaojazana hapa mwezi wa Ramadhani kuja kula mchana barabarani ili kuwaudhi Waislamu. Hakuna a n a y e s e m a . Tu n a f a n y i w a maudhi na karaha ndani ya nchi yetu, bila kuheshimu mila na desturi za nchi yetu. Ukisema Serikalini unajibiwa, Serikali haina dini. Wanzanzibari tumekuwa watumwa, watwana katika nchi yetu kwa wageni wajao kwetu. Na bahati mbaya Waislamu wakisimama kudai haya, Serikali husimama kidedea kuwalaani Waislamu na kuwahujumu kupita kiasi. Serikali haijali wala kutambua kuwa katika nchi kama Zanzibar ambapo Waislamu ni wengi, mila na desturi za Waislamu hao hazina budi kulindwa na kuheshimiwa na kila mtu, licha ya kuwa serikali haina dini, lakini viongozi wanayo dini. Nionavyo, ni wajibu wa kila Muislamu, awe kiongozi wa siasa, wa nchi au raia wa kawaida, ni wajibu kwake kuilinda dini hii. Tuelewe kwamba wenzetu wasiokuwa Waislamu, wameandaliwa kuvuruga juhudi zote za kuimarisha na kuisimamisha dini ya Kiislamu. Na mbinu wanayoitumia ni hii ya kutuita majina mabaya ili kuhalalisha maovu yao. Wazanzibari na Waislamu wote, tuwe macho na tusimame na kamba ya mwenyezi Mungu bila kufarikiana. Kwani tutakaposimama kumnusuru Mola wetu, atatunusuru na kuzithibisha nyoyo zetu. Tukumbuke kwamba, wenzetu w a s i o k u w a Wa i s l a m u hawapendezewi na ustaarabu na utamaduni sahihi wa dini hii, na ndio Mola mtukufu anaposema Hawataridhika hao Mayahudi na Manasara, mpaka muwafuate mila na nyendo zao. Wallwahu a-alam!
7
Na Mama mwanaharakati Desemba 27, 2012 Mtandao wa kupashana habari Siku tatu kabla ya kijana wa miaka 20 Adam Lanza kumwua mama yake, na halafu akafyatua risasi katika darasa lililojaa watoto wa chekechea huko Connecticut nchini Marekani, mwanangu Michael (jina limebadilishwa) mwenye umri wa miaka 13 alikosa basi la kumpeleka shule kwa sababu alikuwa amevaa kaptura yenye rangi zisizostahili. Naweza kuvaa kaptura hii, alisema, sauti yake ikiongeza ukali, chembe nyeusi ya katikati ya jicho ikimeza ukanda wa bluu unaozunguka. Kaptura hii ni buluu ya bahari, nilimwambia. Sare za shule yako ni kaptura nyeusi au za khaki, basi. Waliniambia naweza kuvaa hizi, alingangania. Wewe ni dogi mpumbavu, Naweza kuvaa kaptura yoyote ninayotaka. Hii ni Amerika. Nina haki zangu. Huwezi kuvaa chochote unachotaka, nilisema, kwa sauti ya upole, kumwelewesha. Na kwa vyovyote huwezi kuniita dogi mpumbavu. Hutatumia chochote cha kielektroniki siku nzima, Sasa ingia kwenye gari nikupeleke shuleni. Naishi na mtoto ambaye ni mgonjwa wa akili. Nampenda mwanangu. Lakini ananitisha. Wiki kadhaa zilizopita, Michael alinishikia kisu na kutishia kuniua na halafu ajiue baada ya kumwambia arudishe vitabu vya maktaba alivyochelewesha. Wadogo zake wa miaka 7 na 9 wanafahamu mipango ya usalama - walikimbilia gari na kufunga milango kabla sijawaambia wafanye hivyo. Nilifaulu kukitoa kisu mikononi mwa Michael, na kwa uangalifu nikaokota chochote chenye ncha kali ndani ya nyumba na kuweka katika kasha ambalo kila nikisafiri naondoka nalo. Na muda wote huo alikuwa akiendelea kunitukana kwa sauti kubwa na kutishia kuniua au kunidhuru. Ugomvi huo uliisha wakati maofisa watatu wa polisi wenye vifua vipana na mganga msaidizi walipombana mwanangu aingie kwenye kiti cha gari la wagonjwa la gharama kubwa kupelekwa katika chumba cha dharura cha karibu. Hospitali ya magonjwa ya akili haikuwa na vitanda vyovyote siku hiyo, na Michael akatulia vyema katika
Makala
AN-NUUR
Makala/Tangazo
AN-NUUR
kura ya maoni (Referendum) na majadiliano makali ya kitaifa yatafwata. Kinaeleza kuwa kubwa litakalokua katika mada ni kuundwa kwa Serikali ya Shirikisho la Jamuhuri ya Tanzania. Waandaji wa twasira hiyo wanasema, hapo ndipo muundo wa shirikisho utakapokuwa tayari na Tanzania itakuwa na majimbo matano yakiwa ni Kusini, Kati, Kaskazini, Magharibi na jimbo la Mashariki, ambalo litakuwa na mikoa ya sasa ya Tanga Lindi, Dar es Salaam na Zanzibar yenyewe. Kitabu hicho cha Tutaka ambacho kilitolewa bure, ni dhihirisho kuwa tayari mikakati imeanza kuandaliwa, ili kujenga njia ya makusudi kuelekea katika lengo la kuwa na mabadiliko makubwa. Mabadiliko yatakayojumuisha pamoja na mambo mengine, suala la Zanzibar inachukuliwa yote ndani ya Tanganyika ya sasa. Wenzetu wamo katika kulikamilisha lengo la kuichukua Zanzibar milele na milele. Zanzibar inahitaji Musa aliye Mzanzibar aliyerithi damu ya uzalendo toka tumboni kwa mama yake. Vyenginevyo, tusije kuusaidia mpango wao kupitia sera ya CCM mwishowe ikawa ni vilio.
0715 - 498363
Uongozi wa Shule ya Answaar Islamic Model School inawatangazia waislamu wote nafasi za masomo kwa mwaka 2013, kama ifuatavyo. 1. Shule ya awali ( Nursery School) Kg - 1 and Kg 11 Umri kuanzia miaka mitatu na nusu na kuendelea. 2. Shule ya msingi ( Primary School) Darasa la kwanza hadi la Sita, kwa wale wanaotaka kuhamia nafasi pia zipo. ADA: shule ya awali ( Nursery school) 550,000/= kwa mwaka. Shule ya msingi (Primary school). i) Darasa la kwanza hadi la tano ni Tsh. 650,000/= ii) Darasa la sita na la saba Tsh. 750,000/= ada inalipwa kwa awamu tatu. - Shule ipo kinondoni Studio/ karibu na vijana Social Hall au nyuma ya vijana. - fomu zinapatikana shuleni Kinondoni studio Masjid Answaar. - Tarehe ya USAILI ni Tarehe 6/01/2013, usaili utafanyika shuleni Answaar Islamic Model School, Siku ya Kufungua shule ni Tarehe 14/01/2013. Kwa mawasiliano zaidi piga simu. 0767- 121555,0777-790283, 0712 790283. Au Email answaarislami@yahoo.com au tembelea Tovuti yetu: www.answaarislamic.co.tz Mlete mwanao apate elimu na malezi bora ya Kiislamu
9
Na Said Rajab.
DESEMBA 25 mwaka 2012, Maaskofu wa makanisa takriban yote hapa nchini, walitoa maneno mazito ya vitisho, kejeli na vijembe kupitia ibada zao za Krismasi dhidi ya Serikali ya Tanzania na Waislamu. Maneno hayo kimsingi yametokana na maazimio ya kikao cha nne cha Jukwaa la Wakristo Tanzania TCF, kilichoketi Desemba 6 mwaka 2012, Kurasini jijini Dar es salaam. Ukisoma tamko la Maaskofu kwa makini, kimsingi hakuna hoja yoyote ya maana inayoweza kudumisha amani ya Watanzania. Kwa sababu amani haijengwi kwa kufumbia macho dhulma. Waislamu kwa muda mrefu wamekuwa wakilalamikia dhulma wanazofanyiwa na mfumo usio rasmi serikalini, ambao unawapendelea Wakristo. Waislamu wamekuwa wakitoa ushahidi wa kihistoria, kisayansi, kimazingira na hata kitakwimu kuhusu dhulma hizo. Lakini kichekesho cha mwaka, zaidi ya Maaskofu 35 wanakutana jijini Dar es salaam, wanajadiliana kisha wanaona watoke na vitisho, kejeli na vijembe dhidi ya Waislamu na Serikali, badala ya kuleta hoja za msingi zitakazolinusuru taifa na hatari za upendeleo wa kidini, unaofanywa na mawakala wa kanisa serikalini! Ta m k o l a M a a s k o f u limeonyesha hofu kwamba Waislamu wameshagundua dhulma wanazofanyiwa. Na anayewadhulumu pia wanamjua. Sasa Maaskofu wanajaribu kuficha uhalifu wao kwa kutumia vitisho, propaganda, porojo na vijembe. Hiyo ni namna ya kujihamu tu (Defence Mechanism). Siyo lengo langu hasa kujibu tamko la Maaskofu kupitia makala hii. Kwa sababu tamko lenyewe, kwa kiasi kikubwa, halikuzingatia ukweli wala uhalisia wa mambo, na limesimamia zaidi kwenye propaganda na porojo. Ni sawa na maneno ya kwenye khanga! Wanataka kuchora picha potofu kwenye jamii kwamba Wakristo nchini Tanzania wanaonewa sana na Waislamu! Makanisa yao yanachomwa, wakati serikali ikiaangalia tu! Wanajaribu kupandikiza fikra potofu kwenye jamii kwamba Wakristo ndiyo watu wa amani na Waislamu ni watu wa vurugu! Wanadhani wanaweza kugeuza ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli! Ni ukweli usiopingika kwamba Waislamu wa Tanzania wamedhulumiwa na Mfumo Kristo ulioasisiwa na baba wa taifa. Ukweli huu kamwe hautakuwa uongo kwa sababu
Makala
AN-NUUR
ASKOFU Laizer ya propaganda na porojo za Maaskofu. Na tatizo hili lisiposhughulikiwa kwa dhati, lazima litaleta maafa huko mbele. Waislamu wanapigania haki yao iliyodhulumiwa na katika hili, wanaonekana hawamuogopi yeyote. Hilo Maaskofu walifahamu vizuri sana. Nawapongeza sana Waislamu wa Tanzania kwa juhudi zao za muda mrefu za kubainisha dhulma wanazofanyiwa na Mfumo Kristo, ambazo pamoja na kupuuzwa, lakini sasa zimeanza kuzaa matunda. Harakati za Waislamu za miaka mingi za kupigania haki yao iliyoporwa na mawakala wa kanisa serikalini, haziwezi kuishia hewani. Maaskofu wameliona hilo na bila shaka hofu yao ni kwa sababu Waislamu wameshagundua ubaya wao. Kitendo cha Maaskofu kushindwa kujibu hoja za Waislamu kuhusu dhulma za Mfumo Kristo, na badala yake kuleta porojo za kuhamisha ajenda, ni ushindi mkubwa kwa hoja za Waislamu. Tafsiri yake ni kwamba Maaskofu hawana la kusema kuhusu ukweli wa madai ya Waislamu. Mwanzoni waliamua kuwapuuza Waislamu, wakidhani madai yao yangejia yenyewe kifo cha kawaida. Lakini waliposhuhudia wanavyoendelea kusimama kidete kupaza sauti zao, sasa wameanza kutoa maazimio ya woga kuficha uhalifu uliofanyika. Wanataka kuzima sauti za wanaokandamizwa na hilo kamwe halitawezekana. Wanafanana na Maquraysh wa Makka, ambao walidhani wangeweza kuzuia ujumbe wa Quran kwa kuwakataza watu wasiisikilize: Na walisema waliokufuru: Msisikilize Quran hii inaposomwa na ipigieni makelele isomwapo, huenda mkashinda Qur 41:26. Lakini jambo la kuzingatia, kama vile Maqurayshi wa Makkah, ambao hawakuwa na uwezo wa kupambana na Quran kwa hoja za kiakili, Maaskofu wa Tanzania nao hawana uwezo wa kupambanisha hoja na Waislamu. Vurugu zao zote dhidi ya Waislamu siyo za kikra, zaidi ni propaganda na porojo za kucha ukweli! Lugha zao zimejaa chuki na fitna dhidi ya Waislamu. Kila mnapotaka kujadiliana
kwa haki, kitaalamu, kisomi na kiuadilifu, hawako tayari na zaidi wataendelea kutoa maelekezo na mashtaka serikalini. (Uchonganishi). Mfano halisi wa hilo ulishawahi kutokea hapa nchini, wakati Rais Ali Hassan Mwinyi alipowakutanisha Masheikh na Maaskofu Ikulu jijini Dar es salaam, kuzungumzia tatizo la mihadhara ya kashfa. Maaskofu walikuwa wakilalamika, wakiibana Serikali ipige marufuku mihadhara ya Waislamu waliyodai kuwa inakashifu Ukristo. Waislamu kwa upande wao, walipinga dai la Maaskofu, wakileta hoja kwamba hawakashifu Ukristo, bali wanaelimisha watu kwa kutumia maandiko matakatifu. Busara za Mzee Mwinyi zikamuelekeza kuwaita Wa h a d h i r i w a K i i s l a m u , wanaodaiwa kuukashifu Ukristo upande mmoja, na Maaskofu wanaolalamika upande mwingine, ili kujadiliana kidugu, kiuadilifu na kitaalamu, lengo likiwa kubaini ukweli ili kuondoa mgogoro uliojitokeza. Maaskofu hawakuwa tayari kudhihirisha! Hawakuwa na hoja zinazothibiti na kwa bahati pale propaganda haikuwa na nafasi. Matokeo yake malengo ya mkutano ule hayakukiwa. Hawakurudi tena Ikulu kusaka muafaka hadi Mzee Mwinyi alipostaafu! Tizama, lakini angalia, alipoingia Rais Mwingine Ikulu, waliendesha kampeni zile zile za propaganda ya mihadhara ya kashfa kupitia vyombo vya habari, na matokeo yake Serikali ikaenda kuua Waislamu wasio na hatia pale Msikiti wa Mwembechai mwaka 1998. Wa i s l a m u w a l i u a w a Mwembechai kwa sababu tu ya chuki, tina, propaganda, porojo na ulaghai wa Maaskofu. Wa i s l a m u w a l i p o i t a k a Serikali kuunda Tume ya uchunguzi wa mauaji ya Mwembechai, ili kubaini ukweli wake, Rais Benjamin Mkapa alisema hajaona haja na hoja ya kuunda Tume hiyo. Hivyo ndivyo walivyo. Lakini Prof. Hamza Njozi, alipoandika kitabu kubainisha ukweli wa Mauaji ya Mwembechai, ili Ulimwengu ufahamu kilichotokea, Serikali ya yule yule, ambaye hakuona haja na hoja ya kuunda Tume ya uchunguzi akapiga kukipiga marufuku kusambazwa kitabu hicho nchini! Hawasemi ukweli, lakini pia hawataki hata watu wengine waseme ukweli huo! Hivyo ndivyo walivyo! Siyo sifa ya Maaskofu kulinda na kudumisha amani.
huo imekuwa ikitunzwa na Waislamu, tangu kipindi cha harakati za kupigania uhuru na baada ya uhuru kupatikana. Inajulikana vizuri kwamba, ukiwaondoa marehemu Hassan bin Amir na Sheikh Zubeir Mtemvu, Waislamu wa Tanganyika walikataa kukiunga mkono chama chao wenyewe cha All-Muslim National Union of Tanganyika (AMNUT), ili kulinda umoja wa kitaifa chini ya TANU, ambacho Rais wake alikuwa Nyerere, Mkatoliki. Lakini hali inavyoonekana, Maaskofu wamejiandaa kuleta machafuko makubwa ya kidini hapa nchini, ili wapate kizingizio cha kuwachinja Waislamu wanaopigania haki zao, kwa kutumia mawakala wao serikalini. Lakini Waislamu hawana sababu hata moja ya kupigana vita isiyo na macho, ambayo nadhani Maaskofu wanaitafuta kwa udi na uvumba hapa Tanzania. Ila katika mapambano ya kupigania haki, Waislamu hawarudi nyuma na wako tayari.
mwaka 1965 mjini Mbulu. Makanisa yalikuwa yakifanya kazi kwa karibu sana na Serikali ya kikoloni, ambayo ndiyo iliyomlea Mwalimu Nyerere, ili aje kuwa Rais wa kwanza wa Tanganyika baada ya Waingereza kuondoka. Baada ya uhuru kupatikana, nchi ikiwa chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere, Wa k r i s t o w a Ta n z a n i a wanavuna kile ambacho hawakupanda. Wanafurahia matunda ya uhuru kila sekta kutokana na Mfumo Kristo ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere, akiungwa mkono na mataifa ya Magharibi. Leo wanataka kuaminisha watu kuwa wao ndio wazalendo zaidi kuliko Waislamu! Maaskofu wanaeneza propaganda za sumu kwamba Waislamu wanahatarisha amani na umoja wa Watanzania, licha ya ukweli kwam ba amani na umoja
10
Habari/Tamgazp
AN-NUUR
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili, Alh-haji Ali Hassan Mwinyi, amewataka Waislamu kushughulika zaidi na utafutaji wa elimu kwani kufanya hivyo ndio siri kubwa ya kupata maendeleo ya jamii nzima na taifa kwa ujumla. Alhaji Mwinyi, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo, aliyasema hayo alipokuwa akitoa nasaha zake kwa Waislamu waliohudhuria kongamano la Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.a.w) lililofanyika Lushoto Jijini Tanga. Amesema kuwa, jambo lolote haliwezi kufanikiwa bila kuwa na elimu nalo, hivyo aliwataka Waislamu kujikita katika kutafuta elimu na kutoa elimu ili kuweza kuleta maendeleo ya Taifa kwa ujumla. Aliongeza kuwa Uislamu haukutenganisha elimu, hivyo ni vyema Waislamu wakatoa kipaumbele kwa masomo yote, ili kuweza kuandaa Waislamu walio na maadili mema na wenye uelewa wa dini yao. Aidha amewataka Waislamu kutambua kua elimu ndio siri ya maendeleo kwa taifa na dunia nzima, na ndio maana elimu katika Uislamu imefanywa kuwa jambo la lazima, kama ambavyo Mtume Muhammad
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili, Alh-haji Ali Hassan Mwinyi (wanne kutoka kulia) akiwa katika kongamano la Waislamu Lushoto, mkoani Tanga. Watatu kulia ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Amir Kicho, kushoto kwake ni Sheikh Alhad Musa.Wa kwanza kulia ni Sheikh Ismail Osama, Mkurugenzi wa chuo cha Markaz Chang'ombe kwa kufanya hivyo itakuwa ni sawa na kuiga tabia za Mtume (S.A.W) juu ya uadilifu wake, upole na msamaha aliokuwa akiwasamehe wale waliokuwa wakimkosea. Sheikh Osama, alisema kuwa kumbukumbu ya Mazazi ya Mtume yanayofanyika kila mwaka, yawe na athari kwa Waislamu ili kuthibitisha matunda ya kujifunza na kumfuata Mtume kwa vitendo. Alisema mafundisho yanayopatikana katika historia ya Mtume, hayawezi kupatikana kama mtu atakuwa hajausoma Uislamu na Qur an, historia ( Sira ya Mtume) na hadithi za Mtume Muhammad (s.a.w). Naye Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, amekumbusha juu ya Waislamu kuyafanyia kazi yote yaliyoongelewa katika Kongamano hilo. Aidha alitoa pongezi zake za dhati kwa Sharifu Hussein Al-Badawi, kwa juhudi zake kubwa za kuendeleza dini ya Mwenyezi Mungu na kuitetea. Kongamano hilo lilifanyika Desemba 2 mwaka huu Wilayani Lushoto Tanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na kisiasa, pamoja na mamia ya Waislamu kutoka Lushoto na vijiji vya jirani.
Masjid Muzdalifa Mbezi kwa Yusufu inawashukuru waislamu wote waliofanikisha ujenzi wa msikiti kufikia mahala hapa ulipokia. Lakini pamoja na shukrani hizo bado tunaomba msada kwa waislamu wenye moyo wa kujitolea waendelee kutusaidia ili tukamilishe ulipobakia kwa uwezo wa Allah Inshaalah. Kwa yeyote mwenye kutaka kuchangia chochote ulicho nacho wasiliana nasi kwa namba hizi 0717 649313/ 0713 673216/ 0715 874127 au 0657 531367 au unaweza kuka katika msikitini.
11
Makala/Habari
AN-NUUR
SHUKURANI zote anastahiki Mwenyezi Mungu, na inatosha na rehema na amani ziwakie waja wa Mwenyezi Mungu ambao amewachagua. Baada ya utangulizi huo, miongoni mwa vyanzo ambavyo vimechungwa sana na Uislamu ni upande wa hukumu za kisheria, Juu ya wepesi na kuondoa ugumu na kutatua mambo katika dini, na miongoni mwa mambo magumu ambayo yamefahamika katika baadhi ya dini zilizopita. Mwenyezi Mungu amewafundisha waumini kumuomba yeye. Ewe Mola wetu, usitubebeshe tusiyoyaweza kama
ZAIDI ya vijana 2000 walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya Zanzibar wamepatiwa huduma ya kuwawezesha kuacha matumizi ya dawa hizo, ambapo zaidi ya vijana 400 wameweza kuacha kabisa matumizi ya dawa hizo na wanaendelea na harakati zao za kimaendeleo. Hayo yameelezwa na Makamu wa Kwanza wa R a i s Z a n z i b a r, M a a l i m Seifu Sharif Hamad, Jumapili iliyopita wakati akizindua Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Kudhibiti wa Dawa za Kulevya, katika haa iliyofanyika Jumba la Wananchi Forodhani. Tume hiyo imeanzishwa kufuatia mabadiliko ya sheria namba 12 ya mwaka 2011, juu ya udhibiti wa dawa za kulevya, ambayo kwa sasa inatoa mamlaka kamili ya kisheria katika mambano dhidi ya dawa za kulevya
nchini. Serikali ya Zanzibar imeamua kuandaa programu mbalimbali kwa ajili ya kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya, chini ya osi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa huduma za nyumba za kurekebisha tabia sober houses kwa ajili ya vijana walioamua kuachana na matumizi ya dawa hizo. Alisema hayo ni mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa mpango huo kwa miaka mitatu iliyopita. Hata hivyo Maalim Seif amesema mafanikio hayo hayatokuwa endelevu iwapo harakati za usafirishaji, uingizaji na matumizi ya dawa za kulevya hazitoendelea kupigwa vita. Alisema kuna hatari ya vijana kuendelea kuwa wahanga wa matumizi ya dawa za kulevya iwapo juhudi za serikali za kuleta
Inatoka Uk. 1
taifa. Amewata wajumbe wa Tume hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kukia malengo yaliyomo kwenye kauli mbiu ya Zanzibar bila ya dawa za kulevya inawezekana.
Channel zipatazo 36 zitapatikana kwa uhakika ambapo kutakuwa Channel za hapa nchini, michezo, burudani ya tamthilia na sinema za Kiswahili, Kiarabu Kihindi na Kizungu. Alisema pia kutakuwa na Channel nyingi za habari kama vile BBC, CNN, Al-jazira, Deutschewelle, CCTV na nyenginezo. Wa z i r i h u y o a l i s e m a serikali ya Mapinduzi Zanzibar inafanya kila jitihada, kuona kwamba wananchi hawana sababu ya kuhamanika na kununua vingamuzi ghali na
dhaifu hivyo aliwahakikishia kwamba, wataalamu wa serikali wanahangaika ili kuona kituo cha televisheni cha ZBC TV
wanaendelea kukiona bila ya usumbufu hadi Februari 28,2013. Waziri Mbarouk, alisema mabadiliko ya mfumo wa matangazo ya analogue kwenda digital, yamekuja kufuatia agizo lililotolewa na Shirikisho la Mawasiliano la
Afrika Mashariki (EACO) kuwa, nchi wanachama wa Shirikisho hilo zinatakiwa ziwe zimehamia katika mfumo wa digital ikapo mwaka huu.
AN-NUUR
12
KATIBU Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T) Sheikh Ramadhan Sanze.
wa sherehe za Mapinduzi, ambapo tukio hilo limepangwa kufanyika Machi 08, 2013 Rahaleo, mjini Zanzibar pamoja na kusambazwa kwa vingamuzi katika wilaya zote za Zanzibar kwa ajili ya majabio. Tutasambaza vingamuzi vichache katika Wilaya zote za Unguja na Pemba, ili mafundi wetu waweze kuangalia kama matangazo hayo yanaweza kupokewa katika pembe zote za Zanzibar.alisema Waziri Mbarouk. Alisema kuwa vingmuzi kwa ajili ya matumizi ya wananchi vitaanza kuuzwa mwishoni mwa mwezi wa Januari kwa bei ya shilingi 50,000, vikiwa na punguzo la shilingi 22,000 kutoka bei halisi ya vingamizi hivyo na kutakuwa na kulipia ada ya shilingi 8,000 kwa mwezi mmoja. Vi n g a m u z i 3 0 0 , 0 0 0 vinatarajiwa kuuzwa katika kipindi cha miaka miwili. Alisema kuwa vingamuzi hivyo vitakavyosambazwa, Inaendelea Uk. 11
imewezekana kuwakopesha Waislamu kupitia vikundi zaidi ya shilingi milioni mia tano. Akitoa nasaha zake kwa wakufunzi wa mafunzo ya wanakutayba, Sheikh Sanze, aliwaeleza wahitimu hao kuwa, kuhitimu kwao ni mwanzo wa mafanikio makubwa iwapo wanataka. Kwa upande wake Sheikh Mtoe, alitanabaisha kwamba pamoja na mafanikio yenye tija ambayo yanaanza kuonekana k w a Wa i s l a m u k a t i k a kujiletea maendeleo, lakini wasijisahau kwani kuna wenzao wameshapiga hatua kubwa kuliko hiyo waliyokia. Aliwataka wakufunzi hao kuhakikisha kila mmoja, ahakikishe kwamba mipango na mikakati hiyo ya Kutayba Vikundi na Kutayba Saccos, anaikisha katika Msikiti wake na kuizalisha kwa wengine ambao hawajabahatika kuipata taaluma hiyo. Naye Ustadhi Iddi Uvuruge, ambaye ni Meneja mikopo wa Kutayba Saccos, alisema mpaka sasa wana matawi takriban 23 katika mikoa yote nchini na baadhi ya Wilaya. Alisema kupitia Kutayba, zaidi ya shilingi Milioni mia nne, zimetolewa kama mikopo kwa wanachama mbalimbali wa Kutayba Saccos nchini. Ustadhi Uvuruge, aliitaja mikopo hiyo kuwa ni pesa tasilimu, vifaa vya ujenzi, pikipiki zaidi ya mia moja, magari, bajaji pamoja na nyumba. Akianisha aina ya mikopo wanayoitoa, aliitaja kuwa ni Karbanhasana (mikopo mema), inayohusiana na pesa tasilimu kuanzia elfu ishirini hadi milioni moja. Katika mkopo huu, mwanachama akikopa kiasi hicho anatakiwa kurejesha kiasi hicho hicho bila kuongeza kiasi chochote. Aina ya pili ya mikopo ni Mudhwaraba (Mikopo ya kibiashara). Hii ni mikopo inayozidi kiasi cha shilingi milioni moja. Mkopo huu haitolewi pesa tasilimu, bali mwanachama hukopeshwa bidhaa, vifaa, magari au hata nyumba kulingana na mahitaji ya mwanachama. Akizungumzia changamoto wanazokumbana nazo, meneja huyo alisema baada ya huduma hiyo kuwakia Waislamu wengi nchini, kumekuwa na ongezeko kubwa la Waislamu kutoka sehemu mbalimbali wanaohitaji kukiwa au kufungua Kutayba zao. Changamoto nyingine ni uelewa mdogo wa jamii hususani katika mikopo hii ya Mudhwaraba, ambapo ule utaratibu wa kununua kitu kisha ukamkopesha mwanachama kwa bei ya juu anadhani kuwa bado hiyo ni riba.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.