Professional Documents
Culture Documents
YALIYOMO ................................................................................................................................................ 1
SHUKRANI ................................................................................................................................................ 9
ANGALIZO............................................................................................................................................... 12
UTANGULIZI .......................................................................................................................................... 13
MFUKO WA JIKIMU.............................................................................................................................................. 60
MPANGO WA KUPATA FAIDA ..................................................................................................................................60
ANAYESTAHILI KUWEKEZA ......................................................................................................................................60
KIASI CHA CHINI CHA KUWEKEZA ............................................................................................................................61
HATARI ZA UWEKEZAJI ZA MFUKO ..........................................................................................................................61
GHARAMA YA UNUNUZI..........................................................................................................................................62
GHARAMA YA KUUZA KIPANDE (EXIT LOAD) ..........................................................................................................62
MUDA WA ZUIO (LOCK IN PERIOD) .........................................................................................................................62
UKOMO WA UWEKEZAJI NA NYONGEZA YA UWEKEZAJI ........................................................................................62
MPANGO WA GAWIO KATIKA MFUKO WA JIKIMU .................................................................................................63
MFUKO WA UKWASI............................................................................................................................................ 66
UTANGULIZI .............................................................................................................................................................66
MPANGO WA KUPATA FAIDA ..................................................................................................................................67
ANAYESTAHILI KUWEKEZA ......................................................................................................................................67
KIASI CHA CHINI CHA KUANZA KUWEKEZA .............................................................................................................67
HATARI ZA UWEKEZAJI ZA MFUKO ..........................................................................................................................67
GHARAMA YA UNUNUZI..........................................................................................................................................68
GHARAMA YA KUUZA KIPANDE (EXIT LOAD) ..........................................................................................................68
MUDA WA ZUIO (LOCK IN PERIOD) .........................................................................................................................68
UKOMO WA UWEKEZAJI NA NYONGEZA YA UWEKEZAJI ........................................................................................68
HISTORIA YA MREJESHO WA UWEKEZAJI WA MFUKO WA UKWASI .......................................................................69
JINSI YA KUTUMIA KIKOKOTOZI (CALCULATOR) ILIYO KATIKA TOVUTI YA UTT AMIS ........................................... 83
KIKOKOTOZI CHA UWEKEZAJI WA MWEZI (MONTHLY INVESTMENT CALCULATOR) ..............................................85
MPANGO WA KUWEKEZA KILA MWEZI (MONTHLY INVESTMENT PLAN) ...............................................................90
UTT AMIS NA HATI FUNGANI KIPI KINA MREJESHO MKUBWA ........................................................................... 106
MAMBO UNAYOHITAJI KUJUA KABLA NA BAADA YA KUWEKEZA UTT AMIS ..................................................... 109
MIPANGO NA MIKAKATI YA UWEKEZAJI ...............................................................................................................109
MUDA WA UWEKEZAJI ..........................................................................................................................................110
MATARAJIO YA MAPATO YAUWEKEZAJI ...............................................................................................................110
NIDHAMU YAKO YA UWEKEZAJI ............................................................................................................................111
HALI YA UCHUMI YA MUWEKEZAJI .......................................................................................................................111
MPANGO WA KUWEKEZA MARA MOJA NA MPANGO WA KUWEKEZA MARA KWA MARA ............................... 112
RIBA YA KAMPAUNDI KATIKA MFUKO UNAOTOA GAWIO NA AMBAO HAUTOI ................................................ 128
KUENDELEA KUPANDA KWA BEI YA VIPANDE VYA UTT AMIS ............................................................................ 150
(i) Maeneo ambayo UTT AMIS imewekeza .......................................................................................................151
(ii) Riba kutoka katika hati fungani ....................................................................................................................151
(iii) Gawio kutoka katika hisa .........................................................................................................................153
(iv) Kukua kwa thamani ya hisa ambazo mfuko umewekeza .........................................................................153
MADA YA ZIADA KUTOKA KATIKA KITABU CHA NAMNA BORA YA KUWEKEZA KATIKA SOKO LA HISA .............. 161
MLN- Milioni
Simu: +255713999596
WhatsApp: +255713999596
Email wiseinvestorr@gmail.com
@January, 2022
Haki zote zimehifadhiwa. Huruhusiwi kunakili, kurudufu au kutumia kitabu hiki au sehemu ya
kitabu hiki kwa namna isiyokubalika kiuandishi. Mwandishi ametoa kitabu hiki kwa lengo la
kuelimisha na kinapaswa kutumiwa kwa lengo hilo tu na si vinginevyo.
Kwa ajili ya
nimeweza kuandika kitabu hiki ili kuwanufaisha watu wengi zaidi na maarifa
Pili, ninatoa shukrani za pekee kwa wazazi wangu kwa kunilea vyema na kunipa
msingi imara wa elimu. Tatu, natoa shukrani kwa mdogo wangu Chagamba Abel
ambaye alinipa ushauri wa kitaalam kwenye uandishi wa kitabu hiki lakini pia
Kila kitabu hapo kinauzwa TSH 5000/= na viko katika mfumo wa E BOOK
(PDF), FALSAFA YA UWEKEZAJI (page 54), JINSI YA KUSOMA RIPOTI
ZA FEDHA (page 63).
JINSI YA KUTUMIA KITABU HIKI
Kama unatumia pdf reader au WPS OFFICE basi upande wa kushoto kwenye
bookmarks/table of contents utaona yaliyomo na unaweza kubonyeza mada
yoyote ile na itafunguka.
Kundi la pili huwa wanaona kuwekeza kwa miaka 16 ni mtihani ambao hakuna
anayeweza kuufaulu.
Kama wewe ni mmoja wapo wa watu walio katika kundi mojawapo kati ya hayo
yaliyo juu ungana nami ili nikuonyeshe kuwa ina wezekana kuwa na uwekezaji
wenye mrejesho wa asilimia 39% na kwa kundi la pili wataona kuwa kuwekeza
miaka 16 sio kitu kigumu sana bali ni chepesi mno na wataona kuwa unaweza
kutengeneza utajiri wa kudumu kupitia uwekezaji wa pamoja.
Mfuko huu unakuwa hauna idadi maalumu ya vipande (unit) ambavyo inaweza
kuwa nazo, ninacho maanisha ni kuwa vipande vya mfuko wa aina hii vinaweza
kuongezeka kutegemea na idadi ya watu wanaonunua au vikapungua kutegemea
na idadi ya watu ambao wanauza vipande vyao. Mfano wa kampuni ya namna ni
UTT AMIS. Muhimu kuhusu kampuni ya namna hii ni kuwa muda wowote
unaweza kununua vipande kama utahitaji na muda wowote unaweza kuuza
vipande kama utahitaji kufanya hivyo, kwa sababu hauna idadi maalumu ya
vipande ambavyo inaweza kuwa navyo.
Hii ni aina ya mfuko wa uwekezaji wa pamoja ambao una idadi kamili ya vipande
na haiongezeki kulingana na uhitaji au kupungua pale ambapo watu wanauza
vipande vyao, wakati mfuko huu unaanzishwa unakuwa na idadi maalumu ya
vipande na baada ya vipande vile kuuzwa basi kama ukihitaji kipande lazima
atokee mtu aliye nunua awali ndio akuuzie na kama akiwa hayupo basi hauwezi
kupata vipande,na kama unataka kuuza pia lazima apatikane mteja wa kununua
vipande vyako kama mteja hatapatikana basi hauwezi kuuza vipande vyako.
Mfano, kama mfuko unaanzishwa ulikuwa na vipande 1000 basi kama ukitaka
kununua vipande 100 basi lazima apatikane mtu akuuzie na baada ya kukuuzia
vipande vitabaki 1000. Mfano wa kampuni ya namna hii hapa nchini Tanzania ni
NICOL na TCIL ambazo ziko soko la hisa la DSE.
KIPANDE NI NINI?
Yamkini umekutana na neno kipande au vipande kwenye andiko hili na unajiuliza
kuwa kipande ni nini. Katika uwekezaji, kipande ni umiliki ulionao katika
uwekezaji ambao unafanywa na kampuni ya uwekezaji wa pamoja iliyo wazi
(open ended mutual fund). Mfano, kama mmekusanyika watu 4 na kununua
shamba la heka moja kwa gharama ya milioni moja sasa kutegemea na kila mmoja
amechangia kiasi gani kila mmoja atakuwa na kipande cha shamba kutegemea na
umiliki alio nao, mfano kama umechangia laki 5 basi kipande chako ni nusu na
kama mwingine amechangia laki mbili na nusu basi kipande chake ni robo.
Mfuko kama una ukubwa wa shilingi bilioni moja basi unagawaywa katika
vipande vidogo vidogo ambavyo kwa ujumla wake vinakuwa sawa na ukubwa wa
mfuko, hivi vipande vinauzwa kwa bei ndogo na unaponunua kipande kimoja basi
hiki kipande kinakuwa moja kati ya thamani ya mfuko. Nchini Tanzania tunao
mfuko wa uwekezaji wa Pamoja unaojulikana kwa jina la UTT Amis. Katika
kitabu hiki tutapata fursa ya kujifunza kwa pamoja namna ya kuwekeza kwenye
mfuko huu wa UTT Amis.
UTT AMIS ni kifupi cha Unit Trust of Tanzania Asset Management and
Investor Services. UTT AMIS ni mfuko wa uwekezaji wa pamoja ulio wazi (open
ended mutual fund) ambao ulianzishwa mwaka 2003 kama UTT na baadae
mwaka 2013 ukaiitwa UTT AMIS. UTT AMIS ni taasisi ya serikali iliyo chini ya
Wizara ya fedha na Mipango.
FAIDA YA 1
Kama ukitaka kuwekeza wewe mwenyewe katika hisa lazima uwe na uelewa na
masuala ya hisa, jinsi gani ya kuchagua kampuni ya kuwekeza na jinsi gani ya
kukabiliana na hatari za uwekezaji, muda gani sahihi wa kuwekeza na mambo
kadha wa kadha. Lakini kupitia UTT AMIS unapata nafasi ya kukutana na meneja
mwenye utaalamu wa masuala ya uwekezaji ambaye kazi yake kila siku ni
kusimamia pesa yako, kuhakikisha inawekezwa mahali sahihi na inakupa faida
shindani. Kwa kuwekeza UTT AMIS unaweza kuwekeza leo na ukaamua kwenda
safari ya miaka na ukirudi utakuta meneja amesimamia pesa zako vizuri.
FAIDA YA 2
UKWASI ((LIQUIDITY)
Moja kati ya vitu ambavyo utaipenda UTT AMIS ni urahisi wa kununua na kuuza
vipande, kama umewekeza katika hisa utafahamu ya kuwa ili uweze kununua hisa
lazima awepo mtu wa kukuuzia na kama hakuna mtu wa kukuuzia hisa basi
hauwezi kununua. Pili, kama unataka kuuza hisa lazima awepo mteja wa kununua
na mara kadhaa nimeona watu wanakaa na hisa miezi bila kupata mtu wa
kununua hisa zao ila UTT AMIS ni rahisi mno kununua na kuuza vipande kwani
pale ambapo unanunua vipande ni meneja wa mfuko ndio anakuuzia na kama
tulivyoona hapo juu mfuko ulio wazi (open ended mutual fund) hauna ukomo wa
vipande muda wowote unapohitaji vipande basi unaweza kuvipata. Aidha
kutokana na aina ya mfuko uliowekeza ndani ya UTT AMIS, pale ambapo unataka
kuuza vipande vyako, hauna haja ya kusubiri mpaka mteja apatikane kwani
meneja wa mfuko ndio anayenunua vipande vyako. Kuna baadhi ya mifuko ndani
ya UTT AMIS inakuwezesha kupata pesa yako ndani ya siku 10 za kazi baada ya
kujaza fomu ya kuomba kuuza na kuna mifuko kama mfuko wa ukwasi ni ndani
ya siku 3 za kazi unaipata pesa yako.
FAIDA YA 3
UWEKEZAJI MSETO
FAIDA YA 5
Ukitaka kuwekeza pesa benki ili upate riba ndani ya mwaka mmoja sio kitu cha
ajabu ukapokea riba ya 3% au kama utataka upate riba kubwa basi lazima uwe na
kiasi kikubwa cha pesa ila ukiwa na UTT AMIS kwa kiasi kidogo tu unaweza
kupata faida nzuri ambayo hauwezi kuipata benki huku ukiwa na uwekezaji
mdogo.
Ngoja nitoe mfano, kama una 100,000/= hauwezi kuwekeza katika hati fungani ya
miaka 25 (maana kiwango cha chini cha kuwekeza katika hati fungani ya muda
mrefu ni TSH 1milioni) ila kama ukikusanya rafiki zako 9 wenye laki moja
mnaweza kuwekeza hela yenu kwa pamoja na mkapata mrejesho wa asilimia
15.95% (mrejesho unaotolewa na hati fungani ya miaka 25) kwa mwaka, ambayo
mtagawana kila mmoja kulingana na kiasi chake alichoweka. UTT AMIS pia
inafanya kazi kwa mfumo huu ambapo unaweza kuwekeza katika hati fungani
kwa kiasi cha shilingi 50,000/= tu kupitia mfuko wa hati fungani (bond fund).
Mfano wa pili ni kama unahitaji kuweka pesa benki ili upewe riba kubwa lazima
uwe na kiwango kikubwa cha pesa lakini kupitia UTT AMIS unaweza kuwekeza
pesa kwa riba kubwa kwani pesa yako inakusanywa pamoja na wawekezaji
wengine na inawekezwa kwa pamoja kwa wingi wake.
FAIDA YA 6
Kufanya uchunguzi wa mifuko ya UTT AMIS ni rahisi mno ambavyo hata kama
sio mtaalamu wa uwekezaji unaweza kufuatilia jinsi mfuko unavyoenda bila shida
ikilinganishwa na kufanya uchunguzi wa kampuni ya kuwekeza kupitia soko la
hisa. Kiufupi ufuatiliaji wa uwekezaji wa UTT AMIS ni rahisi sana na hauchukui
muda.
FAIDA YA 7
MWAKA RIBA
1 500
2 500
3 500
4 500
5 500
JUMLA 2500
Hivyo kwa miaka mitano, mwekezaji huyu atapata faida iliyotokana na riba
iliyolipwa kwenye uwekezaji wake wa TSH 10,000/- kiasi cha TSH 2500. Mara
baada ya uwekezaji huu kukamilika, mwekezaji atarudishiwa shilingi 12500/-
ikiwa ni pamoja na fedha aliyoiwekeza. Hati fungani za serikali zinatumia riba
rahisi kulipa watu wanaoikopesha serikali.
Riba nyingine inaitwa riba ya kampaundi, usiombe mtu akukopeshe fedha kwa
riba ya kampaundi utaomba ardhi ipasuke au uwe na nguvu za kutoonekana ili
anayekudai akija asikuone. Wawekezaji makini wanapenda nguvu iliyo katika
riba ya kampaundi. Unaweza ukawa unajiuliza ni kwa nini wanaipenda sana hii
riba?, basi kupitia kitabu hiki tuone riba hii inafanyaje kazi.
Riba ya kampaundi inakuwa na utofauti na riba rahisi kwa kigezo cha kuwa
katika riba ya kampaundi baada ya kupokea riba mwaka wa kwanza ile riba
inakuwa sehemu ya mtaji nayo mwaka unaofuata inapokea riba, mfano wetu hapo
juu kama ungekuwa umeweka hela benki 10000/= kwa riba ya 5% ila ni riba ya
kampaundi ina maana mwaka wa kwanza ungepokea 500/= ila mwaka wa pili hii
500/= inaungana na 10000/= zote zinapokea 5%, kwa hiyo mwaka wa pili itakuwa
5% ya 10500/= ambayo riba yake itakuwa 525 kwa mwaka wa pili.
MWAKA RIBA
1 500
2 525
3 551.25
4 578.8
5 607.75
jumla 2762.8
Nadhani mpaka hapo umeona utofauti uliopo kati ya hizi riba mbili kwani
mwisho wa siku jumla ya hela yako inakuwa 12762.8 ambapo ni ongezeko la
262.8/= unaweza kusema 262.8 sio nyingi tukiongeza miaka 5 tena unaweza kuona
maajabu ya utofauti kwani kadri muda unavyoenda ndivyo tofauti inakuwa kubwa
UTT AMIS inatumia riba ya kampaundi katika mifuko yake na ndio moja ya kitu
ambacho kinafanya UTT AMIS iwe kipenzi cha wawekezaji wengi makini, hapo
mbele tutaona jinsi riba ya kampundi ya UTT AMIS ilivyo.
MREJESHO WA UWEKEZAJI (RETURN ON INVESTMENT) (ROI)
Sidhani kama kuna siku niliwahi kufundisha uwekezaji bila kugusia hii maana ni
muhimu sana, katika kitabu changu namna bora ya kutengeneza hela katika
soko la hisa nimeelezea hii kwa kirefu hapa nitatoa pointi chache tu.
Faida 500000/=
Mtaji 1000000/=
Mfano wa pili
Kuna mtu nilimpa swali nikamuuliza hivi mtu aliyenunua kipande kwa bei ya
TSH 1000/= na baada ya mwaka mmoja akauza kwa bei ya 2000 na mtu alinunua
kipande kwa bei ya 70 baada ya mwaka akauza kipande kwa bei ya 170 nani
amepata faida kuliko mwenzake? akajibu mtu wa kwanza nikajua huyu sio
muwekezaji, kwani wawekezaji tunafikiri tofauti kidogo hebu tuone mirejesho
yao
Mtu wa kwanza
Mtu wa pili
Kati ya 100% na 142% ipi kubwa, kama jibu lako ni 142% basi umeanza kufikiri
kama muwekezaji.
Kuna baadhi ya watu hawalijui hili yeye anachojua ni kuwa kipande kimepanda
bei tu, bila kujua faida yake ni shilingi ngapi, ila unatakiwa ujue kuwa japo
vipande vyote vinaweza kuwa vimepanda bei ila kuna vipande vimepanda bei
kubwa kuliko vipande vingine na unapojua mrejesho wa uwekezaji unakuweka
katika nafasi nzuri ya kujua wapi panakupa faida kubwa na wapi uwekeze ili
upate faida nzuri.
Kwa hiyo unaposikia kuwa mfuko una mrejesho wa 12% au 14% ina maana kuwa
asilimia 12% au 14% ndio inakurudia kama faida kwa mwaka huo, kama ulikuwa
umewekeza 100/= na mrejesho wa uwekezaji ukawa 12% ina maana faida yako ni
TSH 12/= kwa mwaka huo.
Kwa maelezo zaidi ya mrejesho wa uwekezaji unaweza kusoma pia kitabu changu
cha namna bora ya kutengeneza hela katika soko la hisa.
Hii ni njia ya pili ambayo ina mnufaisha muwekezaji hii ni pale ambapo unanunua
kipande kwa bei ya chini na kukiuza kwa bei ya juu. Mfano umenunua kipande
kwa bei ya 100/- na baada ya muda bei ikapanda kufikia 200/= ukauza faida
ambayo umeipata ndio ukuaji wa mtaji na hata kama haujauza hiyo iliyoongezeka
ndio faida yako.
SEHEMU YA PILI
Kwa hiyo tunaposema mfuko umewekeza katika hati fungani au amana za benki
basi mapato yake yana uhakika kwa asilimia kubwa kwa hiyo mfuko huo una
hatari za chini za uwekezaji, na tutaona chini kuwa mifuko hii haina mabadilko
makubwa sana ya mrejesho wake mwaka kwa mwaka.
Katika kitabu changu cha hisa nimezungumzia namna ambavyo uwekezaji mseto
unasaidai kupunguza hatari za uwekezaji.
Kwa hiyo mifuko ya UTT AMIS imegawanyika katika makundi mawili kulingana
na hatari za uwekezaji: hatari za chini kwa mifuko iliyowekeza katika mapato ya
kuaminika na hatari za wastani kwa mifuko iliyowekeza katika hisa na pia katika
mapato ya kuamika. Ukisikia mfuko una hatari za wastani basi ujue una hisa
ndani yake na mfuko ambao una hatari za chini hauna hisa ndani yake.
Aidha, kwenye uwekezaji katika mfuko wa UTT AMIS, kuna mipango ya aina
mbili inayotofautisha vipande vyake. Kuna mpango wa gawio na mpango wa
kukuza mtaji. Mpango wa gawio una maana ya kuwa mifuko iliyo chini ya mpango
huu inalipa gawio kwa wawekezaji wakati mifuko iliyo kwenye mpango wa
kukuza mtaji yenyewe hailipi gawio isipokuwa uwekezaji wake unaongezeka
kutokana na kukua kwa mtaji wa mwekezaji kutokana na bei ya vipande katika
mfuko kupanda. Ikiwa umeamua kuwekeza kwenye mifuko inayopatikana chini
ya UTT AMIS ni dhahiri utakutana sana na maeno haya ya mpango wa gawio na
mpango wa kukuza mtaji, hivyo nitaeleza kwa undani kidogo na kwa mifano
kuhusu hii mipango:-
Mpango wa gawio
Kama mfuko una mpango wa gawio ina maana mfuko una utaratibu wa kulipa
gawio, kwani katika mifuko ya UTT AMIS kuna mifuko miwili ambayo inatoa
gawio na kuna mifuko ambayo haitoi gawio, kwa hiyo ukisikia mfuko una mpango
wa gawio katika maelezo hapo chini basi ujue mfuko huo una toa gawio.
Katika mfuko wa UTT AMIS mpaka wakati kitabu hiki kinaandikwa, kuna
mifuko minne ambayo hailipi gawio ila muwekezaji anapata faida kwa njia ya
kukua kwa mtaji. Mtu mmoja akaniuliza kukua mtaji maana yake nini, iko hivi
unaponunua kipande kwa bei ya 100/= na baada ya kununua bei ikapanda kufikia
230/= ina maana hapo faida yako ni 130/=, hapa haujapewa gawio ila faida yako
unaipata pale ambapo kipande kinakuwa kimeongezeka thamani. Mtu mwingine
akauliza bro chagamba hapa sasa ina maana kama bei inakuwa imeshuka nakuwa
nimepata hasara jibu ni ndio ila tutaona mbele nitakapozungumzia kwa nini
kipande cha UTT AMIS kimekuwa kikipanda siku hadi siku utaona kwa nini
kipande hakiwezi kushuka na kukaa bei ile ile kwa miaka kama ilivyo hisa.
Mpango wa kukuza mtaji ni pale ambapo unanunua kipande kwa bei ya chini na
kinakuwa na kuongezeka thamani wewe unapata faida kwa ile tofauti, kama ilivyo
kwenye hisa kuwa unanunua kwa bei ya chini na unauza kwa bei ya juu.
MAANA YA MANENO MUHIMU
(i) Gharama ya kununua kipande
Hii ni gharama ambayo unakatwa pale ambapo unauza kipande. Gharama hizi
zinajulikana kwa jina la kiingereza la “exit load”. Hii inakuwa ni asilimia kadhaa
ya mauzo yaliyofanyika. Kwa baadhi ya mifuko inatoza gharama hii endapo
muwekezaji atauza vipande vyake.
(iii) Repurchase
Hiki ni kitendo cha kuuza vipande, unapouza vipande ndio inaitwa repurchase,
hapa maana yake ni kuwa meneja wa mfuko ananunua vipande kutoka kwa
muwekezaji, pale unapouza vipande vyako meneja wa mfuko ndio anayenunua
vipande kutoka kwako na hiki kitendo ndio kinaitwa repurchase
Hiki ni Kipindi ambacho unazuiliwa kuuza vipande vyako, kipindi hiki kikiisha
unaruhusiwa kuuza vipande vyako, tutaona kuna mifuko ambayo unazuiliwa
kuuza vipande ndani ya muda fulani.
(v) Acceptance date
Hii ni siku ambayo oda yako ya kuuza vipande au oda yako ya kununua vipande
inapokelewa na meneja wa mfuko au wakala wa UTT AMIS
Una weza kununua vipande siku yoyote ya kazi, siku ambayo soko la hisa, benki
kuu na benki nyingine zinakuwa wazi ila siku ambazo sio za kazi na siku ambayo
UTT AMIS wanakuwa wanafunga vitabu vyao ambayo inatokea mara kadhaa na
inatangazwa hautaweza kununua vipande kwa siku hiyo.
Mara baada ya kueleza kinaga ubaga kuhusu hatari za uwekezaji katika uwekezaji
huu, mpango wa uwekezaji unaozingatiwa na mwekezaji na kujadili maneno
muhimu kwenye uwekezaji kwa njia hii, sasa twende kujadili mifuko mbalimbali
ya uwekezaji iliyo chini ya UTT AMIS ili mpendwa msomaji uweze kujua kila
mfuko kwa upana wake.
MFUKO WA UMOJA
UTANGULIZI
Huu ndio mfuko wa kwanza kuanzishwa kati ya mifuko yote ya UTT AMIS na
mfuko huu ulianzishwa mwaka 2005, mfuko huu ni mfuko wa wazi (open
endend) na wakati unaanzishwa ulianzishwa ukiwa na mpango wa gawio ila
mwaka 2006 ulibadilishwa na kuwa wa mpango wa kukuza mtaji, mfuko huu
wakati unaanzishwa bei ya kipande ilikuwa TSH 70 (hii ni kwa sababu serikali
ilitoa punguzo la bei ila thamani ya kipande ilikuwa TSH 100.
MFUMO WA UWEKEZAJI
Mfuko huu una uwekezaji katika hisa na katika hati fungani za serikali na za
makampuni binafsi. Uwekezaji katika hisa kwenye mfuko huu unatakiwa usizidi
50% ya uwekezaji wote wa mfuko na kiasi kingine kitawekezwa katika maeneo
mengine yenye mapato ya kuaminika.
Mchoro Na. 1: Hali ya mgawanyo wa uwekezaji katika mfuko wa Umoja mpaka kufikia tarehe 30 June 2021
Kama unavyoona katika jedwali juu ni kuwa kiasi cha asilimia 41.2 kimewekezwa
katika hisa katika mfuko huu na 46.2% imewekezwa kwenye hatifungani za
serikali, 9% ziko kwenye hatifungani za makampuni binafsi na takribani 3.5%
zimewekezwa kwenye uwekezaji mwingine.
GHARAMA YA UNUNUZI
Unavyonunua kipande katika mfuko huu hakuna gaharama zozote ambazo
unakatwa, unauziwa kipande kwa bei ambayo iko sokoni.
KUUZA VIPANDE
Unaruhusiwa kuuza vipande vyako siku yoyote ya kazi (isipokuwa siku za
mahesabu au siku ambayo UTT AMIS imetangaza kuwa mauzo hayatakuwepo) na
pesa yako utaipata ndani ya siku 10 za kazi. Kitu kingine ni kuwa, unaweza kuuza
vipande vyako nusu yake au vipande vyote ulivyonavyo, mfano kama una vipande
1000 unaweza kuuza vipande 100 na vipande vingine vikabaki au ukauza vipande
vyote 1000 au idadi yoyote unayoitaka.
UKOMO WA UWEKEZAJI NA NYONGEZA YA UWEKEZAJI
Mfuko huu hauna ukomo wa muda wala ukomo wa kiasi ambacho unaweza
kuwekeza. Maana yake ni kuwa unaweza kuwekeza mara nyingi uwezavyo na
kwa muda wote, kama tulivyoona kiasi cha chini cha kuwekeza ni vipande 10 ila
unaweza kuwa unaongeza kadri uwezavyo hakuna ukomo wa kiasi cha kuwekeza
kwenye mfuko huu.
Jedwali Na. 1: Historia ya mrejesho wa uwekezaji (ROI) wa mfuko wa Umoja mpaka Septemba 30, 2021
UTANGULIZI
Huu mfuko ulianzishwa mwaka 2007. Mfuko huu una mpango wa kuwekeza kwa
miaka 10 yaani baada ya miaka 10 uwekezaji wako unakuwa umefika kikomo na
unaweza kuchukua fedha yako yote lakini baada ya miaka 5 unaweza pia
kuchukua fedha yako hadi asilimia 75 ya hela uliyowekeza. Wakati mfuko
unaanzishwa bei ya kipande ilikuwa TSH 100.
1) Uwekezaji
2) Bima (insurance)
BIMA
Kwa upande wa bima kuna vitu viwili, bima ya maisha (kifo au ulemavu wa
kudumu) na ajali binafsi (personal accident). UTT AMIS wanatoa bima hizi kwa
wawekezaji iwapo kifo, ulemavu au ajali binafsi itatokea kwa mwekezaji. UTT
AMIS wanatumia kampuni inayotoa huduma za bima inayoitwa Alliance
Insurance Corporation Limited.
Kwa kuwa uwekezaji kwenye mfuko huu ni wa miaka kumi (10) mpaka kuiva,
tangu mfuko huu uanzishwe mnamo mwaka 2007, uwekezaji wa kwanza uliiva
(kufika kikomo) mnamo mwaka 2017. Katika mfuko huu, mara baada ya
uwekezaji kuiva, mwekezaji anaweza kufanya lolote kati ya mambo haya
yafuatayo:-
MPANGO WA UCHANGIAJI
Mfuko huu una mpango wa uchangiaji ambapo, mwekezaji anaainisha kiasi cha
fedha anachokuwa anachangia kwenye mfuko kwa miaka yote kumi (10).
Uainishaji wa kiwango cha uwekezaji unafanywa mwanzoni mwa
uwekezaji/wakati wa kufungua akaunti kwenye mfuko. Mfano, kama umepanga
kuwekeza TSH I milioni au kiwango chochote kile katika miaka yote kumi ndio
kiasi ambacho ninakizungumzia. Kiasi hiki mwekezaji anaweza kuamua
kukiwekeza chote kwa mara moja au akawekeza kiasi hiki kidogo kidogo ili mradi
mwisho wa miaka 10 hiki kiasi ambacho mwekezaji ameainisha kitimie. Kwenye
mfuko huu unaweza kuchagua kiasi chochote kile cha uwekezaji ila ni kwamba
kiasi hicho kisipungue TSH 1 milioni. Kiasi kinachowekezwa mara baada ya
shilingi milioni 1 kiwe katika ongezeko la Tsh 1000 na sio chini yake.
Angalizo
ANAYESTAHILI KUWEKEZA
Katika mfuko huu mtu ambaye anaweza kuwekeza ni mtanzania (Resident
Individual Tanzanians) au mtanzania asiye mkazi (non resident individual
Tanzanians) mwenye umri wa miaka 18 mpaka 55.
Hapa mwekezaji anachagua kiasi ambacho anataka kuwekeza katika miaka yote
10 na baada ya hapo unachagua kuwa utakuwa unachangia kila mwezi au kila
baada ya miezi sita au utakuwa unachangia kila mwaka mara moja, na baada ya
kujua muda ambao utakuwa unachangia unaangalia kiasi gani ambacho unatakiwa
uwe unachangia kwa muda ambao umeuchagua.
Tuangalie kama ukitaka kuwekeza TSH 1 milioni ndani ya miaka kumi katika
mpango wa kuchangia kila mwezi, miezi sita au mwaka inakuwaje, angalia jedwali
hapo chini.
Kiasi cha mpango Changia kila mwezi Kila baada ya miezi 6 Changia kila mwaka
1 milioni 8340 50,000/= 100,000/=
Maelezo ya Jendwali
Mfano, kama umeamua kuwa katika uwekezaji wako unataka kuwekeza TSH 1
milioni (ndani ya miaka 10) basi kama utachagua mpango wa kuchangia kila
mwezi itakubidi kuchangia TSH 8340/= na kama utachagua kuchangia kila baada
ya miezi sita ina maana utakuwa unachangia TSH 50,000/= na kama utachagua
kuwa utakuwa unachangia kila mwaka basi itakubidi kuchangia TSH 100,000/=
kila mwaka kwa miaka 10, kusudi hapa ni kuwa baada ya miaka 10 kufika uwe
umechangia kiasi cha TSH 1 milioni kama ulivyoainisha katika mpango wako. Na
kama utachagua kiasi chochote kile basi mahesabu yatakuwa hivyo.
Mfano wa 2
Chakulia unataka kuwekeza TSH 1.5 milioni katika mpango wako wa miaka 10
(ina maana ndani ya miaka 10 uwe umechangia TSH 1.5 milioni) sasa kama
utachangia kila mwezi ina maana ndani ya miaka 10 kuna miezi 120, sasa
unachukua hii TSH 1.5 milioni unagawanya kwa miezi 120 kujua utakuwa
unachangia kiasi gani kila mwezi
Kwa hiyo itakubidi kuchangia 12,500/= kila mwezi ili kutimiza kiasi ambacho
unatakiwa kuchangia
Kama utaamua kuchangia kila baada ya miezi sita ina maana katika miaka 10, kuna
jumla ya vipindi 20 vya miezi sita, hivyo itakuwa TSH 1.5 milioni kugawanya kwa
20 ambayo ni sawa TSH 75,000/= kila baada ya miezi sita.
Hapa unachukua kiasi ambacho unataka kuwekeza kwa miaka yote kugawanya
kwa 10, ambayo ni TSH 1.5 milioni kugawanya kwa 10 ambayo ni sawa na TSH
150000/= kama utachagua kuwekeza mara moja kwa mwaka itakubidi uwekeze
kiasi hicho.
2) UCHANGIAJI WA MARA MOJA
Hapa muwekezaji analipa mwenyewe kiasi cha fedha ambacho anatakiwa kulipa
kutokana na mpango wa uchangiaji wake aliochagua. Mfano, kama umechagua
kuchangia kila mwezi basi unaweza kuwa kila mwezi unapeleka hela wewe
mwenyewe UTT AMIS au kupitia mawakala wake.
Hapa muwekezaji anaweza kuelekeza kuwa pesa itoke benki kwenda UTT AMIS,
na benki itafanya kama alivyoelekeza muwekezaji, Kwa hiyo, badala ya
muwekezaji kuwa anapeleka pesa UTT AMIS, basi benki yake inakuwa inafanya
hivyo kwa niaba yake.
Kwa wale walioajiriwa, mwajiri anaweza kuwa anatumiwa kulipa moja kwa moja
fedha kwenda UTT AMIS.
GHARAMA YA UNUNUZI
Unavyonunua kipande katika mfuko huu hakuna gaharama zozote ambazo
unakatwa, hivyo kipande kinauzwa kwa bei ya soko kwa siku ambayo
muwekezaji ananunua kipande hicho.
Jedwali Na. 2: Historia ya rejesho la uwekezaji (ROI) ya mfuko hadi kufikia Septemba, 30, 2021
B* Katika mwaka wa kumi pia hakuna malipo kama mpango wa uwekezaji ni wa mwaka ila kama ulikuwa na
mpango wa mwezi na kuna kiasi ambacho bado hakijalipwa basi hicho kiasi ndio kitakuwa kama fidia.
Tanbihi: Katika mpango huu wa kuwekeza mara kwa mara fidia ya bima ni kiasi
kile ambacho hakijalipwa katika mpango wako uliochagua ila kiasi cha bima
hakitazidi milioni 25. Hapa ina maana kuwa, kama mpango wako ni milioni 100 na
ukapata ulemavu wa kudumu au kufariki mwaka wa pili wa uchangiaji, basi bima
inayotakiwa kulipwa ni TSH 80 milioni, lakini kwa kuwa kiwango cha juu cha
bima ni TSH 25 milioni basi utapewa TSH 25 milioni kama fidia.
Hapa muwekezaji atapata fidia sawa na kiasi alichowekeza katika mpango wake
ila kiasi cha juu ni TSH 25 milioni ina maana kama muwekezaji ameweka 10
milioni basi atalipwa 10 milioni kama fidia kwa miaka yote 10 ya uwekezaji wake
ila kama amewekeza kiasi zaidi ya 25 milioni basi fidia yake itakuwa milioni 25 tu.
A* hapa muwekezaji kama atapata ulemavu wa kudumu au kifo hakuna fidia itakayotoka isipokuwa kifo au
ulemavu umesababishwa na ajari ambapo fidia itakuwa milioni 10.
Jedwali hapo chini linaonesha mfano wa bima inayolipwa kwa muwekezaji wa
mara moja aliyewekeza kiasi kinachozidi TSH 25 Milioni kwenye mfuko huu
Tanbihi: Katika mpango wa kuwekeza kwa mara moja (single contribution) fidia
ya bima inakuwa sawa na kiasi ambacho muwekezaji amechangia isipokuwa kwa
kiasi cha uwekezaji kilicho juu ya TSH 25milioni fidia itakayolipwa kwa
muwekezaji ni shilingi 25 Milioni.
Kuna bima ya msiba ila hii kutokana na maelezo ya kitabu cha ofa cha wekeza
maisha ni kwa ajili ya wawekezaji ambao walinunua vipande kwa mara ya kwanza
kabisa wakati mfuko unaanzishwa.
Hitimisho kuhusu Bima
KUFUFUA UANACHAMA
Mwanachama anaweza kufufua uanachama wake ndani ya mwaka mmoja toka
siku ambayo alishindwa kulipa kama atalipa michango yote iliyopita tangu
alipoishia. Mwanachama anaweza kutumia nafasi ya kufufua uanachama mara
mbili tu ndani ya kipindi chote cha uwekezaji wake kwenye mfuko. Hii
inamaanisha kuwa ndani ya miaka kumi (10) ya uwekezaji, mwekezaji anazo
nafasi mbili tu za kufufua uwekezaji wake ikiwa atashindwa kuweka mchango
wake kwa wakati.
MFUKO WA WATOTO
UTANGULIZI
Mfuko huu ulianzishwa mwaka oktoba mwaka 2008. Mfuko huu unalenga
kumsaidia mtoto wa kitanzania katika masomo yake. Bei ya kipande wakati
mfuko unaanzishwa ilikuwa TSH 100/=. mfuko huu ni wa wazi (open ended).
Katika mpango huu, mtoto husika atalipiwa pesa mara mbili au mara moja kwa
mwaka kwa njia ya ufadhili wa masomo. Malipo hayo yanalipwa kwa awamu moja
au mbili kulingana na mwongozo wa wazazi au walezi wa mtoto husika. Malipo
haya yanafanywa baada ya mtoto kufikisha umri wa miaka 12. Katika mpango huu
mzazi au mlezi wa mtoto atakuwa na uhuru wa kuchagua kati ya vipindi vitatu
ambavyo mtoto atahitaji kulipiwa huu ufadhili wa kimasomo. Vipindi vitatu ni
wakati mtoto akiwa na miaka 12-18, 19-24, 12-24.
Kwenye skimu hii mzazi au mlezi anaweza kuchagua muda gani atahitaji ufadhili
huu uanze kulipwa kwa mtoto. Mfano, kama unajua kutoka miaka 12 mpaka 18
unaweza kuwa na uwezo wa kumlipia mwanao ada, ila ukahitaji kuwa akifikisha
miaka 19 ndio aanze kulipiwa basi UTT AMIS itafanya hivyo au kama utahitaji
kwa miaka yote yaani kuanzia miaka 12 mpaka 24 mtoto awe analipiwa basi UTT
AMIS itafanya hivyo.
Ili kupata fedha za kulipia mtoto ufadhili wa masomo, UTT AMIS wanauza
vipande ambavyo mwekezaji amewekeza. Hivyo, uchaguzi wa mpango wa
uchangiaji uliofanywa utaathiri kiasi na idadi ya muda wa ulipaji wa ada ya mtoto
husika.
Utofauti wa vipindi vya ufadhili Idadi ya vipindi pamoja na idadi ya ulipaji wa ufadhili
12-18 19-24 12-24
Ufadhili mara mbili kwa mwaka 14 12 26
Ufadhili mara moja kwa mwaka 7 6 13
Jedwali Na. 3: Jedwali linaonesha idadi ya vipindi na idadi ya ulipaji wa ufadhili
Jedwali hapo juu linaonesha namna ufadili unavyofanywa kwa vipindi tofauti
tofauti. Mathalani, kama umechagua kuwa kipindi cha ufadhili wa mwanao kiwe
pale anapotimiza miaka 12 mpaka 24 ina maana kama utachagua awe analipiwa
mara mbili kwa mwaka basi kutakuwa na vipindi 26 vya malipo na kama
utachagua kuwa awe analipiwa mara moja kwa mwaka basi kutakuwa na vipindi
13 vya malipo.
Mfano
Tuchukulie una mtoto ambaye umewekeza vipande 24,000 na ukachagua kipindi
chake cha kulipiwa ufadhili wa masomo kiwe kati ya miaka 19 mpaka 24, hapa ina
maana kuwa kwa mpango wa kulipiwa mara moja kwa mwaka atalipiwa mara 6
na kwa mpango wa kulipiwa mara mbili kwa mwaka atalipiwa mara 12.
Kwa kutumia idadi ya vipande vilivyoainishwa kwenye mfano hapo juu (24,000),
kwa hiyo 24,000 kugawanya kwa 12 ni sawa na 2000. Hivyo, kwa miaka yote, kila
baada ya miezi sita vipande 2000 vitakuwa vinauzwa ili mtoto aweze kulipiwa
ufadhili wa masomo.
Hapa ukichukua vipande 24,000 kugawanya kwa miaka sita ina maana vipande
4000 vitakuwa vinauzwa kila mwaka ili kulipa ufadhili wa mara moja kwa
mwaka.
Aidha, katika mfuko huu, kiwango cha chini cha udhamini wa masomo ni TSH
20000/=. Hii inamaana kuwa, kama muwekezaji atachagua mpango wa udhamini
wa masomo kwa mwaka mara 2 basi kiwango cha chini ambacho kinatakiwa
kulipwa kwa kila udhamini ni 20000/= chini ya hapo utahamishiwa kwenye
mpango wa kukuza mtaji.
Hapa mtoto hatalipiwa kitu chochote na mfuko ila atapata faida kwa ukuaji wa
kipande.
ANAYESTAHILI KUWEKEZA
Anayepata faida katika kuwekeza katika mfuko huu ni mtoto wa kitanzania
mkazi au asiye mkazi mwenye umri chini ya miaka 18. Mzazi au mlezi anawekeza
kwa niaba ya mtoto ambaye yuko chini ya umri wa miaka 18. Mtoto anaweza
kuwekezewa pesa na wazazi wake au walezi au taasisi yoyote ya kiserikali au
isiyo ya kiserikali. Ili kuondoa mashaka yoyote, lazima utambulisho wa mtoto
ambaye ni mnufaika wa uwekezaji huu uwekwe wazi na mtu anayetuma maombi
ya kufungua akaunti kwa ajili ya mtoto.
Kiasi cha chini cha kuwekeza katika mfuko huu ni TSH 10,000/= na uwekezaji wa
nyongeza ni TSH 5,000/=. Tunapozungumzia uwekezaji wa nyongeza maana yake
ni kama unataka kuongeza kuwekeza baada ya kuwekeza kwa mara ya kwanza,
kima cha chini cha kuongeza ni TSH 5000/= ila hakuna ukomo wa kiasi ambacho
unaweza kuongeza kuwekeza.
GHARAMA YA UNUNUZI
Unavyonunua kipande katika mfuko huu hakuna gharama zozote ambazo
unakatwa. Unauziwa kipande kwa bei ambayo iko sokoni. Kama unataka kuuza
vipande basi kiwango cha chini ambacho kinatakiwa kubaki katika akaunti yako
ni vipande 10 kama utafanya mauzo na kiwango ambacho kinaonekana kitabaki ni
chini ya vipande kumi basi uwekezaji wako wote utauzwa na akaunti itafungwa.
Baada ya kuwa uwekezaji umefikia kikomo hapa ina maana mtoto ametimiza
miaka 24 basi anaweza kufanya yafuatayo kwa pesa iliyopo katika akauti yake:-
Mtoto ambaye uwekezaji wake umekomaa anaweza kuamua kuwekeza pesa yake
kwa mtoto mwingine ambaye yuko chini ya umri wa miaka 18 na huyu ambaye
uwekezaje wake umekomaa anaweza kuwa kama mlezi wa huyu mtoto mwingine.
(iii) Kuhamia mfuko mwingine
Kama amekidhi vigezo huyu mtoto ambaye sasa uwekezaji wake umekomaa
anaweza kuhamia mfuko mwingine wowote wa UTT AMIS kama amekidhi vigezo
vya mfuko anaohamia.
Jedwali Na. 4: Linaonesha mrejesho wa uwekezaji (ROI) wa mfuko wa watoto mpaka kufikia Septemba, 30
2021
KUHAMA MFUKO
Unaruhusiwa kuhama kutoka mfuko huu kwenda katika mfuko mwingine endapo
umekidhi vigezo vya mfuko unaohamia. Uhamaji huu unafanyika bila gharama
yoyote. Lakini unapohama kutoka mfuko huu na kwenda katika mfuko mwingine
basi unapoteza haki na faida zote ambazo zinaendana na mfuko wa huu.
MFUKO WA JIKIMU
Mfuko huu ulianzishwa mwaka 2008 na mfuko huu unalenga kumuwezesha
mtanzania kupata faida ya mara kwa mara, mfuko huu unalipa gawio kwa
wawekezaji wake. Mfuko wa jikimu uko wazi kama ilivyo mifuko mingine. Mfuko
wa jikimu wakati unaanzishwa mwaka 2008, bei ya kipande katika mfuko huu
ilikuwa ni TSH 100/=. Mpango wa uwekezaji wa mfuko huu ni 0-100% kwenye
mapato ya kuaminika kama hati fungani, na 0- 35% katika hisa. Mpango huu
unaweza kubadilika pale ambapo meneja anaona ni sahihi kwa ajili ya manufaa ya
wawekezaji.
Maana yake ni kuwa katika faida ambayo inapatikana kuna baadhi itaenda kwa
wawekezaji kama gawio na kiasi kingine kitabaki kwa ajili ya kukuza mtaji maana
kuna watu wanadhani kuwa kama akichukua gawio basi hakuna faida nyingine
zaidi ya hiyo.
ANAYESTAHILI KUWEKEZA
Mfuko huu uko wazi kuwekeza kwa wawekezaji wote binafsi au taasisi na watoto
pia.
KIASI CHA CHINI CHA KUWEKEZA
Kiasi cha chini cha kuwekeza katika mfuko huu kinategemea na mpango
uliouchagua kwa mpango wa gawio kwa miezi mitatu kiwango cha chini cha
kuwekeza ni TSH 2 milioni. katika mpango wa gawio la mwaka kiwango cha chini
cha kuwekeza ni TSH 1 milioni na baada ya hapo kwa mipango ya gawio unaweza
kuwa unawekeza kuanzia 15,000/= kama nyongeza ila haina ukomo, kwa mpango
wa kuwekezewa gawio (annual reinvestment) kiwango cha chini cha kuanza
kuwekeza ni TSH elfu tano(5000/= )na baada ya hapo unaweza kuwa unaongeza
sh 5000/= kama nyongeza
Kama utauza baada ya mwaka mmoja lakini kabla ya mwaka wa pili kuisha
utakatwa 1.5% ya bei ya kipande maana yake kama utauza ndani ya mwaka wa
pili.
Kama utauza baada ya mwaka wa pili ila kabla ya mwaka wa 3 kuisha utakatwa
1% lakini baada ya miaka 3 hautakatwa chochote. Kiwango cha chini ambacho
kitakatwa kama gharama ya kuuza ni TSH 500/=
MIAKA MAKATO
1 2%
2 1.5%
3 1%
Baada ya miak 3 Hakuna makato
Jedwali Na. 5: Historia ya mrejesho wa uwekezaji (ROI) ya mfuko wa jikimu hadi kufikia Septemba, 30, 2021
Vipande vya mfuko huu vinaweza kutumika kama dhamana pale ambapo unataka
kuomba mkopo katika taasisi ya kifedha.
Kila siku ya mwisho ya mwezi wa tatu wa mpango huu ambayo ni siku ya kazi
ndio siku ambayo ina rekodiwa watu ambao wanastahili kupata gawio. Hii
inamaanisha kuwa katika mwaka kuna vipindi vine vya miezi 3, sasa siku ya
mwisho ya kazi ya mwezi Machi, Juni, Septemba na mwezi Disemba ndio siku ya
kurekodi watu ambao wanastahili kupata gawio. Baada ya kurekodi ndani ya siku
kumi za kazi baada ya siku hii ya kurekodi ndio gawio linatoka. Maana yake ni
kuwa kwa kipindi cha Januari mpaka Machi siku ya kurekodi ni siku ya mwisho
ya kazi ya mwezi Machi na baada ya hii siku gawio linatoka ndani ya siku kumi za
kazi.
Kwa kipindi cha mwezi Aprili mpaka Juni siku ya kurekodi ni siku ya mwisho ya
kazi ya mwezi juni na baada ya kurekodi watu wanaostahili kupata gawio. Gawio
linatoka ndani ya siku kumi za kazi.
Kwa kipindi cha mwezi Juni hadi September tarehe ya mwisho ya kurekodi ni
tarehe ya mwisho ya kazi ya mwezi Septemba na baada ya hii tarehe gawio
linatoka ndani ya siku kumi za kazi, hivyo hivyo kwa kipindi cha mwisho
ambacho ni Oktoba mpaka Disemba.
Wawekezaji walio katika mpango wa gawio kwa mwaka hawatapokea gawio kwa
vipindi vitatu vya miezi mitatu kama walio katika gawio baada ya miezi mitatu ila
gawio litakalokuwa linatoka katika kipindi litatumika kuwanunulia wawekezaji
vipande kwa bei iliyopo sokoni na baada ya vipindi vyote vinne kuisha hivi
vipande vilivyonunuliwa vitakatwa (cancleled) na pesa itakayopatikana ndio
itakayotumika kuwapa gawio hawa wawekezaji wa gawio kwa mwaka mara moja.
MPANGO WA KUWEKEZEWA GAWIO(ANNUAL REINVESTMENT)
Hapa katika mpango huu wawekezaji hawatapokea gawio kwa kipindi cha miezi
yote 12 ila gawio ambalo litakuwa linatoka litatumika kuwanunulia wawekezaji
vipande tena.
Kama ilivyo katika mfuko wa hati fungani kuwa sio kwamba ukiweka TSH 2
milioni basi utawekwa katika mpango wa gawio moja kwa moja hapana bali
unaweza kuweka TSH 2 milioni au zaidi ila ukachagua mpango wa kuwekezewa
gawio ni uchaguzi wako.
UTANGULIZI
Mfuko huu wa ukwasi (liquid fund) ulianzishwa 2013 ukiwa na malengo makuu
matatu ambayo ni:-
Kuna maeneo mengi mtu anaweza kuweka fedha yake kwa muda mfupi ila kipindi
anapoitoa kuna uwezekano wa fedha hiyo kupungua kutokana na makato Fulani
Fulani lakini mfuko wa ukwasi unaweza kukupa msaada sana hapa kwani utatuza
fedha zako pasipo kupungua kwa fedha yako wakati wa kuichukua. Mathalani,
unaweza kuwa mkulima wa msimu (unategemea mvua) baada ya kuvuna na
kuuza mazao pesa yako ya mtaji ambayo utatumia kwa ajiri ya kilimo mwaka ujao
unaweza kuiweka katika mfuko huu wakati unasubiri msimu hapa utapata faida
ya ongezeko la mtaji bila kupoteza chochote.
ANAYESTAHILI KUWEKEZA
Mfuko huu uko wazi kuwekeza kwa wawekezaji binafsi na wawekezaji wasio
binafsi, maana yake mtu wa kawaida au kampuni inaweza kuwekeza katika
mfuko huu. Mtu, kikundi, kampuni au taasisi yoyote inaruhusiwa kuwekeza
katika mfuko huu. Mfuko huu unaruhusu hata watoto kuwekeza, hivyo ndugu
muwekezaji kama una mtoto au mdogo wako badala ya kuwa unamnunulia Pipi
na vitu vya hulka hiyo, unaweza kuamua kumfundisha kuwekeza kupitia mfuko
huu.
GHARAMA YA UNUNUZI
Unavyonunua kipande katika mfuko huu hakuna gharama zozote ambazo
unakatwa, unauziwa kipande kwa bei ambayo iko sokoni.
Jedwali Na. 6: Hali ya mrejesho wa uwekezaji uliofanywa na mfuko wa ukwasi mpaka kufikia Septemba, 30
mwaka 2021
UTANGULIZI
Ulishawahi kutamani kuwekeza kwenye hati fungani ila hauna TSH 1 milioni ya
kuwekeza kwani kima cha chini cha kuwekeza kwenye hati fungani za muda
mrefu za serikali ni shilingi milioni moja?. Ikiwa ndiyo, basi UTT AMIS ipo kwa
ajili yako. UTT AMIS wameanzisha mfuko wa uwekezaji wa hati fungani (Bond
fund). Mfuko huu umeanzishwa mahsusi kwa ajili ya kukusanya mitaji kutoka
kwa wawekezaji wengi wadogo kwa wakubwa na kuziwekeza kwenye hati
fungani za serikali. Mfuko huu unaruhusu muwekezaji kuwekeza kwa kiwango
cha kuanzia shilingi 50000/= na kuendelea. Huu ndiyo mfuko mchanga kuliko
mifuko yote iliyo chini ya UTT AMIS kwani mfuko huu umeanzishwa mwaka
2019. Wakati mfuko unaanzishwa bei ya kipande ilikuwa TSH 100/=, ukubwa wa
mfuko mpaka kufikia Juni 2021 ilikuwa ni TSH 94 bilioni.
1) Mpango wa gawio
2) Mpango wa kukua kwa mtaji
MPANGO WA UWEKEZAJI
Mfuko unatoa fursa za kuwekeza katika mipango mitatu
Mpango wa kuwekezewa gawio hapa ina maana utapokea gawio kama mipango
mingine ya gawio ila gawio lako hautalipokea bali litaenda kuwekezwa kwa
kukununulia vipande kwa bei iliyopo. Mfano, kama gawio kwa kila kipande ni
TSH 12 na wewe una vipande 1000 ina maana utapokea gawio la 12000/= hii pesa
hautapewa mkononi bali itaenda kukununulia vipande tena.
MPANGO WA GAWIO
Mpango wa gawio umegawanyika mara mbili
GAWIO
Katika mipango yote mitatu, muwekezaji anapokea gawio ila utofauti ni kuwa
gawio ambalo anapokea mtu aliyewekeza katika mpango wa kuwekezewa gawio
hapewi mkononi bali gawio lake linatumika kumnunulia vipande kwa bei
iliyopo,wakati hiyo mipango miwili iliyobaki gawio wanapewa.
Gawio kila baada ya miezi sita maana yake kila baada ya miezi sita utapokea
gawio na mtu wa gawio kila mwezi atapokea gawio kila mwezi.
Gawio kwa mwaka 2020, 2021 lilikuwa ni TSH 12 kwa kila kipande. Ieleweke
kuwa gawio linaweza kupungua au kuongezea kutegemea na utendaji wa mfuko
kwa mwaka husika. Katika mipango yote hiyo muwekezaji anaweza kuuza baadhi
au vipande vyake vyote.
ANAYESTAHILI KUWEKEZA
Mfuko huu uko wazi kuwekeza kwa wawekezaji binafsi na wawekezaji wasio
binafsi, maana yake mtu wa kawaida au kampuni au taasisi au kikundi cha watu
wote wanaweza kuwekeza katika mfuko huu.
Mchoro Na. 6: Hali ya uwekezaji kwenye mfuko wa hati fungani ulio chini ya UTT AMIS mpaka Juni, 30, 2021
GHARAMA YA UNUNUZI
Unavyonunua kipande katika mfuko huu hakuna gharama zozote ambazo
unakatwa, unauziwa kipande kwa bei ambayo iko sokoni.
Jedwali Na. 7: Mrejesho wa uwekezaji kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa mfuko huu
UNAFUU WA KODI
Katika mipango yote kiwango ambacho unapokea kama gawio hakina makato ya
kodi ya mapato katika mikono ya muwekezaji. Tunafahamu kuwa unapopokea
gawio kutoka katika kampuni ambayo iko soko la hisa unakatwa 5% kama kodi ya
zuio lakini gawio unalopokea kutoka katika mfuko huu halina makato ya aina
yoyote ya kodi.
1) UTT AMIS ina mifuko sita ila ni mifuko miwili tu ndio inayolipa gawio; na
2) Sio watu wengi nchini wanaweza kuwa na fedha ya kuwekeza shilingi
milioni 1 au zaidi ili waweze kupata gawio la kila mwezi.
Ila usijali kwa sababu nahodha wako nipo nitakupa njia ya kutengeneza gawio
lako hata kama hela yako ni kidogo. Ujue gawio ambalo wanatoa UTT AMIS
halina maajabu kabisa (vijana wa mtaani wanasema) kama wewe ni muwekezaji
mwenye nidhamu na unayetunza kumbukumbu zako za uwekezaji unaweza
kutengeneza gawio lako bila wasiwasi. Ngoja nikuoneshe namna ya kufanya hilo;
SABABU ZA KUTAKA GAWIO KUTOKA MIFUKO YA UTT
Kuna sababu nyingi za kwa nini wewe kama muwekezaji unaweza kuhitaji gawio
kutoka katika mfuko mwingine tofauti na mifuko ambayo UTT AMIS imepanga
kuwa ndiyo inayotoa gawio:
Mimi napenda sana mfuko wa ukwasi kwa sababu ya masharti yake kuliko mfuko
wa hati fungani na kwa kuwa mifuko hii ina uwekezaji wa aina moja maana yake
ni kwamba imewekeza katika mapato ya kufanana ila changamoto inaweza kuwa
mfuko wa ukwasi hauna gawio kama ilivyo mfuko wa hati fungani. Muwekezaji
anaweza kuamua kutengeneza gawio lake mwenyewe kwenye mfuko wa ukwasi
kama ambavyo inalipwa kwenye mfuko wa hati fungani.
Sio kwa sababu mfuko unatoa gawio basi mrejesho wake wa uwekezaji utakuwa
mkubwa hapana, kuna mifuko ambayo haitoi gawio ila ina mrejesho wa uwekezaji
mkubwa kuliko mifuko ambayo inatoa gawio. Hivyo, muwekezaji anaweza
kuchagua mfuko ambao hauna gawio ila una mrejesho mkubwa na akatengeneza
gawio lake kwenye mfuko husika.
(iii) Kima cha chini cha uwekezaji kwa baadhi ya vyanzo kuwa
kikubwa
Unaweza kuwa huna millioni 10 ya kuwekeza katika mfuko wa hati fungani ila
unataka gawio kutokana na uwekezaji wako, unaweza kuwekeza kiasi cha fedha
ulicho nacho katika mfuko wa ukwasi kwani unafanana sana na mfuko wa hati
fungani na ukatengneza gawio lako mwenyewe.
Mfano:
Mtaji wako utakuwa unakuwa japokuwa kwa kasi ndogo ila utakuwa unapata
gawio kila mwezi kwa mwaka mzima bila shida na kama tulivyo ona baada ya
kuchukua gawio bado utabakiwa na kiasi cha mtaji wa 6825/= ambacho hiki
kitaenda kuongezeka mwenye mtaji na kufanya mtaji wako kukua na kuwa
506825/=. Hii ina maana mwaka unaofuata utakuwa na gawio kubwa kwani mtaji
wako sasa umekua kiasi.
Kwa maelezo mafupi ni kwamba, ikiwa ukuaji wa mfuko wako kwa mwaka ni
13.5% ina maana kila mwezi mfuko wako unakuwa kwa asilimia 1.125% sasa
ukiamua kuchukua 1% kama gawio kila mwezi, na hii unaipata kupitia kuuza
vipande vyenye thamani ya 1% ya mfuko wako kila mwezi kitakachotokea ni kuwa
utakuwa umechukua faida na mtaji unabaki pale pale na kunakuwa na ongezeko
kidogo la mtaji kwa mwaka. Na hapa unaweza kuamua kuuza asilimia yoyote ile
ya faida kwa muda unaotaka, mtu mwingine anaweza kuamua kuuza asilimia 6
kila baada ya miezi sita au akaamua kuuza asimilia 3 kila baada ya miezi 3.
Kikubwa ni kuwa unauza vipande vyako kulingana na kiasi ambacho unataka
kiwe kama gawio.
MWAKA WA 2
Sasa huu mwaka wa pili unaweza kuamua kuchukua 2% kama gawio, hapa
utabaki na mtaji wako wa kwanza kabisa na faida kidogo au ukaamua kuchukua
1% ya mtaji wa pili wa 506,825/=
Sasa kwa UTT AMIS hasa kwa mifuko ambayo imewekeza katika hisa na baada ya
mwaka kuisha huwa wanafanya ukokotoaji wa faida ambayo kampuni
imetengeneza kwa mwaka huo na baada ya kufanya hivyo, muwekezaji ndiyo
anachagua gawio lake liwe kiasi gani kwa mwaka.
Mfano, mfuko wa umoja kwa mwaka 2021 umekuwa kwa 16.9% sasa wewe
unaweza kuamua uchukue asilimia ngapi kama gawio, unaweza kuamua
kuchukua 6%,9%,10%,12% au 16% kutegemea na mapenzi yako
Mfano halisi
Tuchukue mfano nina vipande 2000 vya umoja nimenunua mwanzoni mwa
mwaka kwa bei ya shilingi 100/= ina maana mfuko wangu una thamani ya
200,000/= na mwisho wa mwaka mfuko wa umoja umekuwa kwa asilimia 20% ina
maana thamani ya mfuko wangu imekuwa kwa 40,000/= sasa kama nitaamua
kuchukua gawio la 10% ambayo ni sawa 20,000/= ina maana nitauza vipande 166.6
kutoka katika mfuko wangu na mfuko wangu utapungua na kubaki na thamani ya
220,000/=.
Kama unavyofahamu uwekezaji wowote ule ambao hauna mipango, huna tija na
nikupoteza muda na pia utashindwa kutumia fursa iliyoko mbele yako.
Katika kipengele hiki nitakufundisha jinsi gani unaweza kutumia kikokotozi hiki
ili kikusaidie katika kupanga uwekezaji wako na hata kukuonyesha ni kiasi gani
unategemea kukipata. Kwa hiyo hii ni moja kati ya kitu muhimu sana na katika
kipengele kinachofuata tutaanza kuangalia namna ambavyo unaweza kutumia
kikokotozi kupanga uwekezaji wako.
Tuanze na jinsi hiki kikokotozi kilivyo, muonekano wake ni kama jinsi unavyoona
hapo chini na kama unavyoona baada ya maneno INVESTMENT ASSUMPTION
CALCULATOR kuna viboksi 4 ambavyo vinaelezea mipango minne ambayo
unaweza kuichagua ambayo ni
Sasa nitaelezea mpango mmoja mmoja hapo juu kwa kina katika maelezo
yafuatayo:-
Kumbuka
Kama wewe ni muwekezaji basi kikokotozi hiki ni muhimu sana kwako sio tu
kwa kupiga mahesabu ya uwekezaji wa UTT AMIS bali hata katika
uwekezaji mwingine ila kitu cha kukumbuka ni kuwa mahesabu ya
kikokotozi hiki ni ya RIBA YA KAMPAUNDI NA SIO RIBA RAHISI.
KIKOKOTOZI CHA UWEKEZAJI WA MWEZI (MONTHLY INVESTMENT
CALCULATOR)
Ukibonyeza kiboksi cha kwanza basi kikokotozi cha uwekezaji wa mwezi
kitafunguka na muonekano wake ni kama unavyoona hapo chini.
Hiki ni kiasi cha pesa ambacho utakuwa unawekeza kila mwezi, mfano kama
unataka uwe unawekeza 50,000/= kila mwezi basi hapa ndio utaiandika hii namba
Hapa unaandika miaka ambayo utakuwa umewekeza katika mfuko huu, mfano
kama unataka kuwekeza kila mwezi 50,000/= katika mfuko wa ukwasi ambao una
wastani wa mrejesho wa uwekezaji wa 14% kwa mwaka na unataka kuwekeza
kwa miaka 30 basi hii miaka 30 utaiandika hapa.
Baada ya kujaza sehemu hizi tatu basi utabonyeza sehemu iliyoandika calculate.
Nabaada ya hapo majibu yatakuja upande wa kulia. Upande wa kulia pia una una
sehemu 3 ambazo zimeachwa wazi ambazo ni:-
.
(v) Invested amount (TZS)
Hiki ni jumla ya kiasi ambacho utakuwa umewekeza kwa miaka yote ambayo
umefanya uwekezaji wako, maana hii ni jumla ya pesa ambayo umekuwa
ukichangia kwa miaka yote.
Hiki ni kiasi cha faida ambacho unakuwa umekipata baada ya kuwekeza kwa
miaka ambayo umeitaja.
hiki ni kiwango cha pesa ambachounakihitaji baada ya muda fulani, mfano kama
mimi nimepiga mahesabu kuwa ili nifikie uhuru wa kifedha basi nitahitaji milioni
150 baada ya miaka 20 ila sifahamu inanibidi niwekeze kiasi gani kwa mwezi ili
nifikie uhuru huo wa kifedha, hii pesa ndio ninaiweka hapa ili iniwezeshe kujua ni
kiasi gani ninatakiwa niwekeze kila mwezi
Hiki ni kiasi cha mrejesho ambao unadhani uwekezaji wako unaweza kuwa
unarudisha kila mwaka, kama tulivyoona katika kikokotozi kilichopita, mfano
kama uwekezaji wako unakurudishia 14% kwa mwaka basi hii namba ndio
utaiweka hapa.
hiki ni kiasi cha pesa cha jumla ambacho utakuwa umewekeza kwa miaka yote,
pesa ambayo ulitoa mfukoni na kuwekeza.
hii ni jumla ya fedha ambayo imepatikana kama faida katika kipindi chote cha
uwekezaji.
Tuone mfano
Chukulia unahitaji milioni 150 ndani ya miaka 20 je ni kiwango gani cha fedha
unatakiwa kuwekeza kila mwezi ili uweze kufanikiwa katika malengo yako ikiwa
mfuko uliowekeza una mrejesho wa 14 kwa mwaka
Majibu yetu ndio hayo hapo juu, ni kuwa ili ufikie malengo yako ya kuwa na
milioni 150 ndani ya miaka 20 basi unatakiwa kuwekeza kila mwezi 113,952/= kila
mwezi na jumla ya fedha ambayo utakuwa umewekeza ni kiasi cha 27 milioni na
faida ni 122 milioni. Sio mbaya kama una nidhamu unaweza kutengeneza milioni
150 kirahisi mno na hapo chini nitakuelekeza njia ambayo unaweza kufikia lengo
lako kwa gharama nusu ya hiyo na pia kama nilivyosema tukipiga mahesabu
halisia unaweza kukuta faida inakuwa zaidi ya hiyo ngoja tutaona hapo chini pia .
Katika huu mfano tugeuze hesabu kidogo kama unakumbuka kwenya kikokotozi
cha uwekezaji wa mwezi tulipiga mahesabu ya kuwa tuna 50,000/= ya kuwekeza
katika mfano huu tugeuze tuseme tunahitaji milioni 136 ndani ya miaka 25 kwa
mrejesho wa 14% kwa mwaka tuone je itatuletea tuwekeze kiasi gani kwa mwezi.
Nadhani umeona utofauti wa hivi vikokotozi viwili, hapa tunaanzia mwisho
kurudi mwanzo na katika kikokotozi kilichopita tunaanzia mwanzo kwenda
mwisho. Nadhani umeona jibu la mfano wetu wa pili ya kwamba kama tunahitaji
milioni 136 kwa miaka 25 na mrejesho wa 14 basi itatubidi kuwekeza 50,000/= kwa
mwezi, sababu iliyofanya tukapata 49,867/= kwa mwezi ni kwa kuwa nimeandika
milioni 136 tu na zile pointi nyingine nikaziacha.
Hiki ni kiasi ambacho unawekeza kwa mara moja, mfano kama pesa unayotaka
kuwekeza kwa mara moja ni 100,000/= basi hapa ndio unaweka hiyo pesa katika
kikokotozi hiki.
Hii ni idadi ya miaka ambayo uwekezaji wako utachukua. Na hapa inaweza kuwa
miaka 2, 5, 10 na kuendelea kama unavyotaka kuwekeza
Hiki ni kiasi cha fedha ambacho umewekeza katika muda wote wa uwekezaji.
Kwa kuwa hapa unawekeza mara moja basi kiasi hiki ni sawa na kile kiasi
ambacho ulikiandika pale mwanzo kwenye kipengele cha investment
(iii) wealth gain (TZS)
Hii ni faida ambayo unakuwa umeipata baada ya uwekezaji wako kuwa umeiva
Mfano,
Ngoja tufanye hesabu ili kuona ni kiasi gani kitapatikana kwenye uwekezaji huu:-
Matokeo ni kuwa baada ya miaka 15 ya kuwekeza TSH 100,000/= kwa mrejesho
wa 15% kwa mwaka pesa yetu imekuwa na kufikia TSH 813,706/= na katika kiasi
hiki faida ni TSH 713,706/=
Hiki ni kiasi ambacho unatakiwa kuwekeza kwa mara moja ili uweze kufikia
malengo yako au kufikia pesa ambayo umeiainisha hapo juu
Hiki ni kiasi cha faida ambacho unakuwa umekipata baada ya miaka yako ya
uwekezaji wako kuisha
Mfano,
Tuchukulie una hitaji kiasi cha TSH 20 milioni baada ya miaka 10 kwenye mfuko
wenye mrejesho wa 15% kwa mwaka. Je ni kiasi gani utahitajika kuwekeza kwa
mara moja ili uweze kufikia malengo yako?
Kwa hiyo utaona ili uweze kupata TSH 20 milioni baada ya miaka 10 kwenye
mfuko wenye mrejesho wa 15% kwa mwaka basi itakubidi uwekeze TSH
4,943,694/= na faida ambayo utaipata ni kiasi cha TSH 15 milioni,
Nadhani mpaka kufikia hapo utakuwa umeona ni jinsi gani kikokotozi cha UTT
AMIS kinavyoweza kurahisisha upangaji wako wa mambo ya uwekezaji.
Sasa kabla hatujaendelea mbele, kuna kitu inabidi nikiseme hati fungani unaweza
kuinunua kwa bei ya chini ya thamani yake (at discount), maana yake mrejesho
wake unakua mkubwa zaidi ila hapa nimechukulia kuwa zinauzwa kwa bei halisi
(at par value) na kama umekuwa unafuatilia hati fungani siku hizi zimekuwa za
moto kwa upande wa bei.
Sasa kwa kuangalia utaona ni kuwa ni hati fungani mbili tu ndio zina mrejesho
mkubwa kuliko mfuko wa ukwasi. Hizi ni hati fungani ya miaka 20 na miaka 25
tu. Kitu kingine ambacho utaona kuwa ni bora kwa upande wa UTT AMIS ni
kuwa huu mrejesho ni wa mwaka mmoja ina maana tukichukulia mtu
anayewekeza katika hati fungani ya miaka 15 kushuka chini Hana mrejesho
mkubwa kuliko aliyewekeza UTT AMIS. Aidha, uwekezaji wa hati fungani ni wa
muda mrefu lakini wa UTT AMIS kama mnakuwa mmewekeza kwa miaka 2 na
baada ya hapo uwekezaji wenu unakuwa umeiva wewe ambaye umewekeza
katika mfuko wa ukwasi unakuwa na faida kuliko aliyewekeza katika hatifungani
ya miaka 2.
Jambo ninalolieleza hapa ni kuwa sio kwamba hati fungani ni bora kuliko
kuwekeza UTT AMIS, wala mtu anayewekeza UTT AMIS sio kwamba ni bora
kuliko anayewekeza katika hati fingani bali kila uwekezaji una ubora wake na
udhaifu wake kwa hiyo sio sahihi kutoa hitimisho la kuwa kwa kuwa UTT AMIS
imewekeza pia katika hati fungani basi ni bora kuwekeza katika hati fungani
kuliko UTT AMIS.
SEHEMU YA NNE
Tumeona UTT AMIS ina mifuko mingi yenye sifa tofauti tofauti na malengo
tofauti, je wewe malengo yako ya kuwekeza ni yapi ili ujue mfuko ambao utakupa
faida zaidi kutokana na kile ambacho umekusudia kukipata. Kama unawekeza
kwa ajili ya mtoto au kwa ajii yako mwenyewe au kwa ajili ya shughuli fulani basi
ni vyema ukawa na picha kichwani nini unataka kwani uwezo wa UTT AMIS
kukusaidia unategema mahitaji uliyonayo. Kuna mtu anataka kuwekeza ili
akistaafu awe na chanzo cha mapato ambacho kitamuwezesha kukidhi mahitaji
yake pale ambapo anakuwa amestaafu.
MUDA WA UWEKEZAJI
Fikiria yule msafiri ambaye anaanza safari akiwa hajui wapi anaishia, yeye anaona
raha kusafiri ila hajui mwisho wa kituo chake ni upi. Huyu ni kama yule
muwekezaji ambaye anawekeza akiwa hajui kuwa uwekezaji wake unaiva lini
yeye anaona raha kuwekeza tu bila kujua ni lini uwekezaji wake utakuwa tayari,
kwani lengo kuu la kuwekeza ni kuwa mwisho wa siku uwekezaji wako
ukusaidie.
Kama unakumbuka wakati tunatumia kikokotozi moja kati ya kitu cha msingi
ambacho kilikuwa katika kile kikokotozi ni muda ambao utautumia katika
uwekezaji wako kwani huu pia utakuonyesha ni kiasi gani unatakiwa kuwekeza
ili ufanikishe malengo yako, lakini ukiwekeza tu bila kujua ni lini uwekezaji wako
unatakiwa uwe umeiva unakuwa hauna hekima ya kiuwekezaji na hauwezi
kupata faida kamili ya uwekezaji wako. Kitakuwa kitu cha ajabu una uhitaji hela
yako ndani ya miaka miwili halafu unaenda kuwekeza kwenye mfuko wa wekeza
maisha.
Mfano
Chukulia watu wawili wenye milioni 100 za kuwekeza ndani ya miaka 20 mmoja
akasema nitawekeza hii milioni moja yote kwa kiasi kila mwezi kwa miaka yote
20 ambayo itakuwa TSH 417,000/= kwa mwezi na mwingine akasema nitawekeza
hii milioni 100 kwa pamoja. Jumla ya pesa ambayo imewekezwa na muwekezaji
wa kwanza na pili ni milioni 100 ila tofauti ni kwamba muwekezaji wa kwanza
amewekeza kiasi chote kidogo kidogo kila mwezi, na muwekezaji wa pili
amewekeza kiasi chote kwa pamoja tuchukulie mfuko walio wekeza una mrejesho
wa 14% kila mwaka.
Mrejesho wa muwekezaji wa kwanza
Turudi kwenye kikokotozi cha UTT AMIS tuone mahesabu yao yanakuwaje, huyu
muwekezaji amewekeza TSH 417,000/= kila mwezi kwa miaka 20 kwenye mfuko
wenye mrejesho wa 14% kwa mwaka.
Sio mbaya ila tuone muwekezaji wa pili ambaye alichagua kuwekeza 100 kwa
pamoja bila kuongeza pesa nyingine
Muwekezaji huyu yeye aliwekeza milioni 100 yote kwa pamoja katika mfuko
wenye mrejesho wa uwekezaji wa 14% kwa miaka 20 tuone uwekezaji wake
umekuwaje
Matokeo ni kuwa muwekezaji aliyewekeza milioni 100 kwa pamoja amepata faida
ya 1.27 bilioni na jumla ya fedha ambayo ataipokea baada ya miaka 20 ni 1.374
bilioni.
Tuone taarifa fupi ya mrejesho wa wawekezaji hawa wawili
Kwa hiyo utaona kuwa ingawa waliwekeza kiasi sawa kwa muda wote ila
muwekezaji wa pili alikuwa na faida mara tatu kumshinda muwekezaji wa
kwanza, wakati muwekezaji wa kwanza alikuwa na faida ya milioni 448
muwekezaji wa pili alikuwa na faida ya bilioni 1.27
Kwa TSH 1 milioni kwa mpango wa kuwekeza kila mwezi huyu muwekezaji
atawekeza 8,340/= kwa miaka yote kumi, turudi kwenye kikokotozi
Tumeona kuwa baada ya miaka 10 ya kuwekeza kila mwezi 8,340/= mwisho wa
siku jumla ya kiwango ambacho kimewekezwa ni TSH 1 milioni na faida baada ya
miaka ni 1.185 milioni na jumla ya pesa atakayopata baada ya miaka ni TSH 2.187
milioni.
Tuone muwekezaji wa pili
Muwekezaji wa pili
Tuone matokeo
Kama uavyoona muwekezaji wa pili ana faida ya TSH 2.7 milioni na jumla ya pesa
ambayo ataipata kwa miaka yote ni 3.7 milioni kwa hiyo utaona kuwa muwekezaji
aliyewekeza kwa mara moja ana pesa nyingi kuliko muwekezaji wa kwanza faida
yake tu ni kubwa kuliko pesa yote ambayo muwekezaji wa kwanza kwa miaka 10
(jumla ya faida na mtaji).
Hitimisho
Kama tulivyoona kuwa kama unawekeza pesa yote kwa mara moja faida yako
inakuwa kubwa kuliko mtu ambaye anawekeza taratibu taratibu kama
mtawekeza jumla ya kiasi ambacho kinafanana na kama mrejesho wa uwekezaji ni
sawa.
Tanbihi
Mfano
Tuchukulie kuna mfuko ambao unakua kwa asilimia 14% kwa mwaka na bei ya
kipande ni TSH 100/= tuone jinsi bei itakavyo kuwa kwa miaka 15 ijayo na tuone
jinsi riba ya kampaundi inavyokuwa na maajabu
Sasa tuangalie wawekezaji watatu ambao walinunua kipande kwa bei ya 100 ila
mmoja akauza mwaka wa 5 na wa pili akauza mwaka wa 10 na mwingine akauza
mwaka wa 20 tuone mrejesho wao unakuwaje:-
Muwekezaji wa kwanza
Huyu alinunua kipande kwa bei yaTSH 100/= na akauza mwaka wa tano kwa bei
ya TSH 192.52/= tuone mrejesho wake, kama unashida na jinsi ya kutafuta
mrejesho wa uwekezaji tafuta kitabu change cha namna bora ya kutengeneza
hela soko la hisa au soma jinsi ya kutafuta mrejesho wa uwekezaj katika kitabu
hiki
Lakini huu mrejesho ni kwa miaka 5, tukitaka kupata mrejesho wa wastani kwa
kila mwaka tunagawanya kwa tano
92.52/5 =18.504%
Muwekezaji wa pili
Huyu pia alinunua kipande kwa bei ya TSH 100/=na akauza mwaka wa kumi kwa
bei ya TSH 370.64/= tuone mrejesho wake
270.64%/10 =27.06%
Kwa hiyo utaona kuwa muwekezaji wa pili alikuwa na wastani wa 27.06% kama
mrejesho wa mwaka mmoja kwa miaka yote kumi.
Muwekezaji wa tatu
Huyu pia aliwekeza kwa bei ya TSH 100 na akauza vipande vyake mwaka wa 15
kwa bei ya TSH 712.83/= tuone mrejesho wake unakuwaje.
Mrejesho
612.83/100)*100 = 612.83%
Hitimisho
Kama tilivyoona katika mfano wetu hapo juu, tumeona ijapokuwa kila mwaka
ongezeko la mfuko wetu lilikuwa 14% lakini kwa sababu ya riba ya kampaundi
mirejesho ya hawa watu imetofautiana na tumeona kuwa kadri unavyo endelea
kukaa katika uwekezaji basi ndivyo uwekekezaji wako unazidi kukupa faida
kubwa , sababu inayofanya mtu akikaa katika uwekezaji kwa muda mrefu awe na
mrejesho mkubwa kuliko wenzake ni kwa sababu pesa yake inachukua muda
mrefu kukampaundi na hivyo mrejesho wake unakuwa mkubwa pia.
Hivyo, ukitaka kufurahia uwekezaji wako katika mifuko ya UTT AMIS basi
unapowekeza wekeza kwa muda mrefu ndio unapata faida zaidi.
Hapa nilichosema ni kuwa mtu anayewekeza katika mfuko wenye hisa kuna
uwezekano kuwa mfuko wake ukapanda sana kwa mwaka fulani kutokana na hali
ya bei ya hisa ilivyo na gawio linavyotoka kwa mwaka Fulani. Kitu ambacho ni
kigumu kukipata katika mifuko ambayo mapato yake ni ya kutabirika, kwa mfano
mfuko ambao umewekeza katika hati fungani za serikali za muda mrefu
unategemewa kwa mwaka unaweza kupokea 15.95% ambacho ndicho kiwango
cha juu cha riba ambacho kinatoka katika hati fungani za serikali. Hata kama pesa
ambayo itapatikana kwa ile miezi sita ya kwanza itawekezwa hatutegemei kuwa
mfuko utakuwa na 25% kama mrejesho kutoka katika hati fungani kwa mwaka
husika, ila katika mfuko wenye hisa uwezekano wa mfuko kukua kwa zaidi ya
25% kwa mwaka upo ijapokuwa uwezekano pia wa mfuko kushuka kwa kiwango
cha juu pia upo kitu ambacho si rahisi kukiona katika mifuko yenye mapato ya
kuaminika.
Hii uwezekano wa mfuko kuwa na mrejesho mkubwa kwa mwaka Fulani ni moja
kati ya faida za mifuko yenye hisa kwani ukijumlisha na riba ya kampaundi kwa
muwekezaji wa muda mrefu katika mifuko hii anaweza kuwa na mrejesho
mkubwa kuliko muwekezaji wa mifuko yenye mapato ya kuaminika.
Tuone mfano
Huu chini ni mrejesho wa mfuko wa umoja kwa miaka iliyopita tangu kuanzishwa
kwake mpaka mwaka 2020 na tukiongeza mwaka 2021 ambapo mfuko wa umoja
umekuwa na mrejesho wa 16.6%. Matokeo ni kama unavyoona hapo chini, kitu
ambacho nataka uone ni kuwa kwa mwaka 2014 mfuko ulikuwa na mrejesho wa
51% kitu ambacho ni kigumu kukipata katika mifuko mingine ambayo haina hisa
ndani yake.
Mfuko wa jikimu
Mfuko wa ukwasi
Hitimisho
Mfano huu tutachukua mfuko wa ukwasi na mifuko yenye hisa tuone mrejesho
wake ungekuwaje kama mfuko wa ukwasi nao ungeanzishwa kwa mwaka sawa
na mifuko ambayo ina hisa.
Mfano wa bei ya kipande ya mfuko wa ukwasi toka 2005 ukianza na bei TSH ya
100/= kwa mrejesho wa 13.5%
MWAKA BEI YA KIPANDE
2005 113.5
2006 128.82
2007 146.21
2008 165.95
2009 188.35
2010 213.77
2011 242.62
2012 275.37
2013 294.54
2014 334.30
2015 379.43
2016 430.65
2017 488.78
2018 554.76
2019 629.65
2020 714.65
2021 811.12
Hitimisho
Kwa mfano wetu tumeona kuwa endapo mfuko wa ukwasi ungeanzishwa mwaka
2005 na ungekuwa na mrejesho wa 13.5 kwa miaka yote basi bei ya kipande
ingekuwa 811.12/= kitu ambacho sio mbali sana na mfuko wa umoja ambao bei ya
kipande ni 740/=. Kwa hiyo utaona kuwa mfuko wenye hisa pia mrejesho wake ni
mzuri tu kama ilivyo mifuko ambayo haina hisa na kuna baadhi ya miaka mfuko
wa umoja ulikuwa na bei ya kipande kubwa kuliko mfuko wa ukwasi. Hapa
tumetoa mfano na sio mrejesho halisi wa mfuko wa ukwasi mrejesho halisi
ungeweza kuwa mkubwa, sawa au mdogo kuliko huu tuliouonesha hapa.
Muwekezaji wa kwanza
MWAKA GAWIO THAMANI YA
MFUKO WAKE
1 12 100/=
2 12 100/=
3 12 100/=
4 12 100/=
5 12 100/=
JUMLA 60
Hitimisho
Kwa wale wataofanikiwa kupata kusoma kitabu hiki, niwakumbushe kuwa tangu
siku uliyoanza kufanya kazi ndiyo ilikuwa siku sahihi ya kuanza kujiandaa
kifedha kwa ajili ya siku za kustaafu. Ikiwa bado hujafanya hivyo, nikutie moyo na
kukumbusha kuwa unapaswa kuanza sasa kwa kuwekeza kwenye fursa
mbalimbali zilizo nchini ikiwa ni pamoja na UTT AMIS. Kwa hiyo katika hili
andiko nitakufundisha ni jinsi gani ujiandae kwa siku zile ambazo utakuwa
umestaafu.
Ndugu msomaji, utakaposoma sehemu hii ninategemea utajifunza maana ya
kustaafu, aina za watu wanaostaafu, makossa wanayofanya wastaafu wengi na
umuhimu wa kujiandaa kwa ajili ya kustaafu.
KUSTAAFU NI NINI
Tunapozungumzia kustaafu kuna watu wengi wanadhani ni mpaka mtu afikishe
miaka 60 au 65 ili aweze kustaafu kufanya kazi kwa lengo la kuingiza kipato cha
kuishi. Kwa miaka hii ya hivi karibu na kutokana na serikali nyingi kuweka
mazingira bora ya kuwekeza, imekuwa kawaida ya watu wengi duniani kustaafu
kutenda kazi wakiwa na umri mdogo kabisa takribani miaka ishirini na tano ya
kuzaliwa. Watu wamekuwa wakistaafu kufanya kazi kwa ajili ya kujipatia kipato
ili waishi. Ikiwa wewe ni mfuatiliaji na unapenda kujifunza kupitia vyanzo
mbalimbali, ukienda kusoma mitandaoni kuhusu “FIRE MOVEMENT” utajua
namna ambavyo vijana wa zama hizi wanavyopambana kuhakikisha wanastaafu
mapema.
Kwa ufupi tu “FIRE” ni financial independence, retire early. Kwa tafsiri isiyo
rasmi ni kuwa kupata uhuru wa kifedha ili kustaafu mapema. Watu walio kwenye
imani hii wanahakikisha kuwa wanatunza na kuwekeza fedha zao kutoka kwenye
vyanzo vyao mbalimbali mapema kwa kadri wawezavyo ili waweze kustaafu
mapema. Njia hii inahusisha kutunza na kuwekeza fedha hadi kufikia asilimia
sabini (70%) kwa kipindi fulani ili kumfanya muwekezaji husika kutengeneza
vyao vya fedha vitakavyomfanya kuishi bila kutegemea kufanya kazi kwa maisha
yake yote.
Hivyo, utaona kuwa katika zama hizi, kustaafu hakutegemei kufikia umri
uliopangwa kisheria isipokuwa inategemea ni kwa kiasi gani umejiandaa kifedha
kwa ajili ya muda ule ambao utaishi bila kufanya kazi.
Hivyo kwa maana hiyo, kustaafu ni kile kipindi ambacho mtu anaacha kufanya
kazi za kila siku kwa ajili ya kujipatia kipato. Sasa basi kundi lolote lile ambalo
upo kati ya kundi la kustaafu kisheria au kustaafu mapema muhimu ni lazima
kuwa na mikakati maalum za kukuza kipato ili wakati wa kustaafu utakapofika
basi uwe na uwezo wa kuishi pasipo kuwa na matatizo ya kifedha.
Kundi lolote ambalo utakuwa hapo juu kuna vitu ambavyo unatakiwa kuvifanya
ila kufanya siku zako za kustaafu kuwa njema kifedha.
Kuna baadhi ya nchi kama sikosei china ikiwa mojawapo, hii mifuko ya pesheni ya
kijamii (social security) ziliondolewa na isipokuwa mfanyakazi ana jukumu la
kupanga kiasi cha fedha ambacho atahitaji baada ya kustaafu. Hali iko tofauti kwa
nchi nyingi za Afrika, mifuko ya kijamii inawatunzia watumishi fedha na wakati
wa kustaafu wanawapatia fedha yote ili wakatumie au wakapange namna ya
kuzitumia. Suala hili limewaumiza wengi kwa sababu wanapokea fedha nyingi
bila kuwa na mipango sahihi iliyotafitiwa kwa lengo la kuwekeza isipokuwa fursa
yeyote inayojongea mbele ya macho ya mstaafu anaichukua na kuwekeza fedha
zake. Kutokana na kuingia kwenye biashara wasizozifahamu wanajikuta
wanapoteza fedha nyingi na kwa takribani miaka miwili ya kustaafu ya kwanza,
wastaafu wengi wanakuwa wamemaliza fedha zao zote. Kwa upande wa wasio
kwenye ajira rasmi ndio kabisa hata wazo la kupanga kuwa kuna siku watastaafu
hawana kabisa na hawa pia huwa hawabaki salama ndio kinachofanya mtu ana
miaka 70 lakini bado anaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujikimu kimaisha
kwa sababu hakupanga kuwa kuna kustaafu. Hivyo ni muhimu kupanga na kujua
kuwa siku moja kuna kustaafu kufanya kazi. Mipango hii ikianza mapema,
inasaidia kuweka unafuu katika miaka ya ustaafu.
Mosi, ili uweze kuendesha biashara na kufanikiwa unahitaji muda kwa ajili ya
kuijenga akili yako ili iwezi kufikiri kama mfanyabishara na pia uwe na ujuzi wa
kibiashara husika. Ujuzi hauwezi kutengenezwa kwa siku moja inahitaji muda.
Sasa unakuta mstaafu ana miaka 40 anafanya kazi kama muajiriwa ila akistaafu
anataka awe mfanyabiashara hapo hapo bila kujua kuwa anahitaji kuwa na ujuzi
ambao utamchukua muda kuujenga ili afanikiwe na ndio maana wengi sana
wanafeli
Pili, mara nyingi huwa inawachukua watu kupoteza biashara moja au mbili ili
kuweza kusimamisha biashara au unakuta biashara nyingi zina kaa miaka 2 au 3
kabla hazijaanza kutengeneza faida wakati huo mstaafu anategemea fedha hiyo
hiyo kujikimu hivyo anajikuta anashindwa kusimamisha biashara ipasavyo.
Sio kitu cha kushangaza kuona msataafu anatumia fedha ya kustaafu kununua gari
la kutembelea, kuoa, kujenga nyumba ambayo haina sura ya kuingiza mapato
ambapo mwisho wa siku anaishiwa pesa. Matumizi yote ya pesa kuna matumizi
ya aina mbili yaani matumizi yenye lengo la kuingiza kipato na matumizi
yanayotoa fedha moja kwa moja kwenye mfuko wa mtumiaji. Mfano, unavyotumia
pesa kuwekeza hayo ni matumizi ila yana sura ya kukuingizia kipato siku za
mbeleni na unapotumia hela kunywa kinywaji basi hayo matumizi hayana sura ya
kukuingizia kipato. Kwa hiyo kama mstaafu unapojiingiza katika matumizi yasiyo
na sura ya kuingiza kipato kwa kiwango kikubwa huku akiwa hana vyanzo
vingine vya mapato, matokeo yake ni fedha itaisha baada ya muda fulani.
Kabla haujapanga unahitaji kiasi gani ukisha staafu lazima ukae chini na kuanza
kupanga kila kitu ambacho unaweza kuwa unakihitaji katika muda wako wa
kustaafu. Hii itakupa picha ni kiasi gani unatakiwa kuwa nacho au fedha yako iwe
katika mfumo gani ili ikuwezeshe kufanikisha malengo yako.
Yafuatayo ni baadhi ya mahitaji ambayo mtu anaweza kuwa nayo kama atahitaji
kustaafu
(i) Matibabu
(ii) Chakula
(iii) Starehe
Tukija kwenye suala la kutalii huo muda sisi hatuna, unakuta tuko busy
kukimbizana na maisha kwa kiwango ambacho inafikia mtu anakuwa kama
amezaliwa ili afanye kazi hana muda wa kupumzika na akistaafu ndio kabisa hana
hata senti ya kutembea hata vituo vya utalii vya nchi yake. Kwa hiyo kama una
pendelea kutembea lazima hili pia liwe katika bajeti yako kwa sababu litakusaidia
kujua ni kiasi gani unahitaji ukistaafu.
(iv) Kutimiza ndoto
Kadri siku zinavyosogea utaona kuwa mahitaji yako yanabadilika hivyo utakuwa
unabadilisha ratiba yako kadri unavyoona mahitaji yanatokea hiyo hapo juu
nimetoa kama picha tu ambayo inaweza kukusaidia katika upangaji
Mfano halisi
Hatua ya pili
Hapa katika hatua ya pili unafanya uchaguzi wa kuwa pesa ambayo itakuwezesha
kujikimu kwa miaka yako ya kusataafu itatoka wapi. Ngoja nikupe mifano miwili
Watu wawili wanaweza kuwa wamepokea TSH 100 Milioni kutoka kwenye
pensheni na mtu wa kwanza akaamua kuiwekeza hii 100 milioni katika uwekezaji
ambao unampa mrejesho wa 12% kwa mwaka na malengo yake ni kuwa atakuwa
anatumia 1 milioni kwa mwezi kwa miaka yote ya baada ya kusataafu. Hapa ina
maana kiasi ambacho atakuwa anatumia kwa mwaka ni kutoka katika faida na
mtaji wake wa 100 milioni utabaki palepale. Na mtu wa pili akaamua mimi pesa
yangu sita iwekeza bali nitaweka benki na nitakuwa nachukua kiasi cha milioni
12 kwa mwaka, au anaweza kuiwekeza pia ila akaamua kuwa atakuwa anachukua
faida na sehemu ya mtaji. Mfano faida kwa mwaka ni 12 milioni yeye anaweza
kuchukua milioni 13 kwa mwaka au zaidi ni uchaguzi wako.
Ila kwa sisi ambao bado tunapanga pensheni yetu ni vyema tukawaza kuwa pesa
ambayo tutakuwa tunaitumia ni faida tu na sio mtaji kwani haujui utaishi miaka
mingapi baada ya kustaafu unaweza kudhani kuwa utaondoka duniani mapema na
hivyo utumie mtaji pamoja na faida ukakuta unaishi miaka mingi zaidi ya ambavyo
umetegemea, hivyo ni bora kuwaza kuchukua faida tu na sio mtaji
Hatua ya tatu
Turudi kwenye mfano wetu, tumeona kuwa huyu kijana ambaye ana miaka 30 ya
kuwekeza katika mahesabu yake ni kuwa kwa mwaka atakuwa anahitaji TSH 12
milioni ili kuendesha mahitaji yake, sasa tukichukulia kwa mrejesho maarufu wa
uwekezaji ni 10% ina maana ili huyu kijana awe na uweze wa kutumia 12 milioni
kwa mwaka ambayo ni faida basi itambidi awekeze milioni 120 wakati wa
kustaafu au awe na milioni 120 wakati wa kustaafu ili kwamba 10% ambayo ndio
mrejesho wa uwekezaji umuwezeshe kupata milioni 12 kila mwaka bila kuathiri
mtaji wake.
Hatua ya nne
Hatua ya nne ni kujua hii milioni 120 tunaipataje ndani ya miaka 30 ijayo
Sasa kuna njia mbili ambazo tunaweza kuzitumia ili kupata hii milioni 120 baada
ya miaka 30 ambayo ndiyo itatuwezesha kupata milioni 12 ambayo tunaihitaji kwa
ajiri ya kuendesha maisha baada ya kustaafu, njia zenyewe ni kama ifuatavyo
(i) Kuwekeza taratibu taratibu
kama tulivyoona wakati tunajifunza kutumia kikokotozi cha UTT AMIS, kuwa
unaweza kuwa unawekeza kidogo kidogo kutokana na uwezo ulionao na baada ya
miaka 30 ukatimiza hii milioni 120. Tuone mfano
Kwa mfuko wenye mrejesho wa12% kwa mwaka itambidi huyu muwekezaji
awekeze 33,995/= kwa mwezi kwa miaka yote 30 ili baada ya hiyo miaka awe na
milioni 120
Kwa mfuko wenye mrejesho wa 13% itambidi awekeze 27,134/= kila mwezi kwa
miaka 30
Kwa mfuko wenye mrejesho wa 10% itambidi awekeze 52,647/= kwa mwezi ili
kufanikisha lengo lake
(ii) Kuwekeza kwa mara moja
Namna ya pili ni ya kuwekeza kwa mara moja, hapa kama una kiasi cha kuwekeza
kwa mara moja unaweza kuwekeza katika mfuko na ukaendelea na mambo
mengine huku uwekezaji wako unakua, tukirudi katika kikokotozi cha UTT
AMIS tunaweza kupata majibu.
Kwa hiyo kwa mfuko ambao una mrejesho wa 13% kwa mwaka itamuhitaji
awekeze milioni 3 na elfu sitini na saba (3,067,806/=)
Hatua ya tano
Kutokana na umri ulio nao na muda ambao unahitaji kustaafu basi unaweza kujua
ni muda gani uliobaki kwa ajili ya kufanya uwekezaji wako na hii itakusaidia
katika kupanga ni jinsi gani uwekeze, katika mfano wetu hapo juu tumeona kuwa
muwekezaji ana miaka 30 na anahitaji kustaafu akiwa na miaka 60 kwa hiyo muda
alio nao kuwekeza ni miaka 30.
Hatua ya mwisho
Ili kujua bei ya kipande inapigwaje tuanze kwa kutengeneza kampuni yetu
kwanza ya uwekezaji kama UTT AMIS kampuni yetu inaitwa WISE INVESTOR
INVESTMENT COMPANY na inaanza na mtaji wa 1 milioni ambao tunanunua
vipande 1000. Kwa haraka haraka mtaji wa TSH 1 na vipande 1000 ina maana
thamani ya kila kipande ni 1000 na kampuni yetu haina deni
Kwa hiyo kampuni yetu inaanza na mtaji wa 1MLN (TSH) na idadi ya vipande ni
1000 na thamani ya kila kipande ni 1000 sasa meneja wa mfuko ambaye ni bro
chagamba anaenda kuwekeza hii hela katika soko la hisa (DSE) na akifika kule
ananunua hisa za CRDB peke yake kwa bei ya 100/= kwa kila hisa na anapata hisa
10000
Kwa hiyo mfuko wetu una hisa 10000 za CRDB na baada ya hapo siku hiyo hiyo
bei ya hisa ya CRDB inapanda kutoka 100/= kwenda 120/= kwa hiyo unaona mfuko
wetu umepanda thamani
Kumbuka hisa zetu tulinunua kwa bei ya 100 na tukawa na hisa 10000 sasa bei
hisa imepanda thamani ina maana mfuko wetu umekua kutoka 1MLN kwenda 1.2
MLN sasa bei mpya ya kipande inakuwaje? inakuwa ni sawa na thamani ya mfuko
kugawanya kwa idadi ya vipande
Kwa hiyo bei mpya ya sasa ya kipande ni 1200/=, baada ya hapo kesho yake bei ya
hisa ya CRDB inapanda tena inatoka 120/= kwenda 130/=, hapo mfuko wetu
umekua tena kwani hisa zetu zimepanda bei kutoka kutoka 120/= kwenda 130/=
Kwa hiyo jumla ya thamani ya mfuko inakuwa 130/= kuzidisha kwa hisa 10000
ambapo thamani mpya ya mfuko ni 1.3 MLN
Baada ya muda CRDB inatoa gawio la 22 kwa kila hisa, na sisi tunapokea gawio
kwa hisa zetu 10000/=
Gawio letu linakuwa 220,000/= ila kumbuka kuna kodi ya zuio tunalipa ya 5%
kwa gawio letu kwa hiyo baada ya kulipa tunabakiwa na 209,000/=
Kwa hiyo mfuko wetu unakua tena kwani tumepata 209,000/= kutoka kwenye
gawio
Kwa hiyo bei mpya ya kipande inakuwa 1.509 MLN /1000 = 1509/=
Hivi ndivyo bei ya kipande inapigwa sasa hili gawio ambalo tumepokea tunaweza
kuliwekeza tena.
VITU MUHIMU VYA KUKUMBUKA
(i) Bei unayoiona leo sio ya leo bali ni ya jana
Kama una kumbukumbu vizuri bei ambayo tumekuwa tunaitumia kufanya hesabu
ni bei baada ya soko kufungwa. Kwa hiyo bei ya leo ndio utaiona kesho ila bei ya
kesho itapigwa jioni baada ya soko kufungwa na itatolewa kesho kutwa. Maana
kuna watu wanadhani wakiomba kununua leo basi bei wakakayo nunulia ni bei ya
leo hapana, bei utakayonunulia ni ile ambayo itatolewa kesho inayoitwa kwa jina
la kiingereza la FORWARD PRICING
Kama unavyojua kampuni huwa ina matumizi kwa hiyo baadhi ya pesa ambayo
inapatikana kwenye uwekezaji inaenda kwenye matumizi, kwa hiyo usidhani
kama kampuni imepokea gawio basi gawio lote litaenda kuwa thamani ya
kipande, baadhi ya pesa inaweza kupunguzwa na kwenda kwenye matumizi hii
haitaonekan katika thamani ya mfuko
katika kupiga mahesabu ya kipande kama mfuko una deni basi tunachukua mali
na kutoa madeni ili kupata mali halizi za mfuko na hizi ndio tunagawanya kwa
idadi ya vipande ili kujua bei ya kipande.
KUSHUKA KWA BEI YA KIPANDE
Kama tulivyoona katika jinsi bei ya kipande inavyopigwa,kama ikitokea katika
mfuko wetu kuna hisa ambayo imeshuka bei basi kinachotokea ni kuwa thamani
ya mfuko inapungua na ikipungua tunavyokuja kupiga hesabu za bei mpya ya
kipande basi utaona kipande kimeshuka thamani mfano
Kama bei ya hisa ya CRDB ilikuwa 130 na thamani ya mfuko ilikuwa 1.3 MLN
ikitokea bei imeshuka mpaka 125 basi na mfuko wetu utapungua thamani kutoka
1.3 MLN kwenda 1.25 MLN kwa hiyo bei mpya ya kipande ni
Kwanza nafahamu huyu mtu ametoa uelewa huu kwenye hisa, kwani katika hisa
kuna kipindi bei ya hisa inaweza kupanda mwaka huu na mwaka ujao ikashuka
zaidi au ikabaki pale pale kwa Muda mrefu. Kwa hiyo mtu wa namna hii
ukimuelekeza kuwekeza UTT AMIS ambako anapata faida kwa ukuaji wa bei ya
kipande anakuwa muoga. Baada ya kufanya uchunguzi nimegundua kuwa bei ya
kipande cha UTT AMIS ijapokuwa inaweza kuwa na kipindi ambacho inashuka
kwa muda ila muelekeo wa jumla ni kuwa bei ya kipande inapanda juu tu haishuki
kama ilivyo katika hisa na hivi ndivyo nilivyofikia katika hitimisho langu.
Kuna sababu 3 ambazo ninadhani zitafanya kipande kiendelee kukua siku hadi
siku:-
Kwa hati fungani ya TSH 1 yenye riba ya 15.95% ina maana kila mwaka mfuko
utakuwa unapokea TSH 159,500/= na hivi ndivyo mfuko wetu utakavyokuwa kwa
miaka 5 ya kwanza kama ilivyo katika jedwali hapo chini, kwa jinsi bei ya kipande
inavyopigwa rejea hapo juu. Hapa inakuwa hivi mwaka wa kwanza mfuko
utapokea 159,500/= na mfuko utakuwa umekua na kuwa na kiasi chaTSH 1,159,500
(milioni moja tuliyoanza nayo na hii ambayo tumeppokea kama riba) sasa bei
mpya ya kipande tunaipata kwa kuchukua thamani mpya ya mfuko kugawanya
kwa idadi ya vipande 10,000 ambapo kwa mwaka wa kwanza bei ya kiapande
inakuwa TSH 115.95/=.
Hivyo hata kama UTT AMIS hailipi gawio unaweza kupata faida na pia
unashauriwa uwekeze ukiwa na malengo ya muda mrefu kwani bei ya kipande
inaweza kushuka mwaka huu ila kiujumla bei ya vipande inapanda siku hadi siku
ukiangalia utendaji wa mifuko hii toka inaanzishwa utagundua kuwa
ninachokisema ni sahihi na hii ni sababu moja ngoja tuangalie sababu nyingine.
JINSI UTT AMIS INAVYOFANYA KAZI
Ukifahamu jinsi UTT AMIS inavyofanya kazi basi hofu ya kuwa kipande
kitashuka kama ilivyo kwenye hisa na utapata hasara inapungua. Tumeona katika
kipengele kilichopita cha mapato ya UTT AMIS kuwa ina sehemu ambayo
inapokea mapato ya kuaminika kama riba ya hati fungani na gawio sasa kitu
kinachoongezeka hapa ni kuwa pesa inayopokelewa pia inawekezwa na hivyo
kufanya mfuko kukua kwa kasi zaidi kwani wanatumia riba ya kampaundi. Ngoja
nitoe mfano wa mfuko ambao unapokea riba na gawio uone kwa nini kwa mjengo
huu wa ufanyaji kazi basi bei ya kipande itaendelea kukua siku hadi siku:-
Mfano
Tuchukulie mfuko ambao umewekeza katika hati fungani kwa mwaka 2019 na
2020. Mfuko huu una ukubwa wa TSH 2 milioni na idadi ya vipande ni 10,000 na
bei ya kipande TSH 200/=. Milioni moja imewekezwa katika hisa za CRDB kwa
bei ya 100 ambapo mfuko utakuwa na hisa 1,000,000/= na nyingine katika hati
fungani ya miaka 25 yenye riba ya 15.95%.
Kwa mwaka 2019 CRDB ilitoa gawio la 17 kwa hisa ambapo kwa hisa 10,000
mfuko ulipata 170,000/= kutoka katika hati fungani mfuko ulipokea 159,500/=.
Jumla ya thamni mpya ya mfuko itakuwa 2,329,500/= na bei mpya ya kipande
itakuwa TSH 232.95/= sasa kinachokuja kuweka utofauti ni kuwa hii pesa
iliyopatikana inawekezwa tena ili mwaka unaokuja faida iwe kubwa zaidi na
hivyo kufanya mfuko uwe na faida ya riba ya kampaundi.
Tuchukulie faida ya mwaka 2019 ilitumika kununua hisa za CRDB kwa bei ya 100,
hivyo mfuko sasa utakuwa na hisa 13,295. Mwaka 2020 CRDB ilitoa gawio la TSH
22/= kwa kila hisa hivyo mfuko ulipokea TSH 292,490/= na kutoka katika hati
fungani, mfuko ulipokea TSH 159,500//= kwa hiyo mfuko utakuwa na kuwa na
thamani ya TSH 2,451,990/= na hivyo kufanya bei ya kipande kuwa TSH 245.199/=
Sasa huu mtindo wa kuwekeza hela ambayo inapatikana kila mwaka ni moja kati
ya sababu ambazo zinafanya mfuko ukuze thamani ya kipande kwa siku hadi siku.
Ukichukua sababu hizo tatu ni rahisi kuona kuwa bei ya kipande haiwezi
kushuka na kukaa hapo hapo kwa miaka kadhaa kwani mapato mengine kama
hati fungani na gawio la hisa yanasaidia kukuza bei ya kipande na hata kama bei
ya hisa ambayo mfuko umewekeza inaweza kushuka. Kama tulivyoona
mchanganuo wa sehemu ambayo mifuko hii imewekeza utaoa hisa haina asilimia
kubwa sana na hivyo kufanya kinachotokea katika hisa kutokuwa na madhara
makubwa kwenye bei ya kipande. Ukiangalia muenendo wa bei za vipande kwa
miaka iliyopita unaweza kuona ya kuwa hili ni sahihi.
Angalizo
Kuna miaka bei ya kipande inashuka katika baadhi ya mifuko kutokana na hali ya
uchumi kwa hiyo kama muwekezaji unatakiwa kulifahamu hili.
(ii) Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
Swali: Je ninaweza kuwa na akaunti katika mifuko zaidi ya mmoja, yaani nikawa
na umoja, jikimu na liquid au mfuko mwingine
Jibu: NDIYO, ila kila mfuko utakuwa na akaunti yake, siyo kama hisa kuwa
akaunti moja ya DSE inakuwa na hisa zaidi ya moja, hapa ukitaka kuwa na mfuko
mwingine unafungua akaunti ya mfuko husika.
Swali: Katika hisa mtu anapata faida pale ambapo ananunua hisa kwa bei ya chini
na kuuza bei inapopanda je kwa vipande vya UTT AMIS ikoje
Jibu: Unaweza kununua pale ambapo bei ya kipande imeshuka, hasa hasa kwenye
mifuko yenye hisa ila kutokana na masharti ya mifuko na pia uendeshwaji wa
mifuko ni ngumu sana kuona poromoko la bei ya vipande kama ilivyo hisa na pia
kama tulivyoona bei ya kipande kwa asilimia kubwa inapanda mwaka kwa
mwaka hivyo sio rahisi kununua bei ikiwa chini na kuuza tena kama ilivyo katika
hisa ijapokuwa bei ya kipande kuna kipindi inashuka
hii ni kwa mifuko ambayo imewekeza katika hisa ya kuwa bei ya hisa inaweza
kupanda au kushuka na hivyo kuathiri thamni ya mfuko
c) Badiliko la kodi
Kuna faida nyingi ambazo UTT AMIS inazipata kwenye upande wa kodi kwanza
katika sehemu ambazo imewekeza na pili kwa wawekezaji ambao wamewekeza
UTT AMIS, ukiwekeza katika soko la hisa kwa sheria za sasa ni kwamba gawio
utakalopokea litakatwa kodi ya 5% ambayo ni unafuu kwa makampuni yaliyoko
soko la hisa ikitokea serikali ikabadilisha sheria ya kodi itaathiri mapato ya mfuko
na pia katika hati fungani za serikali za muda mrefu kuna unafuu wa kodi kama
sheria itabadilika basi na mapato ya mfuko yatabadilika. Kitu kingine ni kodi kwa
upande wa muwekezaji wa UTT AMIS, kwa sasa hakuna kodi anayotoa ila sheria
zinaweza kubadilika siku zijazo.
SAIKOLOJIA NA UWEKEZAJI
Watu wengi wanatamani sana kuwa na pesa nyingi kwa haraka zaidi kitu
ambacho sio kibaya ila sio watu wengi wenye njia ambazo zinaweza kuwafanya
wakapata pesa nyingi kwa haraka ila njia ambazo zinawafaa kutokana na maisha
yao ni njia kama hizi za kuwekeza kwa muda mrefu ila wengi huwa hawazitilii
mkazo na miaka inaenda na kurudi na mwisho wa siku wanakosa ile pesa nyingi
ambao walidhani wangeipata kwa haraka na wanakosa hii pesa nyingi ambayo
ingekuja taratibu.
Kwa hiyo wewe uwe na hekima, ukipata njia ya kukuwezesha kupata hela kwa
haraka ni vizuri ila ukiwa na nafasi ya kuwekeza taratibu hii pia ni njema, kwani
njia zote zitakuletea fedha na pesa ikipatikana siku zote itapata matumizi hata
kama itakuja nyingi kiasi gani.
Tumeona kuwa kupitia UTT AMIS unaweza kuwa unawekeza kidogo kidogo
kwa siku nyingi na ukaja kupata milioni 100 mpaka bilioni, kuna watu watapuuzia
kwa kusema miaka 30 ni mingi sana ila ninakuhakikishia kuna wengi ambao
wanasoma kitabu hiki ambao watafika miaka 30 ijayo na bado watashindwa kuwa
na milioni 100 ambayo kama wangewekeza UTT AMIS wangeipata.
Miaka 30 sio mingi kwani ukianglia hata hii pensheni ambayo wastaafu wanapata
unakuta wameichangia kwa miaka 30 au zaidi sasa kwa nini ushindwe kuwekeza
wewe mwenyewe.
SEHEMU YA SABA
Kama huyu mtu ataamua kununu hisa za 1000/= hii pia itakuwa kama matumizi ila
utofauti wake ni kuwa hii pesa haijatoka mfukoni mwake bali inaenda kuwa
MALI ambayo utaikuta katika ripoti ya hali ya fedha na kama unavyojua mali
huwa ndio inazalisha mapato. Sasa utofauti wa watu hawa wawili ni kuwa
aliyenunua soda amemtajirisha muuza soda ila aliyenunua hisa amejitajirisha
mwenyewe kwani hizi hisa zitaendelea kuwa kwake na kuendelea kuzaa pesa
zaidi na kama akifanya hivi kwa miaka 10 atafika kipindi cha kuwa na vyanzo
viwili vya mapato kimoja ni kile cha kila siku na kingine ni hisa ambazo
ametengeneza ila yule ambaye alikuwa anakunywa soda ni muuza soda tu ndio
anakuwa ametajirika.
Sijasema usitumie pesa kwenye matumizi mengine ila jifunze kujilipa kwanza na
hiyo iwe ndio aina ya maisha unayoishi. Utatengeneza utajiri bila jasho. Mtu
anayetumia hela kununua uwekezaji hana utofauti na mtu ambaye amechukua
fedha mfuko wa kushoto na kuiwekza mfuko wa kulia ambapo inaweza kuzaa
tena.
Tanbihi
HITIMISHO
Natumaini umejifunza mambo mengi sana katika kitabu hiki sasa ni wakati wa
kuyafanyia kazi yote uliyojifunza nikutakie kila la heri katika safari yako ya
uwekezaji na mafaniko katika uwekezaji wako