You are on page 1of 3

MUHTASARI WA MKUTANO WA TANO WA KIJIJI CHA LITUNDU TAREHE

19/07/2016.

AGENDA:-

1. KUFUNGUA KIKAO
2. KUSOMA MUHTASARI WA NYUMA
3. YATOKANAYO
4. KAMATI YA ULINZI NA USALAMA
5. USALAMA WA WATOTO KUPANDA MAGARI WAKATAZWE.
6. HUDUMA ZA JAMII KAMATI
7. TAARIFA YA FEDHA
8. KUFUNGA KIKAO

MUHTASARI NA 1/5/2016 KUFUNGUA MKUTANO

M/kiti katika agenda hii alianza kwa kuwasaslimu wananchi kwa na kuwapa
pole ya safari na kuwapongeza kwa mahudhurio yao mazuri pia aliwataka
wananchi wawe huru katika kuchangia maoni, mawazo na hata ushauri
kutokana na ajenda zilizo kuwa zimeandaliwa katika mkutano na hatimaye
mkutano ulianza mnamo saa 7:00 mchana.

MUHTASARI NA 2/5/2016 KAMATI YA ULINZI NA USALAMA

M/kiti katika agenda hii alitoa maelekezo juu ya ulizi na usalama kuwa ni jinsi gani
viongozi kuwa makini na eneo linalomhusu ili kuepukana na wizi au udokozi wa
ovyoovyo na zaidi ni kuudhibiti kabisa, pia m/kiti aliwaeleza wananchi kuwa hata
kama ni raia unamkuta mtu mgeni katika kaya ya mtu mwenyeji yeyote na
unauhakika ya kuwa hajamripotia katika ofisi ya kijiji kwa maana ya uongozi
wa kijiji au katika kitongoji ni lazima achukuliwe hatua za kisheria kwa
mwenyeji huyo ambaye amemhifadhi mtu mgeni bila taarifa yoyote.

AZIMIO
Wananchi wote kwa kauli moja waliridhia azimio la m/kiti pia walishauri
kuwa ni vizuri mwananchi mmojammoja awe mlinzi wa mali zake na za
mwenzake,pia wananchi waliazimia kuwa endapo kuna mwananchi yeyote
atapiga yowe isiyo na utaratibu wowote atatozwa faini ya tsh 30000/= na
wale wenye tabia ya kuwakamata wanawake porini kwa kuwabaka endapo
wakibainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao .

MUHTASARI NA 3/5/ 2016 USALAMA WA WATOTO KUPANDA MAGARI


WAKATAZWE / KUWAELIMISHA.

M/kiti katika agenda hii aliwaelekeza wananchi kwa makini athari za rifti
kwa watoto kutokana na dunia ya sasa ilivyo basi aliwasihi wananchi kuwa ni
vizuri kila mzazi achukue jukumiu la kumlinda na kumuonya kila mtoto hata
kama sio wake juu ya kuomba lifti kwa watu wasiowajua.

AZIMIO
Wananchi wote kwa kauli moja waliridhia azimio na ushauri wa m/kiti kuwa
endapo mtoto mmoja ataathilika na hizo rifti madhara yatakuwa kwa wote
hivyo wananchi wote wawe na umoja juu ya suala hilo.

MUHTASARI NA 4/5/2016 KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII

M/kiti katika agenda hii alisimama na kuwaelekeza wananchi kuwa kwenye


agenda hii ina mambo mengi na mambo hayo yanafanywa na kamati
husika ambayo inajukumu zito la kuangalia mambo ya kijamii zaidi
wakishirikiana na mtendaji wa kijiji na mambo hayo ni kama yafuatayo :-
1. Utunzaji wa vyazo vya maji
Kuwa wananchi wote wanaolima karibu na vyanzo vya maji pamoja na
mapito ya maji (mto) na wanaolima kwenye malisho na mapito ya
ngombe watatakiwa waitwe ofisini ili kupewa elimu juu ya utunzaji wa
vyanzo vya maji
2. Taarifa ya ujenzi wa ofisi ya kitongoji cha litundu kuwa wameshaanza
ujenzi huo.
3. Kuletewa msaidizi wa ustawi wa jamii kijijini ni agizo kutoka wilayani.
4. Taarifa ya kamati iliyoundwa ya kusimamia watoto wanaoishi katika
mazingira hatarishi.
5. Taarifa ya uanzishaji rasmi wa watoto wa kusoma chekechea wenye
miaka 3-/hata 2, na walimu walioteuliwa ni TEGEMEA KITALIMA na
NEEMA LYODE.
6. Utunzaji wa mazingira ya nyumbani kuwa msisitizo uwe zaidi kwa mtu
binafsi na juhudi ziwe kwa pamoja kuilinda misitu inayotuzunguka.

AZIMIO.

Wananchi wote waliohudhuria katika mkutano huo baada ya kupata taarifa


hiyo walishauri kuwa wananchi wasisitizwe kujitoa katika huduma za kijamii
na utunzaji wa mazingira.

MUHTASARI NA 5/5/2016 KUFUNGA KIKAO


m/kiti katika agenda hii alimuagiza katibu /veo aweze kusoma taarifa ya mapato
na atumizi na mwisho baada ya kuwasomea wananchi aliwataka wananchi watoe
maoni na ushauri .

AZIMIO
Wananchi wote kwa kauli moja waliridhia taarifa iliyosomwa na mtendaji lakini kwa
maoni waliazimia/kushauri kuwa michango hichangwi kwa wakati na tatizo haliko
kwa mtendaji bali ni wenyviti wa vitongoji hivyo basi walishauri wenyeviti wa
vitongoji waiache tabia hiyo mara moja ili kujiletea maendeleo katika kijiji chetu .

MUHTASARI NA 6/5/2016 KUFUNGA KIKAO

M/KITI Katika agenda hii alimaliza kwa kusema anawashukuru wananchi


kwa mahudhurio yao mazuri , maoni , ushauri na hata kwa mawazo yao
mazuri katika agenda zilizo kuwa mezani na baadae aliwatakia safari njema
na jioni njema mnamo saa 11:08 jioni .

..

M/KITI
KATIBU

You might also like