Professional Documents
Culture Documents
1)
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa
fursa uliyonipa kutoa maelezo yangu binafsi katika
Bunge lako Tukufu leo. Ninatoa maelezo haya kwa
mujibu wa Kifungu cha 50 (1) cha Kanuni za Kudumu
za Bunge, Toleo la Aprili, 2013 kinachosema kwamba,
2)
Mheshimiwa Spika, Nilijiunga na Bunge lako
Tukufu kwa mara ya kwanza Mwaka 2015 nikiwa na
lengo kuu la kupaza sauti ya vijana kwenye masuala
yanayohusu nchi yetu na kutetea maslahi ya
Watanzania hususani Wananchi wa Jimbo la Kigoma
Kaskazini na Mkoa wa Kigoma, na Watanzania kwa
ujumla. Nilichaguliwa na wananchi wa Kigoma
Kaskazini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA). Wananchi wa Kigoma
Kaskazini walinichagua tena Mwaka 2010 kupitia
tiketi ya CHADEMA.
3)
Mheshimiwa Spika, kupitia fursa ya ubunge
niliyopewa na wananchi wa Kigoma Kaskazini kwa
udhamini wa CHADEMA, nimejifunza mengi hapa
Bungeni na nje ya Bunge hili. Nimeijua nchi yangu,
4)
Mheshimiwa Spika, Ninawashukuru sana
wanachama wa CHADEMA kwa dhamana mbalimbali
walizonipa ndani ya CHADEMA. Ninawashukuru
viongozi wangu na hasa Mwenyekiti wetu
Mheshimiwa Freeman Mbowe kwa kunilea na
kuniamini kufanya naye kazi kwa kipindi chote tangu
nilipokuwa mwanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, katika chama na hapa Bungeni. Kama
ambavyo nimesema mara nyingi, CHADEMA imenilea
na kunikuza tangu nikiwa na umri wa miaka 16 na
tangu kipindi hicho nimejifunza mengi.
5)
Mheshimiwa Spika, Nichukue nafasi hii
kuwashukuru sana wananchi wa Kigoma Kaskazini
kwa mapenzi yao na imani waliyonipa na
kuniwezesha kukalia KITI hiki ninachokalia ndani ya
Bunge lako Tukufu. Nashukuru kwamba juzi nilipata
fursa ya kipekee ya kuwashukuru kwa imani
waliyonipa kuwatumikia kwa vipindi viwili mfululizo.
Mola atawalipa wananchi wa Kigoma Kaskazini kwa
imani kubwa walioionyesha kwangu na kuniwezesha
kulitumikia Taifa langu kwa namna nilivyolitumikia.
6)
Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu sasa
pamekuwa na msuguano wa kiuongozi kati yangu na
viongozi wangu ndani ya CHADEMA uliosababishwa
na tofauti za kimtazamo juu ya tafsiri pana ya
demokrasia ndani ya chama chetu. Hatimaye tofauti
hizi zilipelekea mwezi Novemba 2013 Kamati Kuu ya
7)
Mheshimiwa Spika, katika hali ya kawaida na
kwa mujibu wa katiba ya chama chetu, ilitarajiwa
kwamba baada ya maamuzi ya Mahakama Kuu,
Kamati Kuu ingekaa na kunipa rasmi mashtaka yangu
yanayohusu uanachama wangu, mimi kuitwa
kujieleza na hatimaye Kamati Kuu kutoa uamuzi
wake. Hata hivyo, mara baada ya hukumu ya
Mahakama Kuu dunia nzima ilitangaziwa na
Mwanasheria wetu Mkuu, kwa niaba ya chama,
kwamba mimi nimeshafukuzwa na sio mwanachama
tena wa CHADEMA. Baada ya hapo viongozi wangu
wametoa matamko mbalimbali yote yakionyesha
kwamba sitakiwi tena katika chama hiki, pamoja na
kwamba hadi ninapoongea hapa leo sijawahi
kukabidhiwa barua yeyote inayonitaarifu kufukuzwa
kwangu katika chama.
8)
Mheshimiwa Spika, kutokana na maelezo ya
hapo juu, ni wazi kwamba uanachama wangu wa
kisiasa ndani ya CHADEMA umeshaondolewa.
Ninaweza kuendelea kupigania uanachama wangu
kisheria na kwa kweli nina sababu na misingi yote
kubaki na uanachama wangu kisheria. Lakini mimi ni
mwanasiasa. Sikuja hapa bungeni kwa sababu ya
kushinda kesi mahakamani. Nilichaguliwa na
wananchi wa Kigoma Kaskazini na ninatambua
kwamba huwezi kuwa mbunge bila udhamini wa
chama cha siasa. Huu ndio utaratibu wa kisheria
tuliojiwekea. Kwa mujibu wa viongozi wangu katika
chama ni kwamba udhamini wa chama changu
umekwishaondolewa.
9)
Mheshimiwa Spika, kutokana na maelezo ya
hapo juu, ninaomba kukutaarifu wewe na Bunge lako
tukufu kwamba sina mpango wa kuendelea kupigania
uanachama wangu wa CHADEMA katika viunga vya
mahakama. Kwa hiyo ninatangaza rasmi leo kwamba
taratibu za kikatiba zitakapokamilika tu nitaachia
uanachama wa CHADEMA, chama nilichokipenda
sana kwa sababu ya kuendelea kukua kwa tofauti za
kiitikadi, kimtazamo na hata kibinafsi kati yangu na
viongozi katika chama changu. Nimeona kuwa
kuendelea kupigania uanachama kisheria ni kutatiza
na kukwaza harakati za mabadiliko hapa nchini katika
wakati ambapo mfumo wa kisiasa unatambua uwepo
wa vyama vingi vya siasa. Kwa kuwa taratibu hizo
sijui zitakamilika lini, natumia fursa hii kuwaaga
wabunge wenzangu.
Mheshimiwa Spika,