Professional Documents
Culture Documents
MACHI 2017
DODOMA
UTANGULIZI
0
nikianza na Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Kyela
ambaye sasa amepewa dhamana ya kuongoza Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mheshimiwa Prof. Palamagamba A.
Kabudi (Mb), Waziri wa Katiba na Sheria. Aidha, natoa pongezi za
dhati kwa Mama yetu Mheshimiwa Salma Kikwete kwa kuteuliwa
kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vile
vile, ninawapongeza Waheshimiwa Wabunge wote waliofunga ndoa
baada ya Mkutano wa Sita wa Bunge la 11.
SEHEMU YA KWANZA
1
6. Mheshimiwa Mwenyekiti, wastani wa mfumuko wa bei ulikuwa
asilimia 5.2 mwaka 2016 ikilinganishwa na asilimia 5.6 mwaka 2015,
ukipungua kutoka asilimia 6.5 Januari 2016 hadi asilimia 5.0
Desemba 2016. Kwa mwezi Februari 2017, mfumuko wa bei ulifikia
asilimia 5.5. Wastani wa riba za mikopo ya mwaka mmoja ambayo
hutolewa na mabenki ya biashara ulipungua kutoka asilimia 14.22
Desemba 2015 hadi asilimia 12.87 Desemba 2016, wakati riba za
amana za mwaka mmoja zilipungua kutoka asilimia 11.16 hadi
asilimia 11.03 katika kipindi hicho. Hivyo, tofauti kati ya riba za
mikopo na amana za mwaka mmoja imeendelea kupungua, kutoka
wastani wa pointi 3.06 za asilimia (percentage points) mwezi
Desemba 2015 hadi pointi 1.83 za asilimia mwezi Juni 2016. Katika
kipindi kinachoishia Desemba 2016, mauzo ya bidhaa na huduma
nje ilikuwa dola za Kimarekani milioni 9,381.6 ikilinganishwa na dola
za Kimarekani milioni 8,921.9 katika kipindi kama hicho mwaka 2015,
sawa na ongezeko la asilimia 5.2. Ongezeko hili lilitokana na
kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa asilia, dhahabu, bidhaa za
viwadani na mapato ya sekta za huduma, hususan utalii.
SEHEMU YA PILI
Miradi ya Kielelezo:
(i) Makaa ya Mawe Mchuchuma na Chuma Liganga
Njombe: maandalizi yote ya ujenzi wa miradi hii yamekamilika,
ikiwa ni pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya malipo ya fidia
kwa wananchi watakaopisha mradi. Vile vile, kampuni ya
Sichuan Hongda (Group) Corporation Ltd, ambayo ndio mbia
katika miradi hii, wametenga jumla ya dola za Kimarekani
milioni 300 kwa ajili ya kulipia sehemu ya mtaji (equity) wao
katika miradi. Hatua iliyobaki ni kukamilisha mazungumzo
kuhusu vivutio vya kodi vilivyoombwa na wawekezaji na bei ya
mauziano ya umeme na TANESCO.
14
Vihatarishi vya Utekelezaji wa Mpango
17
kutekeleza hili, Serikali imedhamiria kuongeza na kuimarisha
ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kuchukua hatua zifuatazo:
Mapato
38. Mheshimiwa Mwenyekiti, Sura ya Bajeti ya mwaka 2017/18
inaonesha kuwa jumla ya shilingi bilioni 31,699.7 zinatarajiwa
kukusanywa na kutumika katika kipindi hicho. Jumla ya mapato ya
18
ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri yanatarajiwa kuwa shilingi
bilioni 19,977.0 sawa na asilimia 63.0 ya bajeti yote. Kati ya mapato
hayo, mapato ya kodi ni shilingi bilioni 17,106.3 sawa na asilimia 85.6
ya mapato ya ndani. Aidha, mapato yasiyo ya kodi na mapato kutoka
vyanzo vya Halmashauri ni shilingi bilioni 2,183.4 na shilingi bilioni
687.3 kwa mtiririko huo. Ili kuhakikisha upatikanaji wa mapato hayo,
Serikali itaendelea kuimarisha usimamizi wa mapato na kuziba
mianya ya uvujaji wa mapato.
Matumizi
40. Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa upande wa matumizi, katika
mwaka 2017/18, Serikali inapanga kutumia shilingi bilioni 31,699.7
kwa matumizi ya kawaida na maendeleo. Kati ya fedha hizo, shilingi
bilioni 19,700.2 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, ikijumuisha
shilingi bilioni 7,205.8 za mishahara ya watumishi wa Serikali na
taasisi na shilingi bilioni 9,461.4 kwa ajili ya kulipia deni la Taifa.
Bajeti ya kulipia deni la Taifa imeongezeka kwa asilimia 18.3 kutoka
shilingi bilioni 8,000 mwaka 2016/17 kutokana na kuiva kwa mikopo
ya miaka ya nyuma iliyogharamia miradi ya maendeleo ambayo
fedha za kulipia mtaji na riba zimetengwa kwenye bajeti ya matumizi
ya kawaida. Matumizi mengineyo (OC) yametengewa jumla ya
shilingi bilioni 3,033 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 2,085.2 ni
matumizi yaliyolindwa na shilingi bilioni 274.9 ni matumizi
yanayotokana na mapato ya ndani ya halmashauri. Aidha, matumizi
ya maendeleo yatakuwa shilingi bilioni 11,999.6 ambapo kiasi cha
shilingi bilioni 8,969.8 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 3,029.8 ni
fedha za nje.
20
HITIMISHO
22