Professional Documents
Culture Documents
27 Juni, 2019
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI
WAZIRI MKU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi
katika kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji na biashara.
Amesema mpaka sasa, hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa kwa lengo la kuweka
mazingira wezeshi ya uwekezaji na biashara nchini.
Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Juni 27, 2019) jijini Dodoma wakati akifungua kongamano
la uwekezaji la mkoa wa Dodoma kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.
Waziri Mkuu amesema mkoa wa Dodoma una barabara za kuaminika za kiwango cha lami
zinazoiunganisha na mikoa mingine pamoja na nchi jirani.
Amesema ujenzi wa mradi wa kufua umeme katika Mto Rufiji ‘Stiegler’s Gorge’ wenye
uwezo wa kuzalisha MW 2,115, utaongeza upatikanaji wa nishati ya uhakika nchini.
Waziri Mkuu amesema anatarajia kuwa kongamano hilo litawezesha kupatikana kwa
wawekezaji mahiri kwa maendeleo ya uchumi na wananchi wa Tanzania.
1
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge alisema katika azma ya Selikali
ya kujenga uchumi wa viwanda wameandaa kongamano hilo ili kutangaza fursa zilizopo.
Dkt. Mahenge alitaja baadhi ya fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Dodoma kuwa ni
pamoja na uwepo wa ardhi ya kutosha kwa ajili ya kilimo, viwanda na taasisi (afya, elimu).
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
ALHAMISI, JUNI 27, 2019.