You are on page 1of 1

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

GAVANA WA BOT HAJAFUNGUA AKAUNTI YA “FACEBOOK”


Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inapenda kuutangazia umma kwamba Gavana wa Benki Kuu ya
Tanzania, Prof. Florens Luoga, hajafungua akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook,
kinyume na taarifa na picha zinazojitokeza katika katika mtandao huo kwa jina lake.
Kwa taarifa hii, tunapenda kuutangazia umma kupuuza chochote kinachopatikana katika akaunti
hiyo bandia inayojiita Florence Luoga, na ambayo inatumia picha mbalimbali za Gavana wa BoT
kinyume cha sheria.
Aidha, Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuwapa pole watu wote ambao kwa namna moja ama
nyingine wameathirika kutokana na yote ambayo yamejitokeza katika akaunti hiyo bandia,
ikiwemo kutumia jina la Gavana Luoga kutapeli na hata kutumiwa ujumbe wa matusi.
Pamoja na taarifa hii, hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa ili kumbaini mhalifu huyu kwa
kutumia akaunti hiyo kuchafua sifa ya Gavana Luoga katika jamii.
Tunauhakikishia umma kwamba, Gavana Luoga hajafungua akaunti kwa jina hilo na hivyo
taarifa zozote zinazotolewa kwenye akaunti hiyo ya Facebook hazina uhusiano wowote na Prof.
Florens Luoga.
Imetolewa na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki
botcommunications@bot.go.tz
Oktoba 29, 2019

You might also like