Professional Documents
Culture Documents
Ndugu Wanahabari,
Aidha katika kutoa ufafanuzi huo Kamishna CP Sabas alisema taarifa hizo za
uongo ambazo zilisambazwa na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema huku
akimtaka kujisalimisha katika kituo chochote cha Polisi, huku akitoa maagizo
kwa Kamanda Polisi Mkoa wa Singida kumtafuta Mh Lema popote alipo na
akamatwe.
3. Rajabu Abasi, (36), alifariki dunia tarehe 14/9/2019 usiku akiwa anapatiwa
matibabu katika Hospitali ya St. Gaspar, Itigi kutokana na tukio la
kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mtuhumiwa aitwaye Mohammed
Abdi, tukio lililotokea tarehe 13/9/2019 saa 3 usiku huko katika Kijiji cha
Mwamagembe. Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi ambapo
mtuhumiwa alimfumania marehemu akiwa na mke wake nyumbani kwa
mtuhumiwa. Mtuhumiwa amekamtwa na upelelezi umekamilika.
7. Mika Saimon, (38), alifariki dunia kwa kukatwa na vitu vyenye ncha kali
katika sehemu mbalimbali za mwili katika tukio lililotokea tarehe
15/11/2019 saa 10 jioni huko Kitongoji cha Idodoma, Tarafa ya Nkonko,
ambapo marehemu aliuawa na mtoto wake aitwaye Saimon s/o Mika kwa
akishirikiana na mama yake mzazi aitwaye Mea d/o Mwarabu pamoja na
rafiki wa mtoto wake aitwaye Robert Elia ambapo walikuwa wanataka
kurithi shamba la baba yao. Watuhumiwa wote watatu wamekamatwa na
upelelezi wa Polisi umekamilika.
8. Mshoma Ngassa, (30), Mkazi wa Itigi alifariki dunia kwa kupigwa kwa
fimbo kichwani na mume wake aitwaye Mariyambelele Senzo katika tukio
lililotokea tarehe 21/11/2019 saa 2:30 asubuhi huko Majiweni, Kata ya
Mitundu ambapo chanzo cha kifo ni wivu wa kimapenzi ambapo
mtuhumiwa akimtuhumu mke wake kutembea na mwanaume ambaye bado
hajafahamika. Mtuhumiwa amekamatwa na upelelezi wa Polisi
umekamilika.
9. John Logion, (60), Mkazi wa Mitundu alifariki dunia katika tukio lililotokea
tarehe 22/11/2019 saa 11 jioni kwenye shamba la mihogo, lilnalomilikiwa na
Anthony Lipiti huko Itigi. Uchunguzi wa awali wa Polisi umebaini kuwa
chanzo cha tukio hilo ni wizi ambapo marehemu alikwenda kwenye shamba
la mtuhumiwa kwa nia ya kuiba mihogo na mtuhumiwa kutumia mwanya
huo kumshambulia kwa kumpiga na kitu kizito kichwani. Mara baada ya
3
tukio mtuhumiwa alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea kwa
kushirikiana na Viongozi wa Eeneo husika.
11. Issa Abdallah (2), ambaye alikuwa mlemavu wa miguu alifariki dunia
tarehe 24/1/2020 saa 12 jioni huko katika Kitongoji cha Ibonoa, Kata ya
Sanjaranda – Itigi kutokana na kunyongwa na mama yake mzazi kwa kile
kinachodaiwa kukosa mahitaji kutoka kwa baba wa mtoto aitwaye Abdallah
s/o Muna, (56), Mnyaturu aliyemtelekeza bila matunzo. Mtuhumiwa
amekamatwa na upelelezi wa Polisi umekamilika
12. Jumanne Ndelemo, (22), alifariki dunia baada ya kukatwa na kitu chenye
ncha kali na kaka yake wake aitwaye Hamisi s/o Ndelemo, kutokana na
kumfumania akiwa na mke wake. Tukio lilitokea tarehe 5/2/2020 saa 3:30
usiku huko katika Kijiji cha Makasuku, huko Sasajila na mtuhumiwa
amwekamatwa na upelelezi wa Polisi umekamilika.
13. Heri Mamba alifariki dunia baada ya kugongwa na pikipiki yenye namba
za usasjili MC 273 CDK aina ya FEKON. Kutokana na uchunguzi wa awali
wa Polisi imebainika kuwa marehemu alikuwa amelewa huku akikatiza
barabarani bila kuchukua tahadhari. Mtuhumiwa Ombeni s/o Chanzi,
Mgogo, (35), mkazi wa Chinyika amekasmatwa na amekiri kutenda kosa
hilo na si kuchinjwa kama ilivyodaiwa kwenye malalamiko.
14. Alex Jonas, (40), dereva bodaboda, aligundulika kufariki dunia tarehe
26/2/2020 saa 1 asubuhi na Uchunguzi unaendelea ili kuweza kubaini
chanzo cha kifo cha marehemu pamoja na wahusika wa tukio hilo.
Katika Taarifa ni za upotoshaji zenye lengo la kuleta taharuki kwa Jamii pamoja
na kuwachonganisha Wananchi na Jeshi lao la Oilisi.
4
Mwisho Kamishna Sabas amesema kuwa hakuna Mwanasiasa au mtu yoyote
atakaetumia Jeshi la Polisi kama kimvuli cha kujipatia umarufu, huku
akiwaonya anasiasa wanaojifanya kuwa ni wasemaji wa Jeshi la Polisi
amewaonya na kusema kuwa jeshi halitamvumilia mtu au kiongozi yoyote
atakaeichafua serikali kwa namna moja au nyingine.